Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar

Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar

Moja ya mambo ambayo mda mwingi nilikushauri ndugu yangu ni hilo la kuamini kila ulichoambiwa bila kufanya utafiti binafsi au shirikishi!

Tangu mwaka 1948 hadi 1953 TAA hakikuwa chama cha siasa kimantiki, kilikuwa ni chama cha harakati za haki za mwafrika wa Tanganyika,

Hilo linapatikana katika filosofia yake!

Baada ya Uchaguzi wa 1953 Anartoughulo Mnazimmoja na Mwalimu Nyerere kushika hatamu za uongozi wa TAA, chama kilianza kubadili filosofia yake kutoka kuwa cha harakati za kudai haki za weuzi, na kuwa cha harakati za ukombozi wa Tanganyika-Chama cha siasa!

Kutokana na mageuzi hayo yaliyokuwa ilikuwa ni lazima chama kibadili jina ilikiwiane na ideology yake, hivyo kikaitwa TANU!

Sasa ndugu yangu upotoshaji unaofanya katika hilo sioni sababu yake,

Kusema TAA iliyumba baada ya Mwalimu kushika madaraka ni uongo


Shukran Yericko; Kisichoelezwa hapa ni kwamba huyu Dennis Phombe despite ukaribu wake na Ally Sykes ndiye kwa nguvu zake zote alimkampenia Nyerere kwenye uchaguzi against Abdul Sykes. Iam sure Dennis knew where he could bet his money!!!! He knew the two well in terms of their potential VALUE. The rest ni sentiments.
 
Shukran Yericko; Kisichoelezwa hapa ni kwamba huyu Dennis Phombe despite ukaribu wake na Ally Sykes ndiye kwa nguvu zake zote alimkampenia Nyerere kwenye uchaguzi against Abdul Sykes. Iam sure Dennis knew where he could bet his money!!!! He knew the two well in terms of their potential VALUE. The rest ni sentiments.

Ndugu yangu,

Kuna kazi ya ziada kweli kuuzuia uongo wa Mohamed Said, kazi hiyo inakuja pale ambapo yeye haamini kuwa tumeamua kumwambia huo ni uongo!

Mwanasiasa aliyezoea kupigiwa makofi hata akiongea upuuzi mbele ya kadamnasi, siku asipopigiwa makofi atapaza sauti akiamini makutano hawajamsikia kumbe wamempuuza!
 
Wanajamvi,
Innalilah Wainnailaihy Rajuun.

Kwa Allah tumetoka na kwake ni marejeo yetu.

Bwana Ally Kleist Sykes amefariki dunia Nairobi.

Hakika kwake tulitoka na kwake marejeo! nawapa pole familia yote ya akina Sykes Allah awape subira na Imani!
Kwa Mohamed Said, kwakuwa umefanya kazi kubwa kuandika upya Historia ya wapigania uhuru wetu akiwemo marehemu Ally Sykes na kaka ake Abdu, nawe nakupa pole kwasababu kwanamna moja au ingine msiba huu unakugusa mojakwamoja Allah akuzidishie subra na Imani na tunamuomba Allah amsamehe madhambi yake Mzee Ally Sykes na amuingize ktk pepo yake tukufu AAAMIN!

Mohamed Said,
Ombi: ili kumuenzi Mzee Ally Sykes ktk siku hizi za matanga nakuomba ukipata wasaa tuwekee wasifu wa Mzee wetu Ally Sykes ili wasiomjua waone mchango wake ktk kupigania uhuru wa nchi hii!
Kuhusu wapi na lini atazikwa shujaa huyu nakuomba tujulishe!
 
Wanajamvi

Kunaupotoshwaji ulifanywa na Ritz kwamaksudi ama kwakutojua juu ya kuripoti msiba wa mzeee wetu Ally Sykes!

Ritz anasema Ally ni mwasisi wa TAA na TANU jambo ambalo sio kweli!

Pamoja nakuwa ulikusudia kuuhabarisha umma juu ya msiba huu,

Lakini upotoshaji wa aina hii usiachwe upite bila kusahihishwa!

AA imeundwa 1929 chini ya Mwalimu Cesil Matola,

1933 AA ilimkasimisha madaraka katibu wake bwana Klest Sykes, hii ni baada ya Matola kufariki,

Mwaka 1948 Klest Sykes anaasisi TAA, na mwaka huohuo anapinduliwa na Daktari kijana Vedasto Kyaruzi anashika urais wa TAA,

Katibu anakuwa Abdul Sykes kaka wa Ally Sykes,

Mwaka 1950 Dr Kyaruzi anahamishwa kikazi kwa nguvu na muingereza nakupelekwa Nzege hiyo ikiwa ni mikakati ya mkoloni kukidhoofisha chama cha TAA, baada ya hapo nafasi ya urais inakaimiwa na Abdul Sykes.

Mwaka 1953 uchaguzi unafanyika na Julius Nyerere anamshinda Abdul Sykes katika uchaguzi huo, hivyo Julius anakuwa rais wa TAA,

Mwaka unaofuata yani 1954 TAA inabadilishwa jina nakuwa TANU na uchaguzi unafanyika tena, Julius Nyerere na Abdul Sykes wanashindana katika kinyang'anyiro hicho na Julius Nyerere anaibuka kidedea hivyo kuwa rais wakwanza kwa TANU,

Hilo likaenda mpaka 1958 katika uchaguzi maarufu kama kura tatu, uliofanyikia jimbo la magharibi (Tabora) Nyerere tena akashinda,

Baada ya hapo Abdul Sykes alijitenga na siasa na kuanzisha chuki dhidi ya viongozi wa TANU hasa Julius Nyerere,

Baada ya uhuru kupatikana, kundi lililokuwa likimuunga mkono Abdul Sykes lilianzisha UASI dhidi ya serikali halali ya TANU,

Kundi hilo lilikuwa na watu wengi walitoka TAA na TANU hasa Shehe Takadir, Shehe Hassan Bin Amir, na wengine wengi!

Kundi hilo baada yakufeli mission yao kisiasa sasa liliamua kutumia misikiti kupandikiza chuki yao,

Chuki hiyo ndio inayoliathiri taifa mpaka hii leo na Ritz ukiwa ni muathirika wayo!


Kufuatia hali hiyo, mkono wa dola ukaanza kuwaandama tena kwa nguvu hii ilifuatiwa na kuunda sheria ya kuweka mtu kizuizini ya mwaka 1962,

Sasa kusema Ally Sykes ndie muasisi wa TAA na TANU ni UONGO

Ally Sykes katika uhai wake hajawahi kushika nyadhifa yoyote ya kisia, kikundi ama jumuiya!

Neno zuri lakutumia nikama ulivyoanza na kichwa cha taarifa hii kuwa MMOJA wa waasisi wa TANU na sio TAA
 
Kadogoo,

..kwa kweli hili ni gumu.

..si tumeambiwa hata Dr.Slaa ana kadi ya CCM na anailipia.

..mimi naipenda CDM siyo kwasababu ni nzuri sana, but kwasababu CCM ni mbaya zaidi.

NB:

..nadhani masuala ya CDM yana thread nyingi sana. tujaribu kutowajadili ktk thread hii.

cc: Ritz, Nguruvi3

Hapana. Mbona hili jibu lake rahisi sana? Soboda ni mzalendo anayeamini kuwa CCM imekwenda mrama. Anaamini kuwa CDM itairudisha nchi kwenye mkondo wa uzalendo zaidi na siyo hizi sera za Kikwete za kuwa kuwadi wa utandawazi.
 
Hapana. Mbona hili jibu lake rahisi sana? Soboda ni mzalendo anayeamini kuwa CCM imekwenda mrama. Anaamini kuwa CDM itairudisha nchi kwenye mkondo wa uzalendo zaidi na siyo hizi sera za Kikwete za kuwa kuwadi wa utandawazi.

Jasusi,
Sobodo ni kada wa CCM au sio?
 
attachment
 
Nguruvi nilikuwa naomba jibu huu mpini wa al Akh Barubaru je bwana mkubwa Nyerere aliyafanya hayo au utasema ni ngano za watoto wa madrasa.
Ndugu yangu aliyosema Barubaru ni uongo na upungufu wa kuelewa.

Kwamba vita ya Kagera ni matokeo ya Nyerere kutaka kumrudisha Obote! kuna Upungufu mkubwa sana wa kuelewa kama si kuzusha mambo katika misingi ya chuki.

Vita ya Tanzania na Uganda ilianza mwaka1973, wakati huo uchumi wa Tanzania ukiwa mzuri sana.
Amin alishambulia Tanzania na wale wa Mwanza na Kagera wanakumbuka nini kilitokea.
Endapo lengo lilikuwa kumrudisha Obote basi huo ndio ungekuwa wakati mwafaka.

Nyerere alikubali suluhu chini ya marehemu Haile Sellasie wa Ethiopia.Kwanini akubali suluhu endapo lengo lilikuwa kumrudisha Obote?

Vita ya Kagera ilianza baada ya Amin kuivamia Tanzania. Ipo nadharia kuwa alichokozwa.
Sidhani kama ni sahihi kwasababu ingalikuwa hivyo basi Tanzania isingepoteza askari na wananchi wake wengi katika hatua za uvamizi.Ingalikuwa imejiandaa vema, hilo halikutokea.Unakumbuka Brigedia wa kizanzibar aliyepelekwa likizo baada ya askari wengi kupoteza maisha katika hatua za kuzuia uvamizi.

Kuhusu suala la Nyerere kutoa pesa za ukombozi, nadhani pia kuna upungufu mkubwa wa kuelewa. Kilichotokea ni kuwa na makazi ya wapigania uhuru waliokuwa wanaungwa mkono na hivyo kuwaruhusu kuweka kambi nchini.
Hayo anayosema Barubaru kuhusu utoaji wa pesa hazina ni hisia zake tu kama zile za kusema hakuna mtoto wa Nyerere aliyekwenda shule achilia mbali kumaliza highschool.

Mnaposema mpini basi lazima mjiulize mbona kuna hoja (a-h) nimeweka Barubaru hagusi amebaki kusema nenda kaangalie joint finance commission! kuna kitu ameficha hapo.

Ukweli unabaki kuwa bajeti ya znz ni bilioni 630 kwa mwaka. Kati ya hizo mapato ni bilioni 120.
Kwa maneno mengine kuna bilioni 530 ambazo inapata kutoka Tanganyika.

Sasa jiulize, kwa serikali ya muungano yenye bajeti ya trillioni znz inachangia nini.
Inachangia nini kwasababu hata wizara ya akina mama na watoto peke yake znz haiwezi kuendesha.

Uchumi wa znz hauruhusu hata senti moja kuingia katika shughulia za muungano.
Unamkamua vipi ng'ombe asiye na maziwa?
Hao wzn hawawezi kulipa umeme leo kuna mtu anatuaminisha wanaweza kuwa na mchango katika muungano.

Jana Rais wa znz Shein amefungua chuko cha kumbu kumbu ya mwalimu Nyerere. Chuo hicho kimejengwa kwa thamani ya sh bilioni bilioni 3.6. Ni pesa za muungano ambazo znz haichangii, narudia haina uwezo wa kuchangia hata senti tano.
Sasa hawa wenye chuki na Nyerere wanaimba lanatullah wakati wanaingia katika katika majengo yaliyojengwa kwa heshima ya Nyerere.

Katika waliohudhuria alikuwepo maalim Seif kinara wa kupinga muungano na kinara wa fadhila za muungano.

Ndio maana narudia kusema
1. ZNZ haina bajeti ya ulinzi na usalama, elimu ya juu, mishahara ya wastaafu na wafanyakazi wa SMZ, huduma za jamii kama umeme, na inapewa pesa za bure kufidia bajeti yake. Pesa ambazo ni mara 3 ya mapato yake.

Hili la kusema nikafanye utafiti, nadhani hamjui kuwa Barubaru anaogopa kusema kuhusu hiyo joint commission akijua kuwa atamwaga mtama kwenye kuku.

Nimelifanyia ytafiti wa kutosha na nasema wazi leo muungano ukivunjika, na tunataka hilo litokee znz wataondoka na mabegi tu na hawana cha kudai. Hawadai bali wanadaiwa.

Znz ni tegemezi kwa Tanganyika ndio maana wanataka muungano wa mkataba, Uswis na Ujerumani, Hong Kong na Botwsana na ujinga wa namna hiyo. Wanafahamu kuwa nje ya muungano si kwamba watafunga mikanda ya Nyerere aliyosema bali wataumia na kuteseka sana.

Hapa ndipo najibu hoja kuwa kama Nyerere aliacha watu wake wafe ili kukomboa nchi za Afrika, basi Mwinyi, Mkapa na Kikwete hawajajifunza kutokana na makosa hayo kwasababu wanaacha Watanganyika wafe wakati wanapeleka pesa kulipia mafao ya wastaafu, mishahara ya wafanyakazi wa SMZ, Ulinzi na usalama, elimu hata umeme wa watu kuchezea bao bure n.k. kama ambavyo basi Nyerere analaumiwa kama ilitokea hivyo.

Endapo tutamsota kidole Nyerere kwa chuki tu basi chuki hizo zitang'ata kwa akina Mwinyi, Mkapa na Kikwete na hadi hapo hakuna mwenye afadhali. Bila kuwataja hao hoja ya Nyerere kuchota pesa na kupeleka kwingine haina mashiko maana Kikwete kachota bilioni 3.6 jana tu kupeleka znz nchi kama Msumbiji, Botswana, S.A na Namibia.

Bunge limeidhinisha bilioni 32 kwenda znz bila kujua zinafanya kazi gani achilia mbali mapesa yasiyo na idadi ya kulipia watoto wa kizanzibar wasome bila mkopo na kupata ajira Tanganyika huku watoto wa kitanganyika wakilipia mikopo kwa gharama ya nafasi zao za ajira kuchukuliwa na wazanzibar. Nyerere hayaupo hapo ni bunge hili lililokaa Dodoma!

Sheikh Faridi nadhani nimerejea mipini yako sasa ni wakti wako umshawishi Barubaru arejee mashoka yangu bila kujificha na kukimbia kwa kutumia neno joint commisison, utafiti n.k.

Inaonekana umefuzu sana somo la mzee la kukwepa hoja na kukikmbia kimbia hovyo.

Tumetoka nje ya mada samahani!
 
Ndugu yangu aliyosema Barubaru ni uongo na upungufu wa kuelewa.

Kwamba vita ya Kagera ni matokeo ya Nyerere kutaka kumrudisha Obote! kuna Upungufu mkubwa sana wa kuelewa kama si kuzusha mambo katika misingi ya chuki.

Vita ya Tanzania na Uganda ilianza mwaka1973, wakati huo uchumi wa Tanzania ukiwa mzuri sana.
Amin alishambulia Tanzania na wale wa Mwanza na Kagera wanakumbuka nini kilitokea.
Endapo lengo lilikuwa kumrudisha Obote basi huo ndio ungekuwa wakati mwafaka.

Nyerere alikubali suluhu chini ya marehemu Haile Sellasie wa Ethiopia.Kwanini akubali suluhu endapo lengo lilikuwa kumrudisha Obote?

Vita ya Kagera ilianza baada ya Amin kuivamia Tanzania. Ipo nadharia kuwa alichokozwa.
Sidhani kama ni sahihi kwasababu ingalikuwa hivyo basi Tanzania isingepoteza askari na wananchi wake wengi katika hatua za uvamizi.Ingalikuwa imejiandaa vema, hilo halikutokea.Unakumbuka Brigedia wa kizanzibar aliyepelekwa likizo baada ya askari wengi kupoteza maisha katika hatua za kuzuia uvamizi.

Kuhusu suala la Nyerere kutoa pesa za ukombozi, nadhani pia kuna upungufu mkubwa wa kuelewa. Kilichotokea ni kuwa na makazi ya wapigania uhuru waliokuwa wanaungwa mkono na hivyo kuwaruhusu kuweka kambi nchini.
Hayo anayosema Barubaru kuhusu utoaji wa pesa hazina ni hisia zake tu kama zile za kusema hakuna mtoto wa Nyerere aliyekwenda shule achilia mbali kumaliza highschool.

Mnaposema mpini basi lazima mjiulize mbona kuna hoja (a-h) nimeweka Barubaru hagusi amebaki kusema nenda kaangalie joint finance commission! kuna kitu ameficha hapo.

Ukweli unabaki kuwa bajeti ya znz ni bilioni 630 kwa mwaka. Kati ya hizo mapato ni bilioni 120.
Kwa maneno mengine kuna bilioni 530 ambazo inapata kutoka Tanganyika.

Sasa jiulize, kwa serikali ya muungano yenye bajeti ya trillioni znz inachangia nini.
Inachangia nini kwasababu hata wizara ya akina mama na watoto peke yake znz haiwezi kuendesha.

Uchumi wa znz hauruhusu hata senti moja kuingia katika shughulia za muungano.
Unamkamua vipi ng'ombe asiye na maziwa?
Hao wzn hawawezi kulipa umeme leo kuna mtu anatuaminisha wanaweza kuwa na mchango katika muungano.

Jana Rais wa znz Shein amefungua chuko cha kumbu kumbu ya mwalimu Nyerere. Chuo hicho kimejengwa kwa thamani ya sh bilioni bilioni 3.6. Ni pesa za muungano ambazo znz haichangii, narudia haina uwezo wa kuchangia hata senti tano.
Sasa hawa wenye chuki na Nyerere wanaimba lanatullah wakati wanaingia katika katika majengo yaliyojengwa kwa heshima ya Nyerere.

Katika waliohudhuria alikuwepo maalim Seif kinara wa kupinga muungano na kinara wa fadhila za muungano.

Ndio maana narudia kusema
1. ZNZ haina bajeti ya ulinzi na usalama, elimu ya juu, mishahara ya wastaafu na wafanyakazi wa SMZ, huduma za jamii kama umeme, na inapewa pesa za bure kufidia bajeti yake. Pesa ambazo ni mara 3 ya mapato yake.

Hili la kusema nikafanye utafiti, nadhani hamjui kuwa Barubaru anaogopa kusema kuhusu hiyo joint commission akijua kuwa atamwaga mtama kwenye kuku.

Nimelifanyia ytafiti wa kutosha na nasema wazi leo muungano ukivunjika, na tunataka hilo litokee znz wataondoka na mabegi tu na hawana cha kudai. Hawadai bali wanadaiwa.

Znz ni tegemezi kwa Tanganyika ndio maana wanataka muungano wa mkataba, Uswis na Ujerumani, Hong Kong na Botwsana na ujinga wa namna hiyo. Wanafahamu kuwa nje ya muungano si kwamba watafunga mikanda ya Nyerere aliyosema bali wataumia na kuteseka sana.

Hapa ndipo najibu hoja kuwa kama Nyerere aliacha watu wake wafe ili kukomboa nchi za Afrika, basi Mwinyi, Mkapa na Kikwete hawajajifunza kutokana na makosa hayo kwasababu wanaacha Watanganyika wafe wakati wanapeleka pesa kulipia mafao ya wastaafu, mishahara ya wafanyakazi wa SMZ, Ulinzi na usalama, elimu hata umeme wa watu kuchezea bao bure n.k. kama ambavyo basi Nyerere analaumiwa kama ilitokea hivyo.

Endapo tutamsota kidole Nyerere kwa chuki tu basi chuki hizo zitang'ata kwa akina Mwinyi, Mkapa na Kikwete na hadi hapo hakuna mwenye afadhali. Bila kuwataja hao hoja ya Nyerere kuchota pesa na kupeleka kwingine haina mashiko maana Kikwete kachota bilioni 3.6 jana tu kupeleka znz nchi kama Msumbiji, Botswana, S.A na Namibia.

Bunge limeidhinisha bilioni 32 kwenda znz bila kujua zinafanya kazi gani achilia mbali mapesa yasiyo na idadi ya kulipia watoto wa kizanzibar wasome bila mkopo na kupata ajira Tanganyika huku watoto wa kitanganyika wakilipia mikopo kwa gharama ya nafasi zao za ajira kuchukuliwa na wazanzibar. Nyerere hayaupo hapo ni bunge hili lililokaa Dodoma!

Sheikh Faridi nadhani nimerejea mipini yako sasa ni wakti wako umshawishi Barubaru arejee mashoka yangu bila kujificha na kukimbia kwa kutumia neno joint commisison, utafiti n.k.

Inaonekana umefuzu sana somo la mzee la kukwepa hoja na kukikmbia kimbia hovyo.

Tumetoka nje ya mada samahani!

Nguruvi nimekusoma lakini katika mpini wako nimegundua unachuki sana na wazanzibar kwasababu point zako zote kinachokukera ni kwanini kuna mgao unaotoka Tanzania bara na kwenda Zanzibar, hata wazanzibar wakisoma hii post yako watakushangaa sana lakini nisikupinge haya ni mawazo yako na ni haki yako ya kikatiba,katiba inasema kila mtu ana haki ya kutoa maoni yake.Tukiridi kwenye mpini wa Barubaru kunakitu hujajibu kama sijakosea alikuuliza ilikuwaje watu wakala ugali wa Yanga na ilikuwaje Nyerere alifeli masuala ya uchumi ni hayo tu kamanda.
 
Wickama,
Hilo ulisemalo la Nyerere wala halina ubishi hata kidogo.

Labda la kujiuliza.

Wakatoliki wa Peramiho walikuwa wapi wakati akina Sheikh
Badi wanapambana na Mwingereza?

Nadhani agenda sasa iko hadhir.

kaka hili swali gumu sana na si saizi yake huyu bwana
 
Wanajamvi

Kunaupotoshwaji ulifanywa na Ritz kwamaksudi ama kwakutojua juu ya kuripoti msiba wa mzeee wetu Ally Sykes!

Ritz anasema Ally ni mwasisi wa TAA na TANU jambo ambalo sio kweli!

Pamoja nakuwa ulikusudia kuuhabarisha umma juu ya msiba huu,

Lakini upotoshaji wa aina hii usiachwe upite bila kusahihishwa!

AA imeundwa 1929 chini ya Mwalimu Cesil Matola,

1933 AA ilimkasimisha madaraka katibu wake bwana Klest Sykes, hii ni baada ya Matola kufariki,

Mwaka 1948 Klest Sykes anaasisi TAA, na mwaka huohuo anapinduliwa na Daktari kijana Vedasto Kyaruzi anashika urais wa TAA,

Katibu anakuwa Abdul Sykes kaka wa Ally Sykes,

Mwaka 1950 Dr Kyaruzi anahamishwa kikazi kwa nguvu na muingereza nakupelekwa Nzege hiyo ikiwa ni mikakati ya mkoloni kukidhoofisha chama cha TAA, baada ya hapo nafasi ya urais inakaimiwa na Abdul Sykes.

Mwaka 1953 uchaguzi unafanyika na Julius Nyerere anamshinda Abdul Sykes katika uchaguzi huo, hivyo Julius anakuwa rais wa TAA,

Mwaka unaofuata yani 1954 TAA inabadilishwa jina nakuwa TANU na uchaguzi unafanyika tena, Julius Nyerere na Abdul Sykes wanashindana katika kinyang'anyiro hicho na Julius Nyerere anaibuka kidedea hivyo kuwa rais wakwanza kwa TANU,

Hilo likaenda mpaka 1958 katika uchaguzi maarufu kama kura tatu, uliofanyikia jimbo la magharibi (Tabora) Nyerere tena akashinda,

Baada ya hapo Abdul Sykes alijitenga na siasa na kuanzisha chuki dhidi ya viongozi wa TANU hasa Julius Nyerere,

Baada ya uhuru kupatikana, kundi lililokuwa likimuunga mkono Abdul Sykes lilianzisha UASI dhidi ya serikali halali ya TANU,

Kundi hilo lilikuwa na watu wengi walitoka TAA na TANU hasa Shehe Takadir, Shehe Hassan Bin Amir, na wengine wengi!

Kundi hilo baada yakufeli mission yao kisiasa sasa liliamua kutumia misikiti kupandikiza chuki yao,

Chuki hiyo ndio inayoliathiri taifa mpaka hii leo na Ritz ukiwa ni muathirika wayo!


Kufuatia hali hiyo, mkono wa dola ukaanza kuwaandama tena kwa nguvu hii ilifuatiwa na kuunda sheria ya kuweka mtu kizuizini ya mwaka 1962,

Sasa kusema Ally Sykes ndie muasisi wa TAA na TANU ni UONGO

Ally Sykes katika uhai wake hajawahi kushika nyadhifa yoyote ya kisia, kikundi ama jumuiya!

Neno zuri lakutumia nikama ulivyoanza na kichwa cha taarifa hii kuwa MMOJA wa waasisi wa TANU na sio TAA


Yericko,

Wala sikujibu hayo mengine.

Unachusha.

Nakuomba msikilize Ally Sykes hapa chini akijieleza alivyoanza siasa 1947 akiwa na umri wa miaka 21:

''It was while serving in the Labour Department that I was in 1951 elected General Secretary as well as TAGSA representative in the Government Establishment Committee. TAGSA was formed in 1927.

Its objectives were to promote understanding between Her Majesty's Government and its African Servants in order to improve Her Majesty's Service and promotion of interest and welfare of the African Government employees.

Europeans and Asians had their own associations with similar objectives but being privileged their associations were not as active as ours. The 1951 TAGSA election elected Thomas Marealle (later to become Paramount Chief of the Chagga) as President and Rashid Kawawa later to become Vice-President of Tanganyika, committee member.

The constitution of TAGSA provided for annual elections. I was returned to office as secretary four times until October 1954 when I had to resign after being transferred to Korogwe. This record was unprecedented. I was the only secretary under TAGSA since its inception in 1927 to have been returned to the post in each election four times.

I would have been returned again and again if it were not for the transfer, which was my punishment for being among the seventeen founder members of TANU. My father had written in his memoirs that it was the government policy that as soon as a civil servant was elected into an office in the TAA he would be immediately transferred up country.

For example in 1940 Njilima was elected President and was transferred to Tanga, while his secretary, Nicolas, was transferred to Moshi and Ndesario, the Assistant Secretary, was transferred to Lindi.


The presidency always changed hands. Stephen Mhando and Dr. Wilbard Mwanjisi were at different times elected presidents. Among active members of TAGSA were Dr. Michael Lugazia and Rashid Kawawa both of them came to play very significant roles in the struggle for independence.

In order to understand the political sentiments of the people of Tanganyika after World War Two we first have to analyse the hardship, which faced the people as a result of the war and then observe the kind of leadership, which was leading the people at that particular time.

The times were hard on average African. There was air of discontent floating in the air. The ex-service men infused into the people new ideas of freedom and basic rights denied to Africans of Tanganyika.

The working class of the urban centre in Dar es Salaam could not make ends meet on their meagre salaries. Yet still unemployment persisted. People looked towards the African Association for solutions to these problems. People turned to the Association because it was the only African organisation, which purported to serve African interests.''
 
Hakika kwake tulitoka na kwake marejeo! nawapa pole familia yote ya akina Sykes Allah awape subira na Imani!
Kwa Mohamed Said, kwakuwa umefanya kazi kubwa kuandika upya Historia ya wapigania uhuru wetu akiwemo marehemu Ally Sykes na kaka ake Abdu, nawe nakupa pole kwasababu kwanamna moja au ingine msiba huu unakugusa mojakwamoja Allah akuzidishie subra na Imani na tunamuomba Allah amsamehe madhambi yake Mzee Ally Sykes na amuingize ktk pepo yake tukufu AAAMIN!

Mohamed Said,
Ombi: ili kumuenzi Mzee Ally Sykes ktk siku hizi za matanga nakuomba ukipata wasaa tuwekee wasifu wa Mzee wetu Ally Sykes ili wasiomjua waone mchango wake ktk kupigania uhuru wa nchi hii!
Kuhusu wapi na lini atazikwa shujaa huyu nakuomba tujulishe!


Kadogoo,

Nakuwekea hapa chini kumbukumbu za Ally Sykes kutoka kinywa chake mwenyewe:
''We realised that one of the most effective ways to confront the British was to mobilise the people. I had a cyclostyle machine hidden at home and I used that for writing and distributing propaganda leaflets to alert the people of what was happening in our country.

We organised a nation-wide campaign to inform the people about the outcome of the Meru Land Case at the United Nations and to seek financial support to enable TAA to send another delegation to the United Nations to present and establish Tanganyika's case as Mandate Territory seeking independence.

In 1953 TAA therefore dispatched Abdu Kandoro, Kirilo and my young brother Abbas Sykes to Dodoma, Mwanza, Bukoba, Ukerewe, Tarime, Musoma and Shinyanga to hold meetings with the people and collect money for the Association.


After failing to persuade the TAA executive to call a meeting we stormed into the offices one afternoon in 1950 and took over the leadership of the Association by force and a meeting was called at Arnautoglo Hall to discuss the TAA and its many problems.

Nothing constructive came out of that meeting because of the presence of a white colonial officer. Hamza Mwapachu, Dr. Lucian Tsere, Dr. Kyaruzi, Dossa, Tewa Said Tewa, Stephen Mhando and many Makerere graduates including some of the old members like Mashado and Schneider Plantan attended this meeting.

We could not deliberate freely in front of the colonial officer. The meeting would have ended in a flop it were not for Schneider Plantan. Not caring whether the white officer sent by the government was listening or not, he proposed to the meeting that a new date should be fixed for TAA members to meet and elect a new leadership capable of facing the colonial government. There was applause all over the meeting hall and the meeting ended.

When the meeting was called Dr. Kyaruzi was elected President and Abdulwahid Secretary. John Rupia, the veteran member of the struggle since the days of the African Association was elected Treasurer and I was elected Assistant Treasurer. But the Association had nothing in its coffers. Kyaruzi and Abdulwahid did what no leadership had ever done before. This leadership formed a committee to deal with all political issues facing the country.

This was the time of the Meru Land evictions and Japhet Kirilo through the Meru Citizen Union had sent a petition to the United Nations fighting the evictions. Abdulwahid contacted Earle Seaton a Bermudan lawyer based in Moshi to represent Meru Citizen Union. Abdulwahid had known Seaton even before he came to Tanganyika. There was a time when Abdulwahid wanted to go to study in America and he used to correspond with Seaton. When Seaton came to Tanganyika the two were already acquainted.

Abdulwahid used Seaton to advise TAA on many issues of the Association. He helped the Association draft the Memorandum to the Constitution Development Committee of Governor Edward Francis Twining and in advising us on constitutional law and the status of mandate territories vis-a vis the United Nations Trusteeship Council.
''
 
Ndugu yangu,

Kuna kazi ya ziada kweli kuuzuia uongo wa Mohamed Said, kazi hiyo inakuja pale ambapo yeye haamini kuwa tumeamua kumwambia huo ni uongo!

Mwanasiasa aliyezoea kupigiwa makofi hata akiongea upuuzi mbele ya kadamnasi, siku asipopigiwa makofi atapaza sauti akiamini makutano hawajamsikia kumbe wamempuuza!


Yericko,
Huyo hapo chini anaezungumza ni Ally Sykes nakuomba msikize msome kwa makini sana:

''In 1953 the TAA leadership elected him (Nyerere) to stand against the incumbent President, my brother Abdulwahid. On 17 April 1953 election was held at Arnautoglo Hall between Abdulwahid and Nyerere. Abdulwahid lost the election by a very narrow margin. In June we announced our executive committee: J.K. Nyerere, President; Abdulwahid Sykes, Vice-President; J.P. Kasella Bantu, General Secretary; Alexander M. Tobias and Waziri Dossa Aziz, Joint Minuting Secretary; John Rupia, Treasurer and I was Assistant Treasurer. Committee members were Dr. Michael Lugazia, Hamisi Diwani, Tewa Said, Denis Phombeah, Z. James, Dome Okochi, C. Ongalo and Patrick Aoko.[1] Nyerere became TAA President and Abdulwahid became his Vice-President.''


[1]Tanganyika Standard, 19 June 1953.
 
kama unanyonya elimu usiishie kubeza yale usiyokubaliana nayo,pinga kwa kutoa hoja ili tunaojifunza tupate kitu,ikiwa huna hoja ishia kusoma ni busara zaidi.

Skia wewe na wenzako,msinipangie lakuongea pale ninapojiskia kufanya hivyo,huyo niliemjibu hivyo meseji kaipata pia,

Kejeli hizi unaziona kwangu tuh??hao wanaomkejeli moh said mnajitia hamuwaoni??

Mind your god damned bussiness..!
 
kaka hili swali gumu sana na si saizi yake huyu bwana

Tume; Shukrani. sasa ndugu yangu issue ilikuwa wazee wa Lindi wamempikia mgeni wao Julius PILAU na kisha kutia dua ya kiislamu. Mzee anadai mchango huu wa wao kumwondoa Mwingereza Kanisa katoliki lilikuwa wapi? Zingatia kuwa 1. Hawa wazee ni waislamu, wanaendesha mambo yao kiislamu 2. Mzee MS hajaonyesha kuwa Kanisa lilialikwa kuleta chakula na kuja kumwombea Julius LIKAGOMA 3. Wazee kama Mareale au John Rupia au Paul Bomani, Bryson, Phombe, Munanka kama walishamkaribisha Julius chakula ni lazima walitia dua ya chakula au kumwombea mgeni wao safari njema Kikiristo au kwa dini zao bila lawama kuwa waislamu wako wapi!!!!

Sasa naridhika tuu na majibu ya Mzee huyu kuwa hayana mahusiano na ardhi tuliyokanyaga. Yanaongozwa na chuki aliyohifadhi kirefu na kanisa katoliki. Sioni uhusiano wa pilau ya wazee hawa wa Lindi na Parokia ya Kikatoliki Masasi as though wao walimnyima Julius Lunch. Sioni LINK.

Vinginevyo zipo hata timu za mpira nchi zimeshasoma Ahlil Badri kwa masula ya kandanda, na wala sijaona lalamiko kuwa Kanisa katoliki liko wapi mbona hatuoni mchango wake!!!
 
Skia wewe na wenzako,msinipangie lakuongea pale ninapojiskia kufanya hivyo,huyo niliemjibu hivyo meseji kaipata pia,

Kejeli hizi unaziona kwangu tuh??hao wanaomkejeli moh said mnajitia hamuwaoni??

Mind your god damned bussiness..!

Jirani yangu pole. Mwenzio nimeshayazoea haya tangu nibahatishe jirani mpya. Nakumiss sana. Ila Chondeeeee Angalia usitumie bunduki kuua mmbu. Haki ya Munguuuuu Big Show!!!!!! Nakusoma (hahahahah). Inaitwa dharura.

cc Kadogoo
 
Nguruvi nimekusoma lakini katika mpini wako nimegundua unachuki sana na wazanzibar kwasababu point zako zote kinachokukera ni kwanini kuna mgao unaotoka Tanzania bara na kwenda Zanzibar, hata wazanzibar wakisoma hii post yako watakushangaa sana lakini nisikupinge haya ni mawazo yako na ni haki yako ya kikatiba,katiba inasema kila mtu ana haki ya kutoa maoni yake.Tukiridi kwenye mpini wa Barubaru kunakitu hujajibu kama sijakosea alikuuliza ilikuwaje watu wakala ugali wa Yanga na ilikuwaje Nyerere alifeli masuala ya uchumi ni hayo tu kamanda.
Sheikh Farid, wznz hawana sababu za kushangaa, wanasababu za kujibu kama kilichoelelezwa ni uongo. Kwa taarifa yako nikupe kumbu kumbu kidogo kwamba wazanzibar wanakubaliana na hoja zangu.

1. Kitendo cha wao kulalamika kuwa wanaonewa na wakati huo huo wanataka kuwa na mkataba na Tanganyika ni kuelewa fika kuwa ndani ya muungano kuna mambo yanayowasaidia sana na hivyo kuiacha Tanganyika ni muhali.

2. Kiongozi wa kuvunja muungano Maalim Seif alipoulizwa na tume ya Warioba kwanini tusikutane EAC yeye alisema muungano wa EAC ni mparaganyiko hadi sasa afadhali huu wetu na pengine tutawavutia wengine kujiunga nao.
Hapa ni kuwa anatambua wazi kuwa huu muungano ni bora hata kama anataka znz ijitenge.

3. Maalim Seif ametofautiana na sera za chama chake za serikali 3 na kuendelea na na suala la mkataba.
Amekisaliti chama anachosimamia lakini usaliti wake una mipaka, kwamba si kuvunja muungano ni muungano wa mkataba.
Kuna kitu anakiona ambacho anakifahamu kupitia mkataba znz itanufaika na wala Si Tanganyika.

4. Katika kongamano la bwawani hotel mwaka 2012, aliyewakuwa waziri katika serikali ya muungano, na mwanachama wa baraza la mapinduzi sheikh Nassor Moyo alitamka katika kipaza sauti kuwa muungano unafaida hasa za kiuchumi, kisiasa na kiutamaduni. Huyu ndiye leo anaitwa fundi seremala kisa kasema muungano una faida.

5. Tarehe hiyo hiyo, Jusa Ladhu, mbunge nguli machachari aliyehudumia bunge na baraza la wawakilishi na katibu wa CUF visiwani alisema kuwa muungano una faida kwa wznz kiuchumi, kijiografia na kielimu.

6. Mansour Himid, kindaki ndaki mwingine wa znz huru naye katika siku hiyo alisimama na kupaza sauti dunia ikamsikia akisema muungano unahitajika na wala hawataki kuvunja bali kurekebisha.

7. Tume ya Wariona imekutana na wznz na ikafikia mahali kuna vurugu. Kisa ni kundi moja likitaka muungano na lingine likitaka sultan arejee kwa kupitia mlango wa uani. Hiyo ni hiari yao, ninachosema ni kuwa uwepo wa makundi hayo unaondoa hoja yako kuwa wazanzibar wakisoma...

8. Hivi karibuni, aliyekuwa waziri kiongozi na sasa waziri katika serikali ya muungano Shamsa vua akiongea na vijana wa CCM alisema muungano una manufaa hasa katika elimu ya juu, kijiografia na kusema mafuta ambayo znz inadhani yapo ni kujidanganya maana bara wameshaanza kuvuna, kwanini wao wznz wasiwe sehemu ya uvunaji huo.

9. Rais Shein amekaririwa akisema muungano unasaidi sana znz hasa suala la ulinzi na usalama na elimu ya juu.
Akaonya matatizo yatakayotokana na kuvunjika kwa muungano.

Sasa makundi na watu hao kama wanasema nadhani ni wznz, hizi tofauti za rangi wanazijua wao.
Vinginevyo utasikia kila anayepinga muungano ni kibaraka kwasababu tu Seif kasema hata kama yeye ameshachukua kitambulisho cha muungano.

Nimeweka mambo machache ambayo mznz anaitegemea Tanganyika, nadhani tupitie moja baada ya jingine ili kuthibitisha ukweli au uongo kuliko kushangaa.

Ima wzn wanaweza kunishangaa kwasababu watajiuliza haya yote yamejulikanaje ili hali ilikuwa ni siri yao.

Kuhusu suala la njaa, nadhani kuna upungufu mkubwa wa weledi.
Mwaka 1974(sikumbuki vema) kulikuwa na njaa iliyoleta kitu kinaitwa kilimo cha kufa na kupona.

Ethiopia iliwahi kupata njaa na aliyeisalimisha mbele ya uso wa dunia ni al marhum Mohmed Amin aliyefariki kwa ajali ya ndege kule Comoro. Huyu ndiye aliionyesha dunia njaa inavyoua kule Somalia.

Mwaka juzi na jana njaa ilipiga Kenya hadi ikabidi waombe msaada wa chakula kutoka Tanzania.
Nakumbuka waziri wao alimfuata JK kule Maramba kuongea juu ya suala hili.

Malawi ilipata njaa ambayo ilibidi UN iingilie kati. Moja ya mashirika yaliyoteuliwa kusamabaza chakula ni S.S.Bkahresa.

Marekani ilikuwa na njaa mwaka jana na kufanya bei ya vyakula iongezeke.

Hali ndiyo hiyo duniani kote kuanzia mashariki hadi magharibi.

Sasa kama hoja ya Barubaru ni kuwa njaa ni kushindwa kiuchumi, nadhani nchi za jirani kama Kenya, Ethiopia, Malawi na hata Zimbabwe zimeshindwa kiuchumi. Lakini haishii hapo, je, kukiwa na balaa la njaa mahali hiyo inatosha kuwa kigezo cha kushindwa kiuchumi?

Na muhimu zaidi ni kuwa katika marais waliofuata baada ya Nyerere, nani amefanya kitu tofauti ambacho tunaweza kusema amezuia njaa.

Pengine Mkapa na Keenja walijaribu kuwa na national reserve ingawa hiyo ni bandeji na wala si matibabu.
Matibabu ni Irrigation, sasa Mwinyi, Mkapa na Kikwete combine wamefanya kitu gani ambacho Nyerere hakukifanya hasa ukizingatia kuwa wao waliikuta nchi ambayo Nyerere kajenga misingi ya baadhi ya mambo.

Misingi hiyo ni stable country as compared to our neighbors, miradi kama ya umeme wa mabwawa, miundo mbinu, huduma za afya na elimu.

Vyote hivyo havijafanywa katika kiwango cha Nyerere kwa utawala wa Mkapa, Mwinyi na Kikwete combine katika miaka zaidi ya 27.

Nadhani umeeelewa.
 
Tume; Shukrani. sasa ndugu yangu issue ilikuwa wazee wa Lindi wamempikia mgeni wao Julius PILAU na kisha kutia dua ya kiislamu. Mzee anadai mchango huu wa wao kumwondoa Mwingereza Kanisa katoliki lilikuwa wapi? Zingatia kuwa 1. Hawa wazee ni waislamu, wanaendesha mambo yao kiislamu 2. Mzee MS hajaonyesha kuwa Kanisa lilialikwa kuleta chakula na kuja kumwombea Julius LIKAGOMA 3. Wazee kama Mareale au John Rupia au Paul Bomani, Bryson, Phombe, Munanka kama walishamkaribisha Julius chakula ni lazima walitia dua ya chakula au kumwombea mgeni wao safari njema Kikiristo au kwa dini zao bila lawama kuwa waislamu wako wapi!!!!

Sasa naridhika tuu na majibu ya Mzee huyu kuwa hayana mahusiano na ardhi tuliyokanyaga. Yanaongozwa na chuki aliyohifadhi kirefu na kanisa katoliki. Sioni uhusiano wa pilau ya wazee hawa wa Lindi na Parokia ya Kikatoliki Masasi as though wao walimnyima Julius Lunch. Sioni LINK.

Vinginevyo zipo hata timu za mpira nchi zimeshasoma Ahlil Badri kwa masula ya kandanda, na wala sijaona lalamiko kuwa Kanisa katoliki liko wapi mbona hatuoni mchango wake!!!

Wickama,
In Sha Allah nipe muda nitakuwekea hapa harakati
za Suleiman Masoud Mnonji, Yusuf Chembera, Bi.
Shariffa biti Mzee, Ali Mnjale, Mohamed Awadh na
wengineo chini ya TANU walivyopambana na fitna
za Kanisa kuwavunja nguvu wananchi wasijiunge na
juhudi za kudai uhuru.

Haya yote yalitokea Jimbo la Kusini mpinzani mkubwa
akiwa Yustino Mponda Liwali wa Newala na kibaraka wa
Waingereza.
 
SHEIKH FARID, Nguruvi3,

..nimetembelea website ya Joint Finance Commission ya Tanzania.nimekutana na taarifa kwamba kwa mwaka 2010/11 makusanyo ya kodi ya mapato Tanzania nzima yalikuwa 1522.1 billion. Mchango wa Znz ktk makusanyo hayo ni 24.1 billion, wakati mchango wa Tanganyika ni 1498.0 billion.

..taarifa kama hizo ndizo zinazotufanya wengine tuamini kwamba Znz inainyonya Tanganyika. binafsi sijui uhalali wa Znz kuwa na 50% ya wajumbe ktk tume ya katiba , au kuwa na wabunge wengi kiasi kile ktk bunge la muungano, unatoka wapi.

cc: gombesugu, Barubaru, Wickama
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom