Mkuu Ritz, heshima kwako
kwanza uelewe sina interest na mambo ya Dini kwangu hayana nafasi
Pili labda nikwambie nimemsoma Moh kwa muda Mrefu na kwenye minakasha yote inayomuhusu Moh nimeifatilia mwanzo mpaka mwisho, katika moja ya maoni yake alizungumzia kuwa nyuma kielimu kwa baadhi ya maeneo yenye Waislam. Na katika kumalizia alilifanya hilo tukio lilikuwa ni makusudi ya Serikali ama niseme ni njama za Nyerere na Kanisa lake la Kikatoliki dhidi ya Waislam
Hiyo hoja ya Mzee Moh imechukuliwa nzima nzima na Waislamu wengi na hata wasomi wakiwemo
DULLAH MSAVIVOR, ukimsoma Dullah anakwambia mamake ndio alimuencourage kupiga shule na alipofika sekondary walijikuta wako (Waislamu) wachache na moja kwa moja aliingia kwenye upepo wa Mzee Moh kuwa Waislam walibaguliwa kuingia Masekondary
Hoja ni kuwa
Utafiti ufanywe wa kujua sababu hasa ni nini?
mimi nilieleza hivi
1) Utamaduni na mila unaweza kuwa ni chanzo kikubwa kwa baadhi ya maeneo kutozingatia Elimu, hili nililiona usukumani miaka ya nyuma kwa wengi kushiriki zaidi kwenye ufugaji na kilimo. pia inaweza kuwa kwenye maeneo yenye Waislamu wengi pia kutozingatia Elimu kutokana na mila ama Tamaduni zao (kuolewa mapema, elimu za unyago na jando) uvuvi?
2) Nilizungumzia Dini pia inaweza kuwa chanzo cha watu kutofatilia Elimu, hapa tatizo kubwa ni nani anatafsiri maandiko ya Dini na anayatafsiri kwa malengo gani?. Kuna imani iliyokuwepo ZAMANI kuwa Elimu ya Kizungu ni ya Kikristo hivyo kwa Muislamu kushiriki hiyo elimu ni sawa na kujisilimisha na kuwa Mmisheni, swali ni kuwa watu wa hayo maeneo wameelimishwa kuwa hilo sio sahihi? na elimu ya Kizungu haihusiani na mtu kusilimu?
Je tafsiri na Mahubiri kama ya kule Nigeria ya BOKO HARAM, yaani Elimu ya Kimagharibi ni haramu ni tafsiri sahihi ya Uislamu? je tunajuaje kama hayo yanayotafsiriwa Nigeria hayatafsiriwi kule Kilwa, Tabora, Kigoma nk?
Nadhani Mzee kama Moh angejitahidi kutumia nguvu na wakati wake kuwaelimisha Waislamu kuhusu umuhimu wa Elimu hasa katika maeneo yenye uvivu na kutozingatia elimu kama kule Kilwa nk, zaidi ya kuwaonyesha kuwa kukosa kwao elimu kumesababishwa na Nyerere na Kanisa lake la Kikatoliki