Wickama, mimi nimewekwa kwenye "shit list" ya
Mohamed Said na sasa nadokezwa kuwa na
gombesugu naye anatayarisha "shit list" yake, nitashangaa kama sitakuwamo humo.
gombesugu anadai kuwa Mohamed Said ametufunza mengi hapa tulokua hatuyajui.
Masikini
gombesugu, hajui kwamba ni
Mohamed Said ndiye kapata funzo humu...kwake historia sahihi ilikuwa ni ya "
wazee wangu" mpaka pale tulipomuelimisha kuwa "
wazee wetu" walishirikiana bila kubaguana kwa misingi yoyote ile.
Kwa aliyefuatilia kwa karibu huu mnakasha na mingine iliyopita ataweza kutambua mara moja hii chuki ya
Mohamed Said kwa Mwalimu Nyerere ni matunda ya simulizi alizozipata kutoka kwa wazee wake. Kama ni kweli baadhi ya madai ya Mohamed Said yanatokana na simulizi kutoka kwa hao wazee wake, ni wazi kuwa walisononeka walipotambua mapema kwamba hawakufikia kiwango cha uwezo na sifa alizokuwa nazo Mwalimu.
Nachelea kusema kwamba kutokusikika kabisa kwa Abdulwahid Sykes baada ya kuundwa TANU hadi uhuru unapatikana, yawezekana ni kielelezo cha alivyoumizwa rohoni na mwamko wa Watanganyika nje ya Dar es Salaam, mimi namwita Mohamed Said muongo...sababu zangu ni hizi
Ukweli ukipiga hodi, uongo hutokomea!
Uongo! Mwaka 1929 Raisi alikuwa
Cecil Matola.
Uongo! Hiyo ilikuwa TANU ya kufikirika, TANU iliasisiwa 7/7/1954
Uongo! Mwalimu alishaikanyaga Dar miaka ya 1940 na kukutana na wenyeji wa mji kama
Dossa Aziz.
Uongo na upuuzi! Mtu atoke nyumbani kwake kununua kitoweo Kariakoo bila senti mfukoni!!
Uongo! Kwa nini uchaguzi wa kumtafuta Rais wa TAA ufanyike miezi michache baadaye?
Uongo na Upuuzi! Lakini kama inasemekana, aliyekusimulia alikudanganya!
Uongo na upuuzi. EAMWS ilikuwa ina wenyewe hadi ilipovamiwa na
AMNUT!
Uongo, upuuzi na aibu! Huku ni kujikweza, yaani Mwalimu aliyepambana na viongozi wakuu wa dunia kwa nguvu za hoja afyate kwa
Mohamed Said!
Uongo! Kwa nini alipotua Dar baada ya vita hakufanya kweli? Je alikuwa na wadhifa gani AA kabla ya mwaka 1948?
Uongo, thubutu! Mambo ya kujitungia tu.
Loo! Kumbe ndio maana wazee walisononeka! Linalogomba ni uongozi wa nchi!
Alaa kumbe!
Nikiamua kukaa chini na kutaja uongo woote wa Mohamed Said, hili jukwaa halitatosha!
cc.
gombesugu.