Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar

Kaleta amani gani wakati Nyerere kaja Dar es Salaam miaka ya 1950 kakuta wazee wanaishi kwa upendo msome Nyerere hapo juu kwenye maandishi ya blue kama kakuta Mzizima kuna vita.
Hata Kenyatta aliwakuta Wakenya wakiishi kwa upendo lakini aliwaachia misingi ya ukabila. Na Kikwete ametukuta tukiishi kwa amani dini zote ataondoka ametuachia uhasama wa kidini. That is the difference.
 
......Mbona tumeyaongelea yote? Hili la balozi ni muhimu kama ulivyolifanya muhimu katika mada.
Mwiba unatoka ulipoingilia maalim!
 

"Akizungumza na Wabunge wa Jamhuri ya Muungano juu ya mada ya 'Fedha za Damu na Kufadhili Ughaidi', Balozi wa Marekani Tanzania Robert Royall alisema..."

Hii ni tofauti na kusema

"Akihutubia Bunge la Jamhuri ya Muungano juu ya mada ya 'Fedha za Damu na Kufadhili Ughaidi', Balozi wa Marekani Tanzania Robert Royall alisema..."

"Kuzungumza na Wabunge" kunaweza kufanyika katika setting mbalimbali. Inaweza kuwa katika semina (kama hili) au katika nyumba ya mtu huko Dodoma n.k Lakini pia haitoi uzito wa "Bunge' kwa sababu kuzungumza na wabunge tu kunaweza kuwahusisha wabunge wawili, kumi, ishirini au hata Bunge zima.

Lakini "kulihutubia Bunge" ni zaidi ya kuzungumza na Wabunge. Ni kuzungumza na taasisi ya Bunge ambayo ni mojawapo ya Mihimili ya Serikali yetu. Ni sawasawa na kusema Balozi huyo aende Ikulu na kumpa Kikwete somo kuhusu hilo somo hapo juu na mtu aandike "Balozi wa Marekani Amweleza Rais juu ya..."

Uzito ambao M. Said amejaribu kuuweka kwa kudai kuwa Balozi wa Marekani amezungumza na Bunge - kitu ambacho hakikufanyika - ni mojawapo ya majaribio yake ya kupindisha na kupika historia ili kutimiza malengo yake ya kidini, yaani uchonganishi.

Kama lugha hapa bado inakupiga chenga naweza kukusaidia tena zaidi mkuu wangu.
 
Sasa ukiwa na mashaka wewe ni nani? Unataka kulazimisha vitu. Barubaru usiyamwagie maji ----- wazee wanaoga.

ahli yangu Ritz punguza jazba nakumbuka kipindi kile nipo skuli tulikuwa watulivu walimu wakiwa wanatupa darsa.

Usihamaki sana al akhiy tuendelee kuwa watulivu kwa maana hii ni kama skuli.

Ni darsa tosha kama darsa ya uchumi sema katika taaluma ya uchumi siasa haitakiwi kuingia

tuendelee na mnakasha, ukweli siku zote huwa unauma.
 
Last edited by a moderator:
 
Last edited by a moderator:
Mohamed Said umesema intelligence report za akina Sykes etc ziko wazi hivi sasa Rhodes House,nategemea kuwa Oxford this weekend and i will peruse through the reports-trust me no stone will remain unturned-hatuwezi kukuachia scott free na hii wholesale brainwashing of unstable heads
 
Last edited by a moderator:
Barubaru inaweza kuwa wewe umeona kiswahili kina mapungufu pengine kwa weledi wako au kiingereza hakikueleweka kwa weledi wako.
Hakuna anayekataa uwepo wa balozi maeneo ya bunge kwasababu si yeye wa kwanza.

Kwa jinsi Mohamed alivyoiweka, wale watu wa Ibadan walishangaa kuona balozi amepewa hadhi kiasi hicho.
Labda unikumbushe, Dr Salimin Amour komandoo alihutubia lini bunge la JMT!

Wilcard amesema kuwa hana kumbu kumbu za balozi yoyote kuhutubia bunge na sikumbuki balozi yoyote.
Mohamed ameiweka hiyo akifahamu kuwa watu wa Ibadan Nigeria hawawezi kuwa na muda wa kutafuta taarifa za nchini kwetu ndogo kama hizo wakati huo akilenga kundi analolitaka la ''kumeza'.

Yeye amekubali kuwa taarifa hiyo aliipata mahali kadhaa na bila kuifanyia tahmini akaibeba kama ilivyo.
Kilichomsukuma ni utamu wa taarifa hiyo uliopelekea yeye kuibeba nzima nzima kwasababu ilikuwa ni sensational news.

Nikukumbushe kuwa huko nyuma Mohamed aliwahi kutueleza kuwa maulidi ya Tabora 1988 yalihudhuriwa na makamu wa Rais bw. Kawawa. Hapa napo alitaka kuonyesha umuhimu wa tukio hilo kwa kutumia jina la makamu wa rais.

Ndivyo alivyoitumia hotuba ya Rehani Waikela(moto wa waislam) ukiwaka katika kuleta hisia kwa kizazi hiki kuwa moto unaweza kuwashwa. Akazidi kumnanga Nyerere kwa kisa cha Warioba asiyejulina na bila credential kuwa waziri mkuu.

Hebu pitia alichoandika Mohamed na kule alikonukuu habari hiyo ya Ibadan.
Utaona wazi kuwa amepindisha ukweli kwasababu Mohamed anakijua kiingereza sidhani kama angelifanya kosa kubwa kiuandishi kama hilo. It was a calculated move to instigate the public.

Huyu ni mtafiti ambaye paper na vitabu vyake amevifanyia utafiti kama anavyodai na vimehaririwa kwahiyo vipo sahihi na si muhimu JF free for all kuvifanyia critic kama anavyodai.

Sasa hapa ndipo tunauliza, je, kabla ya kwenda Ibadan alifanya kautafiti kujua bunge letu linakaa wakati gani na lina taratibu gani katika uendeshaji wake! Hata forgery zina taratibu zake, huwezi andika cheque terehe 37 April 2013!!

Hili linakwenda mahali ambapo mtu atajiuliza, hivi yale yaliyoko kwenye shajara za familia ya Sykes yamechukuliwa kwa uadilifu na ukamilifu wake?

Kama haiwezekani kupata kumbu kumbu za mwaka 1988 au 2003 kwa usahihi, usahihi wa kile tusichokiona kinachosemwa ni ukweli mtupu unatoka wapi.

Hata pale alipoelezwa kuwa huenda ilikuwa semina, Mohamed kwa ima kutojua au kwa jeuri ya kuwa na vitabu katika vyuo mbali mbali alikuja kwa jeuri, bunge lilikaa tarehe kadha wa kadha!

Siyo suala la ubishi au kuchukua phrase moja na kuifanya mada, ni suala la validity and integrity za information zake ambazo hakuna shaka kuwa zinamuondolea msomaji yoyote mashaka juu ya maandiko ya Mohamed.
 

Son of Alaska,
Hilo ni jambo jema sana.

Mimi sina cha kuficha katika maandishi yangu.
Usiishie katika hizo Intelligence Report kuna mengi hapo ya wazalendo wa Tanganyika.

Itakuwa raha kama utaturushia wanaukumbi ili tustarehe pamoja.

Jaribu pia kumtafuta John Iliffe hapo taarifa nillizonazo ni kuwa kwa sasa ni mtu mzima
sana na anaishi peke yake maisha ya kitawa.

Mpe salamu zangu na muombe akuonyeshe ile review aliyoandika kuhusu kitabu changu.
Iliffe anazo baadhi ya nyaraka za Abdulwahid Sykes alizochukua kutoka kwa Daisy.

Itakuwa vyema kama nazo utamuomba akuonyeshe.
 
Hata Kenyatta aliwakuta Wakenya wakiishi kwa upendo lakini aliwaachia misingi ya ukabila. Na Kikwete ametukuta tukiishi kwa amani dini zote ataondoka ametuachia uhasama wa kidini. That is the difference.

Tafsiri yako ya uhasama ni pale Waislamu wanapotumia haki yao ya kidemocrasia kuelezea hisia zao ndani ya jamii. Mlitaka na yeye awashughulikie kwa kuwaua, kuwaweka kifungo cha uraiani, kuwafukuza nchini, kuwanyang'anya mali zao (socialism), kuwakusanya na kuwarundika mahala ambapo hakuna msikiti wa wao kufanya ibada (Vijiji vya Ujamaa) ndio mgemuona si mdini.

Sasa mnahaha kuhakikisha kwamba Mkatoliki anarudi tena madarakani kwa kuwekeza nguvu kwenye CHADEMA ili Slaa achukue nchi na hivyo muweze kupata nafasi nyingine ya kupendelewa na kuendeleza ukandamizaji wenu dhidi ya Waislamu na madhehebu ya dini zingine zisizokuwa Wakatoliki. Mnafahamu kwamba kwa sababu Nyerere hayupo, basi CCM inaweza kumchagua Mkristo ambaye si Mkatoliki kwani wapo wengi tu ndani ya CCM ambao wana uwezo wa kuwa marais.

Mnataka kutuletea Dicteta mwingine (Slaa) kupitia mgongo wa Kanisa ili aje kutumaliza kwani Mkatoliki yeyote yule ana uwezekano mkubwa sana wa kuwa dicteta kutokana na maelekezo kutoka Vatican kama habari hii inavyojieleza WikiLeaks cables confirm collusion between Vatican and dictators - World Socialist Web Site
 
Hata Kenyatta aliwakuta Wakenya wakiishi kwa upendo lakini aliwaachia misingi ya ukabila. Na Kikwete ametukuta tukiishi kwa amani dini zote ataondoka ametuachia uhasama wa kidini. That is the difference.

Jasusi,

Jibu swali Nyerere wakati anatoka Musoma kuja Dar es Salaam alikuta kuna vita au huko alikutoka ndiyo watu walikuwa wakatana mapanga.
 
Last edited by a moderator:
Watu hawaelewi kuwa kuhutubia BUNGE ni tukio la kihistoria. Haliwezi kufanywa na mtu mdogo kama Balozi. Hapa kwetu Tanzania anayeweza kulifanya ni Rais pekee. Makamu wake au Rais wa Zanzibar hata kuingia Bungeni ni lazima azimio la Bunge lipitishwe kwanza. Hata wakiingia humo wanakaa kwa adabu muda wote! Kule Marekani kwenyewe namwona Rais wao anafanya hivo mara moja kila mwaka.

Mzee wetu Mohamed analazimisha liwe hivo makusudi kama alivyolazimisha wazee wake kuwa ni DINI iliwatuma kupigania uhuru wa nchi hii, Mwalimu akawasahau kwa DINI yao,..., huyo ndie mzee Mohamed Said ambaye asipoingia akilini mwako akakusemea, basi atatafsiri ulichokisema kwa namna atavyoona inamfaa kwa agenda iliyo mbele yake.
 

Wild Card,
Basi mnakasha utagota hapo kwenye balozi na bunge au baadhi
ya wabunge.

Huna lolote la kusema kuhusu majibu yangu ya hotuba ya balozi?

Huna la kusema kuwa ingekuwa ni bunge zima sheria ya ugaidi
isingepita?

Au ndiyo kile kisa cha kujenga mlima kutoka kichuguu?
 

Wanajamvi,
Kumekucha!
 
Zali la Mentali ukitaka kuwa muongo mzuri jitahidi kutunza kumbukumbu. Naona kanuni hii wewe imekupita kisogoni. Kudhihilisha haya jaribu kurudia kusoma upumbavu wako hapo juu na huu uliopo hapa chini;
 
Your joined date, 4 April 2013, inaonyesha kuwa umetafuta ID mpya kwa ajili ya mnakasha huu tu, kwa makusudi ya kumwaga CHUKI yako dhidi ya Nyerere!
 

Jojojo sikukatali kwamba mimi ni mjinga kwasababu kwanza mimi elimu yangu ni ya madrasa, kwa taarifa yako katika uislamu huwezi kutenganisha dini na siasa kwasababu uislamu ni dini iliyo kamilika na ni mfumo kamili kwa maisha ya binadamu,masuala ya hukumu yapo masuala ya kibiashara yapo mambo ya mirathi yapo nakusikitikia sana yaani laiti ungelijua nini maana ya uislamu usinge andika hizi pumba lakini kuna jamaa mwenzako kakupa like bila kutumia akili nakuomba usome kwanza uislamu kabla ya shutuma sawa mkubwa.
 
Reactions: Ami
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…