Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar

Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar

Wickama nakuwekea kipande hiki uweze tu kujua tulikoanzia na huyu Mohamed Said na ngano zake...

20th October 2011- Jaribio la mwanzo la Nyerere kutaka kuivunja EAMWS lilikuwa mwaka 1963. Lakini jaribio hilo halikufanikiwa kwa sababu ya mpango uliopangwa na Mufti Sheikh Hassan bin Amir na kutekelezwa na Bilali Rehani Waikela, katibu wa EAMWS Tabora. Mwaka huu wa 1963 EAMWS ilifanya mkutano wake katika ukumbi wa Shule ya wasichana ya Aga Khan. Wajumbe wa mkutano huo walipowasili mjini Dar es Salaam walikuta uvumi kuwa wajumbe wa mkutano wa EAMWS watakamatwa na kuwekwa kizuizini. Chanzo cha uvumi huu hakikufahamika lakini haikuwa vigumu kuhisi.

Baada ya kuvunjwa kwa Baraza la Wazee wa TANU mwaka ule ilikuwa wazi kuwa Nyerere alikuwa amewatupa mkono washirika wake wa zamani na sasa alikuwa akitafuta wapya ili kujenga upya msingi wake wa siasa. Kutokana na mambo yalivyokuwa yakienda ilikuwa ni dhahiri washirika wake wapya hawatakuwa Waislam.Katibu wa EAMWS Tabora, Waikela alipowasili Dar es Salaam kuhudhuria mkutano aliitwa na Sheikh Hassan bin Amir. Mufti Sheikh Hassan bin Amir mbele ya Mzee Ali Comorian, alimfahamisha Waikela kuwa kulikuwa na njama zilizokuwa zikipikwa na Nyerere kumuungamiza yeye na Tewa Said Tewa ili kuvunja EAMWS ipatikane nafasi ya kuanzishwa jumuiya ya Kiislam ya Watanganyika itakayokuwa chini ya wanafiki.

Sheikh Hassan bin Amir alimwambia Waikela kuwa harakati za uhuru zilikuwa zinatekwa nyara na Wakristo kwa manufaa ya makanisa yao. Sheikh Hassan alimfahamisha Waikela kuwa ni lazima yeye afanye kila linalowezekana ili njama za Nyerere zishindwe. Waikela alimuuliza Sheikh Hassan bin Amir kwa nini amechaguliwa yeye kufanya kazi ile. Sheikh Hassan bin Amir alimuambia kuwa yeye ana imani na uwezo wake. Baada ya maneno hayo Sheikh Hassan bin Amir alinyanyua mikono yake juu na kumuombea dua Waikela. Nyerere alikuwa anamfahamu Waikela kwa kuwa alikuwa muasisi wa TANU na alikuwa ametoa mchango mkubwa katika kupigania uhuru.Nchi nzima hasa sehemu za Waislam kulikuwa mpango wa serikali wa kuwavunja Waislam nguvu na kuwakatisha tamaa.

Waikela, kama ilivyokuwa kwa viongozi wengine wa EAMWS alikuwa anasuguana na Mkuu wa Mkoa wa Jimbo la Magharibi, Richard Wambura. Kulikuwa na ujeuri kwa upande wa serikali walipokuwa wanashugulikia matatizo ya Waislam, mbali na mategemeo ya Waislam waliyokuwanayo kabla ya uhuru. Subira ya Waikela ilifikia kikomo pale Wambura alipowatukana Waislam katika mkutano wa hadhara. Baada ya kuhutubia Wambura, Waikela alipanda jukwaani na akaikumbusha serikali isiwe mwizi wa fadhila kwa kusahau jinsi Waislam walivyojitolea muhanga katika kudai uhuru. Serikali ikachukulia hotuba ya Waikela kama usaliti na yenye kuwashawishi Waislam wasiitii serikali. Ilikuwa katika hali hii Waikela mwanachama shupavu wa TANU alijitoa kwenye chama na akaamua kutumia nguvu zake kuwatumikia Waislam kupitia EAMWS.

Ilikuwa wazi kuwa Nyerere alikuwa na habari za msuguano kati ya serikali na Waislam kule Tabora na mtu ambae alikuwa akihusika na msuguano huo. Siku kabla ya mkutano wa EAMWS, Nyerere aliwaalika wajumbe wa mkutano Government House kwa chakula cha usiku. Hao waalikwa walikuwa wajumbe waliochaguliwa mahsusi. Waikela hakuwa mmoja wa hao waalikwa. Nyerere alichukua nafasi ile kuwashauri wajumbe wale waanzishe jumuiya ya Waislam wa Tanganyika ichukue nafasi ya EAMWS. Wajumbe hawa walipoleta katika mkutano hoja ya kuanzisha jumuiya ya Waislam wa Tanganyika, Waikela alisimama na kuipinga hoja ile. Alizungumza vilevile kuhusu uadui wa serikali kwa Waislam na Uislam.

Waikela alimaliza hotuba yake kwa kutoa changamoto kwa wajumbe wamuite Nyerere kwenye ufunguzi wa mkutano ili aje awaeleze wajumbe msimamo wake kuhusu kadhia hii ya chinichini baina ya serikali na Waislam. Baada ya kushindwa kwa hoja ya kuivunja EAMWS wajumbe wa mkutano ikaonekana kuwa ingekuwa vyema Nyerere aitwe kufunga mkutano ule na asomewe makubaliano yaliyofikiwa. Nyerere alifika kufunga ule mkutano na akakutana uso kwa uso na Waikela, ambae alimsomea maazimio ya mkutano. Waikela alimfahamisha Nyerere kuwa umoja kwa Waislam ni fardh ñ wajibu wa lazima. Ni kwenda kinyume na maamrisho ya Allah kuwagawa watu. Baada ya utangulizi huu Waikela huku akimnyooshea Nyerere kidole alieleza uadui unaoonyeshwa na serikali dhidi ya Waislam. Waikela alimaliza hotuba yake kwa kitisho. Alimwambia Nyerere ikiwa Waislam watamgeuka kupambanana yeye hatakuwa na uwezo wa kuwashinda.

Nyerere alitulia tuli pembeni mwa Rais wa Baraza la Tanganyika la EAMWS Tewa Said Tewa akimsikiliza Waikela. Aliposimama kujibu hotuba ya Waikela Nyerere kwa upole alisisitiza msimamo wa serikali wa kutoa haki na usawa kwa raia wake wote. Kwa kiasi fulani Nyerere alikuwa amefanikiwa kupunguza joto kati ya Waislam na serikali. Hotuba ya Waikela na ya Nyerere zikapewa umuhimu mkubwa katika radio. Waislam wengi wakajitokeza stesheni ya gari moshi Tabora kuja kumpokea shujaa Waikela. Alipewa heshima ile kwa kuwa na ujasiri wa kuweza kusimama kidete dhidi ya wale waliodhani kuwa wanaweza kuwakalia Waislam vichwani. Nyerere alihisi ameumbuka na hili lilimchoma moyo sana. Kuanzia hapa Nyerere hakumtazama Sheikh Hassan bin Amir kwa jicho jema. Alingoja nafasi yake ili alipize kisasi. Mwaka ukiofuata, tarehe 20 Januari, 1964 jeshi liliasi.

Nyerere alichukua fursa ile kuwatia kizuizini masheikh walioonekana wanapinga serikali na viongozi wa vyama vya wafanyakazi. Waikela alikuwa mmoja wa wale waliokamatwa na kuwekwa kizuizini. Nyerere kwa wakati ule hakuwa na nguvu ya kumgusa Mufti Sheikh Hassan bin Amir.Wakati ule mwaka wa 1963 shughuli za kueneza dini za EAMWS zilikuwa zikienda vizuri sana. Tabligh ilikuwa chini ya Sheikh Amir bin Juma kutoka Tanga na Wakristo wengi walikuwa wakirudi katika Uislam. Tabligh ilikuwa ikiongozwa kutoka kwa masheikh wa mikoa na wilaya. Fedha za kufanyia shughuli hizi zilikuwa zikichangwa na Waislam wenyewe. Mufti Sheikh Hassan Bin Amir yeye alikuwa akisomesha fikh, mantik, tauhid, na tafsir ya Qurían katika misikiti mbalimbali ya Dar es Salaam Wakati ule Katibu Mkuu wa EAMWS kwa Afrika ya Mashariki alikuwa V.M. Nazarali.

Mwezi Aprili 1964 ujumbe wa hali ya juu wa EAMWS ndani yake wakiwemo Sheikh Hassan bin Amir, Sheikh Said Omari Abdallah, Tewa Said Tewa, Katibu wa EAMWS Abdul-Aziz Khaki na mzee wa TANU Mzee Mwinjuma Mwinyikambi; Makisi Mbwana, Issa Mtambo, Omari Muhaji na Saleh Masasi waliondoka kwenda ziara ya nchi za Kiislam kutafuta msaada wa kujenga Chuo Kikuu cha Kiislam na kuanzisha uhusiano na nchi za Kiislam. Gamal Abdel Nasser alifurahishwa sana na ujumbe wa Tanganyika kiasi kwamba ingawa alikuwa katika matayarisho ya mapokezi ya Waziri Mkuu wa Urusi Kruschev, na ingawa ujumbe wa EAMWS ulikuwa wa kidini zaidi kuliko wa kiserikali, alikutana na ujumbe ule akaupatia ofisi, huduma za simu, na makatibu muhtasi ili waweze kutayarisha mipango yao kwa serikali ya Misri bila shida. Halikadhalika alimuagiza makamu wake Sharbasy afanye makubaliano na EAMWS kwa niaba yake. Serikali ya Misri ilikubali kugharamia ujenzi wa chuo hicho. Mkataba wa makubaliano ukatiwa sahihi mjini Cairo kati ya Tewa Said Tewa kwa niaba ya EAMWS na Makamu wa Rais wa Misri, Sharbasy kwa niaba ya serikali yake.

Serikali ya Misri iliahidi kujenga Chuo Kikuu cha Kiislam ambacho kitamilikiwa na kuendeshwa na EAMWS. Gharama ya mradi mzima uliuwa pauni milioni hamsini na tano za Ki-Misri. Baada ya kukamilisha kazi ile ujumbe ule uliondoka Cairo kuelekea Makka kufanya ibada ya hija. Baada ya kumaliza hija wajumbe wanne walirudi nyumbani na Tewa, Aziz Khaki, Sayyid Omar Abdallah wakaendelea na safari kwenda Aman, Jordan ambako walifanya mazungumzo na Mufti na Waziri wa Aukaf. Kutokea hapo ujumbe ulikwenda Kuwait ambako walikutana na Sheikh wa Kuwait kisha wakaenda Bhaghdad, Iraq na kukutana na rais wake, Abdisalama Arifek. Kutoka hapo ujumbe ulielekea Beirut, Lebabon ambako ulifanya mazungumzo na viongozi wa harakati za Kiislam. Baada ya kutoka Beirut ujumbe ule ulirudi tena Cairo kwa ajili ya kukamilisha makubaliano ya kujenga Chuo Kikuu.


Tarehe 20 Mei, 1964 ujumbe ulirejea Dar es Salaam na kupokelewa na viongozi wa EAMWS na Waislam kwa ujumla. Mkutano wa Halmashauri Kuu ya EAMWS ukaitishwa na Tewa Said Tewa akatoa taarifa yake kuhusu ujenzi wa Chuo Kikuu Cha Kiislam. Siku ya pili Tewa akaitisha mkutano wa waandishi wa habari na kutoa habari za kufurahisha za kujengwa kwa Chuo Kikuu Cha Kiislam kwa vyombo vya habari na kwa Waislam kwa ujumla. Kwa mafanikio haya Tewa akawa amejichimbia kaburi. Matokea haya yalijaza hofu kwa viongozi wa Kanisa. Kampeni za chinichini dhidi ya Tewa binafsi na uongozi mzima wa EAMWS zilianza.

Mara baada ya ujumbe wa EAMWS kurudi kutoka ziara yake, Nyerere alifanya mabadiliko katika baraza la mawaziri na Tewa Said Tewa, Mwenyekiti wa EAMWS upande wa Tanzania akajikuta nje ya serikali. Nyerere akamteua Tewa balozi wa Tanzania katika Jamuhuri ya Watu wa China. Mwezi Januari, 1965 Tewa alikwenda China kuanza kazi yake mpya. Inasemekana uteuzi wa wa Tewa kwenda China ulisababishwa na juhudi zake za kutaka kuwaunganisha Waislam kuwa kitu kimoja chini ya jumuiya moja yenye nguvu. Wakati ule ile mipango iliyopitishwa na mkutano wa Waislam mwaka 1962 ilikuwa ikitekelezwa vyema, shule zilikuwa zimejengwa Ilala, Kigogo na Kurasini, Dar es Salaam; shule zilikuwa zimejengwa Ruvu na Maneromango.

Shule hii ya Maneromango ilikuwa na umuhimu wa pekee kwa sababu hii ndiyo ilikuwa shule ya kwanza ya Waislam kujengwa Uzaramo. Shule za upili zilikuwa zikijengwa Dar es Salaam, Kinondoni na Moshi, Kibohehe. EAMWS ilikuwa vilevile imetiliana mkataba wa makubaliano na serikali ya Misri kuipa scholarship thelathini na tano kila mwaka kwa wanafunzi wa Kiislam kusoma Misri. EAMWS ilikuwa imejenga shule, misikiti, shule za ufundi na hosteli kwa ajili ya wanafunzi katika sehemu nyingi za Afrika ya Mashariki. Kwa hakika EAMWS ilikuwa ikifanya mambo ya maendeleo kwa Waislam.
Hii ndiyo mihadhara ya hoja za nguvu aliyokuwa anayofanya Mohamed Said kutokana na eti utafiti wake wa miaka 15 hadi alipotinga ndani ya ukumbi huu na kuanza kupambana na nguvu za hoja za wana JF. Kuna watu walimeza hizi simulizi porojo mazima mazima na wanashangaa kweli tunapojitokeza watu kuupinga uongo na uchochezi wake! Walishamwamini kwani huko nyuma hakuwahi kuhojiwa hata siku moja! Mwaka 1963, chama cha siasa cha kidini AMNUT ilivunjika na ndio wengi wa wanachama wake walianza kutimkia EAMWS. Walioasi TANU kwa kumpinga Mwalimu walifanya hivyo miaka mitatu kabla ya uhuru, waliunda chama cha siasa cha kidini lakini walikataliwa na wazalendo.

Wickama nakuomba usome hicho kipande alichotoa Mohamed Said kwa utaratibu...hutashindwa kuelewa kwa nini akina gombesugu wanaandika wanayoyaandika. Wickama, tulianzia mbali, hayo ya laana ya ugonjwa wa Mwalimu yalisemwa sana na pacha wake Zali la Mentali ambaye kwa sasa ni ajabu haonekani! Nataka tu nikustue kidogo, si dini ni desturi za asili tu za watu...kuna wale utoto huuvaa kama shati hadi uzeeni...ndiyo, ndivyo walivyolelewa. Hawaoni taabu kuogea dimbwini na watoto, hawaoni taabu kukaa vibarazani na watoto kuwasengenya wasiokuwapo...babu kwa baba, baba kwa mtoto, mtoto kwa kwa mjukuu na mjukuu kwa mtukuu! Ndivyo walivyo...Dini ni kisingizio tu.
 
Wickama nakuwekea kipande hiki uweze tu kujua tulikoanzia na huyu Mohamed Said na ngano zake...


Hii ndiyo mihadhara ya hoja za nguvu aliyokuwa anayofanya Mohamed Said kutokana na eti utafiti wake wa miaka 15 hadi alipotinga ndani ya ukumbi huu na kuanza kupambana na nguvu za hoja za wana JF. Kuna watu walimeza hizi simulizi porojo mazima mazima na wanashangaa kweli tunapojitokeza watu kuupinga uongo na uchochezi wake! Walishamwamini kwani huko nyuma hakuwahi kuhojiwa hata siku moja! Mwaka 1963, chama cha siasa cha kidini AMNUT ilivunjika na ndio wengi wa wanachama wake walianza kutimkia EAMWS. Walioasi TANU kwa kumpinga Mwalimu walifanya hivyo miaka mitatu kabla ya uhuru, waliunda chama cha siasa cha kidini lakini walikataliwa na wazalendo.

Wickama nakuomba usome hicho kipande alichotoa Mohamed Said kwa utaratibu...hutashindwa kuelewa kwa nini akina gombesugu wanaandika wanayoyaandika. Wickama, tulianzia mbali, hayo ya laana ya ugonjwa wa Mwalimu yalisemwa sana na pacha wake Zali la Mentali ambaye kwa sasa ni ajabu haonekani! Nataka tu nikustue kidogo, si dini ni desturi za asili tu za watu...kuna wale utoto huuvaa kama shati hadi uzeeni...ndiyo, ndivyo walivyolelewa. Hawaoni taabu kuogea dimbwini na watoto, hawaoni taabu kukaa vibarazani na watoto kuwasengenya wasiokuwapo...babu kwa baba, baba kwa mtoto, mtoto kwa kwa mjukuu na mjukuu kwa mtukuu! Ndivyo walivyo...Dini ni kisingizio tu.

Mag3; Nashukuru sana. Nilikuwa napitia chapters za kitabu cha Dr. Hassan, hasa ile sehemu ya Sakura na mapinduzi ya Zanzibar. To my suprise, yule mzee Mkwawa anachoongelea ni wazenj waafrika kusukumwa na uzalendo wa kujikwamua na mateso na udhalilishaji kutoka kwa waarabu wa unguja na ndio wakajipanga kupitia mapinduzi. Ndipo anaeleza alivyoshiriki na jinsi walivyopata support toka bara (implying JKN) ku-organize vijana kupitia Pangani. Mzee Mkwawa anaeleza jinsi walivyopinduwa kwa kuanzia na silaha za kuwapora wazenj (askari). Hiki kisa hata Ali Muhsin alikisimulia hivyo. More importantly lakini pia anaiunganisha sana na jitihada za kizalendo kwa wazalendo na nia yao ya kulipa kisasi cha muda mrefu DHIDI YA WAARABU. Haongelei ku-attack UISLAM. Okello anaongelea kuuwa WAARABU hasemi kaua WAISLAMU. Yaelekea palinjengeka chuki ya kikabila. Hapa washikaji wanageuza stori, lengo ni kuua uislamu. Hamna anayesemea wahusiano mabaya kati ya waswahili na waarabu (kisa wote ni waislamu!!!!). Unakuja hilo linaloitwa "jeshi la wamakonde", Ajabu majina ya askari waliopata bahati ya kutajwa na Mzee Mkwawa wote ni waislamu. Walioenda kupindua zenj hivyo hivyo. Jamani, awali ilikuwa inawekwa utadhani hawa "makonde" ni wapagani, hawana dini. Hii ni internet age. Kila kitu ni kwenye keyboard. Kitabu ni hiki hapa.http://kwaheri.files.wordpress.com/2010/05/kwaheri-ukoloni-kwaheri-uhuru.pdf

Ama kuhusu maradhi ya Nyerere hadi kufariki, frankly ni upuuzi na kutaka kugeuza direction ya debate. Lakini namsubiri Zali la Mentali ajibu maswali matano niliyompa. Nina orodha ya manabii waliougua na hata waliofariki kwa maradhi ya taratibu. Itabidi aniambie na aiambie JF kama hao wanabii pia walilaaniwa. Ni hasara ya taqwa yake na nimeshamtahadharisha. Maanake ubishi wa ushabiki huwa hasara.

Ama kuhusu eti kufariki huku mtu anatumia oksjeni machine kumaanisha marehemu kafa kilaana ni dalili kuwa muulizaji ana ufahamu mdogo sana, ni mjinga na ni msiba mkubwa katika dini hii ya kiislamu mtu kutunza na kusambaza mawazo ya kijinga kama haya. Kwa hiyo waliofariki kabla ya mashine hiyo kuanza kutumiwa ndiyo nini hukumu yao? Nina orodha ya viongozi mashuhuri wa KIISLAMU waliofariki huku wakiwa kwenye machine hiyo. Namsubiri huyu bwana kwa vile naona alikuwa ana hamu ya debate. Mimi nataka alete ushahidi wa maandishi sio porojo. Ndipo tutaelewa kuwa wapiga mbizi chini ya bahari, au wapandaji wa milima kama everest ambao wanatumia mitungi ya oksjeni ni Laanakum. Achilia wasafiri wa anga za juu.

Mag3; huu ni ushahidi kuwa mtu akishaiachia akili yake kujua chuki pekee, Mwenyezi Mungu humnyima uwezo wa kuyatazama mambo kiupana. Huyu Mzee wa Sakura (Mkwawa) anaongelea makafara kama kushona paka macho (ushirikina) kutumika eti kuwapumbaza waarabu wakati wa mapinduzi ya zenj (pg 50-70). Kwenye hizi threads wanajizuia tu kusema JKN ndiye ali-supply hawa paka labda toka Butiama. Ndio culture ya waongo.

Somehow kuna persistent efforts za kuwatia hofu waislamu kuwa hawataendelea bila kuivunja taasisi kama BAKWATA. Katiba ya Jamhuri hii haitakazi ndoto. Washikaji, BAKWATA mtaiacha. Nyie Jitahidini ku-manage taasisi yenu (your EAMWS) MLIYOUNDA. Kwani lazima kila mtu awafate?
 
Somehow kuna persistent efforts za kuwatia hofu waislamu kuwa hawataendelea bila kuivunja taasisi kama BAKWATA. Katiba ya Jamhuri hii haitakazi ndoto. Washikaji, BAKWATA mtaiacha. Nyie Jitahidini ku-manage taasisi yenu (your EAMWS) MLIYOUNDA. Kwani lazima kila mtu awafate?

Wickama, ngoja nitengeneze swali la namna nyingine; ni nchi gani ambayo ina chombo kimoja tu cha Waislamu kutetea maslahi yao; chenye kuunganisha Waislamu wa Madhehebu yote? Misri? Iraq? wapi... kwanini ni Waislamu wa Tanzania tu wanatakiwa wawe chini ya chombo kimoja tu? Ukisoma hapo unaweza kuamini kabisa kuwa EAMWS ndiyo ilikuwa panacea ya matatizo yote ya Waislamu; ni kweli? Lakini mbona Aga Khan aliendelea kufanya kazi Tanzania (yeye ndiye aliyekuwa muasisi na mfadhili mkuu wa EAMWS. Kama Nyerere alikuwa na tatizo na Waislamu wa EAMWS (chini ya Aga Khan) kwanini Aga Khan aliendelea kufanya kazi nchini muda wote wa Nyerere na hata kuja karibu kila baada ya miaka michache na kukutana na Rais Nyerere? Au Aga Khan baada ya kuvunjwa EAMWS hakuwa tena Muislamu kwa sababu aliendelea kufanya kazi na Nyerere?

Ni maswali ya kuchokoza tu ndugu zetu ambao wanajaribu kuililia EAMWS... Hivi ile hospitali ya Aga Khan si imekuwepo nchini kwa muda mrefu sana? na shule ya Aga Khan nayo si bado ipo? WAkati shule binafsi zimetaifishwa si serikali ya Nyerere hiyo hiyo iliruhusu kujengwa kwa Shule ya Aga Khan mwaka 1967 ikiwa chini ya uongozi wa Waislamu wa Ismailiya?

Kwanini wanaozungumzia kuvunjwa kwa EAMWS hawazungumzii kabisa uhusiano wa Imam Aga Khan na serikali ya Tanzania chini ya Nyerere? Ni kweli Nyerere hakutaka Waislamu wasifanikiwe lakini bado akamruhusu Imam (kiongozi wa Jumuiya ya Waislamu) kufanya kazi mbalimbali za maendeleo?

Unless of course, kina M. Said watuambie kuwa kina Aga Khan siyo Waislamu safi na hawamtambui Aga Khan kama Imam. Which... will bring us back to EAMWS.
 
Mag3; Nashukuru sana...
Ama kuhusu maradhi ya Nyerere hadi kufariki, frankly ni upuuzi na kutaka kugeuza direction ya debate. Lakini namsubiri Zali la Mentali ajibu maswali matano niliyompa. Nina orodha ya manabii waliougua na hata waliofariki kwa maradhi ya taratibu. Itabidi aniambie na aiambie JF kama hao wanabii pia walilaaniwa. Ni hasara ya taqwa yake na nimeshamtahadharisha. Maanake ubishi wa ushabiki huwa hasara...

...Namsubiri huyu bwana kwa vile naona alikuwa ana hamu ya debate. Mimi nataka alete ushahidi wa maandishi sio porojo. Mag3; huu ni ushahidi kuwa mtu akishaiachia akili yake kujua chuki pekee, Mwenyezi Mungu humnyima uwezo wa kuyatazama mambo kiupana.
Wickama, angalia hapo kwenye bold; yawezekana huyo unayemsubiri ni mwanamama!
 
Last edited by a moderator:
Zali la Mentali,
Kwa nini Mwalimu alitaifisha shule na vyuo vya madhehebu ya DINI?[/QUOTE
Unatakiwa kujibu hoja nilizoziweka na ambazo ninaendelea kuwataka mzijibu kwanza kabla ya kuuliza maswali mengine. Ukiona hoja zimekushinda, basi ujue kwamba hata haya maswali unayouliza hayana maana yoyote!!!!!!!!!!
 
Wickama,
Ni Dr. Ghassany sio Hassan.

Mimi nilikuwa mtafiti msaidizi katika utafiti
wa kitabu hicho.
Mohammed,
Kuna tofauti gani kati ya Hassan (Kiswahili) na Ghassany (Kiarabu)? Isn't it the same name with a cultural alteration? Ndugu zetu Afrika magharibi wamezoea kuita Aminata. Waswahili tunaita Amina. Fatumata. Fatuma. etc
 
Zali la Mentali,

Unamkumbuka Mtanganyika/Mtanzania yeyote aliyewahi kuwa Rais/Mwenyekiti wa TANU taifa hili mbali na Mwalimu?

Rudia tena post yako uliyoniuliza kuhusu upuuzi wa kutaifisha shule wakati MOU ya Serikali na Kanisa inaendana kinyume na usanii huo wa kudai kusambaza elimu kwa watu walioikosa wakati wa ukoloni. Kuvunjwa kwa EAMW kunaendana na kuwanyima haki Waislamu kujiendeleza kimasomo nje ya mfumo Katoliki uliyodhamiria kuwabana kielimu kutumia MOU na mikakati mingine kama ilivyoainishwa na Hayati Kigoma Malima, n.k.

Nimetoka kukuhitaji ujibu hoja kabla hujaniuliza masuali mengine kwenye post hiyo niliyokujibu punde kwa sababu sitaki mtumie usanii kujadiliana na mimi. Kama hamjanijibu hoja zangu za msingi, hamna haki ya kuniuliza masuali mengine kwa sababu maswali yoyote yale mtakayoniuliza sasa hivi tayari majibu yake yako kwenye hoja zangu nilizoziweka hapa.
 
Wickama nakuwekea kipande hiki uweze tu kujua tulikoanzia na huyu Mohamed Said na ngano zake...


Hii ndiyo mihadhara ya hoja za nguvu aliyokuwa anayofanya Mohamed Said kutokana na eti utafiti wake wa miaka 15 hadi alipotinga ndani ya ukumbi huu na kuanza kupambana na nguvu za hoja za wana JF. Kuna watu walimeza hizi simulizi porojo mazima mazima na wanashangaa kweli tunapojitokeza watu kuupinga uongo na uchochezi wake! Walishamwamini kwani huko nyuma hakuwahi kuhojiwa hata siku moja! Mwaka 1963, chama cha siasa cha kidini AMNUT ilivunjika na ndio wengi wa wanachama wake walianza kutimkia EAMWS. Walioasi TANU kwa kumpinga Mwalimu walifanya hivyo miaka mitatu kabla ya uhuru, waliunda chama cha siasa cha kidini lakini walikataliwa na wazalendo.

Wickama nakuomba usome hicho kipande alichotoa Mohamed Said kwa utaratibu...hutashindwa kuelewa kwa nini akina gombesugu wanaandika wanayoyaandika. Wickama, tulianzia mbali, hayo ya laana ya ugonjwa wa Mwalimu yalisemwa sana na pacha wake Zali la Mentali ambaye kwa sasa ni ajabu haonekani! Nataka tu nikustue kidogo, si dini ni desturi za asili tu za watu...kuna wale utoto huuvaa kama shati hadi uzeeni...ndiyo, ndivyo walivyolelewa. Hawaoni taabu kuogea dimbwini na watoto, hawaoni taabu kukaa vibarazani na watoto kuwasengenya wasiokuwapo...babu kwa baba, baba kwa mtoto, mtoto kwa kwa mjukuu na mjukuu kwa mtukuu! Ndivyo walivyo...Dini ni kisingizio tu.

Eti Zali la Mentali haonekani? Soma posts zangu za jana na leo sasa hivi ninazoziposts. WEWE NDIO UMEKIMBIA UWANJA KWA KUSHINDWA KUJIBU HATA HOJA MOJA NILIYOIWEKA MPAKA SASA HIVI. JINGA KABISA WEWE UANAYEKIMBIA KUJIBU HOJA ZA WANAUME WENZAKO (Kama kweli wewe si mwanaume). Mara nyingi nikiwepo humu, ninakuona chini ukiwa live lakini utasubiri mpaka nimeondoka ndipo uanze kuongea utumbo wako.

Sasa najibu utumbo wako uliyouweka hapo juu. Mpango wa kumsimika Nyerere ulitayarishwa na Ukatoliki kupitia wadau wenzake kama CIA (Marekani kama walivyojieleza wenyewe kwamba wanamtegemea Nyerere kusambaratisha Uislamu Zanzibar na wakaweka mpaka blan B kama Wazanzibar wakiyakataa mapinduzi yale haramu. Plan B hiyo ndiyo iliyompa Nyerere kiburi cha kuendelea kuwaua, kuwakandamiza na kuwadhalilisha Wazanzibar na Waislamu kwa ujumla wao alivyotaka na ndiyo inayowapa CCM uhalali bandia wa kuendeleza uuwaji, ukandamizaji na udhalilishaji wa Wazanzibar na Waislamu kwa ujumla wao mpaka leo), Uingereza (Kuleta makomandoo wa kurejesha utawala haramu wa Nyerere baada ya kukataliwa na Wazalendo wakati wa mapinduzi ya 1964) na Ukatoliki kupitia mfumo wao wa kutumia madicteta kuua na kukandamiza watu wasiokuwa Wakatoliki ili waeneze dini yao ambayo haiwezi kuenezwa kwa kutumia hoja bali nguvu.

Suala la Nyerere kuvunja EAMW limeeelezwa wazi kwamba ni maelekezo kutoka Kanisa Katoliki aliyopewa Nyerere baada ya Msimamizi wa Kanisa katika Ukanda wa Africa Mashariki kuwasilisha hofu yake kwa Papa kwamba EAMWS itawafanya Waislamu waendelee kielimu pamoja na mshikamano. Ndipo Nyerere alipopewa maelekeza kutoka Vatican kuhakikisha EAMW inavunjwa. Bila haya wao wana AMECEA ambayo ni taasisi ya Kikatoliki Africa Mashariki iliyojikita katika masuala ya kuwaendeleza Wakatoliki kielimu ukiachilia mbali TEC ya Tanzania. Na AMECEA haijaishia hapo, inaunganishwa hadi Vatican.
 
Barubaru, unanipa pole ya nini? mpe pole nduguyo Zali la mentali anayesema Nyerere ni CHIZI na kuiita hiyo ni hoja inayostahili kujibiwa!

Kwa hiyo kati ya ama UNAFIKI au UCHIZI wewe umechangua kumpa sifa ya UCHIZI si ndiyo? Hoja hii ilijengwa baada ya Nyerere kuamua kujiunga na TAA na kupanda ngazi kwenye chama hicho bila kujua viongozi wa chama hicho ni kina nani na chama kina malengo gani. Acha unazi wa kijinga na elezea kutoka kwenye nafsi yako ili tujue na wewe uko sawa au vipi. Mtu wa aina hiyo atakuwa mzima kweli? Mpaka sasa wakati haujajibu hili swali there is a very fine line between your misbehavior and his.
 
Uingereza (Kuleta makomandoo wa kurejesha utawala haramu wa Nyerere baada ya kukataliwa na Wazalendo wakati wa mapinduzi ya 1964)

Sikutaka kujibizana na huyu jamaa anajiita Zali la Mentali kwa sababu kwanza naona uelewaji wake wa masuala ni wa ajabu sana. Mfano ni hicho kipande nilichonukuu hapo juu kutoka kwa bandiko lake. Kwa hiyo ule uasi wa 1964 ulikuwa ni juhudi za wazalendo kukataa utawala haramu wa Nyerere? Hao wazalendo walikuwa ni akina nani? Na je, uasi uliofanyika wakati huo huo Kenya ulikuwa pia ni juhudi za wazalendo kuukataa utawala wa Kenyatta? Kwa sababu Waingereza vile vile walisaidia kuuzima ule uasi, lakini tofauti na Tanganyika, waliweka kambi za kudumu za kijeshi Kenya. Utajibizanaje na jitu la maoni kama haya?
 
Back
Top Bottom