Nicholas said:
na Koran yenyewe inasema Yesu hakuwa na dhambi..itakuweje huyo mtume mweye dhambi awe mfano bora?
Mitume wote ni Maasuum! hakuna Mtume anayefanya dhambi...ama kuhusu kukosea katika masuala yasiyo ya kiWahyi hilo ni suala jingine.
Mfano ukiangalia Surah Abasa utaona pale Mtume salalahu alayhi wasallam alikuwa amezama katika kuwapa daawah makafiri wakuu wa Kiquraish, katikati ya hii daawah Abdullah ibn Makhtoum (swahaba huyu) akajitokeza na kuanza kumuuliza Mtume swali kuhusu masuala ya dini, Mtume akaamua kuendelea na daawah kwa makafiri kwanza ili baadaye aje kumjibu Abdullah ibn Makhtoum ambaye tayari alikuwa ni Muislamu lakini hakujua kuwa alichotaka Allah ni kupewa kipaumbele huyu Muislamu kwanza kabla ya makafiri.. hii ndiyo sababu ya kushushwa Surah Abbasa na tunaona wazi kabisa kuwa hii si dhambi.
Daud (David) alitoa hukumu kwa kuusikiliza upande mmoja tu bila ya kuusikiliza upande wa pili ndipo akagundua kuwa aliusikiliza upande mmoja tu na kutoa hukmu...tunaona tena hii si dhambi,labda uliite kosa la kiuhakimu wakati wa kutoa hukumu.
Quran 36:
22-24. Walipo muingilia Daudi, naye akawaogopa. Wakasema: Usiogope! Sisi ni wagombanao wawili, mmoja wetu amemdhulumu mwenziwe. Basi tuhukumu kwa haki, wala usipendelee. Na utuongoe kwenye njia iliyo sawa.
Hakika huyu ndugu yangu ana kondoo wa kike tisiini na tisa; na mimi ninaye kondoo mke mmoja. Akasema: Nipe huyo nikufugie! Na amenishinda kwa maneno.
Akasema: Kweli amekudhulumu kwa kumtaka kondoo wako mmoja kuongezea kwenye kondoo wake. Na hakika washirika wengi hudhulumiana wao kwa wao, isipo kuwa walio amini na wakatenda mema. Na hao ni wachache. Na Daudi akajua kuwa tumemfanyia mtihani. Basi akamwomba msamaha Mola wake Mlezi, na akaanguka kusujudu na kutubia"
Ninaweza kuendelea na Mitume wengine ukitaka lakini hutakuta wakifanya dhambi zozote kama vile uzinifu,wizi,ujambazi na maasia mengine.
Nicholas said:
akawaambi ahaikuwa hivyo mwanzo..ila mapokeo tuu ya wazee wao.Kuwa honest bana..Yesu alimaanisha dini pale alipowaambia....vitu kwa kunukuu maandiko..aliwaambia".... imeandikwa..."Na wengi walinyamaza.Kwa vile hawakuwa tena na cha kumhukumu.
Unachosema wewe ni kigeni! kwa sababu karibu kila mtu ndani ya duru za kidini anajua kuwa Mayahudi walimhukumu Jesus (Yesu) kwa ushirikina, uchawi, uzinzi na usaliti. Jisomee mwenyewe wanavyofundishana katika Talmud:
"The Talmud (Babylonian edition) records other sins of 'Jesus the Nazarene':
1) He and his disciples practiced sorcery and black magic, led Jews astray into idolatry, and were sponsored by foreign, gentile powers for the purpose of subverting Jewish worship (Sanhedrin 43a).
2) He was sexually immoral, worshipped statues of stone (a brick is mentioned), was cut off from the Jewish people for his wickedness, and refused to repent (Sanhedrin 107b; Sotah 47a).
3) He learned witchcraft in Egypt and, to perform miracles, used procedures that involved cutting his flesh, which is also explicitly banned in the Bible (Shabbos 104b).