Nguruvi3,
Kuna siku nilikuambia usichanganye tamaduni za watu na Uislam huwezi kuelezea matatizo ya watu wa Kilwa, Mtwara, watoto hawataki kwenda shule ndiyo matatizo ya Waislam wa Tanzania unakosea sana katika hao ambao hawaendi shule na Wakirsto wapo wengi usitake kuwasingizia Waislam.
Hebu nenda mikoa kama Mwanza, Bukoba, Shinyanga, kaangalie jamii ya Kiislam inafanana na jamii ya Mtwara na Lindi.
Matatizo ya Mtwara na Lindi yanajulikana mpaka watu wanakosa msukumo wa elimu siyo Uislam wao kutokana na siasa mikoa ivyo kutupwa na serikali toka ukoloni.
Nguruvi3, matokeo ya darasa la saba kwenda kidato cha kwanza alama za kufahulu uwa zinapatikana wapi.
Nimeongelea matokeo ya kidato cha nne ambayo yapo hapa JF.
Nashukuru sana kuwa unatetea hoja zangu vema sana. Ni kwa sababu hizo naomba uungane nami kumlaani mwandishi wa hiyo makala ambaye amechukua matatizo ya sehemu fulani na kuyafanya matatizo ya waislam.
Kama ulivyosema, huko Bukoba, Mwanza nami naongezea Machame na Mbeya hali ni tofauti sana na kwingineko kama Rufiji Kilwa, Mkuranga na kwingine.
Hivyo basi tatizo kumbe si Uislam wala hujuma kwa Uislam. Tatizo lipo katika jamii accross the board.
Nina maana kama ipo jamii ya wakristo ambayo ipo nyuma basi tatizo si ukristo wao bali maingira waliyopo.
Niliwahi kuandika hapa kuwa nimeishi Peramiho, Magila, Shirati, Bumbuli n.k. huko nimekuta watu ambao hawajakanyaga shule licha ya kwamba ndiko mfumo tuhumiwa''mfumokristo'' ulipo.Kule kwetu Mjasani, Pongwe hadi Pangani nako hakuna tofauti na huko nilikotaja.
Alaa!!! kumbe basi hili ni tatizo la wote na si la jamii fulani.
Tukishaelewa hivyo, sote tusimame na kumkemea mpuuzi yoyote atakayetafuta sababu za kihayawani ili kufanya tatizo la sehemu moja kuwa linasababishwa na upande mwingine hata kama upande husika una tatizo kama hilo pengine kubwa.
Miongoni mwa sababu za kipuuzi ni hizi za kutumia dini.
Kwamba fulani ni John hata kama ni fukara na wala hajaona daftari linakuwaje huyo ana advantage kuliko fulani mwislam.
Kwamba fulani anafanikiwa si kwasababu ya jitihada zake bali dini yake hata kama kichwani hakuna kitu.
Kwamba wale waliofanikiwa kwa kutumia dini wamefanikiwa kwa bahati tu maana majina yao ni kikwazo hata kama ni wataalamu waliobobea.
Tatizo ni kuumba hadithi za kitoto na kijinga za kusema Nyerere alitanguliza wazanzibar wauawe na mwislam Idd Amin.
Kumbe basi leo Talibani wakituvamia wapo wendawazimu watakaosahau Utanzania wao na kujiunga na Taliban hata kama tunajua ni wapuuzi wasioujua uislam.
Haya yanafanywa ili kuleta farki katika jamii. Watanzania bila kujali dini zao wanaumizwa na inflation na wanapigika kikamilifu na maisha. Sasa wanapotokea wapuuzi na kudhani kilo ya siukari inauzwa kwa majina ya dini, hawa hawafai katika jamii yetu, we must denounce them from the very beginning.
Ni kwasababu Somalia iliwappuuza wajinga wa calibre hii ndio maana leo kuna mtoto amezaliwa na ameoa nchini Somalia akiwa anakimbia vita kila siku. Hajui amani ni nini licha ya ukweli kuwa jamii yao ni ya dini moja.
Katika jamii iliyochanganyika kama yetu tukiruhusu tu chuki zikapaliliwa tutauana kwasababu tu wapo wajinga wachache walioamua tuwe hivyo.
Inapofikia mahali Mtanzania anamwita mwenzake adui ujue hapo si kwema.
Lakini Ritz, muhimu si kuficha kichwa katika mchanga huku mwili ukiwa nje. Huko ni kujidanganya.
Unajua wazi kuwa tatizo si Nyerere, Ukristo n.k. kwanini watu waondoe jicho mahali husika na kutafuta simple and stupid reasons to justify their unjustifiable course.
Hivi mtu anaposema Wazanzibar wanachangia elimu ya juu huku tukijua si kweli hawana bajeti hiyo, hapo tunamsitiri mtu huyo kwa heshima gani. Yeye hakutusitiri kutudanganya tunasababu yoyote ya kumsitiri kweli.
Huyu si mpuuzi tu na kama nimekosea tumwiteje!
Mtu anaposimama na kusema commonwelath ni Anglican na Tanzania imejiunga akisahau kuwa Pakistan na Bangladesh kuliko na radicals kweli kweli ni wanachama wa commonwealth anatufikiriaje.
Kwamba mtu anatufanya wajinga wa kuamini kuwa common wealth ni shirika la wakristo huku akijua kuna Francophone na Arab League achilia mbali Latin America.
Huyu mtu anayedhani sisi ni wapumbavu kiasi hicho anahitaji kusetiriwa kweli zaidi ya kumwaga mzima mzima.
Chuki ya mtu binafsi dhidi ya watu wengine iwe yake na ibaki kama yake wala lisiwe suala la kitaifa.
Ni hiari ya mtu kusoma chuki hizo, tusichokivumilia ni kupanda chuki hizo miongoni mwa vijana wetu wadogo wa imani na makabila mbali mbali.
Ritz, fikiria hivi, mtu kapata elimu kutoka shule ya mfumokristo, leo anasimama na kulaani huku akichagiza wenzake wasipeleke watoto kutafuta elimu. Huyu ana heri na waislam kweli. Yeye alikwendaje na kwanini.