Uchumi Unao, Umeukalia....

Uchumi Unao, Umeukalia....

Kwa upande wa uchumi wa taifa, Tanzania tunapaa, midege angani, mabarabara ya juu kwa juu, SGR, Stigler Gorge, Tanzania ya Viwanda tukielekea kuwa nchi ya uchumi wa kati, uchumi wa gesi na Tanzania kugeuka a donor country.

Kwa upande wa ule uchumi ule wa Dada zetu wale wanaokalia, mimi nimewapigania sana ile biashara yao irasimishwe, ihalalishwe, iwekewe utaratibu, itengewe maeneo rasmi, watu wafanye kazi walipe kodi. Jijini Dar Massage zimetapakaa watu wanakuwa Massaged asubuhi, mchana, jioni na usiku kucha, lakini serikali hazipati chochote.


P

Sawa kabisa Pascal,kwa sasa hivi mambo yanayoendelea nchini hata mtoto mdogo anafahamu vile tunauchakata uchumi wetu, je, tunaweza kutabiri kuwa baadae ya muda gani matokeo ya kuchakata uchumi yataleta tija kwa wananchi hadi filed wa chini na kumfanya apate mahitaji yake muhimu (chakula,malazi na makazi?).

Pongezi nyingi sana kwa mkuu wa nchi kuhamasisha uchakataji hasa kwa upande wa miradi hii mikubwa, je shughuli hizi zinamfikia raia hadi wa chini? Simaanishi ajar bure na aletewe mahitaji muhimu na serikali laa hasha,namaanisha mjasiriamali anayejishighulisha kufanya shughuli ndogondogo kujikwamua kiuchumi, anasonga au anakandamizwa na uchumi wa nchi husika?
 
Duh! Kazi kweli kweli!
It's true ni kazi kwelkwel, ila ni kazi halali na ndio ajira inayoongoza duniani kuliko ajira nyingine zote, hivyo sisi wapigania haki huru, hata hawa tinawapigania.

P
 
Uchumi tumeukalia kwa asilimia mia.Fursa hatuzioni.Tanzania tuna upungufu wa mafuta ya kula kwa asilimia 75% lakini Tuna zaidi ya ekari millioni zenye rutuba ya kulima Karanga,Alizeti,Ufuta,mawese nk tunanunua mafuta kwanye Nchi yenye visiwa Malaysia na isiyo na rutuba.Wengi wanatamani kwetu na wakija wanapiga hela sisi hatuoni fursa.Hicho ni kimoja tu kati ya vingi.Au mpaka waje wakolini tena?


Eeenheeee, nilikuwa nataka uchakataji huu, na idadi yetu bado ni milioni 55?

Hivi tunakwama wapi? Tukitaka kukaa mahindi nchi jirani walau tupate pesa mipaka inafungwa, Hata humu ndani watu wengi wamekuja na mada za kukatishwa tamaa na juhudi walizozifanya kwenye kujikwamua kiuchumi matokeo yake wamepoteza mitaji yao huko....

Mabenki yapo yanatoa mikopo, shida ni nini? Tunahitaji masters degree na PhD ili tuuchakate uchumi wetu kuleta maendeleo kwa kila mwananchi? Na hii ilete chachu kwa wananchi waliokata tamaa kujituma hasa wakiona jirani amefanikiwa...

Natamani kitu kifanyike ila najikuta nakwama, elimu ya hamasa na research zilizofanyika zikiletwa kwa wananchi zitawaamsha kujituma na hapo serikali pia itakusanya mapato yake. Naona kuna LAXITY mahali, nachelea kusema siasa zinavuruga Mambo haya sababu sijajikita sana kwenye siasa na hii haimaanishi kuwa nimejikita kwenye uchumi las hasha bali Mahaba yamenichosha pia.... Labda na umri nao umenisonga....

Kasinde Matata.
 
Sawa kabisa Pascal,kwa sasa hivi mambo yanayoendelea nchini hata mtoto mdogo anafahamu vile tunauchakata uchumi wetu, je, tunaweza kutabiri kuwa baadae ya muda gani matokeo ya kuchakata uchumi yataleta tija kwa wananchi hadi filed wa chini na kumfanya apate mahitaji yake muhimu (chakula,malazi na makazi?).

Pongezi nyingi sana kwa mkuu wa nchi kuhamasisha uchakataji hasa kwa upande wa miradi hii mikubwa, je shughuli hizi zinamfikia raia hadi wa chini? Simaanishi ajar bure na aletewe mahitaji muhimu na serikali laa hasha,namaanisha mjasiriamali anayejishighulisha kufanya shughuli ndogondogo kujikwamua kiuchumi, anasonga au anakandamizwa na uchumi wa nchi husika?
Kwa vile kazi ya Kujenga uchumi huwa inachukua muda mrefu, kusema ukweli miaka kumi haitoshi, ndio maana wengine tumeshauri, tukitaka kumfaidi Magufuli, tumuongezee muda, tumpe muda wa Kutosha, akiondoka, aondoke ametuachia Tanzania ya uchumi wa kati.

P
 
Kwa vile kazi ya Kujenga uchumi huwa inachukua muda mrefu, kusema ukweli miaka kumi haitoshi, ndio maana wengine tumeshauri, tukitaka kumfaidi Magufuli, tumuongezee muda, tumpe muda wa Kutosha, akiondoka, aondoke ametuachia Tanzania ya uchumi wa kati.

P


Okay, hapo sawa kwa upande wa nchi kwa ujumla na miradi yake kutokana na rasilimali za nchi.

Je, na wananchi wa hali ya chini nao wasubirie miaka 10 ili kuanza kujikwamua kiuchumi?

Naona kiswahili kigumu halafu nashindwa kuandika kilichopo akilini mwangu, sina shida na kiongozi kukaa madarakani hata miaka 30, ila kuna mahali nilisikia (sijui kama ni uzushi au laah) ila uchumi wa nchi ulipimwa kwa kiwango cha mwananchi kuweza kujimudu gharama zake za siku nikimaanisha mtu huyo anaishi kwa shilingi ngapi kwa siku?

Tuchukulie kibarua aliyeajiriwa kwenye kiwanda cha kukamua mafuta ya kupikia, malipo yake ni ya siku (sina takwimu wanalipwaje) ila akirudi nyumbani ana gharama za kuendesha maisha zinamsubiria... Kodi ya pango, chakula, kama ameoa watoto na mke, elimu ya wanae, nayeye ajiendeleze walau aweke akiba au aanzishe kamradi n.k n.k.

Kipindi cha mzee Mkapa ilisemekana mtu wa hali ya chini anaishi kwa shilingi 1,000/- natamani kujua kwa sasa ni shilingi ngapi.

Nilijaribu kupitia tovuti ya takwimu, benki kuu na wizara ya fedha ila sikufanikiwa kuona kitu.

Anyways uchumi ni mpana sana, na una vigezo vya kuzingatia wakati wa kuuchakata. Eehehehee nimekumbuka elimu ya sekondari.... Ceteris Paribas... Other things remains constant....

Eeehhh acha nikachakate muhogo uchumi ushanivuruga, na hivi wengine hatuna huo uchumi.... Majangaa.
 
Hapo ulipoanza na maneno ya kumuomba Mungu umenikumbisha huu wimbo.



Yeah uchumi ukitumika vizuri huleta manufaa ila ukiutumia vibaya inakuwa sawa na kuukalia tuu, unajikuta unabaki Kuwa masikini.

hahahaaaaaa niko Kijiweni na mzee mmoja hapa tunausikiliza huu wimbo na nakuja hapa naukuta umeuweka imenibidi nifurahi tu.
 
Maombi yafaa yaendane na kunyanyuka na kuuchakata uchumi ili ulete Tina na mabadiliko kwa wananchi wake.

Raia wa nchi nyingi wanatushangaa, tunakuwaje masikini ilhali uchumi tunao? No kiasi cha kuuchakata ipasavyo na kila mwananchi apate sehemu ya mahitaji muhimu, CHAKULA, MAVAZI na MALAZI/MAKAZI. Elimu ni muhimu ila si lazima iwe elimu ya mfumo wa mkoloni. Hata elimu asilia ya namna ya kutumia rasilimali zetu pia ni elimu tosha.

Wananchi wakipata elimu namna ya kulima kilimo cha kisasa,namna ya kuhifadhi mazao kwa muda mrefu, namna ya kutumia ardhi yenye rutuba bila kutumia mbolea na kuizeesha ardhi, namna ya kuvua samaki na kuacha waendelee kuzaana, namna ya kusindika vyakula na kuboresha miundombinu ili maeneo yenye ukame na uhaba wa maliasili wazipate na maisha Kuwa bora kwa kila mtanzania.....

Tunakwama wapi? Mbona uchumi tunao??! Tena wa asilia tuu.

Hapo hujagusa madini.....
Hongera kwa hamasa yako kubwa kwangu
 
Habari za kuikaribisha wikiendi....na poleni na majukumu ya kutwa nzima na wiki nzima.

Kichwa cha uzi ni usemi uliovuma sana miaka hiyoo niko jeshini...na waliotamka usemi huo walikuwa na maana tofauti tofauti.

Tukichukulia kama sentensi ilivyo, mtu anashangaa unakuwaje masikini wakati umezungukwa na bahari,mito,maziwa,misitu yenye wanyama kama vivutio,milima, madini, ardhi yenye rutuba na kustawi mazao mengi...haingii akilini unakuwaje masikini na kula ya wananchi wa nchi husika ni ya sintofahamu....

Wanawake...ilikuwa fumbo kwao, utasikia mtu anamwambia mwanamke, unalia lia shida wakati uchumi unao na umeukalia.....
Siku hizi siusikii huu usemi, nimekumbuka zamani.

Kwa wale wahenga wenzangu, wewe unafahamu maana ipi?

Kasinde

Tafuta mbebez mwenye hela kama Lemutuz aokoe jahazi. Hii ilisababisha dada tunayependana anikimbie. Sababu eti sina future
 
Mabwana wadogo wa instagram na twitter hawawezi kukuelewa unamaanisha nini.

Sisi wahenga tumekosoma vyema. Mwalimu Nyerere alikwenda Zanzibar, akawaambia uchumi mnao lakini mmeukalia. Wazanzibari wakahamaki, yakheee umetutukana yakheee.

Mwalimu akawaambia mmenielewa vibaya, namaanisha maliasili tunazo halafu tunalalamika umaskini.
 
Mabwana wadogo wa instagram na twitter hawawezi kukuelewa unamaanisha nini.

Sisi wahenga tumekosoma vyema. Mwalimu Nyerere alikwenda Zanzibar, akawaambia uchumi mnao lakini mmeukalia. Wazanzibari wakahamaki, yakheee umetutukana yakheee.

Mwalimu akawaambia mmenielewa vibaya, namaanisha maliasili tunazo halafu tunalalamika umaskini.


Heheheheheheee uchumi huu unaleta shida... Kauli ni tungo tata kidogo hehehehee.
 
Times change and speak volumes. Maisha mtihani sana. Mambo yakikugomea unaokoka kama konki ili kuepusha shari


Wengine majina yetu ni nafuu ya shari....

Haikwepekii, umeukaliiiaaaaaa....
 
Back
Top Bottom