Uchumi wa Kati: Waziri Mkuu akisalimiana na bibi Asumin Milanzi huko Ruangwa

Uchumi wa Kati: Waziri Mkuu akisalimiana na bibi Asumin Milanzi huko Ruangwa

Halafu hela hiyo inakwenda wapi kama bado anakuwa ombaomba
Omba Omba yule na wengine kama yeye uwa na matatizo ya Kula madawa ya kulevya.. Kwa kifupi wengi wao mateja.. Omba Omba wa mtoni usomlinganishe na kwetu. Na mpaka sehemu za kuishi za bure zipo ( zinaitwa shelters). Ila wa nakuwa hawataki kukaa kule kwa sababu ya masharti magumu, mf mida ya Kula, kulala, kurudi saa ngapi, kutokunywa pombe nk ndiyo maana unaowaona mtaani.
 
View attachment 1510539

Waziri Mkuu Mh Kasim Majaliwa alikuwa kwenye ukaguzi wa mradi wa kisasa wa kilimo cha mboga mboga , hawa ndio watanzania wa uchumi wa kati , pichani akisalimiana na bibi Asumini ambaye ni mpiga kura wa Ruangwa .
Unatoka hapo, unaingia kwenye vx, basikeli na wakulima wote pembeni wanatimuliwa vumbi na ma VX8! Halafu akifika home mamlo na mavinywaji kwenye friji Kama yote yani! Na masaluti juu!

Kuna watu wana roho ngumu aisee.🤦🏾‍♂️
 
Tunawasubiria October watueleze hayo maendeleo ya vitu yana link vipi na kuboresha maisha yetu,Kama maisha yetu bado hovyo haya maendeleo wanayosema yametusaidia nn.Maendeleo ni lzm yaguse maisha ya watu
 

Attachments

  • 2452889_VID-20200711-WA0010 (1).mp4
    10.7 MB
Dharau ni nini ?
Mkuu, wewe kama umezaliwa na kukulia kwenye nyumba na mazingira mazuri basi ni heri yako, mshukuru Mungu. Sisi wengine tumezaliwa, tumekulia, tumesomea, kwenye nyumba ambazo hata hiyo ni nzuri, kamwe hatuwezi kuwa-look down wazazi wetu na mazingira yao eti kwa lengo la kufurahisha umati wa kisiasa. Ni wapi Tanzania, including majimbo na halmashauri zinazoongozwa na chadema, ambako hautakuta nyumba kama hizo? Au wewe mwenzetu umekulia mjini nini? Sisi wengine tuliotokea kwenye nyumba za tembe huko vijijini tunaona tena hiyo nyumba ni nzuri sana. Mama kapiga hatua ya maendeleo. Wewe endelea kucheka.
 
  • Thanks
Reactions: Tui
Angalia mwamerika huyu anayeishi kwenye nchi yenye uchumi wa juu

View attachment 1510546

Nafikiri kuna haja ya kuiandikia Benki ya Dunia barua ya kupinga kuwa Tanzania haijafikia uchumi wa kati.
Ni tofauti kabisa kumlinganisha yule bibi na huyo Mmarekani.

Huu ni mfano wa hovyo kabisa wa kulinganisha.

Lakini mimi nayaona matumaini makubwa sana kwa yule bibi na familia yake.

Kwanza nyumba yake kuezekwa kwa nyasi si hoja. Hiyo nyumba ilivyo haimuonyeshi kuwa hali yake ya kipato ni duni. Kuna vitu vingine kwenye picha hiyo vinavyoweza kuonyesha kupungukiwa kwa bibi na watu wake

Dar es Salaam yetu ya leo pale kariakoo ni tofauti kabisa na Dar es salaam ya miaka michache iliyopita. Ukitafuta picha za Uhuru 1961, utaiona Kariakoo ile ikiwa na vijumba vya makuti. Magomeni nzima kuondoa 'kota' ilikuwa ni makuti tupu. Leo huyaoni tena.

Na hizi nyuma huko vijijini zimeanza kupotea, ndio maana nadhani hata mleta mada akaona aitumie kama mfano wa hoja yake (ambayo kwa bahati mbaya ni kinyume cha anayoyashikia bango).

Sio hivyo tu, hiyo hiyo Marekani, rudi nyuma miaka 30 tu uangalie hali za maisha ya wananchi wake ni tofauti kabisa na hawa unaowaona leo.

Tanzania yetu hii, ikitulizana, ikaacha kufanya mambo ya hovyo hovyo yasiyofaa (nazungumzia viongozi waliolewa madaraka na kukandamiza wananchi bila ya sababu zozote); ipe miaka kumi, (inawezekana huyo bibi akawa hayupo wakati huo, lakini hilo ni kudra za Mwenyezi Mungu); Lindi hiyo itakuwa tofauti sana na hii Ruangwa ya leo.

Tumefikia kwenye 'inflection point' ambapo tunatakiwa kuanza kuona mabadiliko ya maisha ya watu yakitokea kwa haraka sana.
 
Huyu kwa taarifa yako kila mwisho wa mwezi naenda kuchukua hela ya bure serekalini!
Nashangaa kidogo kwa nini ameutumia huo mfano ambao ni vitu mbalimbali kabisa kumlinganisha na huyu bibi yetu hapa.

Kwanza bibi ni mchapa kazi kwelikweli, hata ukimwangalia tu kimuonekana, bibi na watu wake ni wachapa kazi hodari, lakini nguvu zao zinapotea bila ya kuwafaidisha wao na kuwaletea mabadiliko maishani mwao.
 
Erythrocyte,

Kwa akili tu ya kawaida, kuna uhusiano gani wa maisha ya huyo bibi na nchi kuwa kwenye uchumi wa kati?
WB wanatumia kigezo gani kuiweka nchi kuwa kwenye uchumi wa kati?
Na nchi ikiwa kwenye uchumi wa kati ndio kusema raia wote watalingana kipato?
Hii inathibitisha kwa nini Chadema imekufa na kuanguka kifo cha mende. Sababu imejaza wafuasi na wanachama ambao wanakamasi kichwani.
 
Ni tofauti kabisa kumlinganisha yule bibi na huyo Mmarekani.

Huu ni mfano wa hovyo kabisa wa kulinganisha.

Lakini mimi nayaona matumaini makubwa sana kwa yule bibi na familia yake.

Kwanza nyumba yake kuezekwa kwa nyasi si hoja. Hiyo nyumba ilivyo haimuonyeshi kuwa hali yake ya kipato ni duni. Kuna vitu vingine kwenye picha hiyo vinavyoweza kuonyesha kupungukiwa kwa bibi na watu wake

Dar es Salaam yetu ya leo pale kariakoo ni tofauti kabisa na Dar es salaam ya miaka michache iliyopita. Ukitafuta picha za Uhuru 1961, utaiona Kariakoo ile ikiwa na vijumba vya makuti. Magomeni nzima kuondoa 'kota' ilikuwa ni makuti tupu. Leo huyaoni tena.

Na hizi nyuma huko vijijini zimeanza kupotea, ndio maana nadhani hata mleta mada akaona aitumie kama mfano wa hoja yake (ambayo kwa bahati mbaya ni kinyume cha anayoyashikia bango).

Sio hivyo tu, hiyo hiyo Marekani, rudi nyuma miaka 30 tu uangalie hali za maisha ya wananchi wake ni tofauti kabisa na hawa unaowaona leo.

Tanzania yetu hii, ikitulizana, ikaacha kufanya mambo ya hovyo hovyo yasiyofaa (nazungumzia viongozi waliolewa madaraka na kukandamiza wananchi bila ya sababu zozote); ipe miaka kumi, (inawezekana huyo bibi akawa hayupo wakati huo, lakini hilo ni kudra za Mwenyezi Mungu); Lindi hiyo itakuwa tofauti sana na hii Ruangwa ya leo.

Tumefikia kwenye 'inflection point' ambapo tunatakiwa kuanza kuona mabadiliko ya maisha ya watu yakitokea kwa haraka sana.
ndio maana nyuzi kama hizi Zinaletwa ili wadau mfunguke
 
Omba Omba yule na wengine kama yeye uwa na matatizo ya Kula madawa ya kulevya.. Kwa kifupi wengi wao mateja.. Omba Omba wa mtoni usomlinganishe na kwetu. Na mpaka sehemu za kuishi za bure zipo ( zinaitwa shelters). Ila wa nakuwa hawataki kukaa kule kwa sababu ya masharti magumu, mf mida ya Kula, kulala, kurudi saa ngapi, kutokunywa pombe nk ndiyo maana unaowaona mtaani.
Wewe na wote walicomment kudai kuwa umaskini wa Marekani ni wa madawa ya kuelevya na eti umaskini huo hauwezi kulinganishwa na wa Tanzania hamuijui Marekani na manzungunguza ya kusimuliwa na kuona kwenye TV tu. Wote hamjawahi kuishi Marekani kabisa, kwa hiyo mnadhani maisha ya wenzentu ni ya mtelemko tu.

Nendeni mkatembelee vijiji vya West Virginia, Kentucky na Mississipi kama hamtasema ni afadhali vijiji vya Tanzania ! Lakini umaskini huo wote umo ndani ya nchi yenye uchumi wa juu.

Nilichotaka kueleza huko nyuma ingawa wewe ukabadilisha mwelekeo ni kuwa uchumi wa kati haina maana kuwa watu wote wanaishi uchumi wa kati, ni vile vile pia tulivyokuwa uchumi wa chini, bado tulikuwa na matajiri waliokuwa wanaishi maisha ya uchumi wa juu. Kinachoongelewa hapo ni wastani tu, kuna watakaobaki nyuma na watakaokwenda mbele lakini wastani wake ndio huo wa Kati. Vipimo vyote vya uchumi huwa ni wastani. Hata Marekani yenye uchumi wa juu bado ina maskini wengi sana wengine hata hawajui watakula nini; wanaopata foodstamps zina masharti yake pia. Kwa hiyo usidanganywe kuwa usipokuwa na kazi unalipwa hela kirahisi, kuna vigezo thabiti sana kuhakikisha kuwa hakuna aneyakaa kutegemea hela ya bure tu. Kwa mfano kama unadai yeye anatumia madawa ya kulevya basi kwanza angekuwa ameshakamatwa na hawezi kupewa hela ya bure ya walipa kodi .
 
Ni tofauti kabisa kumlinganisha yule bibi na huyo Mmarekani.

Huu ni mfano wa hovyo kabisa wa kulinganisha.

Lakini mimi nayaona matumaini makubwa sana kwa yule bibi na familia yake.

Kwanza nyumba yake kuezekwa kwa nyasi si hoja. Hiyo nyumba ilivyo haimuonyeshi kuwa hali yake ya kipato ni duni. Kuna vitu vingine kwenye picha hiyo vinavyoweza kuonyesha kupungukiwa kwa bibi na watu wake

Dar es Salaam yetu ya leo pale kariakoo ni tofauti kabisa na Dar es salaam ya miaka michache iliyopita. Ukitafuta picha za Uhuru 1961, utaiona Kariakoo ile ikiwa na vijumba vya makuti. Magomeni nzima kuondoa 'kota' ilikuwa ni makuti tupu. Leo huyaoni tena.

Na hizi nyuma huko vijijini zimeanza kupotea, ndio maana nadhani hata mleta mada akaona aitumie kama mfano wa hoja yake (ambayo kwa bahati mbaya ni kinyume cha anayoyashikia bango).

Sio hivyo tu, hiyo hiyo Marekani, rudi nyuma miaka 30 tu uangalie hali za maisha ya wananchi wake ni tofauti kabisa na hawa unaowaona leo.

Tanzania yetu hii, ikitulizana, ikaacha kufanya mambo ya hovyo hovyo yasiyofaa (nazungumzia viongozi waliolewa madaraka na kukandamiza wananchi bila ya sababu zozote); ipe miaka kumi, (inawezekana huyo bibi akawa hayupo wakati huo, lakini hilo ni kudra za Mwenyezi Mungu); Lindi hiyo itakuwa tofauti sana na hii Ruangwa ya leo.

Tumefikia kwenye 'inflection point' ambapo tunatakiwa kuanza kuona mabadiliko ya maisha ya watu yakitokea kwa haraka sana.

Unejitahidi kuandika, lakini sioni unachojaribu kueleza kuhusiana na picha hiyo. Utajiri wa taifa hauna maana ya utajiri wa mtu mmoja mmoja. Taifa tajiri kama marekani nalo lina maskini kama huyo na vivyo hivyo hata sis tulipokuwa uchumi wa chini bado pia tulikuwa matajiri wengi tu. Uchumi wa nchi nunapimwa kwa averages, na ni lazima kuna watu wenye uchumi wa hini sana, na wale wenye uchumi juu sana lakini kipimo kinachoongelewa ni average tu. Kutafuta watu maskini na kuwatumia kwa extrapolation kuwa nchi yote ni masikini ni ufinyu wa mawazo, kwani unaweza pia kutafuta matajiri wachache akina Bakhressa na kuwa kuwatumia kusema nchi ni tajiri.
 
Back
Top Bottom