Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar

Kipande cha hotuba ya Kikwete...
Lazima mzee wetu Mohamed Said atakuwa anaswali kwenye hiyo misikiti.
 
Nguruvi3
Suruali inakupwaya hiyo ndugu yangu,hebu pandisha juu kidogo,hawa jamaa zako wanaokupigia makofi eti ya kwamba una ubavu wa kupambana na Mohamed Said hawakutakii mema,wanakudhalilisha tuh,

Ubavu wa kukunja ngumi na Moh Said wewe huna,historia hii ishaandikwa na wenye kujisimamia wenyewe kifikra wameuona uhalisia..

Pole sana jamaa yangu..
 
Last edited by a moderator:
Imekuaje mkawa maskini wakati mlielimika? au nanyi mlipitia madrasa na kuishia kunywa gahwa na kashata vibarazani!
kweli huna uwezo wa kufikiri! pole sana kijana. Achana na hilo zee lako chimvi labda utaweza kufikiri kwa kujitemea!
 
Wanaelezwa historia yenye heshima kubwa na iliyofichwa wao hawataki kubali na mwishowe wameishia kukejeli na kukosoa bila mashiko,

Ni khiyari yao kuamini au kutoamin,kukubali ama kutokubali,,

Watu wenye hekima zao wanasema ukimuona mtoto kabebwa mgongoni na ubebeo yeye ananyoosha miguu ujue hataki tena masuala ya kubebwa hata umweleze jambo gani,,

Hakuna wa kuwalazimisha ila tunaamini upande wa pili wa shillingi umefahamika..
 
Bahati nzuri nimebahatika kukisoma hiki kitabu cha ndugu yangu Mohammed Said the life and times of Abdulwahid, Uamuzi wa Busara na vitabu kadhaa vya brother Said i suggest watu wasome sio tu kumuattack. wengi wanajua tu kumuatack na inaonesha dhahiri hawajasoma kitabu chake..
brother Said ameandika kisomi bila kumuatack mtu yoyote wala dini bali amonyesha kwa kiasi kikubwa jinsi gani njia mbalimbali zilitumika kudidimiza wengine.
mnaomuattack brother Said someni kitabu cha padri J.Silvanus kanisa katoliki na siasa za tanzania 1954-1985 utagundua kuwa brother Said yeye ni miongoni tu mwa waliojitolea kusema kweli kosa lake kubwa kawasemea kweli waislamu, ukisoma kitabu cha Silvanus utanielewa kwa nini nimesema kosa la brother Said.
ifike kipind tukubali madhifu ambayo yamewahi tokea na kujitahidi kujenga a better tomorrow,
aliyoandika brother said ni sehemu tu kwa yatakayo andikwa huko mbele na tukumbuke kitabu kama maisha na nyakati za Abdulwaheed ni cha mwaka 1997 sidhani kama Marehemu aliweza au alipata muda wa kukubali au kukanusha yaliyomo ktk kitabu hicho.
Tukumbuke tu maneno haya yalipata kusemwa na Wole Soyinka
"TISHIO KUBWA KWA UHURU NI UKOSEFU WA UKOSOAJI.VITABU NA MAANDISHI NI TISHIO KWA WALE WOTE WANAOTAKA KUUFICHA NA KUUZIKA UKWELI"
 

Kama watu wengine hawakupata nafasi ya kutetea vitabu ni bahati mbaya sana tu. Ila maadam yuko hai huyu bwana atafanya vema kukitetea kitabu chake hapa.
 
Ritz,

Naomba msaada wako, mpaka mtu kuitwa sheikh anapitia vigezo gani? Na sababu kubwa nimemsikia mzee mo said akimuita sheikh, Bilal waikela na huyu yuko hai je? Ni sheikh kweli? Au? tafadhali naomba mwongozo wako. Na usheikh unapatikanaje?
 
Nenda Chadema kaangalie wabunge wa viti maalum kama ukukuta Wakirsto watupu.

Kuna wabunge wa 3 kutoka zanzibar na wengine wengi tu waislam we ni muongo na ni mnafiki sana unachuki sana na cdm, kwa taalifa yako hakuna chama kilichochanganya viongozi wake wa juu kama cdm.
 
habari? yako Bwana ADOYA najalibu kupitia mjadala wenu na mohamed nimzuri kwa lengo la kujenga lakini maswali ya wasomali ni kumtoa nje ya mada.
hivi una jua kwamba 1992 wamarekani waliburuzwa kwenye mitaa ya mogadishu hakukua na matatizo haya unayo yaona pale hila kwa sababu mataifa ya maghalibi khasa AMERICA hile somalia ni HORN of AFRICA ukikamata ni nzuri kwa military base ndio kwa maana yamewafika haya unayoyaona HATA SISI KAMA TUTAKATAA MASILAI FURANI YA AMERICA BASI YATATUFIKA YA WASOMALI,,

Tangu mwaka 1992 wasomalia walianza kupata mazila america walitumia kila hila pamoja ya kupandikiza makundi ya kigaidi ndani ya somalia.mpaka serikali ya somalia hikapinduliwa na wanaoitwa wa babe wavita ambao wanafadhiliwa na AMERICA.wakitumia sera za mabeberu wote ya divide and rule. makundi mbali mbali ya kaanzishwa chini ya koooo mbalimbali za kisomali zenye uchu ya utawala.na wengine wakijalibu kuhikomboa somalia kutoka kwenye mzozo au vita hiyo iliyo leta wasomalia wengi Tanzania nA SEHEMU NYINGINE DUNIANI.


1997..mwaka huu wasomali waliochoshwa na vita na mapingano Viongozi wakimira,wakoo na kidini wakaona nibora kukaa chini na kuangalia kwanini wauane wao kwa wao ? wakapata jibu ni kule kungawanyika kwao nini kitawarudisha pamoja? wakapata jibu ni dini yao kumbuka somalia 100% waislam. wakakubaliana wote wawechini ya kaulimbiu ya umoja wa kiislamu,ndipo hikaanzishwa mahakama ya kislam..

1999-mpaka kufikia mwaka huu hakukua na shida kwa mahakama zakislamu kuwaludisha wasomalia katika umoja wao kwani kundi moja tu ndio lililokataa kujiunga na mahkama za kislamu nalo ni wababe wa kivita.linalofadhiliwa na America vita hikawa ni vibaraka wa America ambao ni THE LORD of War na wa somalia chini ya uongozi wa mahakama za kiislam Wakati huu eneo dogo tu ndio lilokua navita ambalo wababewakivita walikua wana tawala.

2000-mahakama za kiislamu hili chukua eneo lote la somalia na somalia hikawa chini ya utawala wa kiislamu na wasomali wote wakawa kitu kimoja taifa moja na wale wilokuanje wakimbizi wakaanza kurudi somaria Historia INAONENESHA hakuna kipindi ambacho wasomalia waliludi somalia na wageni kwenda somalia kama kipindi hiki cha 1999- 2001.

2001-RAIS wa AMERICA wakati huo GEORGE BUSH akatangaza kuamba kona ya AFRICA inakaliwa na Magaidi na wao hawapati usingizi kwa sababu magaidi wana shikilia sehemu furani duniani vikaanza vikwazo somalia. vikifwatia na vita kali baina ya wasomalia na VIBARAKA WENGINE ETHOPIA...kwa masilahi ya marekani droon zikatumika

2003-ETHOPIA wanaingia somalia wakisaidiwa na America wasomali wanapambana na wavamizi kwako wewe ni kosa hilo
ajabu kweli hii kutete Taifa lako nikosa???

2004 somalia haikaliki tena mahakama za kiislamu zina angushwa na baazi ya viongozi wao wanakamatwa baadhi yao wana kubali matakwa ya AMERICA wanaachwa hai na waliobaki na msimamo wao wana uwawa.

2004-2005 AL-SHABAB tafsiri hisio rasmi(vijana shupavu) Inazaliwa baadhi ya viongozi vijana waliobaki wanabakia na msimamo usioteteleka zidi ya wavamizi wote walioingia somalia kwa masilahi ya marekani

2004-2005-Burundi ,Rwanda Uganda zinaingia Somalia kwa masilahi ya marekani

2010-Kenya inaingia kwa masilahi ya marekani

WASOMALI MATATIZO YAO NI KWA SABABU YA UZALENDO WAO.KWA NCHI YAO

MWISHO
 
Said, nadhani kuna mambo ambayo ima hujayaona, hayaelewi au yamefunikwa na ''mapenzi''
Wenyewe wanasema ukipenda chongo utaita kengengeza.
Hebu tuvunje vunje hii habari yako ili tuone wapi ambapo hatupo pamoja

Hapa unafanya makosa ya kuhisi bila ukweli.
Mimi nimesoma nakala za mwanzo kabisa za vitabu vyake kwa lugha zote. Najua na wengi pia walisoma.

Unakosea unaposema kumu-attack. Hakuna wa kumuattack Mohamed eti kwasababu yeye ni Mohamed na in fact hakuna hata mtu anayeattack vitabu vyake. Kinyume chake watu wanatumia akili zao kutathmini na kutafakuri kama kile wanachokiona au kukisoma ni sahihi.

Mohamed anaweka hoja zake, zile zenye utata ima zinafafanuliwa, zinawekwa sawa au anaulizwa atoe utata. Pengine ungesema watu wana attack hoja zake ningeweza kukubaliana nawe kwasababu katika fikra mtu anatakiwa afanye hivyo si kwa vitabu hata katika fikra zake mwenyewe.

Kwa msingi huo wewe umeandika ukiwa na dhana tayari kuwa anakuwa attacked.
Hapo hutatenda wema kwa wale walisoma na kuelewa na si kulewa vitabu vyake.

Lakini pia lazima utambue kuwa mtu anaye attack hoja ana strong background ya kufanya hivyo na hiyo ni kwa yule tu aliyesoma vitabu vyake akiwa na akili timamu.
brother Said ameandika kisomi bila kumuatack mtu yoyote wala dini bali amonyesha kwa kiasi kikubwa jinsi gani njia mbalimbali zilitumika kudidimiza wengine.
Hapa tayari umeshajiaminisha kuwa kile alichokisema ni sahihi.
Hakuna namna ya kukusaidia kuona vinginevyo ila kukutakia heri na fanaka.

Hizo njia alizoonyesha pengine utupe mfano mmoja tu unaodhani ameonyesha na kuwa ''attacked'' unfair.
Yeye mwenyewe ameshindwa kufanya hivyo pengine wewe unaweza kutusaidia.

Hatari inayokukabili ni kuangalia mambo kwa mapenzi na si kwa ukweli.
Ipo siku Mohamed atakuambia Rais wa kwanza wa Tanganyika alikuwa Oliver Tambo kabla hajahamia Africa kusini kuendeleza mapambano dhidi ya makaburu.

Kwavile utakuwa na hofu ya ku-attack hoja hiyo huku ukiwa na lundo la mahaba itabidi uamini hivyo. Atakayekuambia si kweli huyo attakuwa ame attack Vitabu vya bro Mohamed, ame attack imani yako ya uislam, ame attack mapenzi yako kwa vitabu vyake na ame attack fikra zilizofungwa na atahitajika kusoma tena vitabu vya Mohamed. Kama atakuwa hajakufur na kuwa kafir sijui atakuwa na bahati kiasi gani.

Wasomaji wajiulize, mathalan, Mohamed anaposema Warioba hakuwahi kujulikana nchini kabla ya uteuzi wake kuwa waziri mkuu, akatokea mtu na kuonyesha bila kificho kuwa alikuwa anajulikana na Mohamed akakubali sasa hapo tatizo lipo wapi? Kwamba kueleza usahihi ndio ku attack.

Mohamed, kaweka takwimu, wana JF wakazipitia na kumwambia zina tatizo.
Mohamed akakubali kuwa zina matatizo makubwa sasa hapo tatizo lipo wapi?

Mohamed kaonyesha Nyerere alivyokuwa na chuki na waislam, akapewa nafasi ya kueleza chuki, badala yake akamuelezea Nyerere kama mtu mkarimu sana kwa waislam, sasa hapo tatizo lipo wapi?

Mo kasema John Garang alikuwa mkristo, mtu mmoja kasema ni kweli lakini pia alikuwa mwanafunzi wa UDSM, hapo kuna tatizo lipi?

Mo, kaeleza AA iliundwa na K.Sykes, akatokea mtu na kusema ndiyo Sykes ni mmoja wa waanzilishi lakini mkutano wa kuanzisha chama ulifanyika nyumbani kwa Cecil Matola ambaye alikuwa Rais wa chama na Ramadhani Ali akiwa makamu, Sykes katibu, hivi hapo kuna tatizo gani?

Mo, kaandika kuhusu EAMWS akaulizwa, eh kama Nyerere aliiua je kule Mombasa ilipoanzia aliyeiua ni nani, alikuwa Kenyata au mtu gani? Hakujibu sasa kosa ni la nani yule atakaye ufafanuzi au yule asiyeweza kufafanua.

Orodha hiyo ni ndefu, sijui mwenzetu Said ulikuwa na ushauri gani!
Kwamba ilikuwa bora kukaa kimya tu na kuamini Kawawa alikuwa makamu wa Rais 1988, juzi juzi tu hata wewe ukiwa umeshazaliwa.Endapo hilo hukuona kama kosa, je yele yaliyoelezwa wakati baba yako hajazaliwa unadhani yana usahihi gani?

Na mwisho mbona Mohamed kaeleza kuhusu marehem bibi yake binti Mluguru na jinsi togwa lilivyotamu wakati wa jua hasa ukiangalia wachezaji wa Yanga wakiwa uwanjani au ukiwa unanyolewa na mwingereza pale chini ya ukwaju n.k. hakuna aliye ''mua attack'' Hivi Said, tukae kimya tukiambiwa Rais wa TANU alikuwa Abdul Sykes! real. Eti tukisema tuna attack si Mo tu bali imani nzima ya Uislam!!

Said tuonee huruma muungwana! Tukienda madukani inflation inatuliza, hospitali hakuna dawa, tukirudi nyumbani mgomo wa walimu, tukivuka bara bara dala dala zinanyemelea roho zetu, tukiingia JF Mo anatusubiri kutupiga kamba za ubongo, please tuone huruma Said Mago.
 
Said Mago, kwa kuwa hii ni posti yako ya kwanza kwenye huu mjadala, nitakuomba uzingatie mambo kadhaa kabla ya kukurupuka kwani yaonesha wazi kwamba huu mjadala umeudandia tu na hujaupitia toka mwanzo wake. Huyu Mohamed Said wengine tumeanza naye mbali sana na si hivyo tu tuko baadhi yetu hata umri tunamzidi kwa kiasi kikubwa tu. Yawezekana kwako anaonekana mzee wa busara lakini kwangu na naamini kwa Watanzania walio wengi Waislaam, Wakristo na wasio na dini, wakwe kwa waume, wazee kwa vijana, wa makabila yote zaidi ya mia moja hamsini, Mohamed Said ni zaidi ya mchochezi na mdini, ni mtu wa fitina.

Mohamed Said, akisaidiwa na Mwalimu wake kutoka Pakistani, Malik na vijana wachache wa wakati huo waliokubali kurubuniwa kirahisi kama Prof. Hamza Njozi, Dr. Ramadhani Dau na wengine kadhaa walikaa kitako na kutunga hadithi. Hiyo hadithi ilijengwa katika misingi ya uongo na ulaghai na iliweza kudumu tu kwa sababu walengwa wake hawakuwa tayari kuhoji uhalali na ukweli wake. Leo hii nuru inaanza kuchomoka, giza hiloo linapiga bye bye kwani toka lini giza na mwanga zikachangia sinia? Ukweli unapogonga hodi, uongo uko mashakani na salama yake ni kuaga mapema.

  • Mimi Mag3 niliwahi kumsihi sana Mohamed Said achutame ili huko baadaye atakapoathirika watoto wasishuhudie aibu yake.
  • Nguruvi3 aliwahi kumwonya asipende kuogelea mtoni pamoja na watoto kwani hataweza kutakata kutokana na maji kuchafuliwa.
  • Mwanakijiji alimtahadharisha kuhusu kuwawekea marehemu maneno mdomoni na badala yake ajitahidi kuwahoji wahusika wakingali hai.
  • jasusi alimkanya kutokuwanukuu vibaya waandishi kwani vitabu vipo na asipoangalia vitakuja kumuumbua kwani dunia ni ndogo.
  • Ngongo alimshangaa kwa nini anaangalia kila kitu kwa macho ya kidini na kumwomba ajaribu kuwa mkweli kwa nafsi yake.
  • Nyambala amemkemea tabia yake ya kutunga na kuleta madai ya uongo hapa jamvini lakini masikini wapi, kalewa porojo.
  • sweke, Pasco, Gwalihenzi na wengine, wameshauri, wametahadharisha, wameonya, lakini mmm!...
Kweli, tumejitahidi lakini kama kawaida na kwa upofu na chuki zilizomjaa rohoni hakutusikiliza na badala yake akaamua kuendelea kuoga mtoni na watoto. Ni kweli wako waliokubali awapake na wao uchafu nao wanaona fahari kufanana na yeye lakini nasema na kusisitiza, ni vipofu wachache. Nina hakika kuwa Watanzania kwa umoja wao uliojengeka kwa kipindi kirefu hawatakubali kurubuniwa kirahisi kama anavyodhani na badala yake iko siku atawekwa kitimoto na washiriki wake wote wajibu kwa nini walitaka kulivuruga taifa. Hakuna Mfumokristo...ni zimwi walilojiundia wenyewe ndani ya mioyo yao na sasa wakae kutafunwa nalo.

Mimi yaliyofanyika miaka ya 1940s mpaka tunapata uhuru niliyaishi na kuyashuhudia, sikusubiri kuhadithiwa na watu wenye donge rohoni. Nilipoingia Dar es Salaam kwa mara ya kwanza, Mohamed Said hata mlango wa shule alikuwa hajauona...nimekuta Sindbad Night Club, nimekuta Sombrero Night Club, nimekuta Banda beach, nimekuta Metropole Night Club, nimekupa Gateways Night Club, nimekuta Anatoglu Hall, nimekuta Afrika Hotel original ikitazamana na Lutheran Church kivukoni...maandamano ya kupinga National Service nilikuwapo, mkutano wa kuunga mkono Azimio la Arusha nilihudhuria, jamani wengine tumetoka mbali!

Said Mago, ni kweli umesoma hicho kitabu cha kivukoni? Sisi tumesoma vyote, vya mohamed Said na hicho, na ukweli ni kwamba wengi anaodai wamesahauliwa wametajwa ndani ya kitabu hicho. Kinachogomba ni Mohamed Said kujaribu kupotosha dhana kuwa ni Waislaam ndio waliopigania uhuru wa nchi hii, tena si Waislaam Watanganyika bali wakuja Wazulu, Wamanyema na Wanubi! Huku ni kuwadhalilisha wazee wetu...kumbuka hawa waliletwa Tanganyika na Mjerumani kama mamluki katika jeshi la Kijerumani kupigana dhidi ya Watanganyika. Kwanza Wazulu wenyewe mwanzoni hawakuwa Waislaam mpaka baada ya kuoleana na Wamanyema, je upo mpaka hapo?
 
Sijui kama ulipata nafasi ya kumsikiliza raisi Jakaya Kikwete kwenye hotuba yake ya mwisho wa mwezi March 2013, ametoa majibu kuhusu mfumo wako kristo kwamba ni uwongo tu! na kwamba miskiti mitatu ya dar mumemuombea dua yeye Jk afe!
Mfumokristo ni dhana ya kufikirika ambayo haipo, ila kundi fulani la MS na wafuasi wake wanasema lipo.

Huko nyuma aliko toka kabla ya kuuawa watumishi wa Mungu niliwahi muuliza MS, Hivi hao anawaita wazee wake walipigania uhuru wa Tanganyika kama waislam au Watanganyika, majibu niliyopewa yalikuwa ya kejeli kupita maelezo lkn sasas kadli siku zinavyosonga mbele. Naona kumbe hicho kitabu chake kinamakosa mengi sana ya kihistoria ambayo yanatakiwa yahaririwe kama atataka muhusika.

Hainiingia akilini yeye kuandika kuwa Sinde Warioba, eti alikuwa hajulikani, Hivi MS anataka kutuambia kuwa yeye alipokuwa anaandika hiyo historia alikuwa hajui kuwa Warioba tayari alishafikia kiwango cha jaji katika utumishi wa mahakama, si hilo tu anataka kutuambia kuwa wakati yeye anaandika alikuwa hajui kuwa Jaji Warioba aliwahi kuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali, hivi ni kweli MS alikuwa hajui kuwa Jaji Warioba aliwahi kuwa Waziri wa Sheria katika nchi hii.

Hebu MS naomba unisaidie wewe unaposema mtu huyu anajulikana katika ulingo wa siasa huwa unamaanisha mtu huyo awe ameshika nafasi zipi hasa kisiasa. Naomba majibu sio yale ya nimekusoma
 
Hongera sana bwana Mohamed kwa uchambuzi wako katika hili swala. Kila anapoingia kiongozi (Rais) muislamu hawa wakristo hawishi kumsakama kwa maneno ili aonekane kwa watanzania kuwa hafai, Angalia enzi za Al-hajj Mwinyi na sasa Dr kikwete, Hawaishi kutoa miongozo ya uchaguzi, kauli nzito nzito kwa kiongozi mkuu wa nchi. Mbona wkt wa Ben Mkapa hawakutoa muongozo wa uchaguzi, Wala kauli wanazotoa hivi sasa?! Wanatuchokoza na tumeambiwa (Waislamu) tusianze mpk tuchokozwe!!
 
Katika kile kinachoitwa madai ya waislam hasa kuhusu elimu, zipo tuhuma kuwa wanafunzi wakristo walichukuliwa kupelekwa maeneo yenye waislam na viwango vidogo vya ufaulu.
Hili linaonekana kuwa ni dhulma kwa kuliangalia kama linavyoletwa.

Kinachowashindwa watu kuelewa ni kuwa mfumo wa kugawa nafasi uliletwa makusudi ili angalau kuwepo na uwiano katika makundi na jamii tofauti ambazo zilionekana kuwa nyuma.
Huko nyuma mtihani wa taifa ulikuwa unaangalia kiwango cha ufaulu bila kuangalia mtu anatoka eneo gani.

Kuna nyakati ambapo mkoa mmoja au miwili iliweza kutoa wanafunzi wengi kwenda sekondari pengine kuliko mikoa 10 kwa pamoja. Ilionekana maeneo yasiokuwa na fursa yaliendelea kuwa nyuma. Hii ni pamoja na mikoa ya pwani.

Utaratibu wa nafasi kimikoa ulilenga kupeleka fursa kwa kila mkoa. Ndipo hata viwango vya ufaulu vikawekwa kutokana na ushindani. Mfano, mkoa uliamua kiwango cha ufaulu ili kutimiza namba waliopewa na elimu taifa.
Kama ni wanafunzi 300 basi hata aliyepata 30 lakini akawa ndani ya 300 alikwenda sekondari.

Kwa namna fulani ilionekana kama uonevu kwa baadhi ya mikoa.
Fikiria mkoa ambao kuna mwanafunzi alipata 60 na kuachwa lakini wapo wanafunzi waliopata 45 na kuendelea na masomo.Kwahiyo si kweli kuwa utaratibu huo ulilenga kuhujumu zaidi ya kusaidia.

Kilichotokea ni kuwa wanafunzi kutoka mikoa yenye ushindani walihamia kule kwenye viwango duni.
Hili halikufanywa na serikali bali mwamko wa watu katika jamii zilizoona mbali.
Hapa nadiriki kusema kwa mkoa kama Kilimanjaro, Bukoba na ile ya kanda ya ziwa hii waliifaya sana kuhamishia wanafunzi pwani.

Nimeona kwa macho yangu mkoa kama wa Tanga mwanafunzi akitolewa ili akaolewe na wa kiume kuacha shule kwa ajili ya biashara za kuangalia viunga vya minazi. Narudia nimeona kwa macho yangu na akili nikiwa mtu mzima.

Swali linakuja, kwanini basi mikoa ya pwani ilikuwa na viwango duni?
Je, tatizo ni wale wenye viwango vikubwa kuhamia huko au tatizo ni wenyeji kutothamini elimu na kuwa na viwango duni. Mimi nadhani hakuna anayepaswa kutete uzembe kuwa katika dunia ya sasa basi kila kitu kitakuja katika silver plate.

Nawapongeza wazazi walioona fursa hiyo na nawalaumu wale waliodhani ni vema kuishi na viwango duni.
Tatizo si wahamiaji, tatizo ni wenyeji ambao hawakuwa na mwamko.

Mfano, Kilwa shule imefungwa kwasababu hakuna wanafunzi. Kama shule hiyo ingekuwa na wanafunzi waliohamia 50 pengine isingefungwa na hao ndio wangepata fursa iliyopo na ambayo haitumiwi vema na wenyeji.

Si kweli kuwa wakristo walipeleka watoto huko, hili lilihusu kila mtu mwenye uelewa na mwamko bila kujali imani yake.
Hakuna mwislam aliyeiona fursa hiyo akaiachia eti kwasababu wale wenyeji ni waislam na hivyo walipaswa kuachiwa nafasi hizo. Kama ingekuwa ni rahisi hivyo basi tusingeona rushwa katika taasisi za kiislam katika mambo hayo hayo ya elimu.

Hao wanaosema huo ni mfumo wanasahau kuwa nafasi zinazotolewa na mashirika mbali mbali kwa waislam zimekuwa zintumiwa kwa njia ya ''know who'' na wala si vinginevyo.

Matokeo yake wamechaguliwa vijana walioishia katika biashara za unga huko Uturuki na kwingineko na wala hawajarudi kusaidi jamii zao.

Vipi leo ionekane dhulma wakati ndani ya taasisi za kiislam kuna dhulma na wanajamvi wanaoshahdidia hoja hii mfu wanajua kuwa hilo lipo na linatendeka?

Hoja hii ya nafasi kwa maeneo na wahamiaji kuchukua fursa ni mfu na wala haina mashiko.
Hoja imejengwa ili kuendelea kuwapumbaza watu badala ya kuwaeleza ukweli wa dunia ya leo ya ushindani.

Hakuna anayefanikiwa kwa kudhani jina lake ni sehemu ya Resume. Ni lazima watu waambiwe ukweli hata kama unauma
Ningeshauri taasisi na wasomi wa kiislam wazame katika chimbuko la tatizo na sikutafuta band aid.
 
Kuna mahali nimesoma kuhusu shule za serikali. Kama kawaida imejengwa hoja dhaifu sana na imegusa hata kule watu wasikojua kuwa wengine walishiriki kwa macho na akili zao.

Zimetajwa shule zilizojengwa kwa misaada ya serikali zikatajwa shule kama Ruvu, Kibiti na nyingine za miaka ya 70 kama ilivyosemwa.

Zimerushwa tuhuma kuwa asilimia 80 ya wanafunzi na wafanyakazi wa maeneo hayo ni wakristo.
Sijui asilimia hiyo ilipatikanje kwasababu kuu mbili.

Wafanyakazi wa kawaida wanapatikana kutoka katika eneo husika. Hawa ni kama wapishi madereva na wengine (auxilliary)
Wafanyakazi wa taaluma kama walimu wanapatikana kwa sifa za vyeti vyao.

Zimetajwa shule katika mpangilio ambao unazua maswali kuliko majibu.
Nadhani mwandishi wa habari hiyo hafahamu shule hizo zilijengwa kwa utaratibu gani na zilitumika vipi.

Nimpe kionjo kidogo. Shule za Ruvu, Kilosa, Ifakara na Kibiti zilijengwa kwa msaada kutoka Cuba.
Ukienda katika shule hizo kila kitu ni ''copy' ya kingine.
Shule hizi zilikuwa za mchepuo wa Kilimo.

Utaratibu wa kuchagua wanafunzi kuingia katika shule hizi uligawanywa kwa kanda.
Katika kanda hizo ninakumbuka shule ya Kibiti ilikuwa inachukua kanda ya mashariki(Dar es Salaam, Pwani, Lindi na Mtwara).

Kwa wale waliopitia Ruvu zama hizo nadhani watakuwa wanamkumbuka rafiki yangu Mjale na kule Ifakara Matimbwi.
Si kweli kuwa shule hizo zilichukua randomly, na hii ilifanywa makusudi kuhakikisha kuwa kila kanda inafaidika na msaada huo wa Cuba.Wazee waliokuwa wizara ya elimu na walioshiriki katika kuratibu haya waje hapa waniambie kama si kweli.

Sasa kama kuna kanda iliyokuwa imezembea wakaingia watu wengine, nani wa kulaumiwa?
Hivi kwanini umlaumu mtoto wa kiislam aliyesoma Ikizu akafaulu vizuri.

Kama mwanafunzi alitokea Mkuranga akaenda kusoma Peramiho na akafaulu, tatizo ni huyu aliyekwenda kule au wale wa kule waliozembea kutumia fursa!

Siku zote huwa nasema ni lazima wasomi watumie usomi wao kutafuta suluhu ya tatizo.
Ni jambo baya sana kutafuta suluhu kwa kutafuta visingizio. Tatizo liangaliwe kwa kina na wala si kwa ushabiki.

Mohamed alitoa mfano mzuri sana. Alisema sheikh Kassim alipokuja Dar alikuwa ''mshamba'' maana alishuka kwenye dau na hakujua anaelekea wapi hata baba yake kumfuata.

Alichokifanya ni kwenda kufundishwa ilm na baba yake kumkuta akiwa na maalim. Alipokuja Dar aliwakuta watu wa kariakoo wapo pale, yeye akatumia fursa hiyo na leo anamwandika kama mtu maarufu.

Huyu si alitumia fursa kutoka Bagamoyo! sasa kwanini alaumiwe yeye kuja kuchukua ilm wakati watu wa kariakoo walikuwa na fursa hiyo bila kupanda dau na hawakuitumia.

Vipi leo mwananchi aone Kilwa wanafunzi hawataki shule na yeye kuitumia fursa hiyo kwa watoto wake ionekane kama dhulma. Dhulma iko wapi? Kwanini mtu ajidhulum halafu aseme kadhulimiwa?

Narudia mfano huu kila siku, shule ya Hassan Mwinyi miaka miwili iliyopita ilikuwa na wanfunzi 250 na walim wawili.
Hapa nani anamdhulumu mwenzake! Hivi hapa si kujidhulumu kweli.

Kule mkuranga mwalimu Mkuu mmoja, akisafiri kiranja wake anakuwa makamu mkuu wa shule.
Haya ndiyo ameneo tunaambiwa walidhulumiwa kwa kuleta watoto kutoka nje. Haa! hapa kunadhulma gani jamani! nisaidieni wanajamvi.

Halafu mwl Mbwambo hasemwi kuwa ni shujaa! Walimu wangapi wa mkuranga wamekimbia maeneo hayo.
Nani anadhulumu hapa?

Kunakitu nadhani sikielewi kwasababu kila nikisoma hoja naona zingine kama gurudumu.
Hata nikijaribu kuzichongea miguu na mikono ya miti, hazisimami na wala hazina utetezi.Zinakosa mashiko.
 
Nimeona kwa macho yangu mkoa kama wa Tanga mwanafunzi akitolewa ili akaolewe na wa kiume kuacha shule kwa ajili ya biashara za kuangalia viunga vya minazi. Narudia nimeona kwa macho yangu na akili nikiwa mtu mzima..
Ukianza kuhojiwa kuhusu haya "matukio" utaanza kutoa mapovu na bado utataka tukuamini!

Kama umedanganya kwenye haya mangapi huko nyuma utakuwa umetudanganya?! hufai kujihusisha na Historia ya Tanzania umefeli!
 

Ni kweli mkuu hawa wapo kidini zaidi juu ya uislam na anachofanya muislam wao wanapinga hata kama kinaukweli
 
Hizi ni porojo za kwenye mihadhara ya mjinga mwenzenu Mohamed Said ambaye daima kila kitu anakiangalia kwa jicho la uislam! hizo ni fikra mfu na zinaendeshwa na watu wapuuzi kama wewe na hilo zee lako puuzi Mohamed. Mtu mwenye akili timamu ataiangalia serikali kama taasisina sio kama Kikwete. Na kwa ujinga wenu huo ndio maana mnaishia kushinda miskitini kuombea dua ati watu wafe! pumbavu zenu, mtakufa wenyewe kabla ya hao mnaowaombea wafe.
 

nani anamsakama kati ya wale wanaotokoa nyaraka za kishauri na wanaokaa kuomba duwa na kusoma itkafu ili MUMUUWE?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…