Ni rahisi sana kubomowa, si rahisi kujenga. Ikiwa nyumba inayomchukuwa mtu miaka 2 kuijenga unaweza kuibomowa kwa siku moja tu, sasa piga hesabu nchi iliyobomolewa kwa miaka 44 mfululizo, itachukuwa muda gani kuijenga? Nakwambia miaka 44 kwa kuwa Nyerere 24, chaguo lake la kwanza 10, chaguo lake la pili 10.
Nchi hii ndio kwanza Kikwete kaanza kuijenga ipasavyo, kumbuka kuwa yeye tu hakuwa chaguo la Nyerere na yeye ndiye tunashuhudia akileta mabadiliko ya kweli ya utawala mpaka ya uchumi.
Hata wapigania Uhuru waliosahauliwa na Nyerere na vikaragosi vyake kwa miaka 44 tumeona wakikumbukwa rasmi kwa mara ya kwanza kwenye awamu hii ya uongozi.
Hivi Kikwete anajenga nchi au anaibomoa? Naona kama vile muungano unafia mikononi mwake, umoja wa watanzania unafia mikononi mwake, CCM inafia mikononi mwake. Na maliasili za Watanzania zinaporwa mikononi mwake. Kama huo ndio ujenzi basi tunaomba Mungu atunusuru na balaa linalotusubiri huko mbele.