Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar

Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar

MM,

[TABLE="class: MsoNormalTable"]
[TR]
[TD] Father Smith of the Roman Catholic Church and the Party seem to be of the same mind on this dissension. [1] Both Kiwanuka and Fr Smith are expressing their own personal opinion, not facts. No one denies the fact that some Christians were there. Indeed Christian names appear in the dramatis personae of the play. But no one can deny the truth that they did not occupy centre stage. This work has given a descriptive analysis of the role of urban Muslims in the struggle for independence; their contribution in the founding of TANU; in membership drives and composition which took strong Muslim characteristics.

Dar es Salaam Province TANU Elders Council under its chairman Sheikh Suleiman Takadir had 173 members who were all Muslims.
[2]


[/TD]
[/TR]
[/TABLE]


[1 For the understanding of political parties and the role of culture, groupings, ideology, etc., see
Maurice Duverger, Political Parties, Their Organisation and Activity in the Modern State, (New York,
1963).

[2] See Elder Council Section File 376, Party Archives, Dodoma.

Duh! yaani wazee wote walikuwa Waislamu! sasa wenzao walikuwa wapi jamani? au walikuwa hawataki uhuru?
 
Shekh Mohamed Said, tumalizie basi ile kasheshe ya Sheikh Abubakar Mwilima na Halmashauri kuu ya CCM iliishaje? Mwilima alifukuzwa au alilazimishwa kujiuzulu? au alikamatwa? uliishia pale wajumbe waliporudi baada ya kunwa chai kikao kiliendelea bila ya kugusia hoja ya Mwilima! halafu............

Shekh nawewe bwana wacha kutuanzishia story halafu inapoanza kunoga unaacha! au ndo tayari Yerico ameshaingia barazani na ile lozi na kashata uliyomwandalia imewanogea? (uchokozi kidogo! nadhani inaruhusiwa!)

Heheehee haya bwana!
 
Shekh Mohamed Said, tumalizie basi ile kasheshe ya Sheikh Abubakar Mwilima na Halmashauri kuu ya CCM iliishaje? Mwilima alifukuzwa au alilazimishwa kujiuzulu? au alikamatwa? uliishia pale wajumbe waliporudi baada ya kunwa chai kikao kiliendelea bila ya kugusia hoja ya Mwilima! halafu............

Shekh nawewe bwana wacha kutuanzishia story halafu inapoanza kunoga unaacha! au ndo tayari Yerico ameshaingia barazani na ile lozi na kashata uliyomwandalia imewanogea? (uchokozi kidogo! nadhani inaruhusiwa!)

Z,

Maskahara ni kitu kizuri kinaburudisha.

Yericko haluwa wala kahawa haipiti nimemshushia vitu vya 1950
mzee wake hajaingia Dar es Salaam.

Yeye anasema mzee wake alikuwa na chama hata jina lake silijui.

Tuendelee na kisa cha Sheikh Mwilima na Nyerere...

Sasa waliporudi ukumbini ile aganda Nyerere hakuileta kikaoni.
Mkutano ukaendelea hadi mwisho.

Lakini kuanzia pale Sheikh Mwilima akawa sasa anatafutwa ili
atolewe katika Halmashauri Kuu.

Lile neno aliloleta pale katika kikao lilikuwa jambo nyeti.
Nyerere akiogopa vitu viwili kuhusishwa navyo.

Kitu cha kwanza kuwa historia ya kudai uhuru ni historia ya
Waislam na pili akiogopa kuhusishwa akina Sykes.

Sheikh Mwilima alikuwa kamletea moja ya vitu vinavyomtisha.
Suala la Waislam.

Sasa ukileta katika kikao swala la dhulma dhidi ya Uislam lazima
itabidi mrudi nyuma kwenye kudai uhuru...

Haikupita muda Sheikh Mwilima akatuhumiwa kuwa anafanya biashara
ya kuuza fedha za kigeni kwa njia za haramu na akaitwa Halmashauri
Kuu ajieleze.

Akamkuta Nyerere kwenye kiti anamsubiri.
Huo ndiyo ukawa mwisho wa Sheikh Mwilima katika siasa.
 
Duh! yaani wazee wote walikuwa Waislamu! sasa wenzao walikuwa wapi jamani? au walikuwa hawataki uhuru?

Z,

Nitakuwekea hapa Government Circular No. 5 na No. 6 hizi ndizo
zilikuwa zinawatisha Wakristo kuingia katika siasa.

Hizi circular zilikuwa zinapiga marufuku watumishi wa serikali kujihusisha
na siasa.

Ukikamatwa adhabu ni kufukuzwa kazi.

Abdu ilikuwa kidogo afukuzwe kazi.

Iko siku pale ofisini kwake Kariakoo afisa wa Kiingereza kamwingilia ofisini
anamwambia kuwa ana taarifa Abdu anauza kadi za TANU pale sokoni.

Uzuri wa Abdu Sykes ni kuwa kwanza alikuwa na hela hivyo ule woga kuwa
akifukuzwa kazi atapata tabu haukuweko.

Abdu alikuwa na ulimi mzuri sana wa Kiingereza.

Watu wanasema siku ile tuliona senema ya bure pale sokoni Abdu na Mzungu
walivyokuwa wanapeana maneno.

Kimombo kilivyokuwa kikimtoka Abdu ilikuwa burudani ya aina yake.
Mzungu aliondoka akamwacha Abdu ofisini kwake.

Nina hazina wazee wameniachia kuhusu uhuru wa nchi yetu.
 
Nikukosoe kidogo ndugu yangu, miaka hiyo hakukuwa na siasa Tanganyika bali harakati!

Siasa zilianza rasmi baada ya mwanzoni mwa 1953 hadi 1961

Baada ya filosofia ya TAA kubadilika hasa kwa ujio wa Nyerere aliyekuja na filosofia yake kutoka TAWA

Yericko Nyerere,

Unapishana na historia ya Tanganyika nilichogundua wasomi wengi wa Tanzania hawana ufahamu wowote wa siasa za Tanganyika. Wanafahamu kuanzia mwaka 1961 baada ya Nyerere kuwa rais kupitia historia ya Kivukoni.

Hujui kama wakati wa TAA kulikuwa na mpambano mkubwa wa kisiasa kati ya wanasiasa vijana na wanasiasa wazee katika kushika madaraka na hatimaye wanasiasa vijana wakachukuwa madaraka.

Ngoja nikutajie wa hawa wachache Abdulwahid, Stephen Mhando, Dossa Aziz, James Mkande, Tewa Said Tewa, Ally Sykes, pamoja na wale madaktari watano.

Unataka kutuambia hawa wote walikuwa wanaharakati.
 
Last edited by a moderator:
Yericko Nyerere,

Unapishana na historia ya Tanganyika nilichogundua wasomi wengi wa Tanzania hawana ufahamu wowote wa siasa za Tanganyika. Wafahamu kuanzia mwaka 1961 baada ya Nyerere kuwa rais kupitia historia ya Kivukoni.

Hujui kama wakati wa TAA kulikuwa na mpambano mkubwa wa kisiasa kati ya wanasiasa vijana na wanasiasa wazee katika kushika madaraka na hatimaye wanasiasa vijana wakachukuwa madaraka.

Ngoja nikutajie wa hawa wachache Abdulwahid, Stephen Mhando, Dossa Aziz, James Mkande, Tewa Said Tewa, Ally Sykes, pamoja na wale madaktari watano.

Unataka kutuambia hawa wote walikuwa wanaharakati.

Ritz,

Msamehe Yericko,

Ana maradhi ya ''uoga wa historia.''
Mtie kundi moja na wanahistoria wa Kivukoni.

We uandike historia ya TANU umuache Abdu Sykes...

Umeona vitu nimekuwekea hapa kutoka ''Under the
Shadow of British Colonialism...''

Inawezekanaje tuache historia yote ile?
 
Nimesoma maandiko ya ndugu yangu Mohamed Said aliyoyaweka katika kitabu chake akiitacho Historia ya Uhuru upande wa Pili,
Katika maandishi yake ameonyesha wazi kulazimisha dunia iamini kuwa waislamu wamedhulumiwa katika historia ya Uhuru wa nchi hii,
Katika matakwa yake Mohamed Said anataka historia ya Uhuru ingetazama itikadi za kidini kwanza kabla ya kusimamia maudhui halisi ambayo ni Uhuru,

Nikubaliane nae kuwa historia ya nchi yetu inamapungufu na inahitaji masahihisho, lakini kwa hili la Mohamed si masahihisho bali ni upotoshaji mkubwa, Uchochezi na ni Uhaini kwa nchi. Kwa bahati mbaya bwana Mohamed Said histori anayoisimamia ameiakisi kuanzia miaka ya 1950+ tu,

Hajajishughulisha kuutazama utawala wa Kiingereza wala kuutazama upya utawala wa Kijerumani ambao ndio uliosimika misingi ya utawala na mifumo mingi ambayo leo tunaitumia! Mjerumani mfumo wake wa utawala kwa ASILI ni wa kikristu na kwa Tanganyika walisimama hivyo bila kutetereka! (Yaani mfumo kristu 100%)

Akaja Muingereza na yeye mfumo wa utawala wake wa ASILI ni wakikristu!

Imenilazimu kitabu cha bwana Mohamed Said kiitwacho "Maisha na nyakati za Abdulwahid Sykes 1924-1968" (Historia ya uhuru iliyofichwa ya upande pili) kukiita ni NGANO za masika.

Nitaelezea kwa ufupi jinsi kanisa la Tanganyika lilivyoshiriki harakati za ukombozi wa Tanganyika na madhila liliyokumbana nayo.

Ifahamike kuwa vyama vya harakati za ukombozi Tanganyika vilikuwa vingi sana, na vipo vilivyokuwa vikipingana vyenyewe kwa vyenyewe.

Mwaka 1927 – 1929 kanisa Katoliki nchini chini Joseph Gabriel Zelger, lilibainika kuingiza siasa katika utendaji kazi zake, kitendo hiki kiliwakwaza wakuu wa mamlaka ya kikoloni na kupelekea majasusi wakikoloni wapendekeze aachishwe uongozi wa kanisa nchini. Ni kweli tarehe 12 februari 1929 Zelger alistaafu wadhifawake kwa lazima.

Kisa hiki kinasema, Kanisa lilianzisha mafundisho yenye kuchochea fikra za kimaasi, nalilifanikiwa kuandaa wakufunzi maalumu kwenda katika majimbo yote ya kihuduma Tanganyika, hilo lilipelekea kuleta mtafaruku na dola ya mkoloni wa kiingereza ambapo ilimgharimu kiongozi huyu wa kiroho kuachia madaraka yake.

Alipoingia askofu Edger Aristide Maranta mwaka 1930, ikiwa kama vile mwendelezo wa mtangulizi wake, Askofu Maranda alianzisha harakati za kuwashawishi viongozi wengine wa majimbo kuendeleza kutoa mafundisho yenye kumfanya mtanganyika ajitambue na adai uhuru wake,

Mfano: 23 mei 1938 wakati makanisa saba ya Kilutheri yakiwa kwenye hatua za mwanzo za mchakato wa kuungana, Askofu maranda aliomba kuhudhuria kikao cha tarehe 8 mwezi wa sita kilichofanyika Mjini Arusha, Askofu Maranda aliudokeza mpango ule wa siri wa katoliki katika kikao hicho, japokuwa kulikuwa na hofu ya kutoaminiana, lakini uthabiti wa malengo hayo ulijipembua baadae na kuwa wamafaa.

Juhudi za kanisa kupigania ukombozi ziliendelea kushika kasi huku zikiendeshwa kwa siri sana kwamfumo wa neno la kiroho, na ilipofikia miaka ya 1950+ kanisa sasa lilikuwa tayari linanguvu ya ushawishi kufuatia mafanikio ya harakati za kanisa katika nyanja za ukombozi barani afrika.

Mtihani mkubwa kwa kanisa ilikuwa ni namna gani linaweza kuingia rasmi kudai uhuru wa Tanganyika. Katika kipindi hiki tangu harakati za kanisa zianze, Askofu Maranta pamoja na mapadre wa baadhi ya mikoa, walikuwa tayari ameshafanya juhudi kadhaa za kukutana na Mashehe waliokuwa na ushawishi mkubwa, mfano 05/02/1948, Askofu Maranda alikutana Shehe Issa bin Amir kiongozi wa kiroho katika msikiti wa Ilala - mchikichini. Mazungumzo yao yalihusu harakati za ukombozi, Shehe Issa alimshauri Askofu kuwa ikiwa makanisa na misikiti yanapigwa marufuku na mkoloni kujihusisha na siasa za ukombozi basi watafute baadhi ya vyama vya harakati za ukombozi na waviunge mkono, wazo hilo lilimvutia Askofu lakini akajenga hofu kama je ndani ya vyama hivyo watapata vijana wasomi?.

Siku chache baada ya makutano yake na Shehe Issa, Askofu Maranta aliletewa mapendekezo kutoka kwa Attilio Beltramino kassi wa katoliki aliyehudumu kule Iringa, mapendekezo ya kasisi huyu yalikuwa ni, Umishonari makao makuu uruhusu udurufu wa biblia zisomeke kwa makabila ya wahusika wa eneo, ndani ya biblia hizo yaongezwe mafundisho ya haki ya kujitambua na kujitawala wenyewe. Pendekezo hili lilimvutia sana Maranta hivyo akalipa baraka zake, kwa hakika lilifanikiwa na ndio lilizaa hisia kali za mwamko wa kudai uhuru, mfano biblia ya lugha ya kihehe ilikuwa inaeleza wazi athari za kutawaliwa.

Harakati za Ukombozi za Mwalimu Nyerere zililivutia kanisa na likaamua kumuunga mkono, mfano mwaka 1953 wakati TAA kikiwa chama chenye nguvu, Askofu Maranta alimwalika ofisini kwake Mwalimu Nyerere, walizungumza mengi lakini kubwa nikuwa alimsifu kwa juhudi za kujipambanua bila kuwaogopa wakoloni na akamweleza jinsi kanisa linavyounga mkono juhudi za ukombozi wa Tanganyika, kisha akamshauri kuwa ajaribu kuvishawishi baadhi ya vyama vya harakati za ukombozi viungane ili kuvipa nguvu ya kudai uhuru na kanisa litasaidia.

Wazo la Askofu Maranta lilimkaa Mzee Nyerere na mwaka 1954, alianza juhudi za kuwaunganisha vijana wenzake wa kariakoo ambao walikuwa ndani ya TAA na wenye nguvu ya ushawishi lakini wakikabiliwa na matatizo makubwa mawili katika lengo lao.



Elimu,

Woga



Ikumbukwe kuwa mwaka 1953 baada ya harakati za ukombozi kupamba moto na kamata kamata ya wanaukombozi, Askofu Edger Aristide Maranta alihamishiwa Zanzibar na nafasi yake ikachukuliwa na Vicar Apostolic, lakini bado aliendelea kuwa mshauri imara wa Mwalimu Nyerere. Jambo la kushangaza kama si kufurahisha, mwaka huohuo mwezi wa 8, Edger Aristide Maranta alirudishwa tena Dar es Saalam, na sasa mbinyo dhidi ya ukoloni ikahika mkondo wake.

Mnamo tarehe 7/71954, Vijana (wazee wa kariakoo) wakiongozwa na Julius Kambarage Nyerere, walikubaliana wazo la kuhuisha chama kutoka TAA kwenda TANU, chini ya uratibu wa karibu wa kanisa Katoliki (Askofu Maranta) na Waislamu (Shehe Issa bin Amir)


Mpaka hapo ndugu yangu Mohamed Said angalau umepata picha kwa KIFUPI tu ya harakati za uhuru chini ya kanisa.

Nikipata wasaa nitakuletea picha za Mwalimu Nyerere na Edger Aristide Maranta

Kwanini Kasisi huyu wa kikatoliki Edger Aristide Maranta hatajwi popote katika historia ya nchi? Kwanini kanisa katoliki halilalamiki kutokuwepo kwenye kitabu cha kivuko?

Yote hayo nitakushushia taratibu kadiri mnakasha huu unavyoenda.

Sasa nini kilifuata baada ya uhuru?

Nitaeleza kwakifupi tu:

Mwalimu Nyerere baada ya kukabidhiwa mamlaka kamili ya kushika dola na Malkia wa Uingereza alianza mageuzi ya kubadili mfumo huo kristu hasa mwanzoni mwa 1962 na juuhudi zilishika kasi zaidi mwanzoni mwa 1964 baada ya kuunganisha nchi ya Tanganyika na Zanzibar na kuzaliwa kwa Tanzania!

Juhudi hizi zilikwenda taratibu na kwa ufanisi wa hali ya juu kwakupitia hatua kadhaa ambazo ni pamoja na, kutaifisha huduma za kijamii zote zilizokuwa chini ya makanisa, kuanzisha sera ya elimu ya msingi kuwa ni ya LAAZIMA kwa watanzania wote nk, Kumbuka Mjerumani amekaa zaidi ya karne tatu akitumia mfumo kristu kutawala, Muingereza nae akalowea karne kadhaa akitawala kwa mfumo huohuo, Lakini ndani ya miongo miwili tu ya utawala wa Mwalimu Nyerere huku nchi ikitoka kwenye dimbwi la ukoloni aliweza kubadili sura na mfumo huo wa kikoloni na kuwa wawatanzania wote bila kujali dini, kabila rangi au kanda.

Naomba nimfungue macho na akili rasmi Mzee Mohamed Said huyu mpigania Dini kwa mgongo wa Uhuru wa nchi hii.
Nitaeleza kwa kifupi tu yale anayoyalilia Mohamed Said juu ya WAZEE wake.


Ukweli nikuwa kuanzia mwaka 1955 kulianza kuibuka mlengo tofauti kwa baadhi ya washarika wa ukombozi ndani ya TANU,
Hasa hasa mlengo huo ulikuwa ni kuweka itikadi ya DINI mbele, yaani iwe ndio tiketi halisi yakupigania uhuru na sio Utanganyika wao, na baada tu ya kupata uhuru, baadhi ya wazee waliokuwa beba kwa bega na Mwalimu katika harakati za kudai uhuru WALIASI rasmi sera ya Mwalimu nakuanza kuendesha vita ya chini kwa chini yakumpindua Mwalimu chini DINI.

Mwalimu Nyerere kwakutumia falsafa na malengo yake ya tangu akiwa Shule ya Tabora, Chuo kikuu Makerere na pale Scotland akiwa sambamba na wanaukombozi wasomi wenzie waliweza kuanzisha mfumo stahiki wa kufuta UDINI, UKABILA, Rangi, Ukanda na kisha Waliamua kuwafanya Watanganyika kuwa kitu KIMOJA.

Sasa mgogoro ulikuja kwa WAASI, kwakuwa hawakukubaliana na sera za Serikali mpya ya Mwalimu, wakaziidisha vurugu kwakushawishi makundi kadhaa ya kiroho yaenzi uasi huo, hilo lilipelekea serikali kuchukua hatua madhubuti dhidi yao ambapo mwaka 1962 katika kiwango cha juu cha hekima za Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na waambata wake, waliamua kuanzisha sheria ya kumuweka mtu kizuizini.

Sheria hii ilikuwa na mafaa kwa waasi kwani ililinda hadhi zao licha yakuwa waasi waliostahili vifungo vya maisha au kunyongwa kama ilivyokuwa destuli ya viongozi wengi wa dunia ya pili.
Mashehe wengi walitiwa kizuizini na wengine kufukuzwa nchini na makasisi wengi kupewa onyo kali.
Ifahamike kuwa hilo halikuwakumba mashehe tu kwani uasi huo ulikuwa hata kwa makasisi waliotaka itikadi zao ipewe kipaumbele zaidi na serikali ya Mwalimu Nyerere.

Kazi aliyofanya mzee Nyerere ni kubwa na alikumbana na vikwazo vingi sana kutoka kwa wakatoliki, rejea kitabu cha Van Bergen kuna barua nzito ya Mwalimu Nyerere kwenye faharasi ya 15 kwenda kwa makasisi wa kikatoliki akiwatolea karipio kuu kwakukwamisha juhudi zake, katika hii hakuchukua karne kadhaa kuumaliza mfumo uliodumu kwa mvua na mvua.

Japokuwa hakumaliza chembe za mfumo huu lakini kwangu naona ni zaidi ya 98% alimaliza, palipobaki ni mimi, wewe na wale ndio wenye dhamana ya kumalizia.

Uthabiti na tunu aliyoifanya Mzee Nyerere inathibitishwa kwa Hotuba yake ya tarehe 5 Novemba, 1985 kabla hajastaafu urais, Mzee Nyerere aliwahutubia wazee wa Dar es Salaam. Hotuba hii ilikuwa thabiti na yenye kuvuta nyoyo za waungwa, Baba wa Taifa Mzee Nyerere akikumbuka jinsi Waislam walivyompokea Dar es Salaam kwa mapenzi makubwa ingawa yeye alikuwa Mkristo. Wazee hawa wakiwemo Bin Amir ambae Mohamed Said anamlilia, wengi wao walikuwa wanachama wa zamani wa TANU waliomuunga mkono Nyerere wakati wa kudai uhuru. Mzee Nyerere aliusifia mchango wa Waislam katika kipindi kile kigumu cha kudai uhuru. Nyerere alisemakuwa "upogo katika elimu uliorithiwa na serikali yake kutoka kwa Waingereza baina ya Waislam na Wakristo yeye ameuondosha katika kipindi cha utawala wake":

Inakera kuona wewe Mohamed unarudisha nyuma juhudi za wanaukombozi wetu na kupandikiza chuki miongoni mwa dini hizi mbili!
Faida unayopata ni ndogo na niyakwako tu kuliko hatari inayolikumba taifa hivi leo!
Sipingi kusahihisha historia ya nchi hasa kama kuna mema yaliyoachwa lakini kupotosha na kuchochea kunatulazimisha tuhoji mamlamla za usalama wa nchi zimelala wapi? Leo mapinduzi matukufu ya Zanzibar, Mohamed Said anataka kutuaminisha kuwa Wanamapinduzi hawa wa Zanzibar waliwadhulumu waislamu wa Zanzibar na kuweka mfumo kristu anaodai upo au mfumo huo upo kwa Tanganyika tu?!


Katika kitabu chake bwana Mohamedi ametoa shutuma nyingi sana kwa Hayati baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ikiwemo ya eti Mwalimu katika hotuba yake ya kuaga taifa alitamka wazi kuwa hamjui ABDUL SYKES, Inashangaza sana kwani Mohamed Said anajua wazi ameudanganya umma na kudhihaki wanaukombozi wetu.

Ilikujiridhisha ndugu zangu wadau pitieni sehemu ya Hotuba ya Mwalimu Nyerere ya kuaga taifa tarehe 5 Novemba, 1985 kabla hajastaafu urais aliyoitoa mbele ya wazee wa Dar es Salaam,




‘"Mimi nimeanza siasa na wazee wa Dar es Salaam; na wazee wa Tanzania. Nimeanza nao mapema sana; mapema kweli. Nilirudi kutoka masomoni, Uingereza Oktoba 1952 – miaka 33 nyuma. Wakati huo nikiwa kijana mdogo wa miaka thelathini na kidogo hivi.

Niliporudi nikakubaliana na wamisionari hapo Pugu (sekondari), nifundishe shuleni kwao. Lakini nikiwa shuleni – Chuo Kikuu – nilijua. Niliishaamua kwamba maisha yangu yatakuwa ya siasa. Niliamua hivyo: Nitafundisha kwa muda wa miaka mitatu, nione hali inavyokwenda na kuzoeana na wenzangu kabla ya kuanza maisha ya siasa.

Niliporejea nchini hapo Oktoba, nikaenda Butiama. Januari nikarudi Dar es Salaam. Nikaanza kazi. Nikataka kujua habari za African Association. Mzee Mwangosi anakumbuka. Yeye ndiye aliniambia habari za African Association. Aliisha niambia habari hizo tangu nikiwa Makerere – Chuo Kikuu – nikiwa mwanafunzi.

Pale, mimi na wanafunzi wenzangu tulikuwa tumeanzisha chama kinachoitwa Tanganyika African Welfare Association (TAWA) cha wanafunzi wa Tanganyika; mimi nikiwa katibu wao. Hapa tukaona mambo yanakwenda vizuri kidogo.

Tukaona kwanini TAWA iwe ya wanafunzi peke yao na siyo Tanganyika nzima. Kwa hiyo nikawaandikia baadhi ya watu Tanganyika. Nikasema, jamani ee, tumeanzisha chama, kwanini msianzishe huko matawi ya chama hicho?

Ndugu Mwangosi akapata barua hiyo. Alikuwa miongoni mwa waliopata barua hiyo. Akaniandikia – nikiwa Makerere – akasema: wewe kwanini unataka kuanzisha chama kipya? Kipo chama. Kipo chama cha TAA (Tanganyika African Association).

Kwa hiyo la maana siyo kuanzisha matawi, maana chama kipo na matawi yameenea; la maana ni kwamba hicho chama chenu mfute, na muanzishe tawi la Tanganyika African Association.

KUVUNJWA KWA TAWA

Hivyo ndivyo tulivyofanya. Kwa hiyo mimi nikawa katibu wa katawi ka TAA hapo Makerere. Niliporudi Tabora na kuanza kufundisha pale St. Marys (sasa inaitwa Sekondari ya Milambo), nikachaguliwa katibu wa TAA wa jimbo ambalo makao yake makuu yalikuwa Tabora. Ulipofanyika mkutano wa TAA mjini Dar es Salaam, nilihudhuria nikiwa mjumbe kutoka Tabora.

Kwa hiyo nilikuwa naijua Tanganyika African Association. Nilipokuwa ninaondoka kwenda Ulaya kusoma, nilikuwa nimeishaonja shughuli za TAA. Sasa niliporudi, baada ya kukaa Pugu siku chache, nikaja mjini Dar es Salaam. Nikauliza nani wanaongoza TAA?
Nikaambiwa kuna jamaa mmoja anaitwa Abdul Sykes. Sasa ni marehemu. Abdul ndiye alikuwa katibu wakati huo.

Nilipelekwa na Kasela Bantu - ambaye naye aliteleza-teleza na hatunaye hapa (kwenye mkutano). Kasela Bantu alikuwa mwalimu mwenzangu. Tulifundisha pamoja Milambo. Nilipokuja Dar es Salaam, nikakuta anafanya kazi Redio (Tanganyika Broadcasting Corporation). Ni Kasela Bantu aliyenipeleka kwa Sykes.

Wakati huo mambo yalikuwa yanasinzia kidogo. Kwa muda mfupi mwaka ule, tukafufua-fufua, hasa kutoka Januari. Kufika Aprili, TAA ikafufuka. Tukafanya mkutano hapo Anautouglou. Kwenye mkutano huu wakanichagua kuwa Rais wao – wa TAA.

Ninasema yote haya kwa shukrani kwa wazee. Jamaa hawa walikuwa watu wazima wa Dar es Salaam, na mimi kijana mdogo Mzanaki, na Kiswahili changu si kizuri sana – cha matatizo.

Nimekuja, natoka Ulaya, tena masomoni. Muda mfupi tu jamaa hawa wakaniamini haraka sana – katika muda wa miezi mitatu. Wakanichagua Rais wa TAA. Hapo ndipo nilianza shughuli mpya ya kuandika katiba ya TAA na kuipa madhumuni hasa ya shabaha ya kuleta uhuru.

Baada ya miezi 13, hapo 1954, tukaanzisha TANU. Jina hili lilipendekezwa na akina Abdul Sykes. Walikuwa wamelifikiria tangu zamani, walipokuwa askari vitani huko Burma (Vita vya Pili).

WAZEE NA MSIMAMO

Miezi minne baada ya kuanza kazi Pugu nikawa ninakuja Dar es Salaam, kwa mguu; kila Jumamosi. Baadaye wazee wakanipa baiskeli nikawa ninakuja mjini kukutana na wenzangu; kufanya mikutano.

Hivyo ndivyo tulivyofanya. Wazee wakaniamini upesi sana. Tukawa na uhusiano mkubwa sana. Wadogo wenzangu wengine walikuwa Abdul Sykes, Abass Sykes (mdogo wake), Dosa Aziz – waliokuwa wengi ni wazee.

Katika kuhutubia mikutano yangu, nilikuwa nikisema: Wazee na Ndugu zangu! Wazee hasa ndio walikuwa na mikutano ya awali ya TAA na TANU. Walikuwa na msimamo wa hali ya juu kabisa! Hawakuyumba hata kidogo! Vijana walikuwa na mashaka. Wengine walikuwa na vikazi vyao, waliogopa kuvipoteza.

Nalo jambo lenyewe ni la hatari – la kuzungumzia uhuru! Unaweza ukakosa kazi; na wapo waliopoteza kazi; wengine wakaacha kazi. Akina Rashid (Kawawa) waliona watoke kwenye shughuli hizo tuje tuungane katika chama.

Wazee wa Dar es Salaam, na baadaye wa nchi nzima, wakatuunga mkono, na kila nilipokwenda, watu wa kwanza walionielewa, walikuwa wazee.

Nilikwenda Songea mwaka 1955 mara baada ya kujiuzulu. Huko wazee walinipokea na kunielewa. Nilianza safari za kuitembelea Tanganyika nzima. Nilikwenda Mbeya. Mkutano wangu niliufanya na wazee; kikundi kidogo cha wazee, ndani ya nyumba ya mtu.

Kwa mkutano huu wa Mbeya, wazee wakauliza: Unatafuta nini? Nikawaambia natafuta uhuru. Wale wazee, kwa sababu ya vita vya Maji Maji, na wanakumbuka, kabisa, wakaona mimi ninatafuta jambo la hatari. Tulifanya mkutano wa makini kweli. Wakauliza: Wewe unawezaje kuleta uhuru? Wewe una njia gani kudai uhuru na usitiwe kitanzi na Waingereza?

WAINGEREZA WAONGO

Tulielezana. Nikawaambia ninyi wazee, Waingereza wanawadanganya, Waingereza wametumwa na ule Umoja wa Mataifa uliokufa (League of Nations), waje kuishika Tanganyika kwa muda tu; watusaidie, na wakati tutakapokuwa tayari, watuachie tukajitawale.

Waingereza wanafanya ujanja; hawasemi. Vita vimekwisha (vya Pili) na Umoja wa Mataifa mwingine – mpya (United Nations Organisation – UNO) umewakabidhi Tanganyika kwa shabaha ileile. Sisi siyo koloni lao. Wamepewa dhamana tu.


Kwa hiyo nikawaambia wazee, hakuna haja ya kumwaga damu. Tuwaseme tu! Tuwashitaki kwa waliowaleta hapa kwamba hawafanyi kazi yao; wamesahau kabisa!

Wazee wakauliza: Eh, inawezekana? Nikasema inawezekana. Kazi yetu ya kwanza ilikuwa kuwaambia watu kwamba uwezekano wa kujitawala upo. Hilo lilikuwa la kwanza. Wazee walijua maana ya kujitawala. Walitamani kujitawala, lakini hawakujua waanzie wapi.

Vijana hawakuwa na habari kwamba kujitawala kunawezekana. Kwa hiyo kwa wazee sikuwa na matatizo. Wao hawakuwa na kazi; hawakumwogopa Mwingereza. Hawakuogopa kufukuzwa kazi. Baadhi walikuwa wafanyabiashara.

Mzee John Rupia (marehemu) alikwua mfanyabiashara na kaidi kidogo. Aliwahi kutishwa na kunyang’anywa leseni yake ya biashara. Akaambiwa akiendelea kushirikiana na kijana mwenda wazimu (Julius Nyerere), atanyang’anywa leseni moja kwa moja. Rupia aliwajibu: Potelea mbali!

Nasema yote haya ikiwa njia ya kutoa shukrani kwa wazee na imani yao kwa vijana wakati huo.

Imani hujenga imani. Na mambo haya makubwa ya nchi, kama hayana baraka za wazee hayaendi. Magumu sana. Wanasema ngoma ya watoto haikeshi! Mimi nilipata baraka za wazee tangu zamani. Tangu awali kabisa.

TWAININGI AMEKWISHA

Siku moja, Dosa akanifuata Magomeni (Dar es Salaam). Akasema: Leo wazee wanakutaka. Wapi? Kwa Mzee Jumbe Tambaza. Wanakutaka usiku. Nikasema haya, nitakuja. Nikaenda. Nikakuta wazee wameshakaa; wameniita kijana wao kuniombea dua. Mimi Mkristo, wao Waislamu watupu. Wakaniombea dua za ubani. Tukamaliza.

Tulipomaliza wakasema kuna dua pia za wazee wao. Basi wakanitoa nje. Tukatoka. Zilipomalizika zilikuwa za Korani; sasa zikaja dua za wazee – za jadi.

Walikuwa na beberu la mbuzi. Wamechimba shimo. Wakaniambia simama. Nikasimama. Beberu akachinjwa, huku anaambiwa, “Twining (Twainingi) umekwisha!” (Edward Twining alikuwa Gavana wakati huo). Ndipo nikaambiwa: Tambuka! Nikavuka lile shimo. Hapo nikaambiwa na wazee: Basi nenda zako; tangu leo Twainingi amekwisha!

Sasa mimi Mkristo; hao Waislamu. Na mimi mkorofi-korofi katika mambo haya (ya kutambika). Lakini tulikuwa tunaelewana na wazee wangu hao. Kwa hiyo nilitambuka pale na kuambiwa: Nenda nyumbani salama. Twaining hawezi tena!

Wazee wangu wengine wanakumbuka tulikuwa tunakwenda Bagamoyo. Kwenye makaburi kule! Tunapiga dua huko kwenye makaburi na wazee wangu.

Baadhi yetu mtakumbuka safari moja jamaa wa Kenya, hawa akina Tom Mboya (marehemu) walishitakiwa. Tukasema tuwasaidie. Tuwasaidie vipi? Tukasema tufunge. Tukaomba nchi nzima kufunga siku hiyo. Tufunge! Tukafunga. Hakuna kula. Na siku ya kufunga tulikuwa na mkutano Bagamoyo. Tukaenda huko. Tukafanya mkutano hadi saa 12 jioni.

Baada ya mkutano tukaenda nyumbani kwa Mzee Mohamed Ramia (marehemu). Hapa ndipo tulikuwa tumefikia. Mimi nikamuuliza mzee: Sheikh, una Aspro? Akajibu: Kwa nini unataka Aspro? Nikajibu kuwa kichwa kinaniuma kwelikweli. Akasema subiri.

Tulisubiri hadi saa ya kufuturu. Tukafuturu vizuri. Mzee Ramia akaniuliza: bado unataka Aspro? Nikajibu kichwa sasa hakiumi. Kumbe ilikuwa njaa.

Nawaelezeni haya kwa sababu huko tulikotoka, tulishikamana sana. Tulishirikiana sana na wazee."’



Mohamed Said kuwa mkweli, waambie ukweli watanzania (waislamu) kuwa umetumia mgongo wa Uislamu na Hayati Abdul Sykes, kwakumkashifu na kumdhihaki Hayati Mwalimu Julius Nyerere na kuwasafisha wazee wako walioasi serikali mpya ya Mwalimu ambapo ndipo madhila hayo wakayapata.

Juzi nimemuuliza maswali katika mjadala flani hapa, lakini majibu yake yamenifanya nijiridhishe kuwa Mohamed Said ni muhaini na mchochezi mkubwa wa nchi hii, Ameudhihaki Uislamu nchini na duniani kote,

Nilimuuliza hivi:


Naomba unijibu maswali haya kwaufasaha mwanazuoni Mohamed Said:

1) Uliathirika vipi kwa baadhi ya wazee waliopigania uhuru wa nchi hii kutokuwemo kwao katika histori ya nchi hii kama unavyodai?

2) Taifa na waislamu waliathirika vipi kwa baadhi ya wazee unaodai wewe walipigania uhuru wa nchi hii na hawamo katika historia?

3) Ulijuaje kuwa wazee hao walipigania uhuru ilihali hawapo katika historia stahiki ya nchi hii?

4) Unaposema historia ya uhuru wa nchi hii haiwakumbuki ama haiwatambui, ulitaka wakumbukwe katika maandishi ya vitabu au katika nyaraka za serikali za historia ya uhuru wetu?

5) Unatambua kuwa historia ya nchi yoyote ile duniani huwa wapi?

6) Upeo wako umegota kwenye historia ya waislamu wa Tanganyika na Nyerere tu, au historia ya waslamu duniani kote? Kama ndivyo, je matatizo ya waislamu wa Nigeria, Somalia, Sudani, nk Nyerere ndiye kayapeleka?

7) Je ulichokiandika ni historia ya Uhuru wa Tanganyika au ni historia ya baadhi ya Waislamu wa Tanganyika na mapito yao kisiasa?

8) Kwanini unaulazimisha umma kwa maandishi yako uamini kuwa ulichoandika ndio historia sahihi ya Uhuru wa Tanganyika?

9) Je ni kweli Mohamed Said huwajui na huwatambui wale wazee 17 waliosimama kidete kudai uhuru wa nchi yetu? Je wote walikuwa wakrstu?

Naomba majibu ili tujenge hoja mpya yamjadala huu kwa mafaa ya taifa letu!






Lakini maswali mengine yamsingi yaliulizwa na wadau wengi kama Nguruvi3, Mwanakijiji na moja ya maswali yaliyonivutia ni hapa hapa chini:


By adolay:


Ninakuuliza somalia na nyerere kwasababu waislam wa somalia wanamatatizo makubwa ya kijamii, kisiasa, kieliemu, afya nk

Nani mchawi maana hapa kwetu kwa mujibu wa hadithi zako ni Nyerere. (Tunaongelea matatizo ya waislamu na wanaowahujumu)

Watanzania (Waislam, wakristu pia wa imani zingine na wasio amini) wanamatatizo aghalabu si makubwa kama ya wasomali.

1. Kwanini useme waislam wa Tanzania ni hujuma za nyerere na kwanini wasiwe waislam wa somalia? kunatofauti ya uislam wa somalia na ule wa tanzania?

2. Je katika historia yako ufahamu wako umegota Tanzania kwa hayati JK Nyerere peke yake? kama ndivyo nini ubora na ufahamu wako kujisifu mwanahistoria makini kama sio mbabaishaji?

Tafadhali rejea maswali kutushawishi kwamba wewe ni mkweli na kashifa zako dhidi ya Nyerere ni uwongo na majungu.

Tuanze na Somalia, nataka usome swali uelewe ujibu kama nilivyouliza sio kuniwekea hadithi za maandishi zisizoakisi maudhui ya swali.

1. Nani amewahujumu/aliwahujumu wasomali na uislamu wa somalia mpaka wamefikia hapa walipo je? ni nyerere

2. Ni mfumogani unatumika katika kuitawala somalia kiasi kwamba wamefika hapo walipo ilituutupie lawama

a) Mfumo kristo ndiyo maana wamefika hapo walipo

b) Mfumo islam, mahakama ya kadhi nk

c) hufahamu nakama hufahamu nini mtazamo wako.

Ninakuuliza maswali haya lengo nikutaka kuujuwa ukweli wa pengine Nyerere huyu pia yupo somalia, afghanistan, pakistani, lebanon, syria, libya nk nakwamba machafuko yote yanayoendelea huko ni hujuma za Nyerere na mfumo kristo kama unavyowapotosha watanzania na kuwachochea!

Naomba majibu ya maswali yangu hapo juu kuthibitisha kwamba wewe sio mchochezi na mchonganishi wa waislamu na wakristo kwa kubuni vitu visivokuwepo.

Mohamed Said, baada ya utangulizi huo narejerea maswali yangu ya jana kwa ufafanuzi. Angalizo jibu maswali kama yalivyoulizwa na sio siasa au funika kombe mwanaharamu apite kwa nukuu za maandishi zisizobeba maana wala majibu ya hayo maswali




MAJIBU YA MOHAMED SAID:

quote_icon.png
By Mohamed Said

Umeingiza mambo mengi sana.
Kuna Zanzibar, elimu ya Waislam, matokeo mabaya ya shule za Kiislam, kuchinja.

Itakuwa tabu kufanya mjadala uliokuwa hauna mwelekeo ulionyooka.

Lakini kwa mukhtasari ukitaka historia ya Zanzibar na maendeleo yake itabidi tuanza kwa kuvamiwa
kwa Zanzibar na jeshi mamluki la Wamakonde kutoka Kipumbwi wakifadhiliwa na utawala wa Nyerere.

Kuanzia hapa tutaingia katika tatizo la Muungano na kwa nini leo Wazanzibari wanadai nchi yao.

Kuhusu elimu ya Waislam itatubidi tuje katika njama za Nyerere kuhujumu chuo kikuu cha Kiislam
kilichokuwa kijengwe Dar es Salaam mwaka 1968 na jinsi alivyotumia uongo na ghilba kuvunja EAMWS
na kuunda taasisi kibaraka BAKWATA.

Vipi shule za Waislam hazifanyi vyema inabidi tuje katika hujma ya NECTA kwa wanafunzi wa Kiislam na
tuupitie waraka wa marehemu Prof. Malima kuhusu yale aliyoyakuta Wizara ya Elimu mwaka 1987.

Wizara ya Elimu na NECTA vimegeuzwa vigango vya kanisa.

Kubwa zaidi ni kuwa Waislam kwa muda mrefu hatukuruhusiwa kujioganaizi nje ya BAKWATA kibaraka
wa serikali.

Makanisa mnaendelea kwa kupendelewa na serikali iliyojaza watendaji Wakristo sisi tungepewa hayo
mabilioni ya MoU kati ya Makanisa na Serikali tusingekuwa kama hivi.

Yapo mengi sasa chagua tuanze na lipi katika hayo hapu juu niliyokugusia.

Wajerumani waliwaweka Wayahudi katika ghetto kisha wakawa wanawalaumu kwa uchafu.
Kwenye ghetto hakuna maji wala misala sasa watu wafanyeje?

Mnatusimanga kwa hospitali mnazoendesha kwa hela ya kodi ya serikali kodi inayolipwa na raia
wote.

Tunabanwa na mfumokristo kisha mnatulaumu hatuna maendeleo







Mohamed said

katika pita pita zangu nimekutana na post yako hii ya tare 4 January 2013 #914

Umeongelea kunyanyaswa kwa waislamu katika elimu ni njama ya JK Nyerere - Elimu ya somalia ipo taabani sana na Nyerere hayupo huko

Nakwamba Nyerere alitumia uongo na ghilba kuvunja EAMWS - lakini ghilba wala uongo wa nyerere haupo Somali na inateketea vibaya

Necta imegeuka vigango vya kanisa - Somalia haina vigango vya makanisa katika taasisi zake hususani elimu lakini ipo taabani

Serikali imejaza wakristo kwa upendeleo na kuwaacha waislam - Somalia serikali takribani yote ni waislam hakuna maendeleo

Wakristo
wanawasimanga kwa hospitali zilizo jengwa kwa kodi ya watanzania- wasomali pia wanatoa na kukusanya kodi hakuna afya bora, elem wala siasa safi!

Waislamu wanabanwa na
mfumo kristo
- Somalia kuna mfumogani unaowabana wasiendelee



hivi na kakwambia somali wako nyuma kwa eleimu? kwa ufupi wasomali wamesoma zaidi kuliko watanganyika wapo dunia nzima na ni watafiti , wa madaktari wazuri..japo nchi yao imedhulumiwa na mataifa ya kikiristo kuweka vibaraka na kiuishambulia kuivuruga lakini ....hatuwezi kuwafika ..wasomali.....hebu nambie haswa kuna msomi gani ....unemuona huku Tanzania ukamlinganisha na wasomali ambao wamesoma zamani na kustaarabika kabla watanganyika hwajajua kuvaa nguo....nao hawa wasomali hawajawahi kuwa watumwa na sababu kubwa ni kwa sababu wao wamesoma ..watumwa walifanywa zaidi wale walikua wajinga hawakusoma...chukua mfano wa historia hii hapa ya baadhi ya wasomi na personality za kisomali kabla hamjamtoa ngombe bandani alale nje
Important Islamic figures

kwa ufupi Tanzania hakuna nchi katika nchi za kiislam au zenye chembe ya waislam....mnayo ipita kwa elemu...labda zanzibar nao kwa sababu ya ujinga wao kuungana
 
Kitu pekee ambacho Bw. Mohammed Said ameshindwa kukionesha hadi hivi sasa japo anakidai kwa maneno ni kuwa wazee wa Kiislamu na Waislamu kwa ujumla walipigania uhuru peke yao bila ushirika wa ndugu zao Wakristu. Amejitahidi sana lakini mara zote anajikuta historia inamkatalia...

Angelikuwa na uwezo wa kufuta ushiriki wa wazee Wakristu na wasio Wakristu katika harakati za Uhuru angewafuta... angejaribu kuandika historia ya harakati zaWaislamu peke yao kupigania uhuru angejaribu

Mbona kawataja kwingi tu.

Joseph Mutahangarwa, James Mkande, Stephen Mhando, Vedasto Kyaruzi, John Rupia, Oscar Kambona, Wilbard Mwanjisi. Denis Phombeah, Alexander Tobias, Michael Lugazia.

Hawa wote bila Mohamed Said tusingewafahamu.
 
Yericko Nyerere,

Unapishana na historia ya Tanganyika nilichogundua wasomi wengi wa Tanzania hawana ufahamu wowote wa siasa za Tanganyika. Wanafahamu kuanzia mwaka 1961 baada ya Nyerere kuwa rais kupitia historia ya Kivukoni.

Hujui kama wakati wa TAA kulikuwa na mpambano mkubwa wa kisiasa kati ya wanasiasa vijana na wanasiasa wazee katika kushika madaraka na hatimaye wanasiasa vijana wakachukuwa madaraka.

Ngoja nikutajie wa hawa wachache Abdulwahid, Stephen Mhando, Dossa Aziz, James Mkande, Tewa Said Tewa, Ally Sykes, pamoja na wale madaktari watano.

Unataka kutuambia hawa wote walikuwa wanaharakati.

Ndugu yangu kuna kitu kikubwa sana lazima ukielewe katika siasa,Harakati nk, kitu hicho huitwa SHABAHA/Filosofia/ideology

Huo ndio muongozo wa chama ama kikundi chochote kile,

AA ilikuwa na SHABAHA yake, na TAA ilikuwa na yake mpaka ilipobadilika kuanzi 1953 baada ya Mwalimu kushika urais wa TAA,

Hao vijana ni sawa waligombea uongozi wa chama lakini chama kilichokuwa na filosofia yenye kujikita kudai HAKI na sio UHURU
 
Last edited by a moderator:
MM,

[TABLE="class: MsoNormalTable"]
[TR]
[TD] Father Smith of the Roman Catholic Church and the Party seem to be of the same mind on this dissension. [1] Both Kiwanuka and Fr Smith are expressing their own personal opinion, not facts. No one denies the fact that some Christians were there. Indeed Christian names appear in the dramatis personae of the play. But no one can deny the truth that they did not occupy centre stage.
[/TD]
[/TR]
[/TABLE]

Ok lets talk about the facts if you will...

a. Kuna wakati wowote ambapo Wakristu hawakushiriki katika harakati za Uhuru au katika vyama mbalimbali vya kupigania haki za Wakristu?

b. Kuna wakati ambapo Wakristu hawakuwa viongozi wa juu katika vyama hivyo mbalimbali na hivyo kuwa aktika "centre stage" ya shughuli za vyama hivyo?

It is absolutely absurd and silly to suggest - even remotely - that the names such of those of John Rupia, Dr. Mwanjisi, Dr. Kyaruzi, Stephen Mhando, Clement, na wengine wengi only appear in 'dramatis personae' sijui hata kama ulimaanisha hivyo maana "dramatis personae' ni characters wa mchezo - na haihusishi watu ambao hawakuwa na centre role. Hivyo kina Dossa Aziz, Abdulwahid, Nyerere, Titi Mohammed wote wako kwenye orodha ya characters tu na katika hao walioshika nafasi kuu of course ni Nyerere (star of the show) akiwa na supporting cast kama kina Abdul, Rupia na wengine.

Mchango wa Wakristu katika harakati za uhuru na nafasi zao haiwezekani kupuuzwa, kubezwa au kudunishwa. Kama walivyofanya ndugu zao ndivyo hivyo Wakristu nao walishiriki bega kwa bega na kulipia gharama ile ile ambayo wengine walilipia katika kupigania uhuru. HIstoria inatufundisha jinsi wazee wetu walivyoshirikiana kumpinga ukoloni licha ya tofauti zao za mahali, dini, kabila, na hata hali (status).

Those my dear one are the indisputable facts. You DO NOT have any facts to the contrary. No you don't.
 
Mohamed Said kumbe prophets of doom mko wengi
"
"Church affiliated writers also advance the idea that Nyerere's efforts to cultivate mutual relationships with and between Christians and Muslims religious leaders ensured religious tolerance in Tanzania since independence. However, authors like Fairoz, al-Zinjibari and Said Mohammed, see Nyerere as a serious bulwark against the flourishing of Islam in Tanzania. Foremost they take issue with close association between Islam and slavery in the persona of the Arab in the country's political rhetoric and condemn the elevation of the role of the missionary and its institutions in Tanganyika's liberation
 
Last edited by a moderator:
Mbona kawataja kwingi tu.

Joseph Mutahangarwa, James Mkande, Stephen Mhando, Vedasto Kyaruzi, John Rupia, Oscar Kambona, Wilbard Mwanjisi.

Hawa wote bila Mohamed Said tusingewafahamu.

Are you really serious? Kweli M Said kawaweza; kawaaminisha kuwa watu hawa wote yeye ndio kawataja kwa mara ya kwanza katika historia. Na la kusikitisha zaidi ni kuwa mpo mnaoamini kabisa kuwa Mohammed Said ndiye mtu wa kwanza kuwataja watu hawa na nafasi yao katika historia. That is really sad. Ukiondoa majina machache ambayo labda yanahusiana na watu wa Gerezani na Kariakoo majina ya washirika wa harakati za Uhuru kutoka sehemu mbalimbali nchini yanajulikana kwa muda mrefu yameandikwa kwa kiasi kikubwa tu.

Alichofanya Mohammed Said katika kujaribu kuiandika upya historia hiyo ni kuwagawa wazee wetu kwa misingi ya dini (Waislamu Vs. Wakristu). Anafanya kile ambacho baadhi ya wazee wake wa Kariakoo walijaribu kukifanya mwaka 1958 walipojaribu kuzigawanya harakati hizo za uhuru kwa misingi hiyo ya dini na matokeo yake wakatimuliwa miaka michache baadaye.

Kama unaamini kuwa Mohammed Said ndiye anawataja hawa - tena kwa dharau kuwa hawakuwa na central role kwenye harakati hizo ila wanatajwa tu kama waigizaji kwenye mchezo wa kuigiza - it is in itself tragic.
 
hivi na kakwambia somali wako nyuma kwa eleimu? kwa ufupi wasomali wamesoma zaidi kuliko watanganyika wapo dunia nzima na ni watafiti , wa madaktari wazuri..japo nchi yao imedhulumiwa na mataifa ya kikiristo kuweka vibaraka na kiuishambulia kuivuruga lakini ....hatuwezi kuwafika ..wasomali.....hebu nambie haswa kuna msomi gani ....unemuona huku Tanzania ukamlinganisha na wasomali ambao wamesoma zamani na kustaarabika kabla watanganyika hwajajua kuvaa nguo....nao hawa wasomali hawajawahi kuwa watumwa na sababu kubwa ni kwa sababu wao wamesoma ..watumwa walifanywa zaidi wale walikua wajinga hawakusoma...chukua mfano wa historia hii hapa ya baadhi ya wasomi na personality za kisomali kabla hamjamtoa ngombe bandani alale nje
Important Islamic figures

kwa ufupi Tanzania hakuna nchi katika nchi za kiislam au zenye chembe ya waislam....mnayo ipita kwa elemu...labda zanzibar nao kwa sababu ya ujinga wao kuungana

Notable individuals of the somali....Tanzania yupo Nyerere tu...na yeye ndio mfumo...akikosolewa basi wenye mfumo wote....wanakuja juu...lakini tunamshukuru mzee wetu Ali Hassan Mwinyi...aliupindua kwa kiasi mfumo.......

Abdi YusufHassan – Somali politician, diplomat and journalist. Former Director of IRIN and UNHCR Head ofExternal and Media Relations in Southwestand Central Asia



 
Na kwa taarifa yako Mohamed Said,kwenda kwa Nyerere twice UNO,bulk kubwa ya nauli ilitolewa na Maryknoll sisters
 
Last edited by a moderator:
Are you really serious? Kweli M Said kawaweza; kawaaminisha kuwa watu hawa wote yeye ndio kawataja kwa mara ya kwanza katika historia. Na la kusikitisha zaidi ni kuwa mpo mnaoamini kabisa kuwa Mohammed Said ndiye mtu wa kwanza kuwataja watu hawa na nafasi yao katika historia. That is really sad. Ukiondoa majina machache ambayo labda yanahusiana na watu wa Gerezani na Kariakoo majina ya washirika wa harakati za Uhuru kutoka sehemu mbalimbali nchini yanajulikana kwa muda mrefu yameandikwa kwa kiasi kikubwa tu.

Alichofanya Mohammed Said katika kujaribu kuiandika upya historia hiyo ni kuwagawa wazee wetu kwa misingi ya dini (Waislamu Vs. Wakristu). Anafanya kile ambacho baadhi ya wazee wake wa Kariakoo walijaribu kukifanya mwaka 1958 walipojaribu kuzigawanya harakati hizo za uhuru kwa misingi hiyo ya dini na matokeo yake wakatimuliwa miaka michache baadaye.

Kama unaamini kuwa Mohammed Said ndiye anawataja hawa - tena kwa dharau kuwa hawakuwa na central role kwenye harakati hizo ila wanatajwa tu kama waigizaji kwenye mchezo wa kuigiza - it is in itself tragic.

MM,

Ndugu yangu mimi huniwezi katika historia hii.
Mimi hawa watu wazee wangu nimewaona na nimewasikia wakizungumza.

Mimi hawa ni watu wangu.
Vipi wewe uwajue hawa na historia yao unishinde mie?

We si unaona nilivyokubadilishia dawa?
Sasa nakupa vidonge vipya.

Unasikia mzee anavyosema katika ''Under the Shadow of British Colonialism...''

We hayo utayapata Kivukoni College?
Kutokujua mambo si ujinga.

Shughulilka na wengine.
 
Are you really serious? Kweli M Said kawaweza; kawaaminisha kuwa watu hawa wote yeye ndio kawataja kwa mara ya kwanza katika historia. Na la kusikitisha zaidi ni kuwa mpo mnaoamini kabisa kuwa Mohammed Said ndiye mtu wa kwanza kuwataja watu hawa na nafasi yao katika historia. That is really sad. Ukiondoa majina machache ambayo labda yanahusiana na watu wa Gerezani na Kariakoo majina ya washirika wa harakati za Uhuru kutoka sehemu mbalimbali nchini yanajulikana kwa muda mrefu yameandikwa kwa kiasi kikubwa tu.

Alichofanya Mohammed Said katika kujaribu kuiandika upya historia hiyo ni kuwagawa wazee wetu kwa misingi ya dini (Waislamu Vs. Wakristu). Anafanya kile ambacho baadhi ya wazee wake wa Kariakoo walijaribu kukifanya mwaka 1958 walipojaribu kuzigawanya harakati hizo za uhuru kwa misingi hiyo ya dini na matokeo yake wakatimuliwa miaka michache baadaye.

Kama unaamini kuwa Mohammed Said ndiye anawataja hawa - tena kwa dharau kuwa hawakuwa na central role kwenye harakati hizo ila wanatajwa tu kama waigizaji kwenye mchezo wa kuigiza - it is in itself tragic.

Kibaya zaidi hasemi ukweli wakilicho wasibu hapo wazee wake mpaka wakafukuzwa na wengune kufungwa jela
 
Back
Top Bottom