Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar


G,

Hakijakufikia kisa cha Sheikh Abubakar Mwilima na Nyerere
kuhusu jamii zilizoathirika na ukoloni?

Sheikh Mwilima alilileta suala la Wahzabe, Wabarabaig akawajumuisha
pamoja na Waislam katika Kamati Kuu ya CCM.

Akamuomba mwenyekiti atupie jicho...
Waingereza wana msemo, "the rest is history."

Iko post niliweka baada ya kuulizwa swali na Bi Zubeda.
Itafute.
 
Kumbe wazazi wako ni Wakirstu halafu wewe siyo Mkirstu kwa nini wasikulaani wewe mtoto wao ambao siyo Mkiristu wakimbilie kutulaani sisi.
 
Jasusi,

Hoja ya Wapagani huletwa kama counter weight dhidi ya Waislam.
Sisi hupuuza.

Tunajua hali ya mambo itakapotakata itakuwa ni hoja zetu na serikali
na labda na kanisa.
Kama hoja zenu zingeilenga serikali bila kuathiri watu wengine, hakika tusingekuja hapa jamvini. Lakini sivyo mambo yalivyo, hoja zenu zinalengo ya kupandikiza chuki na kuligawa taifa kwa manufaa yenu binafsi.
 
Kumbe wazazi wako ni Wakirstu halafu wewe siyo Mkirstu kwa nini wasikulaani wewe mtoto wao ambao siyo Mkiristu wakimbilie kutulaani sisi.
 
Kama hoja zenu zingeilenga serikali bila kuathiri watu wengine, hakika tusingekuja hapa jamvini. Lakini sivyo mambo yalivyo, hoja zenu zinalengo ya kupandikiza chuki na kuligawa taifa kwa manufaa yenu binafsi.

G,

Wenye kunufaika wanajulikana.
Acha mzaha.
 
Nashangazwa hata na mimi leo waliozibwa midomo, walionyimwa haki zao wakisema yaliyowakuta inakuwa uchochezi?

Hivi hao wahadzabe, Nyerere aliwafanyia nini kwa miaka 24 aliyokaa madarakani?

Lakini leo Kikwete kawawekea shule kila kata.
Hapo ndipo unapokuwa kipofu kwa ushabiki wa kijinga, ebu nitajie shule moja tu ambayo wahazabe wamejengewa na huyo fisadi wako! Wahazabe wamevamiwa na kunyang'anywa maeneo yao ya asili ya kuwinda kwa sera mbovu za uwekezaji na sasa wanakufa njaa, huyo vasco da gama wako kashindwa hata kuwapa chakula cha msaada.
 


Rais ataka juhudi zaidi za kuondoa Wahadzabe porini

RAIS Jakaya Kikwete amesema shule zinazojengwa katika maeneo ya Wahadzabe, watu wa jamii hiyo wasiachwe wasome peke yao, badala yake wachanganywe na wanafunzi kutoka maeneo mengine.
Alisema hatua hiyo itasaidia kuwafanya wanafunzi wa kabila hilo kujifunza tabia kutoka kwa makabila mengine ya wanafunzi ambao watapelekwa kusoma kwenye shule na pia kuzifanya shule zilizojengwa katika maeneo yao kuendelea kuwa na wanafunzi.

Soma zaidi: Rais ataka juhudi zaidi za kuondoa Wahadzabe porini ~ lukwangule entertainment


Nyingine?

Akizungumzia kuhusu sekta ya elimu, alibainisha kuwa tayari serikali imeshaboresha mazingira katika shule ya msingi Munguli ambayo asilimia kubwa ya wanafunzi wake ni Wahadzabe.

"Katika shule hiyo tumejenga vyumba vitano vya madarasa, mabweni mawili, matanki mawili ya kuvunia maji ya mvua pamoja na vyoo bora," alisisitiza.

Soma zaidi: Miradi ya Wahadzabe kugharimu mil. 26/-

Nyingine?

Napenda ufahamu pia kwa mara ya kwanza Rais Kikwete amewapatia hati za kumiliki ardhi Wahadzabe ambapo hakuna aliyewakumbuka kwa hilo katika awamu zoooote, si Nyerere, Mwinyi wala Nkapa. Walikuwa wakidhulumiwa ardhi zao bila kujijuwa. Cheza na Kikwete wewe?
 
Kumbe wazazi wako ni Wakirstu halafu wewe siyo Mkirstu kwa nini wasikulaani wewe mtoto wao ambao siyo Mkiristu wakimbilie kutulaani sisi.

......

Hapana Ritz, mama yangu kabla ya kuolewa na baba yangu alikuwa muislam, aliolewa na baba ambaye alikuwa sio muumini wa dini yeyote, sasa sijui kama alipoteza uislam wake au vipi! nijuavyo, ikitokea baba akitaka kuchinja ng'ombe(baba alikuwa mfugaji) alilazimika kumuuita mzee wa kiislam amchinje ng'ombe kwa kitoweo.

Sijui alikfanya hivyo kumheshim mama au vipi sina uhakika. Nilichokiandika hapa ni kulaani mgawanyiko unaoletwa na nyie ambao mnaligawa taifa hili katika mapande ya WAO wakristo na NINYI waislam! hii ni hatari sana.

Kwamba wazazi wangu wanilaani kwa kuwa ATHEIST, haina maana kwani mtu ukisha kuwa na umri wa miaka 18, unahaki ya kujiamulia mambo yako! au wewe hulijui hilo? watoto wako wakiukana uislam utawalaani?
 
Kama hoja zenu zingeilenga serikali bila kuathiri watu wengine, hakika tusingekuja hapa jamvini. Lakini sivyo mambo yalivyo, hoja zenu zinalengo ya kupandikiza chuki na kuligawa taifa kwa manufaa yenu binafsi.

.......

Naona mpaka sasa mmeshindwa kuonesha uchochezi na dhihaka za Mohamed Said kwa wapigania uhuru. Tunachokion ni kuenziwa na Mohamed Said kwa wapigania uhuru waliosahauliwa.

Jiulize, kwa historia iliyoandikwa kivukoni kwa kuanzia na kuishia kwa Nyerere huko ni kujenga. Na Mohamed Said anapokuja kuwakumbusha waliosahauliwa ambao walimpokea Nyerere wakamuweka majumbani kwao inakuwa uchochezi?

Huoni kuwa hapo anajenga kwa kukumbusha kuwa Waislaam hawakujali kuwa Nyerere ni mkatoliki, wakamuweka nyumbani kwao, wakala nae wakalala nae, wakamjulisha kwa jamii ya Kiislaam, wakamfanyia kila jema ambalo mgeni hustahili kufanyiwa halafu kawasahau. Fikiri, jiulize, kisha jijibu.
 
Uwe unaandika kama mtu alieenda shule, kwanini unajumlisha hoja za watu? unaposema "mmeshindwa" unamaana gani? nani ameshindwa?
 

1) Kwanza huyo mama'ko alishatoka kwenye Uislaam, Uislaam hauruhusu mwanamke wa Kiislaam kuolewa na asiye Muislaam.

2) Mafundisho hayo ya miaka 18 katika Uislaam hakuna, sisi ni watoto kwa wazazi hata tunapozeeka. Hatuamuwi cha kufanya mzazi asichokitaka labda tu iwe mzazi anataka kutuondoa katika Uislaam na mafundisho yake na hata hapo hadhi yake ya uzazi itakuwa ipo palepale na hatuwezi kuhasimiana nae na badala yake tunatakiwa tuwe wanyeyekevu na kumuonesha lililo sahihi bila hata kumgunia.
 
Uwe unaandika kama mtu alieenda shule, kwanini unajumlisha hoja za watu? unaposema "mmeshindwa" unamaana gani? nani ameshindwa?

Kuanzia mleta mada mpaka wewe na wengine walio kama wewe.

Umeona nimekutajia japo shule "moja" ya Wahadzabe? tena nimekuwekea na picha ya Kikwete alipowatembelea, umeiona?
 

Nisiingie kwa wazazi wako tujadili upande wetu. hii ya mtoto akifikisha umri wa miaka 18 anajiamulia mambo yake mwenye umeipata wapi ni imani yako au dini gani inasema hivyo Uislam hauna umri wa kuwatii wazazi.

Mimi binafsi watoto wangu wakiukana Uislam nawalaani ndiyo mafundisho ya dini yangu mtoto wangu hawezi kuolewa/kuoa mtu wa dini ingine kama atafanya ivyo basi hana radhi na mie.

Hakuna mtu yeyote ambaye anataka kuwagawa Watanzania kwa misingi ya dini hizo ni propaganda zenu watu wanaelezea walivyosahuhulika na dhulma wanazofanyiwa keki ya taifa tule wote kama Watanzania.
 

Bahati sana mimi sio muislam kwa hiyo hayo hayanifungi.
 

Bahati sana mimi sio muislam kwa hiyo hayo hayanifungi.

......

Lakini darsa umepata maana ulisema kuhusu mama'ko kuwa; "sasa sijui kama alipoteza uislam wake au vipi!"

Nina uhakika sasa umeelewa kuwa alipoteza Uislaam wake na pia umeelewa Uislaam unavyowaenzi wazazi na hiyo itakujuza msukumo aliokuwa nao Mohamed Said kuandika historia kuhusu wazee wake "waliosahauliwa" kwa makusudi kabisa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…