Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar

Ritz,

Hebu muuliza huyu ndugu yetu wapi nilipoandika
kuwa msako wa gazeti ulikuwa nyumba kwa nyumba?

Gazeti unalisaka nyumba kwa nyumba au unayanunua
kutoka kwa wauzaji?

Wameelemewa.

Umerudia hili mara nyingi na wapo watu wanaamini bila kuhoji; je ni nani aliyetoa agizo kuwa gazeti lichukuliwe kwa sababu ya makala yako? Waziri wa Habari alikuwa nani mwaka 1988?
 


Nimesema Kiwanuka ndiye aliyechoma moto!
Safi.
Nzuri.

Inachangamsha.
 
J
Na miaka 20 baadae nilipomwandika Abdu Sykes
1988 katika Africa Events (London) magazeti yote
yakakusanywa na kutiwa kibiriti.

Hili nishalieleza hapa JF.

Katika kusimulia kuna watu wanaitwa 'masters of hyperbole'; wewe ni mmoja wao. Sentensi zako au hoja zako zimejaa haste generalizations. Huna misamiati kama "baadhi, kiasi, kundi fulani" n.k. Kwako ni "Waislamu" ukimaanisa kikundi kimoja tu cha Waislamu ambao wako nje ya Bakwata n.k Sasa hapa umesema kwa makusudi tu kuwa "magazeti yote". Sasa unaposema "magazeti yote" manake ni kuwa hata ambayo watu walikuwa wameshanunua yalitafutwa yakanyang'anywa; yale ambayo yalikuwa library yakachukuliwa, yaliyokuwa majumbani au maofisini mwa watu nao yalichukuliwa. Unataka watu waamini kuwa kulikuwa na msako mkali wa gazeti hilo la AE kiasi kwamba magazeti 'yote' yalikusanywa na kutiwa kiberiti.

Lakini katika kujitetea ukasema yalikusanywa toka "News Stand" hukusema "news stands". Ukimaanisha kuwa muuza magazeti mmoja alinyanganywa. Na bahati mbaya hauna ushahidi wowote kuwa ni makala yako ndio ilisababisa gazeti hilo lichukuliwe. Ukiulizwa yalichomwa wapi moto (maana una uhakika yalichomwa moto) huwezi kujibu kwa sababu hakuna gazeti lilicohmwa moto maana tutakuuliza nani alichoma moto - usije kutuambia Nyerere alienda na kusimamia kuchoma moto makala yako!

Histohisia imekutawala hadi umesahau misingi ya uandisi wa historia!
 
Kiwanuka alikuita "mbilikimo?" Ngoja nicheke. Hivi kapotelea wapi jamaa huyu? Last time I met him alikuwa akisoma Syracuse.

Jasusi,

Amini usiamni.
Leo tu marafiki wakubwa.

Kiwanuka yuko University of Dar es Salaam ana hadhiri
pale (part time).

Vilevile anasomesha Centre for Foreign Relations.

Yalimkuta akajua kumbe Mohamed asemayo ni kweli.

Juzi tulikutana msikitini Ibadhi dhuhur.
Ndiyo utamu wa mambo haya.

If you are patient enough you will see the end of everything.
 

Nguruvi,

Nimekubali sina jibu!
Wapi nimeandika hivyo?

Unaweza kuonesha?
Au wewe hukubali majibu yangu?

Unataka unifunze mimi kuhusu discourse.
Unachekesha.

Hebu wewe weka hapa paper hata moja uloandika?
 
Ritz,

Hebu muuliza huyu ndugu yetu wapi nilipoandika
kuwa msako wa gazeti ulikuwa nyumba kwa nyumba?

Gazeti unalisaka nyumba kwa nyumba au unayanunua
kutoka kwa wauzaji?

Wameelemewa.

Mohamed Said,

Hayo maneno wala usiangaike nayo na maneno yao tu ya kujiliwaza na kujifariji lazima waweke ngano zao.

Wamechanganyikiwa kila mmoja anakuja na lake mwingine alikutisha kuwa sasa imefika wakati wa kumuumbua Mohamed Said alivyoona umeamua akabadili kauli yake analalamika unakesha JF.

Mwingine naye anajifariji eti amekuweka kwenye kona sijui kona gani.

Tofauti kubwa kati yako na wao wewe unakuja na maandishi ya historia wao wanakuja na maneno matupu.

Umelisoma tamko lingine la Maaskofu ngoja taleteta jamvini.
 
Aliyekuwa RAis mwaka 1988 ni Mzee Ally Hassan Mwinyi - Muislamu. Aliyekuwa Waziri wa Habari (ambaye angekuwa ndiye aliyetoa agizo la kuzuia gazeti hilo) unakumbuka alikuwa nani?

Mwaka 1988 Nyerere alikuwa hana cheo chochote?
 
Nguruvi,Nimekubali sina jibu!Wapi nimeandika hivyo?Unaweza kuonesha?Au wewe hukubali majibu yangu?Unataka unifunze mimi kuhusu discourse.Unachekesha.Hebu wewe weka hapa paper hata moja uloandika?
Kama ile ya takwimu za waislam vs Wakristo UDSM? Kama ile ya waliochaguliwa darasa la saba DSM!
Unaulizwa sali unajibu kwa swali, hapo kuna discourse knowledge kweli!
 
Kama ile ya takwimu za waislam vs Wakristo UDSM? Kama ile ya waliochaguliwa darasa la saba DSM!
Unaulizwa sali unajibu kwa swali, hapo kuna discourse knowledge kweli!

Nguruvi,

Huwezi kuwa hakimu na wakati huo huo mlalamikaji.
 

Ritz,

Kinshansa 1974.
Ali ulingoni na Foreman.

Daktari wa Ali Dk. Pacheco anamwambia Ali unasikia jamaa
wa Foreman wanamuhimiza akumalize duru ya tatu?

Ali akajibu akasema, ''Kuanzia hapo nitamchukua Foreman
kwenye nchi hajapata kufika. Mimi huyu nampiga.''

Dk. Pacheco akamwambia basi fanya haraka hili jambo lishe.

Ritz,

Mimi naujua uwezo wa hawa jamaa.

Wanachokijua ni kuuliza maswali ya ubabaishaji kwa kuwa
wamejaa hasira.
 

Ritz,

Kinshansa 1974.
Ali ulingoni na Foreman.

Daktari wa Ali Dk. Pacheco anamwambia Ali unasikia jamaa
wa Foreman wanamuhimiza akumalize duru ya tatu?

Ali akajibu akasema, ''Kuanzia hapo nitamchukua Foreman
kwenye nchi hajapata kufika. Mimi huyu nampiga.''

Dk. Pacheco akamwambia basi fanya haraka hili jambo lishe.

Ali akamwambia Dk. Pacheco, ''Usiwe na haraka nataka tujistareshe
kwanza.''

Ritz,

Mimi naujua uwezo wa hawa jamaa.
Nawapururia.

Wanachokijua ni kuuliza maswali ya ubabaishaji kwa kuwa wamejaa
hasira.

Mimi hawa wananistarehesha na kunisaidia kuepuka ''boredom.''
Haya yote niloandika hapa JF hakuna hata mmoja alikuwa anayajua.

Ni mambo mageni sana kwao na kwa hakika yamewastua khasa hili
la Abdu Sykes kuwa kichwa nyuma ya kuasisi TANU.

Wanashindwa kukitema chambo walicholishwa kwa miaka nenda rudi.
 
Katika raundi za mwanzo mashabiki wa Ali walionekana kuwa na fadhaa hasa ikizingatiwa kuwa wakati Ali anaingia ulingoni wengi walikuwa wakiimba ''Ali bumuyee, Ali Bumayee''

Mohamed hili la magazeti ya Africa Events umelileta wewe na si mara ya kwanza au ya pili. Kila mara umejinasibu kuwa magazeti yalichomwa moto kwa makala yako moja.

Nikakuambia kuwa wakati huo nilikuwa nasoma magazeti hayo ya Africa Events na Afirca Now na yalizuiliwa kwa nyakati fulani yote si kwasababu ya makala zako bali makala zilizoonekana kupinga usoshaliti na hasa kuichukulia Tanzania kama mfano. Wakati hayo yakiendelea magazeti kutoka nchi za mashariki yaliendelea kuingia.
Katika magazeti yaliyonisadia sana kuelewa siasa za Nigeria ni pamoja na hayo mawili kwasababu yalikuwa na ushabiki mkubwa sana wa siasa za Nigeria.

Tumekuuliza kuwa mwaka 1988 ndio mwaka yalipopigwa marufuku? Ukasema ndio. Ukweli ni kuwa magazeti hayo yalianza kuzuiliwa kuuzwa nchini kabla ya hapo.

Tukauliza tena nani aliyapiga marufuku, ukasema CCM kupitia Mayanja Kiwanuka.
Tukauliza CCM kama chama iliwezaje kupiga marufuku bila kuiagiza serikali ya CCM? Ukaleta kejeli na matusi.
Ndipo tukasema huna jibu na ukakubali nimeelekeza swali langu mahali pasipo husika ambako ni wewe.

Soma ile post ambayo nimeweka rekodi sawa utaona kuwa hakuna jibu la maana zaidi ya ngonjera na vituko vinavyoshabihiana na hivyo. Hata kwenye ngano ulishatoka.

Kwahiyo hatuna hasira, tunauonyesha ulimwengu kuwa Mohamed anaandika kwa kuficha ficha hisia zake ili auchanganye ulimwengu. Mwanakijiji kaonyesha vizuri sana katika ufafanuzi wa generalization yako.

Hadi ulipobanwa sehem muhimu leo ndio kwa mara ya kwanza umeandika ''yakaondolewa katika news stand'' tena si stands. Yawezekana yaliondolewa katika news stand ya Narung'ombe kwa kukosa wasomaji wewe ukadhani ni kwa makala yako vingnevyo yangekuwa yameondolewa katika stands.

Lengo lako lilikuwa kujenga mazingira ya kumtuhumu Nyerere ambaye ni marehemu lakini mwenyezi mungu ni wa haki kakunyooshea kidole! kama alivyokunyooshea kidole kwa kumsingizia marehem Kawawa.

Mo,hili la Africa events lifike mwisho kama la namba za mitihani, ni ushauri tu wa wewe kujisetiri.
 
Tatizo la Mohamed ni kuwa wakati anaandika tayari pembeni ana script ya kile alichokusudia.

Sasa wakati ukifika anachomeka matukio na wahusika ili vilingane na script ya ngano.
Hapo ndipo anaposahau kwenda maktaba kudurusu ukweli kwasababu ushabiki unakuwa umekolea sana.

Wewe miaka 15 hakuwahi kujiuliza hivi kawawa aliacha umakamu wa kwanza wa rais lini hadi alishe umma ngano kuwa alikuwa maulidini mwaka 1988 kama makam wa kwanza wa rais.

Hili la Africa Events linafuta mkondo huo huo .
Lakini ni mjuzi sana maana script ya pembeni ilikuwa imewalenga Nyerere na mfumokristo dhidi ya kitabu cha Mwislam na Waislam wahusika katika kitabu.

Tayari kwa miaka 15 amekuwa analaghai watu hadi leo anapokubali kuwa ''maswali yanaelekezwa pasipo husika'' na kukubali kuwa magazeti siyo yote yaliyochomwa ni news stand moja ya Tandamti.

Baada ya miaka 15 leo ameshindwa kusema nani alitoa amri na kwa nini.
Siyo kwamba kashindwa, baada ya jaribio la kumhusisha Nyerere na mfumokristo kudhibitiwa kwa hoja thabiti, pembuzi na yakinifu, Mohamed anajua kuwa aliyekuwa Rais ni mzee wake na waliohusika ikiwa ni hivyo ni wazee wake, sasa anabaki ku-generalize ni CCM.

Wanajamvi mkumbuke kuwa ni Mo huyu huyu anayesema CCM ilichoma magazeti kutokana na makala zake za historia ya Sykes ndiye huyu huyu ameeleza kuwa waislam walipita misikitini wakinong'onezana wachague CCM.

Kama unakula ngano bila tafakuri huwezi kuyaona haya maana Mo ni one of the best story teller of our times na anajua sana kuuchanganya umma. All in all hapa hatutamuonea wala kumhurumia facts tu ndizo zitaongea! no more no less.
 
Ndani ya CCM?

Ritz inabidi sasa tukusaidie wewe kufikiri vizuri ndugu yangu. Nyerere alikuwa Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi mwaka 1988 lakini Rais alikuwa ni Ali Hassan Mwinyi na serikali yake. Ukisoma hapa Mohammed Said anasema kuwa uamuzi wa kuondoa gazeti lililokuwa na makala yake ulifanywa na CCM (agizo la Mwenyekiti). Na anasema lilitekelezwa na mtu wa CCM - Kiwanuka na kuwa licha ya Kiwanuka kukusanya makala hizo na kuzichoma moto Kiwanuka huyo huyo aliandika makala kumjibu Mzee Said, sawa. Stori imenoga kwa wanaopenda stori; lakini kwa mtu ambaye chembe za Ubongo zinafanya kazi maswali kadhaa yako wazi:

a. CCM haijawai kuwa na mamlaka ya kuzuia kitabu au andiko bila serikali; yaani serkali inatekeleza mapendekezo ya chama. Kumbuka kuwa kama ilivyokuwa mwaka 1988 ndivyo ilivyo sasa; sheria ya magazeti ya mwaka 1976 ndiyo iliyokuwa ikitumika. MTu pekee ambaye anaruhusiwa kuondoa gazeti au kufungia gazeti ni Waziri wa Habari na mamlaka yake ni ya mwisho (hata mahakamani huwezi kupinga). Sasa, ni Wazirri gani aliyetoa agizo hilo?

b. Tukiachilia hilo la a tujiulize Kiwanuka alikuwa anatekeleza agizo la nani? Kama alikuwa anatekeleza agizo la Nyerere, itabidi ajieleze alipewa na Nyerere wapi? Kama alitekeleza matakwa yake kama afisa mahusiano wa chama je ni lazima Nyerere awe anajua au aliomba baraka? Mtu pekee wa kujibu hili ni Kiwanuka.

c. Lakini kama Kiwanuka alikuwa anatekeleza jambo lililokubaliwa na serikali basi mtu ambaye anapaswa kujua ni Rais Mwinyi ambaye alikuwa kwenye madaraka. JE Mwinyi alitoa agizo hilo? Mtu wa kujibu hili ni Mwinyi, umemsikia Mohammed kaenda kumuuliza?

d. Lakini cha kushangaza na sijui kama umekiona; Mohammed Said huyu huyu anatuambia toleo linalofuatia Kiwanuka aliandika makala kumjibu. Sasa, kama gazeti limepigwa marufuku Tanzania na hakuna wa kulisoma Kiwanuka alikuwa anamuandikia nani?
 

Ha haa haaa ha!!

Mohamed Said ilo lipo wazi kabisa uwezo wako na hawa jamaa hata wajikusanye mia mbili bado hawakuwezi.

Mara ya kwanza walikuwa wanakuita mchochezi kama kichwa cha huu uzi kilivyoandikikwa.

Wakaja na maneno mengine kuwa safari hii utajuta kuja JF.

Wakaja na maneno mengine Mohamed Said ni gaidi wakakutana na mipini ya haja.

Wakaja tena na maneno kuwa karibia utakimbia tumekuweka kwenye kona.

Wakaja tena na maneno wadanganye vijana wadogo lakini siyo sisi.

Wakaja tena na maneno ya matusi Mohamed Said mwehu, kichaa, muongo waheed, amechutama tupu zipo nje, akili zake za madrasa, mnywa gahawa, Sheikh ubwabwa, Ngano.

Sasa hivi wamekuja na style mpya ya maswali ya kitoto ambayo hayana tija yeyote na kuomba msaada kwa wafutialiaji wa huu mnakasha wamchukukie Mohamed Said, ha haa haa.

Hivi mwehu anaweza kuwa muongo mtu kama huyu anawakosesha usingizi.
 
Wala hakuna jazba solution wanatakiwa watoe serikali siyo mimi.

Wewe kweli hamnazo, serikali ni nani?? Sio mimi na wewe?? Kwani hata hao wabunge si wanachukua mawazo yetu na kuyapeleka bungeni?? Yani hata hili dogo namna hii unashindwa kupambanua na kuelewa nafasi yako kama mwananchi. Stop non sense kama huna solution ni bora ufunge mdomo wako maana watu wakikupendekezea solution bado utalalamika milele.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…