Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar

Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar

Wanasema ukiwa muongo, unatakiwa uwe na kumbukumbuku kali sana.

Hapana siwezi kusema uongo.
Labda unaninukuu ''out of context.''

Sina sababu ya kusema uongo.

Hebu Insha Allah niwekee hapa hayo maneno yangu.
 
Nimesoma maandiko ya ndugu yangu Mohamed Said aliyoyaweka katika kitabu chake akiitacho Historia ya Uhuru upande wa Pili,
Katika maandishi yake ameonyesha wazi kulazimisha dunia iamini kuwa waislamu wamedhulumiwa katika historia ya Uhuru wa nchi hii,
Katika matakwa yake Mohamed Said anataka historia ya Uhuru ingetazama itikadi za kidini kwanza kabla ya kusimamia maudhui halisi ambayo ni Uhuru,

Nikubaliane nae kuwa historia ya nchi yetu inamapungufu na inahitaji masahihisho, lakini kwa hili la Mohamed si masahihisho bali ni upotoshaji mkubwa, Uchochezi na ni Uhaini kwa nchi. Kwa bahati mbaya bwana Mohamed Said histori anayoisimamia ameiakisi kuanzia miaka ya 1950+ tu,

Hajajishughulisha kuutazama utawala wa Kiingereza wala kuutazama upya utawala wa Kijerumani ambao ndio uliosimika misingi ya utawala na mifumo mingi ambayo leo tunaitumia! Mjerumani mfumo wake wa utawala kwa ASILI ni wa kikristu na kwa Tanganyika walisimama hivyo bila kutetereka! (Yaani mfumo kristu 100%)

Akaja Muingereza na yeye mfumo wa utawala wake wa ASILI ni wakikristu!

Nitaelezea kwa ufupi jinsi kanisa la Tanganyika lilivyoshiriki harakati za ukombozi wa Tanganyika na madhila liliyokumbana nayo.

Ifahamike kuwa vyama vya harakati za ukombozi Tanganyika vilikuwa vingi sana, na vipo vilivyokuwa vikipingana vyenyewe kwa vyenyewe.

Mwaka 1927 – 1929 kanisa Katoliki nchini chini Joseph Gabriel Zelger, lilibainika kuingiza siasa katika utendaji kazi zake, kitendo hiki kiliwakwaza wakuu wa mamlaka ya kikoloni na kupelekea majasusi wakikoloni wapendekeze aachishwe uongozi wa kanisa nchini. Ni kweli tarehe 12 februari 1929 Zelger alistaafu wadhifawake kwa lazima.

Kisa hiki kinasema, Kanisa lilianzisha mafundisho yenye kuchochea fikra za kimaasi, nalilifanikiwa kuandaa wakufunzi maalumu kwenda katika majimbo yote ya kihuduma Tanganyika, hilo lilipelekea kuleta mtafaruku na dola ya mkoloni wa kiingereza ambapo ilimgharimu kiongozi huyu wa kiroho kuachia madaraka yake.

Alipoingia askofu Edger Aristide Maranta mwaka 1930, ikiwa kama vile mwendelezo wa mtangulizi wake, Askofu Maranda alianzisha harakati za kuwashawishi viongozi wengine wa majimbo kuendeleza kutoa mafundisho yenye kumfanya mtanganyika ajitambue na adai uhuru wake,

Mfano: 23 mei 1938 wakati makanisa saba ya Kilutheri yakiwa kwenye hatua za mwanzo za mchakato wa kuungana, Askofu maranda aliomba kuhudhuria kikao cha tarehe 8 mwezi wa sita kilichofanyika Mjini Arusha, Askofu Maranda aliudokeza mpango ule wa siri wa katoliki katika kikao hicho, japokuwa kulikuwa na hofu ya kutoaminiana, lakini uthabiti wa malengo hayo ulijipembua baadae na kuwa wamafaa.

Juhudi za kanisa kupigania ukombozi ziliendelea kushika kasi huku zikiendeshwa kwa siri sana kwamfumo wa neno la kiroho, na ilipofikia miaka ya 1950+ kanisa sasa lilikuwa tayari linanguvu ya ushawishi kufuatia mafanikio ya harakati za kanisa katika nyanja za ukombozi barani afrika.

Mtihani mkubwa kwa kanisa ilikuwa ni namna gani linaweza kuingia rasmi kudai uhuru wa Tanganyika. Katika kipindi hiki tangu harakati za kanisa zianze, Askofu Maranta pamoja na mapadre wa baadhi ya mikoa, walikuwa tayari ameshafanya juhudi kadhaa za kukutana na Mashehe waliokuwa na ushawishi mkubwa, mfano 05/02/1948, Askofu Maranda alikutana Shehe Issa bin Amir kiongozi wa kiroho katika msikiti wa Ilala - mchikichini. Mazungumzo yao yalihusu harakati za ukombozi, Shehe Issa alimshauri Askofu kuwa ikiwa makanisa na misikiti yanapigwa marufuku na mkoloni kujihusisha na siasa za ukombozi basi watafute baadhi ya vyama vya harakati za ukombozi na waviunge mkono, wazo hilo lilimvutia Askofu lakini akajenga hofu kama je ndani ya vyama hivyo watapata vijana wasomi?.

Siku chache baada ya makutano yake na Shehe Issa, Askofu Maranta aliletewa mapendekezo kutoka kwa Attilio Beltramino kassi wa katoliki aliyehudumu kule Iringa, mapendekezo ya kasisi huyu yalikuwa ni, Umishonari makao makuu uruhusu udurufu wa biblia zisomeke kwa makabila ya wahusika wa eneo, ndani ya biblia hizo yaongezwe mafundisho ya haki ya kujitambua na kujitawala wenyewe. Pendekezo hili lilimvutia sana Maranta hivyo akalipa baraka zake, kwa hakika lilifanikiwa na ndio lilizaa hisia kali za mwamko wa kudai uhuru, mfano biblia ya lugha ya kihehe ilikuwa inaeleza wazi athari za kutawaliwa.

Harakati za Ukombozi za Mwalimu Nyerere zililivutia kanisa na likaamua kumuunga mkono, mfano mwaka 1953 wakati TAA kikiwa chama chenye nguvu, Askofu Maranta alimwalika ofisini kwake Mwalimu Nyerere, walizungumza mengi lakini kubwa nikuwa alimsifu kwa juhudi za kujipambanua bila kuwaogopa wakoloni na akamweleza jinsi kanisa linavyounga mkono juhudi za ukombozi wa Tanganyika, kisha akamshauri kuwa ajaribu kuvishawishi baadhi ya vyama vya harakati za ukombozi viungane ili kuvipa nguvu ya kudai uhuru na kanisa litasaidia.

Wazo la Askofu Maranta lilimkaa Mzee Nyerere na mwaka 1954, alianza juhudi za kuwaunganisha vijana wenzake wa kariakoo ambao walikuwa ndani ya TAA na wenye nguvu ya ushawishi lakini wakikabiliwa na matatizo makubwa mawili katika lengo lao.



Elimu,

Woga



Ikumbukwe kuwa mwaka 1953 baada ya harakati za ukombozi kupamba moto na kamata kamata ya wanaukombozi, Askofu Edger Aristide Maranta alihamishiwa Zanzibar na nafasi yake ikachukuliwa na Vicar Apostolic, lakini bado aliendelea kuwa mshauri imara wa Mwalimu Nyerere. Jambo la kushangaza kama si kufurahisha, mwaka huohuo mwezi wa 8, Edger Aristide Maranta alirudishwa tena Dar es Saalam, na sasa mbinyo dhidi ya ukoloni ikahika mkondo wake.

Mnamo tarehe 7/71954, Vijana (wazee wa kariakoo) wakiongozwa na Julius Kambarage Nyerere, walikubaliana wazo la kuhuisha chama kutoka TAA kwenda TANU, chini ya uratibu wa karibu wa kanisa Katoliki (Askofu Maranda) na Waislamu (Shehe Issa bin Amir)


Mpaka hapo ndugu yangu Mohamed Said angalau umepata picha kwa KIFUPI tu ya harakati za uhuru chini ya kanisa.

Nikipata wasaa nitakuletea picha za Mwalimu Nyerere na Edger Aristide Maranta

Kwanini Kasisi huyu wa kikatoliki Edger Aristide Maranta hatajwi popote katika historia ya nchi? Kwanini kanisa katoliki halilalamiki kutokuwepo kwenye kitabu cha kivuko?

Yote hayo nitakushushia taratibu kadiri mnakasha huu unavyoenda.

Sasa nini kilifuata baada ya uhuru?

Nitaeleza kwakifupi tu:

Mwalimu Nyerere baada ya kukadhiwa mamlaka kamili ya kushika dola na Malkia wa Uingereza alianza mageuzi ya kubadili mfumo huo hasa mwanzoni mwa 1964 baada ya kuunganisha nchi ya Tanganyika na Zanzibar na kuzaliwa kwa Tanzania!

Juhudi hizi zilikwenda taratibu na kwa ufanisi wa hali ya juu kwakupitia hatua kadhaa ambazo ni pamoja na, kutaifisha huduma za jamii zote zilizokuwa chini ya makanisa, kuanzisha sera ya elimu ya msingi kuwa ya LAAZIMA kwa watanzania wote nk, Kumbuka Mjerumani amekaa zaidi ya karne tatu akitumia mfumo kristu kutawala, Muingereza nae akalowea karne kadhaa akitawala kwa mfumo huohuo, Lakini ndani ya miongo miwili tu ya utawala wa Mwalimu Nyerere huku nchi ikitoka kwenye dimbwi la ukoloni aliweza kubadili sura na mfumo huo wa kikoloni na kuwa wawatanzania wote bila kujali dini, kabila rangi au kanda.


Kazi aliyofanya mzee Nyerere ni kubwa na alikumbana na vikwazo vingi sana kutoka kwa wakatoliki, rejea kitabu cha Van Bergen kuna barua nzito ya Mwalimu Nyerere kwenye Appendix 15 kwenda kwa makasisi wa kikatoliki akiwatolea karipio kuu kwakukwamisha juhudi zake, katika hii hakuchukua karne kadhaa kuumaliza mfumo uliodumu kwa mvua na mvua.

Japokuwa hakumaliza chembe za mfumo huu lakini kwangu naona ni zaidi ya 98% alimaliza, palipobaki ni mimi, wewe na wale ndio wenye dhamana ya kumalizia.

Uthabiti na tunu aliyoifanya Mzee Nyerere inathibitishwa kwa Hotuba yake ya tarehe 5 Novemba, 1985 kabla hajastaafu urais, Mzee Nyerere aliwahutubia wazee wa Dar es Salaam. Hotuba hii ilikuwa thabiti na yenye kuvuta nyoyo za waungwa, Baba wa Taifa Mzee Nyerere akikumbuka jinsi Waislam walivyompokea Dar es Salaam kwa mapenzi makubwa ingawa yeye alikuwa Mkristo. Wazee hawa wakiwemo Bin Amir ambae Mohamed Said anamlilia, wengi wao walikuwa wanachama wa zamani wa TANU waliomuunga mkono Nyerere wakati wa kudai uhuru. Mzee Nyerere aliusifia mchango wa Waislam katika kipindi kile kigumu cha kudai uhuru. Nyerere alisemakuwa "upogo katika elimu uliorithiwa na serikali yake kutoka kwa Waingereza baina ya Waislam na Wakristo yeye ameuondosha katika kipindi cha utawala wake":

Inakera kuona wewe Mohamed unarudisha nyuma juhudi za wanaukombozi wetu na kupandikiza chuki miongoni mwa dini hizi mbili!
Faida unayopata ni ndogo na niyakwako tu kuliko hatari inayolikumba taifa hivi leo!
Sipingi kusahihisha historia ya nchi hasa kama kuna mema yaliyoachwa lakini kupotosha na kuchochea kunatulazimisha tuhoji mamlamla za usalama wa nchi zimelala wapi? Hivi tukisema kila mtu aingie katika historia ya uhuru wa nchi hii mbona itakuwa vurugu sana?

Leo tarehe 12/1/2013 tunaadhimisha mapinduzi matukufu ya Zanzibar, Mohamed Said anataka kutuaminisha kuwa Wanamapinduzi hawa wa Zanzibar waliwadhulumu waislamu wa Zanzibar na kuweka mfumo kristu anaodai upo au mfumo huo upo kwa Tanganyika tu?!
Juzi nimemuuliza maswali katika mjadala flani hapa, lakini majibu yake yamenifanya nijiridhishe kuwa Mohamed Said ni muhaini na mchochezi mkubwa wa nchi hii, Ameudhihaki Uislamu nchini na duniani kote,


Nilimuuliza hivi:

Naomba unijibu maswali haya kwaufasaha mwanazuoni Mohamed Said:

1) Uliathirika vipi kwa baadhi ya wazee waliopigania uhuru wa nchi hii kutokuwemo kwao katika histori ya nchi hii kama unavyodai?

2) Taifa na waislamu waliathirika vipi kwa baadhi ya wazee unaodai wewe walipigania uhuru wa nchi hii na hawamo katika historia?

3) Ulijuaje kuwa wazee hao walipigania uhuru ilihali hawapo katika historia stahiki ya nchi hii?

4) Unaposema historia ya uhuru wa nchi hii haiwakumbuki ama haiwatambui, ulitaka wakumbukwe katika maandishi ya vitabu au katika nyaraka za serikali za historia ya uhuru wetu?

5) Unatambua kuwa historia ya nchi yoyote ile duniani huwa wapi?

6) Upeo wako umegota kwenye historia ya waislamu wa Tanganyika na Nyerere tu, au historia ya waslamu duniani kote? Kama ndivyo, je matatizo ya waislamu wa Nigeria, Somalia, Sudani, nk Nyerere ndiye kayapeleka?

7) Je ulichokiandika ni historia ya Uhuru wa Tanganyika au ni historia ya baadhi ya Waislamu wa Tanganyika na mapito yao kisiasa?

8) Kwanini unaulazimisha umma kwa maandishi yako uamini kuwa ulichoandika ndio historia sahihi ya Uhuru wa Tanganyika?

9) Je ni kweli Mohamed Said huwajui na huwatambui wale wazee 17 waliosimama kidete kudai uhuru wa nchi yetu? Je wote walikuwa wakrstu?

Naomba majibu ili tujenge hoja mpya yamjadala huu kwa mafaa ya taifa letu!




Lakini maswali mengine yamsingi yaliulizwa na wadau wengi kama Nguruvi3, Mwanakijiji na moja lililonivutia lilikuwa hili hapa chini:


By adolay:


Ninakuuliza somalia na nyerere kwasababu waislam wa somalia wanamatatizo makubwa ya kijamii, kisiasa, kieliemu, afya nk

Nani mchawi maana hapa kwetu kwa mujibu wa hadithi zako ni Nyerere. (Tunaongelea matatizo ya waislamu na wanaowahujumu)

Watanzania (Waislam, wakristu pia wa imani zingine na wasio amini) wanamatatizo aghalabu si makubwa kama ya wasomali.

1. Kwanini useme waislam wa Tanzania ni hujuma za nyerere na kwanini wasiwe waislam wa somalia? kunatofauti ya uislam wa somalia na ule wa tanzania?

2. Je katika historia yako ufahamu wako umegota Tanzania kwa hayati JK Nyerere peke yake? kama ndivyo nini ubora na ufahamu wako kujisifu mwanahistoria makini kama sio mbabaishaji?

Tafadhali rejea maswali kutushawishi kwamba wewe ni mkweli na kashifa zako dhidi ya Nyerere ni uwongo na majungu.

Tuanze na Somalia, nataka usome swali uelewe ujibu kama nilivyouliza sio kuniwekea hadithi za maandishi zisizoakisi maudhui ya swali.

1. Nani amewahujumu/aliwahujumu wasomali na uislamu wa somalia mpaka wamefikia hapa walipo je? ni nyerere

2. Ni mfumogani unatumika katika kuitawala somalia kiasi kwamba wamefika hapo walipo ilituutupie lawama

a) Mfumo kristo ndiyo maana wamefika hapo walipo

b) Mfumo islam, mahakama ya kadhi nk

c) hufahamu nakama hufahamu nini mtazamo wako.

Ninakuuliza maswali haya lengo nikutaka kuujuwa ukweli wa pengine Nyerere huyu pia yupo somalia, afghanistan, pakistani, lebanon, syria, libya nk nakwamba machafuko yote yanayoendelea huko ni hujuma za Nyerere na mfumo kristo kama unavyowapotosha watanzania na kuwachochea!

Naomba majibu ya maswali yangu hapo juu kuthibitisha kwamba wewe sio mchochezi na mchonganishi wa waislamu na wakristo kwa kubuni vitu visivokuwepo.

Mohamed Said, baada ya utangulizi huo narejerea maswali yangu ya jana kwa ufafanuzi. Angalizo jibu maswali kama yalivyoulizwa na sio siasa au funika kombe mwanaharamu apite kwa nukuu za maandishi zisizobeba maana wala majibu ya hayo maswali




MAJIBU YA MOHAMED SAID:

quote_icon.png
By Mohamed Said

Umeingiza mambo mengi sana.
Kuna Zanzibar, elimu ya Waislam, matokeo mabaya ya shule za Kiislam, kuchinja.

Itakuwa tabu kufanya mjadala uliokuwa hauna mwelekeo ulionyooka.

Lakini kwa mukhtasari ukitaka historia ya Zanzibar na maendeleo yake itabidi tuanza kwa kuvamiwa
kwa Zanzibar na jeshi mamluki la Wamakonde kutoka Kipumbwi wakifadhiliwa na utawala wa Nyerere.

Kuanzia hapa tutaingia katika tatizo la Muungano na kwa nini leo Wazanzibari wanadai nchi yao.

Kuhusu elimu ya Waislam itatubidi tuje katika njama za Nyerere kuhujumu chuo kikuu cha Kiislam
kilichokuwa kijengwe Dar es Salaam mwaka 1968 na jinsi alivyotumia uongo na ghilba kuvunja EAMWS
na kuunda taasisi kibaraka BAKWATA.

Vipi shule za Waislam hazifanyi vyema inabidi tuje katika hujma ya NECTA kwa wanafunzi wa Kiislam na
tuupitie waraka wa marehemu Prof. Malima kuhusu yale aliyoyakuta Wizara ya Elimu mwaka 1987.

Wizara ya Elimu na NECTA vimegeuzwa vigango vya kanisa.

Kubwa zaidi ni kuwa Waislam kwa muda mrefu hatukuruhusiwa kujioganaizi nje ya BAKWATA kibaraka
wa serikali.

Makanisa mnaendelea kwa kupendelewa na serikali iliyojaza watendaji Wakristo sisi tungepewa hayo
mabilioni ya MoU kati ya Makanisa na Serikali tusingekuwa kama hivi.

Yapo mengi sasa chagua tuanze na lipi katika hayo hapu juu niliyokugusia.

Wajerumani waliwaweka Wayahudi katika ghetto kisha wakawa wanawalaumu kwa uchafu.
Kwenye ghetto hakuna maji wala misala sasa watu wafanyeje?

Mnatusimanga kwa hospitali mnazoendesha kwa hela ya kodi ya serikali kodi inayolipwa na raia
wote.

Tunabanwa na mfumokristo kisha mnatulaumu hatuna maendeleo







Mohamed said

katika pita pita zangu nimekutana na post yako hii ya tare 4 January 2013 #914

Umeongelea kunyanyaswa kwa waislamu katika elimu ni njama ya JK Nyerere - Elimu ya somalia ipo taabani sana na Nyerere hayupo huko

Nakwamba Nyerere alitumia uongo na ghilba kuvunja EAMWS - lakini ghilba wala uongo wa nyerere haupo Somali na inateketea vibaya

Necta imegeuka vigango vya kanisa - Somalia haina vigango vya makanisa katika taasisi zake hususani elimu lakini ipo taabani

Serikali imejaza wakristo kwa upendeleo na kuwaacha waislam - Somalia serikali takribani yote ni waislam hakuna maendeleo

Wakristo
wanawasimanga kwa hospitali zilizo jengwa kwa kodi ya watanzania- wasomali pia wanatoa na kukusanya kodi hakuna afya bora, elem wala siasa safi!

Waislamu wanabanwa na
mfumo kristo
- Somalia kuna mfumogani unaowabana wasiendelee




Ndugu yangu Nyerere.

Historia ya Kanisa na harakati za uhuru imekwisha au itaendelea?
Ningependa nami Insha Allah kuchangia katika yale ulotuwekea hapa.
 
Ndugu yangu Nyerere.

Historia ya Kanisa na harakati za uhuru imekwisha au itaendelea?
Ningependa nami Insha Allah kuchangia katika yale ulotuwekea hapa.

Haijaisha mkuu, mimi nimeinyofoa kwa ufupi tu, unaweza kuihuisha tu.

Nakusudia kuwaombeni nyote tunaojadiliana hapa na wengine ili kwapamoja tushirikiane kuandika upya HISTORIA ya nchi yetu na uhuru wake!

Mengi mazuri kutoka kwenye kitabu chako na kile cha Kivukoni tutayanukuu!

Hii iwe kwa maslahi ya taifa letu bila kujali dini, rangi, kabila au vyovyote vile!

Tufanye utafiti pamoja na mwisho wasiku tuje na historia thabiti ya nchi yetu tena yenye kutuunganisha!
 
Haijaisha mkuu, mimi nimeinyofoa kwa ufupi tu, unaweza kuihuisha tu.

Nakusudia kuwaombeni nyote tunaojadiliana hapa na wengine ili kwapamoja tushirikiane kuandika upya HISTORIA ya nchi yetu na uhuru wake!

Mengi mazuri kutoka kwenye kitabu chako na kile cha Kivukoni tutayanukuu!

Hii iwe kwa maslahi ya taifa letu bila kujali dini, rangi, kabila au vyovyote vile!

Tufanye utafiti pamoja na mwisho wasiku tuje na historia thabiti ya nchi yetu tena yenye kutuunganisha!

Kaka Yeriko

Tatizo linakuja sehemu moja tu.

Mtu akishaita utafiti wa mzee Mohamed Said kuwa ni ngano, basi inamaaana kuwa yale yote yalioandikwa ni batili. Sasa kama ni batili, wanashindwa kuwa-acknowledge wazee wa Dar es Salaam, waliompokea babu yako mzee Nyerere, katika harakati za kupigania uhuru wa Tanganyika

Inaonyesha dhahir kuwa wazee wa Dar es Salaam hawatambuki katika "historia" waijuayo wao. Hili ndio linalokwamisha mjadala adhwim kwenda mbele.

Ninawasilisha
 
Kaka Yeriko

Tatizo linakuja sehemu moja tu.

Mtu akishaita utafiti wa mzee Mohamed Said kuwa ni ngano, basi inamaaana kuwa yale yote yalioandikwa ni batili. Sasa kama ni batili, wanashindwa kuwa-acknowledge wazee wa Dar es Salaam, waliompokea babu yako mzee Nyerere, katika harakati za kupigania uhuru wa Tanganyika

Inaonyesha dhahir kuwa wazee wa Dar es Salaam hawatambuki katika "historia" waijuayo wao. Hili ndio linalokwamisha mjadala adhwim kwenda mbele.

Ninawasilisha

Katika safari yangu ya maisha dunia huwa naamini kuwa, hakuna upuuzi ulio upuuzi mtupu!
 
Haijaisha mkuu, mimi nimeinyofoa kwa ufupi tu, unaweza kuihuisha tu.

Nakusudia kuwaombeni nyote tunaojadiliana hapa na wengine ili kwapamoja tushirikiane kuandika upya HISTORIA ya nchi yetu na uhuru wake!

Mengi mazuri kutoka kwenye kitabu chako na kile cha Kivukoni tutayanukuu!

Hii iwe kwa maslahi ya taifa letu bila kujali dini, rangi, kabila au vyovyote vile!

Tufanye utafiti pamoja na mwisho wasiku tuje na historia thabiti ya nchi yetu tena yenye kutuunganisha!

Unajua Brendon Grimshaw mhariri wa Tanganyika Standard alisema nini katika taazia aliyomwandikia Abdu Sykes?

Grimshaw akijuana na Abdu Sykes kwa miaka mingi.
Huyu alikuwa Mwingereza.
 
Hii ni dhihaka...Kama huna ushahidi sema tu huna ushahidi na usizidi kujishushia hadhi. Kuwa mkweli. Kama Cardinal Polycarp Pengo angetoa tamko kama hilo, leo hii ndiyo lingekuwa rejea ya kila kitu kinachohusiana na Mfumo Kristo kama vile vitabu vya Sivalon na Van Bergen...!

[1] Majira, 24 July, 1995. Amidst this conflict between Muslims and the government, it was published by the press that Muslims were to embark on a systematic campaign to elect a Muslim president in the elections of 1995. This in its entirety was a mere psychological warfare unleashed by the Christian Lobby upon Muslim ministers in the cabinet who anyway were far from Muslim politics. The bombardment from the press and within the Parliament was so overwhelming to those Muslims ministers mentioned by Muslims as possible presidential candidates that they had to stand up in the Parliament as Muslims to deny their capability to lead the country and disassociated themselves from the Muslim movement. Prof. Malima refused to be humiliated; he was of the opinion that the move by Muslim ministers was un-called for and unnecessary. To him Muslim ministers were just as qualified as any Christian to aspire for the presidency. His signature was not among those which Muslim ministers issued to the press as binding document of their commitment not to aspire for the highest office in the land. Jakaya Mrisho Kikwete later to become president of the country was among the signatories.



Sifanyi utani.
Hakika maneno hayo nimeyatoa kwenye gazeti la Majira.
 
Haijaisha mkuu, mimi nimeinyofoa kwa ufupi tu, unaweza kuihuisha tu.

Nakusudia kuwaombeni nyote tunaojadiliana hapa na wengine ili kwapamoja tushirikiane kuandika upya HISTORIA ya nchi yetu na uhuru wake!

Mengi mazuri kutoka kwenye kitabu chako na kile cha Kivukoni tutayanukuu!

Hii iwe kwa maslahi ya taifa letu bila kujali dini, rangi, kabila au vyovyote vile!

Tufanye utafiti pamoja na mwisho wasiku tuje na historia thabiti ya nchi yetu tena yenye kutuunganisha!
HISTORIA huwa haiandikwi upya wala kuhuishwa. Historia ya nchi hii tayari ipo. Mtaandika nini kipya? Au mnaweza kuyabadili haya:
Rais wa KWANZA wa TANU- Mwalimu;
Mtu aliyetumwa kwenda UN kudai uhuru wetu- Mwalimu;
Waziri Mkuu wa Kwanza Tanganyika- Mwalimu;
Rais wa Kwanza Tanganyika- Mwalimu;
Rais wa Kwanza Tanzania- Mwalimu;
Na mengine meeengi!
 
Wakati mwingine sisi ndiyo huwa tunakuonea huruma ndugu yangu.
Hapo juu umesema Nyerere si kama hakujibu.
Haya turudi nyuma kidogo kabla sijapigwa ban. Angalia post yangu ya #823 kwenye uzi wa "Maaskofu wakemea udini na ukanda".
Niliquote hii kitu kutoka paper yako.


Linganisha hapo kwenye buluu halafu naomba unifafanulie labda mimi lugha inanichenga

Hakika lugha imekuchezea.
Nyerere hakufanya.

Umeona kitabu cha maisha yake kimechapwa
toka afariki?

Hiyo ndiyo maana yangu.
Lakini hili si kubwa.

Tuendelee na mengine.
 
HISTORIA huwa haiandikwi upya wala kuhuishwa. Historia ya nchi hii tayari ipo. Mtaandika nini kipya? Au mnaweza kuyabadili haya:
Rais wa KWANZA wa TANU- Mwalimu;
Mtu aliyetumwa kwenda UN kudai uhuru wetu- Mwalimu;
Waziri Mkuu wa Kwanza Tanganyika- Mwalimu;
Rais wa Kwanza Tanganyika- Mwalimu;
Rais wa Kwanza Tanzania- Mwalimu;
Na mengine meeengi!

Umesema kweli kwa hayo yote.
Hakuna awezae kukupinga katika hayo.
 
HISTORIA huwa haiandikwi upya wala kuhuishwa. Historia ya nchi hii tayari ipo. Mtaandika nini kipya? Au mnaweza kuyabadili haya:
Rais wa KWANZA wa TANU- Mwalimu;
Mtu aliyetumwa kwenda UN kudai uhuru wetu- Mwalimu;
Waziri Mkuu wa Kwanza Tanganyika- Mwalimu;
Rais wa Kwanza Tanganyika- Mwalimu;
Rais wa Kwanza Tanzania- Mwalimu;
Na mengine meeengi!

Hakuna KIPYA kitachozalishwa katika mpango huo, bali makusanyo yaleyale ya kweli ndio yaunde historia ili kuondoa dhana ya kila mtu/watu kuamini lake katika Historia ya Nchi hii.

Kwaujumla historia huwa inajiandika, tunachofanya sisi nikukusanya tu kumbukumbu hizo nakuhifadhi katika maandishi.
 

Mkuu naomba japo aya moja tuu moja tuu ukinipa ambayo inamakosa ya hesabu kwa Quraan tukufu basi nakupa
laki tano kwa kila aya ambayo utaitowa kwa kila aya ambayo inamakosa ya kihesabu lakini katika bible ninazo nyingi tuu ambazo zina contradict wenyewe kihesabu nitafute nitakupa ref.

Tafadhali iwe nje ya uzi huu. Huu mjadala usipindishwe kwa makosa ya Quran. Sasa hivi ninakwenda Kanisani kufundisha watoto, nikirudi ama kesho asubuhi, nitaku-PM na kukuwekea mada yako special unipe ufafanuzi wa ubishi unaotaka kuanzisha bila sababu za msingi.

By the way nashukuru kuwa tayari umekiri kuwa kuna makosa mengine, ila unakataa ya kimahesabu.
 
By the way nashukuru kuwa tayari umekiri kuwa kuna makosa mengine, ila unakataa ya kimahesabu.
Haya lete hili kosa lolote lile unaloliona lipo kwenye Quran.

Si mimi bali ni Quran yenyewe ndiyo inayowapa changamoto hii zaidi ya miaka 1400 iliyopita ili uingilie na kutafuta kosa kama utaliona
Quran 4:82. Hebu hawaizingatii hii Qur'ani? Na lau kuwa imetoka kwa asiye kuwa Mwenyezi Mungu bila ya shaka wangeli kuta ndani yake khitilafu nyingi"

Mmeshindwa na Mohamed Said wenye Historia ya Tanganyia sasa mnataka kuingilia Quran! haya karibuni.
 
Haijaisha mkuu, mimi nimeinyofoa kwa ufupi tu, unaweza kuihuisha tu.

Nakusudia kuwaombeni nyote tunaojadiliana hapa na wengine ili kwapamoja tushirikiane kuandika upya HISTORIA ya nchi yetu na uhuru wake!

Mengi mazuri kutoka kwenye kitabu chako na kile cha Kivukoni tutayanukuu!

Hii iwe kwa maslahi ya taifa letu bila kujali dini, rangi, kabila au vyovyote vile!

Tufanye utafiti pamoja na mwisho wasiku tuje na historia thabiti ya nchi yetu tena yenye kutuunganisha!

Abdulwahid alipofariki Wizara ya Habari ilitoa taarifa ikieleza kuwa Rais Nyerere
amehudhuria maziko ya Abdulwahid Sykes.

Kingine kinachostaajabisha ni kuwa taarifa ile ilitoa maelezo machache ya uajiriwa
wake katika serikali na kuacha maelezo muhimu ya Abdulwahid katika siasa.

Ilikuwa Mwingereza, Brendon Grimshaw, mhariri wa Tanganyika Standard, ndiye
aliyempa Abdulwahid heshima na hadhi anayostahili baada ya kifo chake kwa
kuchapisha taaízia ambayo ilimweleza Abdulwahid kama: ''mmoja wa wapangaji
wa vuguvugu la kudai uhuru na mmoja wa watu waliomsaidi Nyerere kuingia katika
siasa.''

Taazia ile ilitoa sifa kemkem kwa ukoo wa Sykes katika kuleta maendeleo ya siasa
Tanganyika kwa kusema kuwa, ''msukumo mkubwa wa Waafrika wa Tanganyika kupata
chama cha siasa chenye nguvu ulitokana na juhudi za ukoo wa Sykes.''

Inasemekana taaízia hii iliyompa marehemu Abdulwahid heshima na sifa za uzalendo wa
hali ya juu iliwaudhi baadhi ya viongozi katika TANU.

Viongozi hao wakawa wakisikika wakisema kuwa Ally na Abbas Sykes walikuwa wanajaribu
kumtukuza kaka yao.

(''Tanganyika Standard'' 20th October 1968).

Hali hii ilijitokeza tena wakati CCM ilipokuwa ikitafiti historia yake.

Hassan Upeka,[1]mmoja katika wasaidizi wa utafiti ule alipeleka katika jopo lile la utafiti na
uandishi wa historia ya TANU, mahojiano aliyofanya na Abdulwahid miaka mingi iliyopita
kuhusu historia ya TANU.

Hassan Upeka alifahamishwa kuwa historia inayoandikwa haimhusu Abdulwahid Sykes.
 
Hilo ni kweli Kitabu chake kimemfunga mwenyewe.
Ni kama kumwambia mtu akate tawi alilokalia. Hawezi, inahitaji ujasiri wa aina yake.

Kumbuka amewavuta baadhi ya Waislam kumfuata kwenye huu ubaguzi kutokana na haya anayoandika.
Leo watamwelewa vipi akigeuka?

Ndio maana haishi kukwepa hoja hasa akijua anajadiliana na watu wanaomjua.

hakika
 
Unaweza kutuwekea maelezo hayo kwenye hicho kibao?
Hakika hiyo ni historia muhimu sana.

Ahsante sana.
Nyerere aliitumia gari hiyo 1955-1960,dereva alikuwa Said Tanu,baadaye akaikabidhi kwa Tanu Youth League.Gari inaitwa Austin Morris
 
Back
Top Bottom