Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar


Haina shida mzee wangu naweka pembeni hilo neno!
 
Deleted! duplication.

Nyambala,

Hakika kuna mambo kutoa ushahidi wa mfano wa ushahidi wa mahakama
haiwezekani.

Historia ya Kawawa haifanani na historia ya Sokoine.

Lakini muhimu ni kuwa sikutaki mimi uamini niandikayo ikiwa wewe akili
yako inakataa kuwa nisemayo si kweli.

Mimi ninaandika yale ninayoyajua kwa ushahidi niliokuwanao na kwa jinsi
ninavyochambua mambo.

Kwa ajili hii si lazima tukakubaliana katika fikra.
 



I rest my case.

Kilichobaki nisikilize EGYPTIAN MUSICAL CLUB....''yatima''

Wimbi...

Nimecheka peke yangu.

Umembandika Mr. Tibbs.

Wakati niko St. Joseph's Convent shati langu la shule niiliandika ''Sidney Poitier.''
Wakati umepaa...

Sasa bahati mbaya sina picha ya Abbas Mzee ningekuwekea uwapate vyema Egyptian.
Ingekwenda vyema na ''Yatima''

Vipi ''Fitina Mbaya.''
 

Mzee Mwanakijiji,

Kwenye tamko la Maaskofu wanasema Kanisa Tanzania limo katika kipindi kigumu cha mateso ya kimfumo (systematic persecution)

Tupe "definition" ili tusonge mbele na huu mnakasha.
 
Ami,
Ahsante ndugu yangu kwa kutuanikia mfumokristo.

Wangazija wana msemo maiti hafi ila kwa mzishi wake.

Tumesubiri hadi mzishi ulipowasili na sanda na vyote
vinavyomuhusu maiti.

Kazi kwake aliyekuwa anamkomalia Mohamed Said atoe
"definition."
Mzee Said, toka mtoni usioge na watoto watakutia matope! Katika maelezo ya huyo bwana kuna kitu kweli umeelewa wewe ukiwa muasisi wa neno hilo. Siku zote neno likiwa lina utata hutolewa tafsiri kulingana na mazingira. Wewe kama mtafiti huwezi kuacha umma utafute maana ya neno na kisha useme hiyo ndiyo tafsiri.
In short, Mohamed Said huna definition ya neno mfumokristo. Kama ''mwandishi na mtafiti'' this is too low.
 
Mnyambala hapo nyuma alisema mzee atazungusha zungusha na kuibuka na kitu kingine kuua hoja zinazomkwaza.

Nguruvi,
Nikumbushe kwa hisani yako Warioba ni kipi tusichokubaliana au nilichokosea.
 
Mzee Mwanakijiji,

Kwenye tamko la Maaskofu wanasema Kanisa Tanzania limo katika kipindi kigumu cha mateso ya kimfumo (systematic persecution)

Tupe "definition" ili tusonge mbele na huu mnakasha.

unaniuliza mimi definition kwani ndiyo niliyoyasema; na neno 'systematic persecution' nina uhakika ukitumia muda vizuri wa kugoogle utaona maana yake. Ni neno la kawaida tu la Kiingereza wala halilingani na "Mfumo Kristu".
 
Mohamed hajaeleza John Garang (Alumni wa UDSM) alipokelewa vipi uwanja wa ndege.
Anasema Garang alipewa heshima zote zinazomstahiki mkuu wa nchi. Mohamed sijui amepata wapi hili kwasababu chuo kikuu kina taratibu zake za kupokea wageni wa madaraja tofauti.
Chuo kikuu hakina hakitoi mapokezi ya kitaifa isipokuwa mapokezi yanayolingana na protocol za chuo.

Mohamed anapaswa awaeleze wasomaji 117K je, mapokezi ya John Garang yanatokana na ukristo wake yanawezaje kufananishwa na serikali kuunga Mkono PLO na POLISARIO?
Ni zaidi au ni pungufu! Hii ni kwa mujibu wa Mohamed na kwavile haku-balance habari yake kwa kuhoji watu wa chuo kwanini walifanya anavyosema bado inabaki kuwa ni maoni yake wala si maoni ya waislam.

Hii inatumbusha pale aliposema 10% ya waislam hawakupewa nafasi ya kuuliza jambo.
Kwanza hatujui 10% ameitoa wapi kwasababu kwa mujibu wa maandishi yake waislam ni 20%.
Je, 10% ni wale waliohudhuria mkutano wa Garang au ni jumla ambayo imebadilika kutoka 20%.

Mohamed hakueleza utaratibu uliotumika kuwazuia waislam wasipewe nafasi ya kuuliza maswali.
Lakini kinachoshughulisha fikra za wanaotumia akili ni kuwa kwanini adhani waislam asifikiri wahindi,wapagani na wasioamini?

Huko nyuma Mohamed aliwahi kutuhumu chuo kikuu kwa kusema Lecturers wakristo walipiga marufuku kitabu chake kisitumiwe.
Tuliwahi kumuuliza kama alishawahi kuwasiliana na chuo kupata ufafanuzi, Hakuwa na jibu.
Tukamuuliza ana majina ya lecturers wanaopiga marukufu kitabu chake, hakuwa na jibu.

Sidhani hayo hapo juu atakuwa na jibu.
Kwavyovyote tunachosema hapa ni kuwa ngano hii imeundwa kujenga chuki kwa kutumia matukio halisi na watu wa kweli kwa kupotosha ukweli


 
Hapa umekuja mdoogo kabisa,sio kama zile mbwembwe zako za kawaida unapokuja na uzi mrefu wa kujaribu kujibu nukta baada ya nukta.
Mimi nabang kwenye meza kama Abdulrahman Mwalongo.Nakwabia Nguruvi Toka zako hapa huna JIBU!

Siku zote neno likiwa lina utata hutolewa tafsiri kulingana na mazingira.
Sisi tumetoa definition ya mfumo kristu kulingana na mazingira yetu.Sasa unataka nini tena.?
 

Nguruvi,
Kadri utakavyojenga maswali na kutaka ushahidi...

Nilichotaka wasikilizaji wakijue ni nini kilitokea katika
ziara ya Garang.

Kwangu mimi hilo ndiyo muhimu.
Hayo mengine kwangu si muhimu.

Unataka nikupe majina ya walimu wanaokataza kukifanyia
rejea kitabu cha Abdu Sykes...

Unataka nikupe majina ya maafisa wa Wizara ya Elimu
walokipiga marufuku kitabu changu "Torch on Kilimanjaro."

Haya ndio tujaalie nikishakupa majina yao ndiyo utaniamini?

Mimi katika nafasi yangu katika vita hii kuna mambo hayanishughulishi
hata punje.

Mimi kinachonishughulisha ni kama hivi natoa darsa watu wanasoma na
elimu inapatikana.

Kwangu haya ndiyo muhimu na ndiyo husisitiza kuwa naepuka ubishi kwa
kuwa kwangu mie ubishi hauna tija.

Nadhani umeona hakuna lililoingia jamvini ambalo mie sijaliandikia pp.
Basi hiyo ukutoshe...
 
Usitoke nje ya mada.Suali ilikuwa Ukristu na uislamu ni dini ipi iliyoitangulia mwenzake?.
Kuhusu Yesu (A.S) ni kuwa alikuwa muislamu.
Umeamua kunijibu hivyo ni muhimu usikimbie kwa kisingizio chochote kile.
 
Nguruvi,
Kadri utakavyojenga maswali na kutaka ushahidi...Nilichotaka wasikilizaji wakijue ni nini kiliyokea katika
ziara ya Garang.Kwangu mimi hilo ndiyo muhimu.Hayo mengine kwangu si muhimu.
Muhimu ni kuwaonyesha wasomaji wapi wamepotoshwa.Huwezi kuandika habari za John Garang akiwa UDSM ukaacha kusema huyo ni alumni.
Hapa ulificha kitu ili kuteka akili za watu! Kwa maneno mengine unaelezea mtu usiyejua background yake.
Unamfaham John kama mkristo tu, mengine si muhimu.

Huwezi kutoa madai mazito ya waislam kunyimwa nafasi ukiwa huna proof ya utaratibu uliotumika.
Huwezi kutupa takwimu nyingine(10%) tukameza tena kama zile walizomeza wananchi kwa miaka 15, tukae kimya.

Huwezi kutuambia unaeleza kile tusichokijua na ni ukweli wakati tukijua kuna upotoshaji.

Hayo ambayo si muhimu ni yale usio na majibu nayo, kwa wasomaji ni muhimu.
 

Ami,
Serikali tumewaeleza tatizo la mfumokristo.

Sheikh Ilunga katembea nchi nzima kuwaeleza Waislam
kuhusu mfumokristo.

Kipi kitushughulishe kwa Nguruvi?
 

Nguruvi,
Hapana neno.

Tusibaki hapa hapa tuendelee na mnakasha.
Ila jisemee nafsi yako.

Unaetatanishwa ni maandishi yangu ni wewe na
wengine watatu au wanne.

Wengi wanaelewa.
Angalia uwanja unavyofurika.

Hawaji kusoma maswali kwani maswali siku zote
huwa kitu cha mwisho.

Wanakuja kusikiliza darsa langu.
 
Nukuu hii ndugu yangu ingemfaa sana Mwalimu wenu humu; ni yeye aliyeandika historia akichanganya ukweli, uongo, porojo na hisia zake na kuziita "ukweli"! Ni kipi nilichokisema mimi ambacho si cha kweli? NONE.
Kitu ulichosema ambacho si kweli ni hiki
Nyerere mwenyewe hakujuwa udugunization bali alichagua watu kwa imani zao.Angalia uongo wako hapa

 
Sokoine alifanya kazi na Nyerere kama waziri wake.
Kama sijakosea alikuwa waziri wa ulinzi wakati wa vita.

Sifa moja ya Sokoine ni kuwa mtu ambaye aliweza kusimama na kumwambia Nyerere hiki ndiyo hiki hapana.
Alikuwa ni mzalendo na mchapakazi asiyejilimbikizia mali. Kwa ufupi alikuwa ni mwanafunzi aliyefuzu kutoka kwa Nyerere.

Suala la kwenda kusoma na kurudi hilo mbona ni la kawaida.
Katika vinyang'anyiro vilivyopita baada ya CCM kuweka masharti ya elimu tumeona viongozi wengi wakijiunga OUT kupata elimu zitakazokidhi haja ya aspiration zao.Wengine walitoka Zanzibar na tunawafahamu kwa majina.

Nyerere kumuandaa Sokoine ni suala la maono yake na hapo sijui kwanini Nyerere awe christian Lobby.
Nyerere alifanya kazi na kawawa katika nyadhifa mbali mbali.
Hata wakati anamteua kuwa katibu mkuu sote tulishuhudia akimwelezea Kawawa kwa hisia kali.

Hili lilitokana na ukweli kuwa wajumbe wengi wakati huo waliona Kawawa kama mtu mwenye elimu dhaifu.
Nyerere alisimama naye kidete na sijui kwanini Christian lobby waliliachia hili
.Sokoine did not obtain his masters degree as he was killed in a freak road accident in 1984 while travelling from Dodoma to Dar es Salaam.
Nyerere shed tears openly for all and sundry to see. His succession plan had crumbled.
Na hadi leo Sokoine anabaki kuwa kiongozi maarufu katika historia ya nchi yetu. Wengi walimlilia sana hadharani na hadi sasa wanamkumbuka. Kwa mtu aliyefanya kazi kwa ukaribu na Nyerere katika nyakati ngumu sana sioni kwanini Nyerere akililia hadharani ionekane kama jambo linalohusu wadhaifa na wala si urafiki na ubinadamu.
Nyerere had to look for another candidate to groom fast to succeed him.
If he had a choice he could have by pass Salim Ahmed Salim but the political scenario as at was at that time, there was no way he could have passed Salim.
Salim Ahmed yupo leo na ingewezekana angetupa ushahidi.
Kupanda ngazi kwa Salim ni Nyerere ali m-groom. Hii ilikuwa kuanzia alipoteuliwa kuwa balozi Misri, China n.k
Halikuwa jambo rahisi Nyerere kumteua mtu baki ili awe balozi China kwa kuzingatia mahausiano yake na Mao Tse tung na Chuo Lai.

Nyerere alisimama kidete Salim awe katibu mkuu wa Umoja wa mataifa achilia mbali Rais wa Tanzania.
Hata iliposhindikana,bado mwalimu alimrejesha nyumbani na kumpa nyadhifa mbali mbali.
Nyadhifa zote alizopewa zililenga katika kumjenga hadi alipokuwa katibu mkuu wa OAU.

katika mpambano wa mwisho alioingia katika Urais, watu waliomuangusha ni wajumbe wa NEC kutoka Zanzibar waliombambikia tuhuma mbali mbali. Hadi leo bado anakubalika miongoni mwa Watanzania wote bila kujali mfumo.

Na aliyemvuruga ziaidi ni JK na timu ya mtandao.
Hili hutalisema utalisema la Nyerere. Kwa maneno mengine unakubali kuwa Salim alikuwa na uwezo. Sasa kipi kibaya kama Nyerere aliona mtu mwenye uwezo zaidi ya Mwinyi.
What's wrong with that. Na hapa alikuwa ana deal na waislam sijui christian lobby ilikuwaje.


 
Ami,
Serikali tumewaeleza tatizo la mfumokristo.

Sheikh Ilunga katembea nchi nzima kuwaeleza Waislam
kuhusu mfumokristo.

Kipi kitushughulishe kwa Nguruvi?
Angalia hapo Nguruvi anaanza kuja na habari tofauti badala kukiri kuwa definition ya mfumo kristo ndiyo yenyewe na yeye kaikubali na kushindwa kuijibu.
Yuko wapi Gwalihenzi aje na mkokoteni wake abebe watu wake awatoe nje ya ulingo?.
 
Wanakuja kusoma hoja.
Wanasoma kuwa Warioba alikuwa na credential na wao walijua hivyo.
Aliyekuwa hajui kuwa Warioba alikuwa waziri wa sheria kabla ya uteuzi na mwinyi ni wewe peke yao.

Haya wanayaona kama walivyoona lile la Kawawa kuwa makamu wa Rais mwaka 1988, Marmo kuwa mbunge wa Monduli, Nyerere kuja Dar mwaka 1950, na msomi wa master kubeba hotuba ya bila kuisoma hadi New York. n.k.

Kinachowavuta sana ni pale wanapotambua kuwa takwimu zako ni za kupika na wala hazifuati kanuni achilia mbali weledi wa somo la stats. Wameona jinsi miaka takribani 15 walivyolishwa feki, kwamba mto takwimu hawezi kuzielezea!

Wanakuja kusoma na kushangaa iweje muasisi wa mfumokristo hajui maana yake ni nini.
Na wengine wanashangaa imekuwaje mzee wa US na EU anababaika

Mohamed, kukuuliza maswali ni njia ya majadiliano ambayo kwa mtu anayekimbia hoja kama wewe inamvuta kwenye kona halafu inamwacha kama alivyozaliwa. Hili unalijua.Ulitegemea watu wakae kitako wakisema hewala! wrong palce.

Mtu mwenye ufahamu na kitu anapokuuliza sikwamba hajui ni kwamba anajua na anataka kujua ima unajua kiasi gani au unasimamia wapi. Kama hujui utauliza nini?

Lakini pia hao wasomaji wanaona jinsi hoja zako zinavyobomolewa kama nyumba ya barafu na ndicho kinawashtua.
Wengine hawakujua kuwa hii ni tamthilia mwanana katika umbile la ngano.

Hao watatu wanne wasiokuelewa unaosema ni wale wasiokuelewa ni wale usiowapenda kwasababu wananyong'onyeza hoja zako na kutibua mission yako ya kuasambaza chuki, fitna ,farki kwa mgongo wa dini. No! dini haisemi hivyo.

Kuna hoja nzito zinakusubiri hebu tuwape hao wasomaji raha, zirejee

Mnyambala nadhani atakuwa mtabiri!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…