Wickama,
Kama ni kweli unakwenda kutembelea SUA;nafikiri uliwahi kusema yakuwa ulisomea Pedology....tafadhali mpe salaam zangu nyingi jamaa yangu Dr. Balthazar Msanya.
Mwambie jamaa yako wa Vienna mliokua woote Jarumani early 1990's,nina hakika atacheka saaana!
Tafadhali pia niombee kwa Nguruvi3,ajibu yale maswali ya uchochezi wa amani hapo nchini na labda pia ugaidi niliyomwekea jana dhidi ya wenzenu Yericko n Mwanakijiji!?
Sisi kwa ustaarabu wetu,hatupendi kujaza server kwa kurudia maswali yayokwayayo...kwahiyo Nguruvi3 na Wanajamvi khasa wale wafuatiliao huu mnakasha kwa karibu wanajua madai/shutuma zetu!
Ahsanta sana.
Gombesugu, Mag3 kasema katika hao wanopiga simu kuhusu Lawi basi ajitokeze mmoja. Na kisha kasema mbona haya yameandikwa siku nyingi hakuna aliyeshtuka.
Najaribu kufikiri kuwa hivi mtu akiniita mimi kafir (kama ninavyoitwa na akina al-khiy) au mpagani au imani nyingine, hilo linaweza vipi kufikia mahali pa kunikosesha usingizi au kunituma nikamate simu eti kwa ghadhabu!!!
Endapo hilo linasababisha usumbufu kama inavyodaiwa, basi nakuhakikishia kuwa Wazanzibar watabeba mawe na wala si simu.
Mtu babu yake atolewe roho, mwingine aachwe mjane, wengine mayatima halafu umwambie kuwa mpendwa wao alikuwa msaliti tena unasema msaliti wa dini ili huko aliko adhabu ya mola imshukie vilivyo, huyo kweli akuache bila kukupopoa mawe!
Pili, umesema mimi na Mag3 tunajifanya tunajua kila kitu, pamoja na kauli yako ya kejeli ukweli unatabia ya kujitenga na uongo na wala mwanga na giza havikai pamoja.
Tatu, nashukuru sana kusikia wewe na Mohamed Said(tumeishi na tunaishi) na historia!
basi tudadavulieni haya kwasababu yapo within your reach!
Gombesugu; Professor Msanya ndiye msimamizi wangu wa Masters. Research work tulifanyia Mbinga District, Kitanda village, tulipanda milima na kuchimba soil profiles kiroho mbaya. A very strict scholar. Nashukuru kama mlikuwa wote Ghent. Nikipata fursa nitaku-PM namba yake ya simu umsalimie. Shukran. Kwa Nguruvi nimekusikia.
Wanajamvi,
Nadhani mwenye akili na macho ameona uhalali na uhalisia wa madai yangu yaliyobeba kichwa cha uzi huu yasemayo,
"Uchochezi wa Mohamedi Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar"
Mohame amelidhihirishia jukwaa hili kuwa yeye ni waaina gani katika Tanzania,
Nadhani kwahilo limepita, tumejiridhiya kuwa madai ya Uchochezi wa Mohamedi Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar ni halisi,
Naomba tusonge mbele kuendelea kuuweka wazi Uchochezi wa Mohamedi Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar ili dunia ione na kuelewa huyu mzandiki alivyo!
walahi sheikh wangu hizo bayana zako zinanifurahisha sana... lakini hayo ni mambo yako sheikh wangu...
naona umempa na copy binamu yake sultan Jamshid, al habiby tuendelee na mnakasha...
Mzee Said, hivi huwa unaangalia kandakanda baada ya kuandika paper zako?
Nakumbuka marehem Hussein Tindwa wa Simba alifariki wakati wa mechi moja. Sikumbuki iikuwa Enugu rangers au Ibadan shooting stars!
Turejee katika hoja kama alivyoanisha Wickama bandiko 16544
Sharif ritz umesahau na haya
(1) kanda ya muago
(2) yule mvuvi wa zaid ya miaka 80 kisha akafufuka kuhudhuria kikao cha chama
lol
Bcc, Wamakonde wa kipumbwi
Wanaukumbi;
Haya yalikuwa baadhi ya majibizano kati ya Yericko (post #1 ) na mzee wetu MS. Maswali yote ya ZENJ tuliyomwuliza yalikuwa yana-focus hapo nilipo-bold
Code:By Mohamed Said Umeingiza mambo mengi sana. Kuna Zanzibar, elimu ya Waislam, matokeo mabaya ya shule za Kiislam, kuchinja. Itakuwa tabu kufanya mjadala uliokuwa hauna mwelekeo ulionyooka. [B]Lakini kwa mukhtasari ukitaka historia ya Zanzibar na maendeleo yake itabidi tuanza kwa kuvamiwa kwa Zanzibar na jeshi mamluki la Wamakonde kutoka Kipumbwi wakifadhiliwa na utawala wa Nyerere.[/B] Kuanzia hapa tutaingia katika tatizo la Muungano na kwa nini leo Wazanzibari wanadai nchi yao ........
Kwa MAONI yangu; kwa vile Mwenyewe kasema hatajibu (Majibu kwa Prishaz) maswali haya. Na kumbe maswali haya ndiyo msingi wa kujua jee ufadhili wa Kipumbwi ulilazimishiwa wazenj(ASP) au wao ndio waliyouomba (kutoka TANU) ili Kujadili huo uvamizi aliomwahidi Yericko na dhamana ya usalama wa raia, natoa rai kuwa mada hii (ya zenj) tuachie hapa. Ikianzishwa tena kwa namna yoyote ile ili kudhalilisha kundi lolote basi tutayarudia haya maswali tuliyonyimwa majibu leo mpaka kujua nani kaomba msaada.
Mwenye kusoma na kupima hatakosa pa kushika
cc; Prishaz, Mr Iron, Painkiller, Nguruvi, Jasusi, Ritz, Kadogoo, Yericko,Mag3, Nanren,Sheik Farid,Jokakuu,Son of Alaska, Spike Lee, BigShow, Gwalihenzi
Nimejaribu kupitia posts nyingi kwenye huu uzi lakini sijaona huo uchochezi wa Sheikh Mohamed Said.
gombesugu, Nguruvi3,Muheshimiwa Nguruvi3,
Najua unapenda sasa neno "Ibadan",kumbuka na neno "Chamwino" pia ndugu yangu!?ahaha!!
Ni kweli mimi nilikwenda kwenye hiyo match Uwanja wa Taifa na Babu yetu Shariff Abdallah Al Attas aliekua Mwenyekiti wa Baraza la Wazee wa Club ya Simba kwa miaka mingi mno!
Nafikiri Team iliyocheza siku ile ni Racca Rovers ya kutoka huko huko Nigeria na walishinda 4-2!...
tulipotoka pale Stadium ilinilazim kumshika mkono Babu Shariff kumuingiza ndani ya mutukari/gari maana yeye alikua ni "mgonjwa mno" kwa Simba Sports Club. Pia nafikiri ile ndo ilokua match yake ya mwisho kuhudhuria maskini...baada ya hapo alikua akipenda kusikiza mpira radioni tu.
Hayati Hussein Tindwa maskini nafikiri alifariki on the way to Muhimbili Hospital siku ile ile...Inna Lillahi Wa Inna Illahi Raj'uun
Tafadhali nirekebisha kama unahisi kuna pahala nimekosea japo kiduchu
Ahsanta sana.
Gombesugu upo sahihi ililikuwa ni Racca Rovers, ahsante. Jokakuu ile taarifa ya shaba niliiona. Alisema anashangaa na ni moja ya vitu vinalivyomshangaza katika career yake maana hata kukimbia ilikuwa ni questionable achilia mbali kucheza tena centre back wakati huo tukiita Mkoba!Muheshimiwa Nguruvi3,
Najua unapenda sasa neno "Ibadan",kumbuka na neno "Chamwino" pia ndugu yangu!?ahaha!!
Ni kweli mimi nilikwenda kwenye hiyo match Uwanja wa Taifa na Babu yetu Shariff Abdallah Al Attas aliekua Mwenyekiti wa Baraza la Wazee wa Club ya Simba kwa miaka mingi mno!
Nafikiri Team iliyocheza siku ile ni Racca Rovers ya kutoka huko huko Nigeria na walishinda 4-2!...
tulipotoka pale Stadium ilinilazim kumshika mkono Babu Shariff kumuingiza ndani ya mutukari/gari maana yeye alikua ni "mgonjwa mno" kwa Simba Sports Club. Pia nafikiri ile ndo ilokua match yake ya mwisho kuhudhuria maskini...baada ya hapo alikua akipenda kusikiza mpira radioni tu.
Hayati Hussein Tindwa maskini nafikiri alifariki on the way to Muhimbili Hospital siku ile ile...Inna Lillahi Wa Inna Illahi Raj'uun
Tafadhali nirekebisha kama unahisi kuna pahala nimekosea japo kiduchu Ahsanta sana.
Hint ya kwanza: Nsilo Swai
Tunashukuru kwa elimu tunayoipata hapa JF kutoka kwa Sheikh Mohamed Said. Mwenyezi Mungu akuzidishie hekima na subira hakika kalamu yako imegusa kwingi.
Naam mkuu,Gombesugu upo sahihi ililikuwa ni Racca Rovers, ahsante. Jokakuu ile taarifa ya shaba niliiona. Alisema anashangaa na ni moja ya vitu vinalivyomshangaza katika career yake maana hata kukimbia ilikuwa ni questionable achilia mbali kucheza tena centre back wakati huo tukiita Mkoba!
Maneno mitaani yakaanza Tindwa(R.I.P) ndiye aliyekabidhiwa ''mkoba wa babu'' na akakutana na mikoba ya Nigeria ikamzididi nguvu. Chimbuko la mikoba, sisi na Nigeria halikuanza hivi karibuni, ni historical.
Anyway, shukrani wakuu ni katika kukung'uta jamvi. Turudi ukkaa jamvini
Yericko/Wickama
Naona hili jambo limewakaa sana na kwa hakika naona wanajamvi wengi
wanataka kunisikia.
Bismillah:
''The larger picture shows that the aim of the revolution was to overthrow patriotism in Zanzibaris which was opposed to Britain and Tanganyika under Mwalimu Nyerere.
In the eyes of the British at that time was that Zanzibar was already under the influence of Egypt under Gamal Abdel Nassir which would come to endanger the interest of Britain and its puppets in East Africa.
Sheikh Ali Muhsin was aware of this and that is why when he was being taken to jail he quickly sent someone to his Goan secretary to shred the paper which he had prepared for the Cabinet after his trip from Egypt.
The uncertainty by ZNP-ZPP leadership in the issue of security of Zanzibar wavering between dependence on Egypt and then coming back to Britain who did not want to believe that Zanzibar could be invaded by Tanganyika was the reason which made Zanzibar fall and could not rise up again until now.''
Wanajamvi,
Wameyataka wenyewe kazi kwao.
Tungeshukuru kwa heshima endapo Sweet@Ritz angesaidia kukujibia ili tupate ilm hii adimu japo kiduchu. (ukiondoa histoisia tunashukuru Kiswahili tunachofundwa humu.Prishaz,
Nimekusikia sitojibu maswali yasomaana.