Je wajua kuwa Utafiti huo umefanyiwa review na vyuo zaidi ya 5 Duniyani na vyuo vyenye kuhishimika. Je kama ingekuwa umeandikwa utumbo vyuo hivyo au wasomi hao waliobobea kwenye African history wangejishughulisha nao.
Mbona kitabu cha Uhuru wa Tanganyika kilichotungwa na Chuo cha Kivukoni hakijawahi kufanyiwa review popote pale hata UDSM.
Hakika mnyonge mnyonge lakin haki yake mpeni.
nanga limewaka hili andikeni kitabu kupingana na haya na sio bla bla
Baru,
Hawa hawano kitu.
Mimi nimesimama kwenye kilingo Northwestern University, Chicago
mbele ya mabingwa wa historia ya Afrika.
Nimesimama nikamueleza marehemu Abdulwahid Sykes na yale alofanyia
Tanganyika katika kudai uhuru.
Ukumbi uliwaka moto.
Muslim symbols katika harakati zikiwakata maini Wamarekani.
Nami nilifanya makusudi.
Nilipofika 1948 katika mgomo wa makuli Abdu kiongozi wao akiwa kijana wa
miaka 24 wanafanya kisomo Bonde la Msimbazi kabla ya mgomo nikawasomea
uradi hasbunallah waniimal wakil nikawamalizian na lailahillllah.
Nawaambia Waamerika hii ndiyo silaha wazee wetu waliyomshindia Mwingereza
ambae na nyinyi milipigananae kupata uhuru wenu 1776.
Nikawaambia ndiyo maana iliposadifu kuunda TANU katika kamati ya ndani ya TAA
unamkuta Mufti wa Tanganyika na Zanzibar Sheikh Hassan bin Amir mwaka 1950.
What about Nyerere?
Swali likaja...
Jibu langu: About what?
Ukumbi mzima ukaangua kicheko.
Hawa ni wajuzi ukiwafumbia fumbo wanategua hapo hapo.
Nikawapa na pp nilotoa Chuo Kikuu Zanzibar kuhusu Sheikh Hassan bin Amir.
"...and Mohamed you knew all these people who made history?"
Baru mie nimesimama mbele yao nacheka tu na kumshukuru Allah.
Ati anasimama mtu hapa free for all anataka kunitisha mimi na kitabu
cha kufikirika...