Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar


Ndugu yangu Mohamed Said

Hebu tumia mda kidogo kuangalia huo mkanda kisha angalia aina ya silaha zilizotumiwa!

Mimi ni mjuzi wa silaha, na ninazifahamu silaha tulizorithi toka kwa muuingereza ambozo hadi hivi hii leo zipo!

Hebu angalia video hiyo mzee wangu!
 

Ritz

Tungeomba utulivu na adabu katika hili,

Mimi napata elimu na ninatoa kile nilichonacho!

Nivema kutulia nakuwa msomaji ama unachochote ukijuacho juu ya hili tueleze kuliko kuleta viroja vya kutuvuruga!
 
Last edited by a moderator:
Wickama,
Hilo sijui lakini za Ben Bella zilifika zikashushwa Kunduchi.
Yaweza kuwa ni kweli ziliingizwa hizo silahala kutoka Algeria kwa Ben Bella lakini hazikutumika katika mapinduzi ya Mungu wa Afrika (Okello)

Kumbuka katika baadhi ya machapisho yanasomeka kuwa hata Muingereza alipoamua kuondoa askari wake katika vituo, aliondoka na funguo za ghala la silaha, hivi Okello alikuwa na Silaha kama kumi tu alizonyang'anya kwa baadhi ya askari waliosalia!


Ukini uliza mimi mpaka sasa namuona Okello ndie Mwanamapinduzi halisi wa Zanzibar pamoja na mauaji yote aliyoyaendesha!
 

Wickama,
Unanichombeza halafu useme Qadar...

Kuna movie moja "The Tamarind Seed" Omar Shariff.
Anga za Cold War...

Itafute ipo katika torrent.
 

Yericko,
Nitaiangalia.

Lakini zile za Algeria zilipokelewa.
Hii ni taarifa ya kweli.
 
Ritz

Tungeomba utulivu na adabu katika hili,

Mimi napata elimu na ninatoa kile nilichonacho!

Nivema kutulia nakuwa msomaji ama unachochote ukijuacho juu ya hili tueleze kuliko kuleta viroja vya kutuvuruga!

Yericko,

Na wewe una deserve adabu?

Labda waseme wengine wewe kila siku unaniita mie mfuta viatu vya Mohamed Said.

Hakuna cha kujifunza kwako labda adithi za laura Bush za kuvaa suti nyekundu.
 
Suala la mapinduzi ya Zanzibar lina mchanganyiko sana.
Ukiangalia historia kumekuwa na resentment dhidi ya utawala wa sultan kwa miaka mingi nyuma kabla ya mapinduzi.

Mtakumbuka kuwa wakati Tanganyika wakiwa na AA na huko ZNZ ilikuwepo.
Kwa maneno mengine kulikuwa na similarities za manung'uniko kutoka pande zote ambayo ni dhidi ya ukoloni. Kwa Tanganyika walikuwa Waingereza na huko visiwani Waarabu.

Migogoro ya chaguzi za Zanzibar na hata uanzishaji wa vyama vya siasa zilijikita zaidi katika damu na rangi. Kwamba wapo walioamini kuwa wanahaki ya kutawala na wapo waliopinga hilo.

Tofauti za wanazuoni kutokana na hali hiyo zinakuja katika rangi zaidi kuliko ukweli.
Ukisoma vitabu ambavyo vimeandikwa na watu wenye asili au unasaba na uarabu, mapinduzi yalikuwa haramu.

Ukisoma wengine ambao ni wazawa wa Afrika, mapinduzi yalikuwa halali.
Na tofauti hizo zipo hadi leo ndio maana tunasikia mapinduzi daima, na wengine wakisema mapinduzi ni zao la chuki la Nyerere.

Wazanzibar wenyewe hawakubaliani ndio maana nimekuwa nauliza, kama lengo la mapinduzi lilikuwa kuua Uislam, iweje ZNZ yenye 99% waislam waitukuze siku ambayo Uislam uliuawa na Nyerere?

Hapa hakuna suala la udini kwasababu wote ni waislam, lipo suala la rangi.
Sasa wanaomhukumu Nyerere ni wale wenye chuki tu na Nyerere na hivyo kutaka kumpaka matope.

Vinginevyo basi ZNZ yote siku moja ingesema hakuna mapinduzi wala siku ya mapinduzi wala sherehe za mapinduzi kwasababu ni haram.

Hilo halitokei kwasababu Mapinduzi ni ya wazanzibar na wanayaona ni halali kwa mtazamo wa sehemu fulani ambayo ni kubwa ya jamii hiyo.

Hawa wanaosema Nyerere alifanya hivyo kuua Uislam, hawajibu hoja kuwa kwanini basi Nyerere huyo huyo aunge nkono Palestina na Polisario.

Kwanini basi Nyerere huyo huyo aondoe ''nduguze'' kule Msumbiji, Botswana, Namibia na ku-abolish apartheid kama lengo lilikuwa kuua uislam EAC ili ukristo ushamiri kwingine Afrika mashariki au Afrika yote?
 
Yericko,

Na wewe una deserve adabu?

Labda waseme wengine wewe kila siku unaniita mie mfuta viatu vya Mohamed Said.

Hakuna cha kujifunza kwako labda adithi za laura Bush za kuvaa suti nyekundu.

Hahahaaaha!
 
Yericko,
Nitaiangalia.

Lakini zile za Algeria zilipokelewa.
Hii ni taarifa ya kweli.

The Servants Of Benefiicient Allah s.w are those who walk on the earth's surface in humbleness.and when the ignorant adress to them they say peace...
 


huko kote ambako nyerere alithubutu kutia mguu kungekuwa na UKATOLIKI Asingethubutu kukanyaga abadan asilan...
 

Mkuu hili hata asubuhi leo tulipoanza mjadala huu nilieleza mtazamo wangu kulingana na maandiko mengi niliyosoma pamoja na kuziangalia video hasa ile ya mapinduzi ya Okello, nilisema wazi kuwa katika mijadala iliyotanda siku ya mapinduzi haikuwa DINI bali Rangi, Kabila na mengineyo,

Lakini utata umeibuka hapa hasa baada ya Ndugu yetu Mohamed Said kusema Okello hakufanya chochote bali mapinduzi yaliongozwa na Kasim Hanga akiwa sambamba na Oscar Kambona,

Mimi namuona Okello kuwa ndie muasisi wa mapinduzi, na anasema wazi katika kitabu chake,


Sasa tunahitaji fikra mpya ili kuliweka sawa hili, lakini pia mimi nilionya kuweka mbele itikadi za kiroho itatuondolea uwepo katika mada hii!

Inahitaji ustahimilivu wa kweli ili kung'amua!
 
Kama kawaida yako Mzee Mohamed. Huyu bwana angekuwa Muislam bila shaka yoyote simulizi zako zingekuwa tofauti kabisa! Kwa kuwa ni Mkristo lazima aondolewe awekwe Kassim, Ali,...,

DINI yako imekudhibiti sana. Kumbuka tu kuwa Mungu hana DINI.

WC,
Unaushahidi gani kuwa Mungu hana Dini? thibitisha!
 

Nguruvi,
Kusema siyo kuwa ndiyo iwe kweli.

Hawakupanga mapinduzi Umma Party ya kina Babu aje
apange Okello?

Jeshi lile la Kipumbwi likilishwa na nani na nani alilidhamini
kuja kuipigia kura ASP kisha kuja kufanya mapinduzi?

Aliyewaruhusu kuvamia Zanzibar kutoka Kipumbwi ni nani?
 

Nguruvi; Nilipost mikanda miwili hapa. Mmoja una asili ya kiarabu title; SAVAGE AFRICANS KILL ARABS AND MOSLEMS https://www.youtube.com/watch?v=fJmK_FL91vM

https://www.youtube.com/watch?v=aHqEXc3u6So

https://www.youtube.com/watch?v=-sMDkCSC_5g


Mkanda mwingine Okello yeye na Mungu wa waafrika!!!!, sasa kuna vita ya dini hapa? Hawa walishatengana kama jamii. Mzee Mkwawa wa Kipumbwi anasema tulitaka KUWALIPA WAARABU MATESO WALIYOWAFANYIA MABABU ZETU. Hii gear ya kwamba wameua waislamu ni ya hivi karibuni. Wakati huo hakuna aliyemjali mwenzie kuwa ni mwislamu. Ilikuwa rangi na nasaba. Ni sawa na kumlaumu Mugabe kuwa ZANU-PF iliuwa Anglican Christians (white settlers). Nitafutieni silaha za Algeria kwenye hizi video. Mimi sizioni. Naona zile za kulindia wafungwa. Huo mkanda wa rangi unanitia mashaka. sina uhakinka kama 1964 color videography ilikuwa mitaani. Na hata resolution yake sio kama kamera za enzi hizo.
 

Yericko,

Kuna mashujaa wengine hujapata kuwasikia.
Hebu soma hapa chini kisha tuendelee na darsa:

''Jina la huyu mzee wangu ni Mohamed Omar Mkwawa.

Ilikuwa katika barza yetu ya kawaida ya kunywa kahawa na kula pweza huku tukijadili historia ya Tanzania ambako siku moja Mzee Mkwawa alinambia, "Mohamed nataka nikuambie kitu. Unajua mimi nimehusika sana katika mapinduzi ya Zanzibar?"

Nilimuangalia Mzee Mkwawa kwa makini. Fikra yangu ya utafiti na uandishi ishashtuka haipo tena usingizini. Mzee Mkwawa aliendelea, "Mimi ndiye niliyekuwa nikiwavusha Wamakonde kutoka Kipumbwi kwenda Zanzibar kuipigia kura ASP na wakati wa mapinduzi mie ndiye niliyewavusha Wamakonde kwenda kuipindua serikali ya Jamshid."

Sasa moyo wangu ukaanza kudunda kwa nguvu. Naisemesha nafsi yangu, "Huyu mzee anajua uzito wa maneno haya?" Tuishie hapa.

Kuanzia siku ile nikawa sasa namtazama Mzee Mkwawa kwa jicho jingine na heshima yangu kwake ikawa imepanda maradufu. Nilikuwa nimeshatambua kuwa Mzee Mohamed Omari Mkwawa alikuwa mmoja wa wanahistoria waliosahaulika katika historia ya Tanganyika na Zanzibar...

Yericko,
Tuendelee na darsa letu la historia ya mapinduzi ya Zanzibar na nakuomba uangalie wapi utampachika ''Field Marshal Okello'' katika nyavu hizi abaki salama bila ya kujifungafunga:

Kitu kimoja mashuhuri kwa mashujaa wa harakati za siasa katika Tanzania ni kuwa takriban wote wana hali ngumu sana za maisha. Sikujua vyema hali ya Mzee Mkwawa hadi nilipofika nyumbani kwake na Dkt Ghassany.

Utu uzima na udhaifu wa maisha ulikuwa umempiga barabara. Nilimjulisha Dkt Ghassany kwa Mzee Mkwawa na kuwaacha waendelee na maongezi yao. Niliporudi mchana kumchukua Dkt Ghassany rafiki yangu alinambia nimuache nije jioni kumfuata. Niliporudi jioni nilimkuta Dkt Ghassany amechoka na uso umesawijika.

Tukiwa ndani ya gari yangu tunaondoka nikamuuliza kulikoni. Dkt Ghassany akanambia maneno ambayo hadi leo yamebaki kichwani mwangu,"Mohamed ufunguo wa kitabu changu anao Mzee Mkwakwa na kama nisingeonana nae utafiti wangu wote wa kabla ungelikuwa hauna maana yoyote."


Dkt Ghassany alikuwa amechukuliwa na Mzee Mkwawa katika safari ya zaidi ya nusu karne. Mzee Mkwawa akimshika mkono kwanza kumpeleka Pemba ambako akiwa kijana wa kiasi cha miaka 25 akifanya kazi ya uashi. Huo ndio ulikuwa wakati wa siasa za ASP na Hizbu zimepamba moto.

Mzee Mkwawa alikuwa mmoja wa wachezaji wa ngoma ile hata kama alikuwa anatoka Tanganyika. Dkt Harith akavushwa na kuletwa pwani ya Kipumbwi na Sakura ambako Mzee Mkwawa alikuwa akisimamia kambi ya mafunzo iliyokuwa msituni ya wakata mkonge wengi wao wakiwa Wamakonde, kambi ambayo ilitoa askari waliotumika kuipindua serikali ya Mohamed Shamte 12 Aprili 1964.

Dkt Ghassany hakuwa amejitayarisha kwa haya. Alishangwazwa na uwezo wa kumbukumbu wa Mzee Mkwawa, akitaja majina na mahali na akirudia mazungumzo neno kwa neno kati yake na maofisa wa serikali ya Tanganyika kutoka vyombo vya usalama waliomtia katika operesheni maalum ya kuipindua Zanzibar kutoka Tanganyika.

Majina ya Abdulla Kassim Hanga, Jumanne Abdallah, Ali Mwinyi Tambwe, Victor Mkello, Oscar Kambona na wengine yakawa yanadondoka moja baada ya lingine. Taarifa hizi ndizo zilizommaliza Dkt Ghassany na kumsawajisha uso.

Mimi binafsi nilipigwa na butwaa. Nilibaini kama alivyobaini Dkt Ghassany kuwa Mzee Mkwawa alikuwa hazina na tulikuwa tumevumbua mgodi wa dhahabu. Kazi yetu sasa ilikuwa kuchimba tu. Kumekuwa na uvumi kwa miaka mingi katika duru za wanasiasa wapya na wa zamani na katika wanafunzi wa historia ya Tanzania na Mapinduzi ya Zanzibar kuwa Ali Mwinyi Tambwe alihusika sana katika kupinduliwa kwa serikali ya Zanzibar lakini hakuna aliyejuwa ni kwa kiwango gani na alihusika vipi.

Lakini zito ni kuwa yeye mwenyewe akiudhika sana mtu akimuuliza habari zile. Kwa nini ilikuwa hivyo? Kitabu cha Kwaheri Ukoloni, Kwaheri Uhuru cha Dkt Ghassany kilikuja kutoa majibu. Hakuna binadamu apendae historia yake ihusishwe na mauaji na dhulma na kufutwa kwa nchi yake.

Kwa kipindi cha takriban miaka saba Dkt Ghassany alikuwa akija Tanga kwa mahojiano na Mzee Mkwawa na katika kipindi hicho Mzee Mkwawa alitupeleka Kipumbwi na Sakura na kutuonyesha sehemu zile ambazo walikuwa na kambi na wakifanya mazoezi ya kivita na matumizi ya silaha.

Mkahawa ambao wale wakata mkonge walikuwa wakila chakula cha usiku kabla ya kuvushwa kwa vyombo vya bahari kwenda Unguja bado upo hadi leo ingawa kwa sasa kijumba kile hakitumiki tena kama mkawaha. Endapo itakuja siku serikali ya Zanzibar itataka kuhifadhi historia ya Mapinduzi ya Zanzibar bila shaka moja ya vitu vitakavyokuwa katika makumbusho ni picha ya hicho kibanda.
''
 

Hapo sasa ndio wakati mnasibu wakuyachambua hayo mkuu,

Ikiwa wayajua kwa undani ni vema tukanasibishana na yale tuyajuayo kisha tuibuke na msimamo mmoja kama waswahili na watanzania!

Inapendeza sana! Tusonge mbele...!
 
Yericko Nyerere, mimi mwanzoni nilidhani porojo za huyu mwenzetu zingeishia tu hapa bara lakini duh, uongo una sifa moja mbaya, ukiachwa unaenea kama upepo vile. Ona sasa porojo zimevuka bahari hadi kutua kwenye visiwa vya karafuu. Mimi hapa nabaki nacheka tu...namkumbuka Abdulrahman Babu akipiga tusker zake pale Dar es Salaam Club, akitaka apewe microphone apande stejini atoe burudani akiimba wimbo wa "soul"...baadaye sana nawaona wasaidizi wake wakimshauri kuwa saa ya kuondoka imetimia (wakati huo ni saa tisa usiku hivi) aweze kuwahi ofisini asubuhi...hiyo ni miaka ya 1960s baada ya Muungano!

Mwaka 1967 niko NRB tunaburudika na pilsner baridi huku tukisakata muziki wa Sal Davis (Sal Davis? what's in a name?) katika ukumbi wa Sal Davis Night Spot (Bonanza Club) chumba mviringo mtaa wa Koinange ikipakana na Total House. Waeneza umbea chanzo chao ni simulizi kutoka third party...na unamjua mswahili tena, taja kumi mtaa wa Kipata ukifika mtaa wa Uweje si kumi tena ni maelfu. Swali linalohitaji jibu...je, ni kitu gani kilimleta Field Marshall John Okelo mjini Dar es Salaam? Ni hapo akili na ndoto za Okelo zilipokwaa kisiki, Mwalimu Julius Nyerere!...hizi blah blah ni kama shukhrani ya punda, mateke...!
 
Last edited by a moderator:
NGURUVI NA YERICKO na MS;
Hapa kuna vipande toka CIA report ya 100 days.....Zanzibar (imeshakuwa publicly available tangu 2007) Ukisoma pg 30-40s utakuta haya kuhusu Okello;

“……Okello’s role i n the revolution is probably th e most clearly identifi e d One of t h e rank-and-file rebels he rose to a command position while the coup action was taking place. In the first raid of the revolution , when most of t h e 200 ASP attackers held back from actual combat , he and a group of 25 disaffected ASP ex-members of the police pressed on; in this and other attacks on the various police posts, he demonstrated courage and natural abilities as a street fighter . By the end of t h e day, he was regarded by th e rebels as their hero and commander

“…….A powerful figure a ft e r the revolution--because of his support from &he armed forces--he was unknown and unimpo r t a n t before the revol ut ion The leaders of Zanzibar new government seemed t0 know as l i t t l e about him as t h e rest of the world; t h e i r accounts of h i s background d i f f e r e d markedly. Tanganyikan Minister f o r E x t e r n a l A f f h i s s and Defense Kambona, who was i n close touch with t h e Zanzi b a r r e v o l u t i o n a r i e s , claimed to know nothing about Okello.”


“……..In summary, the Zanzibar revolution was the reaction of ra d i c a l s i n the Afro-Shirazi t r a d e union and youth movements to the Arabist policy of t h e previous government. It was t r i g g e r e d by a rumor t h a t the government planned mass arrests of the A3P leaders on 13 January. The notion t h a t t h e banning of the Umma Party led Babu and h i s followers i n t o armed revolt is probably the main misconception of the revolution; government a c t i o n against the Umma Party was a c o n t r i b u t i n g f a c t o r only i n t h a t S t l e n t credence to the rumor t h a t the government was preparing a s i m i l a r r a i d on the ASP. Although c e r t a i n leaders of t h e ASP, notably Hanga, were a c t i v e l y planning: a r e v o l u t i o n , t h e y do not seem to have taken the i n i t i a t i ve on the night of 11-12 January. Apparently, a group of disgruntled ex-members of the Zanzibar police at an African f e t e t h a t evening w e r e primarily responsible for I n c i t i n g a crowd Of some 200 persons to the point of action against the government Hanga, Karume , and other ASP l e a d e r s , l e a r n i n g of the excited state 01 the Africans at flie .rete, decided to seize the opportunity t o overthrow the governinenit. Bwbu and his followers jumped on the bandwagon the next day. By then, Okello had emerged from obscurity, the mili i t a r y hero of the day”


“…….The actual events of the revolution are well known. Shortly before 3 a . m . , on the morning of Sunday, 12 January 1964, the Ziwani police asmosy was attacked by a small band of Africans led by Okello. After less than two hours of fighting , it and the Mtoni p o l i c e arsenal were taken over and the weapons distributed to the rebels . An attack was then mounted on Malindi police headquarters, the nerve center of the remaining police f o r c e s ; towards dawn, it was reported occupied by the r e b e l s . The next day, the cable office , the airstrip , and the radio station were seized, in t hat order. By late afternoon, the government machinery was paralyzed”


“……..The actual fighting was done by some 600 members Of the youth wing of t h e ASP and some 200 Umma Party members who joined the ranks of the rebels the next morning. These latter groups were g e n e r a l l y better equipped than th e rank-and-file ASP rebels; some were armed with automatic weapons, as well as rifles and pistols. Until the first armory fell, the ASP forces had practically no guns; most or the insurgents fought with pangas or sticks only”.

Kwa hiyo Mzee MS hizo silaha unazosema ndizo wanataja kuwa wenye nazo walifika wakati mambo yeshakwisha. Kuna page wanasema Kambona alistukizwa kuwa mapinduzi tayari na huku yeye anasaka silaha!!!! kwa ajili ya kina ASP. Kuna silaha za Umma Party hazijulikani mwenyewe wala mtoaji. Hao sasa labda ndio walioingia viungani kusaka waarabu. Lakini Okello na hao makomandoo wake 25 walizitwanga kavu kwanza hadi kupora silaha na kuanza kuteka vituo. Hawa pia wameeleza mapinduzi kama matatu yaliyokuwa yamepangwa na kila kundi. Usiku mwema
 

Nashukuru kwa maelezo haya mazuri,

Omar Mkwawa nimemsoma katika kitabu cha Kwaheri Ukoloni, Kwahere Uhuru cha Dkt Ghassany,

Nilimsoma kwa mtazamo wa wastani lakini nashukuru angalau umesisimua vile mlivyoweza kupata habari zake na mapito yake!

Lakini hapa kuna jambo muhimu la kujiuliza ama kuhoji, na hili hata wewe unaweza kujiuliza, wale askari 300 wa Okello waliohudumu katika mapinduzi yale ya awali na makuu, walikuwa ni jumuiko la hao wamakonde wa Mkwawa?

Kama sivyo basi hayo ya Mkwawa yalikuwa ni mapinduzi yapili ama?
 

Yericko,

Kuna mashujaa wengine hujapata kuwasikia.

Hebu soma hapa chini kisha tuendelee na darsa:

Jina la huyu mzee wangu ni Mohamed Omar Mkwawa.

Ilikuwa katika barza yetu ya kawaida ya kunywa kahawa na kula pweza huku tukijadili historia ya Tanzania ambako siku moja Mzee Mkwawa alinambia, "Mohamed nataka nikuambie kitu. Unajua mimi nimehusika sana katika mapinduzi ya Zanzibar?"

Nilimuangalia Mzee Mkwawa kwa makini. Fikra yangu ya utafiti na uandishi ishashtuka haipo tena usingizini. Mzee Mkwawa aliendelea, "Mimi ndiye niliyekuwa nikiwavusha Wamakonde kutoka Kipumbwi kwenda Zanzibar kuipigia kura ASP na wakati wa mapinduzi mie ndiye niliyewavusha Wamakonde kwenda kuipindua serikali ya Jamshid."

Sasa moyo wangu ukaanza kudunda kwa nguvu. Naisemesha nafsi yangu, "Huyu mzee anajua uzito wa maneno haya?" Tuishie hapa.

Kuanzia siku ile nikawa sasa namtazama Mzee Mkwawa kwa jicho jingine na heshima yangu kwake ikawa imepanda maradufu. Nilikuwa nimeshatambua kuwa Mzee Mohamed Omari Mkwawa alikuwa mmoja wa wanahistoria waliosahaulika katika historia ya Tanganyika na Zanzibar...

Yericko,
Tuendelee na darsa letu la historia ya mapinduzi ya Zanzibar na nakuomba uangalie wapi utampachika ''Field Marshal Okello'' katika nyavu hizi abaki salama bila ya kujifungafunga:

Kitu kimoja mashuhuri kwa mashujaa wa harakati za siasa katika Tanzania ni kuwa takriban wote wana hali ngumu sana za maisha. Sikujua vyema hali ya Mzee Mkwawa hadi nilipofika nyumbani kwake na Dkt Ghassany.

Utu uzima na udhaifu wa maisha ulikuwa umempiga barabara. Nilimjulisha Dkt Ghassany kwa Mzee Mkwawa na kuwaacha waendelee na maongezi yao. Niliporudi mchana kumchukua Dkt Ghassany rafiki yangu alinambia nimuache nije jioni kumfuata. Niliporudi jioni nilimkuta Dkt Ghassany amechoka na uso umesawijika.

Tukiwa ndani ya gari yangu tunaondoka nikamuuliza kulikoni. Dkt Ghassany akanambia maneno ambayo hadi leo yamebaki kichwani mwangu,"Mohamed ufunguo wa kitabu changu anao Mzee Mkwakwa na kama nisingeonana nae utafiti wangu wote wa kabla ungelikuwa hauna maana yoyote."

Dkt Ghassany alikuwa amechukuliwa na Mzee Mkwawa katika safari ya zaidi ya nusu karne. Mzee Mkwawa akimshika mkono kwanza kumpeleka Pemba ambako akiwa kijana wa kiasi cha miaka 25 akifanya kazi ya uashi. Huo ndio ulikuwa wakati wa siasa za ASP na Hizbu zimepamba moto.

Mzee Mkwawa alikuwa mmoja wa wachezaji wa ngoma ile hata kama alikuwa anatoka Tanganyika. Dkt Harith akavushwa na kuletwa pwani ya Kipumbwi na Sakura ambako Mzee Mkwawa alikuwa akisimamia kambi ya mafunzo iliyokuwa msituni ya wakata mkonge wengi wao wakiwa Wamakonde, kambi ambayo ilitoa askari waliotumika kuipindua serikali ya Mohamed Shamte 12 Aprili 1964.

Dkt Ghassany hakuwa amejitayarisha kwa haya. Alishangwazwa na uwezo wa kumbukumbu wa Mzee Mkwawa, akitaja majina na mahali na akirudia mazungumzo neno kwa neno kati yake na maofisa wa serikali ya Tanganyika kutoka vyombo vya usalama waliomtia katika operesheni maalum ya kuipindua Zanzibar kutoka Tanganyika.

Majina ya Abdulla Kassim Hanga, Jumanne Abdallah, Ali Mwinyi Tambwe, Victor Mkello, Oscar Kambona na wengine yakawa yanadondoka moja baada ya lingine. Taarifa hizi ndizo zilizommaliza Dkt Ghassany na kumsawajisha uso.

Mimi binafsi nilipigwa na butwaa. Nilibaini kama alivyobaini Dkt Ghassany kuwa Mzee Mkwawa alikuwa hazina na tulikuwa tumevumbua mgodi wa dhahabu. Kazi yetu sasa ilikuwa kuchimba tu. Kumekuwa na uvumi kwa miaka mingi katika duru za wanasiasa wapya na wa zamani na katika wanafunzi wa historia ya Tanzania na Mapinduzi ya Zanzibar kuwa Ali Mwinyi Tambwe alihusika sana katika kupinduliwa kwa serikali ya Zanzibar lakini hakuna aliyejuwa ni kwa kiwango gani na alihusika vipi.

Lakini zito ni kuwa yeye mwenyewe akiudhika sana mtu akimuuliza habari zile. Kwa nini ilikuwa hivyo? Kitabu cha Kwaheri Ukoloni, Kwaheri Uhuru cha Dkt Ghassany kilikuja kutoa majibu. Hakuna binadamu apendae historia yake ihusishwe na mauaji na dhulma na kufutwa kwa nchi yake.

Kwa kipindi cha takriban miaka saba Dkt Ghassany alikuwa akija Tanga kwa mahojiano na Mzee Mkwawa na katika kipindi hicho Mzee Mkwawa alitupeleka Kipumbwi na Sakura na kutuonyesha sehemu zile ambazo walikuwa na kambi na wakifanya mazoezi ya kivita na matumizi ya silaha.

Mkahawa ambao wale wakata mkonge walikuwa wakila chakula cha usiku kabla ya kuvushwa kwa vyombo vya bahari kwenda Unguja bado upo hadi leo ingawa kwa sasa kijumba kile hakitumiki tena kama mkawaha. Endapo itakuja siku serikali ya Zanzibar itataka kuhifadhi historia ya Mapinduzi ya Zanzibar bila shaka moja ya vitu vitakavyokuwa katika makumbusho ni picha ya hicho kibanda.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…