Rapherl
JF-Expert Member
- Jun 20, 2012
- 3,504
- 2,256
Maswala ya Waislam yapi ambayo siyafahamu?
Unamjua vizuri Makamba Jr?
Si kama hayo ya WML!
Makamba si huyu mtoto wa Yusuph Makamba au wewe unamjua yupi aliyekuwa Magogoni?au ulitaka nimjuaje?
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Maswala ya Waislam yapi ambayo siyafahamu?
Unamjua vizuri Makamba Jr?
Si kama hayo ya WML!
Makamba si huyu mtoto wa Yusuph Makamba au wewe unamjua yupi aliyekuwa Magogoni?au ulitaka nimjuaje?
Gombesugu,
Kumbe na wewe umo huvumi tu.
Umenipeleka mbali sana.
Shariff Attas mara ya mwisho kumuona ilikuwa Eid Fitr 1990 mimi na Kleist Abdulwahid Sykes
tulikwenda kufuturu nyumbani kwake asubuhi baada ya sala ya Eid.
Alitupa kisa kizuri sana kati yake na Nyerere pale Sokoni Kariakoo ofisini kwa Abdu Sykes.
Kisa ambacho kila mtu akikisikia atapata simanzi.
Nilifika kijiji cha Blantyre nje kidogo ya Glasgow, Scotland.
Hapa ndipo alipozaliwa David Livingstone na kijiji hiki chote kimefanywa kuwa makumbusho yake.
Nilifanya kipindi na BBC Swahili Service ''Barua Kutoka Glasgow'' kuhusu kijiji hiki na Mkuu wa BBC
Swahili Service siku zile Mzee Neville Helms alikipenda sana.
Hapa Dar es Salaam Mtaa wa Lumumba kuna kijana ana collection ya picha nyingi sana za watu
maarufu walioishi katika huu mwambao wa pwani.
Mimi nina hakika hakuna mtu Afrika Mashariki hii amekusanya picha kama hizo.
Nimeona hata picha ya Al Manzil na wanachama wake nk.
Sheikh Mohammed Said,
Asalaam Alaykum! Tafadhali nijaalia fursa kukuletea bayana yangu hii nyepesi. Niwie radhi maana awali nalisema ningepumzika lakini kuona yale malumbano ya yule "Bibi wa baibui", mambo ya chapati na lile kabati la senti Wallahi nimeshindwa kustahamili!ahaha!! Waswahili hunena; "kisebusebu na kiroho papo".
Naona kila ukiwaambia Jamaa hapo huijui hiyo habari ya huyo "Bibi wa baibui",unalazimishwa na kufanziwa inadi ya kuwa shurti utoe jibu. Ashakum si matusi; mathalan ukinena kuwa yule "Bibi wa baibui" alipata fadhila ile sababu alikuwa ni kimada wa Bwana Nyerere!? Si ndo yatakua yaleyale kwamba una chuki na Mwalimu,unamkashifu na kumfanyia tashtit. "Funika kombe mwanaharamu apite"! Mola takujaalia usije ukangia mtego wao kwa kujibu usolijua au uso hakika nalo.
Nimefurahika na ile safari yako. Napajua uzuri pale Blantyre Lanarkshire. Nastaajabu kuwa Serikali hapo Tanzania ati mpaka leo bado inamuenzi "mvumbuzi" "Dr" Livingstone na kumwachia aendelee kujinasibu na moja ya mitaa yetu maarufu hapo Mzizima!?
Kuna "tambara" chafu mno limemfumka (new evidences has emerged/ been extracted) pale Royal Geographical Society kuhusu unyama ,udhalim,umaluuni,uzandiki na vitimbi vingi mno alofanza huyo swahib yako "Dr" Livingstone!ahaha!!
Nimesikitika mno kuyasikia hayo japo sikushangaa. Aliwatendea mengi machafu wa -Afrika katika hizo safari zake za "uvumbuzi". Nina mawasilano pale na "jamaa" na tunafuatilia hili kwa makini,"mpaka kieleweke"!ahaha!! (niwie radhi maana humu JF nimejifunza mengi na hasa lugha mpya!)ahaha!!
Nalipatwa na "Duaa Al Mustaajaba" niliposikia at hata Mwai Kibaki nae kapewa jina la mtaa/barabara maarufu hapo Mzizima!? Hivi hiyo nchi ina wenyewe kweli!? Ama kwa hakika kuna mengi ndipo, Wazee wetu walinena; "kuwa uyaone"!
Nimefurahi habari za yule "jamaa wa Lumumba Street" mwenye picha kadhaa,Insha Allah nikijaaliwa kufika italazim "tukamwamkue". Nina group photograph ya BBC Swahili enzi zile ikinguruma kikweli,nina hakika itakuwa wengi wao unawafahamu. Mfano Zena Bakhressa na nafikiri Mzee Bin Dallas!?
Nakumbuka mno enzi za Madrasa maarufu kama:Kwa maalim Sakina, Shariff AbdilQadir Juneid,Al baadawy na Al madrasat Al Hassanain!
Ahsanta na nakutakia kila la heri kwa shughuli nzito ulonayo.
CC: Ritz,Ami,Boko Haramu,Mfumo,Kadogoo,Barubaru,The Big Show,Wickama,JokaKuu,Jasusi,Nguruvi3,Mag3
gombesugu,
Miaka mitatu ya nyuma tumemzika Sheikh Shariff Juneid. Msikiti wake Qibrateen mtaa wa Aggey.
Usidharau usichokijua. Hivi kweli leo Mag3 na Nguruvi waunganishe nguvu zao waandikie kitabu patakalika kweli hapa jamvini?
Mzee,
Chutama nikuletee msuli ujisitiri.
Ritz,JokaKuu,
Hebu jiulize kwani iwe watoto wa Kiislam wa Pwani tu ndiyo hawataki shule wasiwe watoto wa Uturuki, India, Pakistani, Indonesia, Dubai, Iran, Saudi Arabia, Misri, Singapore, Qatar.
Ritz,Pitia bandiko la JokaKuu utakutana na neno Waislam.
Hivi wale watoto wanaokataa shule kule Makete, Ludewa, Magu, Nansio, Mwitongo, Nkasi, Kizi, Nyanguge, Njombe, Katoro, Ngudu, Tarime, wote ni Waislam.
Barubaru, mbona unapata taabu kuuelewa huu mnakasha unahusu nini, kinchogomba si Mohamed kuandika historia ya wazee wake, hapana, ni namna anavyowahadaa wananchi kwa madai ya kipuuzi yasiyo na ukweli wowote...hata hivyo naomba kwa niaba ya hao wengine usiowataja nikutake uzingatie mambo matatu muhimu;
gombesugu, maadamu umeamua na wewe kuingia kwenye mkumbo huo huo wa kuwatazama waliokuwa Watanganyika katika misingi ya wao na sisi katika harakati za uhuru, naomba nikukumbushe jambo moja muhimu...huko unakoita mikoani ndiko walipoishi zaidi ya asilimia 98% ya wananchi milioni nane. Kwa idadi ya wakazi wa Dar es Salaam wakati huo, unaweza kuwataja hadi vichanga, hutaweza kufikia idadi ya wakazi wa kadistrict kamoja tu ka Mwanza. Heri mfungue thread mahsusi mtajiane majina yote yale tangia Arab Street, Kichwele, Ring Street, Main Avenue hadi mtaa wa Unter Den Akazien.
- Hicho kitabu, tofauti na ngano za Mohamed Said, kitachambua michango ya Watanganyika wote bila kutanguliza makabila yao, dini zao, eneo wala rangi zao...hakutakuwepo na cha sisi na wao.
- Hicho kitabu kitaongelea michango ya Watanganyika zaidi ya milioni nane kutoka kila kona ya nchi na hakitajikita katika watu wa Dar es Salaam tu ambao walikuwa hawafiki laki moja na nusu.
- Hicho kitabu kikiandikwa kwa staili hii hii alotumia Mohamed Said, nakuhakikishia kitapata upinzani kama huu huu unaoushudia hapa hata kama mwandishi atadai na yeye kafanya utafiti wa miaka 50.
Kwetu wengine tutabaki tukitanguliza Utaifa (Utanganyika) kwanza na kuwatukuza wazee wetu bila kuangalia tofauti zao kama za wenye mji na watu wa kuja au watu wa pwani na watu wa bara.
Baada ya hayo machache naomba turudi tupate maelezo kutoka kwa mwalimu mtoa darsa Mohamed Said, je ilikuwaje katika unaoitwa MfumoKristo shirika la World Muslim League (WML) likaweza kuruhusiwa kufungua ofisi nchini hadi expatriate wake Mburundi akapewa Uraia na pasi ya Tanzania!
Zama vizuri katika historia ya Tanganyika kuanzia Mjerumani kisha rudi tujadiliane upya. Hunajua chochote kuhusu mkutano wa Berlin kuweka mipaka ya nchi na kuzigawa.
Ritz, Mimi nina imani tofauti kidogo. Hadi sasa nafanya sana kazi wilaya ya Lushoto hapa Tanga. Ni wilaya ambayo kwa mujibu wa Thesis ya Pfeiffer (1990) ni asilimia 75% waislamu (kwa sasa nadhani Lushoto ina wakazi sio chini ya 470,000). Lakini mwamko wa elimu Lushoto ni mzuri. Hata tabia ya wazazi kufuatilitia watoto kimasomo sio mbaya. Lushoto familia nyingi hazina utani inapokuja kwenye elimu na hata biashara. Tembelea kariokoo shimoni. Kimaendeleo mabwana hawa wapo mbele. Tanga hii pia zipo wilaya desturi na mwamko ni tofauti kabisa. Sio kwa waislamu au wakiristo. Hapa huenda mchango mkuu ni desturi za jamii husika. Haya nimeyakuta pia Machame, Ugweno, Kamachumu na Babati. Duniani, siifahamu dini inayo-design watu kuwa wavivu, au kuwarudishia maendeleo nyuma. Maendeleo-physical, hayana uhusiano na dini (wajapan, wahindi, wachina largelly sio wakiristo au waislamu). Ni dhana watu wanayounda ili wawatukane au kuwadhulumu baadhi. Hata kwa waislamu, angalia kuwa the most advanced muslim nations ni za Asia (Malaysia, Indonesia na akina Turkey nk)sio za hapa Middle East pamoja na resources walizonazo.
Mfumo Kristo Tanganyika umeanza toka wakati wa mkoloni Nyerere akaja kuundeleza.
Mkoloni wakati anakuja upande mmoja alikuwa mueneza dini ya Kikristo na upande mwingine akiwa na mkataba wa kimataifa wa kupewa eneo hili kulitawala kupitia mkataba wa Berlin.
Bahati mbaya sana tawala zote zimekuwa zikiwapuuza Waislam na madai yao badala ya kuyafanyia kazi.
Tumemsikia Mkapa naye kaja na habari mpya kuwa wakati wa utawala wake alikuwa anatawala kwa haki.
Pamoja na mauaji ya Mwembechai, na Pemba kwake ni haki.
Ritz, Mkutano wa Berlin uliitishwa na Wajerumani ili kukubaliana namna ya kugawana Makoloni kwa amani bila Wakoloni kupigana wao kwa wao. Matokeo ndio Tanganyika, Rwanda na Burundi wakapewa Wajerumani.
Vita ya WW2 Mjerumani aliposhindwa, Tanganyika ikakabidhiwa kwa Waingereza, Rwanda na Burundi zikamegwa kutoka Deutshe Ost Africa (Tanganyika) wakapewa Wabelgiji. Waingereza waliombwa na UNO kuitawala Tanganyika na kuiandaa kwa Uhuru, ndio maana uhuru wa Tanganyika ulidaiwa UNO!
Ritz, wewe unakubali darsa la mtu mmoja tu humu ndani-Mzee Said, wengine hatujui kitu!
gombesugu,
Tafsiri ya kuwa mdini kwa hawa ndugu zetu ni hali ya mtu kuwa Muislam na kujiweka wazi.
Umeishajiuliza kwa nini Wakirsto hawaitwi wadini kwenye huu uzi kwa ni wadini ni Ritz, gombesugu, Boko haram, Kadogoo, Mohamed Said, zomba, THE BIG SHOW,
Lakini wale wanaowaita wazee wetu wana akili za madrasa, wapuuzi, wanywa gahawa, wavivu, washinda vibarazani, hawa wanaitwa wazalendo.