Yericko Nyerere
JF-Expert Member
- Dec 22, 2010
- 17,005
- 20,425
- Thread starter
-
- #1,341
Mie nimefunguka leo!
Si nimeeleza kuwa nina series za Africa Events katika 1980s
magazeti yalikusanywa yakachomwa moto!
Unasema leo nimefunguka!
Nisome kwa utulivu.
Jifunze kunisoma katikakati ya mistari.
Unajua kusoma maandiko magumu?
Unaweza kujifunza.
Mchukue Chaucer kwa kuanzia au Shakespeare.
Faida kubwa utapata.
Ukitaka kuwa mpigaji guitar mzuri jifunze ''cromatics.''
Usijifunze kupiga nyimbo.
Ukitaka kuwa mchezaji mzuri wa mpira jifunze kupiga danadana.
Mpira usiguse chini.
Yericko Nyerere,
Tupo kwenye huu munakasha toka post ya #1 usitafute pakutokea usitake kumuwekea maneno mdomoni Mohamed Said.
Hakuna sehemu yeyote ambao Mohamed Said kamkosea heshima Mwalimu Nyerere kuyasema hayo maneno ya kuvaa kaptula.
Mohamed Said ni muungwana sana anafanya mijadala bila kejeli wala dharau hata kama akubaliani na mtu.
Mkuu nakumbushia tupe jibu basi la waasi waliosamehewa na Mwalimu Nyerere.
Yericko mdogo wangu.
Mimi siwezi kukosa adabu nifike mahali pa kusema maneno
kama hayo.
Nyerere ni umri wa baba yangu kwa hiyo ananizaa.
Sisi Waswahili mama zetu wametufunza adabu lau
kama kuna watu nunda hawasikii.
Mimi siwezi kuingia katika majibishano yasiyo na maana kama hayo.
Hili swali limelitolea kauli hapo nyuma.
Inalelekea Yericko wewe ni kuandika, kuandika, kuandika tu husomi
hutafakari.
Nakuomba hebu kwa dakika moja nifikirie kwa dhana njema.
Soma hapa chini:
''Hayo maneno yanasemwa sana lakini watu wanapoghadhibika.
Ni kukosa adabu na ustaarabu kutoa maneno kama hayo ya
kudhalilisha watu.
Kila mahali watu kama hao wasema ovyo huwezi kuwakosa.
Uniform aliyokuwa akivaa Abdu Sykes kama Market Master
pale Sokoni Kariakoo ilikuwa kaptula stockings na shati jeupe.
Waafrika wengi walikuwa wakivaa hivyo haikuwa kioja kwa
Nyerere.
Lakini kama ulivyosema akutukanae hakuchagulii tusi.''
Yericko Nyerere,
Tupo kwenye huu munakasha toka post ya #1 usitafute pakutokea usitake kumuwekea maneno mdomoni Mohamed Said.
Hakuna sehemu yeyote ambao Mohamed Said kamkosea heshima Mwalimu Nyerere kuyasema hayo maneno ya kuvaa kaptula.
Mohamed Said ni muungwana sana anafanya mijadala bila kejeli wala dharau hata kama akubaliani na mtu.
Mkuu nakumbushia tupe jibu basi la waasi waliosamehewa na Mwalimu Nyerere.
Mohamed ndio maana kuna akina James H. Chase, Mario Puzo n.k.Usinihukumu wewe kwa kauli hiyo ya kusema ''hamuwezi.''
Waachie wanaukumbi wahukumu kama hilo ni tusi.
Narudia kusema tena hamuwezi.
Laiti mngekuwa na historia ya kuandika mfano wa hii ya wazee
wangu kitabu kingekuwa tayari kipo mitaani.
Lakini nakuapia hamuwezi kwa kuwa hamna cha kuandika.
Huwezi kuandika kile kisichokuwapo.
Swali...imedaiwa na Mohamed Said kuwa wazee wake hawakumfahamu kabla ya kukanyaga Dar es Salaaam mwaka 1952, je ni mwaka gani Dossa Aziz alikutana na Mwalimu Julius Nyerere kwa mara ya kwanza?
Mohamed ndio maana kuna akina James H. Chase, Mario Puzo n.k.
Ni kweli kabisa ni ngumu kwa watu wengine kuandika kitu katika ''genre'' isiyokuwepo.
Mfano mtu ataandikaje Non-Fiction na Fiction kwa wakati mmoja?
Hivi Mohamed, wale Wapare waliopambana na mkoloni wao hawakushiriki katika mapambano ya uhuru?
Pili,kuna post yako umetaja majina ya akina Abdu Sykes, Nyerere, Mhando, Dunstan Omar, Dosa Azizi na wengine ukasema walikuwa wanakaa katika barza ya mtaa wa Stanley kujadili Mustakabali wa Tanganyika.
Narudia, Mstakabali wa Tanganyika.
Hapo nyuma ukurusa wa 67 umesema baraza la TANU lilikuwa na Waislam watupu.
Halafu kuna mahali umetaja wazee wako wasiotajwa lakini walishiriki sana kwasabau ya uislam.
Katika idadi ya wazee wako sijaona jina la Vedastus Kyaruzi hata kama aliwahi kuwa kiongozi mkuu wa chama kwa nyakati fulani. Sijaona jina la Paul Rupia au Boman achilia mbali akina Matola n.k.
Hivi huoni kuwa kile unachokipinga ndicho unachokifanya kama Mwanakijiji alivyowahi kusema?
Kwamba unaacha majina kwa mtindo ule ule wa wazee wako kusahulika.
Hivi mtoto wa Bomani au Rupia kweli anaweza kusoma kitabu chako na kuhisi wazee wao wameheshimiwa?
Lakini pia hebu tueleze, Abdul Sykes aliwahi kwenda lini Songea kukutana na Ali Songea Mbando.
Lini aliwahi kwenda Mbeya au Kilimanjaro? Kama hakuwahi kwenda( na assume tu) unawezaje kuandika historia ya wazee wako waislam halafu ukasema ni ya Tanganyika?
Tatu, umesema Abdul Sykes alimtaka sana Nyerere kwa usomi wake. Wakati huo huo unasema alitoka kijijini na hakuna aliyemjua hadi kufundishwa kuvaa ''nguo''.
Tena siku za nyuma uliweka picha ya kuonyesha jinsi alivyokuwa na kaptura.
Well, Labda nikuulize wakati Nyerere anaingia Dar es salaam yeye na Mshume Kiyate nani alikuwa na ufahamu zaidi wa dunia hii?
Nne, hivi wakati Nyerere anaingia Dar na kuingizwa katika siasa na Abdul, ina maana alikuwa hajui lolote kabisa kuhusu siasa?
Samahani hizi ni hoja na sikuona namna ya kuzipanga kwa namna unayotaka. Twende hivyo hivyo ilimradi kila mmoja aelewe na aweze kujibu au kutoa maoni. Natumaini pia hakuna neno ngano mahali popote na hutakwazika.
Inshallah Mzee Said ukumbi wako.
Huko Dodoma, mwaka 1946 Nyerere alifuata nini na alihudhuria kama nani.Julius Nyerere alikutana na Dossa kwa mara ya kwanza 1946 Dodoma kwenye mkutano wa African Association.
Kama sijui si ndio wakati unjiuze?Nakushauri usome kitabu changu.
Inaelekea hujakisoma kitabu changu maana ungesoma usingesema
hayo yote.
Sasa hatuwezi kujadili kitu ambacho wewe hukijui.
Wanaukumbi hili swali nisaidieni na nyinyi kujibu.
Hakuna mtu aliyekuwa anamjua Nyerere katika siasa za Dar es Salaam hadi Abdu alipomleta ofisi ya TAA New Street. Hiki wala si kitu cha kificho watu wote wa Dar es Salaam katika harakati zile za 1950 wanajua.
Bado unasimamia kauli yako kuwa safari ya kisiasa ya Nyerere ilianzia 1953? na aliingizwa katika siasa na kina Sykes? Kabla ya kuja Dar Nyerere aliwahi kuanzisha taasisi au chama chochote kwa ajili ya kupigania maslahi ya waafrika? au kujaribu kujiingiza TAA kabla ya kukutana na Sykes na wazee wa Dar?
Amazing!
Hapana inawezekana huko alikotoka alifanya makubwa. Lakini kwa Dar es Salaam ambako ndiko hasa siasa zilikuwa kali hakuna aliyepata kusikia jina la Nyerere.
Swali...imedaiwa na Mohamed Said kuwa wazee wake hawakumfahamu kabla ya kukanyaga Dar es Salaaam mwaka 1952, je ni mwaka gani Dossa Aziz alikutana na Mwalimu Julius Nyerere kwa mara ya kwanza?
Ukiwa muongo na mchochezi, yabidi utunze kumbu kumbu.Julius Nyerere alikutana na Dossa kwa mara ya kwanza 1946 Dodoma kwenye mkutano wa African Association.
Mzee Mohamed Said inaonyesha kitabu chako baada ya kusimuliwa na mtu mmoja tu wa ukoo wa akina Sykes ukaenda kujifungia ndani tayari kwa kuandika kitabu
Ni kweli Dar es Salaam kwa wakati huo wa harakati za kudai uhuru ilikuwa "predominantly Moslem" lakini pia tusisahau kuwa idadi ya wakaazi wa Dar es Salaam ilikuwa ni chini ya watu 120,000 (laki moja na ishirini) wakati idadi ya Watanganyika ilikuwa zaidi ya watu 8,000,000 (milioni nane!) Hivyo pamoja na TANU kuanzishwa Dar es Salaam, ili iweze kuonekana inawakilisha Watanganyika, ilibidi wapatikane watu kutoka nje ya Dar es Salaam kama Chief Abdallah Said Fundikira (Jimbo la Magharibi), John Ketto, Nesmo Eliufoo (Jimbo la Kaskazini), John Mwakangale (Jimbo la Nyanda za juu Kusini), Lawi Sijaona (Jimbo la Kati), Paul Bomani (Jimbo la Ziwa) na George Kahama (Jimbo la Ziwa) na kadhalika. This was just common sense stepping in.
Hawa watu hawakuokotwa tu, tayari walikuwa viongozi, wasomi na wenye ushawishi mkubwa katika sehemu walizotoka na watu waliwakubali bila kujali dini zao. Kwa jinsi ile ile Mwalimu alivyoweza kuchaguliwa kuwa Raisi wa TANU ndivyo hivo hivyo kiongozi wa kwanza wa tawi la TANU Moshi Jimbo la Kaskazini alichaguliwa Muislaam Mzee Yussuf Ngozi katika eneo ambalo lilikuwa "predominantly Christian" Hatukatai kuwa watu kama Abdulwahid Sykes hawakutoa mchango mkubwa katika harakati za wakati huo, tunachopinga ni upotoshwaji wa makusudi wenye lengo la kupandikiza chuki na uhasama unaofanywa na mchochezi Mohamed Said.
Naomba kwa ufahamisho tu nidokeze kuwa Mohamed Said ni mdogo sana kwangu kiumri na hivyo wakati mambo mengi anayohadithia ni ya kusimuliwa, mimi mengi niliyashuhudia kwa macho yangu. Kati ya waliosisi TANU, tisa kati ya 20 walikuwa wakazi wa Dar es Salaam, lakini wako pia ambao pamoja na kushiriki kikamilifu walikuwa kwenye utumishi ndani ya serikali ya ukoloni na haikuwa rahisi kujitokeza wazi wazi. Katika njama zake Mohamed Said anachanganya mambo mawili...UdaresSalaam na Uislaam na mpaka wakati atakapoweza kufunguka macho na kutenganisha tofauti hii, maandishi yake kwetu wengine yatabaki kama porojo tu.
Sasa wanajamvi, hebu angalieni huu mtiririko;
Ukiwa muongo na mchochezi, yabidi utunze kumbu kumbu.
Kwa nini Julius Nyerere alihudhuria mkutano wa African Association Dodoma mwaka 1946? Kama nani? Akitokea wapi? Je, hakuna mjumbe/wajumbe kutoka Dar es Salaam aliyehudhuria/waliohudhuria mkutano huo? Kama wapo inakuwaje mwaka 1952 (miaka sita baadaye) unadai hakuna hata mmoja kati ya wazee wako wa Dar es Salaam aliyewahi kumsikia Julius Nyerere? Kwa nini unadai kuwa safari ya kisiasa ya Nyerere ilianzia 1953? na aliingizwa katika siasa na kina Sykes? Je uko tayari kukiri kuwa ujio wa Mwalimu ndiko kulileta mwamko, msisimko na mawazo mapya ndani ya TAA? Je uko tayari kukiri uwongo ambao umekuwa ukiueneza kwa chuki kwa watu ambao hawaijui historia sahihi? Do you know even the meaning of the word "truth"?Si kama kuniita muongo nitatahayari.
Kama muongo si mimi. Waongo watakuwa wazee wangu walionisomesha historia hii...
Mimi hutaniona natoa tena kitu hapa. Mawe yote yameshafunuliwa na ukweli umejulikana. Wajerumani wa ZMO wanasemagaje!? Viel Spass noch...Sweke umenitukana tusi baya sana.
Mimi ghadhabu yangu ni kuwa sitojadili
chochote na wewe.
Kwa nini Julius Nyerere alihudhuria mkutano wa African Association Dodoma mwaka 1946? Kama nani? Akitokea wapi? Je, hakuna mjumbe/wajumbe kutoka Dar es Salaam aliyehudhuria/waliohudhuria mkutano huo? Kama wapo inakuwaje mwaka 1952 (miaka sita baadaye) unadai hakuna hata mmoja kati ya wazee wako wa Dar es Salaam aliyewahi kumsikia Julius Nyerere? Kwa nini unadai kuwa safari ya kisiasa ya Nyerere ilianzia 1953? na aliingizwa katika siasa na kina Sykes? Je uko tayari kukiri kuwa ujio wa Mwalimu ndiko kulileta mwamko, msisimko na mawazo mapya ndani ya TAA? Je uko tayari kukiri uwongo ambao umekuwa ukiueneza kwa chuki kwa watu ambao hawaijui historia sahihi? Do you know even the meaning of the word "truth"?
Na sasa tunaanza kugundua kwamba Dosa Aziz alifahamiana na Nyerere mwaka 1946. Kwa hiyo Nyerere alipokuja Dar-es-Salaam 1952 hakuwa mgeni sana kwa wana harakati. In fact tayari alikuwa mwenzao ila tu kwamba hakuwa mtu wa Dar-es- Salaam. Very interesting.Ni kweli Dar es Salaam kwa wakati huo wa harakati za kudai uhuru ilikuwa "predominantly Moslem" lakini pia tusisahau kuwa idadi ya wakaazi wa Dar es Salaam ilikuwa ni chini ya watu 120,000 (laki moja na ishirini) wakati idadi ya Watanganyika ilikuwa zaidi ya watu 8,000,000 (milioni nane!) Hivyo pamoja na TANU kuanzishwa Dar es Salaam, ili iweze kuonekana inawakilisha Watanganyika, ilibidi wapatikane watu kutoka nje ya Dar es Salaam kama Chief Abdallah Said Fundikira (Jimbo la Magharibi), John Ketto, Nesmo Eliufoo (Jimbo la Kaskazini), John Mwakangale (Jimbo la Nyanda za juu Kusini), Lawi Sijaona (Jimbo la Kati), Paul Bomani (Jimbo la Ziwa) na George Kahama (Jimbo la Ziwa) na kadhalika. This was just common sense stepping in.
Hawa watu hawakuokotwa tu, tayari walikuwa viongozi, wasomi na wenye ushawishi mkubwa katika sehemu walizotoka na watu waliwakubali bila kujali dini zao. Kwa jinsi ile ile Mwalimu alivyoweza kuchaguliwa kuwa Raisi wa TANU ndivyo hivo hivyo kiongozi wa kwanza wa tawi la TANU Moshi Jimbo la Kaskazini alichaguliwa Muislaam Mzee Yussuf Ngozi katika eneo ambalo lilikuwa "predominantly Christian" Hatukatai kuwa watu kama Abdulwahid Sykes hawakutoa mchango mkubwa katika harakati za wakati huo, tunachopinga ni upotoshwaji wa makusudi wenye lengo la kupandikiza chuki na uhasama unaofanywa na mchochezi Mohamed Said.
Naomba kwa ufahamisho tu nidokeze kuwa Mohamed Said ni mdogo sana kwangu kiumri na hivyo wakati mambo mengi anayohadithia ni ya kusimuliwa, mimi mengi niliyashuhudia kwa macho yangu. Kati ya waliosisi TANU, tisa kati ya 20 walikuwa wakazi wa Dar es Salaam, lakini wako pia ambao pamoja na kushiriki kikamilifu walikuwa kwenye utumishi ndani ya serikali ya ukoloni na haikuwa rahisi kujitokeza wazi wazi. Katika njama zake Mohamed Said anachanganya mambo mawili...UdaresSalaam na Uislaam na mpaka wakati atakapoweza kufunguka macho na kutenganisha tofauti hii, maandishi yake kwetu wengine yatabaki kama porojo tu.
Sasa wanajamvi, hebu angalieni huu mtiririko;
Ukiwa muongo na mchochezi, yabidi utunze kumbu kumbu.
Huko Dodoma, mwaka 1946 Nyerere alifuata nini na alihudhuria kama nani.