Uchumi wa Tanzania: Je, Ni Kitendawili au Ni Mazingaombwe Kwa Maskini?

Uchumi wa Tanzania: Je, Ni Kitendawili au Ni Mazingaombwe Kwa Maskini?

JLF;

Nimeikubali posti yako na hususa ujumbe wa kubadili attitudes za wabongo. Attitude ya sasa ya kuamini kuwa serikali is a gigantic enterprise with unlimited resources ni lazima iondoke. Serikali ni lazima ifanye vitu inavyoweza kuvifanya kwa ufanisi. Kuiongezea serikali mamlaka katika shughuli ambazo haina uwezo nao kwa kisingizio cha kufuta umasikini ni kujiongezea umasikini.

Tukirudi kwenye majibu ya hoja zangu, kuna alternatives. Lakini kila kitu kina gharama zake. Moja ya alternatives ni kutumia mikopo. Nchi inaweza kutumia mikopo kutoka nje kujenga viwanda. Na baadhi ya viwanda vilivyojengwa kati ya 60-80 vilitumia mikopo. Matatizo ya mikopo ni kuongeza deni taifa. Viwanda vinaposhindwa kutimiza majukumu yake ya kurudisha pesa, ulipaji wa madeni na riba unaweza kuiletea nchi umasikini.


Alternative nyingine ni kutumia misaada ya kutoka nje. Misaada mingi ina masharti yake. Na vilevile tukumbuke kuwa wahisani wana watu wengi wa kuwasaidia. Cha muhimu zaidi kuhusu misaada ni donor fatique. Nchi za scandinavia zilitusaidia, lakini zilipochoka zilianza kutushinikiza kufanya reforms.

Mara nyingi hapa tunatoa mifano ya maendeleo ya viwanda ya China na South Korea. Nchi hizi na zingine za Asian Tiger zilikuwa zinategemea sehemu ndogo ya misaada kutoka nje (2%). Na vilevile hawakuwa na uwiano mbaya wa madeni kutoka nje. Hivyo shinikizo la kutoka nje linakuwa dogo.

Hivyo kwa maoni yangu binafsi si vibaya nchi kuanza kwa kutumia resources zake kwanza. Japokuwa mapato yanaweza yasiwe makubwa, matumizi mazuri ya kipato hicho yataleta mafanikio baadaye. Chukua mfano wa Tanzania. Kwa zaidi ya miaka 30 tuna mashule mengi ambayo hayana waalimu wazuri au wa kutosha. Haya ni matumizi mabaya ya kile kidogo tunachopata. Hii ni kwa sababu wahitimu wa shule hizo hawana manufaa ya kuleta mabadiliko.
Zakumi ni ngumu sana mtu kukuelewa unasimamia wapi katika hoja, samahani kusema hivyo.

Kwanza, umeungana na baadhi yetu kwa kusema serikali itoe nafasi kwa sekta nyingine kuchangia uchumi. Ukisoma bandiko la mwanzo kabisa la Mchambuzi hicho ndicho alichokisema. Akauliza je tutumie mkakati gani katika kuinua uchumi? Inward looking au outward looking. Tena kuna mahali ameta private sectors na SME kwa maana ya nje ya serikali

Ukisoma bandiko nililochangia kuhusu hoja hiyo nikasema serikali ijitoe katika utendaji lakini ijenge mazingira mazuri ya private sectors kutekeleza majukumu yake. Nikasema hakuna sababu serikali ikashiriki katika kutangaza utalii, kinachotakiwa ni serikali kuandaa mazingira ya wadau wa sekta husika kushiriki katika kutangaza utalii.

Lakini serikali haiwezi kujitoa kabisa katika majukumu yake. Mfano, balozi zetu zinaweza kutumika kutoa taarifa za maonyesho ya utalii au maeneo yenye potential za kukuza utalii. Serikali iwasiliane na wadau kwa kuwapa fursa kushiriki na kutangaza utalii.

Pamoja na hayo ili private sector ifanye vema lazima kuwe na incentives kwasababu compettition haitegemei maarifa inatgemea mazingira pia. Kwanini tutoe tax break kwa makampuni ya madini tushindwe kutoa tax break kwa kampuni zitakazotangaza utalii na kweli kufanya hivyo. Je hapo serikali haina jukumu.

Zakumi nadhani unajenga hoja za nguvu na siyo nguvu za hoja. Kama ungefuatilia vema historia ungegundua kuwa miradi mingi iliyofanyika kati ya 60 na 70 ilikuwa misaada kwa kuzingatia kuwa kipindi hicho kilikuwa post independence na nchi nyingi zilishiriki.

Kwa viwanda vilivyojengwa kwa mikopo, mikopo hiyo ilikuwa na masharti nafuu na mingi ilirudishwa mapema sana. Mfano, Mchina alijenga Urafiki, mfaransa akajenga Mutex. Kibaha education ilijengwa na msaada, kama ilivyo reli ya Tanga-Dar n.k.Nimeyaona haya.Hivyo hoja yako kuhusu mikopo ya 60 na 70 haina mantiki.

Na mwisho umetuunga mkono tena kwa kusema tutumie rasilimali zetu kuanza kujenga uwezo wetu. Wote wamesema hilo na Mchambuzi kasema je kuna haja ya specialization ya maeneo ya uchumi? Nilichangia kwa kusema ipo na itasaidia kuejenga uwezo wetu hata kuwa na viwanda.
Nikasema kama tuna kipaumbele kuwa fedha za madini ziwekezwe katika elimu, fedha zitokanazo na gasi ziwekezwe katika miundo mbinu na tuongeze mazao ya biashara na chakula, upo uwezekano wa kujenga uwezo wenyewe. Hoja hiyo ndiyo waliochangia akina gfsonwin na zumbemkuu kuwa elimu ni sehemu ya uchumi.

Basically unakubaliana na hoja nyingi sijui wapi lakini kuna wakati unageuka kama nitakavyokuonyesha bandiko lifuatalo
 
Last edited by a moderator:
Nguruv3;Nimejibu maswali yenu mara nyingi. Nimesema kuwa alichofanya Nyerere wasn't unique. Kilifanyika katika nchi nyingine pia. Zaire, Kenya, Zambia na hata Idd Amin wa Uganda alikuwa na mashirika ya umma. Kuanzisha viwanda ilikuwa ni fashion ya wakati huo. Hivyo basi hata mimi, wewe, mchambuzi, mkandara, kichuguu n.k tungekuwa madarakani, tungefanya vile alivyofanya Nyerere.

Katika miaka ya 60 na 70 kulikuwa hakuna ndondoo na wasomi waliobobea kuhusu uchumi wa nchi za kiafrika.

Hivyo watu walijaribu vile walivyoona vinafaa. Sasa hivi ni zaidi ya 50 toka Tanzania ipate uhuru na ku-data zinazoweza kutumika kujenga sera nzuri za kuleta maendeleo. Miaka ya leo tunajua ni kitu kifanywe na serikali na kitu gani kiwe mikononi mwa watu binfasi.
Katika aya ya kwanza unakubali kuwa hakuna njia nyingine tofauti ambayo wewe ungefanya zaidi ya aliyofanya Mwalimu. Ndiyo maana nasema hukujibu swali kwasababu hukutoa alternative.
Hapa nadhani unaongozwa pengine na hisia binafsi dhidi ya Nyerere kwasababu kwa kutumia facts na data huna.

Lakini pia umepotosha kwa kusema viongozi wa wakati huo walifanya mambo kwa fashion. Ni kipindi hicho tulishuhudia miundo mbinu ikijengwa kama bara bara, reli kubwa nchini, mabwa ya umeme na viwanda. Katika hayo yote hakuna, narudia hakuna serikali iliyofuata imefanya hata robo yake. Hakuna kilichofanywa na serikali ya Mwinyi, Mkapa na Kikwete kufikia hata nusu ya hayo.

Hapa nakuja na data na swali. Mwalimu alijenga reli ya Tanga-Dar, reli ya Tazara, akamimarisha reli ya kati wakati ile ya Arusha-moshi na Moshi Voi zikifanya kazi kama kawaida. Mwalimu alijenga barabara ya Segera-Chalinze na nyingine amabzo hazikuwepo wakati wa mkoloni.

Mabwawa ya kuzalisha umeme yalijengwa, vyuo vikuu na shule za sekondari pamoja na kuhakikisha kuwa vituo vya Afya zaidi ya 300 vikijengwa na kila kimoja kikiwa na huduma muhimu kama magari.
Viwanda na mashirika aliyoacha ni zaidi ya 400.

Hiyo ni mifano michache sana. Sasa niambie kuwa katika kipindi cha awamu ya pili, tatu na nne serikali imejenga mazingira gani ambayo unaweza kuchukua mifano hapo juu na kusema ni zaidi ya 60 na 70.
Na je hayo aliyoyafanya mwalimu yalikuwa ni fashion! kuna fashion ya kujenga mabwawa ya kuazalisha umeme au miundo mbinu kweli.

Lakini pia uende mbali na kutueleza kwa miaka ya sasa kuna wasomi. Katika miaka 10 iliyopita nitajie jambo moja unaloweza kusema limefanywa kisomi kuliko yale ya 60 na 70. Jambo moja tu.
 
@Zakumi ni ngumu sana mtu kukuelewa unasimamia wapi katika hoja, samahani kusema hivyo.

Kwanza, umeungana na baadhi yetu kwa kusema serikali itoe nafasi kwa sekta nyingine kuchangia uchumi. Ukisoma bandiko la mwanzo kabisa la Mchambuzi hicho ndicho alichokisema. Akauliza je tutumie mkakati gani katika kuinua uchumi? Inward looking au outward looking. Tena kuna mahali ameta private sectors na SME kwa maana ya nje ya serikali

Ukisoma bandiko nililochangia kuhusu hoja hiyo nikasema serikali ijitoe katika utendaji lakini ijenge mazingira mazuri ya private sectors kutekeleza majukumu yake. Nikasema hakuna sababu serikali ikashiriki katika kutangaza utalii, kinachotakiwa ni serikali kuandaa mazingira ya wadau wa sekta husika kushiriki katika kutangaza utalii.

Lakini serikali haiwezi kujitoa kabisa katika majukumu yake. Mfano, balozi zetu zinaweza kutumika kutoa taarifa za maonyesho ya utalii au maeneo yenye potential za kukuza utalii. Serikali iwasiliane na wadau kwa kuwapa fursa kushiriki na kutangaza utalii.

Pamoja na hayo ili private sector ifanye vema lazima kuwe na incentives kwasababu compettition haitegemei maarifa inatgemea mazingira pia. Kwanini tutoe tax break kwa makampuni ya madini tushindwe kutoa tax break kwa kampuni zitakazotangaza utalii na kweli kufanya hivyo. Je hapo serikali haina jukumu.

Zakumi nadhani unajenga hoja za nguvu na siyo nguvu za hoja. Kama ungefuatilia vema historia ungegundua kuwa miradi mingi iliyofanyika kati ya 60 na 70 ilikuwa misaada kwa kuzingatia kuwa kipindi hicho kilikuwa post independence na nchi nyingi zilishiriki.

Kwa viwanda vilivyojengwa kwa mikopo, mikopo hiyo ilikuwa na masharti nafuu na mingi ilirudishwa mapema sana. Mfano, Mchina alijenga Urafiki, mfaransa akajenga Mutex. Kibaha education ilijengwa na msaada, kama ilivyo reli ya Tanga-Dar n.k.Nimeyaona haya.Hivyo hoja yako kuhusu mikopo ya 60 na 70 haina mantiki.

Na mwisho umetuunga mkono tena kwa kusema tutumie rasilimali zetu kuanza kujenga uwezo wetu. Wote wamesema hilo na Mchambuzi kasema je kuna haja ya specialization ya maeneo ya uchumi? Nilichangia kwa kusema ipo na itasaidia kuejenga uwezo wetu hata kuwa na viwanda.
Nikasema kama tuna kipaumbele kuwa fedha za madini ziwekezwe katika elimu, fedha zitokanazo na gasi ziwekezwe katika miundo mbinu na tuongeze mazao ya biashara na chakula, upo uwezekano wa kujenga uwezo wenyewe. Hoja hiyo ndiyo waliochangia akina gfsonwin na zumbemkuu kuwa elimu ni sehemu ya uchumi.

Basically unakubaliana na hoja nyingi sijui wapi lakini kuna wakati unageuka kama nitakavyokuonyesha bandiko lifuatalo

Nguruv3:

Msimamo wangu ni kusema kuwa Tanzania ina nafasi ya kuendelea kwa kutumia vizuri opportunities zilipo na kutumia common sense.

Katika msimamo huu sikubaliani na hoja kuwa sera zilizotumia 60, 70, na 80 zilikuwa katika trajectory ya kuiendeleza nchi. Ingawaje sera hizo zilikuwa na nia nzuri zilikuwa na mapungufu makubwa ya kiufundi. Hazikufaa miaka iliyopita na hazifai kwa miaka ya sasa (period). Naomba utofautishe nia nzuri na njia za kiufundi za kutekeleza nia hizo.

Wapo wanaotetea sera hizi kwa kutumia mifano ya China na South Korea. Majibu yangu ni kuwa conditions zilizopo China na Korea hazipo Tanzania.

Kuhusu matumizi ya rasilimali kuna tofauti kubwa. Wapo wanaosisitiza vijengwe viwanda ku-process rasilimali hili kuongeza thamani. Wanaona kuwa serikali ina nafasi ya kuweka sera ya kujenga viwanda hivyo kama alivyofanya Nyerere.

Kwa upande wangu sera za Nyerere hazina nafasi katika maendeleo ya viwanda. Zilipewa nafasi but they failed. Vilevile naamini kuwa kipato kidogo cha rasilimali sio kikwazo cha maendeleo ya Tanzania. Matatizo ya Tanzania ni matumizi mabaya ya kile kidogo nchi inachokipata. Kwa mfano mfumo wa elimu hauonyeshi kuwa tuna nia ya kujitoa kwenye umasikini.
 
Katika aya ya kwanza unakubali kuwa hakuna njia nyingine tofauti ambayo wewe ungefanya zaidi ya aliyofanya Mwalimu. Ndiyo maana nasema hukujibu swali kwasababu hukutoa alternative. Hapa nadhani unaongozwa pengine na hisia binafsi dhidi ya Nyerere kwasababu kwa kutumia facts na data huna.

Lakini pia umepotosha kwa kusema viongozi wa wakati huo walifanya mambo kwa fashio. Ni kipindi hicho tulishuhudia miundo mbinu ikijengwa kama bara bara, reli kubwa nchini, mabwa ya umeme na viwanda. Katika hayo yote hakuna, narudia hakuna serikali iliyofuata imefanya hata robo yake. Hakuna kilichofanywa na serikali ya Mwinyi, Mkapa na Kikwete kufikia hata nusu ya hayo.

Hapa nakuja na data na swali. Mwalimu alijenga reli ya Tanga-Dar, reli ya Tazara, akamimarisha reli ya kati wakati ile ya Arusha-moshi na Moshi Voi zikifanya kazi kama kawaida. Mwalimu alijenga barabara ya Segera-Chalinze na nyingine amabzo hazikuwepo wakati wa mkoloni.

Mabwawa ya kuzalisha umeme yalijengwa, vyuo vikuu na shule za sekondari pamoja na kuhakikisha kuwa vituo vya Afya zaidi ya 300 vikijengwa na kila kimoja kikiwa na huduma muhimu kama magari.
Viwanda na mashirika aliyoacha ni zaidi ya 400.

Hiyo ni mifano michache sana. Sasa niambie kuwa katika kipindi cha awamu ya pili, tatu na nne serikali imejenga mazingira gani ambayo unaweza kuchukua mifano hapo juu na kusema ni zaidi ya 60 na 70.
Na je hayo aliyoyafanya mwalimu yalikuwa ni fashion! kuna fashion ya kujenga mabwa ya kuazalisha umeme au miundo mbinu kweli.

Lakini pia uende mbali na kutueleza kwa miaka ya sasa kuna wasomi. Katika miaka 10 iliyopita nitajie jambo moja unaloweza kusema limefanywa kisomi kuliko yale ya 60 na 70. Jambo moja tu.

Nguruv3;

Ni kiongozi gani wa kiAfrika hakufanya vitu hivyo? Katika kipindi hicho Tanzania was one of the top recipients of foreign aid in sub-saharan Africa. If you want to thank, thank Western Countries and Chinese for doing a wonderful job helping Tanzanians. Without them the country would haven't survived. For example, the health care system and clean water projects were the work of foreign donors. When they stopped everything went down the drain.

Ukisema Nyerere alijenga hiki au kile, you are atalking about 20% of the process. Why don't you tell me about 80% of the process which entails the operational and maintanaince of the process?

Take for example Mufind Paper Mills. Your friend Mchambuzi says that the costs of developing the project was $220 Milion. At the end the country didn't get what it bargained for.

In term of Ujenzi wa Taifa, Tanzanian is a laughing stock.
 
Mchambuzi;


Asante sana kwa kunirahishia maisha. Sera kubwa za ujenzi wa viwanda zilikuwa kwenye concept uliyoitaja - "why import paper wakati it can be produced locally"?

This was the driver. Tulitaka kujitosheleza kwa kila kitu.
We wanted to produce everything locally without understanding business and economic imperatives.

Nilishakueleza katika posti zilizopita kuwa. Viongozi wa nchi na wanachumi wanafungua viwanda kUkidhi hoja za kiuchumi. Lakini uendeshaji wa viwanda unafanywa na business administrators au businessmen kukidhi hoja za kibiashara.

Working temperaments za wachumi au wanasiasa wanaokidhi hoja za kiuchumi ni tofauti na zile za business administrators au businessmen.

In business world "WHY IMPORT, IT CAN BE PRODUCED LOCALLY" isn't a business imperative. Vilevile, viongozi wa nchi wakishatia saini mkataba tayari wamekubali. Hivyo hakuna kisingizio kama hayo yalikuwa sio makosa yao.
Kwanza nikufahamishe kuwa unajenga hoja kwa mtazamo wa kumtuhumu Nyerere na siyo facts.
Umedai pesa nyingi zilitumika kujenga viwanda na hivyo huduma za miji kama kuzoa taka zikazorota. Not true !

Kama hilo ni kweli, kwanini usiseme pesa nyingi zilitumika kujenga miundo mbinu na kuathiri huduma za miji?
By the way kilichoua huduma za miji siyo viwanda, ni siasa ya kuvunja local authority na kuziweka chini ya serikali kuu.

Pamoja na hayo miaka ya 60 na 70 tulikuwa na mazao makuu ya biashara kama mkonge, pamba.
Ukiangalia vigezo vya uchumi utaona kimojawapo ni nguvu ya pesa ukilinaganisha na sarafu nyingine.

Unafahamu jina dala dala limetokana na nini au sh 20 kuitwa pauni(mbau) imetokana na nini.
Ukiangalia na sasa ambapo unasema tuna wachumi kwa kweli inasikitisha.
Hivi kuna wachumi gani wa kukaa na kufikiria vyanzo vya mapato kama vocha za simu, sigara na bia?

Na mwisho kabisa, bandiko lililotangulia umesema hakukuwa na namna ambavyo Nyerere angefanya tofauti kama watu wengine ukiwemo.

Sasa hapa unasema kwavile alikuwa 'signatory hayo ni makosa'.
Makosa yapi ambayo wewe umeshindwa kutuambia ungefanya nini tofauti na yeye?
Hujaweza kusema hata sentensi ushujaa wa kusema ni makosa unaupata wapi.

Nadhani tujikite katika ukweli, hoja na takwimu kuliko chuki kwa mtu. Waganda hawampendi Amin lakini wanapenda sera yake ya uzawa. Ujerumani wanaangalia miaka 60 nyuma wanahoji ubaya wa Hitler kwa misingi yake ya kuwajibika uko wapi?
 
Nguruv3:

Msimamo wangu ni kusema kuwa Tanzania ina nafasi ya kuendelea kwa kutumia vizuri opportunities zilipo na kutumia common sense.

Katika msimamo huu sikubaliani na hoja kuwa sera zilizotumia 60, 70, na 80 zilikuwa katika trajectory ya kuiendeleza nchi. Ingawaje sera hizo zilikuwa na nia nzuri zilikuwa na mapungufu makubwa ya kiufundi. Hazikufaa miaka iliyopita na hazifai kwa miaka ya sasa (period). Naomba utofautishe nia nzuri na njia za kiufundi za kutekeleza nia hizo.

Wapo wanaotetea sera hizi kwa kutumia mifano ya China na South Korea. Majibu yangu ni kuwa conditions zilizopo China na Korea hazipo Tanzania.

Kuhusu matumizi ya rasilimali kuna tofauti kubwa. Wapo wanaosisitiza vijengwe viwanda ku-process rasilimali hili kuongeza thamani. Wanaona kuwa serikali ina nafasi ya kuweka sera ya kujenga viwanda hivyo kama alivyofanya Nyerere.

Kwa upande wangu sera za Nyerere hazina nafasi katika maendeleo ya viwanda. Zilipewa nafasi but they failed. Vilevile naamini kuwa kipato kidogo cha rasilimali sio kikwazo cha maendeleo ya Tanzania. Matatizo ya Tanzania ni matumizi mabaya ya kile kidogo nchi inachokipata. Kwa mfano mfumo wa elimu hauonyeshi kuwa tuna nia ya kujitoa kwenye umasikini.
Bado hujibu hoja Zakumi. Endapo kila alilofanya Nyerere kila kiongozi amefanya nimeuliza kwa kujumlisha maraia watatu ambao kila mmoja 'anafanya kama Nyerere' kuna kitu gani ambacho kwa pamoja(Mkapa, Mwinyi na Kikwete) wamekifanya kwa kulinganisha na sera za uchumi za Nyerere ambacho ni zaidi?
Usisahau kuwa wao walianzia tayari kukiwa na misingi, je wametumia adavantage hiyo vipi kuzidi sera za 60 na 70.

Halafu usishau kuwa hakuna anayesema serikali ijenge viwanda. Kinachosemwa hapa ni kuwa hatuwezi kuwa nchi isiyo na sera au utaratibu. Tumesema serikali haiwezi kuivua jukumu la kutengeneza mazingira mazuri ya kukua uchumi.
Marekani wanatoa incentives kwa wenye viwanda kuviondoa China. Kumbuka hawa ndio mabepari namba 1.

Tunakubaliana kuwa sera za miaka 60 na 70 hazina nafasi. Usichotueleza ni kuwa kitu gani tofauti kifanyike sasa hivi. Mchambuzi katika mada yake ameuliza, je tunahitaji inward looking au outward looking na kwasababu zipi.
Utakapotueleza tunahitaji nini hapo utakuwa umetufunga tusikuulize kama zile za 60 na 70 ni mbaya nzuri za 2013 kulikosheheni wasomi ni zipi.
 
Last edited by a moderator:
Nguruv3;

Ni kiongozi gani wa kiAfrika hakufanya vitu hivyo? Katika kipindi hicho Tanzania was one of the top recipients of foreign aid in sub-saharan Africa. If you want to thank, thank Western Countries and Chinese for doing a wonderful job helping Tanzanians. Without them the country would haven't survived. For example, the health care system and clean water projects were the work of foreign donors. When they stopped everything went down the drain.

Ukisema Nyerere alijenga hiki au kile, you are atalking about 20% of the process. Why don't you tell me about 80% of the process which entails the operational and maintanaince of the process?

Take for example Mufind Paper Mills. Your friend Mchambuzi says that the costs of developing the project was $220 Milion. At the end the country didn't get what it bargained for.

In term of Ujenzi wa Taifa, Tanzanian is a laughing stock.
80 pere cent ya maintenance na operation inaingaiaje kwa sera za wakati huo? Nyerere akiondoka madarakani ameacha mashirika na viwanda zaidi ya 400. Je, waliofuata walifanya nini katika maintenance na operational process?

Mufindi imekufa kwasababu viongozi waliofuata hawakufuata taratibu za ubinafsishaji.
Mbona shamba la Sao hill bado lipo na linatoa malighafi kwa mazao yake kwa viwanda vingine.

Lakini basi utueleze kuwa kipi bora Mang'ula iliyokuwa inasuasua au Mang'ula iliyogezwa kuwa ghala la chumvi.
Huo ndio uwekezaji au ndio mtazamo wa kisomi wa kuendeleza uchumi?
Nani amebinafsisha Mang'ula na kwanini asifanye maintanance na operational tofauti na ile iliyo feli.


Miaka 30 sasa hebu njoo hapa utueleze kuhusu sera za uchumi ambazo unadhani zimefanikiwa kuliko miaka ya 60 na 70 au za Nyerere the least to say
.
 
Zakumi,

Hapo juu, kwa maana nyingine, unakubali kwamba Mwalimu was correct on the drawing board, failure ilikuwa kwenye utekelezaji - unakubali hili by eventually saying kwamba nia ilikuwa ni nzuri, tatizo ni suala zima la ufundi na utaalam;Katika hili, Nguruvi3 amejadili utaalam kwa wakati ule na kuhoji alternative solution, haujaja na jibu bado, which means there was no alternative solution, right? Kumbuka: It has been argued na wanazuoni kadhaa nje ya nchi kwamba kwamba the best way to measure the sucess ya mwalimu ni kwa kuangalia how much convinced wananchi na donors kwamba alikuwa na nia ya dhati ya kuliendeleza taifa lake licha ya changamoto zilizokuwepo wakati ule (hasa nchi yetu kuanza at a very low economic base tofauti na nyingine nyingi na pia uwepo wa vita vya baridi duniani), lakini licha ya hayo, kuelekea end of cold war, aliliacha taifa likiwa na modest level of development and intact in terms of socil and political coherence and stability;

Pia unajadili jinsi gani miradi ilifeli, kwa kutumia mfano wa mufindi pulp and paper factory;ukumbuke kwamba sio kila industrial project ilifeli, mufindi was one of the few white elephant projects engineered na World Bank na such projects zilikuwa na nyingi Africa; Sasa unapolaumu uamuzi wa viongozi ku-sign for such projects, and at the same time unakubali hapakuwa na wataalam wazawa wa kutosha kufanya appraisals n.k, huku ukiwa hauna maelezo ya alternative solutions unatuacha njia panda;

Tatu unasema Katika suala la ujenzi wa taifa, Tanzania is a laughing stock; Siamini umesema maneno haya kwani karibia literature yote iliyopo kuhusu Tanzania and nation buidling inasema kinyume na mtazamo wako, unless ulimaanisha kitu kingine; Do you really understand what nation building means and the process that took place in Tanzania to achieve that?

Pia kuna sehemu unajadili logic ya kiwanda cha mufindi kwamba it was wrong i.e, "why import while it can be produced locally"; Hili nilijadili awali kwa kusema kwamba kuna masuala ambayo unaweza kufanya hivyo ilimradi iwe ni baada ya kujiridhisha na comparative advantage analysis; Vinginevyo, nadhani unaelewa kwamba moja ya changamoto kubwa za sera ya ujamaa hasa katika mazingira ya huduma bure za kijamii ilikuwa ni kasi kubwa ya ongezeko la watu vis a vis kasi ya kukua kwa uchumi;katika mazingira ambayo yalihitaji kujenga take off conditions, hakuna sehemu iliyokuwa muhimu kuisimamia kama sekta ya elimu kwani kama walivyojadili wengi humu, human capital is key, ndio maana nchi kama south korea zilifanikiwa;building human capital must begin with huge investments in primary education, na kwa wakati ule, tafiti nyingi zilionyesha kwamba the biggest educational returns katika uchumi zilitokana na investments in primary education, na sio Tanzania tu bali dunia ya tatu kwa ujumla; Na ilifikia hatua hata world bank wakamwambia mwalimu kwamba tertiary education in Tanzania is a luxury, haina haja ya kujenga vyuo vingi, concentrate on primary education; licha ya hayo, mwalimu kupitia various means akajitahidi sana kupambana na hilo na kuongeza idadi ya sekondari kwa njia mbalimbali, vyuo vya ufundi, taasisi za utafiti n.k;kwa kifupi, kulikuwa na genuine commitment on investments on education, science and technology-nitaleta takwimu juu ya hili;katika nyakati zilizofuata, hili halikuwepo, na hata leo ukiangalia rhetoric and practice ya serikali ni upuuzi tu katika hili.

Zakumi, hakuna human capital ya maana duniani inayopatikana nje ya investments in public education; Tazama marekani na kwingine the role of public sector in education, science, technology and innovation research; sisi tumegeuza elimu kuwa biashara; Waziri Mkuu wa zamani wa Uingerereza aliuliza juzi - "inakuwaje viongozi wengi wa nchi pale UK wanaanza kuwa ni graduates from shule binafsi, tunajenga taifa la namna gani"? Hili ni swali muhimu kwetu Tanzania pia; Ndio maana katika suala zima la shule za kata chini ya Lowassa, kwa mtazamo wangu, the idea was excellent, tatizo utekelezaji; je, tuna kirusi gani katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo?
 
mkuu Mchambuzi post #76 imebeba ujumbe mzito, hivi kiwanda cha mufindi kimeshauzwa? wakuu Nguruvi3 Zakum, Kichuguu tunawasoma, tunapata elimu, mkuu jinga la falsafa anasema anaita!!! na mimi nasema anaita sasa....... twende kazi.....
 
Last edited by a moderator:
80 pere cent ya maintenance na operation inaingaiaje kwa sera za wakati huo? Nyerere akiondoka madarakani ameacha mashirika na viwanda zaidi ya 400. Je, waliofuata walifanya nini katika maintenance na operational process?

Mufindi imekufa kwasababu viongozi waliofuata hawakufuata taratibu za ubinafsishaji.
Mbona shamba la Sao hill bado lipo na linatoa malighafi kwa mazao yake kwa viwanda vingine.

Lakini basi utueleze kuwa kipi bora Mang'ula iliyokuwa inasuasua au Mang'ula iliyogezwa kuwa ghala la chumvi.
Huo ndio uwekezaji au ndio mtazamo wa kisomi wa kuendeleza uchumi?
Nani amebinafsisha Mang'ula na kwanini asifanye maintanance na operational tofauti na ile iliyo feli.


Miaka 30 sasa hebu njoo hapa utueleze kuhusu sera za uchumi ambazo unadhani zimefanikiwa kuliko miaka ya 60 na 70 au za Nyerere the least to say
.

Nguruv3:

Unaboronga. Mimi kuwa critical na sera za Nyerere haina maana kuwa ninazikubali sera za sasa. Vilevile taaluma zilizopo sasa na ambazo hazikuwepo miaka 60, 70 na 80, zinathibitisha kuwa nadharia zilizotumika miaka ya zamani zilikuwa flawed. Kuelezea flaws za miaka ya 60, 70, na 80 haina maana kusema kuwa nadharia za sasa za maendeleo ni perfect.

Vilevile thesis yangu (mtazamo wangu) ni kusema kuwa sera ya 60, 70, na 80 haifai na haziwezi kutumika mazingira ya sasa. Ninachotakiwa ni kuelezea kwanini haifai (period). Kwa muda mrefu, nimetimiza wajibu wangu wa kueleza kwanini hazifai.

Kuelezea alternatives ya sera za 60, 70, na 80 sio wajibu wangu. Huo ni wajibu wa atakayekuja na msimamo wa kuonyesha kuwa kulikuwa na alternative ya sera ya viwanda ya 60, 70, na 80.
 
Zakumi,

Hapo juu, kwa maana nyingine, unakubali kwamba Mwalimu was correct on the drawing board, failure ilikuwa kwenye utekelezaji - unakubali hili by eventually saying kwamba nia ilikuwa ni nzuri, tatizo ni suala zima la ufundi na utaalam;Katika hili, Nguruvi3 amejadili utaalam kwa wakati ule na kuhoji alternative solution, haujaja na jibu bado, which means there was no alternative solution, right? Kumbuka: It has been argued na wanazuoni kadhaa nje ya nchi kwamba kwamba the best way to measure the sucess ya mwalimu ni kwa kuangalia how much convinced wananchi na donors kwamba alikuwa na nia ya dhati ya kuliendeleza taifa lake licha ya changamoto zilizokuwepo wakati ule (hasa nchi yetu kuanza at a very low economic base tofauti na nyingine nyingi na pia uwepo wa vita vya baridi duniani), lakini licha ya hayo, kuelekea end of cold war, aliliacha taifa likiwa na modest level of development and intact in terms of socil and political coherence and stability;

Pia unajadili jinsi gani miradi ilifeli, kwa kutumia mfano wa mufindi pulp and paper factory;ukumbuke kwamba sio kila industrial project ilifeli, mufindi was one of the few white elephant projects engineered na World Bank na such projects zilikuwa na nyingi Africa; Sasa unapolaumu uamuzi wa viongozi ku-sign for such projects, and at the same time unakubali hapakuwa na wataalam wazawa wa kutosha kufanya appraisals n.k, huku ukiwa hauna maelezo ya alternative solutions unatuacha njia panda;

Tatu unasema Katika suala la ujenzi wa taifa, Tanzania is a laughing stock; Siamini umesema maneno haya kwani karibia literature yote iliyopo kuhusu Tanzania and nation buidling inasema kinyume na mtazamo wako, unless ulimaanisha kitu kingine; Do you really understand what nation building means and the process that took place in Tanzania to achieve that?

Pia kuna sehemu unajadili logic ya kiwanda cha mufindi kwamba it was wrong i.e, "why import while it can be produced locally"; Hili nilijadili awali kwa kusema kwamba kuna masuala ambayo unaweza kufanya hivyo ilimradi iwe ni baada ya kujiridhisha na comparative advantage analysis; Vinginevyo, nadhani unaelewa kwamba moja ya changamoto kubwa za sera ya ujamaa hasa katika mazingira ya huduma bure za kijamii ilikuwa ni kasi kubwa ya ongezeko la watu vis a vis kasi ya kukua kwa uchumi;katika mazingira ambayo yalihitaji kujenga take off conditions, hakuna sehemu iliyokuwa muhimu kuisimamia kama sekta ya elimu kwani kama walivyojadili wengi humu, human capital is key, ndio maana nchi kama south korea zilifanikiwa;building human capital must begin with huge investments in primary education, na kwa wakati ule, tafiti nyingi zilionyesha kwamba the biggest educational returns katika uchumi zilitokana na investments in primary education, na sio Tanzania tu bali dunia ya tatu kwa ujumla; Na ilifikia hatua hata world bank wakamwambia mwalimu kwamba tertiary education in Tanzania is a luxury, haina haja ya kujenga vyuo vingi, concentrate on primary education; licha ya hayo, mwalimu kupitia various means akajitahidi sana kupambana na hilo na kuongeza idadi ya sekondari kwa njia mbalimbali, vyuo vya ufundi, taasisi za utafiti n.k;kwa kifupi, kulikuwa na genuine commitment on investments on education, science and technology-nitaleta takwimu juu ya hili;katika nyakati zilizofuata, hili halikuwepo, na hata leo ukiangalia rhetoric and practice ya serikali ni upuuzi tu katika hili;
Zakumi, hakuna human capital ya maana duniani inayopatikana nje ya investments in public education; Tazama marekani na kwingine the role of public sector in education, science, technology and innovation research; sisi tumegeuza elimu kuwa biashara; Waziri Mkuu wa zamani wa Uingerereza aliuliza juzi - "inakuwaje viongozi wengi wa nchi pale UK wanaanza kuwa ni graduates from shule binafsi, tunajenga taifa la namna gani"? Hili ni swali muhimu kwetu Tanzania pia; Ndio maana katika suala zima la shule za kata chini ya Lowassa, kwa mtazamo wangu, the idea was excellent, tatizo utekelezaji; je, tuna kirusi gani katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo?



Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums

Mchambuzi;

Kama sijaendelea, ningependa kukuuliza swali moja. Maendeleo yanaletwa na watu. Je unaweza kunitajia viwanda au mashirika yaliokuwa na mafanikio na viongozi wake na vitu walivyofanya kuleta mafanikio katika viwanda au mashirika hayo? Kati ya mashirika na viwanda 400 anavyopigia domo Nguruv3, nipe orodha ya majina kumi 10 tu
 
Wakuu zangu,

kusema kweli nasikitishwa sana na mjadala ambao kila siku tunamtafuta mchawi wakati sisi wenyewe ndio tunajiita wasomi ambao tunatakiwa kuwa na analysis zinazothibitisha na sio maandishi ya maadui wetu. Sisi ni watoto wanaolelewa na mchawi hivyo tusitegemee kabisa kwamba mataifa makuhwa wanaweza kumsifia Nyerere hata kidogo. Waswahili wanasema Mchawi mpe mwanao akulelee na ndio maana sisi wazima japo mzazi wetu hana sifa nzuri nje. Kila tunapotaka kurudi nyuma kumtazama Nyerere kwa kutumia hadithi za wasiompemda mchawi, ni ishara tosha kabisa ya kwamba lawama zetu zinarudi ktk malezi ya mzazi wetu badala ya kutazama uwezo wake na kwa nini alootwa mchawi ilihali ndio mlezi wetu.

Kuna visa viwili hapa labda niwakumbushe..
1. Kama mnakumbuka wakati wa EAC, Tanzania haikuwa na kiwanda chochote cha uzalishaji isipokuwa mali zote ziolitoka Kenya. Sisi tulikuwa walaji tu na huwezi kuendelea kwa kuwa teja waklti huna msingi wa kukiingizia fedha. Na watu wengi wanamlaumu Nyerere kwa kuvunja EAC bila kupitia kwanza nini kiliajili hadi kufikia yale yale makubaliano ya Kampala ambayo Kenya waliendelea kuyapinga na kuanza matusi kiasi kwamba mwalimu akawaita Manyang'au. Sijui kama mnakumbuka malumbano ya mwalimu na Kenyatta miaka wakati huo kwa wale walokuwa tayari watu wazima. sasa jiulizeni baada ya Ujamaa wa Nyerere tulikuwa na uwezo gani ktk muda mfupi ule na tuache mapungufu maana hata Marekani yenyewe leo hii ina mapungufu kibao chini ya Bush ama Obama. wachumi hawakosi sababu ama kutafuta makosa maana makuzi ya Uchumi hayana pima maji.

Sasa tukirudi ktk kumtazama Nyerere, haada tu ya kuvunjika EAC, tanzania tulianza kuwa na viwanda vyetu wenyewe japo vilianzishwa na serikali lakini wakati huo huo ni wananchi gani walokuwa na uwezo wa kufungua kiwanda wenyewe? kama walishindwa kufungua viwanda wakati wa EAC wangeweza vipi kufungua viwanda baada ya kufa kwa EAC na Mwalimu angeweza vipi kusubiri wananchi watafute mikopo wajenge hivyo viwanda na kukidhi mahitaji ya wananchi?.. Ebu tujiulize hilo kwanza maana ni serikali tu ndio ilokuwa na uwezo wa kuchukua mikopo nje japo yenye masharti magumu.

Na kama Nyerere angejaribu kukubali Ubepari wakati ule basi wakoloni wangeendelea kuwepo nchini wakimiliki uchumi wetu sasa sielewi ni uhuru gani tuloupigania maana wao pekee ndio walokuwa na uwezo. Jingine tujiulize kwa nini Marekani waliutafuta Uhuru wao ikiwa wote walikuwa wazungu, waingereza kama sii uhuru wa Kiuchumi ili kuondokana na kumnufaisha malkia na milki zake. Tafadhalini sana ndugu zangu hasa nyie wasomi kumbukeni tu ya kwamba hatukudai UHURU wetu ili tutawaliwe na mtu mweusi, ama kuipeperusha bendera yetu yenye tangi zetu bali tulidai UHURU wetu ili sisi wananchi wenyewe tuweze kumiliki Uchumi wetu na kwa manufaa yetu

- UCHUMI umilikiwe na wananchi, kinyume cha hapo ni kupotosha maana ya Uhuru wetu.

Wakoloni iwe Mjerumani au Muingereza hawakufanya lolote baya kiutawala na kuwanyima wananchi haki zao isipokuwa uchumi wa nchi yetu ulijengwa ili kuziboresha koloni zao kiuchumi. Kila kilichojengwa ama kuzalishwa nchini kililenga kukuza uchumi wa nchi zao na ndio maana reli ilijengwa toka Kigoma, Mwanza hadi Dat babdarini ili kusafirisha mali na sio watu kwenda makazini. Labda niwaambie tu ya kwamba kutawaliwa ilikuwa kama jinsi sisi binadamu tunavyomfuga kuku, mbuzi au Ngo'mbe. Siku zote huduma zetu ni kumfanya awe mnono zaidi ili siku ya siku atakapotiwa kisu na kumweka sokoni tufaidike. Hivyo basi kama kuku na ng'ombe wangeweza kusema leo, sidhani kama wangemsifia binadamu kwa uhuru walokuwa nao ama malisho na matunzo.

2. Pia tukumbuke kwamba baada ya nchi nyingi duniani kuchukua Ujamaa ktk miaka ya 70, mataifa makubwa chini ya uongozi wa Reagan na Thatcher walitupiga vita vikali sana kutonunua mali zetu Kila kitu kilikosa soko maana hatukuwa na soko zaidi ya Ulaya. Acha mbali mazao yetu hata Diamond ya Mwadui ilikuwa haina bei, kwa hiyo tusimlaumu tu mwalimu kwa UJAMAA bila kutazama mbinu za MAREKANI na UINGEREZA ambao walikuwa wakiishi kama Walanguzi na wakijua wapi kuna masoko. Hata huko vijijini kwetu siku walanguzi wakishusha bei ya nafaka zetu mkulima atakuwa hana jinsi zaidi ya kukubali hasara, hii haina maana kuwa mkulima huyo kachemsha ktk ukulima wake isipokuwa hana uwezo wa kusafikirisha nafaka zake hadi soko la kariakoo ama hajui kama kuna soko kama hilo huko Dar es salaam pia hajui taratibu na mashatri ya uuzaji nafaka hapo sokoni

Mwisho ni kwamba pamoja na kwamba Tanzania yetu hii ina rasilimali na maliasili za kutosha, sisi hatukujipanga kuwa mabepari, hatuna UWEZO toka financial istitution zetu na kwa bahati mbaya hata UBUNIFU hatuna. katika vitu tulowahi kubuni sisi watanzania ni MKOKOTENI tu na wala haina soko zaidi ya kukidhi matatizo yetu ya usafiri. Hizo Benki zetu haziwezi kumkopesha Mtanzania aweze kuchimba dhahabu na kuziuza hata iwe benki kuu ndio iwe mlanguzi. Tazama basi ukisoma historia ya Marekani utaona jinsi wale Ma cowboy walivyokuwa wakiitafuta dhahabu na kwenda benk kuomba mikopo. Hawakutafuta makampuni makubwa kutoka nje isipokuwa walijiwezesha wenyewe.

Kina sisi hata tulipobinafsisha viwanda vyetu, serikali haikutazama mwananchi kwanza bali wageni waloweza kutoa 10% na hata wale wananchi walofanikiwa hawakutazamwa uwezo wao kukiendesha kiwanda isipokuwa dau alopanda na cha juu kwa kiongozi..Ilikuwa ni transformation ya viongozi utoka ktk umaskini badala ya transformation ya nchi kutoka ktk Ujamaa. Hivyo wananchi wengi walonunua viwanda au mali za serikali ktk ubinafsihaji walionyesha tu nia ya kuhodhi kiwanja au mali ile kuitajirisha na viongozi pia kutajirika (utanitowaje)lakini hawakuwa na uwezo iwe kifedha ama kielimu kuendeleza mradi pale serikali ilipokwamba.

Maadam leo hii tumerudisha Utawala wa wageni kiuchumi basi hatuko HURU, na hata siku moja UHURU wa bendera hauwezi kuleta amani nchini isipokuwa UHURU wa kiuchumi ambapo wananchi wenyewe ndio wamiliki wa mali za nchi. Tutaendelea kutawaliwa kiuchumi kwa hiyo mikopo ya misaada, jizo mnazoziita aid na grants ndio magongo tutakayo tembelea hadi siku tutakapo shtuka na kuyaacha. Tanzania yetu bado maskini kutokana na kutawaliwa kiuchumi hakuna jinginelo na hatutaweza kutoka ktk shimo hili katu kwa fikra za kutawaliwa kiuchumi. Ukitazama hata huu mradi wa gas unaotangazwa sana na JK na huyo Muhongo utagundua tu ya kwamba tumeuza UHURU wetu japo hata huyo Mengi alishindwa kuiweka hoja yake wazi kuwaelimisha wananchi jinsi gani mwananchi anapohodhi kisima cha gas italinufaisha taifa. Na poia tukumbuke tu ya kwamba gas, dhahabu au Almasi hazipatikani hovyo duniani. Kwa hiyo tusiogope kukataa misaada na mikataba inayotufunga, maana hao wawekezaji wakiondoka watakwenda wapi kuipata hiyo gas au dhahabu?..watarudi kwetu tu wakisha piga mahesabu yao na kugundua bado faida ipo kisha basi Uchumi wa leo hii ni sioko huria sisi wenyewe tunaweza kuuza mali zetu moja kwa moja China au India bila kupitia Belgium..

Chini ya makubaliano ya JK nawahakikishieni hizo kampuni za nje hazitafikia muda wala wakati wamerudisha fedha yao -HAKUNA maana mkataba hauwapi (time limit) muda wa kumaliza. Hivyo kila mwaka makamupuni hayo wataboresha mitambo yao na wataonyesha ktk vitabu vyao kwamba hawapati faida iwe kwa miaka 30 au 50.

Kwa hiyo UKOLONIMAMBOLEO linatakiwa kuwa somo kubwa kwetu na kama nilivyosema namshukuru Mungu nimeishi na watu hawa na kufanya kazi nao na nafahamu jinsi wanavyofikiria. Maadam wanajua sisi hatuna uwezo kifedha basi tutaendelea kutegemea misaada yao na kamwe hatutaweza kuweka mikataba ya kibiashara..
 
Nguruv3:

Unaboronga. Mimi kuwa critical na sera za Nyerere haina maana kuwa ninazikubali sera za sasa. Vilevile taaluma zilizopo sasa na ambazo hazikuwepo miaka 60, 70 na 80, zinathibitisha kuwa nadharia zilizotumika miaka ya zamani zilikuwa flawed. Kuelezea flaws za miaka ya 60, 70, na 80 haina maana kusema kuwa nadharia za sasa za maendeleo ni perfect.

Vilevile thesis yangu (mtazamo wangu) ni kusema kuwa sera ya 60, 70, na 80 haifai na haziwezi kutumika mazingira ya sasa. Ninachotakiwa ni kuelezea kwanini haifai (period). Kwa muda mrefu, nimetimiza wajibu wangu wa kueleza kwanini hazifai.

Kuelezea alternatives ya sera za 60, 70, na 80 sio wajibu wangu. Huo ni wajibu wa atakayekuja na msimamo wa kuonyesha kuwa kulikuwa na alternative ya sera ya viwanda ya 60, 70, na 80.
Then kama mtazamo wako ni wa sera za 60 na 70 na wala siyo sasa basi upo katika uzi usiokuhusu. Mada ya mchambuzi inaongelea uchumi wa Tanzania kwasasa nini kifanyike na kwasababu gani. Ameuliza maswali yanayohusu zama za leo na wala si za 60 na 70.

Kichuguu ameemeleza vema kuhusu watu wanaolaumu sera za Nyerere bila kufikiri hizo ni zama, na je tufanye nini sasa.
Ni kitu cha ajabu mtu kufanya 'comparison' ya something vs Nothing. Kama hufahamu sera za sasa vipi unaweza kuongelea zilizokosewa. Hapa kuna compare and contrast unachokifanya wewe sicho bali ni kulaumu.

Umekiri kuwa sera za sasa si perefect kama zilzivyokuwa huko nyuma. Kama ni hivyo unadhani tatizo lipo wapi?
Kukataa kueleza sera za sasa kwa mifano inayotoka sera za zamani ni kuukata ukweli.
Heri ya anayejaribu na kushindwa kuliko asiyejaribu kabisa. Sera za kuomba na kupeleka Uswiss hazina nafasi katika dunia ya sasa.

Namalizia kwa kuuliza kuwa je kujenga mabwawa ya kutoa nishati ilikuwa ni fashion kama ulivyosema?
Na kama ni hivyo vipi sasa hivi kuna sera gani mbadala zinazolingana na hizo.

Je, mang'ula machine iliyokuwepo na Mang'ula ghala la chumvi ipi ina afadhali?
Kugeuza kiwanda kuwa ghala la chumvi ndio 'process and operational' ya sera za sasa?
 
Mchambuzi;

Kama sijaendelea, ningependa kukuuliza swali moja. Maendeleo yanaletwa na watu. Je unaweza kunitajia viwanda au mashirika yaliokuwa na mafanikio na viongozi wake na vitu walivyofanya kuleta mafanikio katika viwanda au mashirika hayo? Kati ya mashirika na viwanda 400 anavyopigia domo Nguruv3, nipe orodha ya majina kumi 10 tu
Mchambuzi atakuja. Mimi nataka nikuambie kuwa CRDB, Kilombero sugar, ni katika 10 unayohitaji.

Nina majina ya viwanda zaidi ya 20. Weka swali lako vizuri nitakujibu.
Kwasasa hivi swali halieleweki unakusudia nini kusema mafanikio.
Halafu ujue mafanikio hayapimwi kwa pesa tu, ni suala zima la impact katika jamii.
 
Mchambuzi atakuja. Mimi nataka nikuambie kuwa CRDB, Kilombero sugar, ni katika 10 unayohitaji.

Nina majina ya viwanda zaidi ya 20. Weka swali lako vizuri nitakujibu.
Kwasasa hivi swali halieleweki unakusudia nini kusema mafanikio.
Halafu ujue mafanikio hayapimwi kwa pesa tu, ni suala zima la impact katika jamii.

Unajua kuwa Kilombero sugar kilikuwa ni kiwanda cha mtu binafsi? Unajua CRDB iliokolewa na DANIDA? Bila ruzuku za serikali kusingekuwa na CRDB. Ni ambayo balance sheet yake haikuwa sawa. Naomba endeleze kutoa majina 18 yaliobaki. Na usisahau kuleta na majina ya viongozi wa taasisi hizo waliofanya "miracle wonders".
 
Then kama mtazamo wako ni wa sera za 60 na 70 na wala siyo sasa basi upo katika uzi usiokuhusu. Mada ya mchambuzi inaongelea uchumi wa Tanzania kwasasa nini kifanyike na kwasababu gani. Ameuliza maswali yanayohusu zama za leo na wala si za 60 na 70.

Kichuguu ameemeleza vema kuhusu watu wanaolaumu sera za Nyerere bila kufikiri hizo ni zama, na je tufanye nini sasa.
Ni kitu cha ajabu mtu kufanya 'comparison' ya something vs Nothing. Kama hufahamu sera za sasa vipi unaweza kuongelea zilizokosewa. Hapa kuna compare and contrast unachokifanya wewe sicho bali ni kulaumu.

Umekiri kuwa sera za sasa si perefect kama zilzivyokuwa huko nyuma. Kama ni hivyo unadhani tatizo lipo wapi?
Kukataa kueleza sera za sasa kwa mifano inayotoka sera za zamani ni kuukata ukweli.
Heri ya anayejaribu na kushindwa kuliko asiyejaribu kabisa. Sera za kuomba na kupeleka Uswiss hazina nafasi katika dunia ya sasa.

Namalizia kwa kuuliza kuwa je kujenga mabwawa ya kutoa nishati ilikuwa ni fashion kama ulivyosema?
Na kama ni hivyo vipi sasa hivi kuna sera gani mbadala zinazolingana na hizo.

Je, mang'ula machine iliyokuwepo na Mang'ula ghala la chumvi ipi ina afadhali?
Kugeuza kiwanda kuwa ghala la chumvi ndio 'process and operational' ya sera za sasa?

Nguruv3;

Soma posti zangu uelewe. Kama Wewe na Mchambuzi mngekuja na Novel Approachies za kuendeleza viwanda Tanzania ningekubaliana na nyinyi. Unavyoleta ni vile alivyoacha Nyerere.
 
Wakuu zangu,

kusema kweli nasikitishwa sana na mjadala ambao kila siku tunamtafuta mchawi wakati sisi wenyewe ndio tunajiita wasomi ambao tunatakiwa kuwa na analysis zinazothibitisha na sio maandishi ya maadui wetu. Sisi ni watoto wanaolelewa na mchawi hivyo tusitegemee kabisa kwamba mataifa makuhwa wanaweza kumsifia Nyerere hata kidogo. Waswahili wanasema Mchawi mpe mwanao akulelee na ndio maana sisi wazima japo mzazi wetu hana sifa nzuri nje. Kila tunapotaka kurudi nyuma kumtazama Nyerere kwa kutumia hadithi za wasiompemda mchawi, ni ishara tosha kabisa ya kwamba lawama zetu zinarudi ktk malezi ya mzazi wetu badala ya kutazama uwezo wake na kwa nini alootwa mchawi ilihali ndio mlezi wetu.

Kuna visa viwili hapa labda niwakumbushe..
1. Kama mnakumbuka wakati wa EAC, Tanzania haikuwa na kiwanda chochote cha uzalishaji isipokuwa mali zote ziolitoka Kenya. Sisi tulikuwa walaji tu na huwezi kuendelea kwa kuwa teja waklti huna msingi wa kukiingizia fedha. Na watu wengi wanamlaumu Nyerere kwa kuvunja EAC bila kupitia kwanza nini kiliajili hadi kufikia yale yale makubaliano ya Kampala ambayo Kenya waliendelea kuyapinga na kuanza matusi kiasi kwamba mwalimu akawaita Manyang'au. Sijui kama mnakumbuka malumbano ya mwalimu na Kenyatta miaka wakati huo kwa wale walokuwa tayari watu wazima. sasa jiulizeni baada ya Ujamaa wa Nyerere tulikuwa na uwezo gani ktk muda mfupi ule na tuache mapungufu maana hata Marekani yenyewe leo hii ina mapungufu kibao chini ya Bush ama Obama. wachumi hawakosi sababu ama kutafuta makosa maana makuzi ya Uchumi hayana pima maji.

Sasa tukirudi ktk kumtazama Nyerere, haada tu ya kuvunjika EAC, tanzania tulianza kuwa na viwanda vyetu wenyewe japo vilianzishwa na serikali lakini wakati huo huo ni wananchi gani walokuwa na uwezo wa kufungua kiwanda wenyewe? kama walishindwa kufungua viwanda wakati wa EAC wangeweza vipi kufungua viwanda baada ya kufa kwa EAC na Mwalimu angeweza vipi kusubiri wananchi watafute mikopo wajenge hivyo viwanda na kukidhi mahitaji ya wananchi?.. Ebu tujiulize hilo kwanza maana ni serikali tu ndio ilokuwa na uwezo wa kuchukua mikopo nje japo yenye masharti magumu.

Na kama Nyerere angejaribu kukubali Ubepari wakati ule basi wakoloni wangeendelea kuwepo nchini wakimiliki uchumi wetu sasa sielewi ni uhuru gani tuloupigania maana wao pekee ndio walokuwa na uwezo. Jingine tujiulize kwa nini Marekani waliutafuta Uhuru wao ikiwa wote walikuwa wazungu, waingereza kama sii uhuru wa Kiuchumi ili kuondokana na kumnufaisha malkia na milki zake. Tafadhalini sana ndugu zangu hasa nyie wasomi kumbukeni tu ya kwamba hatukudai UHURU wetu ili tutawaliwe na mtu mweusi, ama kuipeperusha bendera yetu yenye tangi zetu bali tulidai UHURU wetu ili sisi wananchi wenyewe tuweze kumiliki Uchumi wetu na kwa manufaa yetu

- UCHUMI umilikiwe na wananchi, kinyume cha hapo ni kupotosha maana ya Uhuru wetu.

Wakoloni iwe Mjerumani au Muingereza hawakufanya lolote baya kiutawala na kuwanyima wananchi haki zao isipokuwa uchumi wa nchi yetu ulijengwa ili kuziboresha koloni zao kiuchumi. Kila kilichojengwa ama kuzalishwa nchini kililenga kukuza uchumi wa nchi zao na ndio maana reli ilijengwa toka Kigoma, Mwanza hadi Dat babdarini ili kusafirisha mali na sio watu kwenda makazini. Labda niwaambie tu ya kwamba kutawaliwa ilikuwa kama jinsi sisi binadamu tunavyomfuga kuku, mbuzi au Ngo'mbe. Siku zote huduma zetu ni kumfanya awe mnono zaidi ili siku ya siku atakapotiwa kisu na kumweka sokoni tufaidike. Hivyo basi kama kuku na ng'ombe wangeweza kusema leo, sidhani kama wangemsifia binadamu kwa uhuru walokuwa nao ama malisho na matunzo.

2. Pia tukumbuke kwamba baada ya nchi nyingi duniani kuchukua Ujamaa ktk miaka ya 70, mataifa makubwa chini ya uongozi wa Reagan na Thatcher walitupiga vita vikali sana kutonunua mali zetu Kila kitu kilikosa soko maana hatukuwa na soko zaidi ya Ulaya. Acha mbali mazao yetu hata Diamond ya Mwadui ilikuwa haina bei, kwa hiyo tusimlaumu tu mwalimu kwa UJAMAA bila kutazama mbinu za MAREKANI na UINGEREZA ambao walikuwa wakiishi kama Walanguzi na wakijua wapi kuna masoko. Hata huko vijijini kwetu siku walanguzi wakishusha bei ya nafaka zetu mkulima atakuwa hana jinsi zaidi ya kukubali hasara, hii haina maana kuwa mkulima huyo kachemsha ktk ukulima wake isipokuwa hana uwezo wa kusafikirisha nafaka zake hadi soko la kariakoo ama hajui kama kuna soko kama hilo huko Dar es salaam pia hajui taratibu na mashatri ya uuzaji nafaka hapo sokoni

Mwisho ni kwamba pamoja na kwamba Tanzania yetu hii ina rasilimali na maliasili za kutosha, sisi hatukujipanga kuwa mabepari, hatuna UWEZO toka financial istitution zetu na kwa bahati mbaya hata UBUNIFU hatuna. katika vitu tulowahi kubuni sisi watanzania ni MKOKOTENI tu na wala haina soko zaidi ya kukidhi matatizo yetu ya usafiri. Hizo Benki zetu haziwezi kumkopesha Mtanzania aweze kuchimba dhahabu na kuziuza hata iwe benki kuu ndio iwe mlanguzi. Tazama basi ukisoma historia ya Marekani utaona jinsi wale Ma cowboy walivyokuwa wakiitafuta dhahabu na kwenda benk kuomba mikopo. Hawakutafuta makampuni makubwa kutoka nje isipokuwa walijiwezesha wenyewe.

Kina sisi hata tulipobinafsisha viwanda vyetu, serikali haikutazama mwananchi kwanza bali wageni waloweza kutoa 10% na hata wale wananchi walofanikiwa hawakutazamwa uwezo wao kukiendesha kiwanda isipokuwa dau alopanda na cha juu kwa kiongozi..Ilikuwa ni transformation ya viongozi utoka ktk umaskini badala ya transformation ya nchi kutoka ktk Ujamaa. Hivyo wananchi wengi walonunua viwanda au mali za serikali ktk ubinafsihaji walionyesha tu nia ya kuhodhi kiwanja au mali ile kuitajirisha na viongozi pia kutajirika (utanitowaje)lakini hawakuwa na uwezo iwe kifedha ama kielimu kuendeleza mradi pale serikali ilipokwamba.

Maadam leo hii tumerudisha Utawala wa wageni kiuchumi basi hatuko HURU, na hata siku moja UHURU wa bendera hauwezi kuleta amani nchini isipokuwa UHURU wa kiuchumi ambapo wananchi wenyewe ndio wamiliki wa mali za nchi. Tutaendelea kutawaliwa kiuchumi kwa hiyo mikopo ya misaada, jizo mnazoziita aid na grants ndio magongo tutakayo tembelea hadi siku tutakapo shtuka na kuyaacha. Tanzania yetu bado maskini kutokana na kutawaliwa kiuchumi hakuna jinginelo na hatutaweza kutoka ktk shimo hili katu kwa fikra za kutawaliwa kiuchumi. Ukitazama hata huu mradi wa gas unaotangazwa sana na JK na huyo Muhongo utagundua tu ya kwamba tumeuza UHURU wetu japo hata huyo Mengi alishindwa kuiweka hoja yake wazi kuwaelimisha wananchi jinsi gani mwananchi anapohodhi kisima cha gas italinufaisha taifa. Na poia tukumbuke tu ya kwamba gas, dhahabu au Almasi hazipatikani hovyo duniani. Kwa hiyo tusiogope kukataa misaada na mikataba inayotufunga, maana hao wawekezaji wakiondoka watakwenda wapi kuipata hiyo gas au dhahabu?..watarudi kwetu tu wakisha piga mahesabu yao na kugundua bado faida ipo kisha basi Uchumi wa leo hii ni sioko huria sisi wenyewe tunaweza kuuza mali zetu moja kwa moja China au India bila kupitia Belgium..

Chini ya makubaliano ya JK nawahakikishieni hizo kampuni za nje hazitafikia muda wala wakati wamerudisha fedha yao -HAKUNA maana mkataba hauwapi (time limit) muda wa kumaliza. Hivyo kila mwaka makamupuni hayo wataboresha mitambo yao na wataonyesha ktk vitabu vyao kwamba hawapati faida iwe kwa miaka 30 au 50.

Kwa hiyo UKOLONIMAMBOLEO linatakiwa kuwa somo kubwa kwetu na kama nilivyosema namshukuru Mungu nimeishi na watu hawa na kufanya kazi nao na nafahamu jinsi wanavyofikiria. Maadam wanajua sisi hatuna uwezo kifedha basi tutaendelea kutegemea misaada yao na kamwe hatutaweza kuweka mikataba ya kibiashara..

Mkandara;

Nimefanya debates na wewe kwa zaidi ya miaka 10. Toka enzi ya bcstimes. Tatizo lako unajisahau. Mara nyingi unaelezea jinsi ulivyofanya biashara zako kipindi cha Nyerere. Umeshasema ulitoa bidhaa Tanzania na kuzipeleka Kenya, Zambia, Zimbabwe.

Binafsi kama wahujumu wengine, ulijitengeneza faida kubwa. Lakini vitendo vyako havikuwanufaisha watanzania wengine au supply chain ya ugawaji wa bidhaa Tanzania. Vitendo kama hivi pamoja na sera mbaya za serikali ndivyo vilivyoua viwanda. Leo unapiga kelele kumtetea Nyerere.

Hivyo kusema kuwa tusitafute mchawi wakati tunajua kuwa sera na vitendo vya watu walio-implement sera hizo zilikuwa ni mismatch sio kujitendea haki.

Kama mkoloni hatutakii mema, kwanini China,South Korea, Taiwani zanaendelea.
 
Mkandara;

Nimefanya debates na wewe kwa zaidi ya miaka 10. Toka enzi ya bcstimes. Tatizo lako unajisahau. Mara nyingi unaelezea jinsi ulivyofanya biashara zako kipindi cha Nyerere. Umeshasema ulitoa bidhaa Tanzania na kuzipeleka Kenya, Zambia, Zimbabwe.

Binafsi kama wahujumu wengine, ulijitengeneza faida kubwa. Lakini vitendo vyako havikuwanufaisha watanzania wengine au supply chain ya ugawaji wa bidhaa Tanzania. Vitendo kama hivi pamoja na sera mbaya za serikali ndivyo vilivyoua viwanda. Leo unapiga kelele kumtetea Nyerere.

Hivyo kusema kuwa tusitafute mchawi wakati tunajua kuwa sera na vitendo vya watu walio-implement sera hizo zilikuwa ni mismatch sio kujitendea haki.

Kama mkoloni hatutakii mema, kwanini China,South Korea, Taiwani zanaendelea.
Zakumi naona sasa hoja umeihamishia kwangu japo ni mfano unaotaka kulenga ubovu wa sera za mwalimu.

Kitu kimoja tu unashindwa kuelewa kwamba nia na lengo ya sera za mwalimu ilikuwa kwanza tujitosheleze sisi wenyewe kwa mahitaji yetu. Na sisi walanguzi hatukuwa ktk kundi la wahujumu uchumi isipokuwa tuliviwezesha viwanda vyetu kuuza mali zao. kumbuka tu tulinunua mali zile viwandani na kwenda kuziuza nje kasha fedha zinarudi nyumbani. Na ktk mzunguko huo wavuvi walifaidika, viwanda vilifaidika japo wananchi wengi walikosa huduma hizo wakipanga mawe ktk foleni madukani.

Hivyo usinilalamikie miye kiuchumi isipokuwa tulifanya isivyotakiwa wala haikupangiwa mali ile kuuzwa nje. Pato la viwanda au mashirika lilibakia pale pale maana waliuza mali zao japo sii kwa walengwa... Nitaendelea kumtetea Nyerere kwa sababu alikuwa na nia nzuri na alielewa uwezo wa wananchi ktk uzalishaji. Wakulima ambao walikuwa asilimia 80 hawakuwa na uwezo mkubwa wa kununua mali ktk kiwango chake na ndio maana kila kitu kilikuwa karibu na bure..Utawala wa Nyerere ulikuwa kama NGO kutuhudumia wananchi wasiojiweza, hilo tukubali tusikubali.

China, South Korea na Taiwan wameweza kuendelea kwa sababu wameunda mfumo mpya wa kuuza mali zao nje badala ya wao kuwa wahitaji tu. Uchumi wowote utakuwa zaidi ikiwa unauza zaidi ya unavyotumia lakini sisi toka Enzi hatukuweza kumudu mahitaji yetu ya ndani na kwa bahati mbaya zaidi tumeingia ktk imports zaidi ya Exports. bado fikira zetu ni kukidhi mahitaji yetu na ndio maana tunakula hadi mbegu.

Na kinachotuangusha sasa hivi ni kutegemea wawekezaji kutoka nje ambao hakuna mzunguko wa fedha ndani zaidi ya wao kuchota na kupeleka nje iwe mashirika ya simu au migodi ya dhahabu na gas. Nenda TRA utaambiwa hadi leo hii serikali yetu inategemea imports ktk makusanyo ya kodi zake kuliko exports tena mara 10 pamoja na kuwa na miradi mikubwa. Sisi ni Taifa tegemezi kwa njia zote za kiuchumi hivyo kutufanya mateja badala ya wazalishaji..
 
JLF;

Tukirudi kwenye majibu ya hoja zangu, kuna alternatives. Lakini kila kitu kina gharama zake. Moja ya alternatives ni kutumia mikopo. Nchi inaweza kutumia mikopo kutoka nje kujenga viwanda. Na baadhi ya viwanda vilivyojengwa kati ya 60-80 vilitumia mikopo. Matatizo ya mikopo ni kuongeza deni taifa. Viwanda vinaposhindwa kutimiza majukumu yake ya kurudisha pesa, ulipaji wa madeni na riba unaweza kuiletea nchi umasikini.


Alternative nyingine ni kutumia misaada ya kutoka nje. Misaada mingi ina masharti yake. Na vilevile tukumbuke kuwa wahisani wana watu wengi wa kuwasaidia. Cha muhimu zaidi kuhusu misaada ni donor fatique. Nchi za scandinavia zilitusaidia, lakini zilipochoka zilianza kutushinikiza kufanya reforms.


.
Nadhani hoja iliyopo ni juu ya upande upi tunaotakiwa kuwekeza nguvu zetu kubwa katika kukuza uchumi wetu, Je, tuwekeze zaidi kwenye Outward Strategies au Inward Strategies? Mkuu Zakumi, kwa alternatives ulizozisema hapo juu ni wazi una-support Outward Strategies kwani hakuna mkopo wala msaada unaopatikana kwa sasa nje ya kukubaliana na Outward strategies. Ukimfuata Mchina atakuambia umfungulie milango kwanza, sawa na USA, UK, UN, n.k Masharti ambayo hutanguliza maslahi ya mtoaji kwanza na kumsahau mpokeaji. Wenzetu faida ya mikopo na misaada yao kwetu ni kupata ZIADA, likini sisi ni MRIDHIKO tu wa chochote tupatacho hata kama ni 1/100 ya tulichovuna (zao la unfair and false maafikiano)

Swali bado liko palepale, je tuna ubavu wa kutosha kupambambana na masharti yao kuyageuza kuwa na manufaa zaidi kwetu? Je tunaweza kukwepa HILA za makusudi zinazoambatana na masharti yao? Binafsi sioni uwezekano wa hawa watoa mikopo na misaada kuendelea kutuletea misaada na mikopo pale watakopoona tunaitumia vizuri kutunufaisha. Wataisitisha tu! Wapi tutasimama? Siku zote nguo ya kuazima haistili............................! Kama ulivyosema kwamba kila kitu kina gharama zake, katika hili gharama yake ni kukiuza kizazi chetu kijacho, maana itawalazimu kuanza tena upya. Kwanini tusijiuze sisi leo? Kwa maana tulishakuwa wafu muda mrefu sana, kwanini tusijitoea kwa kizazi chetu kijacho?


JLF;

Hivyo kwa maoni yangu binafsi si vibaya nchi kuanza kwa kutumia resources zake kwanza. Japokuwa mapato yanaweza yasiwe makubwa, matumizi mazuri ya kipato hicho yataleta mafanikio baadaye. Chukua mfano wa Tanzania. Kwa zaidi ya miaka 30 tuna mashule mengi ambayo hayana waalimu wazuri au wa kutosha. Haya ni matumizi mabaya ya kile kidogo tunachopata. Hii ni kwa sababu wahitimu wa shule hizo hawana manufaa ya kuleta mabadiliko.

Hapa napata tabu kidogo kukuelewa, nachojua kwa nchi kutumia rasilimali zake kwanza ni nje ya kutegemea mikopo wala misaada, hapo juu umetaja kama njia mbadala, ni wazi kuna ukinzani. Binafsi nakubaliana nawe kwa zaidi 100% ya hiki ulichokisema kwenye aya ya mwisho. Lakini mimi naamini hivi, kitendo cha kutumia resources zetu binafsi kukuza uchumi wetu, ndio Inward Looking Strategies(sijui kama kuna tafsiri nyingine-kwangu hii ian mashiko zaidi)

Hii njia ina changamoto nyingi mno, kama ulivyotaadharisha Mkuu wangu, lakini ni njia sahihi ya kupata suluhisho sahihi na la kudumu la matatizo yetu mengi sana kama sio yote. Tutahitaji ku-accumulate our own capital from our own resources, si siri tena kwamba tuna mtaji mdogo sana hasa katika nguvukazi na teknolojia (kipindi tunalazimishwa kuingia kichwakichwa kwenye utandawazi tulikenua meno na kuimba shangwe, hatukujua ni kumfundisha mtu kuvuta sigara wakati hana uwezo wa kuinunua-ati ni Time Factor)

Kama mtaji wetu ni duni, ni wazi production yetu itakuwa low and poor. Kukiwa na poor and low production automatically kutakuwa na poor services. Hapo sasa ndio tunaweza kushuhudia kiongozi wa nchi akiburuzwa barabarani akidharilishwa na kupotezwa kabisa. Ndipo patokeapo wachache wenye jeuri ya kushikilia hatima ya maisha ya wenzao. Ubinafsi-Hila, Wizi, Visasi, Unyonyaji, n.k.

Hapa ndipo Ubunifu wa hali ya juu sana unapohitajika, Kwanza ni katika kucheza na ATTITUDES zetu raia na Pili ni katika kufanya TIMING ya implementation ya strategies! Eneo hili ndilo binafsi nalofikiri lilikwamisha Azimio la Arusha na Nyerere!

Katika Attitudes ni lazima Fikra zetu zisukwe kikamilifu kabisa katika kukifikiria kizazi chetu cha kesho na si matumbo yetu leo! Sisi ni wafu tayari katika dunia hii ya Ubeberu, hatuna cha kupoteza ila kama tutaacha kuwafikiria watoto wetu! Nyanja tatu kuu katika kusuka mind zetu kufikia vile tunavyotaka ni Elimu, Sanaa, na Vyombo Vya Habari (katika hili demokrasia ndio sumu mbaya sana). Ni lazima tufanyie mapinduzi Fikra zetu kama kweli tunataka ukombozi wa Kweli. Ikumbukwe kuwa Maendeleo ni Kuthaminiwa kwa UTU wetu, si KITU.

Katika kufanya Timing, ni baada ya kuwa na proper Inward Strategies, ni lazima kuwe na good timing katika ku-introduce sera baada ya sera, makakati baada ya mkakati. Ni lazima uwe na hakika ya namna kile unachowasilisha kitakavyopokewa na raia. Ni kucheza na Attitudes, raia wapo tayari kusikia nini na kutekeleza nini! HESABU! Si mchakato wa muda mfupi kama wanavyopiga domo wanasiasa wetu wa leo.

Kama dhahabu, tunahitaji kupita motoni. Tusimame leo maana tulishaanguka, Tushikane hima maana Tulishapotezana. Tuthubutu, maana ndio Nguvu Yetu. Ubunifu haujawahi kufika mwisho, Tukikaa chini Tukaumiza vichwa, Tunaweza. Nguvu yetu ni Umuja na Kuthubutu. a4afrika

Mungu wetu yu tayari kutupigania vitani.
Anaita sasa!
 
Last edited by a moderator:
Nadhani hoja iliyopo ni juu ya upande upi tunaotakiwa kuwekeza nguvu zetu kubwa katika kukuza uchumi wetu, Je, tuwekeze zaidi kwenye Outward Strategies au Inward Strategies? Mkuu Zakumi, kwa alternatives ulizozisema hapo juu ni wazi una-support Outward Strategies kwani hakuna mkopo wala msaada unaopatikana kwa sasa nje ya kukubaliana na Outward strategies. Ukimfuata Mchina atakuambia umfungulie milango kwanza, sawa na USA, UK, UN, n.k Masharti ambayo hutanguliza maslahi ya mtoaji kwanza na kumsahau mpokeaji. Wenzetu faida ya mikopo na misaada yao kwetu ni kupata ZIADA, likini sisi ni MRIDHIKO tu wa chochote tupatacho hata kama ni 1/100 ya tulichovuna (zao la unfair and false maafikiano)

Swali bado liko palepale, je tuna ubavu wa kutosha kupambambana na masharti yao kuyageuza kuwa na manufaa zaidi kwetu? Je tunaweza kukwepa HILA za makusudi zinazoambatana na masharti yao? Binafsi sioni uwezekano wa hawa watoa mikopo na misaada kuendelea kutuletea misaada na mikopo pale watakopoona tunaitumia vizuri kutunufaisha. Wataisitisha tu! Wapi tutasimama? Siku zote nguo ya kuazima haistili............................! Kama ulivyosema kwamba kila kitu kina gharama zake, katika hili gharama yake ni kukiuza kizazi chetu kijacho, maana itawalazimu kuanza tena upya. Kwanini tusijiuze sisi leo? Kwa maana tulishakuwa wafu muda mrefu sana, kwanini tusijitoea kwa kizazi chetu kijacho?




Hapa napata tabu kidogo kukuelewa, nachojua kwa nchi kutumia rasilimali zake kwanza ni nje ya kutegemea mikopo wala misaada, hapo juu umetaja kama njia mbadala, ni wazi kuna ukinzani. Binafsi nakubaliana nawe kwa zaidi 100% ya hiki ulichokisema kwenye aya ya mwisho. Lakini mimi naamini hivi, kitendo cha kutumia resources zetu binafsi kukuza uchumi wetu, ndio Inward Looking Strategies(sijui kama kuna tafsiri nyingine-kwangu hii ian mashiko zaidi)

Hii njia ina changamoto nyingi mno, kama ulivyotaadharisha Mkuu wangu, lakini ni njia sahihi ya kupata suluhisho sahihi na la kudumu la matatizo yetu mengi sana kama sio yote. Tutahitaji ku-accumulate our own capital from our own resources, si siri tena kwamba tuna mtaji mdogo sana hasa katika nguvukazi na teknolojia (kipindi tunalazimishwa kuingia kichwakichwa kwenye utandawazi tulikenua meno na kuimba shangwe, hatukujua ni kumfundisha mtu kuvuta sigara wakati hana uwezo wa kuinunua-ati ni Time Factor)

Kama mtaji wetu ni duni, ni wazi production yetu itakuwa low and poor. Kukiwa na poor and low production automatically kutakuwa na poor services. Hapo sasa ndio tunaweza kushuhudia kiongozi wa nchi akiburuzwa barabarani akidharilishwa na kupotezwa kabisa. Ndipo patokeapo wachache wenye jeuri ya kushikilia hatima ya maisha ya wenzao. Ubinafsi-Hila, Wizi, Visasi, Unyonyaji, n.k.

Hapa ndipo Ubunifu wa hali ya juu sana unapohitajika, Kwanza ni katika kucheza na ATTITUDES zetu raia na Pili ni katika kufanya TIMING ya implementation ya strategies! Eneo hili ndilo binafsi nalofikiri lilikwamisha Azimio la Arusha na Nyerere!

Katika Attitudes ni lazima Fikra zetu zisukwe kikamilifu kabisa katika kukifikiria kizazi chetu cha kesho na si matumbo yetu leo! Sisi ni wafu tayari katika dunia hii ya Ubeberu, hatuna cha kupoteza ila kama tutaacha kuwafikiria watoto wetu! Nyanja tatu kuu katika kusuka mind zetu kufikia vile tunavyotaka ni Elimu, Sanaa, na Vyombo Vya Habari (katika hili demokrasia ndio sumu mbaya sana). Ni lazima tufanyie mapinduzi Fikra zetu kama kweli tunataka ukombozi wa Kweli. Ikumbukwe kuwa Maendeleo ni Kuthaminiwa kwa UTU wetu, si KITU.

Katika kufanya Timing, ni baada ya kuwa na proper Inward Strategies, ni lazima kuwe na good timing katika ku-introduce sera baada ya sera, makakati baada ya mkakati. Ni lazima uwe na hakika ya namna kile unachowasilisha kitakavyopokewa na raia. Ni kucheza na Attitudes, raia wapo tayari kusikia nini na kutekeleza nini! HESABU! Si mchakato wa muda mfupi kama wanavyopiga domo wanasiasa wetu wa leo.

Kama dhahabu, tunahitaji kupita motoni. Tusimame leo maana tulishaanguka, Tushikane hima maana Tulishapotezana. Tuthubutu, maana ndio Nguvu Yetu. Ubunifu haujawahi kufika mwisho, Tukikaa chini Tukaumiza vichwa, Tunaweza. Nguvu yetu ni Umuja na Kuthubutu. a4afrika

Mungu wetu yu tayari kutupigania vitani.
Anaita sasa!


Mkuu JLF;

Uchumi wa nchi kama saba au zaidi za kiafrika unakuwa kwa kasi kubwa sana. Moja ya nchi hizo ni Tanzania. Chanzo cha kukua kwa uchumi huu ni mahitaji makubwa ya commodities zinazotoka Afrika kama vile madini, kahawa, Cocoa n.k

Pamoja na ukuaji wa uchumi, nchi hizi zinakabiliwa na matatizo makubwa katika kuboresha maendeleo ya jamii. Bado watu wengi ni masikini. Wachumi wetu kama Mchambuzi wanatuletea hoja ya kitu gani kifanywe. Anatusisitiza tufungue viwanda ambavyo vitatoa ajira kwa watu na vilevile kuongeza thamani ya vile tunavyouza nje. Na kusisitiza anatoa mifano ya nchi mbalimbali kama vile China and South Korea.

Kwa maoni yangu binafsi. Maendeleo ya China na South Korea katika masuala ya viwanda, hayatokani na sera za viwanda peke yake. Yanatokana na sera zingine za serikali ambazo sisi tunapuuzia toka tumepata uhuru. Kwa mfano China na South Korea zinatoa elimu bora ya shule za msingi. Kwenye mitihani ya kimataifa wanafunzi wao wanafanya vizuri kuliko wanafunzi wa kutoka nchi Ulaya Magharibi au Marekani ya Kaskazini.

Kutokana na kupuzia elimu zenye skills, hakuna mwekezaji atakayekuja Tanzania na kuwekeza viwanda vinavyohitaji skilled labour. Ni serikali inayoweza kuanzisha miradi ya viwanda vya kutumia skills bila kuwa na watu wenye skills. Kwa mfani miaka 60, 70 na 80 lilifanyika zoezi hili na matokeo yake yalikuwa deadly.

Hivyo kwa maoni yangu, ningependelea Tanzania iendelee kuuza malighafi kama inavyofanya sasa. Japokuwa mauzo ya malighafi hayaleti kazi kwa watanzania wengi, matumizi mazuri ya kile kinachotokana na mauzo ya malighafi yanaweza kusaidia kuongeza skills na capabilities za nchi ambazo zitatumika katika upanuzi wa viwanda au sekta zingine miaka ijayo.
 
Back
Top Bottom