GimbeSugu
Nijambo jema lakini mafaa zaidi ni kujua nini walifanya katika harakati za uhuru na mchango wao.
Muheshimiwa Yericko Nyerere,
Nashukuru kwa ujumbe lonitumia,ama kwa hakika nafurahika kila kinitupia maswali japo umenibadili jina kiduchu!!ahaha!!
Nafikiri hiyo sasa ndio shughuli ya
wanaHistoria mahiri kama
Sheikh Mohammed Said,
Professor Mushi na wengineo kufuatilia na kufanza kazi zao kwa utuo. La muhimu Serikali iwajali na kuwapa misaada ya hali na mali kufanikisha shughuli zao bila ya kuzongwa na ma-Politicians au watu wa Kanisa na Misikiti. Nasi tulobaki tujaribu kuwakubali na kuwapa moral support kwa manufaa ya taifa letu.
Japo kwa uchechefu wangu, najua kwa yakini wengi kati ya hao
Wazee wetu tunaowakumbuka na hata wale
tulowasahau;walikua na
taaluma mbalimbali,walifanza mengi mno pita kiasi na walijitoa muhanga mkubwa kwa nchi yao bila ya kujali matabaki au tafauti zao.
Ukiondoa wale "Mandava",wengi ya hao
Wazee wetu walikua ni; Merchants,Thinkers,Seafarers,Civil Servants,Artists,Pianists,Poets,others from Noble/Aristocracy families,Land owners,Traders,Activists,Scholars,Etymologists,Musicians,Teachers,Akidas,Liwalis,Town Criers Lexicologists and many other. Ndo maana mimi siku zoote niko so proud na hao Wazee wetu na sisikilizi kabisa ile
"Historia za wazungu/wakoloni",ati walipokuja walikuta Wazee wetu woote wanaishi juu ya miti na wala hawajui kusoma wala kuandika!? Inanikumbusha yalowakuta ma-Irish kutoka kwa
Oliver Cromwell!!
Napata wasiwasi pale ninapoona jitihada za
Sheikh Mohammed,tena kwa kuanza kuandika kuwataja wa
Tanganyika kiduchu tu na inaleta tafrani je huko twendako tutafika kweli!?
Ahsanta.
CC: Ami,Barubaru,Mwanakijiji,Sheikh Mohammed Said,Ritz,JokaKuu,Jasusi,Mfumo,Kadogoo,Boko Haram,The Big Show,Wimbi la Mbele,Nguruvi3,Mag3