Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar

Wewe umeshaonyesha dalili zote za kuwa mtoto si ridhiki kwa kulialia humu jamvini kuomba watu walewale unaowatukana wakusaidie kunidhibiti mimi. Sasa ndio maana naoengea kwa lugha ambayo utaielewa vizuri kwani ndio matendo yako.
Poor imbecile boy! how comes you don't comprehent small things! nobody asked anybody to stop your hooliganism as that is your inborn character! keep on exposing yourself here.
 

Nasikitika sana tena sana!

Umenidhihaki sana mimi na familia yangu!

Sipendi kuingia ndani kujadili masuala binafsi ama ya kifamili yangu kwakuwa si sehemu yake!

Nimesimama katika uzi huu kama mtanzania niliyezaliwa katika ardhi hii na mwenye asili halisi ya nchi hii!

Kwamujibu wa katiba ya nchi hii ninayo haki yakujadili masuala ya nchi yangu yakiwemo ya kisiasa, uchumi, afya nk!

Nimetumia haki hiyo hiyo kumkanya Mohamed Said na kuihabarisha dunia na watanzania wenzangu kile ninachokifahamu juu ya historia ya nchi hii na historia ya waasisi wa Taifa letu! Na kila mmoja wetu anayo haki yakukieleza kile akijuacho kwenye historia ya Uhuru.

Hakuna mwenye haki miliki ya historia ya uhuru wetu, tuulinde ukipotoshwa ama tukiona uchochezi tuukemee kwa nguvu zote!

Sijabeba undugulaizesheni kwenye mada hii ndiomana huko nyuma ya mjadala huu ulizuka udadi huu wa kuiacha mada na kutaka kunijadili mimi, lakini nikawasihi wadau tutulie kwenye mada iliyopo!

Nakusihi na wewe utembee katika hoja kuu ambayo ndio inayotuweka hapa!

Adabu na staha katika mijadala ya lugha adhimu ya kiswahili inamafaa zaidi kuliko kiburi na mawaa!
 

Swali lake halikuwa hivyo kwamba nani wanakiongoza chama sasa hivi. Lilikuwa nani wanaongoza TAA. Ni maswali mawili tofauti kabisa.

Sasa mimi nazungumzia kipindi kile alipokuwa Pugu akifundisha. Hakuwa mwanachama wa TAA? Hakuwa na mawasiliano yoyote na viongozi wa TAA mpaka aje kuuliza suali kama hilo wakati ameacha ualimu na kuja Dar?
 

Unaposema TAA unamaanisha nini zaidi ya CHAMA?

Sasa nikufahamishe upya mkuu,

Hapa sasa ndio matumizi ya MANTIKI kwa msomi hutumika,


Swali hilo aliliuliza pindi tu yakurejea kutoka masomoni Scotland sio baada ya kuacha ualimu,

Isome kwa makini hiyo hotuba utabaini kuwa mwalimu alikuwa akisimulia mapito yake kisiasa na aliposema kuwa aliporejea kutoka masomoni aliuliza nani wanakiongoza TAA?

Hiyo inamaanisha kuwa ni baada tu yakurejea kutoka ughaibuni!

MANTIKI imefanya kazi yake!


Tuendelee mkuu!
 

Kwa nini wewe udhani una haki peke yako na Mzee Mohamed hana? Kwa nini umuite mchochezi na mhaini wakati anatoa mawazo yake kuhusu siasa za Tanzania?
 

Ngoja tumsome Nyerere mwenyewe mimi siwezi kutaja

Hivyo ndivyo tulivyofanya. Kwa hiyo mimi nikawa katibu wa katawi ka TAA hapo Makerere. Niliporudi Tabora na kuanza kufundisha pale St. Marys (sasa inaitwa Sekondari ya Milambo), nikachaguliwa katibu wa TAA wa jimbo ambalo makao yake makuu yalikuwa Tabora. Ulipofanyika mkutano wa TAA mjini Dar es Salaam, nilihudhuria nikiwa mjumbe kutoka Tabora.

Kwa hiyo nilikuwa naijua Tanganyika African Association. Nilipokuwa ninaondoka kwenda Ulaya kusoma, nilikuwa nimeishaonja shughuli za TAA. Sasa niliporudi, baada ya kukaa Pugu siku chache, nikaja mjini Dar es Salaam. Nikauliza nani wanaongoza TAA?
Nikaambiwa kuna jamaa mmoja anaitwa Abdul Sykes. Sasa ni marehemu. Abdul ndiye alikuwa katibu wakati huo.
Nyerere kaishakutajia labda kwa kukusaidia vyeo wakati huo vilikuwa ni viwili tu rais na katibu
 
Intellectually dead bastard!

Gwalihenzi unanifurahisha sana ha ha haa.... umekimbilia kwenye kithungu huyo ndio ZALI LA MENTALI a.k.a "MCHIMBA CHUMVI" anasema na usemi wa mbuzi,mbuzi akigoma kwenda unadhani anaambiwa kwa maneno anakula kiboko sasa zali anachapa viboko tu safari hii UTAONGEA MPAKA KICHINA!
 
A wise adage goes that "One ought not to argue with a fool as people may not notice the difference"
 

Some kwaumakini swali langu,

Nimeuliza na mkuu Nguruvi3 aliuliza kuwa ni nani kati ya wanaoitwa wazee wenu aliwahi kuongoza AA,TAA,TANU ama chama chochote kile Tanganyika/Tanzania kwa nafasi ya Urais ama Uenyekiti na akaitwa kiongozi wa uasisi?

Lakini unajibu kwakusema nafasi ya Katibu?? Kweli umelielewa swali mkuu?
 
Quote:

By Yericko Nyerere

Mkuu, huyo Ritz ni mfuta viatu wa mkombozi wao Mohamed Said, hawezi kukujibu zaidi yakumpigia makofi Mohamed Said


Haya ni Baadhwi ya matusi na kejeli kutoka kwa ndugu zetu.

Cc. gombesugu,
 
Quote:

By Yericko Nyerere

Mkuu, huyo Ritz ni mfuta viatu wa mkombozi wao Mohamed Said, hawezi kukujibu zaidi yakumpigia makofi Mohamed Said


Haya ni Baadhwi ya matusi na kejeli kutoka kwa ndugu zetu.

Cc. gombesugu,

Hoja nilizoziweka hapo hazina mafaa bali hii unayoita matusi?

Vipi hutaki kuzijibu au unapata elimu kimya kimya ndugu?
 
Zali lamentali

Vipi umeishiwa hoja ama unapata elimu kimya kimya?

Ulikuja kwa ghadhabu sana lakini ukaanza kupoa nakisha kutoweka,

Vipi shekhe wangu, tuendelee na mjadala hatua kwa hatua hoja kwa hoja!
 

Yericko,
Ukiwa utajituliza na kuacha jeuri tunaweza tukafanya mnakasha mzuri
wenye adabu na heshima.

Bahati mbaya naona mjadala umeteka hisia zako pakubwa sana.
Suala AA kuasisiwa na Kleist si mimi nilosema hilo.

Hilo kalisema yeye mwenyewe Kleist katika kumbukumbu alizoacha na
baadhi ya nyaraka hizo zimehifadhiwa Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam,
East Africana.

Ikiwa utapenda fika hapo chuoni kasome ''The Life of Kleist Sykes,'' pia
ukipenda soma Iliffe (ed) ''Kleist Sykes The Townsman,'' katika Modern
Tanzanians.

Yote hayo kaandika mjukuu wa Kleist, Daisy Sykes akisaidiwa na baba yake
Abdu Sykes kabla hajafariki mwaka 1968.

Hilo la Nyerere kusahau cheo cha Abdu tulikubaliana kuwa utaleta audio.
Mimi nitazungumza kuhusu hilo In Shaa Allah baada ya kusikiza hiyo audio.

Nilikuwa sitaki kusema lakini nitakupa kitu kidogo.

Shariff Attas na Nyerere wakifahamiana vyema pale Sokoni Kariakoo na hadi
nyumbani kwa Abdu Sykes pale Mtaa wa Aggrey.

Walikuwa na kawaida ya kula chakula cha mchana pamoja Shariff Attas na Nyerere
nyumbani kwa Abdu.

Abdu alikuwa harudi nyumbani kula kwa hiyo Shariff Attas na Nyerere kila siku walikuwa
wakiongozana kwenda kula chakuka cha mchana pamoja nyumbani kwa Abdu.

Baada ya uhuru kupatikana iko siku Nyerere akakutana na Shariff Attas pale New
Street Ofisi ya TANU.

Nyerere katika kusalimiana na Shariff Attas alimuuliza Shariff Attas ikiwa wanafahamiana.
Shariff Attas alimjibu Nyerere kuwa hawajapatapo kukutana.

Nyerere alikuwa kamsahau rafiki yake wa zamani Shariff Attas.

Ni kisa kirefu lakini hapa hakuna haja ya mimi kukieleza.

Ama hilo la kuwa Nyerere ndiye aliyeasisi TANU New Street na kuwa TANU haina historia
yoyote na Abdu na Vita Kuu Vya Pili mimi halinipi tabu wala sitakubishia una haki ya kusema
unachoamini.

Hilo la Balozi wa Marekani na kuhutubia Bunge unaweza kufanya tafsiri upendayo lakini ukweli
ni kuwa alikuwapo bungeni na aliwasilisha mada juu ya ugaidi.

Mwisho nakusihi uwe mtulivu tufanye mnakasha wa heshima.
 
Mkanda mzima wa namna Yerico alivyobanwa na wazee wa kahawa na haluwa mwishowe akakimbia.Someni kwa furaha.

2) Kuwa Mwalimu rejea kutoka Scotland alisema hakumbuki Abdul Sykes alikuwa na cheo gani katika TAA, Ni UONGO.

Ukweli nikuwa mwalimu ameeleza wazi katika hotuba ya muago kwa wazee wa dar kuwa Abdul alikuwa katibu mkuu wa TAA.
Soma maelezo halisi ya Nyerere
Mwishowe Yerico akajaribu mbinu za akina Mwanakijiji na Nguruvi kujinasua na kibano bila mafanikio

Baada ya kuona ukweli Yerico anawakumbuka wenzake akidhani watarudi kumsaidia.Hapo hakuna wa kukuokoa.
 

Wanajamvi na wote waliobahatika kukisoma kitabu cha Iliffe (ed) "Kleist Sykes The Townsman" katika Modern Tanzanians.

Watakuwa pamoja nami kuwa Illiffe alihariri tu kitabu hicho lakini msimulizi mkuu ni Daisy Sykes mjukuu wa Klest Sykes, mtoto wa Abdul Sykes!

Ukisoma kitabu kile ukura wa tatu tu unasomeka "Klest Plantana Sykes ni MMOJA wa WAASISI wa AA,

Zingatieni hasemi ni MUASISI wa AA bali ni MMOJA wa waasisi wa AA!

Sasa sehemu inayofuata Daisy kapotosha kuwa Klest P. Sykes alikuwa rais wa kwanza wa AA, ama alipotosha kwakutojua ama kwa maksudi kama ilivyo kwa muambata wake Mohamed Said!

Katika kitabu hicho anatajwa Mghana Dr Agrey kama mmoja wa chachu za kuundwa kwa AA!

Lakini kwa maksudi Mwalimu Cesil Matola anafifishwa kuwa ni mmoja ya waasisi tu hatajwi kuwa ndie rais wa mwanzo,

Wakati huo mshangao unazidi kuja pale inapoelezwa kuwa makutano ya mwanzo yalifanyika nyumbani kwa Mwalimu Cesil Matola!

Unaweza kujiuliza maswali mengi, mfano

Kwanini Daisy hakutaka kumjua kiundani Cesil Matola mtu ambae kinachotajwa kuwa kiliasisiwa na BABU yake kilifanyikia nyumbani kwake?

Sasa Mohamed Said unakitafasiri kile alichokiandika Daisy ambae kimtazo na kihulka juu ya Mwalimu Nyerere mnalingana kuwa ni UKWELI?

Pitia chapisho la Iliffe kwa umakini bila chembe ya hisia zako utaona ukweli wa mambo mkuu!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…