well said, well done!
Mimi nimeona Wakurya wakidanganya umri ili waende Kagera! Nimeona kwa macho.
Nimeona matajiri wakitoa ng'ombe kwa ajili ya chakula cha wanajeshi, mabasi yakitolewa kupeleka wapiganaji.
Kule barabara ya 10 na 11 sikuona hamasa kama nilizoziona Tarime, Kyabakari, Nyamongo n.k. lakini haina maana hawakwepo Wabondei au wasambaa.
Sasa akitokea mtu aka single out Wakurya na kuandika historia ya vita ya Kagera kwa kutumia Wakurya tu na kisha kusema ndiyo historia ya vita ya Kagera na kwamba huo ni ukweli, inafikirisha sana.
Kwa wanajamvi, tunathamini mchango wa kila mtu lakini basi mchango wa mtu fulani usitumike kumdhalilisha mwingine.
Uhuru wa Tanganyika ni nyumba ya matofali na kwamba kila tofali lilikuwa na nafasi yake muhimu na isemwe hivyo.
Hapa ndipo watu hawaelewi na kuishia katika ''nyie na sisi''
Hatuwezi kuwa na taifa la nyie na sisi. Rwanda hawakuweza, Bosnia hawakuweza, Nigeria ni matatizo tupu n.k.
Hata pale walipo akina ''sisi'' kama Somalia bado wamegawanyika kwamba Wasengeli wanasema sisi, wabaidoa wanasema nyie. Mtoto amezaliwa na sasa ni askari hakuna muafaka. Jamani, huko ndiko mnataka tuelekee?
Kama ndiko, basi tuelewesheni nani mshindi wa maeneo hayo!