Kwa kile ninachojua, historia huwekwa vitu muhimu vya kusaidia jamii fulani. Hii historia ya 'Uhuru wa Tanganyika upande wa pili' kama alivyosema mwandishi alipenda tuwatambue wazee wa kiislamu ambao walishiriki kwenye kupigania ila juhudi zao kwa bahati mbaya au kwa makusudi hazikutambuliwa. Sikufurahishwa na alivyosema 'watu hawapendi kusikia kuwa uhuru ulipiganiwa na waislam', sidhani kama hili ni kweli kwa sababu hata bila kuambiwa naamini watanganyika kwa kipindi hicho walikuwepo wakristo wengi pia. Kwenye siasa kuna mambo mengi, hata vikiandikwa vitabu vingapi vya tukio la kuonekana moja bado utabaki ukweli uliojificha kwa maslahi ya wahusika. Kama ambavyo Abul Sykes alishindwa kuweka bayana na Nyerere alivyoshindwa kusemea vizuri na mwandishi kukiri kutosema kabisa aloambiwa au alosoma katika kutafuta habari hizi. Si rahisi kwa gafla watu waliokaa pamoja kufanya mambo wasisemeshane na aliyeonewa au aliyeguswa na tatizo kulinyamazia.
Pamoja na hayo, miaka hamsini sasa imepita na zaidi ya miaka kumi mshutumiwa afariki. Leo kiongozi mwingine jamii moja na wanaoonewa akiri si yeye anayeongoza serikali na tatizo limedumu kwa miaka hata baada ya mshutumiwa kuondoka madarakani na kufariki na viongozi wengine kushika. Inawezekana kabisa si wazo binafsi lililompelekea kutenda kwa uonevu bali kuna nguvu ya nyuma kama inavyoonekana sasa na kwa viongozi wengine waliopita. Nadhani juhudi zingelekezwa huko kuliko kuishia kuwaona hawa wasaliti pengine tungepewa sisi ingekuwa hivyo.
Kupambana na adui kwa hitaji maandalizi ya kikosi vizuri, nadhani wakati waislam wanajiandaa kudai haki yao ni bora wangeanza juhudi za kujijenga ndani kwanza katika matatizo yao ya ndani, umoja na elimu nadhani ni vitu muhimu kufikia hili.
Kwa uzoefu binafsi kutoka shule mbili za serikali za jinsia moja, tuliishi vizuri katka shule ambayo jamii ilipana kwa uwezo binafsi na si dini na nilikuwa kati ya wanyonge katika shule ambayo dini na dhehebu, kabila, uwezo wa kifedha viliweka nafasi yako katika jamii bila kujali uwezo wako. Si vizuri kuzipa dini zetu nguvu kutawala mawazo ya jamii tunaharibu juhudi za maendeleo. mi ni kati ya wenye bahati ya kuwa na ukoo wenye dini mchanganyiko pande zote mbili, heshima na upendo ndio vinatulea.
Ahsante kwa fikra zako.
Ukikataa kuwa Waislam ndiyo walioongoza mapambano ya uhuru tunarudi palepale tulipoanzia
na mimi ikabidi niandike kitabu hiki ambacho leo ndiyo kimezua yote haya humu JF.
Hili la Waislam kuwa mstari wa mbele dhidi ya ukooni sikulisema mimi.
Kleist Sykes aliandika kumbukumbu zake vipi alianzisha African Association 1929.
Kumbukumbu hizi zikaja nyambuliwa na mjukuu wake Daisy Aisha Sykes zikatiwa
katika kitabu alichohariri John Iliffe ''Modern Tanzanians,'' ''Kleist Sykes ''The Townsman.''
Ndani ya kitabu hiki Kleist anasema kuwa viongozi wa African Association walikuwa Waislam
kwa kuwa Wakristo walionywa wasijiingize katika siasa.
Kwa hali hii hata TAA ilipokuja kubadilishwa kuwa TANU 1954 Waislam walikuwa ndiyo wanachama
wa mwanzo wa TANU.
Hiyo pembeni wanachama wa mwanzo wa TANU walikuwa wanachama wa Al Jamiatul Islamiyya fi
Tanganyika (Muslim Association of Tanganyika).
Hata viongozi wa mwanzo wa TANU walitoka Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika akina Idd Faiz Mafongo,
Ali Mwinyi Tambwe na wengine wengi.
Ilibidi viongozi wa TANU Jimbo la Kusini Sheikh Mohamed Yusuf Badi, Masudi Mnonji, Yusuf Chembera
na Salum Mpunga waweke mkakati maalum kuivunja fitna ya Kanisa Katoliki Jimbo la Kusini ili wawaachie
Wakristo kuingia TANU.
Kitabu changu kimeeleza hili kwa kirefu.
Najua historia hii hapendezi sana kwa baadhi ya watu na wangependa isisemwe.
Juu ya hilo huo ndiyo ukweli.
Sina haja ya kueleza zaidi katika hili.
Pili historia hii anuani yake siyo ''...upande wa pili...'' hayo ni maneno kajiaandikia
Nyerere wa humu JF usiyatie maanani.
Hakika kulikuwa na Wakristo katika TANU lakini hawakuwa katikati ya jukwaa.
Fanya utafiti wako hili utalitambua.
Sitokujibu yote uliyoandika.
Lakini ikiwa unapenda kujua historia ya uhuru wa Tanganyika soma kitabu cha maisha ya
Abdu Sykes.