Mohamed,
Suala la EAMWS na Sheikh Amir linazidi kuchukua sura mpya.
Kwanza niwaambie wanajamvi kuwa kufuatana na maandishi ya Ziddy, kuna wakati Sheikh Amir alikuwa na ugomvi na Mwanafunzi wake sheikh Chaurembo kutokana na masuala ya KISIASA.
Ni wazi kuwa halikuwa suala la TANU, swali linabaki ni masuala gani ya kisiasa nje ya TANU na kwanini sheikh aliyekuwa mwanachama wa TANU awe na sura nyingine ya kisiasa nje ya TANU?
Pili, Sheikh alikuwa mwanachama wa Al-Jamiyya Islamiyya fil Tanganyika. Na pia alikuwa mwanachama wa Al-Dafiwa fil Islamiyya. Vyama hivi vya kidini vina uhusiano mkubwa sana na familia ya Sykes.
Kuna nyakati Abdul Sykes alikuwa katibu wa Al-Jamiyya Islamiyya fi Tanganyika.
Uhusiano wa Sheikh Amir na familia ya Sykes ndipo ulipozidi kuuma.
Mnakumbuka pia kuhusu AMNUT. Ingawa Mohamed anakanusha kuwa Sheikh Amir hakuwa mwanachama wa AMNUT ningependa pia akanushe kuwa wanafunzi wa Sheikh hawakuwa wanachama na viongozi wa AMNUT.
Kwa mantiki ni kuwa kulikuwa na uhusiano kati ya Sheikh Amir, Familia ya Klesit na AMNUT.
AMNUT walikuwa sympathizers wakubwa wa Abdul na wengi ni wanafunzi wa Amir.
Angalia hiyo triangle vizuri sana.
Kutokana na uhusiano huo chuki ya Abdul Kushindwa na Nyerere katika chaguzi na ukweli kuwa sheikh naye alikuwa katika TAA sub political committee ndiko kuliwaunganisha na kumzuia Sheikh Amir kukataa nafasi alizopewa na Nyerere ili kuendesha siasa za pembeni.
Kukataa nafasi katika serikali kulikuwa ni kosa kubwa sana kisiasa na kidini.
Sheikh aliporejea kutoka Egypt aliahidiwa pauni 55 millions egyptian Pounds.
Kama angekuwa katika serikali hiyo ndiyo ingekuwa fursa nzuri sana ya kuendeleza mradi wa ujenzi wa chuo kikuu.
Angeabaini mbinu zote chafu au basi kuomba msaada zaidi pale ilipobidi. Hakufanya hivyo kwasababu alikuwa na political agenda nje ya TANU kama alivyobainisha Comorian na mgogoro na mwanafunzi wake Chaurembo juu ya mambo ya kisiasa
Hakukuwa na sababu za yeye kufanya siasa za vichochoroni kama alivyonywa na sheikh Comorian mara baada ya kurejea kwake safarini.
Kwa mujibu wa Ziddy, kulikuwa na migogoro ndani kwa ndani kati ya Sheikh Amir na Sheikh Chaurembo hata kabla ya mradi wa kuanzisha chuo kuanza, na ni migogoro hiyo iliyoua mpango mzima wa kujenga chuko kikuu.
Mohamed Sadi anaposema Nyerere alikuwa na mpango wa kuua mradi wa EAMWS si kweli. Si kweli kwa facts kuwa:
- Kulishaanza migogoro ya kisiasa nje ya TANU kati ya Sheikh Amir na Wanafunzi wake iliyohusu siasa nje ya TANU.
- Nyerere asingeweza kuruhusu viongozi wa serikali akiwemo Tewa Said Tewa kuambatana na Sheikh ambaye alishajulikana ana siasa za pembeni kwenda kuomba msaada wa kujenga chuo kikuu.Haiingii akilini Nyerere aruhusu viongozi wake ndani ya serikali halafu aje kuzuia chuo.
- Mohamed anadai Tewa alipewa ubalozi ili kuua mpango mzima wa ujenzi wa chuo cha EAWMS. Anachosahau ni kuwa Tewa alipewa nafasi ya ubalozi miaka 3 baaada ya ziara ya Egtpt. Endapo mpango huo ungekuwa kama anavyodai basi angemuondoa mapema zaidi.
Limezuka suala la sheikh Amir kuwa Walii. Hilo nasema kwa mujibu wa watu wa imani yake kama limetokea ni sawa. Kinachoshughulisha akili ni kuwa walii ni mtu mwenye sifa zisizo na shaka.
Sheikh Amir alitiliwa shaka sana na watu wa mikoani kuhusu matumizi ya pesa makao makuu alipokuwa kinara.
Hilo ndilo lilianza kumega mikoa ya Tanga, Bukona na Iringa. Linathibitika katika madai ya mikoa hiyo yaliyotakiwa kutimizwa kabla ya kurudi ndani ya EAMWS.
Madai hayo yakieleza wazi kuwa vyanzo na matumizi ya pesa za EAMWS lazima yawekwe wazi. Sasa kwanini Walii atiliwe shaka na je hapo bado hishma yake inabaki katika uwalii akiwa na strings attached
Kuna hoja za Mohamed kuhusu kuzuiliwa na kuonewa. Maswali yanayozuka ni mengi sana ambayo hayana majibu ya maana kwa anayetumia akili
- Kwanza, hivi Ansar Sunn ni watu wa imani gani? Mbona wao wana miaradi na hata TV stesheni na wala hawajazuiliwa na kanisa au serikali.
- Hawa mashia ni wa imani gani mbona hawajazuiliwa na serikali au kanisa kuwa na miradi yao sehemu zote nchini?
- Hawa Ismailia ni wa imani gani, mbona hawajazuliliwa kuwa na miradi nchi nzima
- Hivi kwanini mlezi wa EAWMS amerudi na kupewa plot kwa ajili ya chuo kikuu.
- Kwanini malalamiko yapo kwa watu nje ya makundi hayo hapo juu.
Na mwisho, labada niulize hivi ilie misaada inayotoka nje kama Saudia na ile inayotolewa na matajiri wa hapa nchini kama ZAKA, imetumika vipi katika investment ya mambo ya social ambayo leo inaweza kuombewa ruzuku serikalini kama za mashirika mengine.
cc.Zumbemkuu, kuna nyuzi uliomba nifunguke!
cc Jokakuu, Shariff Ritz, Almaarufu Gombesugu, Wickama,Jausi, Mag3, Who,gfsowin,Prisharz, Hon Al-khyis'