Gombesugu, umejitahidi sana kujificha katika pazia. Tulikwambia kuwa ni suala la muda true color zitajitokeza na sasa zimejitokeza. Bandiko lako hili hukuwa na sababu ya kutumia neno mtu au watu. Hili umemlenga Nguruvi3.
Mimi nipo na Mohamed siku nyingi na moja kati ya mambo hayanisumbui ni kudharauliwa, kutukanwa au kudhalilishwa.
Mambo hayo hayanisumbui kwasababu kama kuna mtu mmoja ananielewa si tatiziki na 10 wasionielewa Hili ni kosa lile lile la kila mara. ''baadhi yetu akina nani? Hivi akitokea kaka yako hakubaliana na Mohamed huyo ni ''baadhi yetu'' au inakuwaje.
Nadhani kama umesoma vizuri kuhusu Mohamed, dhima ya andiko lake ni chuki, farki, tashtiti n.k. Kama unachukia chuki basi Mohamed hafai kuwa ''baadhi yetu''. Kwanini ndugu yangu usisimame katika ukweli?Hapa tuna uelewa tofauti na ni vema tukasadiana. Endapo kuna kitu kimefanyika kisayansi, methodically basi tunakuomba sana utusaidie. Na hapa nitakuuliza kitu kimoja. Je, upo tayari nikuwekee habari ya Mohamed utuelezee kisayansi ili utusaidie kitaalauma na ki-uwanazuoni kuonyesha chuki na dhalili anazofanyiwa?
Kama utakuwa tayari nifahamishe.Si kweli, labda kama unamuongelea Mohamed. Mohamed anajulikana jamvini kwa kauli za ''sina ujuzi'', nimekusoma, tuendelee na darsa, hilo tuliache kwanza, inasemekana, andika kitabu, nimekwenda ulaya, nimekula na wazungu n.k. katika kukimbia hoja.
Mfano, mumekomalia Makerere, nimeweka mnakasha niliokuwa nao na Mohamed,si hoja imekwisha!
Nimewauliza kwani harakati ni kitu gani hakuna aliyeeleza, hoja ikaisha. Nafahamu unachukia sana hoja za Mohamed kubomolewa lakini spade iitwe spade na siyo big spoon.Ukweli ni sehemu ya dini na imani kwa waumini.
Wala usiseme jamaa sema Nguruvi3. Nimeweka hoja hiyo kwasababu imesemwa kuwa waislam hata walisoma wananyijmwa nafasi. Nikasema basi kama yupo Zoologist ajitokeze maana kuna shirika '(siyo mimi linahitaji mtu)Katika kufanya spinning zile zile za Ritz nawe umeniwekea maneno. Hilo sijali kwasababu kumbu kumbu zipo.
Narudia kama kuna Zoologist ajitokeze, kama hakuna shirika hilo hilo linatafuta local epidemiologist hasa mwenye background ya vetenary. Kama hakuna basi hapo ndipo mahali pa kuanzia kwanza kujiuliza kwanini? Nimesema waislam specifi kwasababu ndio wenye malalamiko ya kupea nafasi za menial job hata kama ni qualified kama alivyosema Mohamed.Nimeongeza Epidemiology na zaidi kama yupo mtu wa Eng-Agric aliye na utaalamu katika combine harvester naye pia ajitokeze na qualification zake tusaidiane.And respectful Muslims to add on.
Hapo juu umelalamika sana kuhusu matusi, kwa bahati mbaya na hili nakusamehe umerudia kile kile usichokitaka.
Gombesugu, Uislam ni dini ya mwenyezi mungu. Uislam hauna miliki au hati miliki isipokuwa kwa muumini. Baru baru aliwahi kusema si kila mwislam ni muumini lakini kila muumini ni mwislam. Uislam unasimama katika amani, haki na ukweli.
Uislam si ushabiki na Uislam umesisitiza katika kutafuta maarifa. Maarifa yaweza kupatikana hadi China. Maarifa si ushabiki, ni utambuzi na ufahamu. Kila anayekwenda kinyume na mafunzo ya Allah anamhalifisha Mwenyezi Mungu.
Uislam hauzui kusema au kukubali ukweli. Na hakika hiyo ni moja ya hidaya ya mwenyezi mungu kwa waja wake.
Hakika yule anayesimama katika ukweli basi atakuwa ameiona nuru na atakuwa miongoni mwa waja wema.
Mohamed Said akisema, yule mwenye elimu ana bahri, hivyo usichoke kujifunza na wala usijizuie kujifunza.
Kujifunza kunahitaji ustahamilivu hekima na busara. Hasira, jwazba na unyonge ni silaha mbaya unapokuwa katika kujifunza. Jifunze kila kilichopo katika mazingira yako, kiwe ndani ya msikiti, kanisa, sinagogi au Jamatini.
Basi tumuombe mwenyezi akunusuru na hasira na matusi, ili sote tuwe waja wake.
Mimi nimekusamehe kwasababu hakika hakuna mtimilifu miongoni mwetu wanadamu.
Masalaam, msalimie Ahli na nduguzo.
Muheshimiwa Nguruvi3,
I'm quite impressed with your brain power to try comprehend what
Islam is and
its teaching and who
Muslims are.
Ahsanta kwa kunijuza jitihada zako za kujaribu kuwasaidia kwa kuwatafutia ajira/vibarua
waIslam hapo
Tanganyika.
Nashukuru pia kwa
kunisamehe kwa kuhisi kwako kuwa maelekezo yangu ya awali yalikua na "
elements" za hasira na kashfa dhidi yako.
Ile habari ya kunitaka mimi nikiandike upya kitabu cha
Sheikh Mohammed Said "kwa njia ya kisayansi" ili kifahamike uzuri,ahsanta kwa kunipa cheo hicho japo ni kikubwa mno dhidi yangu. Kama utarejea kwenye bayana yangu ya awali kwa
Sheikh Mohammed Said nalieleza uchechefu wangu na ku
-declare kuwa nipo kwa kujifunza!
Pia nachelea isijekua ile habari ya Rais wenu
Bw W. Mkapa,
alipotuamrisha ati tumwandikie madai na dhiki zetu
"kwa njia ya kisayansi". Tulipomaliza na kumkabidhi akatujibu, ati yeye binafsi hana uwezo wa kuyashughulikia na
Serikali haiyamudu maana ni "
magumu mno na ni ya kiHistoria". I have never come across the most ridiculous comment made by a sitting
President my entire life!!
Kuhusu yule
Alhaj Rukara wa
WML,nilikufahamu maswali yako kwa
Sheikh Mohammed Said,japo naye kwa ustaarabu alikujibu kuwa hazijui "zile habari".
Nafikiri kwa upande mwingine inalazim tuwasamehe hawa ndugu zetu wa
kirundi na
kinyaRwanda maana yaelekea ndio "dasturi na mazoea" yao, kuwa makwao pakitulia basi hurejea.
Nafikiri unakumbuka habari ya
Prof. Silas Lwakabamba wa
UDSM baadae
KIST na sasa hivi ni mmojawapo wa watu wa karibu saana na
Kagame na ana cheo/mamlaka nyeti pale
Kigali-Rwanda.
Tujitahidi na kujiepusha kidogo kuwa
selective tunapotoa mifano. Huyo
Lwakabamba naye vitimbi na ghilba zake haitofautiani kabisa na shutuma na madai ulotoa dhidi ya
Alhaj Rukara na labda kupita. Alikua ni kama "
James Bond" fulani hivi. Shughuli nyingi nyeti alizowahi kutumwa na Serikali na
Consultancy kadhaa alikua akizipitisha kwanza kwa
Kagame na
Rwanda tangia yupo pale
UDSM. Huyu ni mkristo mzuri tu kama alivyokua
Alhaj Rukara ni mu-Islam mzuri pia. Nafikiri hatuna haja ya kufungua mnakasha mwingine ati kujadili na kupeana definitions za Gaidi,Mchochezi,mwanaharakati au Jasusi!?
Mifano ni mingi tu kuanzia misimamo ya kina
Reagan na
Thatcher dhidi ya
Mandela kipindi kile mpaka leo tunafikia baina ya wa-
Afrika wenyewe kwa wenyewe! Kwa hiyo yawezekana kabisa kuwa; huyo umuonae wewe ni gaidi,mwanaharakati hatari na mchochezi,wengine wanamuona
mpigania haki na ni
mkombozi wao!! Kwa ufupi huyo
Prof. Silas Lwakabamba mnya
Rwanda,ambae miaka mingi baadhi ya jamaa walikua wakiamini kuwa ni mzalendo halisi,mkristo mtakatifu na msomi mahiri, "
sisi wengine" tulishajua madhila na ujasusi wake dhidi ya nchi yetu. Japo kwa bahati mbaya kelele zetu zoote wakti huo zilipuuzwa kwa kuitwa
wadini!?
Kwahiyo nakufahamu "kiasi" juu ya kilio chako dhidi ya
Alhaj Rukara.
Tafadhali tuendelee na mnakasha ili tusiende nje ya
mada/shutuma alizoleta
Yericko Nyerere. Punguza kumbana
Sheikh Mohammed kuhusu hilo suala la
Alhaj Rukara na
WML,na kishasema haijui hiyo habari.
Ahsanta kwa kunisikiza
uchechefu wangu na nakutakia siku njema
mTanzania mwenzangu.