Mohamed Said
JF-Expert Member
- Nov 2, 2008
- 21,967
- 32,074
Niasidie mzee wangu, ni kweli kuwa mzee Kreist Mbuyane alikufa maji Ruaha Iringa akiwa katika mapambano na Mkwawa?
Nguruvi.Mohamed,
Suala la EAMWS na Sheikh Amir linazidi kuchukua sura mpya.
Kwanza niwaambie wanajamvi kuwa kufuatana na maandishi ya Ziddy, kuna wakati Sheikh Amir alikuwa na ugomvi na Mwanafunzi wake sheikh Chaurembo kutokana na masuala ya KISIASA.
Ni wazi kuwa halikuwa suala la TANU, swali linabaki ni masuala gani ya kisiasa nje ya TANU na kwanini sheikh aliyekuwa mwanachama wa TANU awe na sura nyingine ya kisiasa nje ya TANU?
Pili, Sheikh alikuwa mwanachama wa Al-Jamiyya Islamiyya fil Tanganyika. Na pia alikuwa mwanachama wa Al-Dafiwa fil Islamiyya. Vyama hivi vya kidini vina uhusiano mkubwa sana na familia ya Sykes.
Kuna nyakati Abdul Sykes alikuwa katibu wa Al-Jamiyya Islamiyya fi Tanganyika.
Uhusiano wa Sheikh Amir na familia ya Sykes ndipo ulipozidi kuuma.
Mnakumbuka pia kuhusu AMNUT. Ingawa Mohamed anakanusha kuwa Sheikh Amir hakuwa mwanachama wa AMNUT ningependa pia akanushe kuwa wanafunzi wa Sheikh hawakuwa wanachama na viongozi wa AMNUT.
Kwa mantiki ni kuwa kulikuwa na uhusiano kati ya Sheikh Amir, Familia ya Klesit na AMNUT.
AMNUT walikuwa sympathizers wakubwa wa Abdul na wengi ni wanafunzi wa Amir.
Angalia hiyo triangle vizuri sana.
Kutokana na uhusiano huo chuki ya Abdul Kushindwa na Nyerere katika chaguzi na ukweli kuwa sheikh naye alikuwa katika TAA sub political committee ndiko kuliwaunganisha na kumzuia Sheikh Amir kukataa nafasi alizopewa na Nyerere ili kuendesha siasa za pembeni.
Kukataa nafasi katika serikali kulikuwa ni kosa kubwa sana kisiasa na kidini.
Sheikh aliporejea kutoka Egypt aliahidiwa pauni 55 millions egyptian Pounds.
Kama angekuwa katika serikali hiyo ndiyo ingekuwa fursa nzuri sana ya kuendeleza mradi wa ujenzi wa chuo kikuu.
Angeabaini mbinu zote chafu au basi kuomba msaada zaidi pale ilipobidi. Hakufanya hivyo kwasababu alikuwa na political agenda nje ya TANU kama alivyobainisha Comorian na mgogoro na mwanafunzi wake Chaurembo juu ya mambo ya kisiasa
Hakukuwa na sababu za yeye kufanya siasa za vichochoroni kama alivyonywa na sheikh Comorian mara baada ya kurejea kwake safarini.
Kwa mujibu wa Ziddy, kulikuwa na migogoro ndani kwa ndani kati ya Sheikh Amir na Sheikh Chaurembo hata kabla ya mradi wa kuanzisha chuo kuanza, na ni migogoro hiyo iliyoua mpango mzima wa kujenga chuko kikuu.
Mohamed Sadi anaposema Nyerere alikuwa na mpango wa kuua mradi wa EAMWS si kweli. Si kweli kwa facts kuwa:
- Kulishaanza migogoro ya kisiasa nje ya TANU kati ya Sheikh Amir na Wanafunzi wake iliyohusu siasa nje ya TANU.
- Nyerere asingeweza kuruhusu viongozi wa serikali akiwemo Tewa Said Tewa kuambatana na Sheikh ambaye alishajulikana ana siasa za pembeni kwenda kuomba msaada wa kujenga chuo kikuu.Haiingii akilini Nyerere aruhusu viongozi wake ndani ya serikali halafu aje kuzuia chuo.
- Mohamed anadai Tewa alipewa ubalozi ili kuua mpango mzima wa ujenzi wa chuo cha EAWMS. Anachosahau ni kuwa Tewa alipewa nafasi ya ubalozi miaka 3 baaada ya ziara ya Egtpt. Endapo mpango huo ungekuwa kama anavyodai basi angemuondoa mapema zaidi.
Limezuka suala la sheikh Amir kuwa Walii. Hilo nasema kwa mujibu wa watu wa imani yake kama limetokea ni sawa. Kinachoshughulisha akili ni kuwa walii ni mtu mwenye sifa zisizo na shaka.
Sheikh Amir alitiliwa shaka sana na watu wa mikoani kuhusu matumizi ya pesa makao makuu alipokuwa kinara.
Hilo ndilo lilianza kumega mikoa ya Tanga, Bukona na Iringa. Linathibitika katika madai ya mikoa hiyo yaliyotakiwa kutimizwa kabla ya kurudi ndani ya EAMWS.
Madai hayo yakieleza wazi kuwa vyanzo na matumizi ya pesa za EAMWS lazima yawekwe wazi. Sasa kwanini Walii atiliwe shaka na je hapo bado hishma yake inabaki katika uwalii akiwa na strings attached
Kuna hoja za Mohamed kuhusu kuzuiliwa na kuonewa. Maswali yanayozuka ni mengi sana ambayo hayana majibu ya maana kwa anayetumia akili
- Kwanza, hivi Ansar Sunn ni watu wa imani gani? Mbona wao wana miaradi na hata TV stesheni na wala hawajazuiliwa na kanisa au serikali.
- Hawa mashia ni wa imani gani mbona hawajazuiliwa na serikali au kanisa kuwa na miradi yao sehemu zote nchini?
- Hawa Ismailia ni wa imani gani, mbona hawajazuliliwa kuwa na miradi nchi nzima
- Hivi kwanini mlezi wa EAWMS amerudi na kupewa plot kwa ajili ya chuo kikuu.
- Kwanini malalamiko yapo kwa watu nje ya makundi hayo hapo juu.
Na mwisho, labada niulize hivi ilie misaada inayotoka nje kama Saudia na ile inayotolewa na matajiri wa hapa nchini kama ZAKA, imetumika vipi katika investment ya mambo ya social ambayo leo inaweza kuombewa ruzuku serikalini kama za mashirika mengine.
cc.Zumbemkuu, kuna nyuzi uliomba nifunguke!
cc Jokakuu, Shariff Ritz, Almaarufu Gombesugu, Wickama,Jausi, Mag3, Who,gfsowin,Prisharz, Hon Al-khyis'
Ninachokulaumu ni kuwa hukujishughulisha kuangalia Uislamu nao unasemaje kuhusu suala la UDUGU KATIKA UISLAMU!Ingawa Mohamed anakanusha kuwa Sheikh Amir hakuwa mwanachama wa AMNUT ningependa pia akanushe kuwa wanafunzi wa Sheikh hawakuwa wanachama na viongozi wa AMNUT.
Kwa mantiki ni kuwa kulikuwa na uhusiano kati ya Sheikh Amir, Familia ya Klesit na AMNUT.
AMNUT walikuwa sympathizers wakubwa wa Abdul na wengi ni wanafunzi wa Amir.
Angalia hiyo triangle vizuri sana.'
Je? ilikuwa halali kwa muislam Kreist Mbuwane kushirikiana na makafir kwenda kumpiga vita muislam mwenzie Mkwawa? Je Kufa maji kwa Mbuwane ilikuwa adhabu ya Allah dhidi ya dhulma aliyokuwa anafanyiwa Mkwawa na makafir?Maulaga ni kweli Kleist Mbuwane alikufamaji
Mto Ruaha.
Walipofika mtoni walitanguliza ng'ombe kuvuka
kupima kimo cha maji.
Ng'ombe walivuka salama na ndipo walipoingia
majini na yeye Kleist maji yakamsomba.
Mohamed Said,Ritz,
Mie si wa kujibizana na huyu.
Hana moja alijualo katika hayo ayazungumzayo.
Rashid Kayugwa kabla hajafa aliwaeleza Waislam
mpango mzima ulivyosukwa.
Kayugwa alistaghfiru na akawa anaswali Mtoro hadi
umauti ulipomfika.
Huyu mtu anaejidai anajua sana nakuachieni nyie.
Hapa aelewi kuwa Al-Jamiyya Islamiyya fil Tanganyika na Al-Dafiwa fil Islamiyya ndiyo waasisi wa AA. TAA. TANU. kwa kumsaidia mweka hazina wa Al-Jamiyya Islamiyya fil Tanganyika Mzee Iddi Faiz Mafongo na ndiyo mweka hazina wa TANU hawa wazee wote walikuwa wakiishi kama ndugu kwa ushahidi msome Nyerere mwanywe hapa chini.Pili, Sheikh alikuwa mwanachama wa Al-Jamiyya Islamiyya fil Tanganyika. Na pia alikuwa mwanachama wa Al-Dafiwa fil Islamiyya. Vyama hivi vya kidini vina uhusiano mkubwa sana na familia ya Sykes.
Kuna nyakati Abdul Sykes alikuwa katibu wa Al-Jamiyya Islamiyya fi Tanganyika.
Nadhani wanaukumbi mmeona siyo familia ya Sykes peke yake ambao walikuwa karibu na hizi taasisi za dini kwa ushahidi mwingine hebu hapa chini tuangalie kazi zipi zilizokuwa zinafanywa na Mufti Sheikh Hassan Bin Amir kupitia hizo taasisi."Mimi nimeanza siasa na wazee wa Dar es Salaam; na wazee wa Tanzania. Nimeanza nao mapema sana; mapema kweli. Nilirudi kutoka masomoni, Uingereza Oktoba 1952 – miaka 33 nyuma. Wakati huo nikiwa kijana mdogo wa miaka thelathini na kidogo hivi.
Al-jamiatul Islamiya (Muslim Association of Tanganyika), andAd-Daawatul Islamiya (Muslim Call) and also the East African Muslims Welfare Society (EAMWS). By using these Societies, Sk, Hassan visited many Countries making Daawa for Muslims and non Muslims. His one student Sk. Ramadhan b. Jaafar told me that Sk. Hassan converted 7 million peoples to Islam. I asked him 7 million or 7 hundred thousand? He told me " Sk. Hassan himself told me that 7 million" (Interview. 2002).
Wanajamvi kwa faida yenu na kwa taifa tunaomba ndugu yetu atupe ushahidi kwa haya maneno yake japo kiduchu atutajie majina ya hao ambao anasema walimtilia shaka Sheikh Hassan Bin Amiri na atufahamishe hizo pesa na mali zililiwa zilkuwa kiasi gani.Sheikh Amir alitiliwa shaka sana na watu wa mikoani kuhusu matumizi ya pesa makao makuu alipokuwa kinara.
Hilo ndilo lilianza kumega mikoa ya Tanga, Bukona na Iringa. Linathibitika katika madai ya mikoa hiyo yaliyotakiwa kutimizwa kabla ya kurudi ndani ya EAMWS.
Madai hayo yakieleza wazi kuwa vyanzo na matumizi ya pesa za EAMWS lazima yawekwe wazi. Sasa kwanini Walii atiliwe shaka na je hapo bado hishma yake inabaki katika uwalii akiwa na ''strings attached''
Naona baada ya kuishiwa hoja unalazimisha lete ushahidi kuwa Mufti Hassan Bin Amir alikua AMNUT siyo kuja na maneno matupu hili kukamilisha matakwa yako.Uhusiano wa Sheikh Amir na familia ya Sykes ndipo ulipozidi kuuma.
Mnakumbuka pia kuhusu AMNUT. Ingawa Mohamed anakanusha kuwa Sheikh Amir hakuwa mwanachama wa AMNUT ningependa pia akanushe kuwa wanafunzi wa Sheikh hawakuwa wanachama na viongozi wa AMNUT.
HIS LIFE AND ACHIEVEMENTS
Sk. Hassan b. Ameir (1890-1979) died on October 8,1979, he was undisputedly one among the international scholars, mubalighs, educationists and Muslim writers in East and Central Africa. He is remembered with ever smiling face and pleasant manners among his students and Muslims of this region as a whole. People who wanted to shake his hand or kiss him or discuss about current views of Islamic education surrounded him everywhere he went. His reputation extended beyond the boundaries of East Africa, from Egypt in the north and South Africa in the south, to Burundi, Ruanda and Congo where he conducted darsas now and then when his Headquarter was in Dar es Salaam at the Ngazija/Commorian Mosque before he was deported to Zanzibar (1968) to complete his ten remaining years of life. His name, conduct and Islamic education theory and ideas spread to every corner of Tanganyika and East Africa because of his great work as a Mubaligh in the East African Muslim Welfare Society -EAMWS- (1945-1968). "Perhaps the most popular teacher in terms of numbers of students in Tanzania (at least after 1940, when he moved there from Zanzibar) was Sk. Hassan b. Ameir Al-Shirazi. His popularity stems from his having traveled extensively throughout East Africa to teach. He eventually settled in Dar es Salaam, where he opened his well patronized Madrasat al Shiraziya in the Commorian Mosque." (August H. Nimtz Jr. 1980. 23).
Je? ilikuwa halali kwa muislam Kreist Mbuwane kushirikiana na makafir kwenda kumpiga vita muislam mwenzie Mkwawa? Je Kufa maji kwa Mbuwane ilikuwa adhabu ya Allah dhidi ya dhulma aliyokuwa anafanyiwa Mkwawa na makafir?
Ndugu Uthman, natoa rai kwako na kwa watu wengine kuwa waangalifu katika kufanya uchambuzi wa masuala mazito kama haya.
Ukiamini kuwa sheikh Chambera alitoa hoja ya kanisa kupinga uhuru kama kanisa, au kuamini kuwa kwavile fulani ni mwislam basi jitihada zake katika uhuru zilichagizwa na Uislam, mwisho wa siku unaweza kujikuta katika maswali usioweza kuyajibu na hivyo hoja zako zikawa teke teke.
Nikukumbushe kwanza ya kuwa siasa na dini kuna wakati zinaingiliana na si kila wakati.
Sheikh Amir, Mufti wa Tanganyika alipingana na wanafunzi wake mmoja wapo akiwa Sheikh Chaurembo juu ya mambo ya kisiasa. Nikuulize, je hilo lilitosha kumuondoa Chaurembo katika Uislam! (Hili la ugomvi wa mwl na mwanafunzi lina hoja naiweka kiporo)
Hili la kusema watu wa imani nyingine ni potofu sana. Si lazima ukubaliane na Mohamed ili uwe mwislam. Na si kila anayekataa habari za Mohamed ni mtu wa imani nyingine. Mbona wapo wa Imani nyingine wanakubaliana na Mohamed?
Sasa kama ukisema watu waliopigania uhuru walichagizwa na Uislam, na nadhani imani inaruhusu kutodhulumiwa, kuna school of thought itakayouliza, hivi znz kituo cha watumwa kuelekea bara Arab kwenye Uislam achilia mbali znz yenyewe kama kitovu cha Uislam East and central Africa, unyama huo ulifanywa kwa Uislam au ulifanywa na watu waliokuwa waislam?
Hebu tuanzie hapo bwana Uthaman
Ndugu yangu Nguruvi3,
Kuna sababu za msingi zilizosukuma taasisi za kiislamu na waislamu kwa ujumla kupambana na ukoloni kwa nguvu zote ukilinganisha na dini nyingine.Lazima ufahamu kwamba wakoloni walipokutana Berlin 1884-85 moja katika ajenda zao kubwa kabisa ilikuwa ni kuhakikisha ustawi wa ukristo katika makoloni yao na kufanya jitihada za kuukandamiza uislamu.Infact all participants regarded islam as the most serious enemy of european colonisation in Africa.
Waislamu ndio jamii ilyoathiriwa zaidi na ukoloni hapa Tanganyika,kwa hiyo siajabu kuonekana wao ndio walikuwa mstari wa mbele kupinga ukoloni.
Kwa mchambuzi wa kweli ulichambua jambo kwa ukweli wake badala ya kuficha baadhi ya vitu kwa visingizio vya udini.
Ukweli unabaki kuwa ukristo ilikuwa ni dini iliyosimamiwa na wakoloni na wakristo walipewa upendeleo mkubwa,na ndio maana makanisa mengi hayakujitokezakuupinga ukoloni.Ila wakristo wengi waliupinga ukoloni kama wao bila kupewa msukumo makanisani.
ahsanta.
[SIZE=+0]@Mohamed Said, Nguruvi3,
..huyu hapa Dr.Njozi.
..nadhani hapo nilipomnukuu panatosha kwa ajili ya mjadala wetu.
Wanajamvi,
Someni Mwembechai Killings Njozi ameweka kila kitu
kuhusu "kuwasha mwenge" chanzo chake na kasherehesha.
Bahati mbaya niko nje na sina lap top yangu vinginevyo hakika
ningebandika taarifa hii.
Ndugu yangu Nguruvi3,
Kuna sababu za msingi zilizosukuma taasisi za kiislamu na waislamu kwa ujumla kupambana na ukoloni kwa nguvu zote ukilinganisha na dini nyingine.Lazima ufahamu kwamba wakoloni walipokutana Berlin 1884-85 moja katika ajenda zao kubwa kabisa ilikuwa ni kuhakikisha ustawi wa ukristo katika makoloni yao na kufanya jitihada za kuukandamiza uislamu.Infact all participants regarded islam as the most serious enemy of european colonisation in Africa.
Waislamu ndio jamii ilyoathiriwa zaidi na ukoloni hapa Tanganyika,kwa hiyo siajabu kuonekana wao ndio walikuwa mstari wa mbele kupinga ukoloni.
Kwa mchambuzi wa kweli ulichambua jambo kwa ukweli wake badala ya kuficha baadhi ya vitu kwa visingizio vya udini.
Ukweli unabaki kuwa ukristo ilikuwa ni dini iliyosimamiwa na wakoloni na wakristo walipewa upendeleo mkubwa,na ndio maana makanisa mengi hayakujitokezakuupinga ukoloni.Ila wakristo wengi waliupinga ukoloni kama wao bila kupewa msukumo makanisani.
ahsanta.
Mzee MS; Baada ya salaam. It is unfortunate sielewi kama hiki kitabu kiko on sale nilisoma somewhere kama vile kilizuiliwa sometime, am I right? Kama kinauzwa I could get a copy.
Unaweza ukatupa ushahidi zaidi kuonesha kwamba lengo moja wapo la wakoloni kuja Africa ilikuwa ni kuudhibiti uislam?
Inawezekana walienda pia South East Asia kudhibiti hinduism na Buddhism?
Uthman; Ukiunda theory inatakiwa ifanye kazi elsewhere. Hayo majibu yako kwa Nguruvi hataeleza kwanini Italy iliivamia Ethiopia kui-colonize huku nayo ni a Christian country. Haitaeleza waingereza kuitawala India, Australia, South Africa, New Zealand. Au Wareno ku-colonise southern America au Wajerumani kuwavamia wenzao huko Europe.
La msingi lazima ujue kila mwanadamu ana uchu wa kuondoa kudhulumiwa. Zimbabwe, Namibia, Angola, kote mapambano yalikuwa ni almost 100% Christians against Christians lakini mmoja ni colonizer. Wasaudia waliwapiga na kuwaondoa waturuki kwa ili hali wote ni moslems 100%.
Please be very objective unapo-analyse such issues.
Nanren,soma katika makubaliano ya Berlin 1884-5 hicho kipengele kipo.tuliposomeshwa historia shuleni kilifichwa makusudi
Ritz,
Mie si wa kujibizana na huyu.
Hana moja alijualo katika hayo ayazungumzayo.
Rashid Kayugwa kabla hajafa aliwaeleza Waislam
mpango mzima ulivyosukwa.
Kayugwa alistaghfiru na akawa anaswali Mtoro hadi
umauti ulipomfika.
Huyu mtu anaejidai anajua sana nakuachieni nyie.
Gombesugu,
Jana nilialikwa Radio Al Nur Masjid Sahaba Zanzibar nifanye
kumbukumbu ya marehemu Ally Sykes tulikwenda mubashara.
Tulikuwa live.
Jamaa walisisimka sana na zilopoanza simu ndiyo ikawa hekaheka
nguo kuchanika.
Nilifungua na uhusiano wa Ally Sykes na Zanzibar Club 1950 akiwa
na uhusiano na akina Himidi Msoma, Dr. Hassan Kingwaba, Dr.
Ahmed Rashid, Ahmed Rashad Ali, Ali Muhsin, Abdillah Masoud Smuts,
Ali Khamis, Mzee Mwinyi Mpiringo, Wadud na wengine wengi.
Nikamaliza na yaliyotokea baada ya mapinduzi...
Mzee wetu MS kuliko kusema Nguruvi3 anajidai anajua sana ni vema ungempinga kwa hoja ili sisi wanafunzi tuzidi kufaidika, asante