Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar

Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar

Wickama,

Kama ni kweli unakwenda kutembelea SUA;nafikiri uliwahi kusema yakuwa ulisomea Pedology....tafadhali mpe salaam zangu nyingi jamaa yangu Dr. Balthazar Msanya.

Mwambie jamaa yako wa Vienna mliokua woote Jarumani early 1990's,nina hakika atacheka saaana!

Tafadhali pia niombee kwa Nguruvi3,ajibu yale maswali ya uchochezi wa amani hapo nchini na labda pia ugaidi niliyomwekea jana dhidi ya wenzenu Yericko n Mwanakijiji!?

Sisi kwa ustaarabu wetu,hatupendi kujaza server kwa kurudia maswali yayokwayayo...kwahiyo Nguruvi3 na Wanajamvi khasa wale wafuatiliao huu mnakasha kwa karibu wanajua madai/shutuma zetu!

Ahsanta sana.

Gombesugu; Professor Msanya ndiye msimamizi wangu wa Masters. Research work tulifanyia Mbinga District, Kitanda village, tulipanda milima na kuchimba soil profiles kiroho mbaya. A very strict scholar. Nashukuru kama mlikuwa wote Ghent. Nikipata fursa nitaku-PM namba yake ya simu umsalimie. Shukran. Kwa Nguruvi nimekusikia.
 
Gombesugu, Mag3 kasema katika hao wanopiga simu kuhusu Lawi basi ajitokeze mmoja. Na kisha kasema mbona haya yameandikwa siku nyingi hakuna aliyeshtuka.

Najaribu kufikiri kuwa hivi mtu akiniita mimi kafir (kama ninavyoitwa na akina al-khiy) au mpagani au imani nyingine, hilo linaweza vipi kufikia mahali pa kunikosesha usingizi au kunituma nikamate simu eti kwa ghadhabu!!!

Endapo hilo linasababisha usumbufu kama inavyodaiwa, basi nakuhakikishia kuwa Wazanzibar watabeba mawe na wala si simu.
Mtu babu yake atolewe roho, mwingine aachwe mjane, wengine mayatima halafu umwambie kuwa mpendwa wao alikuwa msaliti tena unasema msaliti wa dini ili huko aliko adhabu ya mola imshukie vilivyo, huyo kweli akuache bila kukupopoa mawe!

Pili, umesema mimi na Mag3 tunajifanya tunajua kila kitu, pamoja na kauli yako ya kejeli ukweli unatabia ya kujitenga na uongo na wala mwanga na giza havikai pamoja.

Tatu, nashukuru sana kusikia wewe na Mohamed Said(tumeishi na tunaishi) na historia!
basi tudadavulieni haya kwasababu yapo within your reach!


Muheshimiwa Nguruvi3,

Nashukuru tena kwa bayana yako hii dhaifu na nyonge mno...poleni saana!

Unajua yakuwa Mag3,kwa kitambo sasa analeta informations/statistics za urongo na upuuzi,khasa tangia yalipoanza malumbano ya khabar za Zanzibar.

Binafsi nilikua nikimdodosa kiustaarabu....lakini kama kawaida yenu,kwakuwa mmeshaaminishwa yakuwa Watu wa Madrassa woote hawajui kitu/hawajasoma,kuna baadhi ya Viwavi wenzenu hapa wakafikiri ati mimi naulizia vile kwasababu sijui hizo khabar au sources zake!?ahaha!!

Sasa Shariff Ritz,ameamua kumfungulia shughuli kwa hiyo acha kumtetea huyo Mag3 wako!? Jaribu kufikiria for a second kama hizo informations za urongo angeleta Sheikh Mohammed ingelikua vipi wewe na wafuasi wako!?

Punguza au ukiweza tafadhali acha kabisa spinning,hivi nani aliewahi kukwita wewe ni Kafir hapa jamvini ndugu yangu Nguruvi3!? Wewe mwenyewe binafsi mara ngapi unaandika posts khalafu unaweka Cc;...kwa Makafir woote!? Hivi unakua na maana gani!?

Mimi binafsi hapahapa jamvini,nilishawahi kumwambia mtu fulani yakuwa asitumie kabisa hilo neno...na kwakuwa huyo mtu alijisema yeye ni Muislamu,basi pia nikamnyambulia kiduchu baadhi ya vitu/mifano kutoka kwenye Uislamu.

Jaribuni kuwa waungwana na kukumbuka shukran/fadhila japo kiduchu ndugu zetu,au mnataka kuwa kama Nyerere a.k.a "Baba wa Taifa"!?

Unadai yakuwa Sheikh Mohammed;ati atapigwa mawe na WaZanzibary!?ahaha!!

Nakufahamisha yakuwa Wazanzibary;huwajui/hamuwajui na hamtawajua maisha yenu yoote! Ningekwambia mengi lakini leo huu mji niliopo ni ugenini, na jua limetoka uzuri mno...nahitaji kwenda kula Ice Cream kiduchu.

Lakini kwa kifupi,Sheikh Mohammed,Unguja/Zanzibar yoote ni kwao saana tena saana. Hayo mawe utapigwa/mtapigwa nyinyi "machogo" kama ulivyowahi kujiita wewe mwenyewe hapa jamvini!

Mwambie Mag3;atake radhi Wanajamvi na aache kutoa excuse za kitoto...ati ooh "nikipata nafasi" nitajibu hoja zao!...excuse me!?ahaha!!

Nawewe ndugu yangu Nguruvi3;nakuheshimu mno...lakini nakusihi kuanzia sasa unapofanza mawasiliano nami au kujibu posts zangu nafikiri ni bora uiniwekee post yoote/nzima,sababu nakhis Wanajamvi wasije kuwa misled na "majibu" utoayo kwangu.

Nimefurahika mno kukusikia tena.

Nakuombeni jibuni maswali yoote mliyoyakalia kwa kitambo sasa;kumbuka huu mnakasha ni kuhusu Uchochezi,Ugaidi na Uhaini!?

Ahsanta sana.

Cc;Ritz
 
Gombesugu; Professor Msanya ndiye msimamizi wangu wa Masters. Research work tulifanyia Mbinga District, Kitanda village, tulipanda milima na kuchimba soil profiles kiroho mbaya. A very strict scholar. Nashukuru kama mlikuwa wote Ghent. Nikipata fursa nitaku-PM namba yake ya simu umsalimie. Shukran. Kwa Nguruvi nimekusikia.


Wickama,

Ahsanta nitafurahi saana,fanya hivyo ukipata nafasi plse!

Pia nitampa malalamiko ya visa anavyonifanzia mwanafunzi wake kila kukicha hapa jamvini!?ahaha!!

Tuendelee na mnakasha.

Ahsanta.
 
Wanajamvi,

Nadhani mwenye akili na macho ameona uhalali na uhalisia wa madai yangu yaliyobeba kichwa cha uzi huu yasemayo,

"Uchochezi wa Mohamedi Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar"

Mohame amelidhihirishia jukwaa hili kuwa yeye ni waaina gani katika Tanzania,

Nadhani kwahilo limepita, tumejiridhiya kuwa madai ya Uchochezi wa Mohamedi Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar ni halisi,

Naomba tusonge mbele kuendelea kuuweka wazi Uchochezi wa Mohamedi Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar ili dunia ione na kuelewa huyu mzandiki alivyo!



Yericko,

Tafadhali jaribu kuupa hishma huu mjadala/mnakasha pia nasisi Wanajamvi wenzio.

Tafadhali acha kabisa kujipa matumaini au kujaribu ku-summarise/conclude huu mnakasha au madai ambayo unajua kabisa hatujafikia popote wala kujadili lolote,na wewe binafsi na wafuasi wako mmeshindwa mpaka sasa kuyathibitisha!!

Kumbuka kuna Wanajamvi wengi saana na watazamaji ambao hawaoni hayo madai yenu dhidi ya Sheikh Mohammed kuwa yana ukweli ndani yake!

Mimi binafsi nakuona wewe ndie mchochezi wa amani hapo nchini,na pia nina hakika wapo wengi wenye msimamo/mtazamo kama huu!

Nakusihi tena,thibitisha kwa kina au kwa nyaraka zozote ulizonazo yakuwa Rais Jakaya Kikwete ndie anayemkingia kifua Sheikh Mohammed ili kuleta/kuendeleza chokochoko na uchochezi hapo nchini kama ulivyodai/unavyodai hapa jamvini!?

Huu mjadala,ni wa maana saana,kwahiyo usijaribu kuufanza kama vile ni majadiliano ya vijiweni au mashabaki wa football...lazim tufuate steps zoote. Lakini sio unakurupuka tu wewe binafsi au na kikundi chako kudai ati ooh!...tayari leo ndo tushaona Ugaidi,uchochezi na uhaini wa Sheikh Mohammed!? Mbona unaleta mambo ya kitoto ndugu yangu!?

Shariff Ritz amekuletea sets za maswali na bado anayo mengineyo mengi mno...unadai ati huwezi kumjibu kwakuwa wewe "una Ilm kubwa saana" kushinda yeye!?ahaha!!

Kama hicho ndicho kigezo/excuse ya kutojibu maswali ya Wanajamvi...kwa hiyo usipatwe na staajabu pale Sheikh Mohammed akitumia kigezo hicho hicho anapokataa kupoteza muda wake kujibu visuali vyako vya kitoto...au wewe Ilm yako ni kubwa saana kushinda Watu woote wa Madrassa!?ahaha!!

Ahsanta sana.

Cc;Ritz
 
walahi sheikh wangu hizo bayana zako zinanifurahisha sana... lakini hayo ni mambo yako sheikh wangu...
naona umempa na copy binamu yake sultan Jamshid, al habiby tuendelee na mnakasha...


Mkuu wa Chuo,

Nakupenda pita kiasi ndugu yangu,na wala sitarajii kukurubisha malumbano yoyote juu yako Muhibu wangu.

Sasa mbona kunitaja Gombesugu kwenye shughuli zenu za kununuliana madera ya XXL na huyo mwenzio Shariff Ritz Ibn Shamran!?

Tafadhali,kipenzi changu Mkuu wa Chuo,sinitese kwa kuntaja kila mara. Mie wala sikusoma asilan,kwahiyo hata kiniletea bayana zako adimu takujibuje la Aziz wangu!?

Huyo Hajjy Jamshid,wala sina udugu nae maana mimi natokea Mwisenge kabila Muzanaki. Lakini kama unamtamani kumuona basi Insha Allah atapewa salamzo aje kukuamkua kwenye aderesi yako.

Ahsanta sana,na nakutakia singizi mnono.

Cc;Ritz
 
Mzee Said, hivi huwa unaangalia kandakanda baada ya kuandika paper zako?
Nakumbuka marehem Hussein Tindwa wa Simba alifariki wakati wa mechi moja. Sikumbuki iikuwa Enugu rangers au Ibadan shooting stars!

Turejee katika hoja kama alivyoanisha Wickama bandiko 16544



Muheshimiwa Nguruvi3,

Najua unapenda sasa neno "Ibadan",kumbuka na neno "Chamwino" pia ndugu yangu!?ahaha!!

Ni kweli mimi nilikwenda kwenye hiyo match Uwanja wa Taifa na Babu yetu Shariff Abdallah Al Attas aliekua Mwenyekiti wa Baraza la Wazee wa Club ya Simba kwa miaka mingi mno!

Nafikiri Team iliyocheza siku ile ni Racca Rovers ya kutoka huko huko Nigeria na walishinda 4-2!...

tulipotoka pale Stadium ilinilazim kumshika mkono Babu Shariff kumuingiza ndani ya mutukari/gari maana yeye alikua ni "mgonjwa mno" kwa Simba Sports Club. Pia nafikiri ile ndo ilokua match yake ya mwisho kuhudhuria maskini...baada ya hapo alikua akipenda kusikiza mpira radioni tu.

Hayati Hussein Tindwa maskini nafikiri alifariki on the way to Muhimbili Hospital siku ile ile...Inna Lillahi Wa Inna Illahi Raj'uun

Tafadhali nirekebisha kama unahisi kuna pahala nimekosea japo kiduchu

Ahsanta sana.
 
Sharif ritz umesahau na haya
(1) kanda ya muago
(2) yule mvuvi wa zaid ya miaka 80 kisha akafufuka kuhudhuria kikao cha chama
lol
Bcc, Wamakonde wa kipumbwi


Hasanalis,

Salaam Al Akhiy.

Wallahi,nimeipenda mno hii bayana yako adimu.

Tatizo ni kuwa hawa jamaa zetu hawataki/wamegoma kujibu maswali yetu kabisaa!?

Huyo Mvuvi alojifanya kufufuka kama Yesu/Nabii Isa,ili tu aje kuhudhuria vikao vya Tanu hapa duniani!?ahaha!!

Khalafu wanataraji na kulazimisha mtu yeyote mwenye akili yake timamu ati aamini maneno ya huyo Yericko wao!?ahaha!! Wot a joke!

Ahsanta.

Cc;Ritz
 
Wanaukumbi;
Haya yalikuwa baadhi ya majibizano kati ya Yericko (post #1 ) na mzee wetu MS. Maswali yote ya ZENJ tuliyomwuliza yalikuwa yana-focus hapo nilipo-bold

Code:
By Mohamed Said 
Umeingiza mambo mengi sana.
 Kuna Zanzibar, elimu ya Waislam, matokeo mabaya ya shule za Kiislam, kuchinja.

 Itakuwa tabu kufanya mjadala uliokuwa hauna mwelekeo ulionyooka.

 [B]Lakini kwa mukhtasari ukitaka historia ya Zanzibar na maendeleo yake itabidi tuanza kwa kuvamiwa kwa Zanzibar na jeshi mamluki la Wamakonde kutoka Kipumbwi wakifadhiliwa na utawala wa Nyerere.[/B]
 
Kuanzia hapa tutaingia katika tatizo la Muungano na kwa nini leo Wazanzibari wanadai nchi yao ........

Kwa MAONI yangu; kwa vile Mwenyewe kasema hatajibu (Majibu kwa Prishaz) maswali haya. Na kumbe maswali haya ndiyo msingi wa kujua jee ufadhili wa Kipumbwi ulilazimishiwa wazenj(ASP) au wao ndio waliyouomba (kutoka TANU) ili Kujadili huo uvamizi aliomwahidi Yericko na dhamana ya usalama wa raia, natoa rai kuwa mada hii (ya zenj) tuachie hapa. Ikianzishwa tena kwa namna yoyote ile ili kudhalilisha kundi lolote basi tutayarudia haya maswali tuliyonyimwa majibu leo mpaka kujua nani kaomba msaada.

Mwenye kusoma na kupima hatakosa pa kushika

cc; Prishaz, Mr Iron, Painkiller, Nguruvi, Jasusi, Ritz, Kadogoo, Yericko,Mag3, Nanren,Sheik Farid,Jokakuu,Son of Alaska, Spike Lee, BigShow, Gwalihenzi

Naaam naaaam naaaaam!

Asante sana kwakukumbusha tulikotoka nakisha kuanua jamvi juu ya mapinduzi ya Zanzibar!

Tusonge mbele, tusigande kwa hili kwakuwa jibu limepatikana!
 
Tunashukuru kwa elimu tunayoipata hapa JF kutoka kwa Sheikh Mohamed Said. Mwenyezi Mungu akuzidishie hekima na subira hakika kalamu yako imegusa kwingi.
 
Nimejaribu kupitia posts nyingi kwenye huu uzi lakini sijaona huo uchochezi wa Sheikh Mohamed Said.
 
Muheshimiwa Nguruvi3,

Najua unapenda sasa neno "Ibadan",kumbuka na neno "Chamwino" pia ndugu yangu!?ahaha!!

Ni kweli mimi nilikwenda kwenye hiyo match Uwanja wa Taifa na Babu yetu Shariff Abdallah Al Attas aliekua Mwenyekiti wa Baraza la Wazee wa Club ya Simba kwa miaka mingi mno!

Nafikiri Team iliyocheza siku ile ni Racca Rovers ya kutoka huko huko Nigeria na walishinda 4-2!...

tulipotoka pale Stadium ilinilazim kumshika mkono Babu Shariff kumuingiza ndani ya mutukari/gari maana yeye alikua ni "mgonjwa mno" kwa Simba Sports Club. Pia nafikiri ile ndo ilokua match yake ya mwisho kuhudhuria maskini...baada ya hapo alikua akipenda kusikiza mpira radioni tu.

Hayati Hussein Tindwa maskini nafikiri alifariki on the way to Muhimbili Hospital siku ile ile...Inna Lillahi Wa Inna Illahi Raj'uun

Tafadhali nirekebisha kama unahisi kuna pahala nimekosea japo kiduchu

Ahsanta sana.
gombesugu, Nguruvi3,

..YES, ilikuwa ni Simba vs Racca Rover.

..Prof.James Shaba aliwahi kunukuliwa kuwa moja kati ya mambo yaliyomshangaza in his career ni uchunguzi alioufanyia mwili wa marehemu Hussein Tindwa.

..anadai Hussein Tindwa alikuwa na tatizo la moyo na yeye Prof anashangaa ni jinsi gani aliweza kumudu kucheza mpira miaka yote hiyo, tena a very demanding position as center back.

..ktk nchi zilizoendelea labda tatizo la Tindwa lingeweza kuonekana mapema na kuwa fixed.

..je, mechi hiyo ilikuwa ni baada ya Simba kuwatoa Mufulira Wonderers??

..hebu, tuhabarishe vituko vya mechi ya Simba na Mufulira.
 
Muheshimiwa Nguruvi3,

Najua unapenda sasa neno "Ibadan",kumbuka na neno "Chamwino" pia ndugu yangu!?ahaha!!

Ni kweli mimi nilikwenda kwenye hiyo match Uwanja wa Taifa na Babu yetu Shariff Abdallah Al Attas aliekua Mwenyekiti wa Baraza la Wazee wa Club ya Simba kwa miaka mingi mno!

Nafikiri Team iliyocheza siku ile ni Racca Rovers ya kutoka huko huko Nigeria na walishinda 4-2!...

tulipotoka pale Stadium ilinilazim kumshika mkono Babu Shariff kumuingiza ndani ya mutukari/gari maana yeye alikua ni "mgonjwa mno" kwa Simba Sports Club. Pia nafikiri ile ndo ilokua match yake ya mwisho kuhudhuria maskini...baada ya hapo alikua akipenda kusikiza mpira radioni tu.

Hayati Hussein Tindwa maskini nafikiri alifariki on the way to Muhimbili Hospital siku ile ile...Inna Lillahi Wa Inna Illahi Raj'uun

Tafadhali nirekebisha kama unahisi kuna pahala nimekosea japo kiduchu Ahsanta sana.
Gombesugu upo sahihi ililikuwa ni Racca Rovers, ahsante. Jokakuu ile taarifa ya shaba niliiona. Alisema anashangaa na ni moja ya vitu vinalivyomshangaza katika career yake maana hata kukimbia ilikuwa ni questionable achilia mbali kucheza tena centre back wakati huo tukiita Mkoba!

Maneno mitaani yakaanza Tindwa(R.I.P) ndiye aliyekabidhiwa ''mkoba wa babu'' na akakutana na mikoba ya Nigeria ikamzididi nguvu. Chimbuko la mikoba, sisi na Nigeria halikuanza hivi karibuni, ni historical.

Anyway, shukrani wakuu ni katika kukung'uta jamvi. Turudi ukkaa jamvini
 
Tunashukuru kwa elimu tunayoipata hapa JF kutoka kwa Sheikh Mohamed Said. Mwenyezi Mungu akuzidishie hekima na subira hakika kalamu yako imegusa kwingi.

Mshume Kiyate,

Amin Amin Amin ndugu yangu.

Ni wajibu wetu kueleza hii historia ili ijulikane.
Nashukuru JF kwa kweli wametusaidia pakubwa.
 
Gombesugu upo sahihi ililikuwa ni Racca Rovers, ahsante. Jokakuu ile taarifa ya shaba niliiona. Alisema anashangaa na ni moja ya vitu vinalivyomshangaza katika career yake maana hata kukimbia ilikuwa ni questionable achilia mbali kucheza tena centre back wakati huo tukiita Mkoba!

Maneno mitaani yakaanza Tindwa(R.I.P) ndiye aliyekabidhiwa ''mkoba wa babu'' na akakutana na mikoba ya Nigeria ikamzididi nguvu. Chimbuko la mikoba, sisi na Nigeria halikuanza hivi karibuni, ni historical.

Anyway, shukrani wakuu ni katika kukung'uta jamvi. Turudi ukkaa jamvini
Naam mkuu,

Tunakung'uta vumbi la kimbembe cha siku nne za kujadili Mapinduzi matukufu ya Zanzibar

Tumejiridhisha vyakutosha, na amekiri kiutu uzima kuwa yeye (Mohamed Said) ni MCHOCHEZI na MFITINI wakuogopwa Tanzania
 
Yericko/Wickama
Naona hili jambo limewakaa sana na kwa hakika naona wanajamvi wengi
wanataka kunisikia.

Bismillah:

''The larger picture shows that the aim of the revolution was to overthrow patriotism in Zanzibaris which was opposed to Britain and Tanganyika under Mwalimu Nyerere.

In the eyes of the British at that time was that Zanzibar was already under the influence of Egypt under Gamal Abdel Nassir which would come to endanger the interest of Britain and its puppets in East Africa.

Sheikh Ali Muhsin was aware of this and that is why when he was being taken to jail he quickly sent someone to his Goan secretary to shred the paper which he had prepared for the Cabinet after his trip from Egypt.

The uncertainty by ZNP-ZPP leadership in the issue of security of Zanzibar wavering between dependence on Egypt and then coming back to Britain who did not want to believe that Zanzibar could be invaded by Tanganyika was the reason which made Zanzibar fall and could not rise up again until now.''


Wanajamvi,
Wameyataka wenyewe kazi kwao.
 
Yericko/Wickama
Naona hili jambo limewakaa sana na kwa hakika naona wanajamvi wengi
wanataka kunisikia.

Bismillah:

''The larger picture shows that the aim of the revolution was to overthrow patriotism in Zanzibaris which was opposed to Britain and Tanganyika under Mwalimu Nyerere.

In the eyes of the British at that time was that Zanzibar was already under the influence of Egypt under Gamal Abdel Nassir which would come to endanger the interest of Britain and its puppets in East Africa.

Sheikh Ali Muhsin was aware of this and that is why when he was being taken to jail he quickly sent someone to his Goan secretary to shred the paper which he had prepared for the Cabinet after his trip from Egypt.

The uncertainty by ZNP-ZPP leadership in the issue of security of Zanzibar wavering between dependence on Egypt and then coming back to Britain who did not want to believe that Zanzibar could be invaded by Tanganyika was the reason which made Zanzibar fall and could not rise up again until now.''


Wanajamvi,
Wameyataka wenyewe kazi kwao.

Hayahaya waungwana,

Mambo yamelipuka kwa uzuri,

Mohamed Said sasa ameamua kuingia ulingoni nakujibu hoja zetu!

Ngoja nimsome kwakutulia kisha nitarejea kwa uchambuzi wamajibu yake!
 
Back
Top Bottom