Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar

Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar

Jasusi,
Sikujua kama yule Bi Mkubwa amefariki.

Akinijua vyema na kunipenda kama mwanae.
Mara ya mwisho nilimuona kasimama nje ya
nyumba yake pale Regent na tukasalimiana.

Namkumbuka na gari yake Peugeot akiwabeba
wanae kuwaleta kwenye parties zetu.

Jasusi nakurudisha nyuma...
Mick Jagger and The Rolling Stones.

Wakati umekwenda.

Duuh,
Umenikumbusha mbali. Mick Jagger and the Rolling Stones. I was Mick Jagger pale Aga Khan.
Ndiyo watafute akina Esta na Pati Mzena nadhani bado wapo hapo Dar. Msiba ulikuwa wiki iliyopita.
 
Ritz,

Salaam. Nakufahamu na nakusikiza kwa yakin. Mimi najua mengi mno wala sitie shaka. Andrew Nyerere,ni rafiki mkubwa wa Mzazi wangu,nafikiri niliwahi kusema hapo awali.

Huyo jamaa ni psychological fragile,angalia tu ile mada yake halafu ameweka Sheikh Issa Bin Ameir badala ya Sheikh Hassan Bin Ameir...kama kwenye legal technicalities basi Barrister mahiri anakwambia Case dismiss!

Hapa kilichobaki kwa ufupi ni kurembeana fedhuli na kibri kingi tu,labda zaidi wanatumia udhalimu wao wa kumuuliza makhanatha Sheikh Mohammed ili wamuumize kichwa.

Takriban yoote alozungumzia Zali la Mentali a.k.a Mchimba Chumvi,ndo yale yale alokua anadarsisha Sheikh Mohammed takriban miezi minne. Tafauti yeye Zali la Mentali kawaendesha kindava na kimchakamchaka wa nguvu,ndo maana unaona kijasho chembamba kinawabubujika.

Yule kunguni wa hoja a.k.a Abu Jahal,mimi pia nilimtoa maanani kitambo pale alipoleta ule uTarime/Ukabila wake,na ati kujaribu kumtetea Nyerere tena kwa kutumia Khadith na Qur'aan tukufu. Yule Kunguni Wallahi ni Khabith Al maar.

Nyerere aliwahi kufanza mema kiduchu,lakini dhahma wa min'karadas,dhuluma na madhila aloleta ni mengi mno pita kiasi na yanawasulubu watu wengi mno hapo Tanzania mpaka kesho.

Inastaajabisha na ni viroja pasi mfano,hao mashangingi wa shughuli kutukataza kumjadili huyo Nyerere kama vile sisi hakuwa Rais wetu!? Hawa watu maluuni saana.

Tena kama wana maarifa wampe shukran saana Sheikh Mohammed,maana najua anayo mengi lakini kahifadhi moyoni tu. Na haiingii akilini hata chembe ati watu tusimjadili Nyerere,mtu aloleta nakma na zilzala ziso mipaka hapo Tanzania na kwingineko.

Embu waambie wachungulie japo kiduchu,Biography ya JFK by Pro. Micheal O'Brien. Halafu waone huyu jamaa alivyomnyambua JFK,kuanzia Mababu na Mabibi zake woote tokea Ireland,mpaka kutaja makuwadi wake tangia Sec. School mpaka Hollywood. Kaoredhesha mpaka rangi za vichupi/bikinis walizokua wanavaa vimada wake!

Labda tafauti inakuja pale yakuwa; tamaduni za wenzetu na sisi pana khitilafa kubwa mno. Lakini tukifika hapa,itakua tunajibana soote hasa pale tunapotoa mifano mara kwa mara,na jamaa kuanza kulinganisha hapo Tanzania na nchi nyingine za ughaibuni na hasa watu na mataifa ya Magharibi. Na bila ya kufanza hivi,tutawezaje kuzungumzia History!?

Kwa kifupi,Sheikh Mohammed hakumtusi Nyerere ati kwa kusema alikua akisaidiwa kitoweo na nduguye Bwana Mshume Kiyate,hasha!

Halafu wanakuja hawa viwavi wa hoja,ati mara tunachanganya mada,mara tushawahi kujibu tuhuma za Nyerere,mara kafungueni thread nyingine. Hawaoni huyu kinyonga mwenzao anapoleta makhanatha ya hadthi za ugaidi na kutuumiza vichwa kwa kiswahili chake cha kujifunzia Secondary School. Mimi binafsi niliwahi kunena na kutahadharisha mambo kadhaa hapo awali,lakini nikaonekana mtoto wa Madrasa,halafu kajiunga only couple of weeks ago,atatwambia nini sisi mashangingi wa shughuli hii!!

Habari za Nyerere ni nyingi mno wala hazishi kwa hapa Jf hata siku moja.

Kama Jasusi ataamua kusema ukweli hapa jamvini,basi alete kisa cha Nyakyoma,Mohammed Enterprises. Hii kesi naijua kiundani na kiunagaubaga. Mzee wangu alishughulika nayo. Na kama patamwagwa vitu hapa,nami nitamwaga vitu halafu nitakupeni watu mkawaulize.

Nyerere alimshangaza saana Zacharia Maftah(former Director of Anti Corruption Squad),alipoamua ghafla kuhamisha file ya Nyakyoma ipelekwe kwa Abdallah Nungu(alikua Mwenyekiti wa Tume Ya Kudumu ya Uchunguzi Wa Viongozi). Alifanya kusudi kumuokoa nduguye Nyakyoma kwani alijua yakuwa Maftah ilikua anamfunga miaka mingi saana. Wakati Maftah anaifata ile file kwa Abdallah Nungu,ati anaambiwa file imeitwa State House na iko mikononi kwa Mwalimu. File inatoka kwa Nyerere tayari imenyofolewa makaratasi ushahidi takriban woote haumo. Huyo ndiye Nyerere. Matokeo yake akamzidshia utajiri uso kifani Mohammed Enterprises na kufa kwa Gapex maskini mpaka kesho!

Kwa wale wajuvi msokubali hoja za watu wa Madrasa,tafadhali kawaulizeni Joyce Shundi(Kamanda wa Takukuru Dar),Zacharia Maftah, Mzee Butiku au Timothy Apiyo na wengineo wengi walio sehemu nyeti za Serikali. Hawa woote nawajua na nawaheshimu vizuri mno ni Wakristo watiifu tu.

Nyerere alikua analazimisha kwa kibri na kuchukua meli ya kiraia ya Serikali Ya Mapinduzi Zanzibar,ili akamsaidie rafiki yake Samora dhidi ya Renamo pale Mozambique. Ile meli ilikua inabebeshwa silaha nyingi na za hatari,Wanajeshi na ndani yake kulikua na wafanyakazi wa kiraia wa kawaida kabisaa. Hawa wafanyakazi woote mpaka Captain walikua tu wanapewa taarifa masaa machache kabla ya safari na bila ya kufahamishwa destination mpaka wafike Dar port ndio wanashtukizwa. Hapa kama kuna wataalamu wa Maritime Insurances,pia mtashangaa hiyo meli ilikua inachukua cover ipi na hao wafanyakazi wa kiraia ndani yake walikua wako-covered kivipi!? Hiyo meli imenusurika mara kadhaa na mizinga ya Renamo.

Nyerere,alimstaajabisha mpaka Mzena(Usalama wa Taifa enzi ya Mwalimu),pale alipoamrisha IGP wake Hamza Aziz awekwe chini ya surveillance bila ya ushahidi au sheria yoyote. Ndio maana ile siku Hamza Aziz alipopata accident,alipokwenda kumuona Nyerere huku anajitafunatafuna,ndipo Nyerere alipomwambia Hamza kabla hujasema lolote fungua hiyo bahasha hapo. Ndani ya ile bahasha palikua na photographic evidence,inamounyesha sura halisi ya Hamza Aziz,gari yake na mpaka plate numbers. Picha ile ilipigwa na Mzungu mmoja ati alikua akifanya kazi pale BP - Kurasini!?

Kwa masuala haya muulizeni Mzena mwenyewe kama yuhai. Mkitaka zaidi nitakupeni majina ya watu makhusus tena Wakristo wenzenu mkaulize.

Kuna jamaa mmoja hapa,nae alikuja na hoja yake mbuzi kutaka kuonyesha ati "vitimbi" vya Sheikh Yahya Hussein. Kuna mengi saana pita kiasi...lakini chukua hii tu kiduchu.

Sheikh Yahya Hussein,alishughulika saana kumsaidia Nyerere kuzima lile jaribio la mapinduzi la 1982. Sheikh Yahya Hussein alitumia saana influence na connections zake kwa Sheikh Abdallah Saleh Al Farsy, Kenyatta,Moi,Njonjo,Usalama wa Taifa wa Kenya na wengineo wengi mno pale Kenya ili kuleta habari huku na kule na pia kuwakamata na kuwarejesha nchini baadhi ya watuhumiwa. Na kuna vitu vingi mno in between vilikua vinafanyika. Ukitaka zaidi nitakufungulia kwa undani,halafu nitakuonyesha udhaifu,Ukabila na roho mbaya ya Nyerere uko wapi.

Halafu,anakuja yule Mrema, mtu mgeni kabisa wa politics za Mzizima na Kariakoo kumkamata Sheikh Yahya Hussein bila ya jambo lolote la maana. Mpaka Lawrence Gama(former DG Usalama wa Taifa na nyadhifa nyingine nyingi tu hapo Tz,pia Jasusi ataeleza alimuoa nani ndani ya family ya Nyerere),alisikitika saana upumbavu wa Mrema kuingilia vitu alivyokua havijui. Kumbe Mrema alikua hajui maskini yakuwa anamfanyia Kitwana Kondo kazi yake,ambae wakati huo ndio alikua Rais wa nchi kuliko huyo Mwinyi mwenyewe. Kitwana Kondo alinyang'wanya mke na Sheikh Yahya Hussein during 60's.

Hizi habari kwa undani muulizeni Dominick Gama au Sinde Warioba. Maana nasikia Mzee Gama Lawrence amefariki. Na kwa wale wa Chadema,kamuulizeni Mabere Marando na atakufahamisheni yeye wakati huo alikua nani!? Au Shahidi X...Mzee Maige!

Kwa hiyo msione watu tumekaa kimya,ati mkafikiri tumevamia tu hili jamvi au hatujui mambo au huyo Nyerere wenu hatumjui au mambo nyeti takriban yoote, ati kwa sababu tu ni watoto wa Mdarasa. Tunafanya staha tu kiduchu. Kwa sababu wengi hawa ni Wazee wetu kama anavyosema Sheikh Mohammed Said. Hiyo nchi sisi wengine ni haki yetu na tuna uchungu nayo kupita hivyo mnavyohisi.




Ahsanta.

Cc: The Big Show

Gombesugu; Hii article ni nzuri sana. Una kipaji cha kujieleza and i love it. Nimeitwanga "like" Keep it up.
 
Duuh,
Umenikumbusha mbali. Mick Jagger and the Rolling Stones. I was Mick Jagger pale Aga Khan.
Ndiyo watafute akina Esta na Pati Mzena nadhani bado wapo hapo Dar. Msiba ulikuwa wiki iliyopita.

Jasusi,
Nitawatafuta kuwapa pole.

Oh...hearthrobs!
Hahahahahahaha...
 
Sheikh Mohammed,

Asalaam Alaykum Al Akhiy.

Nipokelea bayana yangu hii dhaifu kwako.

Nimekufahamu na nimesikitika. Hawa jamaa kila tunapowaambia kuwa hawa watu woote sisi ni Wazee wetu,nafikiri hawafahamu asilan kuwa tunamaanisha nini.

Ndo maana mimi tangia nilipongia nalikubali kuwa chini yako ili nikusikive kwa utuvu na nitape Ilm. Nikaonekana ati ni Mfuasi wa Madrasa sitaki kutumia maarifa na wala "Historia ya Tanzania" ati siijui!?ahaha!!

Kuna wakti ulizungumzia na kujiuliza Zohal gani ilowasibu hawa jamaa. Sina hakika lakini najua pana ile "Zohal Sumaku" ambayo ni mughali kukutoka ikishaganda. Au pia pana "Kisirani Shida",nayo pia ni bahri nyingine.

Leo nasafiri nakwenda pale Westerplatte Danzig(najua unaijua kwa uzuri historia ya pahala hapa,hasa kunako wiki ya mwanzo ya WWII),kwa weekend na family hapa...Insha Allah tarejea siku ya Jumanne Penye uhai na majaaliwa.

Lile neno Shangingi,wala si neno baya wala si matusi asilan. Naona jamaa hapo limewakera lakini nishiwataka radhi. Hili neno asili yake khasa ni Wamasai. Ni neno la fahari kubwa kwa Wamasai kuitwa Sangiki...lakini Insha Allah tuyaache maana nayo pia ni bahri nyingine.

Nakutakia Kheir na fanaka na mapumziko mema ya W'end Insha Allah.



Ahsanta

Gombesugu,
Ahsante kwa yote.,
 
Nguruvi3,
Nakutumia bayana hii fupi kukwambia mie sikutukana na wala sikuzungumza "Kiarabu" asilan. Ni sawa vile mtu asojua mambo vizuri ati akamtuhumu Mwingereza kuwa katukana kwa kutumia ki-French au ki-Latin!?

Lakini napenda kuchukua fursa hii kwako binafsi, na wengineo nyoote mlojihisi dhuluma imekinza mioyoni mwenu kutokana na ile bayana yangu. Labda nilikua na muhma wala si hamaki asilan,na ndo udhaifu wa kibinadamu.

Kuhusu hiyo "ajali",nisingependa tuirudie tena...kwa sababu kadhaa na hishma ya wahusika ambao mimi ni watu wangu wa karibu. Lakini kama utatumia fikra,usomi ulonao na mantiki na pia kuondoa Udini na Ukabila;basi ni muhimu saana ujiulize. Hivi ni kwanini Nyerere aliamua kumuweka chini ya Surveillance IGP wake mwenyewe takriban kwa miaka kadhaa. Bila ya huyo IGP kushukiwa au kufanza lolote baya,na bila ya kufuata ushauri wa Marehemu Mzee Mzena ambae alipinga saana jambo lile!? Mzena alimfahamisha Nyerere implications na consequences za jambo hilo,na je IGP akipata fununu itakuwaje na tutatoa justification gani!? Vipengele vya Sharia vilipoletwa,Nyerere hakutaka kabisa kusikia. Bahati nzuri kwa Nyerere,IGP hakujua hii kitu mpaka siku ile alipopatwa na "ajali" na kwenda kukutana na Nyerere na baada yake ndio akagundua "tambara" zima. Tuwache haya mambo tafadhali,huwezi jua jinsi Mzee Mzena na Hamza Aziz walivyokua kikaribu na kuheshimiana kikazi. Lakini baada ya haya kutokea palikua na friction na indifference kubwa baina yao...pia iliathiri "makundi fulani" ndani ya Idara zao. "Funika Kombe Mwanaharasha apite"...wewe ni mtu mzima tuyaache haya mambo,hao woote ni Wazee wetu soote ok!

Msalimie Mag3,natumai nae pia amenisamehe kwa kile "Kiarabu" cha kwenye bayana.
Ahsanta.

Gombesugu,
Huwezi kujua mapenzi ya Hamza Aziz kwangu.

Sote tumezaliwa Kipata na sote tukipenda muziki
wa Nat King Cole.

Juu ya tofauti wa umri wetu tukizungumza as equals.

Akinitania kwa mke wangu, "Mohamed you have taste
for good looking ladies..."

Nami huwa simwachi namjibu namwambia, "I have picked
that from you!"

Tena akinitania hivi mbele ya binti zake kwenye diner table.

Akiwa na jambo zito tunakwenda kwenye majlis yake pwani
tunaangalia bahari.

Kwenye kibanda kile ndipo Hamza Aziz alikuwa anafunguka khasa.

Sasa baadae nikajajua kwa nini tukiwa ndani ni maskhara na tukiwa
majlis ni serious business.

Ndani mwake nahisi alikuwa na hofu ya bugs.
Sasa baada ya kukusoma ndiyo inanijia wazi kabisa.

Ikajanipitikia kuwa Hamza Aziz alikuwa anataka niyajue baadhi ya mambo
asije kwenda nayo kaburini.

Hiyo bugging kanipa mkanda mzima lakini siyo hiyo album yako....
Nimeburudika pia na showdown yake ndani ya Halmashauri Kuu ya TANU...
Akanambia yote chanzo ilikuwa yeye kukataa kumkamata Sheikh Hassan
bin Amir.

Nina mengi...
Hawa ndugu zetu ni wageni katika mambo haya.

Hao walikuwa wazee wetu walioipigania nchi hii kuitoa mikononi mwa Waingereza.
 
Mzee Ms, baada ya Salaam. Nashukuru kwa maneno mazuri. Haya ya kina Babu na Wazenj na Mapinduzi mimi wala siyazungumzi (angalau kwa leo). Infact moja ya kitu nachotamani kitokeze kwenye tume ya kina Waryoba ni kuwa tupige kura ya kubaki au tusibaki na muungano na kama tunabaki nao uwe ni upi. Sioni taabu kukuambia ikitokea fursa hiyo, mimi ni mmoja wa watakaopiga kura ya kuuvunja. Kikubwa ni kuwa i would rather live alone rather than with a bitter and unhappy neighbor. The sooner mabwana hawa wakipewa chao nitashukuru. Then they can fulfill their "tarnished" dreams. Mimi nasubiri fursa ya kura. Kuhusu suala la wewe kuandika issues za Sheikh na Nyerere lazima niwe mkweli sijasoma umeandika nini. Lakini tangu ukomae na ukatoliki wake, then kuhamia kwenye Kupishwa chumba alae na Ally, then Nyerere kukopa hela za mboga kama part ya "struggle against the British colonialism" i will seriously treat your coverage on him with caution. And you can easily see why. Shukran.

Wickama,
Ni bahati mbaya na sijui kwa nini umeumizwa na stori
hii ya Kariakoo na Nyerere kulala chumba cha Abbas.

Hii ndiyo ilikuwa ghera ya TANU...

Hapo Kariakoo Nyerere anakwenda kwa Market Master
Abdu Sykes na Abdu kapu anamkabidhi Mzee Abdallah
aliyekuwa mesenja pale.

Dakika kumi kapu lishatakata.

Najua ni ugeni wa kujua mila za wazee wetu ndiyo unahisi
labda Nyerere kadhalilika.

Soma kitabu changu kisa hiki kakieleza Nyerere mwenyewe
katika kuwasifu wazee wangu.

Pole sana kama nimekuumiza.
Haikuwa nia yangu.
 
Ritz,

Salaam. Nakufahamu na nakusikiza kwa yakin. Mimi najua mengi mno wala sitie shaka. Andrew Nyerere,ni rafiki mkubwa wa Mzazi wangu,nafikiri niliwahi kusema hapo awali.

Huyo jamaa ni psychological fragile,angalia tu ile mada yake halafu ameweka Sheikh Issa Bin Ameir badala ya Sheikh Hassan Bin Ameir...kama kwenye legal technicalities basi Barrister mahiri anakwambia Case dismiss!

Hapa kilichobaki kwa ufupi ni kurembeana fedhuli na kibri kingi tu,labda zaidi wanatumia udhalimu wao wa kumuuliza makhanatha Sheikh Mohammed ili wamuumize kichwa.

Takriban yoote alozungumzia Zali la Mentali a.k.a Mchimba Chumvi,ndo yale yale alokua anadarsisha Sheikh Mohammed takriban miezi minne. Tafauti yeye Zali la Mentali kawaendesha kindava na kimchakamchaka wa nguvu,ndo maana unaona kijasho chembamba kinawabubujika.

Yule kunguni wa hoja a.k.a Abu Jahal,mimi pia nilimtoa maanani kitambo pale alipoleta ule uTarime/Ukabila wake,na ati kujaribu kumtetea Nyerere tena kwa kutumia Khadith na Qur'aan tukufu. Yule Kunguni Wallahi ni Khabith Al maar.

Nyerere aliwahi kufanza mema kiduchu,lakini dhahma wa min'karadas,dhuluma na madhila aloleta ni mengi mno pita kiasi na yanawasulubu watu wengi mno hapo Tanzania mpaka kesho.

Inastaajabisha na ni viroja pasi mfano,hao mashangingi wa shughuli kutukataza kumjadili huyo Nyerere kama vile sisi hakuwa Rais wetu!? Hawa watu maluuni saana.

Tena kama wana maarifa wampe shukran saana Sheikh Mohammed,maana najua anayo mengi lakini kahifadhi moyoni tu. Na haiingii akilini hata chembe ati watu tusimjadili Nyerere,mtu aloleta nakma na zilzala ziso mipaka hapo Tanzania na kwingineko.

Embu waambie wachungulie japo kiduchu,Biography ya JFK by Pro. Micheal O'Brien. Halafu waone huyu jamaa alivyomnyambua JFK,kuanzia Mababu na Mabibi zake woote tokea Ireland,mpaka kutaja makuwadi wake tangia Sec. School mpaka Hollywood. Kaoredhesha mpaka rangi za vichupi/bikinis walizokua wanavaa vimada wake!

Labda tafauti inakuja pale yakuwa; tamaduni za wenzetu na sisi pana khitilafa kubwa mno. Lakini tukifika hapa,itakua tunajibana soote hasa pale tunapotoa mifano mara kwa mara,na jamaa kuanza kulinganisha hapo Tanzania na nchi nyingine za ughaibuni na hasa watu na mataifa ya Magharibi. Na bila ya kufanza hivi,tutawezaje kuzungumzia History!?

Kwa kifupi,Sheikh Mohammed hakumtusi Nyerere ati kwa kusema alikua akisaidiwa kitoweo na nduguye Bwana Mshume Kiyate,hasha!

Halafu wanakuja hawa viwavi wa hoja,ati mara tunachanganya mada,mara tushawahi kujibu tuhuma za Nyerere,mara kafungueni thread nyingine. Hawaoni huyu kinyonga mwenzao anapoleta makhanatha ya hadthi za ugaidi na kutuumiza vichwa kwa kiswahili chake cha kujifunzia Secondary School. Mimi binafsi niliwahi kunena na kutahadharisha mambo kadhaa hapo awali,lakini nikaonekana mtoto wa Madrasa,halafu kajiunga only couple of weeks ago,atatwambia nini sisi mashangingi wa shughuli hii!!

Habari za Nyerere ni nyingi mno wala hazishi kwa hapa Jf hata siku moja.

Kama Jasusi ataamua kusema ukweli hapa jamvini,basi alete kisa cha Nyakyoma,Mohammed Enterprises. Hii kesi naijua kiundani na kiunagaubaga. Mzee wangu alishughulika nayo. Na kama patamwagwa vitu hapa,nami nitamwaga vitu halafu nitakupeni watu mkawaulize.

Nyerere alimshangaza saana Zacharia Maftah(former Director of Anti Corruption Squad),alipoamua ghafla kuhamisha file ya Nyakyoma ipelekwe kwa Abdallah Nungu(alikua Mwenyekiti wa Tume Ya Kudumu ya Uchunguzi Wa Viongozi). Alifanya kusudi kumuokoa nduguye Nyakyoma kwani alijua yakuwa Maftah ilikua anamfunga miaka mingi saana. Wakati Maftah anaifata ile file kwa Abdallah Nungu,ati anaambiwa file imeitwa State House na iko mikononi kwa Mwalimu. File inatoka kwa Nyerere tayari imenyofolewa makaratasi ushahidi takriban woote haumo. Huyo ndiye Nyerere. Matokeo yake akamzidshia utajiri uso kifani Mohammed Enterprises na kufa kwa Gapex maskini mpaka kesho!

Kwa wale wajuvi msokubali hoja za watu wa Madrasa,tafadhali kawaulizeni Joyce Shundi(Kamanda wa Takukuru Dar),Zacharia Maftah, Mzee Butiku au Timothy Apiyo na wengineo wengi walio sehemu nyeti za Serikali. Hawa woote nawajua na nawaheshimu vizuri mno ni Wakristo watiifu tu.

Nyerere alikua analazimisha kwa kibri na kuchukua meli ya kiraia ya Serikali Ya Mapinduzi Zanzibar,ili akamsaidie rafiki yake Samora dhidi ya Renamo pale Mozambique. Ile meli ilikua inabebeshwa silaha nyingi na za hatari,Wanajeshi na ndani yake kulikua na wafanyakazi wa kiraia wa kawaida kabisaa. Hawa wafanyakazi woote mpaka Captain walikua tu wanapewa taarifa masaa machache kabla ya safari na bila ya kufahamishwa destination mpaka wafike Dar port ndio wanashtukizwa. Hapa kama kuna wataalamu wa Maritime Insurances,pia mtashangaa hiyo meli ilikua inachukua cover ipi na hao wafanyakazi wa kiraia ndani yake walikua wako-covered kivipi!? Hiyo meli imenusurika mara kadhaa na mizinga ya Renamo.

Nyerere,alimstaajabisha mpaka Mzena(Usalama wa Taifa enzi ya Mwalimu),pale alipoamrisha IGP wake Hamza Aziz awekwe chini ya surveillance bila ya ushahidi au sheria yoyote. Ndio maana ile siku Hamza Aziz alipopata accident,alipokwenda kumuona Nyerere huku anajitafunatafuna,ndipo Nyerere alipomwambia Hamza kabla hujasema lolote fungua hiyo bahasha hapo. Ndani ya ile bahasha palikua na photographic evidence,inamounyesha sura halisi ya Hamza Aziz,gari yake na mpaka plate numbers. Picha ile ilipigwa na Mzungu mmoja ati alikua akifanya kazi pale BP - Kurasini!?

Kwa masuala haya muulizeni Mzena mwenyewe kama yuhai. Mkitaka zaidi nitakupeni majina ya watu makhusus tena Wakristo wenzenu mkaulize.

Kuna jamaa mmoja hapa,nae alikuja na hoja yake mbuzi kutaka kuonyesha ati "vitimbi" vya Sheikh Yahya Hussein. Kuna mengi saana pita kiasi...lakini chukua hii tu kiduchu.

Sheikh Yahya Hussein,alishughulika saana kumsaidia Nyerere kuzima lile jaribio la mapinduzi la 1982. Sheikh Yahya Hussein alitumia saana influence na connections zake kwa Sheikh Abdallah Saleh Al Farsy, Kenyatta,Moi,Njonjo,Usalama wa Taifa wa Kenya na wengineo wengi mno pale Kenya ili kuleta habari huku na kule na pia kuwakamata na kuwarejesha nchini baadhi ya watuhumiwa. Na kuna vitu vingi mno in between vilikua vinafanyika. Ukitaka zaidi nitakufungulia kwa undani,halafu nitakuonyesha udhaifu,Ukabila na roho mbaya ya Nyerere uko wapi.

Halafu,anakuja yule Mrema, mtu mgeni kabisa wa politics za Mzizima na Kariakoo kumkamata Sheikh Yahya Hussein bila ya jambo lolote la maana. Mpaka Lawrence Gama(former DG Usalama wa Taifa na nyadhifa nyingine nyingi tu hapo Tz,pia Jasusi ataeleza alimuoa nani ndani ya family ya Nyerere),alisikitika saana upumbavu wa Mrema kuingilia vitu alivyokua havijui. Kumbe Mrema alikua hajui maskini yakuwa anamfanyia Kitwana Kondo kazi yake,ambae wakati huo ndio alikua Rais wa nchi kuliko huyo Mwinyi mwenyewe. Kitwana Kondo alinyang'wanya mke na Sheikh Yahya Hussein during 60's.

Hizi habari kwa undani muulizeni Dominick Gama au Sinde Warioba. Maana nasikia Mzee Gama Lawrence amefariki. Na kwa wale wa Chadema,kamuulizeni Mabere Marando na atakufahamisheni yeye wakati huo alikua nani!? Au Shahidi X...Mzee Maige!

Kwa hiyo msione watu tumekaa kimya,ati mkafikiri tumevamia tu hili jamvi au hatujui mambo au huyo Nyerere wenu hatumjui au mambo nyeti takriban yoote, ati kwa sababu tu ni watoto wa Mdarasa. Tunafanya staha tu kiduchu. Kwa sababu wengi hawa ni Wazee wetu kama anavyosema Sheikh Mohammed Said. Hiyo nchi sisi wengine ni haki yetu na tuna uchungu nayo kupita hivyo mnavyohisi.




Ahsanta.

Cc: The Big Show
GOmgesugu,

..hebu tuliza munkari.

..siyo vizuri kutoa kauli za hasira namna hiyo.

..pamoja na hayo, kuna mambo umeyaandika hapo ningependa ufunguke zaidi.

..haswa suala la Hamza Aziz[r.i.p], Shekhe Yahya, Kitwana Kondo, Nyakyoma, na Mohamed Enterprise.

..kuna mahali unadai Kitwana Kondo alikuwa na nguvu kuliko Raisi Mwinyi!! WHAAAT!!?? R U KIDDING ME!!?

NB:

..kuhusu suala la meli ya SMZ kutumika kwa shughuli za KIJESHI, naomba uzingatie kwamba ULINZI na USALAMA ni masuala ya MUUNGANO.

..zaidi, naomba nitahadharishe kwamba Samora Machel hakuwa mkatoliki, bali Wareno aliokuwa akipigana nao ndiyo majority Wakatoliki. pia uzingatie kwamba Wareno walikuwa sehemu ya NATO.

..Umemlaumu Mwalimu Nyerere kwa kumsaidia Samora Machel. Je, una mtizamo gani kuhusu Raisi Mwinyi kumsaidia Joaquim Chissano baada ya Samora kuuwawa??

cc: Nguruvi3, Jasusi, Wickama
 
Last edited by a moderator:
GOmgesugu,

..hebu tuliza munkari.

..siyo vizuri kutoa kauli za hasira namna hiyo.

..pamoja na hayo, kuna mambo umeyaandika hapo ningependa ufunguke zaidi.

..haswa suala la Hamza Aziz[r.i.p], Shekhe Yahya, Kitwana Kondo, Nyakyoma, na Mohamed Enterprise.

..kuna mahali unadai Kitwana Kondo alikuwa na nguvu kuliko Raisi Mwinyi!! WHAAAT!!?? R U KIDDING ME!!?

NB:

..kuhusu suala la meli ya SMZ kutumika kwa shughuli za KIJESHI, naomba uzingatie kwamba ULINZI na USALAMA ni masuala ya MUUNGANO.

..zaidi, naomba nitahadharishe kwamba Samora Machel hakuwa mkatoliki, bali Wareno aliokuwa akipigana nao ndiyo majority Wakatoliki. pia uzingatie kwamba Wareno walikuwa sehemu ya NATO.

..Umemlaumu Mwalimu Nyerere kwa kumsaidia Samora Machel. Je, una mtizamo gani kuhusu Raisi Mwinyi kumsaidia Joaquim Chissano baada ya Samora kuuwawa??

cc: Nguruvi3, Jasusi, Wickama

jokaKuu,'
Hii ya Kitwana Kondo kuwa na ushawishi mkubwa ndani ya serikali ya Mwinyi ni kweli kabisa. Mzee Bomani aliwahi kulalamika kuwa baraza la mawaziri lilikuwa likipitisha uamuzi lakini baada ya Kitwana Kondo kukutana na Mwinyi wanasikia yanayotangazwa na RTD ni tofauti na yale waliyokubaliana.
 
Wickama,
Ni bahati mbaya na sijui kwa nini umeumizwa na stori
hii ya Kariakoo na Nyerere kulala chumba cha Abbas.

Hii ndiyo ilikuwa ghera ya TANU...

Hapo Kariakoo Nyerere anakwenda kwa Market Master
Abdu Sykes na Abdu kapu anamkabidhi Mzee Abdallah
aliyekuwa mesenja pale.

Dakika kumi kapu lishatakata.

Najua ni ugeni wa kujua mila za wazee wetu ndiyo unahisi
labda Nyerere kadhalilika.

Soma kitabu changu kisa hiki kakieleza Nyerere mwenyewe
katika kuwasifu wazee wangu.

Pole sana kama nimekuumiza.
Haikuwa nia yangu.

Heshima yako. Ni kwamba nimeongelea hadithi kutoendana na objective ya unacholenga kueleza. Kama Kitabu ni "Jitahada ya Wamakonde kukuza zao Mkonge" i believe heroes wako utawaelezea hata wakikopa hela wapanue mashamba ya mkonge. Ikija kuwa wanaonekana wanakopa ili wanywee pombe, then naona kama kuna mismatch ya objective na narration. Kwa Nyerere na mwenyeji wake Sykes, similarly i would not hesitate kuipokea kama ni sehemu ya struggle ya wabongo kumpinga Mkoloni katika mtindo wa kuwa yeye na Sykes au na yeyote walivumulia kama haya (including ......visa kama hivyo vya masokoni) kama sehemu ya barabara yao kuendea lengo lao la kukomboa nchi. Lakini i dont find that spirit in the narration. Hapa lazima nikubali kuwa kila jamii ina mtazamo wake tofauti na inategemea kila mtu kazoea nini. Binafsi it is an area ambayo i do not suffer in the least as Wickama. Naongelea "stance" ya reporting. Huenda wala huihitaji nachosema in view kuwa hatufanyi review ya kitabu hapa.
 
jokaKuu,'
Hii ya Kitwana Kondo kuwa na ushawishi mkubwa ndani ya serikali ya Mwinyi ni kweli kabisa. Mzee Bomani aliwahi kulalamika kuwa baraza la mawaziri lilikuwa likipitisha uamuzi lakini baada ya Kitwana Kondo kukutana na Mwinyi wanasikia yanayotangazwa na RTD ni tofauti na yale waliyokubaliana.

Jasusi
Mbona picha niliyoipata kutoka kwenye simulizi za Mohamed Said ilikuwa kama vile maamuzi ya Rais Mwinyi yalikuwa yakifuata "alichotaka" mkatoliki Nyerere? Au hata Mzee Kitwana Kondo naye alikuwa mkatoliki?!¿¡?
 
Last edited by a moderator:
GOmgesugu,

..hebu tuliza munkari.

..siyo vizuri kutoa kauli za hasira namna hiyo.

..pamoja na hayo, kuna mambo umeyaandika hapo ningependa ufunguke zaidi.

..haswa suala la Hamza Aziz[r.i.p], Shekhe Yahya, Kitwana Kondo, Nyakyoma, na Mohamed Enterprise.

..kuna mahali unadai Kitwana Kondo alikuwa na nguvu kuliko Raisi Mwinyi!! WHAAAT!!?? R U KIDDING ME!!?

NB:

..kuhusu suala la meli ya SMZ kutumika kwa shughuli za KIJESHI, naomba uzingatie kwamba ULINZI na USALAMA ni masuala ya MUUNGANO.

..zaidi, naomba nitahadharishe kwamba Samora Machel hakuwa mkatoliki, bali Wareno aliokuwa akipigana nao ndiyo majority Wakatoliki. pia uzingatie kwamba Wareno walikuwa sehemu ya NATO.

..Umemlaumu Mwalimu Nyerere kwa kumsaidia Samora Machel. Je, una mtizamo gani kuhusu Raisi Mwinyi kumsaidia Joaquim Chissano baada ya Samora kuuwawa??

cc: Nguruvi3, Jasusi, Wickama

Hapa niwe mkweli 100%. Kama unatoka Tarime as i do, which i have noticed is an irritation to some, it is unwise to contribute here. Good Luck.
 
Last edited by a moderator:
Jasusi
Mbona picha niliyoipata kutoka kwenye simulizi za Mohamed Said ilikuwa kama vile maamuzi ya Rais Mwinyi yalikuwa yakifuata "alichotaka" mkatoliki Nyerere? Au hata Mzee Kitwana Kondo naye alikuwa mkatoliki?!¿¡?

Now you are talking. We need proof Kitwana Kondo was not Catholic.
 
Last edited by a moderator:
GOmgesugu,

..hebu tuliza munkari.

..siyo vizuri kutoa kauli za hasira namna hiyo.

..pamoja na hayo, kuna mambo umeyaandika hapo ningependa ufunguke zaidi.

..haswa suala la Hamza Aziz[r.i.p], Shekhe Yahya, Kitwana Kondo, Nyakyoma, na Mohamed Enterprise.

..kuna mahali unadai Kitwana Kondo alikuwa na nguvu kuliko Raisi Mwinyi!! WHAAAT!!?? R U KIDDING ME!!?

NB:

..kuhusu suala la meli ya SMZ kutumika kwa shughuli za KIJESHI, naomba uzingatie kwamba ULINZI na USALAMA ni masuala ya MUUNGANO.

..zaidi, naomba nitahadharishe kwamba Samora Machel hakuwa mkatoliki, bali Wareno aliokuwa akipigana nao ndiyo majority Wakatoliki. pia uzingatie kwamba Wareno walikuwa sehemu ya NATO.

..Umemlaumu Mwalimu Nyerere kwa kumsaidia Samora Machel. Je, una mtizamo gani kuhusu Raisi Mwinyi kumsaidia Joaquim Chissano baada ya Samora kuuwawa??

cc: Nguruvi3, Jasusi, Wickama

Jokakuu; kuna mahali naweza pata reference ya chochote hapo juu? Sounds like good stuff
 
Last edited by a moderator:
Now you are talking. We need proof Kitwana Kondo was not Catholic.
Unajua hadithi za kusimuliwa na kuumba umba zina matatizo sana. Gombesugu anadai Kitwana Kondo alikuwa na nguvu zaidi ya rais Mwinyi. Mohamed anasema Nyerere alikuwa anaongoza kwa remote na Mwinyi alikuwa hana ''say''.
Baadhi ya waislam wanasema ni ngumu sana kuvunja mfumokristo kwasababu wakristo wameushika. Gombesugu anathibitisha kuwa Kitwana Kondo ndiye alikuwa na Serikali.

Njozi anamsifu Kitwana Kondo kusimama kidete kutetea waislam. Mohamed anasema CCM ilimsusa akapoteza ubunge kwa msimamo wake wa mambo ya dini. Gombesugu anasema kulikuwa na Ugomvi na Sheikh Yahya kuhusu mabinti enzi hizo.Mohamed anasema walinong'onezana kuichagua CCM iliyomtosa Kitwana Kondo.

It's all confusing huwezi kujua nani anasema nini kwasababu story zinabadilika with time and kind of conversation.

Ndio maana huwaita ''half baked wasomi'' kwasababu nao wameingia katika mkumbo wa hadithi za vijiweni like any othe illiterate in the street.
 
Hapa niwe mkweli 100%. Kama unatoka Tarime as i do, which i have noticed is an irritation to some, it is unwise to contribute here. Good Luck.

..sasa unakuwa unawapa nguvu wale wanaougua ubaguzi na udini.

..mimi watu wa namna hiyo huwa nawalipizia heshima na lugha ya staha.
 
Ndio maana huwaita ''half baked wasomi'' kwasababu nao wameingia katika mkumbo wa hadithi za vijiweni like any othe illiterate in the street.

Nguruvi kweli umetuchoka anyway sikukatalii ni mtazamo wako labda kwasababu sisi ni watu wa madrasa kwasababu kwenu mtu akisoma madrasa ni mjinga sanaaa dah safari ni ndefu
 
Heshima yako. Ni kwamba nimeongelea hadithi kutoendana na objective ya unacholenga kueleza. Kama Kitabu ni "Jitahada ya Wamakonde kukuza zao Mkonge" i believe heroes wako utawaelezea hata wakikopa hela wapanue mashamba ya mkonge. Ikija kuwa wanaonekana wanakopa ili wanywee pombe, then naona kama kuna mismatch ya objective na narration. Kwa Nyerere na mwenyeji wake Sykes, similarly i would not hesitate kuipokea kama ni sehemu ya struggle ya wabongo kumpinga Mkoloni katika mtindo wa kuwa yeye na Sykes au na yeyote walivumulia kama haya (including ......visa kama hivyo vya masokoni) kama sehemu ya barabara yao kuendea lengo lao la kukomboa nchi. Lakini i dont find that spirit in the narration. Hapa lazima nikubali kuwa kila jamii ina mtazamo wake tofauti na inategemea kila mtu kazoea nini. Binafsi it is an area ambayo i do not suffer in the least as Wickama. Naongelea "stance" ya reporting. Huenda wala huihitaji nachosema in view kuwa hatufanyi review ya kitabu hapa.

Wickama,
Nimekuelewa.

Lugha inashabihiana na utamaduni.
Kuna wakati nilikuwa natumia usafiri wa ofisi na jamaa ofisini.

Hawa jamaa wote wanatoka bara.

Tunapita Kariakoo.
Nawaona jamaa zangu.

Katika mila zetu aliyepanda chombo ndiye aula zaidi kutoa salamu.
Mimi nikifanya hivyo lakini kwa sauti ya juu kidogo.

Nasema, ''Abdallah Hashim Asalaam Aleikum.''

Hawa jamaa zangu wananiuliza (wamekereka kidogo) ''Why are you
shouting?''

Nami nawajibu, ''I am not shouting that is how we salute each other
short of that I would be considered snobbish.''

Hawaelewi.

Basi mie nikawa nawaambia, ''Nyie maadam mmekuja kuishi huku kwetu
lazima mjifunze na mila zetu.''

Walikuwa hawapendi wakichomwa sana na maneno yangu na katika wale
wengine ni wakubwa zangu katika kazi.

Juu ya hayo mie si mtu wa kujidhalilisha na walikuwa wakisema sana nawapa
hii nawaambia, ''Haya ni mafunzo katufunza Mtume SAW.''

Ilikuwa raha sana.
Hawa jamaa hawatanisahau.

Walikuwa wakati mwingine wakisema, ''Mohamed sisi hatujapatapo kukutana na
Mswahili wa aina yako.''

Sasa sijui ile ilikuwa ''compliment'' au nini.

Wickama,
Mimi nimekuelewa na mimi nakuomba unielewe.
 
Back
Top Bottom