Mohamed Said
JF-Expert Member
- Nov 2, 2008
- 21,967
- 32,074
Hizo ni sehemu ya ngano unazowapumbaza vijana wetu na kupandikiza chuki na uasi,
Kipi cha mafaa kwa tungo hizo? Manti ya kweli hazisimami sambamba na historia ya uhuru bali zinazaa tabaka puuzi ndani ya historia halisi ya uhuru.
Rejea ushauri wangu kwenye mchango wangu hapo juu, unamafaa kwako na kwa vizazi vyako bila kuwasahau maamuma uliowabeba katika mjadala wetu.
Mimi nimejifunza mengi kutokana na mjadala huu, mengi kutoka kwa wenzangu na mie wenye mlengo wa kati lakini hata mengine kutoka kwenu wenye mlengo kushoto na wenye msimamo mkali.
Simama kama mtanganyika/mtanzania, usisimame kama mpita njia, kumbuka na elewa fika kuwa,
"Mchuma janga hula na wakwao"
Yericko, Mag3,
Hamuwezi kupambana na mimi katika medani ya usomi kwa kuwa
nyinyi mna maneno mimi nina vitabu na papers.
Mimi nimeandika vitabu na mada nimewasilisha katika vyuo ndani
na nje ya nchi yetu.
Hapa JF hapatoshi andikeni mtambulike ndipo mtaweza kusema
kitu mkasikilizwa na dunia vinginevyo mtakuwa mnamwaga vumbi
bure.
Hamna kitu.
Aminini maneno yangu.
Kama hicho kitabu kweli mnaandika ni mwanzo mzuri.
Kwa hali hii mie nimeingia uvivu kujadiliana na nyinyi.
Tunajadili nini baada ya miaka 15 kitabu kinasomeshwa?
Itabakia mwimbo maarufu wa uchochezi, uchochezi,
uchochezi...