Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar

Wewe unasema huna dini halafu unataka kuwapangia wenye dini yao.

Waislam ndiyo wameamua kufanya ivyo hata kama jambo lenyewe ni dogo kama punje ya mchele.

WildCard mambo ya Waislam yanakukera sana.
Wala usije ukadhani wazee wetu hawa waliyafanya haya kwa sababu ya DINI yao. Mzee Mohamed kawapachika UDINI wazee hawa ili kuhalalisha agenda yake kuu ya kulipiza kisasi kwa Mwalimu.

Waislam wote wangekuwa wema kiasi hiki tusingeyashuhudia ya akina Gadaffi, Muislam mwenzao ndani ya Jamhuri ya Kiislam ya Libya. Kutoa ni moyo wa mtu tu. Sio DINI wala KABILA inayomfanya mtu awe na moyo wa kutoa.
 

Mbona unachanganya mambo sasa Gadafi katoka wapi tena Mohamed Said kaandika kitabu kuwaenzi wazee wetu kwa kupigania uhuru wa Tanganyika hata nyie huko Musoma mna haki ya kuwaenzi wazee wenu.
 
Mbona unachanganya mambo sasa Gadafi katoka wapi tena Mohamed Said kaandika kitabu kuwaenzi wazee wetu kwa kupigania uhuru wa Tanganyika hata nyie huko Musoma mna haki ya kuwaenzi wazee wenu.
Huko Musoma ndiko walikotoa hicho kifaa kilichokuja kubadili game zima la kusaka uhuru wa Tanganyika. Hao wazee wake walitumwa na DINI yao?
 
Huko Musoma ndiko walikotoa hicho kifaa kilichokuja kubadili game zima la kusaka uhuru wa Tanganyika. Hao wazee wake walitumwa na DINI yao?

Hicho kifaa ndiyo kipokelewa na hawa wazee wazalendo wa Kariakoo msome Nyerere hapo juu kwenye maandishi ya blue.
 
MM,

Labda unipe jibu.

Ilikuwaje historia hii niliyoandika mimi ikawa haifahamiki
na mashujaa hao niliowataja hadi leo hawajaadhimishwa?

Napenda kujibu swali la mheshimiwa Mzee Said kama ifuatavyo. Kwa vile swali lake linadhania mambo kadha wa kadha naomba niainieshe mambo ambayo ni ya msingi na ya tofauti baina yetu kuhusiana na maandishi yake (points of contention)

a. Ulichoandika wewe kwanza siyo historia; ni histohisia. Umetumia matukio ya historia kuelezea hisia zako. Sasa kila mwanadamu ana hisia zake na hivyo hakuna mtu mwingine anayeweza kuwaangalia watu wale wale wa kihistoria (historical figures) na akatoa tafsiri ile ile hasa kama kuna tofauti kubwa ya hisia baina ya watu.

b. Kwa vile hukufuata kanuni za uandishi wa kihistoria (historical method) basi uandishi wako wa aina ya simulizi, vijembe, na kukisia hauwezi kuandikwa na mtu mwingine yeyote. Ukisoma John Illife aliyeandika kwa kufuata kanuni za historia na uandishi wako wewe tofauti ni kama bahari na mlima. Yeye aliandika kitabu cha historia kweli kweli.

c. Kwa vile umeamua kutumia dini kuangalia historia na kuilezea ni wazikuwa mtu mwingine asiyetumia dini anaweza kuangalia matkio yale yale unaoyaona wewe na akayapa tafsiri nyingine kabisa. Mimi niliposoma kitabu chako cha Sykes kwa kweli nilivutiwa na masimulizi ya majina ya watu mbalimbali. Lakini sikuvutiwa kabisa na ushawishi wa hoja. Katika kujenga hoja kwa kweli una udhaifu mkubwa mno kwani badala ya kutumia reason kujenga hoja unatumia 'emotional appeal' na ndio maana umewapata wengi kwa kugusa dini, imani yao.

d. Kwa vile matukio mengi unayoyasimulia yanatokana na yale unayodai ni mang'amuzi yako binafsi (personal experience) au ya kuambiwa (hearsay) na hivyo vyanzo unavyotumia haviwezi kuhojiwa na wanataaluma wengine ni wazi kuwa hicho unachodai ni historia kitabakia cha kwako peke yako. NInaamini udhaifu wako mkubwa kabisa katika uandishi wako ni hili - the failure to make it possible for other scholars to access the sources you claim to have used to get some information - for either these sources are dead, hidden or exclusively known to you.

Kutokana na hayo basi ni vigumu na haiwezekani mtu mwingine kuandika kuhusu wazee wako namna hiyo. Hata hivyo, inawezekana kabisa mtu kuandika historia ya Tanganyika kwa umakini mkubwa na kutaja baadhi ya majina uliyonayo vizuri zaidi.

Pamoja na hayo ni ukweli pia kuwa umejitahidi kuweka kumbukumbu ya wazee wako na kuyaacha majina yao yatajwe katika historia. Haya ni mafanikio yako makubwa - hata kama ndani yake umeweka limau, pilipili, mdalasini, tangawizi na pilipili manga.

0
 
Binafsi sijaona uchochechezi aliofanya Mohamed Said zaidi ya kuandik historia ya kile anachokiamini.
 
Last edited by a moderator:
Hicho kifaa ndiyo kipokelewa na hawa wazee wazalendo wa Kariakoo msome Nyerere hapo juu kwenye maandishi ya blue.
Wazee wa Mohamed, hasa akina Sykes hawakuwa na UDINI hata chembe. Mzee Mohamed kaamua kuwatundikia drip ya udini wengine wakiwa makaburini tayari!
 
Hicho kifaa ndiyo kipokelewa na hawa wazee wazalendo wa Kariakoo msome Nyerere hapo juu kwenye maandishi ya blue.
naona ngano za Mo. zimeanza kufanya kazi kule zenji tusubiri hapa bongo!
 
Binafsi sijaona uchochechezi aliofanya Mohamed Said zaidi ya kuandik historia ya kile anachokiamini.
Asingeiita ni HISTORIA ya WAISLAM waliosahaulika ndani ya TANU na Tanganyika wakati mdogo wake Abdu amekuwa balozi wetu Ulaya kwa miaka mingi tu!
 
Umesahihisha nini sasa hapa tuambie AA imeanzishwa lini na Matola alikuwa rais lini.

Kama AA kilikuwa chama cha starehe kwa watu weusi huyu mzungu Sir D Cameron kaingiaje kwenye chama cha starehe cha weusi.

Mnamo 1929 sir Cameron aliamua kuwaweka pembezoni mwa starehe za weupe na hasa baada yakuona anakereka kuwaona weusi hao wakiwa jirani sana na maeneo yao muhimu ya burudani na starehe,

Katika kuwaweke mbali aliamua kuwaanzishia kikundi/chama chao cha kushughulikia starehe zao, na Matola akawa ndie kiongozi wao wa kwanza mpaka 1933 alipofariki,

Mwaka 1933 ndipo vibaraka wa mjerumani akina Klest Sykes ambao ni wazamiajia wa Afrika ya kusini waliingia ndani ya chama hiki nao wakaja na malengo yao ambayo ni kudai haki katik himaya za muingereza, katika kuhakikisha dai lao linatiwa nguvu, waliazimia kubadili jina la chama/kikundi liendanena malengo yao na kuwa TAA.
Mwalimu Nyerere alipojiunga na TAA nae akaja na filosofia yake toka chama chake cha TAWA ya kudai uhuru wa Tanganyika.
Ndilo chimbuko la kubadili jina la TAA na wakaanza kupendekeza majina na kuangukia TANU jina lililotolewa na Abdul aliyekuwa nalotangu akiwa Burma vitani,

Swali tusilokuwa na jibu mimi na wewe ni je Abdul alikuwa na ndoto ya chama chenye filosofia gani kabla ya makutano yae na Nyerere?
 

Kwa ninavyoelewa mimi,hisia inajumuisha mambo ya kufikirika tu,kwahiyo unataka kusema kuwa aliyowaandika Mohamed Said ni wahusika wa kufikirika tu. Sasa kama ni histohisia tuambie wale wazee hawakuwepo kwenye mchakato huo?
 
Last edited by a moderator:
Asingeiita ni HISTORIA ya WAISLAM waliosahaulika ndani ya TANU na Tanganyika wakati mdogo wake Abdu amekuwa balozi wetu Ulaya kwa miaka mingi tu!

Angeiitaje,tusaidiane mkuu.
 
Kwa ninavyoelewa mimi,hisia inajumuisha mambo ya kufikirika tu,kwahiyo unataka kusema kuwa aliyowaandika Mohamed Said ni wahusika wa kufikirika tu. Sasa kama ni histohisia tuambie wale wazee hawakuwepo kwenye mchakato huo?

Umeelewa vibaya; ningetaka kusema 'kufikirika' ningesema hivyo. Nikutofautishie kati ya kufikirika na kuhisia?
 
Wazee wa Mohamed, hasa akina Sykes hawakuwa na UDINI hata chembe. Mzee Mohamed kaamua kuwatundikia drip ya udini wengine wakiwa makaburini tayari!

Hizo ni fikra zako na una uhuru wa kuongea chochote wala hakuna wa kukupiga.

Kama wewe unavyosema hauna dini nani kakupinga sasa wewe na watoto pamoja familia ya Abdulwahd Sykes sijui tumuamini nani.

Tafsiri yako ya UDINI ni mtu kuwa Muislam.
 
Umeelewa vibaya; ningetaka kusema 'kufikirika' ningesema hivyo. Nikutofautishie kati ya kufikirika na kuhisia?

Niwie radhi kwa kukuelewa vibaya. Naomba nikuulize,wazee hawa hawakuhusika kwenye mchakato wa kudai Uhuru?
 
Niwie radhi kwa kukuelewa vibaya. Naomba nikuulize,wazee hawa hawakuhusika kwenye mchakato wa kudai Uhuru?

HIvi umedandia hii mada katikati? umesoma wapi ambapo tumesema wazee hawa hawakuhusika katika mchakato wa kudai uhuru? Hivi nikikuuliza - Je Nyerere hakuwa kiongozi wa wapigania uhuru wa Tanganyika wakiwemo wazee hawa nitakuwa nimekkuuliza swali zuri?
 
Hizo ni fikra zako na una uhuru wa kuongea chochote wala hakuna wa kukupiga.

Kama wewe unavyosema hauna dini nani kakupinga sasa wewe na watoto pamoja familia ya Abdulwahd Sykes sijui tumuamini nani.

Tafsiri yako ya UDINI ni mtu kuwa Muislam.
Nimekuonyesha mara kadhaa kuwa sina ugomvi na Uislam. Nina ugomvi na watu wanaotumia DINI zao kwa malengo na dhamira iliyo nje ya DINI zao. Uanzishwaji wa TANU na kudai Uhuru wa Tanganyika hakuna uhusiano na DINI yoyote nchi hii. Ni kweli kuwa walioanzisha mchakato huu walikuwa na DINI zao lakini sizo zilizowatuma kuyafanya haya.

Ndio maana, tangu mwanzo wa TANU na baada ya uhuru wale waliojaribu kumtazama Mwalimu kwa dini yake walikataliwa na watu wa DINI zote.

Mwalimu naye hakuwaangusha WATANGANYIKA. Akaupiga vita UDINI na UKABILA kwa nguvu zake zote kwa kutumia Katiba na sheria zilizokuwepo. Hakuwaachia polisi au UwT kulifanya hili peke yao kama anavyaoagiza Kikwete wetu wa sasa.
 

Sasa kama ndiyo hivyo kwanini hujajibu swali la msingi la Mohamed Said kuwa kwanini wazee hawa hawakuandikwa kwenye historia?
 

WildCard,

Hakuna udini wowote inakuwa ngumu kuwataja hawa Wazee wetu bila kutaja Uislam wao ndiyo kitu ambacho hutaki kukisikia.

Kuna Masheikh wameshiriki kutafuta uhuru ukiwataja hao umetaja Uislam bahati mbaya hilo linakuwa gumu kutenganisha harakati za uhuru na dini ya Kiislam itabidi uwe mvumilivu tu ndugu yangu huwezi kuzuia mvua.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…