Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar

Islam gani huyu wa Upanda. Au yule mwenye duka opposite Msikiti Ngazija.

Anayeishi Ali Khan street


Barubaru,

Salaam.

Sina hakika huyu unaemzungumzia wewe. Nimjuaye mimi ni Bwana Islam jamaa zao kina Prof. Abdilrahman Babu. Mara ya mwisho nakumbuka akikaa pale Maweni Str. Upanga na alikua na Madrassa. Hiyo ya duka ni kweli,lakini nikumbukavyo duka lake lilikua ubavuni pa Al Masjid Maamur pale Malik Road Upanga.

Ni mtu mwenye bashasha mno. Nakumbuka kuna siku nilkwenda kwake kumfuata Sahib yangu mwanae Eddy Islam. Nilipobisha hodi akanifungulia yeye Sheikh Islam mwenyewe. Nikamwamkua,na nikamuuliza je Sheikh Eddy nimemkuta!?
Japo akinifahamu uzuri,lakini akanijibu;kumradhi Bwana mdogo labda umepotea njia maana huyo "Sheikh wako" Eddy hakai humu. Maana humu ndani kuna Sheikh mmoja tu,na ndie mimi.
Nami sikumwacha,nikamjibu kama Sheikh Mathias Mnyampala ali-qualify kuitwa Sheikh basi namimi kwanini nisimwite ndugu yangu Eddy Sheikh!?ahaha!! Wallahi,alicheka mno...akanambia wewe ulikua mtulivu lakini sasa umekua Maluuni saana!ahaha!!

Pale Ally Khan,kama uliwahi kuishi pia palikua na yule Mzee mstaarabu mno wa Kihaya...Mzee Bulengero,lakini alifariki kitambo maskini.
 

Zali la mentali "utamshukia kama mwewe" ha ha haa...baereze baalewe wengi wameshaingia mitini CHEZEA MCHIMBA CHUMVI
 
Gombesugu,
Dk. Amour Abdallah Amour amefariki jana usiku Dar na kesho
Maziko Unguja.

Inalilah wainailaihy rajiun.

Sheikh Mohammed,

Asalaam Alaykum. Ahsanta kwa kunijuza khabari ya msiba huo mzito kwetu soote. Nimepata simanzi mno.

Tuliwahi kupata khabari mapema hapa,maana yule Aunt yangu ambae yupo hapa kwa mapumziko kiduchu alipigiwa simu toka Unguja. Inna Lillahi Wa Inna Illahi Rajiun.

Vipi Dr. Abdalllah Dahoma nae yupo,nipa salaam mno kikutana.

Shukran.
 
Zali la mentali "utamshukia kama mwewe" ha ha haa...baereze baalewe wengi wameshaingia mitini CHEZEA MCHIMBA CHUMVI

Boko Haram,

Asalaam Alaykum Al Akhiy.

Nakufuatilia bayana zako hapa jamvini. Lakini mara nyingi hufurahi unapozungumza hicho ki-Congo.
Taratibu jamaa wasije kukufuatilia makaratasi ya uraia wako!ahaha!!

Ahsanta.
 

Katika swali lako kwangu kuhusu mantiki uliyodai nimeiweka juu ya majibu yangu kwako juu hotuba hiyo, sikukujibu baada ya kubaini kasoro za kiuelewa wa baadhi ya misamiati ya lugha adhimu ya kiswali!

Kwanza ili twende sawa naomba tuwekane sawa juu ya hili,

1) Unajua maana ya MANTIKI na husimama wapi katika hoja?

NB:

Kile nilichokijibu pale awali hakikuhitaji matumizi ya MANTIKI,

Nilipigwa butwa pale ulipohoji kuwa ni mantiki gani niliyotumia kujibu vile!

Napenda mjadala wa adabu na staha,

Haya tusonge ndugu!
 

Kwa wanajamvi wapya hebu msomeni huyu jamaa anavyowatukana wazee wetu.

Cc... gombesugu.
 
Last edited by a moderator:
Boko Haram,

Asalaam Alaykum Al Akhiy.

Nakufuatilia bayana zako hapa jamvini. Lakini mara nyingi hufurahi unapozungumza hicho ki-Congo.
Taratibu jamaa wasije kukufuatilia makaratasi ya uraia wako!ahaha!!

Ahsanta.

Gombesugu, waaleykum salaam ndugu yangu hayo ni maneno tu al akhiy wakinifuatilia sana nafanya hijra mbona mtume alifanya hijra kutoka Makka akaenda madina na kuna maswahaba walikuja mpaka Afrika hapo Ethiopia mimi hilo halinibabaishi mkubwa.
 

Ritz,

Asalaam Alaykum. Wallahi hii Fatwa uloiweka hapa ni nzito kwa wenye kujua. Mimi nilipoiona nalipatwa na kisunzi.

Naomba umsamehe yule Abu Jahal,maana tayari keshadhurika kitambo kama tulivyoona vile vitimbi vyake hapa jamvini. Maana ana maradhwi,na maradhwi yake ni makubwa mno kwa wenye kujua na kutambua.

Ahsanta.
 
Kwa wanajamvi wapya hebu msomeni huyu jamaa anavyowatukana wazee wetu.

Cc... gombesugu.

Ritz,

Alaa! Kumbe ulo "ustaarabu" woote wa Nguruvi3 na Mag3 khabari zao ndo hizi. Lakini haina neno wenzao wanayaona. Tukisema sisi tunaambiwa watu wa Madrassa hatwishi kulalama.

Jana nilimwandikia Nguruvi3,na nilimzungumza khabari hizi za matusi japo kiduchu. Nina imani amenifahamu.

Shukran.

Cc; Ami,Nguruvi3,Mag3
 
Kwa wanajamvi wapya hebu msomeni huyu jamaa anavyowatukana wazee wetu.

Cc... gombesugu.

Kusema ukweli kwenu ni kuwatusi hao wazee/waasi?

Je ni uongo?

Haya nitajie kati ya wanaoitwa wazee wenu ambae aliwahi kuongoza AA, TAA, TANU ama CCM katika ngazi ya Urais au Uenyekiti ambayo ndio ngazi kuu ya uongozi wa kichama!

Narudia tena kukwambia hao wazee walikuwa waasi wa serikali mpya ya Mwalimu Nyerere, na walionja nguvu ya dola huru ya Mwalimu!
 
Last edited by a moderator:

Nguruvi3,

Salaam ndugu yangu. Nalikua napitia baadhi ya majambo hapa jamvini,ndipo ghafla nikakumbana na hii bayana yako.

Yaelekea huo "mkoba wa Ibadan" umekuchoma mno ndugu yangu. Maana huishi kuutaja!?ahahaa!

Ahsanta.
 

Yericko akiongea Mag3 yeye hatukani lakini Zali la mentali akiongea unamwambia aongee kwa staha "mkuki kwa nguruwe"na katika huu mnakasha unajifanya unatetea utaifa lakini si kweli wewe ni "DOUBLE FACE"
 
Yericko akiongea Mag3 yeye hatukani lakini Zali la mentali akiongea unamwambia aongee kwa staha "mkuki kwa nguruwe"na katika huu mnakasha unajifanya unatetea utaifa lakini si kweli wewe ni "DOUBLE FACE"

U double face upo sehemu gani ndugu?

Nguruvi3 ametukana nini hapo?
 
Yerico ameishiwa kabisa na hoja,ndio maana akajitoa kimasomaso kwa kutubembeleza tujadili mradi wake wa kitabu cha ugaidi kinachofadhiliwa na Marekani.Lakini naona watu tumemuelewa bado tunapiga za mgongoni mpaka ainue mikono kuwa hakuna uchochezi wa Mohammed bali ilikuwa ni uzushi wake tu.Na akiri kuwa alitumwa kutaka kupotosha ukweli.
Masheikh zangu wa Upanga,kariakoo na kwengineko endeleeni kumkaba nasi vijana wenu twaona juhudi zenu.Allah tawalipa katika dunia na akhera kwa kutetea ukweli.
 

Katika hotuba yake aliuliza nani wanaongoza TAA baada ya kurudi kutoka masomoni na baada ya kuwa Pugu. Kuuliza suali hilo ina maana alikuwa hawajui ni nani viongozi wa TAA. Sasa alipokuwa Pugu alikuwa amesimama shughuli za siasa za TAA mpaka afikie kiasi cha kutowajua ni nani wanaongoza chama kilekile alichoamua kujiunga nacho tangu yuko Makerere?
 

Sina kinyongo na michango yenu hapa,

Kila hoja hapa inajibiwa sawa na ujazo wake!

Uchezi wa Mohamed Said upo wazi na tumeueleza tangu post ya mwanzo kabisa!

Ikiwa hujauona naomba nikupe kwakifupi tu!

1) AA iliasisiwa na Klest Sykes, Ni UONGO.

Ukweli nikuwa iliasisiwa na mwalimu Cesil Matola

2) Kuwa Mwalimu rejea kutoka Scotland alisema hakumbuki Abdul Sykes alikuwa na cheo gani katika TAA, Ni UONGO.

Ukweli nikuwa mwalimu ameeleza wazi katika hotuba ya muago kwa wazee wa dar kuwa Abdul alikuwa katibu mkuu wa TAA.

3) Kuwa TANU iliasisiwa BAMA na Abdul Sykes, Ni UONGO,
Ukweli nikuwa TANU imeasisiwa tarehe 7/7/1954 pale Mtaa mpya leo pakiitwa Lumumba chini ya Julius Kambarage Nyerere

4) Kuwa Balozi wa USA aliwahi kulihutubia Bunge la Tanzania 2003, Ni UONGO

Ukweli nikuwa balozi wa USA nchini hajawahi kulihutubia bunge la nchi hii, zaidi ya kisemina cha wabunge wa CCM tu cha kushinikiza upitishwaji wa sheria ya ugaidi nchini kilichofanyika kwenye ukumbi mdogo wa Pius Msekwa.

Hayo bado hujaona uchochezi wa Mohamed Said?
 

Yericko,

Sasa huoni yakuwa kuna wakati unajichanganya mwenyewe!? Nahisi hii "definition ya matusi" ni pale tu inapoku-suit wewe!?
Nakukumbusha yakuwa; hapa baadhi yetu tunatoka katika matabaka,makabila,mila,dasturi na tamaduni tafauti.

Hapo awali hapa jamvini palikua na kishindo na kebehi kadhaa dhidi ya Sheikh Mohammed,yakuwa kwanini kataja kuwa Nyerere alikua akisaidiwa kitoweo na Mshume Kiyate na pia kwanini alitaja yakuwa Nyerere alikua hana pa kulala ikalazim asaidiwe chumba cha Abbas Sykes,alikua hana uwezo akitembea kwa miguu tokea Pugu mpaka Kariakoo,akasaidiwa baiskeli na mengineyo machache ambayo hata huyo Nyerere mwenyewe aliwahi kutamka hadharani. Wewe na jamaa zako wengi mlihamaki pasi mfano.

Kama una maarifa,hishma,na mapenzi makubwa mno kwa Nyerere kiasi cha kumnasibisha na Unabii... basi tafadhali nakusihi ndugu yangu punguza nyendo zako. Maana hapa dignity ya huyo Nyerere unazidi kuididimiza kila kukicha.

Unamzidisha ukiwa na machungu hata huyo Mama Maria. Maana hishma na mapenzi yoote alokua nayo kwa Mzazi mwenzie Nyerere,lakini sasa wewe umejitokeza na umeonyesha yakuwa Nyerere kumbe alikua si Mkristo mtiifu wala hakuwa mwanandoa muadilifu na pia alikua na Vimada na umezaliwa wewe mtoto wa nje ya ndoa!?

Ndugu yangu Yericko,kama utatumia ustaarabu japo kiduchu basi wahurumie ndugu zako wa Mama mwingine(Andrew Nyerere na wenzie). Najua wanateseka na kupata uchungu mkubwa kwa jinsi wewe unavyosababisha "kumuanika" Mzazi wao hapa jamvini.

Natumai utanifahamu japo kiduchu.

Tuendelee na mnakasha.

Cc;Ami,JokaKuu,Nguruvi3,Mag3,Barubaru,Jasusi,Boko Haram,Kadogoo,Zali la Mentali,Ritz,The Big Show,Sheikh Mohammed Said,Sideeq,Uthman

Ps;
Nakuhakikishia wewe humjui Rais Nyerere kiundani kama wamjuavyo baadhi ya Wanajamvi hapa! Kumbuka yakuwa Nyerere alikua ni Rais wa nchi,kwa hiyo kuna vitu vingi mno wewe "mwanafamilia" huwezi kuvijua alotenda "Mzazi wako".
 
 

Nikuweke sawa kwenye maelezo yako,

Sio kwamba mwalimu aliishi Pugu ndipo akaenda masomoni, la hasha bali aliishi Tabora ndipo akaenda masomoni na aliporejea ndipo alifikia Shule ya Mtakatifu Frances pale Pugu na alidumu kwa mwaka mmoja tu na nusu kisha akaachana na kufundisha!

Akiwa pugu hajawahi kuwa kiongozi wa chama chochote bali alijihusisha na shughuli za kisiasa kwa kuja kuzifanyia Dar!

Hoja yako kuu ni kuwa iweje mwanachama na kiongozi kanda ya mashariki ya chama cha TAA aliyesafiri nje ya nchi ndani ya miaka mine tu aliporejea akaanza kuulizia wanaokiongoza chama chake kitaifa?

Jibu langu nikuwa, ndani ya kipindi ambacho Mwalimu yupo Masomoni, serikali ya kikolini ilikuwa inavisambaratisha vyama vya harakati za ukombozi,

Hivyo TAA ilikuwa imekumbana na zengwe hilo baada ya rais wake msomi na daktari wa kwanza kabisa Mtanzani Vedasto Kyaruzi kuhamishwa kituo chake chakazi na kupelekwa Kahama,

Katika anga za harakati za kimataifa TAA ilikuwa imeparaganyika.

Ndiomaana msomi na muhitimu wa kwanza wa PHD ya uchumi Tanganyika/Tanzania Mwalimu Julius Kambarage Nyerere aliporejea ilikuwa kwanza kuulizia habari za chama alichokiacha miaka mitatu minne iliyopita!

Na katika kuuliza alianza na "nani wanakiongoza chama sasa hivi?"

Ndipo akaambiwa jamaa mmoja anaitwa Abdul Sykes,

Kumbuka katika kpindi hicho mtu huyu aitwae Abdul Sykes alikuwa si mzoefu kwa siasa za Nyerere zaidi ya Dosa Azizi na wengineo kama Dr Kyaruzi nk!

Bila shaka kwakifupi umenipata na ndio MANTIKI ya hotuba ya Mwalimu Nyerere.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…