Tulishasema basi nyamaza kulia na ufute machozi,yule balozi aliekahutubia alikuwa ni
Nguruvi3,au hujaridhika bado?? Umeishiwa sana...
Kwakweli ninalia, na sababu za kulia ni kuona jinsi gani watu wanayangalia matatizo ya jamii katika jicho la makengeza.
Kwamba hawatafuti suluhu wanatafuta mahali pakupoozea ima machungu yao binafsi au kufanya biashara zenye hatari kwa taifa hili.
Ukisoma maandishi mengi ya Mohamed ambayo yamedhihirika kujaa upotoshaji, watu wanayafumbia macho kwasababu tu pengine kuyapinga ni kupinga maandiko matakatifu. Sina sababu ya kurudia yale yote aliyopotosha lakini kila uchao kuna jambo jipya linajitokeza.
Hakuna aliyejua kuwa Sheikh maarufu alipewa nafasi na Nyerere akakataa, kinachosikika ni yeye kufanyiwa fitna.
Hakuna anayeeleza chanzo na kifo cha EAMWS kule kilipoanzia bali kifo hicho mwaka unaotajwa bila sababu za mashiko.
Hapa ndipo Mohamed ameshika akili za watu wengi na nakiri wengi kwasababu yeye ni Orator mzuri sana kiasi kwamba hatoi nafasi ya mtu kufikiria zaidi ya kumeza.
Nineshauri wale wanaodhani kuwa mtu hakamiliki bali akubaliane na Mohamed wafikirie mara mbili mbili.
Huko nyuma tumeonyesha jinsi gani ushabiki ulivyomgubika kiasi cha kutaka kuufanya ulimwengu wote ni mazuzu.
Hilo suala la Ibadan nalirudia kwasababu kuna watu hawakubali kuwa hakukuwa na kitu kama hicho.
Paper iliwasilishwa lakini maudhui yana matatizo sana. Na wala si hilo tu, tunaweza kurudi nyuma na kuangalia mambo mengi sana ambayo Mohamed ameyaandika kwa nia ya ushabiki wala si elimu.
Wickama alipojaribu kuliangalia suala kwa mtazamo wake yeye akaitwa Abu Jahil kwamba ni mhaini mkubwa.
Kila anayejaribu kuyaangalia mambo kwa mtazamo tofauti na Mohamed huyo anaondolewa katika uislam kwanza.
Watu wasichoelewa ni kuwa uislam unasiitiza katika haki na ukweli.
Kama mtu anadanganya ili kufarkanisha jamii, je huyo anautimiza uislam kama ilivyoandikwa?
Ni kwasababu za kutokuwa na independent mind ndiyo maana kuna matatizo katika jamii ya waislam.
Narudia katika jamii ya waislam na si Uislam.
Leo utasikia BAKWATA ni adui, ukweli ni kuwa ndani ya makundi mbali mbali kuna uhasama ambao unasubiri tu BAKWATA iondoke ili iuhasama huo ushamiri haswa.
Hebu niulize, hivi kamati ya mali za waislam inatetea mali zipi zaidi ya zile zilizohalifiwa na waislam?
Kuna kiwanja kimeuzwa na waislam, kikanunuliwa na waislam leo tunaambiwa ni kutokana na mfumokristo.
Kuna habari kuwa BAKWATA haina support ya waislam, sasa kama haina na inajulikana ni kibaraka wa serikali kwanini basi serikali ishikilie watu 3 au 7 na kwa masilahi gani. Kama BAKWATA haina support basi isingekuwepo lakini uwepo wake una maana ya kuungwa mkono. Iwe sahihi au la ukweli utabaki kuwa wanaungwa mkono na waislam kama waislam wasiounga mkono. Uislam na waislam kuna wakati havitegemeani. Baurbaru ameeleza usilam ni nini na uumini ni nini.
Kuna matatizo BAKWATA, lakini basi lazima watu wawe wakweli kuwa si BAKWATA tu hata ndani ya Baraza kuu kuna matatizo. Haiwezekani baraza hilo liwe na taasisi lukuki na taasisi hizo chini ya baraza ziendelee kupingana.
Njia rahisi ya kuficha ukweli ni kusingizia mfumo na wala si kutafuta chanzo halisi cha matatizo.
Ningedhani kuwa ni wakati sasa wa waislam wa Tanzania kufanya haya ili kuweza kupata suluhu ya kweli
1. Kwanza, baadhi yao kuachana na chuki kwasababu si sehemu ya uislam
2. Kukubali kuwa suluhu ya matatizo yao itatokana na wao wenyewe.
3. Kukubali kushirikiana kama inavyoamrisha dini na hapa naomba kusahihishwa, washikamane katika kamba ya mwenyezi mungu.
4. Wakubali mabadiliko na wakaribishe wasomi katika kuongoza taasisi zao.
a) wasomi wa dini wachukue majukumu ya dini na wao ndio waongeze sehemu hiyo muhimu ya imani
b)wasomi wa elimu zingine wapewe nafasi za kuongoza taasisi ili kupata viongozi wenye weledi kwa nyakati tulizo nazo
Huu si wakati wa kuwa na viongozi wahamasishaji wa vurugu, bali wenye vision na mission.
5. Waislam wakatae kurubuniwa na makundi yanayochochea hisia, chuki na vurugu kwani Usilam hausemi kuhusu uzushi, uongo, unafiki na farki. Badala yake Uislam unapinga hayo.
6. Huu ni wakati wa kufikiri kulingana na nyakati. Haina maana kufikiri kuhusu chuo kikuu cha kufikirika wakati chuo kikuu kilichopo kina matatizo. Kwanini watu wasielekeze nguvu zao kule kuliko hai bali watumie muda wao kufikiria kitu cha kuaminishwa ambacho hakina maelezo yanayojitosheleza.
7. Waislam waitimize dini yao kwa upendo, kwani uislam ni amani na upendo. Wasione haya kukemea maovu hata kama yanafanywa na waislam wenzao. Mathalan, watu wanaona haya kusema kuwa alichokisema Ilunga si sahihi wanabaki kutafuta sababu za maalumaa. Kwa mwislam ukweli ni haki anayopaswa kutendewa na kuitenda.
8. Waislam wajiulize kwanini baadhi yao hasa wa madhehbu mengine kama Shia, Ismaili wanafanya vizuri na kwanini wale wengine wawe mafundi na manguli wa vurugu bila kuwa na mchango mwingine wa maana katika jamii zao.(Nitarukiwa hapa, nasimama na kauli yangu)
Ni wakati wa kutenda yale yalihimizwa na kuacha yaliyokatazwa kama ilivyoandikwa
Gombesugu karibu sana Kicheba kwa mzee Mhina . Inshallah nimekuandalia nguru(siyo Nguruvi).
Panapo majaaliwa nitakuwa barabara ya 10 kabla ya kurudi Magila. Ninahamu sana na Ngogwe, kibandameno na Mahiza.
Bonde kwema atakaye na aje.