Inawezekana kweli hukuwa na hasira nisamehe ndugu yangu.
Mimi nitafute uhalali wa nini kwa kutaka nini na kwa nani.
Nitafuta kuungwa mkono na nani na kwa lipi?
Hii historia ndiyo ilivyo hivyo hivyo huwezi kuibadili.
Sheikh Hassan bin Amir alikuwapo, Sheikh Suleiman Takadir,
Sheikh Mohamed Ramia, Sheikh Mohamed Yusuf Badi na masheikh wengi tu
walikuwa TANU mstari wa mbele.
Ali Migeyo, Dharura bint Abdulrahman, Mama bint Maalim, Halima Selengia,
Amina Kinabo,Zena Maua, Abdallah Rutababzibwa, Sued Kagasheki, Hawa
Bint Maftah, Tatu bint Mzee, Shariffa
Bint Mzee Msham Awadh, Rajab Sisso...
Hawa hamuwajui lakini walikuwapo na walikuwa mstari wa mbele kupambana
na ukoloni.
Baraza la Wazee wa TANU lilikuwapo na walikuwa Waislam watupu.
Haya yote ni ukweli wa historia haukwepeki.