Uchumi wa Tanzania: Je, Ni Kitendawili au Ni Mazingaombwe Kwa Maskini?

Uchumi wa Tanzania: Je, Ni Kitendawili au Ni Mazingaombwe Kwa Maskini?

gfsonwin

Nitakujibu lile uliloniuliza;

Tatizo la Kariakoo sasa hivi ni matokeo ya mchanganyiko wa rushwa na kukosekana kwa utawala wa sheria. Kwa muda mrefu kodi zilikuwa zinalipwa kwa kukadiriwa na afisa kodi ambaye anamuomba mfanya biashara amkatie 25% ya kodi halisi, halafu ailipe serikali 25% na yeye mfanyabiashara kusevu 50%. Kwa hiyo wafanyabisahara wengi hawakuzowea kulipa kodi; rushwa ilishawaharibu. Vile vile ni tatizo la kukosekana kwa utawala wa sheria kwa vile wamezowea kuwa wanaweza kukaidi sheria bila madhara yoyote yale. Tatizo ni pale serikali inataka kuwekza udhibiti sehemu moja na kuacha mapengo sehemu nyingine. Inatakiwa utawala wa sheria unform kwa wote katika skta zote.
 
Last edited by a moderator:
Zakumi, haya ni majibu yangu kwa bandiko lako #18 :



Mkuu Zakumi,
Its obvious kwamba wewe ndio unaboronga kwani nitajirudia tena: Unaangalia suala zima la industrialization in Tanzania kwa jicho la Liberalization, Marketization and Privatization, suala ambalo halikuwepo miaka hiyo; Katika dunia ya tatu, main anthem was developmental state ambapo nchi zilijengwa under STATE CAPITALISM (including the current Asian Tigers); Hivi unaelewa jinsi gani mataifa makubwa (yaliyoendelea) yalifanikiwa kufanya hivyo kupitia protectionism? Do you understand anything about the argument for infant industries? Hata hawa asian tigers tunaowajadili hapa, sio kwamba walifungua milango kwa njia ya “RUKSA” bila mipaka; Zakumi, You have to wake up and smell the Coffee;
Bila ya wewe kujinasua toka katika giza hili (i.e. kuishi dunia ya Liberalization, Marketization and Privatization – as if it has always been there, kamwe hauta appreciate malengo yaliyokusudiwa chini ya Ujamaa, let alone mafanikio katika maeneo kadhaa; Fanya utafiti uelewe kwanini donors walimiminika kwa wingi in terms of misaada na uwekezaji baada ya kutangazwa kwa azimio la Arusha, na sio kabla ya hapo;

Na hoja yako awali kwamba kilichofanyika Tanzania wasn’t something new ni ishara kwamba haufanyi utafiti wa kutosha; Tanzania iliwavutia west na Ujamaa na Kujitegemea kwasababu it was a unique approach: Ujamaa opposed capitalism and shunned Marxism; Kwa wakati ule, kulikuwa na njia kuu mbili za kupiga hatua kimaendeleo kwa nchi maskini: Aidha accelerate integration of your economy into the global capitalist system (the colonial way), of which mkuu Zakumi, without reservations, unaona hiyo ndio njia sahihi OR, disengage/delink from this system through socialist policies; Again, the fact that Ujamaa opposed Ubepari and at the same time Shunned Marxism ilivutia watu wengi sana, na hata wewe ungekuwa unaishi nyakati zile, hakika usingepingana na hili; tatizo ni kwamba unafanya analysis “baadae sana”;

Hoja yako juu ya “stress test” katika nyakazi zile za ujenzi wa taifa na uchumi baada ya maafa ya ukoloni haina mashiko kabisa, kwani again, unaishi katika muktadha ambao haupo sahihi kufanya such an analysis. Naomba nijirudie tena kwamba - hata kwa nchi kama Marekani na Uingereza, Sekta ya Umma ilipewa kipaumbele kuliko sekta binafsi kwa kipindi kirefu sana kufuatia kumalizika kwa vita vya pili vya dunia (1945), na mageuzi makubwa yalikuja letwa na Thatcher (UK) na Reagan (USA); Nini uchambuzi wako wa stress test kwa wenzetu hawa? Kumbuka, hata sekta ya umma kwa mataifa haya ilianza kupata misuko suko, lakini tofauti na sisi, mbali ya wao kuwa na uwezo mkubwa kiuchumi na utaalamu katika masuala ya sera, pia yalipata fursa to reform at their own pace vinginevyo yangeanguka; Mwalimu Nyerere aliomba kufanya the same na ndio maana Tanzania ilikuwa ni moja ya nchi za mwisho kabisa kupokea Structural Adjustment Policies spearheaded by the World Bank and IMF;



Nashukuru umekuja na hoja hii, kwani inapingana na hoja yako ya awali ambayo ulibeza sana viwanda ambavyo wengi wetu tulijadili kwamba vilikuwa na umuhimu licha yaw ewe kuviponda kama viwanda visivyokuwa na maana katika uchumi – sigara, bia n.k; Kumbuka, hivi vilikuwa ndio viwanda kwanza kukimbiliwa na wawekezaji, na ndio kwa kiasi vimekuwa bado sustained na ni miongoni mwa tax payers wakubwa nchini; kama alivyojadili Nguruvi3, viwanda vingine vingi vimeishia kuwa maghala ya kuhifadhia chumvi, na akakuhoji kwanini, huku wewe ukitokomea bila ya majibu;



Hivi kwanini Mkapa alikimbilia kubinaifisisha mabenki yaliyokuwa chini ya umma katika awamu yake? Kwa kiasi kikubwa, wanachofanya wawekezaji ni kilekile kilichokuwa kinafanywa na wakoloni.



Haupo in touch with reality; hata a simple search on google itakueleza kwamba our approach to development chini ya sera ya ujamaa na kujitegemea ilikuwa “UNIQUE”; Mengine nimejadili hapo juu;



Utafiti niliofanya ni kwamba – we experienced growth in the industrial sector late 1960s to mid 1970s ambapo mchango wa sekta hii kwa pato la taifa (GDP) ulifikia peak ya 13%; Hapo awali ulikuja na takwimu zisizo sahihi kwamba hatujawahi kuwa na mchango wa sekta hii kwa GDP ya Zaidi ya 7%; Kwahiyo nukuu yako hapo juu kuhusu uzalishaji wa sekta mbalimbali kuanza kuborongo in mid 1970s ni sahihi, na ndio maana STATE CAPITAL ikadumaa, lakini sio kabla ya hapo;



Hivi kweli unaelewa role of Foreign AID katika maendeleo ya nchi kama South Korea?



Ni kweli kwamba uzalishaji na matumizi yetu havikulingana; Lakini jiulize why? Ni kwa sababu (na hii ipo all over the development literature – Tanzania ilijaribu to capture the peasants without coercion; Nchi nyingi zilizofanikiwa na viwanda, hata Britain, walifanya kinyume; Rejea matukio ya enclosure system ambayo ilikuwa ni very chaotic; Ni baadae sana Mwalimu akashawishika kufuata approach hii pale alipoanzisha vijiji vya ujamaa kwa nguvu, lakini baada ya muda mfupi, he abandoned this strategy kwani pia ikawa counterproductive; So capturing peasants (kisera) ikawa tatizo, na not capturing peasants (kisera), inaendelea kuwa tatizo hadi leo; So hoja yako kuhusu matumizi kuwa makubwa kuliko vipato ni kwa sababu – Mwalimu ilibidi atumie method nyingine, hasa ile ya kuwashawishi to engage in production of marketable surplus in exchange of free social services (elimu, afya, maji…); Hii ikapelekea failure to produce a marketable surplus; Hoja ya msingi hapa mkuu Zakumi ni kwamba, pamoja na mapungufu ya Mwalimu kisera, mengi are justified kwani we have structural weaknesses in our economy, na ndio maana hadi leo serikali imekwama – inapinga ujamaa wa Mwalimu lakini haiji na mbadala wa kweli wa kumuinua mwananchi; na wewe kwa bahati mbaya upo in the same wagon;



Kwa kweli, ni wewe ndio unalazimisha, lakini muhimu Zaidi, mtazamo wako sio sahihi na unashangaza kidogo; For any country, industrialization ni muhimu sana kutokana na mambo kama vile high economic returns, greater production, employment linkages and productivity improvement kupitia technological adaptation; Malengo ya Mwalimu na viwanda ilikuwa to disengage from international capitalism kama milivyojadili awali ili tuweze ku gain economic independence (tofauti na mfumo ulioacha na mkoloni) i.e. mkakati wa ku restructure uchumi wetu ambao ulikuwa based in primary commodity that aimed to serve former colonial powers; Zakumi, kwa wakati ule, mtazamo huu ulikuwa na tatizo gani?
Juhudi za industrialization zililenga kwenye processing ya mazao ya kilimo na pia import substitution ya basic industries – hasa viwanda ambavyo vinge promote our capacity kuwa self reliane in industrial production pamoja na viwanda ambavyo vinge fulfill basic needs za binadamu kwa watanzania walio wengi – food, shelter, clothing etc; Viwanda vya namna hii were envisaged not only kuwa the corner stone of our county’s industrial structure upon which viwanda vingine vingeweza endelezwa, bali pia kutengeneza linkages muhimu ambazo zinge penetrate katika uchumi kama vile employment n.k;

Mambo hayakuwa mabaya mpaka ilipofikia mid 1970s kama ulivyojadili hapo juu, lakini ni bahati mbaya sana unajadili mapungufu yaliyojitokeza domestically na kupuuza masuala yaliyokuwa yanaendelea in the international scene;



Unaweza kuja na hiyo model waliyopendekeza kwenye sekta ya elimu kisha ufanye analysis ingetusaidiaje relative to mafanikio chini ya sera ya mwalimu?

Vinginevyo katika suala la maendeleo ya uchumi, mwalimu alichukua ushauri wa hao unaowaitia utalaam: Moja ya makubaliano baina ya mkoloni (Britain) na Nyerere ilikuwa ni sisi kuendelea na sera zile zile za mkoloni; Na utambue pia kwamba 5 years development plan adopted in 1962 ilikuwa imeandaliwa na wataalam unaowazungumzia, lakini matokeo yake kiuchumi yakawa disastrous; Nitarudi kujadili hili kwa kina na kwa takwimu, vinginevyo kufeli kwa utaalam huu wan je pamoja na maugomvi makubwa ya cold war yakapelekea external assistance kwa nchi nyingi duniani (including Tanzania) kuanza kukauka; Hapo ndipo Mwalimu akaamua kuja na Azimio la Arusha ambalo liliamsha interest za donors kuliko kipindi cha awalil Nikipata nafasi, nitarudi kujadili haya kwa kina;

Neo-Nyerere AKA Mchambuzi;

Ni wewe unayesema kuwa naangalia industrialization kwa kutumia darubini ya Liberalization, Marketization and Privatization. Hayo ni maneno yako. Sikuzaliwa nikiwa nimeshikilia hiyo darubini. Nilianza kwa kuamini nguvu ya viwanda. Na kushindwa kwetu kulinifanya nijiulize kwanini? Kwanini wengine wanafanikiwa na sisi tunashindwa. Majibu niliyopata yanaonyeshwa kuwa kuna external and internal factors. Hatuwezi control external factors. Lakini tunaweza kuangalia internal factors. Hivyo darubini yangu imejengwa kwa kuangalia internal factors zetu na kuzilinganisha na internal factors za nchi kama USA, Japan, na China. Ukweli wa mambo hatukuwa na mazingira ya kufanya industrialization.

Mchumi anaweza kusema kuwa South Korea na China ziliendelea kwa sababu walijenga viwanda. Hivyo tukijenga viwanda Tanzania, Tanzania nayo itaendelea kama South Korea au China. Mwanasiasa anaweza kusema kuwa Marshall Plan ilisaidia ujenzi wa Ulaya baada ya vita vya pili vya dunia. Hivyo tuki-apply Marshall Plan katika nchi za kiafrika, nazo zitaendelea.

Ideas kama hizi zinatengeneza sauti kusikiliza lakini the devil is in detail. Uchumi ni eco-system. Ni wajibu wa kiserikali, iwe ya kijamaa au kipebari, kuna nurture hiyo eco-system. Ni lazima serikali iwe na capability na vilevile utamaduni wa kuwajibika.

Kwa maoni yangu katika miaka ya 60, 70 na 80 hatukuwa na capability na utamaduni wa kuwajibika. Yoyote anayesema kuwa tulikuwa tayari anaongopa. Katika kipindi cha sasa capability hipo lakini hakuna utamaduni wa kuwajibika.
 
Mimi ningependa kuchangia kidogo katika uchumi wa Tanzania.

Nisingependa kurejea nyumba kwenye makosa makubwa yaliyofanywa kiuchumi na viongozi waliopita. lakin kubwa kwa sasa na kuwaandaa watu kwa kuwapa ilmu ya uchumi, Utii wa sharia ni muhimu sana na hili litaondoa ile dhana ya kulindana na kuoneana aibu, Kuweka mipango madhubuti ya kukuza uchumi na wa Tz kuwa na uzalendo na mapenzi ya dhati kwa nchi yenu. Kisha kuweka sera nzuri ambao wengi mumezichambua katika mada hii.

Kwani bila hiyo foundation. hamtaweza kuendelea hata kidogo.


Nitapita baadae baada ya kusoma zaidi michango ya wanaukumbi
 
Mkuu gfsonwin,

Bandiko #115 umeleta suala muhimu sana ndani ya mjadala; Ningependa kulijadili briefly, na kwa mtazamo tofauti kidogo:

Kwa mtazamo wangu ambao pengine ni finyu, kinachoendelea ni ishara kwamba kuna existence of injustice tax system in Tanzania; Pengine tuangalie, je nini umuhimu wa taxation kwa taifa?

Taxation inatakiwa kutusaidia kama taifa - to link solidarity from local level (jamii) all the way to the national level (serikali); Kupitia uhusiano huu, kunakuwa na majadiliano na mashauriano (negotiations) kupitia "social contract" ambayo inaweka wazi haki na wajibu wa serikali (state) kwa raia, na raia kwa serikali; katika muktadha huu, unagundua kwamba kumbe "Tax is supposed to be Distributed Wealth, not just Government Money; Hali hii isipokuwepo, matokeo yake ni resistance, non – compliance on part of tax payers; Kwa Tanzania, KODI is government money, not distributed wealth;

Mkuu gfsonwin, fiscal-social contract niliyojadili hapo juu ni litmus test kubaini iwapo there is representative government kwani taxes connects rights to reality; Bila ya mapato ya kutosha, haki za raia kama vile usalama, afya, elimu, maji, n.k vitabakia kuwa ndoto; Lakini tunapozungumzia mapato – a just tax system lazima ikusanye mapato kutoka vyanzo vyote – income taxes, capital gains, property, royalties from extractive industries, financial transactions n.k; A just tax system must treat walipa kodi wote equally and fairly – locals, multinationals according to similar rates na kutoza all sources of income ili kutengeneza a level playing field; Kwa Tanzania, kuna matatizo katika fiscal-social contract, na pia tax payers are not treated equally and fairly;

Solution ni kwa serikali kuhakikisha kwamba perception ya wananchi inageuka kutoka imani kwamba "KODI NI FEDHA ZA SERIKALI, na kwenda kuwa KODI IS ALL ABOUT WEALTH DISTRIBUTION; Kuna njia nyingi za kufanikisha such a redistribution lakini kuu ni pamoja na hizi zifuatazo:

1. Uwepo wa progressive tax rates ambapo wealthier individuals should pay more and vice versa…
2. Kodi itumike kutoa universal access to public goods ambazo Zakumi amezijadili hapo awali, hasa elimu, afya, maji ili kuondoa matabaka yaliyopo sasa ambapo wenye nacho na wasicho nacho wanatumia huduma zisizofanana;
3. Pia serikali ije na scheme itakayosaidia mikopo ya wanafunzi kwa wale wanaostahili, soft loans za ujasiriamali kwa wale wanaostahili, and income grants kwa wale wanaostahili, sio kwa mtindo wa sasa ambapo mikopo kwa wanafunzi na mabilioni ya Kikwete yanaenda kwa wajanja wachache; Hali hii inaumiza sana wananchi kwani kimsingi, hiyo ni kodi yao;

Yakifanyika haya na mengine muhimu, tutafanikiwa kuja na a just tax system na kutatua matatizo ya resistance and non-compliance;
 
ni kweli uchumi wa nchi wa wakati tunapata uhuru ulitegem,ea zaid misaada sawa lakin pia hata mtotom aliyezaliwa hupewa maziwa yasiyoghoshiwa nikiwa na maana kwamba utoto huanza kwa kukaa kisha kutambaa na ndipo usimame.

hivi Mchambuzi na Mkandara watanibishia kwamba hakukuwa na sababu ya kuwa na viwanda ama kuwa na viwanda kwa wakati ule ilikuwa ni makosa??

binafsi unless kwamba am getting old na uwezo wangun wa kufikiri unazidi kudumaa but the truth is mwl did the right thing kwa wakati huo, lets name viwanda vilivyokuwapo ingawa vilipata changamoto ya ujinga uliokuweppo miongonui mwa wengi lkn it was much better manake that was one way ya kuelekea kukuza taifa liwe na uchumi huru.

nafikiri tukianza kutaja tyoka enzi za RTC, MAGUNIA, COFFEE CURING, URAFIKI, TANZANIA PACKERS, TANARIES ETC huoni kama hata kama havikuwa na mchango mkubwa kiuchumi but vilitakiwa kuendelezwa ili vije vitufae baadae??

unaona sera ya Mwinyi free market ilikuwa sawa na mimi naikubali but unapoongelea free je ni free market ya kuagiza tu ama na wewe una supply??
manake angesema free markert huku na siye tunasupply ingekuwa sawa ila free market kwa kuingiza tu thats bull shit to me......

hebu kwanza tuangalie % ya import na export enzi za mwl kisha tuje tukompee na za mzee ruksa tuone.

Ukweli ni kwamba misingi ya mwl kwa enzi zile ilikuwa ni mizuri sana na kama tungepata maboresho kidogo toka pale ilipokuwa tungekuwa mbali sana lkn kuua kabisa ile misingi ndio chanzo cha matatizo yetu leo. imagine hata kiberiti tunaagiza nje from kenya?? kiberiti cha kibo match hakina ubora hadi unajiuliza hivi mwl aliondoka na akili za watu ama ilikuwaje??

Sikatai sera za mwl kukosolewa lkn pia napingana zaid na kukosolewa kwa sera zake kwa aina ya kuzikaa na kuzifisha bila kuziboresha ili ziweze kwenda na wakati.

Mimi nakupa mfanio mdogo tu nimezaliwa kijijini sana huko Hai machame nazaliwa nakuta home kwetu kijijini kuna simu lile la kuzungusha la mezani, ila baada ya tu ya mzee ruksa kuingia alianza na posta na simu wakati huo kuifanya anachojua yeye sile idara ya simu ikahujumiwa ikafa ikawa nyaya zake ndizo tunazoanikia nguo na kibaya zaid mtu akitaka kupiga simu basi anakwenda kufunua lile handaki la cable anapiga simu kwa kuchezea hadi simu ikawa mufilisi. thanks to Mkapa alokuja kuifufua na kuifanya kuwa ni kitebgo kinachojitegemea na sio posta na simu tena.

sasa hii inanipa picha kwamba hata kama mwl alikuwa na mapungufu but aliweza kusimamaia vitu vikaonekana na vikawepo ila wanasiasa wa leo wote wanasimamia matumbo yao tum na hakuna anyejali hata mmoja.

sera za mwl zikirekebishwqa kuwenda na wakati zingeyytufikisha mbali ila kwa kufuata sera za dunia sijui dunia inaenda wapi na sisi tunaenda tu kama vipofu hatufiki. kwanza sion sababu ya kucopy na kila aina ya uchumi wa dunia unavyoenda cant we be creative kwa kiasi cha kuwa na mfumo wetu ambao kwenye mfumo wa mwenendo wa uchumi duniani unafiti lkn pia kwetu sisi unatupa maisha bora zaid??
Mkuu ondoa hilo la Mkandata kukubishia maana binafsi yangu namuunga na namuelewa sana Nyerere alichotaka kufanya miaka ya 70 japo watu wengi wameshindwa kuelewa outside forces zilivyokuwa vikitupiga vita WAJAMAA..

Ni nguv hizi hizi zilizomweka Mandela na viongozi wote wa ANC ktk list ya ma - Terrorist, hawa hawa hawa waliomwita Magret Thatcher Iron lady kwa sababu ya siasa zake dhidi ya nchi maskini na pengine niseme Reagan apewe sifa zaidi kwa kueneza sera za BUY AMERICAN brand nyumbani wakati wao wanauza mali nje. UKikataa kuitamvua Israel unawekwa ktk kundi la black list hata kama!..yaani miaka ya 70 SIASA ilichafua nchi zote za KIJAMAA kama unavyoona leo ktk nchi za KIARABU.. Huwezi kusema Mfalme wa Saudia ni mzuri ama ana sera nzuri kuliko AhmadinaJad wa Iran pasipo kuzingatia jinsi siasa zinavyotumika kudhoofisha uchumi wa nchi moja na nyingine kukua japo hawana sera nzuri wala Utawala bora.

Will always stand with Mwalimu Nyerere, sema tu nakubali kwamba alifanya makosa makubwa sana kukabidhi nchi kwa wahuni, Nyerere alikuwa na mapungufu makubwa ktk kuwasoma WANAFIKI na malimbukeni hasa baada ya kuingia UBEPARI maana hatukuuzsoma kaa tulivyouzoma UJAMAA..Na ssidhani kaa hadi leo kuna mwanasiasa yeyote nyumbani amewahi kuandika kitabu kuhusu UBEPARI na ukafundishwa mashuleni kama tulivyosoma UJAMAA..Sasa nambieni nyie wasomi uytaweza vipi ku apply elimu zenu ktk somo ambalo hamkulisoma na kujua jinsi mazuri ya UBEPARI na jinsi utakavyo fanya kazi zaidi ya kujua UBAYA wake tu kulingana na mafundisho ya UJAMAA?
 
Last edited by a moderator:
Nguruvi3 hebu nisaidien jambo hapa mimi naona hata hawa skilled labour force iliyopo kwa miakam hii 30 ni hovyo kabisa manake badala ya kukuza nchi tumefifisha nchi.

kwanza labda Zakumi aseme je kwasasa hivi nchi yetu kama ilivfyo inasafirisha nini nje ya nchi kama bidhaa?? je sisi kama nchi tuna viwanda gani ambavyo vinaweza kukompete na vyenye mnitaji mikubwa?

hivi kuuza juice na maziwa na ice cream ndicho ambacho tunakitegema as a nation?? hivi kuuza sigara na bia ndo kitu pekee for 30yrs kweli??

Nauliza swali kwann leo hii hatuna BORA kile kiwanda cha viatu ambacho kilikuwa kinatumia ngozi za tanarries?? hvim kuh=na sababu ya mtanzania wa leo kuvaa mtumba kiatau licha ya kwamba klila siku idadi kubwa ya ng'ombe na mbuzi, swala wanachinjwa?

ipo wapi sababu ya mtu kutumia malindi salt licha ya uvunza yetu kuwa na uwezo wa kutoa chumvi ya kutosha?

nauliza ipo wapi sababu ya kuagiza daftari toka Kenya licha ya KIBO paper kuwepo?

ipo wapi sababu ya kuagiza tiles na gypsum toka nje ilihali gypsum powder ipo hapo bagamoyo na tanga??

kuna haja gani ya kutumias spanmish ama italian tiles ilihali tunazo tanga stones na montemorillonite clay?? tunayo ceramic powder kweli tuagize vigae nje?? baada ya miaka 50 ya uhuru?? unless tuko wapumbavu na kuna watu wanafurahia upumbavu wetu na yumkini ndio maana tumekuja na kipengele kwamba hakunaga mtu anayepata sifuri tukafuta div 0 na kukubali kuwa nchi ya kwanza duniani yenye alama ndozo kabisa za ufaulu.

hivi kwa ukubwa wa eneo la bahari tulio nao kweli kuna haja ya sisi kuwa hapa tullipo?? marine scientist can tell tuna kiasi kikubwa sana marine resources nyingi sana, kila siku meli za kichina zinaondoka na pearls sasa hivi kwan sisi hatuhitaj hizi pearls?? nani amewah kusemea hili jamani nyie hamjui tu lkn ukweli ni the most expensive kito cha kwenye maji na huuzwa kwa thaman kubwa sana lkn sasa sisi tuko kimyaa wachina wanaenda kutengeneza na kuuza ulaya imekuwa kama enzi zile za watu kuchezea almasi mdako?? baada ya miaka 30 ya tunao waita wenye sera nzuri??
gfsonwin , kuna mambo nimeacha hata kuhoji kwasababu kila nikiuliza sipewi majibu yanayolingana na maswali.

Kuhusu hoja zako, nimeahi kuuliza hivi hawa wasomi tulio nao wamefanya nini ambacho tukiweka katika mizani tunaweza kuona tofauti kati ya sasa na zamani. Hakuna jibu.
Nimehoji kama sera za mwal kuhusu viwanda zilikuwa mbovu, zipi za sasa ambazo ni mbadala mzuri. Hakuna jibu

Nimehoji unawezaje kuuza pamba ikiwa na magugu ili hali huna hata 'jineri' za kusafisha hiyo pamba? Nikajibiwa tuuze malighafi tu. Nikahoji hivi mchanga unaosafirishwa nje ndio uuzaji wa mali ghafi, hakuna jibu.

Nimehoji kama mwalimu alikosea kuanzisha viwanda na waliofuata wakaamu kuuza, nini matokeo ya uuzwaji wa viwanda hivyo? Je, kuvigawa viwe maghala ya chumvi ndio njia bora kuliko kile kilichofanyika, hakuna jibu.

Tunapoangalia viwanda tunaangalia katika monetary value na kusahau faida nyingine zitokanazo.
Hata kama pato lilikuwa dogo kuliko misaada, sasa hivi ni miaka 30 tangu amendoka Mwl na miaka 50 ya uhuru ,kuna tofauti gani ya misaada ? Na je ile 10% ya viwanda vya mwl inapatikana wapi kwa sasa?
Au ndio kuweka kodi kwa vocha za simu kukifanwya na maprofesa ndio uchumi endelevu baada ya mwalimu!

Hapa pia pana underline hoja ya skilled labor inayohitajika na ni sehemu ya uchumi. Je, tunahitaji skilled labor kama ya kuchaji kodi katika vocha ya simu. Hivi miaka 30 tangu mwl aondoke hakuna anayefikiria chanzo kingine cha kodi zaidi ya sigara, bia na vocha za watoto wa sekondari! ndio skilled labor tofauti na ya mwl hiyo.

Nikirudi katika viwanda, maendeleo ya jamii yalitegemea sana viwanda vya mwl. Mji wa Mang'ula kama mfano ni matokeo ya viwanda.

Mwanza ilijengwa sana na Mwatex kwa 'trickle down effect' kuanzia kiwandani hadi kwa mkulima.
Mji kama wa Moshi ulikuwa 'live' 24 hr kwa treni kufanya kazi za kuchukua na kupeleka bidhaa.

Morogoro imekuwa kwa viwanda kama Maturubai, Polyster n.k. Arusha ilikuwa vivyo hivyo.
Dar watu walikuwa na shift work siku hizi baada ya 11 jioni ni viti virefu. Nani utamsikia amekwenda shift.

Enzi hizo wanafunzi walikwenda katika viwanda kufanya tempo.
Lakini kubwa zaidi ni wanafunzi kupata uzoefu wa kuingia katika labor force wakiwa na nidhamu za kazi.

Siku hizi mwanafunzi wa chemical engineering au mechanical sijui anafanya internship au field work wapi.
Hata wale wa utawala na uongozi, wahasibu n.k wamebaki kukimbizana katika serikali na kujifunza bureacracy na si skilled labor kama wanavyodai.

Tumeua general tyre na sasa tunaagiza matairi ya mitumba kutoka Uarabuni. Kama ni mapya ni kutoka China, wakati zao la mpira linakufa Tanga. Huo ndio tunaita usomi wa kileo na kuuza malighafi nje. Ipi hiyo?

Niseme impact ya viwanda ukiiweka katika pesa tu huwezi kuiona. Ukiiweka katika uchumi na kijamii ni kubwa kuliko tunavyodhani. Hatuwezi kuona faida hizo kwasababu tume ji tune kumtuhumu na kumhukumu mwl tukisoma karatasi kwa makengeza tena tukiruka kurasa. mwisho tunasema 'verdict- mwalimu is guilty of all 400 counts'

Tukiuliza wapi mbadala ili tuweze kupata hukumu ya haki kwa mwalimu, tunajibiwa ' hiyo si kazi yetu' kazi yetu ni kuonyesha makosa ya 'mhaini' Nyerere.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Mchambuzi napitia hoja za bandiko lako #124 kuhusu kodi kidogo.
Kwamba kuna injustice tax system in Tanzania, hilo halina mjadala. Anayelipa kodi Tanzania ni yule asiyeweza kukwepa kama wafanyakazi wa serikali, wafanyabiashara wenye shughuli za uzalishaji n.k.

Injustice inatokana na tax evasion ambayo ni zao la corruption na irresponsible government.
Wanaofaidika ni wafanyabiashara ambao hutegemewa kupeleka kodi tofauti na anayechinjwa katika pay slip.
Mfanyakazi anabeba mzigo wote wa tax evasion na tax exemptions ambazo zote hazijaleta tija kwa nchi.

Namtetea Mtanzania anayeona kodi ni pesa za serikali. Hivyo ndivyo ilivyo kwasababu mtanzania wa kawaida haoni kodi yake inafanya nini.

Hakuna mahali anapoweza ku justify matokeo ya kodi yake. Ukienda vijijini watu wanasema tutafute mfadhili wa kufanya ABC. Wanaamini anayesaidia japo kuziba mashimo ya bara bara ni mfadhili na si serikali yao.

Namtetea Mtanzania kwasababu inapotokea bilioni 27 zikatoka hazina na serikali haijui zimetokaje na nani ametoa, kuna sababu gani za kudhani kodi anayolipa mtu inahifadhiwa na kutumika kama ilivyo kusudiwa?

Ili kundilisha mtazamo wa wananchi kuhusu kodi ni lazima waone zinafanya kazi gani katika 'public goods'
Sidhani kuwa kuna sababu za progressive tax rate.

Tatizo lipo katika corruption na irresponsible government.
Kwanini tuwe na progressive tax rates tukisahau embezzlement and mismanagement inayotaokana na serikali.

Kuna sababu gani za kuweka kodi zaidi kwa wealthier wakati kodi hizo zinatoka hazina hadi Uingereza bila mtu kujua na hata zinaporudi hakuna anayejua zimerudishwa vipi.

Kuna sababu gani ya kuweka progressive tax rate itakayotupatia billion 500 wakati kuna tax evasion bandarini inayokadiriwa kuwa 1.8 trillion.

Hoja hapa ni kuwa kwanini tukazane kujaza ndoo maji wakati tunajua inavuja.
Je si vema kuanza kuziba kwanza!

Kuhusu serikali kuja na mikopo laini kusaidia wanafunzi, hili nasema ni 50/50.
Linaweza kuwa kama la mabilioni ya JK ambayo sijui kama yametoa matokeo yoyote ya kiuchumi.

Nadhani serikali ingeshirikiana na taasisi ku identify potential area ambazo zikipewa mikopo zinaweza kuwa exemplary and sustainable

Kwa mfano, kwanini serikali isiachie taasisi zijiendeshe zenyewe huku ikitoa mikopo laini.
Nakumbuka Kibaha education centre ilikuwa mfano mzuri sana wa shughuli za ujasiria mali.
Kwa bahati mbaya ilikuwa ni sehemu ya serikali na hivyo kuwa katika bureaucracy ndio maana haifanyi vizuri.

Kwanini,Mlingano Tanga, Ukiliguru, Uyole, Naliendele zisiwe taasisi nje ya serikali na zikapewa kazi ya kuendeleza kilimo kwanza kwa mifano huku serikali ikijenga mazingira ya kufanikisha miradi hiyo bila kujiingiza katika uendeshaji wake.

Katika nchi za wenzetu research and development zinafanywa na taasisi .
Hata kama kutatoke individuals bado wanatakiwa wategemee taasisi katika kujiendeleza.

Kilichotakiwa kufanywa ni serikali kuwatumia wataalamu na taasisi zao kuja na policy ambazo zinafanya kazi zikiwa na planning, orientations, pilot studies na verifications.

Waambie SUA kuwa tunahitaji kilimo kwanza. Nini kifanyike, kwa njia zipi, changamoto ni zipi na wapi serikali isaidie kwa maana inapobidi. Halafu wape jukumu ukisubiri matokeo 'big results'
Anayeshindwa anawekwa pembeni.

Sidhani kama kilimo kwanza ni suala la mtu kusimama bungeni na kusema tu.
Matokeo ya mipango hiyo hovyo ni kuingiza matrekta substandard, kuwapa watu bila elimu au uwajibikaji kwasababu ni mali ya umma n.k.
 
Last edited by a moderator:
Wakuu nimepata kipande hiki kutoka gazeti la the Citizen.
Mkapa, Mogae na Obasanjo wakizungumza.

Haya ni baadhi ya maneno ya Mogae ambayo tumeyajadili huko mwanzo kama mada ya Mchambuzi inavyoeleza.

Citing his country, Mr Mogae noted that many African countries have failed to benefit from their immense mineral resources because they did not plan from the word go.


"When we discovered minerals we decided to talk and agree on what we were going to do with revenue from the resources," he added.


"We agreed that the revenue should be used for national development.
We even singled out areas which should be financed using the income from minerals."


After making decisions and plans, the leaders were all committed to ensuring that the decisions and plans were implemented to the later.
 
Back
Top Bottom