THE BIG SHOW
JF-Expert Member
- Feb 28, 2012
- 16,950
- 13,527
Sifa za kijinga! kunywa wine umeona issue eti ndio ma great thinkers upumbavu mtupu saa nyingine muwe munaficha upumbavu sio kilakitu ni cha kuleta hapaRitz,
Mimi sivuti bangi, lakini nampenda Bob Marley. It is the message in his song and not his lifestyle that moves me. Kilevi changu ni wine, basi. Hata bia ya safari siku hizi sinywi baada ya makaburu kuichakachuwa.
Jasusi,
Naamini unajua kuwa sijawahi kugusia ustaarabu wa Nyerere katika
mjadala huu.
Huwa sifurahishwi na maneno yanayoweza kumvunjia adabu mtu mzima.
Kumbe historia ya nchi hii ilipotoshwa kiasi hiki??
Tunashukuru sana leo kuja kuufahm ukweli,sasa hao wanaosema chuki za MOHAMED SAID,,
Chuki ziko wapi??
Katika mihadhara yako hujawahi kusahihisha hili au hata kuonekana kulikemea... na hivyo kwa mtu ambaye anazungumzia heshima kwa wazee wake inaonekana ni kukubaliana nalo... hasa unapoleta stori za Mtu mzima kwenda sokoni bila senti hata moja mfukoni akitumaini kuokota njiani...
KI,
Wakati mwingine mie hujisemea huenda hawa jamaa wanabisha kwa kutokujua.
Nimeeleza kuwa Abdu Sykes akifahamiana na Jomo Kenyatta katika miaka ya 1950
mdogo wake Ally akimjua Kenyatta Nairobi katika miaka ya 1940s mwishoni.
Nawaambia Ally Sykes akiandikiana na Kenneth Kaunda 1953.
Imepita taharuki nzito.
Jamaa wamekuwa kama wamepigwa na radi ya saa saba mchana jua kali.
Ndugu zangu wananishika uongo.
Kote ninakopita ulimwenguni nikieleza haya maswali huwa yanalenga kutaka
taarifa zaidi.
Hapa nyumbani naitwa "mwongo," "mzandiki," "mchochezi."
Wanatamani kuwa historia hii ingeanza na Nyerere.
Tujalie tuikatae historia hii...
Ndiyo tutakuwa tumejenga au tunabomoa muruwa wetu?
Ritz,
Binadamu ana asili ya kusahau haraka naona niwakumbushe yaliyotokea Mwembachai
huenda wakakumbuka na kutafakari:
[SIZE=+0]After Eid prayers on 29 January 1998 Muslims at the Mwembechai mosque held an Eid Baraza. The Baraza discussed the recent government ruling on Eid prayers. Later, Muslims went on with the usual Eid festivities of visiting friends and enjoying sumptuous meals. On that day there was inter-religious dialogue neither at Mwembechai nor Mtambani. However, a week later, on 8 February, 1998 Padre Camillius Lwambano of the Mburahati parish in Dar es Salaam said that on Eid day he passed by Mtambani mosque in Kinondoni and Mwembechai mosque in Magomeni and heard how "The Lord Jesus Christ was being ridiculed by Muslim preachers in their public lectures." His emotionally-charged claims were broadcast over Radio Tumaini, which is owned and run by the Roman Catholic Church. Padre Lwambano denounced the government for giving empty promises on the issue of Muslim preachers. He gave the government two alternatives: to ban blasphemous public talks and take severe measures against Muslim preachers; or to make a public admission of its failure to put an end to blasphemy in the country. That was Sunday, 8 February, 1998.[/SIZE]
[SIZE=+0]On the following day the government issued a two-pronged statement. In the first part, all Christians in the country were asked to accept the governments sincere apology for the deep religious anguish they went through on Eid day. In the second part the government promised to take stern measures against all Muslim preachers who organised the blasphemous talks on that day. The statement was issued by the Dar es Salaam Regional Commissioner, Lt. Yusuf Makamba. That was Monday, 9 February, 1998. On the following day the Dar es Salaam Regional Police Commander, Mr. Alfred Gewe issued another statement which was actually a footnote to the government statement of the previous day. Mr. Gewe emphasised that the government measures would be very harsh and far-reaching. That was Tuesday, 10 February, 1998. After nightfall on the same day the arrest of Muslim leaders began. The Imams of Mtambani, Kibo and Mwenge mosques were taken out of their houses and arrested in the small hours of the morning. On 11 February, 1998 a large contingent of armed policemen surrounded Ubungo Islamic High school at midnight, and unnecessarily harassed the students and teachers. They said they were looking for Sheikh Shaaban Magezi, a Muslim preacher of comparative religion. They were told that Sheikh Magezi was neither an employee of the school nor a student. And of course they did not find Magezi in the school premises. To keep themselves busy, they decided to storm into the neighbouring house of an old man, Sheikh Abdulrahman Kileo. They harassed him and his wife, Mama Zainabu. They searched his house for about two hours, they found nothing of interest and left.[/SIZE]
[SIZE=+0]Around 3.00 p.m. in the afternoon of Thursday 12 February, 1998 a group of about twelve uniformed and armed policemen raided Mwembechai mosque and abducted Sheikh Shaaban Magezi who was chatting with friends outside the mosque. There was no public lecture on that day, and except for the people who were offering prayers inside the mosque, there was no public gathering at the area. Within an hour after Sheikh Magezis abduction, a large band of policemen, including the para-military police force surrounded the mosque. As the whole mosque was cordoned off by heavily armed policemen, Muslims who were praying inside the mosque, fearing that they might be attacked, decided to remain in the mosque. As one of them said later, "We could not risk coming out of the mosque, because the police could maim us and then claim we had attacked or provoked them. We believed by staying inside the mosque no one could accuse us of having provoked or attacked them." Their guess was wrong. Around 8.00 p.m. more armed policemen were brought to the area. The situation became tense and many passers-by were arrested.[/SIZE]
[SIZE=+0]Around 1.00 a.m. the government ordered the Tanzania Electrical Supply Company (TANESCO) to cut power supply in the mosque. When the whole area was plunged into pitch darkness the policemen threw irritant and tear gas bombs into the mosque. People who were in the mosque were confused. At that point the policemen broke into the mosque and beat up the Muslims and dragged them into the police vans. In that operation many Muslims, especially old men and women sustained heavy injuries. By daybreak the government had discovered that the majority of those arrested and injured were very old Muslim women. Why did the government order its police force to storm into the mosque and beat up innocent worshippers? What was their crime? An explanation had to be found. In the morning the Minister for Home Affairs, Mr. Ali Ameir as well as the Dar es Salaam Regional Police Commander, Mr. Alfred Gewe issued a statement that the government ordered a power black out and a police raid into the Mwembechai mosque because it was suspected that some "ruffians and criminals" had taken refuge inside it.[/SIZE]
[SIZE=+0]On Friday, 13 February, 1998 the entire Mwembechai area was infested with plain clothes policemen. The large presence of policemen intensified the fear of Mwembechai residents and especially of Muslims who were going for Friday prayers at Mwembechai mosque with the previous nights crackdown still very fresh in their minds. Nevertheless, Muslims turned out in great numbers. They cleaned the mosque which was besplattered with blood puddles and other stains. The Friday prayers were conducted without incident. After the prayers the Imam informed the Muslims of what had happened the previous night. Among other things he told them that many old Muslim men and women were arrested and were still being held by the police. They deliberated on the matter and decided that their immediate attention should be on bailing out those who were taken into police custody. It was decided that all those who had their Identity Cards with them should together go to the police station to apply on bail the release of their fellow Muslims who were apprehended the day before. This discussion was public and the police were fully aware of what was decided. When Muslims came out of the mosque and started going to the police station as agreed upon, they were without any warning attacked by the police and many more were arrested, thrown into police vans and driven away. Confusion ensued. A large contingent of policemen from the Field Force Unit was brought in. They immediately and indiscriminately started beating up people around the Mwembechai area and throwing teargas bombs in the streets. And as this was going on more and more people were being arrested. The brutality of the police provoked the anger of the people, including non-Muslims. They started throwing stones to the police. The police responded by opening fire on the people. And as we have already pointed out above, the commanders specifically ordered the policemen to shoot and kill.[/SIZE]
Ahsante kwa kuweka mambo sawa.
Ubarikiwe.
Jasusi swali la msingi kabisa hilo. Humu kuna michango inayoonyesha chuki za wazi kwa Hayati mwalimu Nyerere na kutaka kumdhalilisha kuwa Ustaarabu na ujanja alikuja kuufahamia kwa wazee wa Kariakoo jambo ambalo si kweli.Hivi, kule Scotland na baridi yote ile Nyerere alikuwa akivaa kaptura tu mpaka alipofika Dar?
Lakini wewe una nini na wazee wangu wewe?
Ati "ataokota."
Jasusi swali la msingi kabisa hilo. Humu kuna michango inayoonyesha chuki za wazi kwa Hayati mwalimu Nyerere na kutaka kumdhalilisha kuwa Ustaarabu na ujanja alikuja kuufahamia kwa wazee wa Kariakoo jambo ambalo si kweli.
Hata hivyo,kama alivyosema Mag3 hapo juu bado Nyerere atabaki ndani ya 5 bora ya viongozi mashuhuri na wazalendo kupata kutokea barani Afrika. Hilo hata watu waandike vitabu vyao hawawezi kulifuta kwa sasa.
Inaonekana basi wazee wako walikuwa na heshima ya kweli na mapenzi kwa Nyerere kuliko nyinyi watoto wao. Lakini kama wazee wako ndio hawa wazee wa Kitanganyika ambao walipendana kweli na udugu wa kweli na ndugu zao Wakristu; hawa ambao hawakutaka kumdhuru Nyerere - sababu ya Ukatoliki wake - akikaa katikati yao; hawa wazee ambao walikuwa tayari kwenda kulinda Kanisa ili Nyerere asali pale na wakienda naye kwenye kufanya dua na matambiko; hawa wazee hawa huko waliko lazima wakushangae unayoyasema dhidi ya Nyerere na kumdunisha mbele ya Waislamu watu ambao Nyerere aliwapenda, walimpenda, alisimama nao na yeye akasimama nao hadi mauti. Hii faraka uliyoianzisha wewe wala haina sifa wa kujitamba. Unapaswa ufikirie mara mbili unavyotumia majina ya wazee wetu hawa kuwagawanya Watanzania na kuchochea fitna kati yetu bila kuchoka.
Leo maskini wa Mungu unafurahia unaposikia vijana wa Kiislamu - pasi ya kujua - wanamlaani Nyerere, leo mzee unafurahia kusikia Nyerere anaitwa Dhalim ukiamini unafanya jema? Leo Nyerere anatukanwa na kubezwa kwa sababu ya histohisia ya maandishi yako na unasimama kutumia jina la wazee kuhalalisha?
Lahaula! Mzee Said mrudi Mungu, mwingi wa rehema, mwenye kusamehe madhambi yetu na mwenye kutujalia neema ndogo ndogo na neema kubwa kubwa! Atakupa nafasi usaidia kuliponya taifa lako ambalo kwa kutumia mikuki yako ya maeneno umelijeruhi na sasa damu inamwagika huku ukiwafurahia marafiki zako ambao wametangaza kutaka kuwaua ndugu zao Wakristu pasi ya sababu yoyote ile. Mwenyeewe unajiaminisha kuwa unafanya hivyo kwa jina la Dini..
Mzee Said mwombe toba Mnyezi Mungu!!
Katika mihadhara yako hujawahi kusahihisha hili au hata kuonekana kulikemea... na hivyo kwa mtu ambaye anazungumzia heshima kwa wazee wake inaonekana ni kukubaliana nalo... hasa unapoleta stori za Mtu mzima kwenda sokoni bila senti hata moja mfukoni akitumaini kuokota njiani...
MM,
Matatizo yalianza baada ya uhuru kupatikana.
Nimeeleza kwa kirefu yote katika kitabu changu.
Mpaka inaingia 1980s TANU inaandika historia
yake hawa wazee wangu wakafutwa kabisa.
Tusijirudie tutawachosha wasikilizaji.
Insha Alla watafika 100,000.
Ndugu yangu ni ngumu sana kutafuta wapi umweke Mohamed Said.Unatakiwa kumfahamu kabla ya kumchukulia dhamana.Bukyanagandi;5816766]Ndugu Mohamed Said is not some monster; sijui kwa nini baadhi ya wana JF wanamuogopa kupindukia - yeye kaandika kitabu chake baada ya kufanya utafiti kwa madhumuni ya kurekebisha pale palipo pinda, sasa kama baadhi ya wasomaji wanaona kuna vitu ambavyo havijafafanuliwa vizuri, cha kufanya ni kumuomba atoe maelezo ya ziada au wenye kujua mengine ya ziada wamshauri arekebishe vipengere ambavyo vimekaa ndio sivyo alafu msikilizeni anatesema nini
Mkuu, Malumbano haya yanatija sana kwasababu moja kubwa. Kuzuia upotoshaji kwa vizazi vijavyo, kuzuia maafa yatokanayo na upotoshaji na kuzuia ongezeko la wapotoshaji duniani.lakini tujikita katika malumbano ambayo hayana tija yoyote au kumsema vibaya, actually ninacho ona mimi ni as if kuna ushindani wa aina fulani vile - kama dunia inakubali kihistoria kwamba Wamerikani ndio walikuwa wa kwanza kutua mwezeni, sasa tatizo liko wapi!! Hata mimi zamani nilikuwa na mawazo kama hayo hayo kwamba ukombozi wa Taifa letu dhidi ya Waingereza alianzia mwaka 1954 na akina Paul Bomani, Rashid Kawawa, Titi Mohamed, Kambona na Nyerere nk - hiyo ndiyo historia tulikuwa tunaisikia tukiwa shule ya msingi!! Nilikuja kushtuliwa kutoka usingizini baada ya kukutana na mzungu mmoja (Mwingereza) nikiwa nje masomoni, ikabidi nifanya kazi ya ziada kuelewa ni kitu gani hasa kilikuwa kinajiri wakati wa ukoloni wa Waingereza ndani ya Tanganyika, hicho ndio kilinifanya kidogo nitofautiane na nyinyi katika misimamo yenu.
Ndugu yangu kupitia JF na mnakasha huu Mohamed has been brought to his knee by admitting mistakes, accepting facts and most important he has purge and expunge some of his rhetoric and toxic materials.Hili la bwana Jericko kusema kwamba ndugu Mohamed Saidi ana uwezo wa kunilisha ngano za masika (hapa sijui unamanisha nini!! Najua kiswahili changu kiko a bit rusty lakini hapo nimetoka kapa)! Mkuu Jericko naweza kuelewa your concern katika hilo, lakini nataka kukuhakikishia kwamba ndugu Moh hana uwezo wa kulisha watu mambo ambayo hawayataki kuyasikia - lakini ukiona wasomaji zaidi ya 8K wamepitia uzi huu so far ujue kuna jambo, kumbuka wengi wao wanasoma tu bila ya ku-comment chochote!
Kwanza tumshukuru sana mzee wako kwa uzalendo wake wa kulitumikia taifa hili hata pale alipoweka maisha ya watoto wake kama wewe on the line.Mkuu labda nikufahimishe kwamba najua mambo mengi kuhusu Taifa letu, kwa kulezwa na baba yangu mzazi ambaye aliwahi kuwa Mwalimu pale Tabora mmoja wa wanafunzi wake alikuwa ni Baba wa Taifa, Mh.Kambarage alipokwenda masomoni Makerere mzee wangu alihamishiwa Sekondary ya Bwiru Mwanza - hapo alikutana na mwalimu mwenzake ambaye alikuwa sijuhi ndugu au mjomba wa Kambarage sikumbuki vizuri (lakini nafikili Andrew anaweza kuwa na kumbukumbu kama aliwahi kuzungumza na baba yake kuhusu huyo mwalimu jamaa yao) sasa Kambarage alipokuwa anakuja likizo kutoka Uganda alikuwa na kawaida ya kupitia Bwiru kwa jamaa/ndugu yake huyo kumtembelea na kukutana na mzee wangu kwa mara nyingine, baadae mzee wangu alibadirisha kazi na kuajiliwa katika mambo ya Public Relations na Serikali ya Kingereza na akawa na access kubwa ya Public Addressing Systems na vifaa vingine, kwa hiyo Kambarage alipokuwa anatembelea mikoani akifika kwetu mzee wangu alikuwa anampatia Nyerere system hizo kutangazia wananchi kinyume cha matakwa ya mwajiri wake i.e Wakoloni hivyo hakujali kupoteza ajira yake pindi Waingereza wangepata tetesi kwamba anamsaidia Kambarage, hivyo mzee wangu alikuwa anamfahamu vizuri Kambarage.
Nikushukuru kwa kutambua kuwa kuna ya ukweli na ya uongo.Sasa mzungu wa watu alikuwa na maslahi gani katika kunieleza ukweli huo; kwa nini hatutaki kukubali kwamba mambo mengi aliyo andika ndugu Moh yana ukweli ndani yake - ndugu zangu kwani tukikubali tutapoteza nini? Turekebisha pale penye mapungufu au palipo sahaulika bila ya kujali kama mleta marekebisho ni mwislaam, mkristo au mpagani.
Ndugu yangu ni ngumu sana kutafuta wapi umweke Mohamed Said.Unatakiwa kumfahamu kabla ya kumchukulia dhamana.
Hakika kama humuopopi MS kuna tatizo. Huyu ni mtu anayeweza kusimama na kuhadithia kuwa maziwa ya ng'ombe yanatoka katika mafenesi na si ngombe hundreds times.
FYI Mohamed is a master mind behind the turmoil seen recently.
He is a gifted story teller with incendiary power.
Ni kwasababu ulizosema tumekuwa na MS mara kadhaa tukitaka kurekebisha pale palipopinda. MS hakubali hilo kwasababu ya madai kuwa anatoa mada Ulaya. Kila tukimtaka ataoe maelezo ya ziada ima anshindwa au anapindisha ukweli na wakati mwingine anakimbia kama si kutoka nje ya swali, hoja au mada.
Hivi ninavyokuambia kuna hoja na maswali lukuki aliyoshindwa kuyajibu, kuyatetea au kutolea maelezo japo kwa fikra. Silaha kubwa ya majaliano aliyo nayo ni kuandika sana na kualikwa ulaya.Mtamwambia nini ninyi wamatumbi!
Badala ya kuwashambulia wanaotaka record ziwe straight ungemshauri MS asimame kidete kutetea hoja zake kwa mantiki. Nadhani umesoma na kuona contradictions nyingi kwa MS mwenyewe na ya mwisho ni hiyo niliyoweka akakana maneno yake achilia mbali wale anaowasemea kumkana bila yeye kujielewaMkuu, Malumbano haya yanatija sana kwasababu moja kubwa. Kuzuia upotoshaji kwa vizazi vijavyo, kuzuia maafa yatokanayo na upotoshaji na kuzuia ongezeko la wapotoshaji duniani.
Niseme kwa nafsi yangu ambayo nina hakika wengi ndipo wanaposimamia. Alichokiandika Mohamed ni historia ya matukio ambayo yalikuwepo. Kleist Syke alikuwepo, Abdul Sykes alikuwepo n.k. Hakuna anayekataa uwepo wa baadhi ya matukio hayo kwasababu historia haiumbwi inajiumba.
Lakini basi hivi tukubali tu kuwa Rais wa kwanza wa AA ni K.Sykes alimyemkabidhi mtoto wake A.Sykes TAA halafu TANU! Kupitia malumbano haya wengi wamejua huo ni uongo, uzushi na uzandiki mzuri tu.
Kwa mfano huo mmoja katika ya mamia unataka tukae chini na kumeza tu! Please tuonee huruma nduguzo.
Akili zetu tutazitumia wapi na lini!!Ndugu yangu kupitia JF na mnakasha huu Mohamed has been brought to his knee by admitting mistakes, accepting facts and most important he has purge and expunge some of his rhetoric and toxic materials.
FYI hii si mara ya kwanza kuwa na mnakasha na MS na kila mara wasomaji wameongezeka. Maana yake si kuwa wanamsoma MS, wapo waliomsoma na sasa wanatazama upya kurasa walizosoma.
Wapo wenye maswali ambayo kupitia mjadala wanapata ufahamu wa sehemu ya pili.
Muhimu sana ajenda, nia na dhamira ya Mohamed sasa vipo wazi kuliko wakati mwingine wowote.
Ngano ni masimulizi matamu ya kusadikika yanayotumia mazingira na yasiyoweza kuthibitika, kuthibitishwa, kutetewa au kujitetea zaidi ya ujumbe wake kumfanya msikiliza ayafurahie.Kwanza tumshukuru sana mzee wako kwa uzalendo wake wa kulitumikia taifa hili hata pale alipoweka maisha ya watoto wake kama wewe on the line.
Huyu ni one too many katika wale tunawaowaongelea na kuwatetea.
Hakika kupitia yeye na wenzake sote tupo huru tena kama taifa.
Maelezo haya yanatusadia kututetea pale tunaposema harakati za uhuru zilizagaa nchi nzima na si Tandamti, Kidogo chekundu au Narung'ombe kama MS anavyouaminisha ulimwengu.
Lakini pia unatutetea ya kuwa wazalendo kama baba yako hawakufanya hayo kama wakristo,waislam au Wanyamwezi.
Hapa ndipo tunapoachana sana na MS kwa kutaka kuibadili hsitoria, kufifisha heshima za watu na kukweza watu bila sababu.
Baba yako alifanya hayo kwa faida yako wewe na sisi sote bila kujali kabila, dini, Umanyema au Unubi.
Ndivyo malefu ya watu walivyofanya kote nchini.Ni tusi kubwa kwa watu kama baba yako pale tunaposikia kuwa kama si wazulu, wamanyema na wanubi tusingepata uhuru.
Baba yako hajaeleza fadhila zake kwa Nyerere, yeye amebaki kuwa rafiki wa Nyerere.
Leo tunaambiwa Nyerere alikwenda sokoni bila kujua kuwa anapaswa kuwa na fedha na wewe unataka tuamini tu kwasababu imeandikwa.
Tunachosem ni kuwa wazalendo wapewe heshima zao kama Watanganyika na si kwasbabu ni Wazulu, Wamanyema au Wanubi. Wazalendo waheshimiwe kwa mchango wao na si kwa imani zao kama ilivyokusudiwa kutugawa kutoka kwa MS.
Na yaandikwe ya kweli si kuficha baadhi, kusingizia, kuzua au kuweka maneno midomoni mwa marehem kwasababu tu hawawezi kujitetea.
Sijui kama baba yako au wewe mnadai nafasi pekee katika taifa hili kwasababu tu mzee ali risk kutoa vifaa vya sauti.
Sijui kama mna madai ya kwanini ninyi hamjapewa uwaziri n.k. kwasababu tu ya historia.
Na wala sijui kuwa mnaonewa na kudhulumiwa kwasababu ya historia ya mzee wako.
Kama sivyo, kwanini MS atake hayo yatokee? Kwamba yeye anapaswa kuwa waziri kwasababu babu yake aliongoza mgomo wa bandari!Nikushukuru kwa kutambua kuwa kuna ya ukweli na ya uongo.
Nadhani mimi na wengine hatuna tatizo na yale ya ukweli, tatizo letu lipo katika yale ya uongo.
Tupo hapa kurekebisha yale yenye mapungufu, but we don't have the right partner.
Sisi tunasimamia ukweli, MS anasimamia agenda yake so we don't have the common ground.
May be it's time you reach MS and convince him to join us regardless of our social differences for the betterment of this nation.Please let him understand that bigotry, hatred, incendiary comments, fallacy and the likes are contrary to Islamic teaching, they're inhumane and ''toxic asset'' we can pass on to next generation.
Huo mstari wa mwisho niliokazia, hapo ndipo MS asipokubaliana nawe.
Agenda yake ni kudhalilisha jamii nyingine na kuleta mifarakano, vipi akubali marekebisho yatokayo huko.
Ameandika kitabu ku-attack wakristo sasa atakubali vipi maoni ya watu wenye imani tofauti na yeye.
Nimalizie kwa kusema tatizo ni MS si wale wanaotaka kuweka record straight!
Unaambiwa marehem Miriam Makeba hakuwa anatumia hiyo bange yako.Wewe si upo Marekani siku ukija Tanzania beba begi la bangi uone airport watakufanyaje. Hapo ndiyo kwenye upuuzi hata kama huna ujumbe gani kama unatumia madawa ya kulevya kazi bure.
Vijana wengi wamepotea kwa sababu ya bangi kwako wewe bangi siyo tatizo.
Wewe mbona utajakusikia ukimkemea mwenzako Mag3 ambaye mnashirikiana humu kupambana na Mohamed Said amesema ni matusi makubwa kuwataja Abdalwahid Sykes na Mshume Kiyate.
Kwako wewe unaona kawaida sababu wametajwa wazee wa Kiislam.
Hapa ndiyo jamaa ya Kiislam inapowaona nyie ni maadui wao wakubwa.
Hampo wengi, upo wewe, Dullah, Zomba na Ritz!Wewe usiwe na shaka,wengi tunaosoma na kupima tumeyaelewa na Insha allah tutakuwa mabalozi wa kuwafikishia wengine walio mbali na wasio na uwezo wa kupatikana katika vyanzo kama hivi vya habari na elimu..
Waache waendelee kukejeli wewe endelea kutoa elimu na insha allah jazaa yako ni kubwa sana kwa mola..
Hampo wengi, upo wewe, Dullah, Zomba na Ritz!