Uchumi bado Umekaza? Vodacom yajiondoa kudhamini Ligi Kuu Tanzania Bara

Uchumi bado Umekaza? Vodacom yajiondoa kudhamini Ligi Kuu Tanzania Bara

Kampuni ya Mawasiliano Vodacom imelitaarifu Shirikisho la Mpira wa miguu Tanzania Kuwa haina nia ya kuendelea kuidhamini ligi kuu Tanzania Bara maarufu kama Vodacom Premier League ikitoa sababu ya mwenendo mbaya wa Biashara.

Ni uchumi? Bwana Bakhresa kayatoa kwenye uchumi upi mabilioni atakayoyaweka kwenye Mpira?
Itakuwa ni vyema AZAM akadhamini ligi kuu ya TANZANIA halafu timu zinazoshiriki zirudi kama zamani, ziwe timu ishirini [ 20 ].
 
Ndiyo nasema mbona Azam tv huonesha mechi za hao jamaa, sasa atazuiaje TBL kuweka bango lake uwanjani?

Simba na yanga wana sportpesa (betting, haramu) lakin mechi zao anaonesha!

May be Azam anataka logo yake ndio iwe kifuani pia (who knows) ili atangaze biashara zake vizuri zaidi.
Sio bango ishu ni tittle ya ligi itabadilika na kuwa TBL premier league..na nimesema inasemekana Azam aliweka figisu kidogo ili TBL wasipewe ligi..sikumaanisha kuwa ana uwezo 100pc wa kuzuia.
 
Msimu kesho ndio ulikuwa mwisho wa.mkataba miaka mitatu Kati ya TFF na Vodacom ...mazungumzo ya kurenew mkataba yalikuwa yanaendelea.. hoja ikaja Media partner anatoa bonus kubwa zaidi ya mdhamini mkubwa pamoja na kucover vitu vingi zaidi...so akatakiwa as a main partner aongeze dau lake..jamaa wakakimbilia kutaka wawe co- main sponsor na Azam ..wao waendelee kutoa hio 80-90 tu kwa.misimu ijayo...inaonekana Kama Vodacom alikuwa anataka kuendelea lkn pesa hana..so akaona kuliko Kuja kuaibika mbeleni huko bora aweke tamati msimu huu ..huku kwa msimu ujao walikubali kufanya mutual termination na TFf ..

Nataman Sana pepsi waichukue ligi hii..ama kampuni yeyote ya vinywaji..au bank ...

Japo kimsingi milioni 500 za Azam ni sawa na miiba kwa wadhamini wengine..aisee...inamaana mdhamini Mkuu akijitokeza awe na uhakika wa kutoa zawadi ya Bilioni 1 kwa Bingwa..ama milioni 800 Kwa kuanza.
 
Wale wote waliosherekea bakhresa kuzamisha billion 225,

Wajiandae na msiba wa vifurushi,


JAMAA keshaanza tayari,
Lazima atafute namna ya kurudisha ile pesa yake.
Uko sawa, kuna watu walifurahia mkataba bila kuangalia side B, wacha movie liendelee
 
Si mlisema Azam kaweka pesa kiduchu na mkataba wake na Tff ni mrefu sana,sasa hii ni fursa kwa wapiga domo kuonesha kwa vitendo kwa kutoa pesa kufadhili Ligi kuu.
 
Kama sikosei, wiki chache zilizopita iliandikwa magezetini kwamba mwaka huu Vodacom wasingetoa gawio bila shaka kutokana na faida kiduchu waliyokuwa wamepata!

Sasa ukichanganya na mzigo uliowekwa na Azam, si ajabu TFF walitaka mzigo unaoeleweka kutoka Vodacom na sio ule wa mshindi kupata vimilioni vingapi sijui!

Ukichanganya yote hayo, unashauriwa usione aibu kutoka nduki kama kupigana ngumi huwezi manake kila siku wanaodhalilika na kichapo ni wale wanaoona aibu kutimua mbio.
Hao Tff watoe sasa huo mpunga mrefu
 
Ndiyo nasema mbona Azam tv huonesha mechi za hao jamaa, sasa atazuiaje TBL kuweka bango lake uwanjani?

Simba na yanga wana sportpesa (betting, haramu) lakin mechi zao anaonesha!

May be Azam anataka logo yake ndio iwe kifuani pia (who knows) ili atangaze biashara zake vizuri zaidi.
Mkuu kwani wewe ni mgeni na Watanzania? Watanzania ni mabingwa wa kulisha watu maneno na kila kitu watu wanakijua juzi tu hapa walisema mtu ukidhamini ligi ya bongo unapata faida lukuki leo mtu anajitoa anapata hasara!!!!!

Sasa ngoja tusubiri wale wachambuzi kwanini Voda inapata hasara wakati ukidhamini ligi yetu unapiga mpunga mrefu?
 
Mechi za Taifa stars zinaonyeshwaga na Azam?..yaani Tff ana mkataba wa kudumu na Azam wa kuonyesha games na other contents za Taifa Stars??..


Ulishawahi kuona matangazo ya bia au kamari kwenye channel mama za Azam?
Ila ya vizuia mimba yapo, maajabu hayatakaa yaishe kwenye hii dunia
 
Na wao Vodacom si wanauza vocha zao n.k
SHIDA ipo wapi?
Wewe unatangaza biashara zako kupitia ligi.
Mwenzio anauza decoder zake.
Hamuwezi kuwa Sawa.
Wanapata fursa ya milage mkuu
So in return wanapata wateja wengi wa product za bakhresa
 
Back
Top Bottom