Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar

Kadogoo,
Yule alikuwa akiitwa Malekia ambae alikuwa akivaa sare za jeshi
nadhani ni huyu unaemkusudia.

Kadogoo; Nimekulia Moshi. Mzee Malekia wakati tunakua (tukiwa wadogo) tuliambiwa alirukwa akili through mambo ya WWII (vita kuu ya Pili). Walikuwa yeye na mwingine anaitwa Micheal (huyu alikuwa amejaza misuli na mara nyingi akijishughulisha kwenye bustani ya manispaa au mara nyingine utamkuta karibu na mnara wa saa. Mzee Malekia binafsi nilimwona akitunza sana mabustani na maua pale kwenye mnara na alikuwa akikukuta unatupa takataka ovyo basi ni yeye na wewe. Lakini pia ilikuwa ni baadhi ya siku. Siku zingine ndizo hizo alizokuwa anavalia zile sare za Jeshi na Kutembea mjini amebeba misalaba, au baadhi ya kama zana. The last time i was in Moshi niliuliza sana habari zake (huu ni mwaka jana around
around april). Niseme kuwa nilijawa na utata kama yupo hai au keshakufa, huyo niliyeonyeshwa kuwa ndiye Malekia nilimkuta jirani na duka moja yanatazamana na soko kuu lakini huu upande unaozitizama TAXI. Hakuwa yule wa zamani (kama ni yeye). Huyu alikuwa mchafu, mchovu, hoi, kalala kwenye baraza ya hilo duka hapo nje. Nilijizuia sana kulia pale mbele ya wenzangu. As tiny boys we loved this Mzee so much. Mzee Maiko niliambiwa alishafariki.
 
Jasusi
Mbona picha niliyoipata kutoka kwenye simulizi za Mohamed Said ilikuwa kama vile maamuzi ya Rais Mwinyi yalikuwa yakifuata "alichotaka" mkatoliki Nyerere? Au hata Mzee Kitwana Kondo naye alikuwa mkatoliki?!ΒΏΒ‘?
Nanren,

..inategemea unataka kujenga hoja gani.

..zaidi, yote hayo ni katika kukoleza hoja husika.

..kwa mfano, kuna waandishi wanadai kwamba CCM maana yake ni Catholic Church Movement!! hiyo ni ktk kujenga hoja kwamba Tanzania tunatawaliwa na mfumo Kristo.

..mfano mwingine ni ile hoja ya MOU. ili hoja hiyo ikolee anayetajwa ni Lowassa peke yake. Raisi aliyekuwa madarakani wakati huo hatajwi. Mawaziri wengine ambao wakati huo wizara zao zilikuwa zinaguswa na uamuzi huo hawatajwi.

..wanaofanya hivyo they know what they r doing. wanajua kwamba walengwa wao hawana muda na uwezo wa kufuatilia na kuhakiki madai wanayoyatoa.

cc: Jasusi, Wickama, Nguruvi3, Mag3



..
 
Last edited by a moderator:
platozoom
Ni kweli unayosema.
Kuna stories nyingi sana za vijiweni ambazo mtu anaweza kuzisikia zikirudiwa rudiwa, na hadi anazeeka anafikiri ni kweli.
Siku moja nilikutana na mzee mmoja pale Morogoro akawa anashupalia kuwa India na China zilipigwa marufuku kushiriki mashindano ya mpira kimataifa eti kwa vile wahindi wachawi, mshambuliaji anaweza akapiga shuti kipa akaona mipira mitatu, akidaka huu, mwingine unaingia-gooaal. Eti wachina wanafanana sana kiasi kuwa wanaweza kubadilisha timu nzima. Mzee alikomaa na hiyo story, pamoja na mimi kumhakikishia kuwa nimekaa kwenye hizo nchi, na ukweli ni kuwa, hawajui tu mpira wa miguu, na sio hobby yao.

Mimi huwa napenda kupita pita kwenye hivi vijiwe vya mjini. Basi siku nyingine nikasikia mtu anadai eti ukanda wa pwani, kuna mafuta mengi sana, ila hatuwezi kuchimba kwa vile mwamba wa mafuta ndio huo huo umefika uarabuni, kwa hiyo waarabu watakosa mafuta sisi tukichimba, na huwa wanatupa pesa nyingi ili tusichimbe.

Siku nyingine nikasikia mtu anang'ang'ania story za uongo kuhusu Mzee Mwinyi, eti alioa mtoto wa Kitwana Kondo (ambaye alisoma Jangwani sec). Hizi stori zote zinasimuliwa na wazee wa makamo humo vijiweni, na watu wanaamini. Kwa hiyo si ajabu mtu akija na mihasira yake (na "ha ha ha ha" nyingi za kinafiki) akidai stori zake za kijiweni ndio ukweli mtupu. Na sisi tutaendelea kuhoji mantiki na consistency and logic katika hizo simulizi. Waache watukane tu...
 
Last edited by a moderator:
Basi hata wangekuwa na some humility, wadanganye tu, lakini wasilazimishe kwa ubavu.

Mtu anakueleza kitu kisicho na logic, halafu ukihoji, anakuwa mkali na matusi juu. Mara akuite wewe ni mkristo, wewe Chadema, Nyerereist, mara ooh "mnamwona Nyerere ni Mungu wenu", "Mnafikiri Nyerere alikuwa hakosei", na maneno mengine mengi yasiyo na tija. Hata tukirudia mara kadhaa, kuwa Nyerere alikuwa ni binadamu na alikuwa na mabaya yake na mazuri yake, wao watasema tunamtetea tu. Ukweli ni kuwa haiwezakani Joka Kuu uibe kuku, basi ndio tuanze kukupakazia kila kitu, kwamba ulibaka, uliua, ulitesa n.k kisa tu eti kwa sababu tunakuchukia kwa kuiba kuku. Hivi si ajabu jamani, mijitu inapozusha kuwa tulipigana vita ya uganda kwasababu tulitaka kumwondoa muislam??

Na je si unafiki, kukiita chama cha mapinduzi Catholic church movement at one time, and the other time, unajifanya unapambana na mfumo katoliki, wakati mwingine, unakipigia kampeni chama hicho hicho ili kishinde uchaguzi, na baadaye unaomba uongee na serikali hiyo hiyo inayoongozwa na catholic church movement eti wakuondolee dhulma?
 

Na pia inategemea mahali na au uhusika.
Kwa mfano mwandishi atasema Nyerere aliwatia ndani huyu na yule (hapo kama waliotiwa ndani watu wa Imani yake), Serikali haitamkwi wala Waziri wa mambo ya ndani hatajwi kwa sababu ni wa Imani yake.

Baadaye kwenye mtiririko huohuo itasemwa Serikali imefanya baya hili na lile lakini Mwinyi hatajwi kama Rais. Baadaye
atasema Polisi wanawanyanyasa watu wa Dini yake lakini IGP hatajwi.

Ndiyo hapo mwandishi huyohuyo anakwambia CCM ni Catholic Church Movement lakini anawashawishi waumini wenzake waichague, ajabu hiyo Catholic Church Movement ina Ndugu zao ambao ni Viongozi kuanzia juu kabisa mpaka wa matawi.

Na kwa mantiki hiyo Mwenyekiti wa Catholic Church Movement (CCM) ni Askof, Makamu wake Askof Msaidizi, Katibu Mkuu ni Kiongozi wa Walei..........na hao wengine Viongozi wa mitaa ya Kipata, Mtendeni, Kisutu, Gerezani n.k ni Maparoko!!!

Kabla sijasahau MS pia anaita Polisi - Church Armed Wing wengine mtanisaidia Kiongozi wake wa juu tumwiteje kwa muktadha huo!!
 

Platozoom,
Inakuwa wepesi unaponyambua ulipendalo kujenga hoja.

Tatizo ni kubwa sana.
 
Mohamed Said
Naomba kukuulizia your personal experience, katika maisha yako toka ukiwa mdogo:
1. Ulishawahi kudaharauliwa na wenyeji wa enzi hizo (wazaramo, waswahili, waarabu na wahindi) ukiwa mdogo, kwa sababu tu ya kuwa mmanyema ambaye asili yake ni bara?

2. Katika interaction yako na wasio waislam, hasa kile kipindi unasoma kwanzia shule ya wakatoliki, na hata vyuo vya serikali, ulishawahi kubaguliwa na kudharauliwa kwa vile tu wewe ni muislam?

Natanguliza shukrani.
 
Last edited by a moderator:
Nanren,
Swali zuri lakini binafsi mno.

Kwanza nikusahihishe kuhusu mimi.
Mimi ni generation ya tatu kuzaliwa Tanganyika.

Babu mkuu wangu alikuja Tanganyika 1880s mwishoni
kama askari wa Jeshi la Wajerumani.

Alikuwa askari katika boma Shirati na hapo ndipo alipozaliwa
babu yangu.

Kwa hiyo kama umekusudia natoka bara hii ndiyo asili yetu.
Mimi nimezaliwa Dar es Salaam na nimekulia hapo.

Kuhusu mie kubaguliwa.
Mie nimebaguliwa kama wanavyobaguliwa Waislam wengine.
 

Mohamed Said
Asante kwa majibu mazuri.
Nilishakusoma siku nyingi kuwa wewe ni mmanyema wa dar kwa hiyo kimsingi wewe ni mwenyeji wa DSM. Hata hivyo bado asili yako ni ya bara sawa tu vijana wa "dot com"ambao ni wachaga, wahaya, wanyamwezi, wasambaa, na wengineo ambao wamezaliwa kizazi cha tatu au cha nne hapo dar, lakini bado tunasema wana asili ya bara hata kama hawajawahi kufika huko. Nilitaka kujua kama umewahi kudharauliwa kwa maneno kama "wakuja" au "mmbara" au "mnyika" n.k

Hapo juu umetoa "blanket statement " kwamba umebaguliwa kama waislam wengine. Je unataka kumaanisha kuwa waislam wote wanabaguliwa na wasio waislam?
Na je ubaguzi upo kwa wasio waislam dhidi ya waislam tu? Hamna kinyume chake? Na hakuna dharau au ubaguzi "within" makundi ya dini?
Mzee, naulizia tu from you own experience...
Asante kwa mara nyingine.
 
Last edited by a moderator:

Nanren,
Umeleta barza nzuri lakini nina hofu kiasi.

Umeniwekea dema unanifananisha mie na
wenzangu kutoka bara...

Unataka niingie demani unitie mkononi.

Lakini huwezi kunifananisha na hao.
Mimi Mmanyema.

Nanren umeyataka mwenyewe usilete ugomvi
wala usigune.

Hayo mengine tuyaache.
 
Hata ungempamba vipi, Mzee Mohamed Said anabakia kuwa muongo wa kutupwa na aliutumia uwongo kinyume na maagizo ya dini yake! Mzee mzima amedharirika hapa!

Mzee Said nimemkuta kwenye mjadala huu na bado yupo anaendelea kuwaelezeni historia ambayo hamtaki kuisikia. Mimi sina hata wiki tatu tangu niingie kwenye mjadala huu. Baada ya kualikwa na Ritz kwa kuni mention ndio nikajua kuna mjadala huu unaendelea. Sasa kwa kipindi hicho kifupi nilianza kwa kuuliza maswali mepesi mepesi kwa kutumia ushahidi wa mleta thread ambaye alianzisha mjadala huu. Aliposhindwa kujibu hoja zangu sikushangaa kwa sababu niliewa kwamba ngoma niliyoipiga ni nzito na hamna mtu yeyote mwenye akili timamu atakayeweza kuijibu. Kumuhakikishia hili nikamueleza kwamba kama wewe hujaelewa ninachosema, waulize washkaji zako (gwalihenzi, nguruvi3, jasusi, mzee mwanakijiji, etc) wakusaidie ninaposema kwamba Nyerere ama ni MNAFIKI au ni CHIZI nina maana gani? Kama ningekuwa nimetukana kwa kuhitimisha mtizamo wangu baada ya kuisoma hotuba ya Nyerere bila kuhalalisha msimamo wangu kwa kutumia hotuba hiyo hiyo iliyowekwa kwenye hii thread, basi timu hiyo niliyoitaja kwenye mabano ingekuwa imeshanimaliza na ningekimbia hii thread bila kuaga. Nasema hivyo kwa sababu nimetukanwa sana baada ya kuelezea msimamo wangu bila ya waliokuwa wananitukana kujenga hoja dhidi ya msimamo wangu kwa nini wana haki ya kunitukana? Wote hao walishindwa kujibu hoja hiyo kwa sababu wangejaribu kuijibu wangeishia kuonekana wao ni MACHIZI zaidi ya Nyerere!!!!!!!!!!!!

Sasa kumuita Mzee Said ni muongo kwa kile alichokieleza kwenye kitabu chake wakati nyie mnashindwa kutetea kile mlichokieleza kwenye thread hii ambacho hakifiki hata robo ya kurasa moja ya kitabu alichokiandika Mzee Said hamuoni kwamba nyie ndio mna matatizo ya ziada?
 

Naona umeamua kutukana matusi kutumia lugha ya Kiingereza (Illitereate) kwa sababu akili yako ya panzi inavyokutuma ni kwamba yatapunguza ukali wa matusi uliyoamua kutukana watu ukitumia lugha ya Kiingereza!!!!!!!!!!!!! Cha ajabu ni kwamba nyie ndio vinara wa kusema mmetukanwa hata neno Shanginghi likitumika wakati neno shangingi kwa asili yake hasa ni gali la kifahari!!!!!!

Sasa turudi kwenye mada yako. Joka kuu alishangaa kwa nini Songambele awe juu ya Mwinyi? Jasusi akamjibu kuonyesha kwamba ni kweli Songambele alikuwa juu ya Mwinyi. Sasa hawa mbona ukuwaweka kwenye kundi la "illiterate" badala yake ukaamua kuwa target Waislamu peke yao?

Ukishindwa kujibu hoja usitegemee kwamba utakuwa na uwezo wa kuzunguruka vichwa vya watu walewale ambao umeshindwa kujadiliana nao kwa hoja. Suluhu pekee ni wewe kujibu hoja zilizokuwepo mbele yako na sio kutafuta upenyo wa kisanii kutafuta uhalali wa wewe na washirika wako kuendelea na mjadala ambao technically mmeukimbia!!!!!!!
 

Hittler had a generation that directly served under him including Catholic Church. They were par-excellence her working force!!!!!!!!!!!!! That is why Germany is so much behind super powers in contemporary world!!!!!!!! Need I say more?
 

Tumetoa ushahidi hapa kwamba Nyerere alikuwa ana report mpaka kwa viongozi wa Kanisa Katoliki Vatican kuwathibitishia kwamba Kazi waliyomtuma ya kuwapendelea Wakatoliki dhidi ya dini na madhehebu mengine yote ya dini ya Kikristo alikuwa anaifanya kikamilifu na akawatuma watu wapeleke ujumbe Vatican. Bila shaka wale waliotumwa na Nyerere walitumia kodi ya Watanzania wote kusafiri mpaka Vatican kupeleka ujumbe kutoka kwa Nyerere!!!!!!!!!!!

Sasa huoni kwamba Nyerere alivuka zaidi ya mpaka huo wa Africa Mashariki na akaunganisha mfumo Katoliki mpaka Vatican?
 
Naenda kupumzika. Tutaonana siku nyingine. Kazi ya kuchimba chumvi ni ngumu kweli kweli si mchezo!!!!!! Ila tutaendelea kuwekana sawa mpaka kieleweke!!!!!!!!!!!!
 
Tatizo la nyie mnaomwabudu Mohamed Said ni kwamba mmejinyima wenyewe uwezo wa kufikiri na kujenga hoja zenye mashiko, mnaishia kumshangilia Mohamed tu hata kama anasema uwongo wa kukithili. Imeoneshwa waziwazi hapa jamvini uwongo wa Mohamed... Mohamed anasema balozi wa Marekani aliwahi kulihutubia bunge, jambo ambalo sio kweli, akadai Kawawa alikuwa makamu wa raisi mwaka 1988, nalo halikuwa kweli, kwamba Warioba alipewa u waziri mkuu wakati alikuwa hajulikani, nalo hili imedhihilisha kwamba haikuwa kweli, Kwamba Malima ndie alieanzisha namba za mitihani NECTA, halikadharika haikuwa kweli. Tumwiteje mtu asie sema kweli kama sio muongo!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…