Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar

Sheikh Mohammed Said,Nalipatwa na "Duaa Al Mustaajaba" niliposikia at hata Mwai Kibaki nae kapewa jina la mtaa/barabara maarufu hapo Mzizima!? Hivi hiyo nchi ina wenyewe kweli!? Ama kwa hakika kuna mengi ndipo, Wazee wetu walinena; "kuwa uyaone"!
Haaa! hapa ndipo nasema matatizo ya waislam mara nyingi baadhi yao huyakuza bila sababu za msingi.

Tumesikia kuhusu taasisi za kiislam kufanyiwa hujuma. Tumeuliza je, WML !
Watu wamekimbia hawataki kabisa kuliongelea hilo kwasababu wanajua kulikuwa na uchafu nyuma yake.
Wanakimbia ukweli ili kutafuta mahali pa kunyooshea vidole.
Tumesikia wakitajwa akina Commonwelath, world church council n.k.
Hili la Wolrd Muslim linafunikwa funikwa kwasbabu linahusu uhalifu na uharmia ndani ya wanaonung'unika

Ni kwa mtazamo huo huo Gombesugu naye anapatwa na mshangao wa barabara kuitwa Kibaki.
Mwaka jana tukiwa na mnakasha na Mohamed, alisema barabara ya Mshume Kiyate imerudishwa baada ya waislam kulalamika.Akamtuhumu sana Nyerere kwa kufuta majina kama ya Kiyate na akina Bibi Titi Mohamed.

Leo Gombesugu naye anatafuta mahali pa kujishikiza kwasababu Nyerere keshafariki.

Hii barabara imejadiliwa na baraza la madiwani wa Kinondoni, Jiji na mkoa.
Aliyekuwepo katika kutoa hadhi hiyo ni pamoja na Rais Kikwete, Meya wa Jiji, Meya wa Mnaisapaa ya Kinondoni n.k.

Hatukuwahi kusikia mzee yoyote wa Dar es Salaam akisimama kupinga. Hatukuwahi kusikia taasisi yoyote ikisimama kohoji.Kwa maneno mengine wakazi wote wa Dar es Salaama akiwemo Mohamed Said walikubaliana na hili.

Ninachokifikiria hapa sijui nani atabeba lawama maana nikiangalia kwa haraka haraka hakuna mkono wa mfumo na Nyerere hayupo tena.Mtego zaidi ni kutambua kuwa mkazi wa pwani ndugu JK anayeijua historia ya Pwani ndiye aliyekabidhi.

Hili ni tatizo la wakazi wa Dar es Slaama kama basi ni tatizo!
Sasa hebu njooni na hadithi za kuunga unga ili tujue nani amefanya nini na kwanini.

Acheni mambo haya jamani, jamii ina matatizo mengi sana ya kushughulikia. Majungu na fitna havitasaidia kabisa.
Tatizo likiwa ndani ya nyumba yako unachukua hatua na si kusimama na kuangalia jirani kapika nini ili iwe sababu!

NB
***Mohamed, WML bado lina utata, tusipoliongelea basi itabidi tufute habari za EAMWS katika maandiko yetu** ha ha ha
 
JokaKuu na Wimana,
Nawasoma vema sana wakuu.
Inapofikia mahali watu wanakubali kuwa tatizo la elimu si dini bali mambo mengine basi tumepiga hatua kidogo.

Leo wale wale waliokuwa wanasema maeneo ya waislam yameonewa , wamekuja hapa na kutuonyesha maeneo ya wakristo yaliyoonewa pia. Hili ni jambo jema sana kwasababu ni mwanzo wa kufikiria tatizo hili kama tatizo la jamii na si la imani. Na siku zote nimekuwa naeleza hivyo kuwa ukishaangalia jambo kwa jicho la makengeza basi ni ngumu sana kuona kwingine.

Ningekubaliana sana na watu kusema ili twende pamoja kuna umuhimu wa kuwa na mkakati wa elimu kwa maeneo yaliyoathirika na si maeneo yenye majina ya aina fulani. Halafu from there watu wasonge mbele.

Mama Salma alipojenga shule ya bweni Msata, ameona tatizo lipo wapi. Kwamba wapo watoto hawapewi nafasi huko makwao kujifunza bali wao kujifunza mambo ya ndoa zaidi na pengine kuozeshwa katika umri wa shule.
Anajaribu suluhu kwani katika 100 anawezapata 10 ambao nao watabadilisha wenzao kama yeye. Hii ni moja ya approach za tatizo. Pengine kuna nyingine basi kila mmoja wetu aje na yake.

Lakini darsa zima linapokimbia shule au shule kufungwa halafu ukasukumia lawama NECTA ni utunduwazi, uzezeta na umahaluni wa kiwango bora sana katika nyakati zetu.
 

Ahsante,
gombesugu

Kuhusu Ustadh Latif , UDSM wana utaratibu wao wa kuhoji mambo ila kwa kusema hivyo unacho imply ni kwamba at least majority ya wahudhuriaji ni wakristo na wamemzomea kwaajili ya uislam wake(certainly sio kwa kumpinga Nyerere akiwa 'kigodani' as that would be appalling na umeishasema ana mapenzi na historia ya Nyerere) kama kweli ni kwa sababu ya uislam basi mbona wasimzomee issa gulamhussein shivji.

kama ilivyo katika mambo mengi tanzania kwa sasa na kwa kila mmoja wetu hapa, sote kadiri muda unavyoenda unafika wakati inakua vigumu kujadili jambo lolote bila kujitambulisha wazi uko upande upi kati ya makundi haya mawili ya dini yaani mkristo au mwislam hata katika mnakasha tumeingia ktk kasumba ya 'pande mbili' kama wa kumlaumu ni Moh au Yericko au sie wachangiaji sina hakika. Nasema hivi kwasababu looking at the narrative in your comments - deep as you try to barry it, your seething antagonism towards the 'status quo' (which many of those from Moh's side have doubed as 'mfumo kristo') is obvious and indeed you have taken a side too in the process mkubwa kama ilivyo kwa kila mmoja wetu. Na sina haja wala siwezi kumlaumu yeyote kwa hilo kwani kama nilivyosema ni matunda ya utamaduni tulionao watanzania wa kudhani mijadala ya kidini ni dhambi (sidhani kama ina tija ukiacha kuendesha mjadala wazi juu ya jambo kwasababu tu ya nature ya subject matter kwa hivyo tutaishia kuwa kama china).
Na pia ni kwa sababu hii kuu nadhani mnakasha huu hutoweza kupata nafasi yoyote katika kigoda cha mwalimu kwasababu hauwezi hata kupita mchakato wa awali kutokana na mahudhui ya kitabu chenyewe kuwa yenye mrengo wa kidini [si kwamba mambo yanayomhusu Nyerere hubagua waislam au rangi : issa shivji ndiye yuko 'kigodani' yeye hajabaguliwa, salim ahmed salim mweyekiti taasisi ya mwl n.k] na sababu nyingine ni kama hiyo na ambayo tumekua tukiilalamikia hapa kwa muda mrefu ni taaluma: uhakiki na uhariri ya maandiko ya Moh mara nyingi umeulizwa maswali ya kimsingi kama historical methods alizotumia (mie alinijibu nimechelewa katika mnakasha nikaridhika siwezi kuwasemea wengine ) pia wengi wamedispute mambo mengine mengi ameyakubali mengine na mengi mengine ameyakalia kimya.

Hatahivyo huna haja ya kuwa mtaalamu wa historia kuelewa nature ya uchochezi wa maandiko yake, hususan suala la kujaribu kuwaweka mbele ya juhudi za ukombozi wa tz wazee wake na uislamu kwa ujumla na kwa kufanya hivyo kuudharau yeye mwenyewe 'mchango' wa wakristo hasa kwa kumshambulia mwl nyerere. Mie ningekua katika upande huo wa pili wa fence ningejiuliza retrospectively huyu mzee, hii historia yake ina nature ya kibaguzi na ni twainfold [ inawabagua wakristo na inawabeba sana wazee waislam 'wa dar'] utajua akimaliza na wakristo atakuja kwa wazee wenu akiwatetea wake 'wa dar' na inanikumbusha fasiri ya Julius Kaisari, mara tu Mark Anthony alipomaliza kuwadanganya Brutus na wenzake kuwa atawatetea kwa wananchi akatoka akaenda kwa wananchi na kuwachochea kwao kina Brutus na nchi ikabaki kwake na Octavian -- na Nyerere akijua fika kisa cha 'mark anthony' hakutaka kuirudia historia and was quick to secularize the country for good. Na haya ya Moh ni maneno ya mkosaji amelishwa na wazee kila mmoja na nung'uniko lake.

Kizuri kinachotokana na mnakasha huu ni uelewa kuhusu juhudi zilizopo kubadili historia ya nchi yetu na hata zaidi kuwafahamu wale walioisaliti (hao wazee) na kushindwa kwao. Ila pengine kwao wachache waliokikubali hicho kitabu (ambacho Moh anasistiza ni historia ya wazee wake na sie tuandike zetu) wataisherehekea kama ndio hasa historia isiyojulikana/iliyosahaulika ya tanzania. Whatever side you take the irony is that with all the buzz and excitement : its very unlikely there will be any new converts, resolutions or concessions from among the participants. but I assure you Moh has a lot to answer for in addition to the concessions he has made.

Kuna msemo unasema "patriotism is the last refuge of the scoundrels". In fact its very easy to play 'the patriot' na kwa lugha yetu ningeusema "uzalendo ndilo kimbilo la mwisho la madhalimu wasio na sababu kwa nia yao mbaya". Hitler convinced everyone that 'jews' and 'jehova witnesses' e.t.c were the problem that they were not 'patriots enough'. Kitabu cha Moh hakijaribu kuonesha juhudi za mkristo, machifu, wala makabila mengine makubwa yaliyo na wakristo wengi kwa sifa zilezile wanazomwagiwa wazee wake --huenda ni kwasababu ya mapana ya sifa zinazomwagwa upande mmoja kutotoa nafasi kwa kitabu hichohicho kusifia upande wa pili; au kwasababu ya ufinyu wa mahudhui ya kitabu chenyewe kishindwa kujumuisha juhudi za wengine au pengine ni kwasababu ya lile tunalolihofia, well hapo bado Moh hajaweza kututegulia kitendawili cha kitabu chake.
 
Mwenyezi Mungu akujaze kila kheri na nia yako nzuri. This is one of the best statements ever made in this thread. I will also avail own resources for this noble goal.

Wickama,
Hebu angalia hii hapa chini:

Kutoka "Tanganyika Political Intelligence Summary, March 1952":

"...it is reported that the Secretary of the Association, Abdul Wahid Sykes has
dispatched letters to all branches asking members for suggestions under
the following heads for a memorandum to be prepared for the Royal
Commission..."

"...Abdul Wahid Kleist Sykes, Secretary of the African Association who, as
reported in last month's summary (paragraph 20) was going on safari up
country, visited Mwanza, where he met Paul Bomani, President of the
Bukoba African Association, and accompanied him to Bukoba. Sykes then
visited Kampala alone.....on 8[SUP]th[/SUP] March, a secret meeting was held, attended

by leading members of the Mwanza Branch..."

(Hizi ni taarifa kutoka Rhodes House Library, Oxford kutoka majalada ya
kikachero ya Waingereza baada ya miaka 50 yanawekwa wazi kwa mtafiti
yeyote kuyasoma na kufanya nakala akipenda.)

Kuna mengi siwezi yote kuyaweka hapa.


 
gombesugu, how much I wish the above was true for, had it been so, the kind of discussion currently taking place in this thread, would never have seen the light of day. Kama nilivyosema mwanzo kuhusu post yako ya kwanza kabisa, mimi Mag3 niliipokea kwa moyo usio na doa and my greatest expectation was for you to be for real! Ungekuwa umeufuatilia huu mnakasha kwa umakini na ukomavu kama huu uliouonesha hapo juu, hungekuwa na shaka lolote kujua sisi wengine tunatetea nini na tunapinga nini.

Kwetu wengine tuliozaliwa 1940s, huko kunikuta humu mtandaoni tu, kungefawafanya vijana wanaonitupia maneno ya kejeli wajiulize mara mbili mbili. Ni wazee wangapi wa rika yangu walioshuhudia mathalani computer zikiundergo metamorphosis kutoka zilizojaza nyumba nzima hadi sasa zinaweza kuwekwa kwenye mifuko ya shati. Ni wazee wangapi waliopata bahati ya si kuziona tu bali kufanya nazo kazi when computers were anything but user friendly...nakueleza haya ili uelewe kitu kimoja, hiyo historia anayojaribu kusimulia Mohamed Said, wengine tuliiishi, we lived it na kwa rehema za Muumba bado tupo.

Hiyo ndio maana gombesugu, nina ujeuri wa kuita koleo kwa jina lake...a spade deserves to be called by its name...I have had the priviledge of witnessing most of it! Nilitaka tu kuweka hili sawa...tuendelee na mjadala.
 
Mohamed Said umemuelewa Mag3,yeye hakusimuliwa history na wazee wake-he was there in person when history was unfolding,many salutes Mag3
 
Last edited by a moderator:
great thinkers tunaomba ilm-some of us are in the dark


"Hapa ndipo tunasema Sheikh Amir kama alivyo Maliki na Rukara hawakuishi nchini kwa kufuata misingi na taratibu za kisheri.Taratibu zilizowawezesha wao kuishi na kufanya uharamia ni zile zile anazolalamikia Mohamed chini ya mfumokristo.

Lakini pia kuhusu WML hapa kuna funzo linalokataa kabisa maandishi na dhana nzima ya Mohamed kuandika kuhusu wazee wake.

Kilichomkuta sheikh Amir ni sawa na kile cha Maliki na Rukara.
Tunafaham kuwa Rukar alipata kibali cha kuishi na kufanya atakayo katika mfumo kristo"
 
Mohamed Said-kumbe hii african association ni product ya mission quarter?

"Rupia's house, situated at Likoma Street and Magila, is where the African Association was founded in 1929. The house still stands today though not in its original structure"
 
Last edited by a moderator:

No no Mzee MS, I love your posting. Ujazwe Kheri. This is what we have all along said. Look, this movement to Mwanza, Kampala, meeting Bomani, Lake zone officials, hii ni very good news. These people worked as Tanganyikans and Christians or Moslems later. Many thanks
 
Serikali inaongozwa na Muislaam lakini, kwa wafuasi wa Mohamed Said, madai kuhusu MfumoKristo yako pale pale...bila shaka, kwao, hii ina maana kwamba;

  • hata kama mawaziri wote wangekuwa Waislaam, madai yangebaki palepale!
  • hata kama makamanda wote wa polisi wangekuwa Waislaam, madai yangebaki pale pale!
  • Hata kama wakurugenzi wa TISS wote wangekuwa Waislaam, madai yangebaki pale pale!
  • hata kama majaji wote wangekuwa Waislaam, madai yangebaki pale pale!
Ugomvi sio dhidi ya Kikwete na serikali anayoiongoza, hapana, ni dhidi ya MfumoKristo!
Lawama si dhidi ya Jakaya Mrisho Kikwete, hapana, ni dhidi ya Julius Kambarage Nyerere!
Chuki si dhidi ya chama tawala CCM, hapana, ni dhidi ya chama cha upinzani Chadema.
 
Ni jinsi gani mfumo Kristu unatengeneza wasomi mahiri Waislamu, wafanyakazi na watumishi mbalimbali ambao ni Waislamu na hata kutengeneza Rais, Mawaziri, Majaji n.k ambao ni Waislamu? Ni kwa namna gani mfumo wa kibaguzi unatengeneza nafasi bora na za juu kabisa za wale wanaobaguliwa?

Unless, mfumo huo umeshindwa kazi yake ni hauna nguvu unayodhaniwa kuwepo. Fikiria: Kama kweli kungekuwepo Mfumo Kristu na ungekuwa na nguvu unayodaiwa kuwa nayo, Kikwete aliweza vipi kuwa Rais mara mbili mfululizo?
 
Wapo wenzetu tunaposema Mohamed Said anatumia ulaghai katika uandishi wake kwa lengo la kuleta chuki katika jamii kwa mgongo wa dini, wapo wanaodai tunatukana. Katika post hii naanza kuleta nukuu za uongo ambazo Mohamed Said amezitumia kupotosha ukweli na hivyo kuwalaghai vijana kuamini kwamba ni kweli kuna MfumoKristo unafanya kazi kuwabagua Waislaam. Naanza na madai yake kuhusu Marehemu Profesa Kigoma Malima;


Wanajamvi naanza mjadala ndani ya mjadala...naomba tuanze kwa kujadili ukweli wa madai yake hapo juu, karibuni.

cc. Gwalihenzi, Wickama , gombesugu, Ritz, Nguruvi3 , THE BIG SHOW, Ngongo, Jasusi, Mzee Mwanakijiji, Nyambala, Son of Alaska, Ami, Kadogoo, platozoom, mfumo, Boko haram, Rapherl, Yericko Nyerere, Mundungus Fletcher, Remote, Barubaru, Wimana, Geeky na wafuatiliaji wote wa huu mjadala.
 
Last edited by a moderator:

Mag3 that will be exteremely nice na Mwenyezi Mungu akujaze afya ya kufanya jambo hili. Good Luck, am listening. Somebody should tell me; Nyerere was the most educated in the TANU leadership, infact the 1st Masters degree in the country. He was the most skilled debater of his time hadi kupata respects za kina Sykes, Rupia, Bhoke Munanka, Seaton, Amir Jamal, Kambona, Lord Twining etc. We also saw the then Governor of Tanganyika complaining kuwa uchache wa wajumbe wa kiafrika kwenye Legco ilichangiwa pia na wao kutomudu ku-debate kwa Kiingereza. Hali wa watanganyika wetu kwa kiingereza tangu enzi hizo haikuwa nzuri. It beats all logic kuwa wanakamati wa TANU, far inferior in education to Julius eti wamwandikie Nyerere hotuba ya kupeleka UNO. Some birds can believe that. But surely not all. Kama walichangia mawazo yao kama TANU (which is normal and commendable) does that amount to the level ya kuhangaika kumdhulumu Nyerere haki uandishi wa hotuba hii? Nawakumbusha TENA wanajamvi maana ya MDINI; Mtu yeyote anayetoa au kumnyima mwingine fursa/haki yake kwa kigezo kuwa mlengwa wanafanana au wanatofautiana kwa imani ya dini. Somebody is lying!!!!!
 
Mag3;6117470]Wapo wenzetu tunaposema Mohamed Said anatumia ulaghai katika uandishi wake kwa lengo la kuleta chuki katika jamii kwa mgongo wa dini, wapo wanaodai tunatukana. Katika post hii naanza kuleta nukuu za uongo ambazo Mohamed Said amezitumia kupotosha ukweli na hivyo kuwalaghai vijana kuamini kwamba ni kweli kuna MfumoKristo unafanya kazi kuwabagua Waislaam. Naanza na madai yake kuhusu Marehemu Profesa Kigoma Malima;
Wanajamvi naanza mjadala ndani ya mjadala...naomba tuanze kwa kujadili ukweli wa madai yake hapo juu, karibuni.
Mag3, wakati mjadala ndani ya mjadala unaanza, napenda kuweka nukuu za watu hao wawili ambao wanatetea kitu kimoja.
Tafadhali msomaji naomba upitie mistari ya Wimbi la Mbele na Mohamed Said kwa umakini sana halafu uniambie kama kuna consistency ya madai.

Mag3, kwa assumption naomba tukubaliane kuwa namba ya watoto wa kiislam ilikuwa zaidi ya 50%.
Madai haya yametolewa na'' marehemu profesa'' Kuna mambo ya kujiuliza.

1. Idadi hiyo aliipata vipi? Je ni kweli kuna mahali Malima ali document habari hizi.
Je, hakuna uwezekano Mohamed alipika data kama alivyopika za nyuma?

Nasema hivyo kwasababu kuna mahali Mohamed kasingizia UDSM kuwa kati ya mwaka 1970-1980 kuna miaka miwili ambayo chuo kikuu hakina takwimu za watu waliosajiliwa(Ushahidi upo).
Sasa kama aliweza kufanya hivyo kwa chuo kikuu kilichopo hadi leo atashindwaje kumsingizia marehemu Malima!

2. Endapo Malima kweli alitoa data hizo basi kuna uwalakini katika uwezo wake wa kufikiri kama profesa.
(nasema endapo alisema hayo Mohamed anayosema leo)

Uwalakini ni kuwa ametafuta chanzo cha tatizo kana kwamba tayari alikuwa na ''clue''.
Upo uwezekano kabisa kuwa shule au darasa linaweza kuwa na wanfunzi 100 na wote wakafeli.

Tumeona Morogoro ambako baada ya miaka 20 shule moja ya msingi imefaulisha kwa mara ya kwanza.
Hadithi kama hizo zipo katika sekondari n.k.

Kwa mtazamo huo 50% si kigezo cha kuonyesha kuwa mbele ya safari lazima representation ya 50% iwe 50%.
Lakini basi Profesa alipaswa atueleze kama aliondoa (rule out other factors) vigezo vingine kabla ya kurukia NECTA.

Kwa mtu anayetaka kufanya utafiti kama huo, NECTA ingekuwa sehemu ya mwisho kabisa baada ya kumaliza sehemu nyingine. Kwahiyo enrollment haina maana kuwa lazima outcome yake iwe sawa unless alikuwa na hint kuwa tatizo lipo NECTA. Na kama hivyo bado swali linabaki ni kigezo gani kilitumika kumpa hint na je alitumia uwezo wake wa kitaaluma kujua ukweli kabla ya kuingia katika sakata hilo?

Sasa hili la namba za mitihani, nadhani Mohamed anajua kuwa si kweli, hata ''Wimbi la mbele'' amethibitisha hilo kwa kusema namba zilianza kutumika na majina huko nyuma kabla ya Malima, akimaanisha kuwa namba zilikuwepo kuanzia huko nyuma. Kama ni kweli au la, ukweli unabaki kuwa namba za mitihani hazikuja na Malima.

Vinginevyo Mohamed aje akanushe. Ikumbukwe Mohamed aliunga mkono hoja ya ''wimbi la mbele'' sasa tunashindwa kuelewa anasimama wapi!

By the way Mohamed, hili la WML bado lipo ukirudi tutaendelea nalo sambamba na hili la Mkuu Mag3.
 

Nguruvi,
Anaetakiwa kutujibu Waislam ni serikali.

Sisi kwa sisi tutazunugushana kwa kauli za kukinzana tu.
Tutazungushana humu mwaka mzima.
 

Wickama,
''Kuandikiwa...''

Pako mahali imesemwa ''kuandkiwa?''
Nani anasema uongo?
 

Wickama,
Yapo mengine hujasema.

Hebu isome kwa utulivu historia hiyo ya Abdu Sykes katika post hiyo.
Lipo kubwa la kusema zaidi.
 

Son...
Ndipo mkutano wa kwanza wa kuunda African Association ulipofanyika.

Ukitaka habari zaidi msome Daisy Sykes katika Iliffe, Modern ''Tanzanzians''
''Kleist Sykes:The Townsman.''
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…