Gwalihenzi
JF-Expert Member
- Oct 21, 2011
- 5,125
- 1,301
Jibu zuri analo Mohamed Said!Katiba ya jamhuri ya muungano inasema kila mtu ana haki ya kutoa maoni hiyo ni haki yakona ni mawazo yako sikukatalii mimi ninavyo zichukulia hoja za mzee MS ni sawa na wewe unavyo zichukulia hoja za Nguruvi3,lakini hujajibu swali langu!
Wickama,
Sasa kama ni hivi,tuchukulie vipi yale ma-scandals,unafiki,dhuluma,unyama,ugaidi na machafu mengineyo mengi mno yafanyikayo pale ndani ya Vatican na baadhi ya Makasisi wakubwa mno wa Kikatoliki wakishiriki!?
Nafikiri unaifuatilia kiundani History na lifestyle ya pale Vatican!? Maana majambo mengi mno yafanyikayo mle ndani yanalalamikiwa saana tena kwa miaka mingi mno na watu wa dunia nzima!
Je unafikiri ile Psychology ya pale Vatican na baadhi ya wale Makasisi wake "wachafu",ina uhusiano upi au inamwakilisha vipi Mkristo/Mkatoliki mtiifu mno,mvuja jasho tena maskini pita kiasi,labda wa kutoka Ngaramtoni,Montevideo/Uruguay au Mwisenge!?
Nafikiri tuyaache haya majambo ndugu yangu. Nina imani tumefahamiana japo kiduchu.
Ahsanta.
Cc;Ritz
Ngongo,
Awali ya yoote,nakukumbusha yakuwa japo nilishakusamehe zile kashfa na kebehi ulizonifanzia mara kadhaa hapa jamvini,tena bila hata ya kutumia hoja yoyote... lakini bado sijasahau.
Hilo neno Kamanda,binafsi nahisi limekaa kishari na kuashiria vita/mabaya!? Kwani sisi soote si tupo hapa kutafuta amani na suluhu!? Au wewe ndugu yangu umedhamiria vita hapa jamvini!?
Bakhti mbaya,ile bayana yangu nafikiri wewe binafsi na hata Wickama,hamkunifahamu labda kwa utuvu.
Kwa hakika pale nilikua nasisitiza hoja yangu kwa kunyambulisha vitu kadhaa,katika majadiliano yalokuwapo nafikiri baina yangu, JokaKuu,Iron na Wickama siku chache nyuma.
Kwa kifupi ndugu yangu Ngongo,nilikua nasisitiza yakuwa hata Nyerere kwa kuonyesha mchango unique wa Wazee wetu/Wana Mzizima,ndipo pale alipopatwa na ile guilty conscious probably...siku ya hotuba ya "muago" akataja baadhi ya Wazee wetu na kwa majina fadhila zao kwake na Taifa.
Kwa sababu wengi wenu mnamalumu Sheikh Mohammed,ati anabeza harakati za hao Wazee wa Mikoani/Vijijini...mimi sikubaliani nanyi asilan.
Ndipo nikasema,kama ni hivyo basi wa kulaumiwa ni Nyerere. Kwani katika ile Speech yake ya Muago,kwanini hakutaja hao Wazee wa Mikoani/Vijijini na hizo Family za hao Ma-Chief!? Au nae pia alibeza michango hiyo ya Vijijini!?
Unataka kuniambia ati Nyerere Mkristo mtiifu,alitamka vile kuwapa sifa za bure wale Wazee wetu...kwani hakujua michango na harakati nyingine zozote hapo Tanganyika kama vile za Makanisa,Ma-Chief na Makasisi!?
Ndipo nikasema yakuwa Nyerere ametuachia kigugumizi...maana yake amekuachieni nyinyi kigugumizi. Maana utapingana vipi na maneno au maelekezo ya "Baba wa Taifa"....kwamba Wazee wa Mzizima,ndo wao walomstiri na kumfadhili pita kiasi ndugu yao na mwenzao!?
Naona ndugu yangu Wickama,nae anadai kwamba atleast Gombesugu amethibitisha yakuwa Nyerere alifanya fadhila kwa hao Wazee!?ahaha! Kutajwa jina kwa mchango wako ni haki, na kufanyiwa fadhila ni vitu viwili tafauti.
Nafikiri hiyo sehemu pia ishawahi kunyambuliwa kiundani hapa jamvini.
Yeye Nyerere kuwataja wale Wazee ilikua ni lazima,kwasababu hii ni Historical fact,ya kwamba hata kama kuna "Plots" au harakati nyingine zozote zilizokuwapo sehemu nyingine mbalimbali hapo Tanganyika wakti huo,lakini utakuwa "Maluuni wa Kitaaluma"/Academic dishonesty,kuthubutu kufananisha na yale yalokua yakifanzwa na Wazee wetu/"Wana Kindakindaki" a.k.a Wana Mzizima.
Unataka kuniambia yakuwa Nyerere ati aliwapenda saana Wazee wachache wa KiIslamu kutoka D'Salaam,kuliko hata Wazee wa kutoka Mara au Makasisi wa Peramiho!?ahaha!!
Halafu leo anatokea Yericko,kutwambia ati Nyerere alifanyiwa matambiko makubwa saana na Makasisi!ahaha!!...Jinsi Nyerere alivyokua Mtiifu na mwadilifu wa Kanisa lake,halafu ati asahau hata kutaja hiyo "michango mikubwa" akumbuke tu michango ya Dini moja!?
Najua kabisa Nyerere asingefanza hivyo asilan!
Ndipo pia nilimpa mfano wa kistaarabu,ndugu yangu JokaKuu,kuhusu wale ndugu zetu na Wazee wa Kaskazini walivyoshughulika na ule mgogoro "wao"wa Ardhi kule Meru.
Kumbuka,wao wakti huo inawezekana kabisa walikua pia wana uwezo mzuri hata wa kifedha kuliko baadhi ya sehemu nyingi za Tanganyika...lakini waliamua kujitenga kikanda na kushughulika ki-selfish na huo mgogoro wao huko Kilimanjaro. Ndo maana hata Chadema labda wamerithi dasturi hiyo mbaya!
Lakini wakaamua kupeleka mtu/Mwakilishi wao kipekee bila hata ya klujali au kuhusisha/kushirikisha nguvu zoote na harakati kwa pamoja kwa maslahi ya Tanganyika na Watanganyika woote!?
Nyerere,soote tunajua yakuwa alikua ni "mwerevu wa kisiasa"...nina hakika ya kuwa haya yoote aliyajua kiundani mno na alizingatia saana!...nafikiri pia yaliwahi kumsumbua kichwa japo kiduchu!
Hivi unafikiri,kama wale Wazee wa kaskazini walopeleka Mwakilishi wao kipekee(japo Passport ililazim itolewe/wasaidiwe na Abdilwahid Sykes hapo D'Salaam),kama wangefanikiwa yale maombi/matakwa yao pale UN,Historia yoote ya Tanganyika ingekua vingine hivi leo...na labda Tanganyika pia isingekua nchi moja kama hivi tuijuavyo leo hii!?
Kwa kumalizia kiduchu,ile hotuba ya muago ya Nyerere,kiujumla Waislam takriban woote waliichukulia kama ni kejeli na dhihaka kwao. Zile imbalances na ahadi nyingi walizotegemea,kuahidiwa au kupanga na Nyerere nafikiri havikutimia.
Unajua Ngongo,imenilazim kunena/"kufunguka" hivi vitu ni tu sababu wewe umenidodosa mno. Lakini huwa sipendi na wala si dasturi yangu. Nafikiri ndo maaan pale nilipomjibu JokaKuu kwa ustaarabu/indirectly na kugusia kiduchu hii khabari,lakini wewe hukufahamu mantiki ya yale maelekezo yangu.
Lakini hapo namwachia Sheikh Mohammed Said,maana yeye hiyo ndio field yake kama Mtafiti na MwanaHistoria.
Nafikri ndugu yetu The Big Show nae pia huko awali,aliwahi kuyazungumzia haya masuala kwa kina.
Napenda tumwache Sheikh Mohammed aendelee kuchambua kiundani. Pia Kumradhi labda kama una suali lolote nakusihi pia muelekezee yeye.
Nashukuru kwa kunisikiza huo uchechefu wangu.
Ahsanta.
Cc;Ritz,The Big Show, Sheikh Mohammed Said,Wickama,JokaKuu
Nimeielewa hoja yako Mkuu,hata wewe umeelewa mantiq ya Baru Baru na gombesugu pia,sema unataka kuweka nakshi na kututoa nje ya mstari..
Baru Baru hoja yake kuhusu uchumi wa waislam iko wazi sana,ameegemea zaid kwenye mambo ya biashara kwa kias flan kama sijaelewa tofauti,na ndio kwa maana nakuambia ya kwamba hilo la biashara na uimara wake waislam ndio hasa msingi wao mkubwa awe msomi au asiwe msomi...
Hoja ya gombesugu ni kutengwa kwa waislam kwnye mfumo wa uongozi na serikali ambao serikali hii wameurith kutoka kwa wakoloni na kuwageuza waafrika na watanzania wenzao kuwa ni watwana na wao kuwa mabwana kwenye sytem ya nchi hii kisa tuh hao watanzania wenzao wamejipambanua kuwa na imani ya uislam..
Wickama,
Nashukuru kwa maelekezo yako kiduchu.
Nimekufahamu kiasi,natumai nawe pia umenifahamu.
Ndugu yangu Wickama,sitakutusi asilan! Hayo maneno kwenye bayana yangu wala si matayarisho ya chochote kama ulivyodai. Nahisi hapa "utabiri wako" umekwenda mrama!?
Nakusihi tuendelee na mnakasha wetu kwa staha.
Ahsanta.
Cc;Ritz
Ritz
Nilishasema huna qualification za kughani na mie katika masuala nyeti ya historia
Wewe tubaki kupigiana ngano za mitaa ya kipata na nyamwezi tu
Wickama,
Haina neno,lakini naona umeamua kuhamisha goal posts!? Punguza ujanja!
The way you retreated, you remind me of this:
"I could have become a Soldier if I had waited;I knew more about retreating than the Man who invented retreating"- Private History of a Campaign that failed. By Mark Twain.
Hicho kichefuchefu chako taratibu sijetapikia hapa jamvini.
Ahsanta.
hapo nilipo bold.
Sidhani kama kuna haja tena ya kukujibu wakati wewe mwenyewe huwezi kuthibitisha ila kwa kauli ya haielekei.
Spike,
Kila jambo linakwenda kama Allah alivyolipanga.
Haya ninayoandika mimi leo hii Abdu Sykes aliyaeleza katika ule mpango wa TANU
pale Mwalimu Kihere, Dossa Aziz, Abdu Sykes na Nyerere walipokubaliana iandikwe
historia ya TANU.
Nyerere akamuagiza Dk. Kleruuu afanye kazi na Abdu wakamilishe mswada.
Ofisi yao ilikuwa ile ofisi ya TANU pale Kariakoo na Lumumba.
Abdu alianza kuandika na alianza historia ya TANU kama nilivyoianza mimi.
Nyerere haikumfurahisha....
Mradi ukafa na Abdu hakunyanyua tena kalamu kuandika historia ile hadi anaingia
kaburini.
Nusu karne imepita leo tumekusanyika jamvini huu mwezi wa tano unaingia hatuna
ila tunamtaja Abdu kwa kila hali kiasi wengine wamemkejeli kwa kumwita "Rambo."
Ala kuli hali Abdu Sykes Allah kamrejesha katika historia ya chama alichokiasisi kwa
njia ya kushangaza sana.
Historia ya uhuru sasa si kama ile ya Kivukoni.
Gombesugu,
Ahsante ndugu yangu kwa kipande cha Mark Twain.
Nilikuwa na rafiki yangu James Brenan tunatoka Iowa
City kwa gari ndogo tunakuja Chicago.
Tulipofika mto Mississippi akawa ananionyesha.
Mimi kwa mzaha nikamwambia kuwa asijishughulishe
kwani nilipokuwa mtoto mimi na rafiki zangu Tom Sawyer
na Huckleberry Fin tukiogelea pale.
Ungeuona ule uso wa sahib wangu ulivyopigwa na mshangao!
Naamini umenielewa.
Swadakta yaa akhuy,
Anachotaka kubainisha ni kuchanganya mambo kimakusudi kabisa. lakin mimi nimechambua kiuchumi zaidi na nimempa room ya kukosoa kama ataona nimekwenda tenge. lakin hakufanya hivyo.
Labda cha kumuongezea kuwa Biashara katika Uislam imeelezwa sana na aina gani za biashara na namna ya kuzifanya na hata namna ya kuhifadhi kumbukumbu na namna ya kuweka benki na mifumo yote ya uchumi. na hilo ndilo lipo hewani.
Ahsantum kwa kunielewa na kusaidia kumuelimisha mwenzetu.
maa salaam
Mzee MS; Ungemuuliza anashangaa nini. Mwenzio huenda hakuwa anashangalia mambo ya kuogelea misisipi utotoni pengine alidhani anaangalia zombie ambalo ni brain dead. hahahahahah
Y. Nyerere,Chuma kinachowaka na kuchoma mamilioni ya fedha za Wa Tz huku kikieneza magonjwa ya zinaa na hatari unathubutu kuja hapa na kuusifia Mwenge? unaweza kunitajia hata angalau faida moja ya mwenge? mpaka leo najiuliza ninani aliyeleta wazo la kuwasha mwenge na kuuzungusha nchi nzima huku watu wazima wenyeakili zao wanaukimbiza na kunyanganyana!Nafikiria sana,Mohamed Said na wafuasi wake wanashindwa kutambua kuwa wapo washarika wengi sana wa harakati za Uhuru lakini hawatajwiHivi leo Mmalawi Mzee Nyirenda aliyeupandisha mwenge wa Uhuru mpaka kilele cha Mlima Kirimanjaro katika Nyakati za Uhuru angekuwa ni Muislamu ingekuwaje?
MS,Asanta na shukurani kubwa kwako kutupasha khabari kubwa za Shujaa wetu marehemu Ally Sykes! Allah akulipe kila la kheri duniani na akhera! Mzee Ally Sykes Alla amsamehe madhambi yake na kumpa pepo yake inshaallah kazi aliyoifanya si ndogo!na kaswali kadogo Sheik MS, hapo juu umetaja jina la Chif Makwaia, jee. kuna uhusiano wowote kati yake na Mwandishi Makwaia wa Kuhenga wa channel 10?Gombesugu,Taazia hii nimemwandikia Mzee wangu Ally Kleist Sykes:[FONT=&]Historia ina kawaida ya kujirudia. Ally Sykes mmoja wa waasisi wa TANU, mmoja wa wale watu wasiozidi takriban saba walikuwa katika kamati ya ndani ya TAA iliyounda TANU, mmoja wa wafadhili wakuu wa TANU, mmoja wa askari na hapa nalitumia neno 'askari'' kwa maana yake halisi kwa kuwa ni Ally Syke ndiye TAA hadi TANU ikimtegemea kwa kutekeleza mambo ya hatari dhidi ya Waingereza, amefariki dunia. Ally Sykes ndiye alikuwa akipewa kazi za hatari za kumwaga 'sumu na -----'' dhidi ya serikali. Sumu na ----- huu yalikuwa makaratasi aliyokuwa akichapa nyumbani kwake usiku makaratasi ambayo Waingereza waliyaita makaratasi ya 'uchochezi.'' Waingereza na makachero wake walikuwa wanamjua Ally Sykes vizuri. Waingereza walikuwa wakijua kuwa alikuwa na medali ya mlenga shabaha bingwa aliyopata Vita Kuu ya Pili ya Dunia. Huyu ndiye Ally Sykes mzalendo muasisi wa TANU ambae sahihi yake ndiyo iko katika kadi ya TANU ya Baba wa Taifa, amefariki Nairobi Jumapili iliyopita alikokwenda kwa ajili ya matibabu. [/FONT] [FONT=&]Siku ile ile ya Jumapili milango ya mchana mchanga kabisa kabla ya adhuhr taarifa ikawasili Dar es Salaam kuwa Ally Sykes amefariki dunia. Ghafla mji wa Dar es Salaam alikozaliwa na akaendesha harakati zake dhidi ya ukoloni wa Waingereza ukgubikwa na simanzi. Kila simu iliyokuwa ikipokelewa na wengi ilikuwa ni kutaka kuthibitisha kifo kile. Binafsi simu zikaanza kumiminika kwangu za kunipa pole. [/FONT] [FONT=&] Hadi kufika jioni habari zikawa zimeenea mji mzima kuwa ni kweli Ally Sykes hayuko tena duniani. Haukupita muda siku ile ile maiti ya Ally Sykes ikawasili Dar es Salaam kwa ndege ya kukodi ikiwa imesindikizwa na mkewe Bi Zainab na baadhi ya wanae wakiongozwa na mtoto wake wa kwanza wa kiume Abraham Sykes. Siku ya pili Jumatatu magazeti yote yalikuwa yametoka yakiwa hayana taarifa yoyote ya kifo cha Ally Sykes. Hii iliwashangaza watu wengi sana isipokuwa mimi. Sikushangaa kwa kuwa nilikuwa najua siasa za historia inayomzunguka Ally Sykes kwa miaka mingi hususan kuhusu mchango wake binafsi na wa kaka yake marehemu Abdulwahid Sykes katika harakati za kuasisi TANU na kudai uhuru wa Tanganyika.[/FONT] [FONT=&]Historia ina kawaida ya kijurudia. Haya ya kupuuza kifo cha Ally Sykes yalimkuta pia kaka yake Abdulwahid alipofariki mwaka 1968. [/FONT][FONT=&]Ally Sykes alikuwa mtu maarufu kupita kiasi. Alikuwa kwanza ana umaarufu wa kuzaliwa. Kazaliwa Dar es Salaam Gerezani, mtoto wa mjini. Kisha alikuwa maarufu kwa nasaba. Baba yake Kleist Sykes alikuwa mmoja wa watu mashuhuri katika siasa zote za Dar es Salaam katika miaka ya ya mwanzo ya 1900 hadi alipofariki mwaka 1949. Baba yake alikuwa maarufu kwa kuwa alilelewa na Affande Plantan askari kiongozi katika jeshi la Wajerumani lilokuja Tanganyika na Herman Von Wissman wakati Wajerumani walipoingia kuitawala Tanganyika. Kleist alikuwa ndiye katibu muasisi wa African Association mwaka 1929 chama kilichokuja baadae kujibadili na kuwa TANU Ally Sykes akiwa mmoja wa hao waasisi. Baba yake Kleist aliasisi Al Jamiatul Islamiyya Fi Tanganyika (Umoja wa Waislam wa Tanganyika) na kupitia jumuia hii akajenga shule ya kwanza ya Kiiislam Dar es Salaam, shule ambayo ilisomesha Qur'an pamoja na masomo ya kisekula. Hii Al Jamiatul Islamiyya ndiyo iliyotoa viongozi wa kwanza kuiendesha TAA na baadae TANU katika harakati za kudai uhuru. Ally Sykes kwa mazingira na makuzi haya akawa maarufu kama alivyokuwa baba yake. Lakini kubwa zaidi na hili ndilo kwa bahati mbaya ndilo linalojulikana zaidi kwa sasa ni utajiri ambao Allah alimruzuku toka akiwa kijana mdogo sana katika miaka ya 1950 alipoanza biashara kwa kuanzisha kampuni yake binafsi iliyoitwa Sykes Sales Promotion Consultancy. [/FONT] [FONT=&]Inajulikana na wengi Ally Sykes na kaka yake Abdulwahid Sykes ndiyo watu wa mwanzo kumpokea Julius Nyerere alipokuja Dar es Salaam mwaka 1952. Nyerere alifika nyumbani kwa akina Sykes kwa utambulisho na hii ilijenga urafiki ambao ulipitiliza na kuwa udugu mkubwa wa mapenzi ya dhati si baina yao tu bali hata kwa wake na mama zao. Mama yake Nyerere Bi Mugaya hakuwa akipungua nyumbani kwa Mama Abdu Bi Mrurguru biti Mussa Mtaa wa Kirk. Halikadhalika Maria Nyerere hakuwa akipungua nyumbani kwa aidha kwa Bi Zainab mkewe Ally Sykes Mtaa wa Kipata au kwa Bi Mwamvua mkewe Abdulwahid Sykes Mtaa wa Aggrey. Wakati huu Abdulwahid ndiye akiwa rais wa TAA na harakati za kuanzisha TANU zimepamba moto achilia mbali hila na fitna za Waingereza kuwatokomeza viongozi shupavu wa TAA kama Hamza Mwapachu, Dk. Vedast Kyaruzi, Dk. Wilbard Mwanjisi nje ya Dar es Salaam kukivunja nguvu chama. Ndiyo maana TANU ilipokuja asisiwa mwaka 1954 Ally Sykes kadi yake ya TANU ikawa namba 2, Nyerere namba 1, Abdulwahid Sykes kadi yake namba 3, Dossa Aziz kadi namba 4, John Rupia kadi yake namba 7. Historia hii haikuja bure ina maelezo marefu ambayo hapa hayataweza kuenea.[/FONT] [FONT=&]Kipindi hiki Ally Sykes alikuwa Katibu wa Tanganyika African Government Servants Association (TAGSA) na vilevile alikuwa mwakilishi wa chama hicho katika Kamati ya Uajiri ya Serikali (Government Establishment Committee). Thomas Marealle ndiye alikuwa rais wa TAGSA na Rashid Kawawa alikuwa mwanakamati. Wanasiasa hawa vijana Ally Sykes akiwa mmoja wao wenyewe walijipa jina, 'Wednesday Tea Club'' wakikutana kila siku ya Jumatano kunywa chai pamoja na kutumia wakati ule kupanga mikakati ya kuwang'oa Waingereza katika ardhi ya Tanganyika. Kupitia Ally, Abdulwahid na Dossa Aziz Nyerere akaweza kujuana na wenyeji wa Dar es Salaam maarufu katika hao ni Sheikh Hassan bin Amir, Mshume Kiyate, Jumbe Tambaza, Sheikh Suleiman Takadir, Clement Mtamila, Bi. Titi Mohamed, Tatu biti Mzee na wengineo. Lakini historia ina kawaida ya kujirudia. [/FONT] [FONT=&]Kifo cha Ally Sykes kimepuuzwa na vyombo vya habari kama nilivyoeleza awali kuwa hata kifo cha kaka yake Abdulwahid Sykes alipofariki mwaka 1968 magazeti ya TANU (wakati ule 'The Nationalist'' na 'Uhuru'') chama alichokiasisi kwa jasho, damu na fedha zake magazeti haya yalipuuza kifo hicho. Kuna watu katika TANU katika kipindi kile walikuwa wanajaribu kuifuta historia ya kupigania uhuru wakitaka kuondoa mchango wa Abdulwahid na Ally Sykes katika historia ya uhuru. Hata hivyo 'Tanganyika Standard'' gazeti ambalo ndilo liliokuwa likilinda maslahi ya ukoloni Tanganyika, ndilo lililoandika taazia ya Abdulwahid Sykes. Mhariri wa Tanganyika Standard Brendon Grimshaw hakuweza kustahamili fedheha ile, aliandika taazia ambayo itaishi zaidi ya miaka miaka mia moja na zaidi. Taazia ile ilitikisa fikra Makao Mkuu ya TANU Mtaa wa Lumumba na ikawakera wengi. Grimshaw alisema katika taazia yake kuwa TANU imeundwa pakubwa kwa mchango wa ukoo wa Sykes. [/FONT] [FONT=&]Narudia tena. Historia ina kawaida ya kujirudia. Mwaka wa 1968 wakati Abdulwahid anafariki Waislam walikuwa wako katika taharuki kubwa ya kile kilichokujajulikana kama 'mgogoro wa East African Muslim Welfare Society (EAMWS) taharuki iliyojaa simanzi kwa kuwa Mufti wa wakati ule Sheikh Hassan bin Amir mmoja wa masheikh viongozi katika TANU alikuwa kakamatwa na kufukuzwa nchini kwa amri ya Nyerere. Wakati haya yakijiri, Tewa Said Tewa na Bi.Titi Mohamed viongozi wa juu wa EAMWS walikuwa wakiandamwa na Nyerere na hapakuwa na uelewano mzuri baina yao. Ajabu ni kuwa umauti umemkuta Ally Sykes katika hali kama ile ile iliyokuwapo wakati kaka yake alipofariki dunia mwaka 1968 wakati nchi ikiwa katika mgogoro wa EAMWS kishindo ambacho kilidumu takriban miezi mitatu. Ally Sykes kafa wakati nchi ipo katika taharuki kwa kile kinachodaiwa 'uadui baina ya Waislam na Wakristo.'' Kwa hiki kifo cha Ally Sykes bila shaka wahariri wa magazeti walikuwa wameshughulishwa katika kutafuta habari mpya za 'kuchomwa makanisa'' na 'ugomvi wa kuchinja,'' hawakuwa na muda wa kufuatilia msiba wa muasisi wa TANU marehemu Ally Sykes. Lakini iweje hali iwe kama vile miaka saba tu baada ya uhuru kupatikana nchi iingie na taharuki ya kiasi kile na hivi sasa taharuki ile ijirejee upya tena ikishuhudiwa na waasisi wa harakati za ukombozi? [/FONT] [FONT=&]Ilikuwa nimemaliza kuandika kitabu kuhusu maisha ya kaka yake Ally Sykes kitabu kilichokujajulikana kama 'The Life and Times of Abdulwahid Sykes (1924 - 1968) The Untod Story of the Muslim Struggle Against British Colonialism in Tanganyika.'' Ally Sykes alinikabidhi nyaraka zake katika utafiti wa maisha ya Abdulwahid Sykes.[/FONT] [FONT=&]Nyaraka hizi mpaka Ally Sykes anakufa zilibaki kuwa sehemu ya malalamiko yangu kwake kuwa hazikustahili kuwa mikononi kwake na kazifungia katika 'safe'' zake. Nilikuwa nikamwambia mara kadhaa inagawa hakutaka kunisikiliza kuwa nyaraka hizi ni mali ya taifa la Tanzania lazima azikabidhi serikalini kwa kuhifadhiwa na kuwekwa Tanzania National Archive (TNA) kama urithi wa kizazi kijacho. Yeye siku zote akinambia, 'Mohamed hizi nyaraka ninaogopa nikiwapa serikali watazichoma moto.'' Alikuwa na sababu ya kusema vile. Nyaraka za Ally Sykes zinakwenda nyuma kiasi cha miaka mia moja kuanzia siku babu yake Sykes Mbuwane alipotia mguu katika ardhi ya Tanganyika kutoka meli ya kvitia ya Wajerumani pale Pangani akitokea Msumbiji. Nyaraka zile zina barua za wanasiasa wa mwanzo katika Tanganyika achilia mbali habari za baba yake. Ukianza kufunua majalada yale hutachoka kupekua karatasi baada ya karatasi. Nyingine zimechoka kwa umri mrefu. [/FONT] [FONT=&]Katika majalada yale utakutana na wazalendo na machifu, utakutana na wasiasa wenye asili ya Kiasia na Waingereza wenyewe waliokuwa watawala. Katika nyaraka zile utawaona na utawasikia watu hawa wakizungumza na wewe: Dk Joseph Mutahangarwa, Chief Abdieli Shangali wa Machame, Paramount Chief Thomas Marealle wa Marangu, Chief Adam Sapi Mkwawa wa Wahehe, Chief Harun Msabila Lugusha, Dk. Wilbard Mwanjisi, Abdulkarim Karimjee, Dk Vedas Kyaruzi, Liwali Juma Mwindadi, H.K. Viran, Stephen Mhando, Dossa Aziz, Ivor Bayldon, Yustino Mponda, Ivor Bayldon, Rashid Mfaume Kawawa, Bhoke Munanka, Rashid Kheri Baghdelleh, Robert Makange, Saadani Abdu Kandoro, Malkia Elizabeth, Chief Secretary Bruce Hutt, Gavana Edward Twining, Gavana Ronald Cameron, Mwalimu Thomas Plantan na ndugu zake - Schneider Abdillah Plantan na Ramadhani Plantan, Mwalimu Mdachi Shariff, Mwalimu Nicodemus Ubwe, Kassela Bantu, John Rupia, Hamza Kibwana Mwapachu, Othman Chande, Leonard Bakuname, Stephen Mhando, Oscar Kambona, Peter Colmore, Albert Rothschild, Ali Mwinyi Tambwe, Alexander Thobias, Japhet Kirilo, Joseph Kimalando, Ian Smith, Roy Welensky, Jim Bailey, Kenneth Kaunda, Meida Springer, John Hatch, Gretton Bailey, Brig. Scupham, Dome Okochi Budohi, Annur Kassum, Nesmo Eliufoo, Yusuf Olotu, Joseph Kimalando, Julius Nyerere na wengine wengi wakubwa kwa nyadhifa walizokuja kukamata katika Tanganyika huru na wale walioanguka njiani. [/FONT] [FONT=&]Ukikaa na Ally Sykes na mkapitia jina moja baada ya jingine utapata habari za wazalendo na watu hawa na historia yao yote na kwa hakika hiyo ndiyo historia ya uhuru wa Tanganyika na historia ya kweli ya TANU. Ally Sykes alikuwa anawajua watu hawa vilivyo. Atakuambia yupi alikuwa kibaraka wa Waingereza na yupi alikuwa mpiganaji wa kweli. Atakueleza nani alikuja katika siasa kwa uzalendo na nani alikuja kwa ajili ya kutafuta maslahi yake binafsi.[/FONT] [FONT=&]Ally Sykes kabla hajafa alikuwa keshamaliza kuandika historia ya maisha yake. Mswada huu unaitwa, 'Under the Shadow of British Colonialism in Tanganyika.'' Mchapaji alipomaliza kuhariri mswada ule aliomba kitabu kibadilishwe jina kiitwe, 'Dreams Unfulfilled.'' Mhariri alinipigia simu kutola Nairobi akanambia kila akimsoma Ally Sykes alikuwa anamwona Ally Sykes katika majonzi kwa kuwa ndoto aliyokuwanayo wakati akipigania uhuru wa Tanganyika ndoto ile haikukamilika. Aliniomba nimuombe Ally Sykes jina la kitabu libadilishwe. Kwake Ally Sykes suala halikuwa kugawana vyeo ndani ya chama cha siasa na kisha katika Tanganyika huru. Suala lilikuwa kwa Mwafrika kuwa huru katika nchi yake bila ya kubughudhiwa na mtu yeyote yule. Mwaka 1953 ilikuja shinikizo kubwa kutoka kwa Ivor Bayldon kuunda chama kitakachojumuisha wananchi wa rangi zote katika Tanganyika. Ally Sykes alikuwa akisema laiti kama wangekubali kumeza chambo kile historia ya Tanganyika ingekuwa nyingine na TANU isingeliasisiwa pale New Street mwaka 1954 katika nyumba ile ambayo ilijengwa na kukamilika mwaka 1933 wakati wa uongozi wa baba yake; na Nyerere asingelikuja kuwa kiongozi wa nchi hii. 'Laiti Bwana Abdu na Hamza Mwapachu wangelikubaliana na ule mpango wa akina Ivor Bayldon na Nazerali uongozi wa nchi huu ungelitoka ndani ya Baraza la Kutunga Sheria la wakoloni, usingelitoka kwetu sisi Waafrika wazalendo wenye uchungu na nchi hii na huenda rais wa Tanganyika angelikuwa Chief David Kidaha Makwaia na Nyerere angelibakia kuwa mwalimu wa shule pale Pugu.'' Ivor Bayldon baada ya kushindwa kuwapata wanachama wa TAA alikuja baadae mwaka 1955 kuunda United Tanganyika Party (UTP) chama kilichokuja kupinga TANU. Hii ndiyo namna nyaraka za Ally Sykes zinavyozungumza na wewe unapozisoma na pale yeye mwenyewe anapokupa maelezo hutaacha kupigwa na butwaa na mshangao. [/FONT] [FONT=&]Nilipata kumuuliza Ally Sykes kama anajua ni fedha kiasi gani alizopata kutumia katika TAA na TANU jibu alonipa ni kuwa hajui wala hajuti. 'Hizo fedha si kitu kikubwa. Kubwa ni njama ambayo niliundiwa na Waingereza wawili Dk Hughes na Dk Frank kutaka kuniua wakati nikifanya kazi Kibongoto Infectious Disease Hospital, Moshi. Unajua Waingereza kwa kweli walikuwa wamechoka na hili jina letu. Kila Gavana aliyekuja kutawala Tanganyika alikuwa lazima atapambana na jina hili. Baba yetu aliitwa kuhojiwa na kila gavana aliyekuja kutawala Tanganyika kuanzia mwaka 1927 hadi 1947. Kati ya mwaka 1929 hadi 1947 Mzee Kleist aliitwa kuhojiwa mbele ya 'tribune'' mara tatu kuhusu harakati za wafanyakazi, yeye akiwa katibu wa Railway African Civil Service Union. Waingereza walikuwa wamechoka sasa na sisi wakaaamua kuniua kwa kuniambukiza kifua kikuu. Hawa madaktari wawili walikuwa wakiniita mimi 'rafiki yake Nyerere'' ambaye kwao wao alikuwa adui mkubwa sana. Wakati ule kunasibishwa na Nyerere halikuwa jambo jema. Hicho kilikuwa kitu cha hatari na cha kutisha sana. Mimi sikuwa nakataa kuwa Nyerere alikuwa rafiki yangu. Kwa Waingereza hiyo ilikuwa kama vile kujinasibisha udugu na Adolf Hitler. Hii ilikuwa mwaka 1956 na ingawa mimi nilikuwa nimepewa uhamisho kufanyakazi Kibongoto, Moshi ili kuniweka mbali na TANU pale New Street bado nilikuwa nikijitahidi kukijenga chama pale nilipokuwapo. Mimi na Bwana Abdu, Dossa, Mzee Rupia, Nyerere na Baraza la Wazee wa TANU chini ya Mwenyekiti wake Sheikh Suleiman Takadir tulikuwa tukiitumikia TANU kwa nguzu zetu zote na ni wakati huu ndipo nilipompiga muuguzaji wa kike Mzungu Ocean Road Hospital kwa ajili ya ubaguzi wake na matokeo yake nikasimamishwa kazi na niliporejeshwa nikapelekwa uhamishomi Mtwara kama adhabu '' [/FONT][FONT=&][/FONT] [FONT=&]Mtu usingeweza kuchoka kumsikiliza Ally Sykes anapohadithia historia ya mapambano dhidi ya ukoloni. Ilipokuwa sasa inakaribia kupatikana kwa uhuru anasema, 'Allah akanifungulia milango zaidi kwa kuwa sasa nikishirikiana na rafiki yangu Peter Colmore na kampuni yake ya High Fidelity Productions kutoka Nairobi tukawa tumeshika biashara yote kubwa ya uwakilishi wa makampuni makubwa yaliyokuwa Afrika ya Mashariki - Coca Cola (East Africa) Ltd; The Cooper Motors Corporation Ltd; The Shell Company of East Africa Ltd, Aspro Nicholas Ltd; Gailey and Roberts Ltd; Bata Shoes Company Ltd; Kenya Broadcasting Service, Cotton Lint and Seed Marketing Board, Raleigh Industries of East Africa Ltd; na tulikuwa wawakilishi Kenya wa Tanganyika Broadcasting Corporation (TBC) lakini mafanikio yana matatizo yake hii nilikujajua baadae sana uhuru ulipopatikana. Sisi tuliokuwa mstari wa mbele tukawa hatuhitajiki tena na husda na fitna ikaingia baina yetu sisi waasisi wa TANU na Nyerere '' Haikuwa rahisi kuacha kumsikiliza Ally Sykes akiieleza historia ya TANU, uhusiano wake na Nyerere na yote yaliyotokea hadi aakafutwa kabisa katika historia ya uhuru wa Tanganyika.[/FONT] [FONT=&]Hatuwezi kummaliza Ally Sykes. Ally Sykes aliishi maisha kamili. Allah alimruzuku kila kitu na akampa dunia. Mguu wake ulikanyaga pale alipotaka. Mimi binafsi nimeshuhudia nguzu zake kwa macho yangu mwenyewe. Wazungu wakimtetemekea na akiwatuma kazi na wakimtumikia kwa adabu na unyofu wa hali ya juu. Mmoja wa jamaa za Ally Sykes, Mzee Ahmed Rashad Ali alipata kunambia kuwa Ally Sykes akiwatuma Wazungu toka ujana wake na anapowaita kuja kula nyumbani kwake wakija na adabu zao kamili. Juu ya haya yote Ally Sykes alikuwa na ibra moja - hakuwa mtu wa kujiona. Hukuweza kupima nguvu na uwezo wake kwa kumtazama. Nilisikitika sana mazikoni pale Makaburi ya Kisutu. Wale waliompuuza Ally Sykes na kuufanya mchango wake si lolote si chochote ndiyo walipewa heshima ya wao kuwa mbele pale makaburini katika kumsindikiza katika safari yake ya mwisho na kusoma hotuba. Rafiki zake aliokuwanao siku zote, Abdallah Awadh, Ali Mbarak, Shomari, Abdu Faraj, Boi Juma Risasi, Harudiki Kabunju, Hussein, Abdu Kifea, Abdallah Jabir, Muharram Kocha, Muharram Mkamba, Abdubari, Salim Hirizi kuwataja wachache waliwekwa mbali na jeneza na kaburi na watu wa Itifaki wa Ikulu nafasi yao ikachukuliwa na wanasiasa na viongozi wa juu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM). Ilikuwa aibu kubwa kwa CCM kuonekana hawapo katika kumzika Ally Sykes mwanachama wa TANU kadi namba mbili na mzalendo wa kweli aliyemwandikia na kumkabidhi kadi namba moja ya TANU Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere. [/FONT] [FONT=&]Ally Sykes alimpenda na kumuheshimu sana kaka yake na katika maisha yangu ndiyo mtu pekee niliyemsikia kila akimtaja kaka yake anatanguliza neno, ''Bwana.'' Kwake yeye Abdulwahid alikuwa 'Bwana Abdu'' kila alipomtaja. Ally Sykes amezikwa pembeni mwa kaburi la kaka yake Bwana Abdu.[/FONT] [FONT=&]Tunamwomba Allah amlaze Ally Kleist Sykes mahali pema peponi.[/FONT] [FONT=&]Mohamed Said[/FONT] [FONT=&]22 Mei 2013[/FONT][FONT=&]Ally Kleist Sykes[/FONT][FONT=&]1926 - 2013[/FONT][FONT=&]Mzalendo Muasisi wa TANU aliyemwandikia na Kumkabidhi Julius Nyerere Kadi ya TANU Na. 1[/FONT]
RITZ,Nyundo zote hizi ulizomgonganazo Yericko kichwani! kwakuwa kachunwa uso ama hatajibu au atakuja na uongo mwingine!Yericko Nyerere,Naona bado unaedelea na porojo zako unaogea maneno mengi bila ushahidi wa data za kutosha ngoja nidadavue kiduchu bayana zako.Wanajamvi hebu hapa chini tumsome Nyerere mwenyewe anavyoelezea harakati za uhuru wetu hakuna anayesema kuwa walikuwa wanapigania uhuru wa dini hawa wazee waliokuwa wanamjenga kijana wao Nyerere walikuwa Waislam.Wanajamvi mpaka Nyerere anatangulia mbele ya haki ameelezea mara moja tu dua aliyofanyiwa na Wazee wa Dar es Salaam haya maneno Yericko sijui kayatoa wapi chini hapa tumsome Nyerere mwenyewe.Wanajamvi tuendelee kumsoma Nyerere mwenyewe hapa chini halafu tulinganishe na haya maneno ya ndugu yetu Yericko. Yericko Nyerere, hapa chini naona umemua kwadanganya wanajamvi hawo niliobold hawakuwemo kwenye hiyo safari Abbas Sykes alikuwemo kwenye hiyo safari lakini kutokana hujui chochote ameamua kijiandikia.Ahsantum...
AAAA, Yericko hapa ndipo ulipofika? tutafika kweli?RitzNilishasema huna qualification za kughani na mie katika masuala nyeti ya historiaWewe tubaki kupigiana ngano za mitaa ya kipata na nyamwezi tu
Duh, naona mambo yanazidi kunoga, JF ni zaidi ya tuijuavyo na kweli duniani kuna mambo.. gombesugu hata wewe una uthubutu wa kutamka maneno kama hayo hapo juu! Kama ingekuwa ni swala la kuzikana kwa uongo, mbona mwalimu wako wa darsa Mohamed Said keshazikwa zamani na kusahaulika siku nyingi tu! Unakumbuka listi ya uongo wake uliodumu miaka 15 hadi ilipovinjari kwenye anga za JF! Lakini hayo tuyaache, nina maswali manne tu kwako wewe, ma Shariff na ma AL Akhiy wote katika mnakasha huu;Yaani kwa kifupi credibility ya Yericko ni kiduchu mno. Kumbuka ni yeye pekee mpaka sasa hapa Jamvini alodai na kutoa informations mbovu/za urongo...
Lakini nime-noticed amefanya correction kule kwenye kianzio cha mada hii, tangia siku ile ulimpobainishia ukinyonga wake!ahah!!...ama kweli kutahayari si kufa...la si hivyo maskini ndugu yetu Yericko angalikua nae tumeshamzika hivi sasa!?
AAAA, Yericko hapa ndipo ulipofika? tutafika kweli?