Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar


Mkuu nimeshachangia sana; mimi sina tatizo naishi na wayahudi; wakristo; wahindu na wasioamini Mungu

Chama
Gongo la mboto DSM
 
Mkuu nimeshachangia sana; mimi sina tatizo naishi na wayahudi; wakristo; wahindu na wasioamini Mungu
Chama
Gongo la mboto DSM
Samahani chama, ni vile tu imedaiwa na wanafunzi watiifu wa Mohamed Saidi kuwa yeyote asiyekubaliana na ngano anazozimwaga humu hafai kuitwa Muislaam!
 
Last edited by a moderator:
Samahani chama, ni vile tu imedaiwa na wanafunzi watiifu wa Mohamed Saidi kuwa yeyote asiyekubaliana na ngano anazozimwaga humu hafai kuitwa Muislaam!


Ukumbuke pia kuwa litmus test ya Mohammed na wengine wanaoshabikia simulizi lake ni kuwa Muislamu siyo Muislamu kama anapingana na 'wazee wake' Bw. Said au yule ambaye hakubaliani na the revisionist narrative ambayo Mohammed Said ameitengeneza. Ukimsoma sana ni kuwa Waislamu hawawezi kuwemo BAKWATA; na Waislamu ni lazima wakubaliane na kina Ponda na Farid, na lazima waamini uwepo wa dubwasha liitwalo Mfumo Kristu. Muislamu yeyote asiyekubaliana na kumkejeli, kumdunisha au kumbeza baba wa taifa hawezi kuwa Muislamu.

Kwa mtazamo wa hawa Uislamu siyo tena Kumwamini Mungu Mmoja na Mtume wake na haihusiani tena na kujisalimisha kwa Mnyezi Mungu. Kwao Uislamu umegeuzwa kuwa suala la nani anakubaliana na masimulizi ya Mohammed Said nani hakubaliani. Utaona kuwa katika wale wanaokubaliana na masimulizi haya wote wana alama zile zile:


  • a. Kejeli kwa Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere (hawawezi kamwe kujenga hoja bila kumdunisha Nyerere)
  • b. Chuki dhahiri dhidi ya Wakristu (hata kama ni ndugu zao wa damu)
  • c. A revisionist outlook ya historia yetu (Sykes ndiye muasisi wa taifa, Waislamu ndio wapigania uhuru pekee, na Dar-es-Salaam ndio mahali pekee walikotaka uhuru; na Wakristu hawakutaka Uhuru isipokuwa baada ya kukaribishwa na Waislamu wa Dar)
  • d. Wengi (kama siyo wote) bado ni watu wa CCM; chama kile kile kinachodaiwa kuendesha dhulma dhidi ya Waislamu ndicho hicho hicho kinakumbatiwa; serikali ile ile 'iliyounda BAKWATA' ndio hiyo hiyo inatarajia itatue matatizo ya "Waislamu". Utaona pamoja na malalamiko yao yote hutawasikia wanataka kuiondoa CCM madarakani!

Hizo ndizo alama zao...

Bahati mbaya wapo Maelfu kama sio mamilioni ya Waislamu ambao hawajalazimishwa kukubali alama hizi na wanaendelea kunufaika na kulitumikia taifa lao kwa uadilifu mkubwa; bado wanamuenzi Baba wa Taifa na bado wanatambua ushiriiiano wa wazee wote - bila kuwabagua kwa mahali, dini, au rangi - katika kupigania uhuru wa Taifa letu na umoja wetu.
 
zomba
Hebu nikumbushe tena zile sifa za mnafiki.
Halafu nikumbushe na lile neno la kiarabu mnalotamka kumlaani baba wa Taifa-siju lanatui nini.
Halafu jipime...

Nilikuwa natamani leo hii awepo na aone ni nani aliye mbora wa kupanga. Tazama Jasusi alivyoandika juu huko kuhusu kina Mkapa walivyomnini sijui.

Nani asiyejuwa kuwa wakina Mkapa ndio vipenzi na walio bora kwa Nyerere? Kulikoni? hata chembe ya uchungu haikujii kwa hayo? Amma kweli aliyenena "kikulacho ...." hajakosea.
 
Mkuu nimeshachangia sana; mimi sina tatizo naishi na wayahudi; wakristo; wahindu na wasioamini Mungu

Chama
Gongo la mboto DSM

...wewe umesha athirika na "mfumo kristo"........nyinyi ndio Waislamu jina......mnashirikiana na ma-kafir.......
 

MM,

Hayo usemayo si kweli.

Kitabu changu kipo na atakae ukweli atakisoma.
Post zangu zimo humu ndani.

Atakae kujua msimamo wangu Insha Allah anaweza kuzisoma.
 

Jasusi,

Kama Kanisa Katoliki lilisaidia harakati msaada huo ulikwenda kwa Nyerere moja kwa moja.
Mweka Hazina wa TANU wa kipindi kile Idd Faiz Mafongo hakupata kupokea senti hata moja
kutoka kanisani.

Hilo la kukataza waumini wake ni ''documented'' na watu waliopambana na fitna hiyo ni akina
Suleiman Masudi Mnonji, Msham Awadhi, Yusuf Chembera na wengine na ni baada ya safari
ya Nyerere Kusini 1955 na 1956 ndipo TANU ikaweza kuwaingiza akina Mhaiki sehemu za Masasi,
Newala, Nachingwea na kwengineko sehemu ambazo Ukatoliki ulikuwa na nguvu.

Hebu tujikumbushe:

[TABLE="class: MsoNormalTable"]
[TR]
[TD] Conspiracy Theory

[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="width: 601"] At the moment there are two books in existence written by non-Muslims which proves that Christians have used their positions in the government to subvert Islam and Muslims.

Jan P van Bergen in his book, Development and Religion in Tanzania, (1981)
[1] divulges very incriminating information on former President Nyerere.

The book gives details of how during his rule Nyerere used to have private confidential meetings with Bishops to discuss the future of Tanzania. In those meetings Nyerere is reported to have assured Bishops of his continued support to Christianity.

The work reveals how Nyerere guaranteed Christians a privileged position and backed his promise by appointing them to important positions in his government and party.

This book was on sale at the Catholic Bookshop, Dar es Salaam, and was hurriedly withdrawn from sale after it was realised that it was revealing highly confidential and sensitive information on Islam.

[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="width: 601"] The second book is by Dr John C. Sivalon, who in his expose, Kanisa Katoliki na Siasa ya Tanzania Bara 1953 Hadi 1985, [2] unmasks a conspiracy in the government to subvert Islam.

Sivalon revealed that the Catholic Church as far back as 1961 was worried by two prospects.

First, was the unity between the Muslim madhheb (sect) of Sunni, Bohora, Ismailia and Ithnasheri in Tanganyika; and the second, was the transfer of the headquarters of the East African Muslim Welfare Society (EAMWS) from Mombasa to Dar es Salaam.

The Church was worried that the resources in the hands of rich Asian Muslim community in East Africa, coupled with the political power of African Muslims, particularly in Tanganyika, would endanger Christian interests in East Africa.

The Church therefore declared Islam as its enemy in the country and plotted to thwart its progress.
[3]
[/TD]
[/TR]
[/TABLE]

[1]Jan P van Bergen, Religion and Development in Tanzania, (Madras, 1981). passim.
[2] John C. Sivalon, Kanisa Katoliki na Siasa ya Tanzania Bara 1953 Hadi 1985, (Ndanda, 1992).
[3]Ibid. p 37.
https://www.jamiiforums.com/#_ftnref4
 

Mohamed,
Nyerere pia alikuwa akikutana mara kwa mara na mashehe wa Kiislamu. Kila sherehe ya Waislamu alialikwa na alikwenda. Nakumbuka kuna wakati katika miaka ya 70 alivaa kile kibandiko kinachowanasibisha waislamu. Does that make it such that he had confidential meetings with Islamic leaders? Hata baraza la wazee wa Dar-es-Salaam amelianzisha yeye. Sasa hapo kukutana na viongozi wa Kanisa katoliki inakuwaje conspiracy kusubvert Uislamu? Hiyo ni dhana ambayo umeshindwa kuitolea ushahidi. Na kama alikuwa na lengo la kusubvert uislamu iweje amrithishe uongozi mwislamu mwingine na kufanya kampeni nchi nzima akisifia usafi wake?Tumalizie kwa kutoa hiyo documented evidence kuwa kanisa katoliki lilikataza waumini wake kushiriki katika harakati za uhuru. Kwangu mimi bado haiingii akilini. Hata kama unasema msaada wake ulitolewa kwa Nyerere binafsi lakini wakati huo Nyerere was TANU and TANU was Nyerere. Hii haipingiki. Rejea tena mfano wa Machel na ukatoliki wa Msumbiji na Nyerere na ukatoliki wa Tanganyika. Tofauti ni day and night. So let us give credit where it is due. The Catholic church contributed positively to the uhuru efforts of Tanganyika. Najua hupendi kusikia hilo lakini ndio ukweli wenyewe.
 

Zomba,
Isikupe shida. Hata katika dini yetu Yuda alikuwa karibu sana na Yesu kiasi cha kuweza kumbusu shavu. Sisi tuliomfahamu Benjamin Mkapa kabla ya kuwa rais wa Tanzania tunasononeka na tunaendelea kusononeka mkapa kesho.Isingekuwa kwa ufisadi wa Mkapa hivi leo tusingekuwa na kilaza huyu mnamwita Kikwete.
 
MM,

Hayo usemayo si kweli.

Kitabu changu kipo na atakae ukweli atakisoma.
Post zangu zimo humu ndani.

Atakae kujua msimamo wangu Insha Allah anaweza kuzisoma.

Niliyoyasema ni kweli; na maandishi yako ni mashahidi wa hayo yote. Huwezi kuyakwepa. Hakuna kijana Muislamu ambaye hajui sana historia yetu au hajapata nafasi ya kujifunza kufikiri vizuri akasoma kitabu chako halafu bado akawapenda ndugu zake Wakristu, bado akamheshimu Nyerere au akatukuza mchango wa wapigania uhuru wote. NONE. Angalia tu mashabiki wako wote hapa wana sifa hizo hapo juu baada ya kukusoma...

Huwezi kutoka upande mchongoma halafu uje udai ukoka uote...
 

Mag3,

Hakuna njama zozote mtu kama wewe umejaa chuki dhidi ya Waislam na Uislam hakuna Muislam ambaye anajitambua anaweza kuungana na wewe.

Mabandiko yako humu jamvini wanakuweka wazi jiulize wote humu mnaompinga Mohamad Said, kwa nini hakuna Muislam jibu unalo.

Hata mkiwa kule kwenye Chadema yenu adui yenu mkubwa ni Zitto Kabwe sababu ni Muislam.

Nadhani nimekujibu muruwa.
 
Last edited by a moderator:

Unaona sasa mnavyodanganya wewe na mwenzako Mag3, siku zote mkiwa na fikra moja mnakubaliana kila upuuzi.

Haya ulioandika ndiyo kejeli na dhihaka kwa Waislam na Uislam unatumia ubongo wako kutupa majina na alama ili ufanikiwe unachokiandika.

Ndiyo maana nakuambia wewe na Waislam wapi na wapi umesikumwa na chuki zako mpaka kuandika haya.

Mimi binafsi marafiki wangu wengi ni Wakiristo kuliko Waislam na nifanyanayo kazi tunasaidiana kwa pamoja.
 
Last edited by a moderator:
Hayo usemayo si kweli.
Kitabu changu kipo na atakae ukweli atakisoma.
Post zangu zimo humu ndani.
Atakae kujua msimamo wangu Insha Allah anaweza kuzisoma.
Mohamed, mimi naujua msimamo wako na hapa naainisha hoja za MM kwa uchache sana kwa kutumia hoja zako ili kukutendea haki.

A.Kejeli kwa baba wa taifa
- Kwamba alianza siasa alipokutana na Sykes na alikuja Dar kuanza siasa huku watu wa mjini tayari wana mapambano.
-Kwamba alipewa hotuba akaisome UN, yeye hakushiriki kuandika wala ku-review, alikuwa kipaza sauti tu.
-Kwamba alikwenda sokoni bila kujua bidhaa zinanunuliwa, aliyemuokoa ni mshume Kiyate
- Kwamba, alinyooshewa bakora Anatouglo na Rehani Waikela.
-Kwamba alikuwa mdini na alidhalilisha wazee wa kipata, mkunguni na Gerezani
-Kwamba alifika Dar mara ya kwanza 1950 na kabla ya hapo hakujua Dar ilikuwa nchi gani
-Kwamba hakushiriki kuanzisha TANU,Chama kilianzia Burma na wala hakuwa rais wa kwanza wa TANU
-Kwamba alitoa hotuba ya kuaga wazee na kusema hamjui Sykes ni nani
-Kwamba aliua EAMWS kwa maagizo ya kanisa ili kuuhujumu Uislam
-Kwama aliwaweka kizuzini na magereza masheikh bila sababu na hivyo kuwa mwendawazimu
kwa uchache wa kuorodhesha. Twende hoja namba 2

B.- Kutothamini mchango wa wakristu kama akina Lugazia, Cecil Matola, Dr Kyaruzi, Mhando, Dunstan, Kirlo n.k na kuwaondoa katika orodha ya wazee wako kwasababu tu ya dini yao.
- Kuwasingizia wakristo kuwa hawkushiriki shughuli za Uhuru asilani kwa kuogopa vinbarua na kanisa
-Kwa kuficha ukweli kuwa shirika la Maryknoll lilitoa ticket ya Nyerere kwenda New York
-Kumshambulia Mkapa kama Mhariri na kumwacha Ali Maswanya kama waziri wa mambo ya ndani
-Kuweka dhana ya mfumokristo ulioshindwa kuthibitisha kwa mantiki na ushahidi uwepo wake.
-Kusingizia Malima alivunja mfumokristo wizara ya elimu kwa kuanzisha namba za mitihani
-Kuita baraza la mitihani NECTA kama kigango cha kanisa bila kuwa na ushahidi
-Kudai kuwa jeshi la polisi ni mkono wa kanisa hata kama viongozi waliosimamia operesheni hizo ni waislam
- Kudai kuwa EAMWS iliuawa na kanisa bila kuwa na ushahidi wa maneno, nukuu, karatasi au kiwacho.
-Kusingizia kanisa kuwa kuawa kwa EAMWS ili kumaliza ndoto za chuo kikuu ni mkono wa kanisa
-Kusingizia kuwa BAKWATA ilundwa kwa mkono wa kanisa bila ushahidi.
-Kukubali jaribio la Nyerere kuondoshwa uongozini na radicals wa TANU kwasababu tu ni mkristo
--Tukio la awamu ya kwanza lilimhusu Mkatoliki Nyerere, awamu ya pili Mzee wetu, awamu ya tatu Mkatoliki Mkapa na awamu ya nne serikali.

C.''Revistionist outlook ya history''
-Kwamba mapinduzi ya ZNZ ni kazi ya Nyerere na wala sio Wazanzibar ili kuua Uislam
- Kwamba Nyerere alikuja Dar mwaka 1950 wakati huo ni uongo dhahiri shahiri
-Kwamba Nyerere alianza siasa baada ya kukutana na Sykes huo nao ni uongo dhahiri shahiri
-Kwamba Nyerere hakuwa katibu wa AA na wala hakujulikana makao makuu
- Kwamba AA ilianza na Sykes na kuishia kwa Sykes kama TAA
-Kufuta ukweli kuwa Nyerere ni miongoni mwa waanzilishi wa TANU
-Kwamba ni Dar peke ndipo uhuru wa Tanganyika ulipopiganiwa
- Kuficha ukweli wa wapigania uhuru wengine ambao mchango wao kwa taifa hili ni mkubwa sana.
-Kuficha ufisadi wa nyumba ya D.Cameron uliofanywa na familia ya Sykes
-Kuficha ukweli kuhusu kufukuzwa kwa sheik Amir

D: Wengi wa waislam ni CCM
- Umesema mlinong'oneza misikitini msimchague Mkatoliki na mkafanyikiwa
- Ulisema mtoto wa CCM, TANU ndiye aliyeua EAMWS ili kuua uislam
-Kwamba CCM a.k.a TANU iliyoua EAMWS, Baraza la wazee wa TANU ndio hiyo mlionong'onezana kuichagua misikitini
-Kwamba mwaka 2000 hadi 2005 Masheikh mliichukia CCM kwa dhulma katika elimu, mkahamasishana kuiunga mkono CUF.
Leo dhulma ile ile ipo mnahamasishana misikitini kuitetea CCM.

Haya ni kwa uchache tu na haraka haraka, nikiwa na muda nitachimba hadi yale uliohimiza suluhu ama sivyo UN,AU watatia timu kusuluhisha vita.

Msimamo wako kumuunga mkono Ilunga dhidi ya mauaji ya maaskofu upo hapa.
Msimamo wako kuhusu historia ya Tanganyika iliyopiganiwa na wazee wako tu ipo hapa.
Msimamo wako kuhusu Christian Hegemony upo hapa.

Msimamo wako kutetea utafiti wa Warsha ambayo wewe ulikuwa mshiriki upo hapa.
Msimamo wako juu ya fikra za Malik ambaye ni mkufunzi wako upo hapa na kwamba ndiye aliyeongoza utafiti.
Msimamo wa ushiriki katika kuandika kitabu cha Ghessany ambacho umekinukuu mara nyingi upo hapa.
Msimamo wako kuhusu uzushi wa namba za mitihani upo hapa.
Msimamo wako kuhusu hotuba ya Nyerere kumkana Sykes upo hapa jamvini Yarabi!

Lakini muhimu zaidi msimamo wako wa kukataa hoja zinazokinzana na zako upo hapa.
Msimamo wako kukimbia maswali yatakayo ibua ukweli uliofichika upo hapa.
Na msimamo wako kukiri kuwa haya ni mawazo yako na wala si ukweli wa kuaminiwa na kila mtu tunao hapa.
Msimamo wako kuhusu kutoktokuwa na hotuba ya Rehani waikela upo hapa.

Katika hayo kama lipo nililokuonea liseme, sitajibu kwa maneno yangu nitavuta uzi na quotation.

Khairi inshallah wasalimie maswahib wote hapa Kariakoo panapo majaaliwa tutawatembelea karibuni.

Masalam
 
Nguruvi3,

Unaandika uongo mwingi wakati mwingine inakuwa ngumu kukubali unachokiandika.

Jana umewataadhalisha humu jamvini kuwa Marik wa Pakistan ndiyo mfadhili mkubwa wa Masheikh wanaoenda kusoma Pakistan.

Kwa faida ya wanaotusoma kama hizo habari zako ni za kweli tutajie majina mawili tu ya hao Masheikh wanaosoma Pakistan.

Usipotaja mabandiko yako takuwa nayachukulia kama ngano tu.
 
Last edited by a moderator:
Nisingependa kutaja majina kwasababu maalumu kabisa, nielewe hivyo.

Hata hivyo nakupa homework moja. Angalia masheikh ''vijana'' katika misikiti inayozunguka kariakoo.
Ritz, nina uhakika na ninachosema ndugu yangu. Huyu Malik unamsikia mimi namfahamu.

Mfano, nimesema kuwa Malik aliwahi kusema, harakati za waislam wa Tanzania ili zifanikiwe lazima zianzie chini mitaani kwa kuwahamasisha na wala si juu. Nikasema anayekataa kauli hiyo anisute! hakuna! wewe hujajifunza kitu hapo ndugu yangu!

Ritz, nimekusoma hapo nyuma kuhusu swali hilo nikakaa kimya nadhani umeona kama weak point ya kunishambulia! trust me, you're not informed !

Hebu jiulize kwanini kuondoshwa kwa Malik hakupigiwi upatu sana kama kuondoshwa kwa sheikh Amir!

Ritz mimi si mgeni tena hapo mjini, najua kula chapati siku nyingi, gahwa n.k.
 

Nguruvi,


Humjui Sheikh Malik wala alichokuwa anasomesha.

Insha Allah napitia kumbukumbu zangu nitaweka kitu
kuhusu Sheikh Malik.

Ila zingatia kitu kimoja.
Uislam hauwezi kufunza dhulma.

Uislam siku zote unasimama kwenye uadilifu hata kwa
yule asiyemuamini Allah.
 
Nakubaliana nawe kabisa kuwa Uislam kama dini hauwezi kufunza dhulma.
Lakini Waislam wanaweza kuutumia Uislam kwa njia zisizo za kiislam kufunza dhulma.

Uadilifu katika Uislam haushii katika kuvaa kanzu na baraghashia, uadilifu ni mwenendo mzima wa maisha ya mwanadamu kuanzia kauli na matendo yake. Kauli tu inatosha kumghafilisha mja na kumuondoa katika uadilifu.
 

Unataka kutueleza kuwa Kikwete ni chaguo la Mkapa na Mkapa ni chaguo la Nyerere lililo "mkolimba"? Unajichanganya unajuwa?

Hayo yote tisa, kumi ni kuwa tungetamani Nyerere awepo na ajuwe ni na nani mbora wa kupanga, usemi wako unazidi kuyakinisha kuwa kila alilofanya Nyerere lilishindwa. Unanisisitizia kuwa hata kipenzi na chaguo lake "Mkapa" nalo lilikuwa ni "failure" Sijui kwa nguvu za nani?

Ndio maana ya mimi kusikia uchungu sana wa kifo chake, labda angelikuwa hai angetanabahi kuwa yuko wrong kwa sana tu. Hii inanikumbusha maneno ya Darwesh Kibendera.
 
Samahani chama, ni vile tu imedaiwa na wanafunzi watiifu wa Mohamed Saidi kuwa yeyote asiyekubaliana na ngano anazozimwaga humu hafai kuitwa Muislaam!

Mbona kuna mengi ambayo sikubaliani na mohamedi Saidi hilo halinifanyi mimi nisiwe muislamu; imani yangu haitokani na mafundisho ya mohamedi Saidi, mimi ni muislamu kama kuna kitu ambacho sikielewi najua wapi pa kutafuta majibu; sina muda wa kujiingiza kwenye majibishano ya kidini; mohamedi Saidi anaongelewa waislamu walionewa bahati mbaya mimi sipo kwenye kundi hilo na wala sitokani kwenye familia ya kifisadi ila naishukuru sana serikali ya Tanzania na sera za elimu za Mwalimu Nyerere ndizo zimenifikisha hapa kikubwa niliwasikiliza sana wazazi wangu wakati wananisisitiza kwenda shule nilikwenda na si mimi tu pamoja na wadogo zangu; nawapa ushauri wa bure msije mkachinjana kwa imani za kidini dini na siasa havijichanganyi msidanganye; wanaonufaika na vurugu hizo ni watu wachache sana ila wanatumia ujinga wa wengi

Chama
Gongo la mboto DSM
 
Last edited by a moderator:

Nguruvi,

Kwa hivyo ulivyoandika nakupa ushauri.

Hebu tengeneza paper na utie footnote
kukazia hoja zako toka maandishi yangu.

Kwa njia hii tutakuwa na kitu thabit na
pahala pa kuanzia mnakasha mpya.

Ikiwa wewe mwenyewe huwezi muombe
Mwanakijiji ambae umemnukuu akusaidie
pamoja na wengine.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…