Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar

Uchochezi wa Mohamed Said na dhihaka kwa Wapigania Uhuru wa Tanganyika na Zanzibar

Wickama,
''waislam'' lakini ni wepesi sana wa kupiga nderemo na vifijo kwa kile wanachokisikia

Khair Inshallah naendelea kunya glasi ya maji ya ndimu na asali kama alivyonena Gombesugu. Lau kana haitalate afueni nitapata kikombe cha shurbati cha Shariff Ritz!

Nitatulia mavune yakiondoka lakini sitatulia nikiona uongo, upotoshaji na uzandiki kwa miaka mingine 15 ukitamalaki, never!!


Muheshimiwa Nguruvi3,

Nipa fursa hii kukanusha na kupinga vikali hayo maneno hapo juu nilipo-bold!!

Hata siku moja sitaweza kukwambia yayo,au labda tu kuna pahala ulikosea harufi kiduchu!?...na umekusudia vingine!?

Tafadhali nijuza ili moyo wangu nituame.

Maana sitaki nijeonekana na Wanajamvi wenzetu yakuwa nimekutusi,hasha!...kwanza nitajuaje yakuwa una maradhi hayo!?

Pole nyingi kwa yayo.

Ahsanta.

Cc;Wickama,Ritz
 
Gombesugu,
Kuna mwanafulani sijui kutaka kunitisha au kuni impress kanijibu kwa jeuri
kwa Kizungu cha Victorian England.

Basi mie nacheka naona vituko vya karagosi kalewa tembo.
Nikamwambia mbona hiyo ina harufu ya Dickens tena "Bleak House?"

Kashika adabu yake hajanirejea tena.
Kabaki kunitukana.

Nami simpatilizi nashika hamsini zangu.
Maalim wangu Sheikh Haruna kanifunza.

Anasema tusi halina jibu.
Madrasa ina raha zake.

Ahsante ndugu yangu.

Unafurahia kujibu tusi?
 
Muheshimiwa Nguruvi3,

Salaam sana ndugu yangu.

Niwie radhi,nimevamia kiduchu haya majadiliano yenu na nduguyo Uthman.

Tafadhali nijuza hiyo siasa na dini, ni wakati upi huwa zinaingiliana na wakati upi huwa hazitakiwi kuingiliana. Na je vigezo hivyo hutolewa na nani na ni vipi!?

Pia kama umeamua kuyarejesha hayo mambo ya utumwa na kumwekeshea darsa Ustadh Uthman,basi nakusihi muanzie na haya hapa chini:

1494 when King John of Portugal and the Catholic Mornachs of Spain sign the Treaty of Tordesillas diving the world between them.

Vasco Da Gama,kutokana na ile mila na dasturi zao za mirathi,hakuweza kuwa mrithi wa family yao,maana yeye hakuwa wa mwanzo kuzaliwa. Alipatwa na kizaazaa na mughala kwa muda.

His alternatives!? Well,there's always the Priesthood.
He goes as far as the Rites of Tonsure.

On july 1497,the King holding Court in Montemer,entrusts Vasco Da Gama with the command of expedition.

The following day,"The day of Our Lady",Vasco attends massive Mass in Belem and assumes command of the fleet;the flagship "Saint Gabriel".....the rest is bloody History!

Christopher Columbus;on every Island he set foot on planted a Cross,"making the declaration that are required"-The Requerimiento, to claim the ownership for his Catholic Patrons in Spain.

If the Indians refused or delayed their acceptance(or understanding) the Requerimiento continued:

I certify to you that,with the help of GOD,we shall powerfully enter in your country and shall make war against you...and shall subject you to the yoke and obedience of the Church...and shall do you all mischief that we can,as to vassals who do not obey and refuse to receive their LORD and resist and contradict him!

Nashukuru kwa kunisikiza ndugu yangu.

Ahsanta.

Cc;Ritz,Uthman

Asalaam aleykum al akhy Gombesugu nilikuwa nakusoma kwa chat nikiwa mapumzikoni ahsanta ndugu yangu endelea kutupa mipini.
 
Asalaam aleykum al akhy Gombesugu nilikuwa nakusoma kwa chat nikiwa mapumzikoni ahsanta ndugu yangu endelea kutupa mipini.

Boko Haram,

Asalaam Alaykum Al Akhiy.

Wallahi,nalipatwa na huzuni nyingi niliposoma kwenye post yako fulani asubuhi hii, yakuwa hawa jamaa wa Jf kumbe walikufungia!?

Kama hizo ndo dasturi zao,basi watapoteza saana reputation yao...

Sisi "Team yetu" tupo kiduchu mno kwa hapa Jamvini,halafu pia wanatufanzia njama za kufungia baadhi ya ma-Strikers wetu muhimu kama wewe Al Akhiy!ahaha!!

Haina neno,la muhimu umerejea salama nami nduguyo nimefarijika mno kukusikia tena.

Tuendelee na mnakasha Insha Allah.

Ahsanta.
 
Muheshimiwa Nguruvi3,

Nipa fursa hii kukanusha na kupinga vikali hayo maneno hapo juu nilipo-bold!!

Hata siku moja sitaweza kukwambia yayo,au labda tu kuna pahala ulikosea harufi kiduchu!?...na umekusudia vingine!?

Tafadhali nijuza ili moyo wangu nituame.

Maana sitaki nijeonekana na Wanajamvi wenzetu yakuwa nimekutusi,hasha!...kwanza nitajuaje yakuwa una maradhi hayo!?

Pole nyingi kwa yayo.

Ahsanta.

Cc;Wickama,Ritz

Nadhani ilikuwa ni makosa ya kiuandishi tu sio kuwa alidhamiria kutoa maana ufikiriavyo!
 
Kila binadamu ana historia yake.mHistoria hiyo yaweza kuwa mbaya au nzuri. Hata hivyo jambo moja ni kweli juu ya historia, kuwa historia imepita na hatuwezi kubadilisha kilichohistoria. Jambo la kweli ni kwamba tunaweza leo tukasimamia katika ukweli ili tuwe na historia nzuri miaka 50 au 100 ijayo. Nimshukuru Mohamed Said kwa maelekezo ya kitabu. Nitakisoma.

Pamoja na hayo, nina mambo machache ninayotaka kusema hapa.
1. Ukiangalia kwa kina mtiririko wa mada hapa, utagundua kuwa haswa haswa ni kati ya Uislamu na Ukristo. Kwamba Nyerere alifanya jitahada za makusudi, si tuu kutowatambua wiaslamu waliopigania uhuru, bali pia kuwakandamiza waislamu katika maendeleo. Wapo ambao hawataki kutamka kuwa Nyerere ni baba wa Taifa na wengine wanamtamka kwa kejeli. Vyovyote vile iwavyo, hili halimwongezei wala kumpunguzia kitu Nyerere na ukweli unabaki kuwa amekuwa raisi wa kwanza wa Tanzania, na dunia imemtambua kuwa alikuwa mstari wa mbele katika kupigania uhuru wetu.

2.Kuhusu malalamiko ya waislamu wa muda mrefu sidhani kwamba Nyerere anapaswa kubeba mzigo huo pekee. Pia hawezi kukwepa kabisa maana amekuwa raisi wa kwanza kwa miaka zaidi ya 20. Sababu za kwanini waislamu wanaona wapo nyuma ni nyingi na nyingine zimechangiwa na waislamu wenyewe. Hebu tazama waislamu wa Moshi/Arusha na wale wa mkoa wa Lindi! Kwanini maendeleo yao ni tofauti ingawa wote ni waislamu? Kwanini fursa zao kuendelea ni kubwa kwa baadhi ya maeneo na maeneo mengine ni ndogo?

3.Matatizo ya waislamu hayatatatuliwa kwa waislamu kusema 'ni wakati wetu sasa'. Kwamba 'wametukandamiza' vya kutosha. Hayawezi pia kutatuliwa kwa vikao vya wakristo na waislamu. Wala serikali haiwezi kutatua matatizo ya waislamu. Nionavyo mimi, suluhu ipo kwa waislamu wenyewe. Kwanza katika umoja wao watambue nini vipaumbele vyao. Waanze kuvitekeleza halafu tuone serikali gani itawazuia na kwasababu gani. Lawama hizi hazitawapelekea popote. Mimi nimetembea Kigoma, Tabora, Morogoro, Pwani, Lindi, Kilimanjaro nk. Nimeona misikiti mikubwa sana katika vijiji ambavyo maisha ya watu wake ni duni. Sasa nikajiuliza, kama upo uwezo wa kujenga haya, kwanini wasiende hatua moja zaidi kuhusu shule, zahanati, vyuo nk nk? Jukumu la serikali libakie kuwa ni kutoa fursa sawa, yaani ardhi, ruzuku, rasilimali watu nk nk

4. Upo mkakati wa kusema sasa raisi awe Mwisalmu. Kama kweli tunataka maendeleo lazima tuwaze zaidi ya hapa. Tumekuwa na maraisi wawili waislamu. Na tumeona Kikwete aliwekwa kimkakati (Hata Lipumba amekiri hilo). Na kwakweli amefanya mengi katika hayo. Bado sisi tumekuwa wakwanza kulalamikia mfumo Kristo! Kumbe kuwa na raisi mwislamu na mawaziri wote, na hata wakuu wa mikoa bado inaweza isisitatue matatizo yetu. Zipo nchi zinazoongozwa na dola ya kiislamu lakini bado malalamiko yapo kila kukicha.Tunahitaji kama taifa kuwaza beyond our religions.

5.Nimeangalia mafundisho ya baadhi ya mashekhe na hata baadhi ya michango ya watu hapa, utaona chuki ya wazi dhidi ya watu wa dini mbili hizi. Sioni kama chuki itatusaidia. Wapo ambao wamehoji kwanini baadhi ya waislamu walishirikiana na makafiri! Kwa chuki hizi,matatizo yetu hayaishi. Wengi hapa ni wasomi. Hivi kweli ukinichukia mimi kama Mkristo ndio unapataje maendeleo?

Ndio maana nasema maendeleo ya waislamu yatapatikana kama waislamu wenyewe watakaa, wakaainisha vipaumbele vyao na wakaanza kuvifanyia kazi. Serikali ifanye kazi ya promoter! Na maendeleo ya waislamu na wakristo yataonekana wazi kama Tanzania kwa ujumla wake itaendelea. Tukijiangalia kwa jicho la Uislamu na Ukristo, mwaka 2061 na hata 3011 tutakuwa bado tunazungumzia jambo hili, na pengine katika hali mbaya zaidi.

Inawezekana nimetoka nje ya mada, lakini nadhani ni vyema tushauri pia nini kifanyike ili baadae tuwe na historia sahihi ya nchi yetu. Mahali nimekosea naomba nisahihishwe, maana mimi ni kijana bado na pengine nimetawaliwa na hoja mufilisi!



Mwanasharia Iron,

Your words sound great and read well.

However,you seems to overlook some Historical facts. Non Muslims in this country especially Christians are beneficiaries of the Colonial White Supremacy structure/s.

Muslims been allienated and marginalized for decades from Socio-economic mainstream.

The process,structure or system has never been reversed effectively todate.

I know some of you like to think,that was a long time ago,lets sweep it under the rug and move on. It's not that simple Sir!

Some of you would have us/Muslims believing we do it on our own. "Pull yourselves up by your bootstraps,sort your own problem/s and move on"!

You know what,you lot didn't make it on your own. We better not believe you!

Ahsanta.

Cc;Boko Haram
 
JokaKuu,

Salaam sana ndugu yangu.

Sasa kama hakuna yeyote mwenye kupinga/kubisha yakuwa D'Salaam ndio ilokua "Central Command" kama ulivyoiita,kwanini tunashinda hapa jamvini kutwa kucha na baadhi yenu kuthubutu kufananisha zile harakati zilizokuwapo pale Mzizima na huko Mikoani/Vijijini!?

Unaposema na kukubali yakuwa D'Salaam ndio ilokua "Central Command" ni vizuri mno. Maana huu ni ukweli usopingika,japo nahisi yawezakuwa ukapata matata na shutuma toka kwa wenzio hapa jamvini!?

Ndio maana hata Nyerere alipobaini umuhimu na ukweli huo,akakimbia toka Mwisenge na kuhamia Mzizima.

Sasa la muhimu hapa ni kutambua kwa yakini,yakuwa hiyo "Central Command" ilikua sio infrastructures tu,la hasha!

Hapa sasa ndipo Sheikh Mohammed anapoingia na kubainisha tena kwa kitaaluma,yakuwa hiyo "Central Command"; ilikua ni watu,na watu hao walikua ni Wanamji/Wazee wetu na takriban woote walikua ni WaIslamu na pia walikuwa ni Watanganyika/Wazanzibary. Pia walikuwa ni Waungwana wenye sifa nyingi mno zisizo mipaka.

Kwani wewe unafikiri kabla ya Nyerere kufika D'salaam hao Wazee wetu walikua hawana Kiongozi/Viongozi wao!? Mimi sioni kama hili suala lina-qualify hata kuitwa "mzozo" kama unavyodai!?

Mimi binafsi mpaka hapo sioni tatizo wala utata wowote asilan,labda kama kuna mtu ana chuki binafsi za mambo fulani au kama pia kuna mtu atayaangalia haya mambo kwa jicho la Udini na hasada!?

Nafikiri Sheikh Mohammed, pia ametujuza mara kadhaa na wala hana ubishi na "umahiri wa Nyerere" na vyeo vyoote alivyowahi kuwa navyo tangu kuhamia D'Salaam,kikiwemo na kile cheo cha "Baba wa Taifa".

Lakini yeye Sheikh Mohammed kama ni Scholar/Historian,kenda mbali zaidi na kutafiti/kunyambulisha kwa kina;athari,madhila,dhuluma,unafiki,vicheko,furaha na pia vingine vingi alivyofanza Nyerere kwa wale wenyeji wake/ Wazee wetu hapo Mzizima.

Nafikiri pamoja na mitizamo yetu tafauti lakini pia tumshukuru mno huyu Mtafiti/MwanaHistoria Sheikh Mohammed Said.

Nimefurahi kuzungumza nawe ndugu yangu JokaKuu,napenda mno uungwana na ustaarabu wako.

Niwie radhi kwa huo uchechefu wangu.

Ahsanta.

Cc;Ritz,Sheikh Mohammed Said,Sheikh Farid,Maulaga
gombesugu,

..mimi nadhani wazee "wetu" kutoka bara wasingefika D'Salaam, basi Tanu ingebaki hukohuko kwa hao unaowaita wazee "wenu."

..kumbuka kwamba unaowaita wazee "wenu" wamenukuliwa wakidai kwamba walikuwa na draft ya madai ya uhuru wa Tanganyika, wasijue wafanye nini na draft hiyo, mpaka walipompata mtu wa bara[Kambarage mtoto wa Burito] aliyechukua draft hiyo na kwenda kuiwasilisha UN.

..zaidi, rejea taarifa alizotoa John Illife kwamba kuna wakati 2/3 ya michango ya wanachama wa Tanu ilikuwa inatokea SUKUMA LAND. Kipindi hicho nadhani Wasukuma walikuwa wanakadiriwa kuwa 1/3 ya wanachama wa Tanu.

..pamoja na kutoa mchango mkubwa zaidi ktk kuendesha Tanu, sijawahi kusikia ndugu zetu wa Sukuma Land wakigombea wapewe sifa zaidi, nafasi nyingi zaidi za uongozi, au kipande kikubwa zaidi cha rasilimali za nchi hii.

..Utata na "mzozo" ninaouona mimi ni hizi juhudi za kudunisha mchango wa Mwalimu Julius Nyerere, pamoja wa wa-Tanganyika wasio na asili ya D'Salaam, ktk harakati za uhuru wa nchi hii.

cc: Mag3, Wickama, Nguruvi3, Ritz, THE BIG SHOW
 
Last edited by a moderator:
Mwanasharia Iron,

Your words sound great and read well.

However,you seems to overlook some Historical facts. Non Muslims in this country especially Christians are beneficiaries of the Colonial White Supremacy structure/s.

Muslims been allienated and marginalized for decades from Socio-economic mainstream.

The process,structure or system has never been reversed effectively todate.

I know some of you like to think,that was a long time ago,lets sweep it under the rug and move on. It's not that simple Sir!

Some of you would have us/Muslims believing we do it on our own. "Pull yourselves up by your bootstraps,sort your own problem/s and move on"!

You know what,you lot didn't make it on your own. We better not believe you!

Ahsanta.

Cc;Boko Haram
gombesugu,

..unadai kwamba Waislamu wamekuwa ellianated na marginalized for decades.

..wakati huohuo Barubaru haishi kutukumbusha kwamba UCHUMI wa nchi hii umeshikwa na WAISLAMU.

..mimi nashauri mkae kikao wewe na Sheikh Barubaru mtupe suluhu ya madai yenu.

cc: Jasusi, THE BIG SHOW, Mag3, Ritz, Nguruvi3
 
Last edited by a moderator:
gombesugu,

..mimi nadhani wazee "wetu" kutoka bara wasingefika D'Salaam, basi Tanu ingebaki hukohuko kwa hao unaowaita wazee "wenu."

..kumbuka kwamba unaowaita wazee "wenu" wamenukuliwa wakidai kwamba walikuwa na draft ya madai ya uhuru wa Tanganyika, wasijue wafanye nini na draft hiyo, mpaka walipompata mtu wa bara[Kambarage mtoto wa Burito] aliyechukua draft hiyo na kwenda kuiwasilisha UN.

..zaidi, rejea taarifa alizotoa John Illife kwamba kuna wakati 2/3 ya michango ya wanachama wa Tanu ilikuwa inatokea SUKUMA LAND. Kipindi hicho nadhani Wasukuma walikuwa wanakadiriwa kuwa 1/3 ya wanachama wa Tanu.

..pamoja na kutoa mchango mkubwa zaidi ktk kuendesha Tanu, sijawahi kusikia ndugu zetu wa Sukuma Land wakigombea wapewe sifa zaidi, nafasi nyingi zaidi za uongozi, au kipande kikubwa zaidi cha rasilimali za nchi hii.

..Utata na "mzozo" ninaouona mimi ni hizi juhudi za kudunisha mchango wa Mwalimu Julius Nyerere, pamoja wa wa-Tanganyika wasio na asili ya D'Salaam, ktk harakati za uhuru wa nchi hii.

cc: Mag3, Wickama, Nguruvi3, Ritz, THE BIG SHOW

Nafikiria sana,

Mohamed Said na wafuasi wake wanashindwa kutambua kuwa wapo washarika wengi sana wa harakati za Uhuru lakini hawatajwi

Hivi leo Mmalawi Mzee Nyirenda aliyeupandisha mwenge wa Uhuru mpaka kilele cha Mlima Kirimanjaro katika Nyakati za Uhuru angekuwa ni Muislamu ingekuwaje?
 
Last edited by a moderator:
gombesugu,

..unadai kwamba Waislamu wamekuwa ellianated na marginalized for decades.

..wakati huohuo Barubaru haishi kutukumbusha kwamba UCHUMI wa nchi hii umeshikwa na WAISLAMU.

..mimi nashauri mkae kikao wewe na Sheikh Barubaru mtupe suluhu ya madai yenu.

cc: Jasusi, THE BIG SHOW, Mag3, Ritz, Nguruvi3


Haisaidii hata ukiamua kujitoa ufaham na kupindisha hoja hiyo,masuala ya biashara waislam ni kama utamaduni wao tuh,na katika kitabu chao kina hadi miongozo ya kutosha namna gani ya kuendesha biashara hizo kwa haki na usawa..
gombesugu mnywa ghahawa amelizungumza hilo kwenye system ya serikali...

Punguza mihemko...
 
Last edited by a moderator:
Mkuu gombesugu hapa utagombana na Mzee wetu wa gerezani Mohamed Said yeye anasema Nyerere hakuwakumbuka wazee wake wala hakuwataja kabisaaaaaaaaaa.Wewe unasema aliwapa "heshma ya kipekee na kuwataja tu wazee wa Mzizima na khasa waIslam kwenye hotuba ya muago tena huku akiwataja majina na nasaba zao"

Hakika gombesugu umemuumbua mchana kweupe Mzee wetu wa Gerezani.Namsubiri kwa hamu kubwa sijui atasema nini baada ya kamanda wake kumgeuka.Mzee wetu hodari sana wa lugha najua lazima atakuja na misamiati mipya ya Gerezani ha ha ha ha.

Ngongo,

Awali ya yoote,nakukumbusha yakuwa japo nilishakusamehe zile kashfa na kebehi ulizonifanzia mara kadhaa hapa jamvini,tena bila hata ya kutumia hoja yoyote... lakini bado sijasahau.

Hilo neno Kamanda,binafsi nahisi limekaa kishari na kuashiria vita/mabaya!? Kwani sisi soote si tupo hapa kutafuta amani na suluhu!? Au wewe ndugu yangu umedhamiria vita hapa jamvini!?

Bakhti mbaya,ile bayana yangu nafikiri wewe binafsi na hata Wickama,hamkunifahamu labda kwa utuvu.

Kwa hakika pale nilikua nasisitiza hoja yangu kwa kunyambulisha vitu kadhaa,katika majadiliano yalokuwapo nafikiri baina yangu, JokaKuu,Iron na Wickama siku chache nyuma.

Kwa kifupi ndugu yangu Ngongo,nilikua nasisitiza yakuwa hata Nyerere kwa kuonyesha mchango unique wa Wazee wetu/Wana Mzizima,ndipo pale alipopatwa na ile guilty conscious probably...siku ya hotuba ya "muago" akataja baadhi ya Wazee wetu na kwa majina fadhila zao kwake na Taifa.

Kwa sababu wengi wenu mnamalumu Sheikh Mohammed,ati anabeza harakati za hao Wazee wa Mikoani/Vijijini...mimi sikubaliani nanyi asilan.

Ndipo nikasema,kama ni hivyo basi wa kulaumiwa ni Nyerere. Kwani katika ile Speech yake ya Muago,kwanini hakutaja hao Wazee wa Mikoani/Vijijini na hizo Family za hao Ma-Chief!? Au nae pia alibeza michango hiyo ya Vijijini!?

Unataka kuniambia ati Nyerere Mkristo mtiifu,alitamka vile kuwapa sifa za bure wale Wazee wetu...kwani hakujua michango na harakati nyingine zozote hapo Tanganyika kama vile za Makanisa,Ma-Chief na Makasisi!?

Ndipo nikasema yakuwa Nyerere ametuachia kigugumizi...maana yake amekuachieni nyinyi kigugumizi. Maana utapingana vipi na maneno au maelekezo ya "Baba wa Taifa"....kwamba Wazee wa Mzizima,ndo wao walomstiri na kumfadhili pita kiasi ndugu yao na mwenzao!?

Naona ndugu yangu Wickama,nae anadai kwamba atleast Gombesugu amethibitisha yakuwa Nyerere alifanya fadhila kwa hao Wazee!?ahaha! Kutajwa jina kwa mchango wako ni haki, na kufanyiwa fadhila ni vitu viwili tafauti.

Nafikiri hiyo sehemu pia ishawahi kunyambuliwa kiundani hapa jamvini.

Yeye Nyerere kuwataja wale Wazee ilikua ni lazima,kwasababu hii ni Historical fact,ya kwamba hata kama kuna "Plots" au harakati nyingine zozote zilizokuwapo sehemu nyingine mbalimbali hapo Tanganyika wakti huo,lakini utakuwa "Maluuni wa Kitaaluma"/Academic dishonesty,kuthubutu kufananisha na yale yalokua yakifanzwa na Wazee wetu/"Wana Kindakindaki" a.k.a Wana Mzizima.

Unataka kuniambia yakuwa Nyerere ati aliwapenda saana Wazee wachache wa KiIslamu kutoka D'Salaam,kuliko hata Wazee wa kutoka Mara au Makasisi wa Peramiho!?ahaha!!

Halafu leo anatokea Yericko,kutwambia ati Nyerere alifanyiwa matambiko makubwa saana na Makasisi!ahaha!!...Jinsi Nyerere alivyokua Mtiifu na mwadilifu wa Kanisa lake,halafu ati asahau hata kutaja hiyo "michango mikubwa" akumbuke tu michango ya Dini moja!?
Najua kabisa Nyerere asingefanza hivyo asilan!

Ndipo pia nilimpa mfano wa kistaarabu,ndugu yangu JokaKuu,kuhusu wale ndugu zetu na Wazee wa Kaskazini walivyoshughulika na ule mgogoro "wao"wa Ardhi kule Meru.

Kumbuka,wao wakti huo inawezekana kabisa walikua pia wana uwezo mzuri hata wa kifedha kuliko baadhi ya sehemu nyingi za Tanganyika...lakini waliamua kujitenga kikanda na kushughulika ki-selfish na huo mgogoro wao huko Kilimanjaro. Ndo maana hata Chadema labda wamerithi dasturi hiyo mbaya!

Lakini wakaamua kupeleka mtu/Mwakilishi wao kipekee bila hata ya klujali au kuhusisha/kushirikisha nguvu zoote na harakati kwa pamoja kwa maslahi ya Tanganyika na Watanganyika woote!?

Nyerere,soote tunajua yakuwa alikua ni "mwerevu wa kisiasa"...nina hakika ya kuwa haya yoote aliyajua kiundani mno na alizingatia saana!...nafikiri pia yaliwahi kumsumbua kichwa japo kiduchu!

Hivi unafikiri,kama wale Wazee wa kaskazini walopeleka Mwakilishi wao kipekee(japo Passport ililazim itolewe/wasaidiwe na Abdilwahid Sykes hapo D'Salaam),kama wangefanikiwa yale maombi/matakwa yao pale UN,Historia yoote ya Tanganyika ingekua vingine hivi leo...na labda Tanganyika pia isingekua nchi moja kama hivi tuijuavyo leo hii!?

Kwa kumalizia kiduchu,ile hotuba ya muago ya Nyerere,kiujumla Waislam takriban woote waliichukulia kama ni kejeli na dhihaka kwao. Zile imbalances na ahadi nyingi walizotegemea,kuahidiwa au kupanga na Nyerere nafikiri havikutimia.

Unajua Ngongo,imenilazim kunena/"kufunguka" hivi vitu ni tu sababu wewe umenidodosa mno. Lakini huwa sipendi na wala si dasturi yangu. Nafikiri ndo maaan pale nilipomjibu JokaKuu kwa ustaarabu/indirectly na kugusia kiduchu hii khabari,lakini wewe hukufahamu mantiki ya yale maelekezo yangu.

Lakini hapo namwachia Sheikh Mohammed Said,maana yeye hiyo ndio field yake kama Mtafiti na MwanaHistoria.

Nafikri ndugu yetu The Big Show nae pia huko awali,aliwahi kuyazungumzia haya masuala kwa kina.

Napenda tumwache Sheikh Mohammed aendelee kuchambua kiundani. Pia Kumradhi labda kama una suali lolote nakusihi pia muelekezee yeye.

Nashukuru kwa kunisikiza huo uchechefu wangu.

Ahsanta.

Cc;Ritz,The Big Show, Sheikh Mohammed Said,Wickama,JokaKuu
 
gombesugu,

..mimi nadhani wazee "wetu" kutoka bara wasingefika D'Salaam, basi Tanu ingebaki hukohuko kwa hao unaowaita wazee "wenu."

..kumbuka kwamba unaowaita wazee "wenu" wamenukuliwa wakidai kwamba walikuwa na draft ya madai ya uhuru wa Tanganyika, wasijue wafanye nini na draft hiyo, mpaka walipompata mtu wa bara[Kambarage mtoto wa Burito] aliyechukua draft hiyo na kwenda kuiwasilisha UN.

..zaidi, rejea taarifa alizotoa John Illife kwamba kuna wakati 2/3 ya michango ya wanachama wa Tanu ilikuwa inatokea SUKUMA LAND. Kipindi hicho nadhani Wasukuma walikuwa wanakadiriwa kuwa 1/3 ya wanachama wa Tanu.

..pamoja na kutoa mchango mkubwa zaidi ktk kuendesha Tanu, sijawahi kusikia ndugu zetu wa Sukuma Land wakigombea wapewe sifa zaidi, nafasi nyingi zaidi za uongozi, au kipande kikubwa zaidi cha rasilimali za nchi hii.

..Utata na "mzozo" ninaouona mimi ni hizi juhudi za kudunisha mchango wa Mwalimu Julius Nyerere, pamoja wa wa-Tanganyika wasio na asili ya D'Salaam, ktk harakati za uhuru wa nchi hii.

cc: Mag3, Wickama, Nguruvi3, Ritz, THE BIG SHOW


Swadakta tuuh..
Nawewe kama unaona ya kwamba wasukuma wameachwa kupewa nafasi kwenye historia ya nchi hii muda na uhuru wa kuandika bado unao,uwanja unao mkuu,andika utufahamishe watanzania...

Kwanin Moh Said ameandika kwa ushahid na hoja za ushahid waz waz mumuone mchochez na mpuuzi??

Ondokeni basi muwaachie wale wanaothamin elimu hii waipate,ama la kama unakuja kupinga njoo upinge kwa hoja mujarabu...
 
Haisaidii hata ukiamua kujitoa ufaham na kupindisha hoja hiyo,masuala ya biashara waislam ni kama utamaduni wao tuh,na katika kitabu chao kina hadi miongozo ya kutosha namna gani ya kuendesha biashara hizo kwa haki na usawa..
gombesugu mnywa ghahawa amelizungumza hilo kwenye system ya serikali...

Punguza mihemko...

..nadhani hujaelewa hoja yangu.

. gombesugu anadai Waislamu wametengwa.

. Barubaru anadai Waislamu wameshika hatamu za uchumi wa nchi hii.

..kuna utata hapo, na mimi naomba ufafanuzi tu kwa hao wahusika wawili.
Ritz, Nguruvi3, Wickama, Mag3
 
Last edited by a moderator:
gombesugu,

..unadai kwamba Waislamu wamekuwa ellianated na marginalized for decades.

..wakati huohuo Barubaru haishi kutukumbusha kwamba UCHUMI wa nchi hii umeshikwa na WAISLAMU.

..mimi nashauri mkae kikao wewe na Sheikh Barubaru mtupe suluhu ya madai yenu.

cc: Jasusi, THE BIG SHOW, Mag3, Ritz, Nguruvi3

JokaKuu,

Ndugu yangu,mimi nimeingia hapa jamvini peke yangu na nitaondoka peke yangu.

Hivyo vikao unavyonipangia...vinakhusu nini!?

Maneno yoote nisemayo au yakuumizayo,inabidi umlaumu Nyerere. Mimi nasoma na kufuatisha hiyo Khutba yake mwenyewe ambayo mwanae tena wa kumzaa mwenyewe Yericko Bin Nyerere Bin Burito,ndio kaiweka mwanzoni kabisa mwa Mada hii!?

Ahsanta.
 
JokaKuu,

Ndugu yangu,mimi nimeingia hapa jamvini peke yangu na nitaondoka peke yangu.

Hivyo vikao unavyonipangia...vinakhusu nini!?

Maneno yoote nisemayo au yakuumizayo,inabidi umlaumu Nyerere. Mimi nasoma na kufuatisha hiyo Khutba yake mwenyewe ambayo mwanae tena wa kumzaa mwenyewe Yericko Bin Nyerere Bin Burito,ndio kaiweka mwanzoni kabisa mwa Mada hii!?

Ahsanta.
gombesugu,

..nimekuelewa!!

..tuendelee tu mnakasha kwenye maeneo mengine.

..thanks!!
 
Last edited by a moderator:
Nafikiria sana,

Mohamed Said na wafuasi wake wanashindwa kutambua kuwa wapo washarika wengi sana wa harakati za Uhuru lakini hawatajwi

Hivi leo Mmalawi Mzee Nyirenda aliyeupandisha mwenge wa Uhuru mpaka kilele cha Mlima Kirimanjaro katika Nyakati za Uhuru angekuwa ni Muislamu ingekuwaje?

Yericko,

Kama huyo Mzee Nyirenda angekua Muislamu,basi nina hakika Historia ya Kivukoni isingemtaja asilan!...na labda kama ingemtaja basi labda sentensi moja tu,kama walivyofanyiwa wale Waislamu wengine!ahaha!!
 
gombesugu,

..nimekuelewa!!

..tuendelee tu mnakasha kwenye maeneo mengine.

..thanks!!

JokaKuu,

Nakuomba usikereke ndugu yangu.

Ili tusonge mbele ni bora kuambiana ukweli utakaochoma leo,kuliko kukaa kimya kudanganyana mapenzi yaso kweli.

Sisi soote ni wamoja,nami binafsi nakuheshimu mno ndugu yangu JokaKuu.

Nashukuru kwa kunifanzia ustahamilivu na kunisikiza.

Ahsanta.
 
JokaKuu,

Nakuomba usikereke ndugu yangu.

Ili tusonge mbele ni bora kuambiana ukweli utakaochoma leo,kuliko kukaa kimya kudanganyana mapenzi yaso kweli.

Sisi soote ni wamoja,nami binafsi nakuheshimu mno ndugu yangu JokaKuu.

Nashukuru kwa kunifanzia ustahamilivu na kunisikiza.

Ahsanta.
gombesugu,

..naunga mkono hoja asilimia 100.

..i am humbled kwa heshima uliyonipa.

..tuendelee na mnakasha.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom