GOmgesugu,
..hebu tuliza munkari.
..siyo vizuri kutoa kauli za hasira namna hiyo.
..pamoja na hayo, kuna mambo umeyaandika hapo ningependa ufunguke zaidi.
..haswa suala la Hamza Aziz[r.i.p], Shekhe Yahya, Kitwana Kondo, Nyakyoma, na Mohamed Enterprise.
..kuna mahali unadai Kitwana Kondo alikuwa na nguvu kuliko Raisi Mwinyi!! WHAAAT!!?? R U KIDDING ME!!?
NB:
..kuhusu suala la meli ya SMZ kutumika kwa shughuli za KIJESHI, naomba uzingatie kwamba ULINZI na USALAMA ni masuala ya MUUNGANO.
..zaidi, naomba nitahadharishe kwamba Samora Machel hakuwa mkatoliki, bali Wareno aliokuwa akipigana nao ndiyo majority Wakatoliki. pia uzingatie kwamba Wareno walikuwa sehemu ya NATO.
..Umemlaumu Mwalimu Nyerere kwa kumsaidia Samora Machel. Je, una mtizamo gani kuhusu Raisi Mwinyi kumsaidia Joaquim Chissano baada ya Samora kuuwawa??
cc:
Nguruvi3,
Jasusi,
Wickama
JokaKuu,
I can confirm without knowing you and where you are /your location that,you know nothing about the Government inner workings and its system.
Una maana ipi unaposema "nifunguke zaidi"!? Haya kwetu ni matusi yaso kiasi ndugu yangu. Au ndo
Kiswahili cha kisasa na cha mjini!?
Masuala ya
Nyakyoma na Mohammed Enterprises,tayari nilishamalizana na
Jasusi(ambaye kwa sababu mzijuazo wenyewe ndie mnaemuamini zaidi kuliko mimi wa Madrassa).
Pia lile suala la
Mzee KK ,Jasusi alitumia ustaarabu na kuniepushia
Premier League na nyinyi.
Jasusi amekuthibitishia tena akakupa na mfano wa matamshi ya
Mzee Paul Bomani.
Inaelekea umevamia hoja zangu kwa pupa. Hayo mambo ya Meli ya
SMZ mbona nilikupa kiduchu tu. Nina mengi saana. Pale nilikua tu naonyesha ukaidi wa
Nyerere kiduchu tu kwa kutokufuata kwake
Sharia/Ushauri,kama ulipata wasaa wa kuangalia zile points zangu kwa kina!?
Habari za
Mozambique,nakusihi fanya sabra tuimalize shughuli hii. Halafu nikupe darsa,nitakuanzia tangia kifo cha
Eduardo Mondlane pale
D'Salaam,Internal struggle na mtafaruku ndani ya
Frelimo,kuhusishwa kwa
Nyerere kwenye kifo cha Mondlane,ukaribu na prefference/choice ya Nyerere kwa
Samora Machel,unyama na ushenzi uso mfano ulofanywa na
Majeshi ya Tanzania dhidi ya wananchi na raia wasio na hatia wa
Mozambique,
mkono wa Nyerere/influence na jinsi alivyosababisha
RENAMO na FRELIMO kuendeleza vita na khitilafu baina yao na mengineyo mengi.
Nina picha nipo pale
Estadio da Machava formerly known as Estadio Salazar 1975. Wanajamvi,niwieni radhi ningeiweka hapa lakini ni
group photograph na wahusika wengine itakua si busara asilan kuwaanika hapa.
Ile habari ya
sheikh Yahya Hussein uliyoitaka ni ndefu mno na mambo ni mengi saana. Ule ulikua ni mfano tu wa hoja. Nakuongezea tena kiduchu. Sheikh Yahya Hussein,ni mmojawapo wa Watanzania wachache mno,waliokua wanamsaidia
Nyerere dhidi ya makaburu wa South Afrika ndani ya
South Afrika.
Sheikh Yahya Hussein, kwa kutumia
influence na connection yake kwa
King wa Swaziland,alifungua "
offices" ndani ya
South Afrika miji tafauti,
Lusaka na
London ili kuwasaidia
ANC kama alivyotaka na kuomba
Nyerere. Nafikiri wengi wenu mnakumbuka jinsi gani ilikua ni
risk kubwa mno kufanza mambo hayo wakati huo wa vikwazo dhidi ya Makaburu na kama je kama Makaburu wenyewe wangemgundua!?
Sheikh Yahya Hussein ni katika Watanzania wachache wakti huo alokua na passports za
UK,Swaziland,Kenya...na zoote hizo alipewa na
Marais/Wafalme wa nchi hizo mkononi mwake.
Kama unahitaji tena hizi "
habari za vinyozi wa Kipata na Mkunguni";nifahamishe nami tajaribu kutafuta fursa. Itanilazim siku nyingine nikuonyeshe kwanini nilisema
Nyerere alikosa fadhila au kumkumbuka
Sheikh Yahya Hussein!?
Ahsanta na tuendelee na mnakasha.