Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar

Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar

Sheikh Mohammed Said,

Salaam sana.

Hapa pana mambo mengi mno yenye kuleta rabsha kiduchu na vichekesho vingi. Nafikiri unakumbuka ile bayana yangu ya awali kwako,sababu nilichelea kuingia mambo kama haya ya udini,kutaja majina na kuwaadhiri jamaa zetu toka family mbalimbali tunazozistahi na mikanganyiko mingi saana,na matokeo yake tupo nje kabisa na hii mada/shutuma dhiki yako.

Imekua kama mtego wa panya sasa,anangia alokuwamo na asokuwamo!ahaha!!

Nimecheka pasi kiasi na yale majibu ulotoa kuhusu hiyo habari ya mmanyema mkristo. Nafikiri Sheikh Mohammed labda kitambo hujenda tembea pale Ujiji kuona "mabadiliko". Mimi binafsi pia pana pahala kwingi nahitaji nikatupie jicho Insha Alaah penye uhai na maajaliwa.

Hii habari ya makabila, ama kwa hakika imenichekesha kiduchu hasa ulipotaja Wangazija Wakristo. Unajua pale Comoro siku hizi pana wale "Wangazija pori" ambao huenda pale "kununua baraza" na kujinasibu Ungazija pasi kiasi. Ukizungumza na Bwana Ahmed Rajab atakuchekesha zaidi juu ya habari hizi.

Nafikiri hata ndugu zetu wa kiZaramo zamani nao walikua na dasturi na ustaarabu kama huo wa kukaribisha "wabweshu" na kuita "udugu wa khiyari". Tena walikua wakifanza na sherehe kubwa mno siku ya kutimiza huo "udugu". Napenda saana tamaduni na mapenzi yalokuwapo zamani baina yetu.

Sijui lini utapata fursa tuwekee na habari za mapinduzi ya Zanzibar,hasa wale wamakonde wa Kipumbwi,Ushongo na Sakura walotumiwa kuua ndugu zetu na kumuweka madarakani yule Mnyasa alokuja Unguja mtoto wa mgongoni(yaleyale ya Musharaf kuja Pakistani mtoto wa mgongoni halafu kuwafanzia watu hadaa). Ndugu na jamaa zetu wengi walitolewa roho na yule dhalim.

Uncle yangu Commando Amour Dougheish,ndo alokua akamkamate yule Mnyasa toka pale Ikulu na kumpeleka pale Idara ya habari - Rahaleo, halafu atangaze kuwa nchi isharejeshwa na imo mikononi kwa wananchi wenyewe. Wallahi,lile jambo mpaka leo najuta halikufanikiwa.

Basi Insha Allah tuendelee na mnakasha.

Ahsanta.

Kiongozi, tukubaliane kimsingi tu kuwa makabila na dini zetu hazina tija ktk mustakabali mwema wa Taifa na jamii zetu. Taifa na makabila yetu yana mchanganyiko wa ajabu sana, kusimamia hoja dhaifu kama "hakika hakuna Mmanyema, Mgoma, Mtongwe au Mkayamba Mkristo au Muislamu" ni hoja duni sana ambayo wajinga wengi huzisimamia na kutofautiana kiasi cha kuuana hata kama wametoka familia moja.
Hoja kama hiyo inapoibushwa na mtu mwenye elimu na umri wa Sheikh Said, ambaye ametengeneza wafuasi wengi ambao miongoni mwao hawana uwezo wa kuhoji lolote linaloibuliwa naye, wenye hekima lazima tuhoji, tujiulize lengo lake ni nini na kutoa majibu mwafaka hata kwa hoja yake dhaifu ili kuwapa ufahamu hata wale wajinga.
 
Mwanakijiji.

Nimeisoma sana Historia ya tanganyika na hakukuwa na vita vikubwa ambavyo vilihitaji mtu au watu watumike kuleta amani kama ilivyokuwa kwa Kenya na Uganda ambavyo kulikuwa na tabaka za makabila. Tanganyika hakukuwa kabisa na tabaka hizo za ukabila kiasi cha kuifanya nchi kukosa amani.

Labda nidadavulie Ni amani gani aliyoileta Nyerere ambayo ilikuwa haipo kabla ya uhuru wenu? Na amani hiyo ilikuwa inavurugwa na nani? Nasubiri darsa lako hapa.


CC.. Nguruvi3, Ritz, Mohamed Said,


Inawezekana mwenzako anadhani MAJI MAJI WAR n etc zilikuwa ni vita vya kikabila,
Aje atupe darsa hilo,hata sisi tunasubiria kwa ham pia...
 
Ndugu yangu yaani nilipatwa na mshutuko kusoma kuwa balozi wa Marekani aliwahi kuhutubia bunge. Afadhali umelileta.

Mohamed Said, Balozi wa marekani alihutubia Bunge lini?

Pole sana ndugu ya Nguruvi3 kwa kupata mshutuko tumshukuru Allah akufanyie wepesi usije kupata maradwi mengine kama kiarusi na sukari haya yote yanaletwa na mshutuko.

Nakushauri siku ingine ukipata mshutuko basi kunywa vijiko vitatu vya asali mbichi.

Balozi Royall alihutubia bunge la Tanzania tarehe 15 May 2003.
 
Sheikh Mohammed Said,

Salaam sana......




Nimecheka pasi kiasi na yale majibu ulotoa kuhusu hiyo habari ya mmanyema mkristo. Nafikiri Sheikh Mohammed labda kitambo hujenda tembea pale Ujiji kuona "mabadiliko". Mimi binafsi pia pana pahala kwingi nahitaji nikatupie jicho Insha Alaah penye uhai na maajaliwa.

Hii habari ya makabila, ama kwa hakika imenichekesha kiduchu hasa ulipotaja Wangazija Wakristo. Unajua pale Comoro siku hizi pana wale "Wangazija pori" ambao huenda pale "kununua baraza" na kujinasibu Ungazija pasi kiasi. Ukizungumza na Bwana Ahmed Rajab atakuchekesha zaidi juu ya habari hizi......

Ni dasturi ya siku nyingi Makabila kudharauriana.
Mfano, Waha, Wahangaza, Warundi na Wanyarwanda, mtu asiye wa kabila lao huitwa Mnyamahanga, Wachaga huwaita Chasaka, Wagogo huwaita Wakonongo nk...

Lkn kwenye Imani ni tofauti sana, mtu huamua kuamini anachoamini, leo anaamua kumwamini ng"ombe kama mungu wake, kesho akaamini Jua au Mwezi kama mungu wake.

Kwa hoja za Sheikh Said na utavyoshangaa kukuta Wangazija Wakristo ambao utawaita Wangazija Pori nashindwa kukuelewa hao Wairaq na Wairan Wakristo.
 
Balozi wa Marekani hajawahi kuhutubia Bunge la Jamhuri ya Muungano; niko tayari kusahihishwa. Lini Balozi Royall alihutubia Bunge la Tanzania? ili tupitie hansard.

Mzee Mwanakijiji,

Unabisha tu kubisha sababu kasema Mohamed Said au unabisha ili unataka kufahamu.

Sasa nakata kisu kwenye mfupa usipende kuonga swiming pool na watoto wadogo chukua hii.

Balozi Royall alihutubia bunge la Tanzania tarehe 15 may 2003 na mada yake ilikuwa "Blood Money and Financing Terrorism."

Cc.. gombesugu, Kadogoo, Ami, Barubaru,
 
Last edited by a moderator:
Mzee Mwanakijiji,

Unabisha tu kubisha sababu kasema Mohamed Said au unabisha ili unataka kufahamu.

Sasa nakata kisu kwenye mfupa usipende kuonga swiming pool na watoto wadogo chukua hii.

Balozi Royall alihutubia bunge la Tanzania tarehe 15 may 2003 na mada yake ilikuwa "Blood Money and Financing Terrorism."

Cc.. gombesugu, Kadogoo, Ami, Barubaru,

Ritz,
Hivi hawa jamaa wanajua kuwa mimi nilipata mwaliko nikatoe mada Chuo Kikuu Cha Ibadan.
Hivi hawa jamaa hawajiulizi vipi nimealikwa mie...

Hivi hawa jamaa wanadhani mimi nitafunga safari na nisimame kwenye kilinge kisha niseme
maneno ya kutunga?

Laiti wangelikuwa si wachovu wa kufikiri hawakuwa hata na haja ya kuleta swali lile la Balozi
wa Marekani hapa jamvini.

Utafiti mdogo tu wangelipata jibu.
Naogopa kuwapa sifa yao kamili isijeonekana natumia lugha zisizopendeza.

Sishangai hadi leo wanashindwa kuandika hata kitabu kidogo cha historia
au pitio la kitabu changu kunipinga.

Wao wamekuwa kama Hakimu Nasoro Kiruka.
Maswali,mswali, maswali...
 
Ni dasturi ya siku nyingi Makabila kudharauriana.
Mfano, Waha, Wahangaza, Warundi na Wanyarwanda, mtu asiye wa kabila lao huitwa Mnyamahanga, Wachaga huwaita Chasaka, Wagogo huwaita Wakonongo nk...

Lkn kwenye Imani ni tofauti sana, mtu huamua kuamini anachoamini, leo anaamua kumwamini ng"ombe kama mungu wake, kesho akaamini Jua au Mwezi kama mungu wake.

Kwa hoja za Sheikh Said na utavyoshangaa kukuta Wangazija Wakristo ambao utawaita Wangazija Pori nashindwa kukuelewa hao Wairaq na Wairan Wakristo.

Wimana,
Unanipeka mbali sana.

Mwanamme wa Kimanyema akioa mke si Mmanyema basi ndugu zake
watamwangalia huyo mama kama ana tambo yaani ana kile kimo cha
binti wa Kimanyema.

Akiwa ana mwili mdogo watanong'onezana kusema, ''Kinyangarakata.''
Yaani, ''Ah si lolote.''

Udhaifu wetu wa kibinadamu.
 
Ritz,
Hivi hawa jamaa wanajua kuwa mimi nilipata mwaliko nikatoe mada Chuo Kikuu Cha Ibadan.
Hivi hawa jamaa hawajiulizi vipi nimealikwa mie...

Hivi hawa jamaa wanadhani mimi nitafunga safari na nisimame kwenye kilinge kisha niseme
maneno ya kutunga?

Laiti wangelikuwa si wachovu wa kufikiri hawakuwa hata na haja ya kuleta swali lile la Balozi
wa Marekani hapa jamvini.

Utafiti mdogo tu wangelipata jibu.
Naogopa kuwapa sifa yao kamili isijeonekana natumia lugha zisizopendeza.

Sishangai hadi leo wanashindwa kuandika hata kitabu kidogo cha historia
au pitio la kitabu changu kunipinga.

Wao wamekuwa kama Hakimu Nasoro Kiruka.
Maswali,mswali, maswali...

Mohamed Said,

Wewe endelea kutoa darsa jikite zaidi kwa wasomaji wa huu munakasha kuweka bayana historia yetu ya Tanganyika.
 
Last edited by a moderator:
Kadogoo,

..wewe una kengeza la UDINI.

..kama sheria ya Ugaidi inawahusu Waislamu, kama unavyodai, kwanini basi Lwakatare na Ludovick wanashtakiwa kwa sheria hiyo wakati wao ni Wakristo??

..umejaribu kupotosha utetezi wa Tundu Lissu kwa Lwakatare.

JOKAKUU,

Swali hilo hata Tundu Lisu kaishangaa Serikali kumkamata Lwakatare kwa ugaidi wakati sheria hiyo inawahusu Waislamu tu!
 
Kuna wakati binadamu huwa tunapitwa na jambo fulani...Unaweza kunisaidia/kunikumbusha labda ni waislam wangapi hapa Tanzania wameshafikishwa mahakamani au wameshashtakiwa kwa kutumia hii sheria ya Ugaidi?

SWEKE,
Suala sio kufikishwa au kushtakiwa! suala ni kuwa kuna sheria ya ugaidi iliyopitishwa na Bunge la Tanzania kwa ajili ya Waislamu tu! sasa kama yuko aliyekamatwa au kushtakiwa hilo unatakiwa uiulize Mahakama!
 
BY Nguruvi3""Aya ya pili anaongelea kuhusu waislam kwa ujumla. Mohamed hajui kuwa katika waislam wapo BAKWATA, Ismailia, Bohora, Shia na Sunni na kwamba hicho anachokiongelea ni kikundi chake na wala si waislam.
Jitihada zake ni kuonyesha ulimwengu uzito wa jambo hili kama tutakavyoona. ""

Usichanganye mambo na kuweka histohisia zako nguruvi3,bakwata ni chombo chenu kilichowekwa na nyerere kusimamia maslahi yenu na si maslahi ya waislam..
hilo lipo wazi na tunalitamka kwa kifua mbele kabisa,tatizo lako unajikanyaga kanyaga,unapiga hatua tano mbele kisha unarud hatua 25 nyuma,jitulize,hebu tulizana..

kwani Mufti Issa bin Shabani Simba si Muislamu?????
 
gombe sugu nimekukubali mkuu! Umenibania shekhe wangu mwenye uelewa mdogo wa masuala ya uchambuzi wa kisiasa,yeye anajua 2 uislam ambao wao ni asilimia 26 tu ya nchi nzima.
 
nafikiri kama utatumia busara kidogo na kutazama ni lini namba zilianza kutumika katika mitihani ya Tanzania na kuachana na kuandika majina na kutazama wakti huo nani alikuwa waziri wa Ilmu utaligundua hilo. Kwani Hata wizara ya ilmu ya Tanzania watakusaidia hilo wala haliitaji mjadala. Ila kwa mimi nakwambia ilikuwa kipindi Prof malima akiwa waziri wa Ilmu. Fanya uchunguzi utaligundua hilo.

Suala la Warioba naye yupo hai unaweza ukamuuliza tu kwani miongoni mwa aliosoma nao darasa moja Chuo kikuu (marhum Brigadia mang'enya ) mimi niliwahi kumuuliza kuhusu huyo hakuwa na jipya zaidi ya ukabila tu ulimbeba kama ilivyokuwa kwa akina Nyirabu na wengine kutoka mkoa huo enzi za JKN.

Barubari, samahani naomba unijibu hili swali; ulimaliza shule ya msingi mwaka gani?

Mimi nilimaliza Shule ya Msingi mwaka 1985 na nilitumia namba!
 
Hii sheria haina ulazima wa kufikishana mahakamani.Askari akihisi tu fulani ana mawazo ya kigaidi anaweza akauwa na hatiwi hatiani.
Vile kwamba haijatekelezwa kikamilifu basi ni kutokana na ubinadamu tu wa polisi wengi wa kitanzania.Wenzao wachache wameifanyia majaribio kule Zanzibar na hapa Dar es salaam.

AMI,
Wenzetu Kenya sheria hii ya ugaidi haikupitishwa na bunge sababu ya uzalendo na ushupavu wa wa Kenya wa kukataa kuburuzwa na Marekani! lakini hata hivyo Shekh Robo kauwawa kwa kupigwa risasi barabarani baada ya kushinda kesi ya tuhuma za ugaidi Mahakamani! swali la kujiuliza nani kamuuwa Shekh Robo?
 
  • Thanks
Reactions: Ami
Wacha uongo wewe, kama hakukua na vita, akina Milambo ma Mkwawa walipanuaje milki zao za utawala? au unamaanisha nini unaposema hakukuwa na vita hapo zamani?

GWALIHENZI;

Kwa hiyo Nyerere ndie alikuja kupatanisha makabila yaliyokuwa yakipigana sio? au ulimaanisha nini?
 
Nguruvi,
Ndugu yangu punguza ghadhabu, jitulize na andika kwa utulivu na kwa adabu.

Vinginevyo utageuka kuwa Lancelot Gobbo.
Si unamkumbuka huyu mtu katika ''Merchant of Venice'' ya William Shakespeare?

Nilieleza habari zake hapa JF.

Umesema mengi lakini nitakujibu moja.
Hili la Balozi Robert Royall.

Balozi Royall alihutubia Bunge la Tanzania tarehe 15 May 2003 na mada yake
ilikuwa ''Blood Money and Financing Terrorism.''

Nitakuongeza kitu.

Hiyo paper yangu iliyozua swali lako ndiyo lilikuwa jibu la hotuba ya Robert Royall
na ndiyo sababu ya kukumatwa uwanja wa ndege Dar es Salaam mwaka 2007
nilipokuwa narejea kutoka Tehran.

Nakutakia siku njema na utulivu wa fikra.

MZEE MWANAKIJIJI;

Haya umepata jibu lako kuhusu Balozi wako! ndio ulitaka kusema nini vile!
 
Back
Top Bottom