Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar

Last edited by a moderator:
Ndugu yangu huu ni uwanja mpana wa fikra kila mwenye chochote kuhusu historia ya Tanganyika anakimwaga jamvini watu tunajifunza.

Kama na wewe una vitu vya historia ya Tanganyika ruksa utupe darsa hakuna mashindano humu watu tunajifunza.
Tujifunze kwa kukubali yale tuliokosea kuyarekebisha au hata kukiri tu kwamba wakati flani tulikosea. Tuweke DINI zetu kando.

Dini hazikutusaidia kurudisha UHURU wa NCHI hii. Dini hazikutusaidia kuunda AA, TAA, TANU au CCM.

Dini zimetugawa. Dini zimetufarakanisha. Dini zimetutenganisha.

Wanaohusisha HISTORIA ya TANU au ya NCHI hii na dini zao ni wa kuogopwa kama ukoma. Hawatufai. Hawatatufaa. Tuwapuuze. Tuwatenge. Hatua na sheria kali ziwaaandame hadi kwenye makaburi yao.
 

WildCard,

Naomba unipe darsa kidogo sisi wengine tunajifunza kutoka kwenu.

Ni mara ngapi Nyerere alitaka kupinduliwa?
 
Last edited by a moderator:
WildCard,

Naomba unipe darsa kidogo sisi wengine tunajifunza kutoka kwenu.

Ni mara ngapi Nyerere alitaka kupinduliwa?
Mimi nakumbuka mara tatu. 1964, 1969(?) na 1982. Hakutaka kupinduliwa yeye, serikali yake ndio iliyotaka kupinduliwa. Tena waliotaka kuipindua serikali yake mara zote tatu wengi wao walikuwa WAKRISTO wenzake!
 
Mimi nakumbuka mara tatu. 1964, 1969(?) na 1982. Hakutaka kupinduliwa yeye, serikali yake ndio iliyotaka kupinduliwa. Tena waliotaka kuipindua serikali yake mara zote tatu wengi wao walikuwa WAKRISTO wenzake!

Naomba unitajie majina ya hao watu waliotaka kumpindua Nyerere kwenye ivyo vipindi vitatu. Ni kweli mahakama ziliwakuta na hatia.
 
Mimi nakumbuka mara tatu. 1964, 1969(?) na 1982. Hakutaka kupinduliwa yeye, serikali yake ndio iliyotaka kupinduliwa. Tena waliotaka kuipindua serikali yake mara zote tatu wengi wao walikuwa WAKRISTO wenzake!

Wildcard naomba unisaidie kidogo, 1964 lile lilikuwa jaribio la mapinduzi au ni maasi ya wanajeshi? Maana kama ingekuwa ni jaribio la mapinduzi hakukuwa na kipingamizi hasa baada ya Rais kuondoka Ikulu. Mie fikra kwa fikra zangu nilidhani maasi yale yalikuwa askari kupigania maslahi yao dhidi ya viongozi wao ambao wengi walikuwa bado ni Waingereza.
Hayo mengine ni majaribio hasa ya mapinduzi.
 
Naomba unitajie majina ya hao watu waliotaka kumpindua Nyerere kwenye ivyo vipindi vitatu. Ni kweli mahakama ziliwakuta na hatia.
Majina yote siwezi kuyakumbuka. Mwaka 1964 yalikuwa ni maasi ya kikosi kizima pale Colito, sasa Lugalo. Kiongozi wa maasi yale hakupata kujitokeza wazi. Jaribio lile likazimwa.

Mwaka 1969(72?) walikuwemo ndugu wa OK akina Michael Kamaliza, Colonel William Makori Chacha, Bibi Titi Mohamed,...

Mwaka 1982 walikuwa ni vijana wasomi jeshini akina Capt Roberts, Lt Maganga, Zacharia Hans Pope,..., wakiongozwa na tapeli mmoja wa Kihaya, Uncle Tom Lugangira, ndugu yake Cardinal Rugambwa!
 
Mohamed Said,

..mimi nadhani watu wanaona una "ill motives" pale unapojaribu kumdunisha Nyerere huku ukitumbukiza mambo ya udini-udini.

..zaidi unaposhindwa at least kuji-disassociate na kauli za watu kama Ustaadh Ilunga Kapungu, ndivyo unavyozidisha suspicions hizo.

..hivi umesikiliza ile video ya Ustaadh Ilunga? Umeridhika na jinsi anavyowaelimisha vijana wa Kiislamu kwamba kitendo cha Mwamwindi kumuua mkuu wa mkuu wa mkoa ni cha kishujaa? Hivi matendo yale ya kuweka maiti ktk buti la gari halafu kwenda polisi na kuwaambia, "nimewaletea "----" wenu," ni mambo ya kuelezwa kwa MAWAIDHA YA SWALA yoyote ile???

cc: Pasco, Nguruvi3, Ritz
 
Last edited by a moderator:

Wild Card,

Hakika unayosema ni kweli.

Hakuna anaeweza kusema haya yangu mimi ndiyo yenyewe hakuna mwengine.
Huo hautakuwa usomi.

Hilo neno ''vikabrasha'' umelisema kwa hamaki na ninaweza kuelewa ghadhabu
zako.

Huo wote ni ubinadamu.

Lakini ''Sykes Papers '' si ''vikabrasha.''

Hakika ni nyaraka muhimu sana ambazo John Illife wa Chuo Kikuu Cha Cambridge
kazitumia sana katika kuijua historia ya Tanganyika.

Mimi ni katika watafiti wachache ambao wamepata bahati ya kuzipitia na nimezisifia
kwa kuandika maneno haya:


[TABLE="class: MsoNormalTable"]
[TR]
[TD] ''These records were kept in a safe which I was informed remained untouched for over thirty years. Going through the files I was amazed by Ally Sykes' obsession with record keeping.

Every piece of paper with information was kept, however trifling it may have seemed during the struggle - a 1954 pencil note from Zuberi Mtemvu to Ally Sykes, informing him of a discussion he had with Nyerere about him and TANU; a 1953 money order receipt from Ally Sykes to Japhet Kirilo during the Meru Land Case; an undated copy of the letter from the TAA to Queen Elizabeth signed by the entire executive (the President, Julius Nyerere, Vice-President Abdulwahid Sykes, General Secretary Dome Okochi, Assistant Secretary Dossa Aziz, Treasurer John Rupia, Assistant Treasurer Ally Sykes) congratulating Her Majesty on her coronation; a 1952 letter from Rashid Mfaume Kawawa from Bukoba to Ally Sykes informing him of the political situation in the Lake Region; a 1963 letter from Lady Judith Listowel; letters from Kenneth Kaunda, Julius Nyerere, Kasella Bantu, Thomas Marealle ... the list is endless.

This habit was apparently inherited from his father who used to file each and every piece of paper which had any information worth noting.

[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="width: 752"] It is a pity that I could not get access to Abdulwahid's diaries, which I understand had many entries in shorthand and are untranscribed.

I was also not able to obtain World War I memoir of Kleist Sykes.

There is no doubt whatsoever that these documents are invaluable.

It is my hope that one day these important documents on the history of the Party and of our nation will find their way to the Tanzania National Archives for the benefit of future generations."

[/TD]
[/TR]
[/TABLE]

Wild Card,

Nimekuwekea bold ili uzinduke na ujiondoe kwenye hamaki zisizo na sababu uone kwa macho
yako mwenyewe hivyo ''vikabrasha'' vya Sykes vimehifadhi habari za watu gani katika historia
ya Tanganyika.

Lakini hii si hoja.

Ikiwa wewe au wa mfano wa wewe ana zaidi ya yale niliyoyaona mimi katika ''vikabrasha'' vile
uwanja huu hapa na atuwekee nasi tutasoma.

Sasa turudi kwa Nyerere.
Nyerere alitaka kuandika historia ya TANU lakini vilivyokwamisha hamu yake ni hivyo ''vikabrasha.''

Aliyoyasoma katika historia ile iliyokuwa ikiandikwa pale New Street na Abdu Sykes na Wilbert Kleruu
hayakumpendeza.

Historia ya mwamko wa Waafrika ilianza na African Association 1929 na katibu muasisi akiwa Kleist
Sykes baba yake Abdu.

Kwa taarifa yako Nyerere kaandika maisha yake kabla ya kufa.
Tusimame hapa lau kama unataka zaidi utasema nami Insha Allah nitakueleza yale niyajuayo.
 

WildCard,

Nashukuru tuendelee na darsa hawa wa 1969 alikuwemo Kambona ambaye alihukumiwa bila kuwepo mahakamani na wengine Bibi Titi Mohamed, Michael Kamaliza, Gray Mattaka, Eliya Chipaka, Prisca Chiombolo, hawa walikataa rufaa wakashinda kesi. Vipi walilipwa fidia na serikali?
 
Mkuu Remote, hilo mbona lipo wazi na ndio mkakati wa mahubibiri ya chuki na fitina yanayoenezwa na hawa viumbe wawili!
 
Mkuu Ritz mapinduzi ya mwaka 1982 washiriki ni

(1) Lt Eugene Maganga kama sikosei huyu kashatangulia mbele ya haki.

(2) Seleman Kamando

(3) Zakaria jina la pili nimelisahau unajua muda mrefu umepita

(4) Vitalis Mapunda

(5) Mbogoro

(6) Kajaji Badru

(7) Hatty MacGhee (jina halisi Hatibu Hassan Ghandi) Huyu alikuwa ni Pilot

(8) Capt Christopher Kadego

(9) Mohamed Tamimu aliuwawa katika harakati za kukamatwa

(10) Rugangira huyu alikuwa ni mfadhili wa mapinduzi.



Naomba unitajie majina ya hao watu waliotaka kumpindua Nyerere kwenye ivyo vipindi vitatu. Ni kweli mahakama ziliwakuta na hatia.
 
Last edited by a moderator:

Joka Kuu,
Hilo la dini ndiyo maisha yangu.

Hayo ya Sheikh Ilunga na Kleruu kwa hakika mimi naingiaje humo?
Mimi ninayoandika si nyote mnayajua?

Hayo hayatoshi hadi nizungumze hata yale yalosemwa na wengine?
 
Mkuu Jokakuu, ukiisikiliza ile video ilivyoandaliwa hakika ni seansational tupu. Ilipoongelewa mauaji ya Dr Kleruu utasikia sauti ''akampiga risasi.. ghruuuuuuuuu!'' kuonyesha kilichotokea kwa sauti za risasi. Hakuna uhakiki kuwa sauti za risasi zilirindima kwa namna video inavyoonyesha, kilichofanyika ni kuongeza hamasa na ''ushujaa wa mwamwindi''. Kwa kiongozi wa dini video ile asingeihusisha na mhadhara wake hata kidogo.
Hata kama Dr Kleruu alikosea(assumption) je Ilunga anataka kusema ile ndio njia sahihi waislam wanatakiwa kuifuata?

Labda nikukumbushe kuwa katika maelezo ya kuundwa kwa UTP, Mohamed ameorodhesha majina ya watu waliopelekewa barua za kujiunga ambao wengi ni wazee wake. Hilo halina tatizo!

Mstari wa mwisho akasema ''Nyerere hakupelekewa barua''. Maana yake ni kujenga mazingira ya kumweka Nyerere katika hatia ya ima hakupelekewa kwasababu alikuwa tayari ana uhusiano na kiongozi wa UTP au hakuwa muhimu sana kupelekewa barua kama Abdul Sykes.
Katika watu wote kwanini Mohamed amem ''single out'' Nyerere peke yake na wala si Dr Kyaruzi au Mwingine!
Jibu ni rahisi, Nyerere ni target na jitihada zote ni kumdunisha ili kuwapandisha wengine.

Hapo nyuma kuna post Mohamed kasema ''Nyerere alipewa uongozi na Sykes''. Tunafahamu kuwa kulikuwa na uchaguzi na Nyerere alimshinda Sykes, sasa alipewa uongozi kwa maana ipi?

Mimi nadhani role ya kila mmoja inasimama yenyewe bila kumdhalilisha mtu mwingine.
Uzuri wa historia ya kweli ni kujidhihiri na haihitaji nakshi au utuli.

Pamoja na dunia na vyombo vya habari wakiwemo waandishi na wasomi kuandika kwa nguvu zote mabaya ya Idd Amin na Hitler bado historia inawatetea kwa kila walillofanya kwa nchi zao baya au zuri.
Historia inawatetea na si mtu kwasababu historia inasimama yenyewe haiumbwi au kunyumbuliwa.
 
Ritz,

..ikiwa ni hivyo basi mkono wa dola ulikuwa haichagui dini ya mtu.

..kinachoshangaza hapa ni Mohamed Said kuleta mambo yake ya udini, akidai ni waumini wa dini moja tu waliokuwa wakishughulikiwa na dola.

..mimi sina uhakika kama kuna watu waliowekwa kizuizini kwa muda mrefu kama Balozi Christopher Kassanga Tumbo. lakini u would rarely hear Mohamed Said akimtetea huyu, anatetea wa dini yake tu.
 
Last edited by a moderator:

Rapheri,

Si kweli kuwa sitaki kuona michango ya Mwanakijiji.
Nimeacha kumjibu kwa kuwa kanitukana.

Hii ndiyo hulka yangu.
Kwa kuwa sina ujuzi wa matusi mtu akishanitusi namkwepa.

Labda wewe hunijui.
Mimi nausudu sana majadiliano ya heshima.
 

Kumbe huna hoja kaa pembeni na tutapiga kelele hadi ubalozi huo uondolewe !!!!
 
Reactions: Ami

Mkuu Ngongo,

Maganga kweli ni marehemu sasa mwaka 2004 alijiunga na Chadema na mwaka 2005 aligombea ubunge Tabora Mjini kupitia Chadema.

Kuna mmoja kati hawa ana biashara zake pale Mbezi.
 
Last edited by a moderator:
Nguruvi, Nitakuwekea hapa ile barua ya Ivor Bayldon ili usome nimesema nini katika kitabu changu. Kuandika yale mlokuwa hamyajui si kudhalilisha mtu. Naelewa mnatabika na historia hii kwa kuwa hamkutegemea kuwa kulikuwa na historia nyingine. Wewe si wa kwanza kupata mshtuko kwa yale ulosoma kutoka kwangu. Wengi tu wamekipenda kitabu changu kwa ajili ya kuleta yaliyokuwa hayajulikani. Ingekuwa naandika maneno ya kudhalilisha kitabu kisingepita. Kingeishia kwenye fikra zangu.
 
Joka Kuu,
Hilo la dini ndiyo maisha yangu.

Hayo ya Sheikh Ilunga na Kleruu kwa hakika mimi naingiaje humo?
Mimi ninayoandika si nyote mnayajua?

Hayo hayatoshi hadi nizungumze hata yale yalosemwa na wengine?
Mohamed Said,

..huu mnakasha ni endelevu, na ndiyo maana umefika kurasa 500+ na maelfu ya wasomaji.

..zaidi umeandika mambo muhimu sana kiasi kwamba inawalazimu wasomaji wako wakujue wewe mwandishi ni mtu wa aina gani.

..sasa katika hili zoezi la kutaka kukujua mwandishi wetu, kukujua zaidi ya jina lako, ndiyo unaona yanaibuka maswali mengine kama hii hoja ya video ya Ustaadh Ilunga.

..Kuna mahali umesema unamheshimu Ustaadh Ilunga, na kwamba ktk "darsa" lake huwezi kufungua kinywa chako. Sasa ndiyo na sisi tukauliza: hivi Ustaadh Ilunga anapomsherehesha Mwamwindi na mambo aliyomfanyia Kleruu, wewe una mtizamo gani? Je, akitoa "darsa" hilo bado utapiga goti ukiwa kimya hata kuguna ushindwe???

cc: Nguruvi3, Ritz
 
Last edited by a moderator:
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…