Uchumi wa Tanzania: Je, Ni Kitendawili au Ni Mazingaombwe Kwa Maskini?

Uchumi wa Tanzania: Je, Ni Kitendawili au Ni Mazingaombwe Kwa Maskini?

mkuu gfsonwin pole sana, kama mkuu Kichuguu alivyosema tatizo ni uongozi, kwa kuthibitisha hilo tumtizame waziri mulugo mteule huyu wa serikali ya ari zaidi, kasi zaid na nguvu zaidi, kama kiongozi huyu mwenyewe hayupo serious na elimu yake, atawezaji kuwa serious na Elimu ya wengine? atawezaji kuongoza taasisi ya elimu ikiwa elimu yake binafsi aliyoipata haimuongozi?
Elimu ya nchi hii, kamwe haitaweza kuinuliwa na mwanasiasa hata siku moja, tena elimu yetu ikiwezekana lisiwe jambo la kisiasa.

Nasema lisiwe jambo la kisiasa nikimaanisha kwamba watendaji wake wawe mawaziri ambao sio wafuasi wa chama cha siasa na ili kupatikana waombe kazi wafanyiwe usaili na awajibike kulingana na kazi ambayo sisi tunampa na sio ambayo iko kwenye ilan za vyama vyao.

Naboreka sana kuona VIHIYO ni wengi sana kwenye serikali ambao pia hawako dedicated na kukuza elimu ya taifa hili. inatia uchungu sana kumkuta mtu kama Mulugo anabishana na Prof Mchome kwa mawazo ambayo aliyapata kwenye kikao cha baraza la mawaziri tena nje ya katibu mkuu halafu anakuja kusema eti msimamo wa serkali kweli hii inatupa picha gani?? sisi tumekuwa wajinga kwa kukaa kimya ifike mahali tuseme tumechoka tunahitaj mabadiliko ya haja
 
Wakuu, naomba mniwie radhi kwa kutoweka kidogo kwenye mjadala huu muhimu kwa mustakabali wa taifa letu;Naona mjadala umepamba sana moto, nitajitahidi kurudi baadae kujadili masuala mbalimbali kwa kina (yani kuchangia mawazo yangu kutokana na hoja mbalimbali zilizotolewa na wadau mbalimbali); Ningependa tuuangalie uchumi wetu kwa mtazamo wa mtanzania wa kawaida - je, ni kitendawili au mazingaombwe? Kwani iwapo ni kitendawili, basi ni suala la kukitegua tu kupitia reforms zinazoendelea, lakini iwapo ni mazingaombwe, basi reforms pekee hazitoshi, badala yake tunahitaji to undergo a structural transformation; Ningependa kusikia mawazo yenu juu ya mtazamo wangu huu;

Nitarejea tena kwa kujadilia masuala muhimu kwa kina, ila kwa sasa - Nikitazama kwa haraka haraka, maoni ya wengi yapo katika maeneo yafuatayo katika kuelezea kwanini hatujapiga hatua:

*Lack of trickle down policies kufanikisha impact of economic growth imfikie mwananchi wa kawaida (mfano, Kobello);

*Utekelezaji wa mfumo wa kibepari na madhara yake katika jamii inayokosa prerequisites needed for take off ( mfano, Mkandara, karibu kwenye mjadala);

*Kwa kiasi fulani, poor leadership baada ya mwalimu kuondoka madarakani Nguruvi3, nipo sawa hapa?); Kichuguu nae anagusia suala hili;

*Kwa kiasi kikubwa, bad foundation iliyojengwa na Mwalimu katika mikakati ya kujenga misingi ya kukuza na kuendeleza uchumi wenye manufaa kwa walio wengi Zakumi, nipo sawa hapa?);

*Ukosefu wa sera na mipangilio ya kushirikisha umma au serikali kwa niaba yao katika suala zima la matumizi ya rasilimali za taifa (mfano Ngongo), huku pia akijadili suala zima la lack of fiscal discipline;

*Deficiencies in human capital or lack of investment in education (kwa mfano Nguruvi3, @kichuhuu gfsonwin, @zembemkuu, Zakumi);

*Ukosefu wa serikali katika ushiriki wa uzalishaji kwenye uchumi (mfano Ngongo), mtazamo ambao kwa kiasi fulani unaendana na wa Nguruvi3, na kupishana na Zakumi; kwa maana nyingine, participation ya serikali as a marginal regulator na mkusanyaji tu kodi (tena barely)inachangia mambo kutokuwa swa, tofauti kama serikali ingekuwa strategically & selectively involved in production, facilitation/providing an enabling environment for the indegenous private and SME sectors kushiriki katika uchumi unaopigiwa makofi na wanasiasa wa ccm;

*Umuhimu wa science and technology and innovation policies and strategies gfsonwin), ambayo mimi nadhani hii ni issue #1 kwa umuhimu wa taifa letu kujipanga ingawa sio wengi waliojadili suala hili la role of STI;

Kuna masuala mengine mengi ambayo mtaniwia radhi kama nimesahau kuyataja; Yote haya yanajadiliwa kwamba ndio sababu ya msingi kwanini hatuoni madhara ya kukua kwa uchuni kwa mwananchi wa kawaida huku takwimu zikidi kuonyesha kwamba karibia 90% ya watanzania wanaishi under $2 a day (chini ya shillingi elfu nne kwa siku); nadhani tukizingatia mahitaji ya kila siku ambayo ni muhimu kwa their livelohood strategies (nauli, vocha, chakula), haya tu matatu ni ngumu kuyapata kwa uhakika kila siku;

Last but not least, nigusie masuala mawili: Kwanza ni hoja ya Nguruvi3 kwamba export promotion is a must do strategy, na kwamba ni muhimu kujikita katika maeneo ambayo we have a comparative advantage (ardhi, utalii, madini n.k); Hapa ningependa kusikia zaidi kutoka kwake on how we can balance between producing for exports and meeting local needs katika muktadha ambao our market is flooded with Chinese products; Kwa kugusia kidogo tu, south africa kwa kiasi fulani wanajitahidi ku balance between the two, sisi changamoto zipo wapi? Nguruvi3 kajadili masuala ya viwanda kufeli kutokana na high input costs, je kuna masuala mengine? Anajadili pia juu ya umuhimu wa kujenga core competency katika maeneo fulani ili tuwe competitive, je ni suala la human capital development peke yake?

Suala la pili hapa nalopenda kugusia ni hoja ya Zakumi katika bandiko #1 3 ambapo anasema kwamba mkakati wa Mwalimu didn't make sense i.e the mixture of import substitution and exports promotion strategy; Ningepenga kufahamu iwapo failure kwa mtazamo wake ilianzia kwenye drawing board au katika implementation; Pia Zakumi amejadili kwamba unapokosa jamii isiyo na skilled labour, basi ni lazima ku export raw materials and natural resources ili uweze ku import expertise, talent na capital; Mkuu Zakumi:

Pamoja na mapungufu ya mwalimu, lilipokuja suala la rasilimali za taifa na wananchi, aliamini zaidi katika haki ya mungu kuliko haki ya mzungu;hali hiyo ikatoweka baada ya yeye kutoweka;

Lakini pamoja na hayo, mara tu baada ya uhuru, tulielezwa na bwana wakubwa nje kwamba role ya serikali should be to create an enabling environment to attract wawekezaji wa nje;tukaambiwa kwamba - sababu kwanini sisi maskini na tuna uchumi duni ni kwamba - hatuna capital;lakini we had abundant labor;ili kuendelea, ni lazima tukaribishe capital kutoka nje; na ili kufanikisha hilo, ni lazima tu create the necessary incentives - tax holidays, easy repatriations of profits, strict labour laws to keep workers' discipline in check, etc; tukafanya yote hayo mwanzoni mwa 1960s; kwa mfano, moja ya sheria za kwanza kupitishwa na bunge la TANU ilikuwa ni foreign investments(protection) act ya mwaka 1962 pamoja na preventive detention act mwaka huo huo;baadae kidogo a variety of anti strike laws nazo zikaja; pamoja na haya yote Zakumi, foreign investors wakatupotezea kwa namna fulani, hivyo tukashindwa kutumia mkakati wako kikamilifu uliosheheni hoja kwamba (rejea bandiko lako #1 3):

Unapokuwa na jamii lacking skilled labour, YOU MUST export raw materials and natural resources so that you import expertise, talent and capital
;

Na hapa sasa hoja ya Nguruvi3 dhidi ya hoja yako itakuwa na mashiko:

By the time tunaingia katika azinio la arusha, kulikuwa na very little foreign investments zimeingia nchini; cha ajabu ni kwamba, inflow ilianza kushika kasi baada ya azimio la arusha! (Rejea takwimu zilizopo); katika miaka ya 1960s-70s, tukawa tuna move erratically baina ya import substitution na export oriented industrialization kwa kutumia STATE CAPITAL, na kidigo local private capital na fedha nyingi kama mkopo toka nje pamoja na private management contracts;miradi hii (mingi), ilikufa, hilo tunajua, na ni kwa sababu nyingi tu za ndani na nje ya nchi; tukiacha hili la sababu kwa muda, tuangalie matokeo:

*We manage to establish mass good industries kama textile, oil, leather etc kwa mafanikio makubwa sana; kumbuka, most mass good industries zilijengwa kwa state capital, very little came from loans and foreign capital; Cha ajabu ni kwamba: kufuatia liberalization, marketization and privatization, a process of de-industrilization set in; again, more useful industries built na state capital as discussed hapo juu were the hardest hit, why? Because of nyerere? Cha kuchanganya akili watanzania - george kahama alikuwa ni kiongozi aliyesimamia na kuratibu our industrilization chini na NDC in the 1970s;huyu huyu baadae in late 1980s akapewa tena jukumu la kusimamia de-industrilization lama mkubwa wa kwanza wa IPC (investment pronotion centre), leo ikiitwa TIC, akiwa na Karabani kama deputy wake; Kingine cha kutushangaza wananchi - waziri kighoda ndiye aliyesimamia uuzwaji wa viwanda hivi in the 1990s kuelekea karne ya 21 (2000); leo hii kapewa dhamana ya kufufua viwanda nchini; ndio maana naishia kuuliza, hivi kwa maskini wa tanzania, uchumi wetu ni kitendawili au mazingaombwe?

Mwisho - je matatizo na changamoto tulizojadili humu, je zinahitaki kipi kati ya haya:
*Reforms (tuendelee katika kuamini kwamba reforms can work and deliver to the poor as long as kuna political will)? Au
*Structural transformation? au this can come about kupitia reforms?
*Revolutionary ideas?


Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
Mchambuzi, Nirejee tena baada ya kuwasoma wanajamvi walionigusa kwa namna moja au nyingine.

Mkandara : Nakubaliana na dhana yako ya ujamaa na ubeapri.

Kwa bahati mbaya sisi hatupo katika sehemu ya yote mawili. Kundi letu ni la 'kuchanganyikiwa'


i)Ubepari-kuishi kwa mikopo. Tumechagua ubepari na tunaishi kwa mikopo,hatutumii mikopo hiyo kujikwamua. Robo inakwenda Uswiss au kuonekana katika ofisi za CAG. Hakuna public investment bali ni tumbo street

ii)Ujamaa- kuishi kwa kile ulichonacho. Hatuishi hivyo kwasababu tuna vitu kama serikali kubwa, tumeua viwanda hata vya sabuni au kahawa. Tunatumia fedha nyingi kufuja na marupurupu n.k.

Hakuna saving kwa kile tulicho nacho.


Maswali ya Mchambuzi yanakuja; Endapo tuna resources kama human capital na natural resources wapi tatizo letu lilipo?Kichuguu katoa jibu moja rahisi sana na muhimu sana, Uongozi

Zakumi
; Sera za Nyerere kuhusu viwanda zilishindwa.
Sikubaliani na hili. Ninakubaliana na Kichuguu tulishindwa kuendeleza sera nzuri kwa kuzifanyia maboresho.

i)Leo tunaagiza nyama kutoka Uarabuni na Brazili,tunauza ng'ombe huko na bado tunao wengi.
Je, Tanganyika packers haikupaswa kufanyiwa maboresho badala ya kufanywa 3 star hotel.


ii) Tunanunua viberiti kutoka Pakistan. Kwanini hatukufanyia maboresho Kibo match kwa kutumia Sao hill?

iii) Tumeua Kilimanjaro machine/Mang'ula, je hatuhitaji vipuri hadi tuagize sub satndard kutoka China?

iv) Tumeua Maturabai Morogoro na Moshi tanneries, tunaagiza maturabai kutoka china na tunauza ngozi ili tuletewe bidhaa za ngozi kwa bei ya laki 2 kwa pair. Hapo Nyerere alishindwa nini. n.k n.k

gfsonwin- Hakuna investment kwa kutumia resources zetu. Tatizo letu ni kutokuwa na mipango ya nini kiwe kipaumbele na kwa njia gani kama alivyouliza Mchambuzi.

Tunatakiwa tupange kama kilimo ndio njia yetu basi madini yanaweza kutupatia investment katika elimu, utalii katika afya n.k. Lazima tuwe na mkakati tunalenga nini na kwasababu zipi. Sasa hivi hatujui tunafanya nini ndio maana wataalamu wanafikiria sigara na bia kukidhi bajeti. Kama si aibu sijui ni kitu gani.


Zakumi, ukitaka kuua taifa lolote usitumie silaha utaonekana mbaya, peleka kifo cha elimu.

Badala ya kufikiria kupandisha viwango vya elimu ili kupata competitive students tunashusha kwa div 5 kwasababu za kisiasa. Impact ya jambo hili i kubwa katika uchumi kuliko inavyodhaniwa.


Taifa kubwa kama Marekani linaposhtuka kuhusu elimu sisi hatupaswi kuwa na waziri anayefaulisha kwa kiwango cha div 5. Jibu la tatizo hili kama sehemu ya uchumi analo Kichuguu nalo ni Uongozi.

Nimalizie kwa kusema hakuna awamu iliyofanya vema katika uchumi kuliko awamu ya kwanza.
Hakuna taifa lililoendelea bila kwanza kuanza kujiendeleza ndani hasa katika elimu na miundo mbinu.


1) Elimu; viongozi wa sasa ni investment ya awamu ya kwanza na hata vizazi vyao ni sehemu ya investment hiyo
2) Miundo mbinu: Awamu ya kwanza ndiyo iliyowahi kujenga miundo mbinu kuliko awamu zote tatu zilizofuata kwa pamoja.

i) Uwekezaji katika nishati ya umeme
ii)Ujenzi wa reli na barabara.

Kuna tofauti ya ujenzi na ukarabati. Ukarabati hufuatia ujenzi na wala siyo ujenzi.

iii) Uwekezaji katika viwanda vidogo kwa ajili ya matumizi ya ndani, kukuza ajira na kuongeza tahamani za bidhaa ziuzwazo nje.

Nini kifanyike
a) Lazima tubadilike na tupate uongozi wenye mission and vision plus commitment
b)Tufanye specialization ya kile tunachokusudia kiuchumi
c)Tuishi kulingana na hali yetu ikiwa ni pamoja na serikali ndogo yenye tija isiyo na gharama
d)Tuwe na ujasusi wa kiuchumi na si delivery unit isiyotoa mchango bali tathmini.


Nguruv3:

Kuhusiana na elimu tunakubaliana. Kuhusiana na viwanda Nyerere alichemsha. Na katika posti zangu nimejaribu kuonyesha kuwa hakuwa pekee yake. Kwame, Kaunda na Mobutu walichemsha.

Katika ngazi ya kitaifa ya utengenezaji wa sera, viwanda vinaanzishwa kukidhi economic imperatives. Kwa mfano viwanda vitatoa ajira. Viwanda vitatumia local raw materials etc etc.

Katika ngazi ya uendeshaji wa viwanda vyenyewe, viwanda vinanzishwa kukidhi business imperatives. Moja ya hizo imperatives ni kupata faida.

Ukitaka kupata picha ya viwanda vya umma, chambua imperatives katika ngazi zote mbili. Viwanda vingi vilikuwa na malengo mazuri ya uchumi wa kitaifa. Lakini uendeshaji wake ulikuwa sio wa kibiashara.
 
Elimu ya nchi hii, kamwe haitaweza kuinuliwa na mwanasiasa hata siku moja, tena elimu yetu ikiwezekana lisiwe jambo la kisiasa.

Nasema lisiwe jambo la kisiasa nikimaanisha kwamba watendaji wake wawe mawaziri ambao sio wafuasi wa chama cha siasa na ili kupatikana waombe kazi wafanyiwe usaili na awajibike kulingana na kazi ambayo sisi tunampa na sio ambayo iko kwenye ilan za vyama vyao.

Naboreka sana kuona VIHIYO ni wengi sana kwenye serikali ambao pia hawako dedicated na kukuza elimu ya taifa hili. inatia uchungu sana kumkuta mtu kama Mulugo anabishana na Prof Mchome kwa mawazo ambayo aliyapata kwenye kikao cha baraza la mawaziri tena nje ya katibu mkuu halafu anakuja kusema eti msimamo wa serkali kweli hii inatupa picha gani?? sisi tumekuwa wajinga kwa kukaa kimya ifike mahali tuseme tumechoka tunahitaj mabadiliko ya haja

Nchi zote wanazotolea mifano hapa kama China, Taiwan,South Korea zilianza na watu wenye strong personalities and results oriented. Toka Tanzania imepata uhuru, viongozi wanatoa maamuzi baada ya maamuzi lakini hawafuatilii utekelezaji wake. Na hilo ndio tatizo kubwa.
 
Nguruv3:

Kuhusiana na elimu tunakubaliana. Kuhusiana na viwanda Nyerere alichemsha. Na katika posti zangu nimejaribu kuonyesha kuwa hakuwa pekee yake. Kwame, Kaunda na Mobutu walichemsha.

Katika ngazi ya kitaifa ya utengenezaji wa sera, viwanda vinaanzishwa kukidhi economic imperatives. Kwa mfano viwanda vitatoa ajira. Viwanda vitatumia local raw materials etc etc.

Katika ngazi ya uendeshaji wa viwanda vyenyewe, viwanda vinanzishwa kukidhi business imperatives. Moja ya hizo imperatives ni kupata faida.

Ukitaka kupata picha ya viwanda vya umma, chambua imperatives katika ngazi zote mbili. Viwanda vingi vilikuwa na malengo mazuri ya uchumi wa kitaifa. Lakini uendeshaji wake ulikuwa sio wa kibiashara.
Ok, kwahiyo basically tunakubaliana kuwa strategy ya nyerere ya import substitution kuelekea exports promotions ilikuwa sound and viable.

Kilichokosekana na management bora. Kwa mantiki hiyo nakubaliana nawe.
Hapa ndipo Kichuguu amesema tulipaswa tuboreshe yale mazuri kwa kuyafanya kwa njia nzuri zaidi.

Kwanini viwanda vya sigara na bia vipo hadi sasa na vimefanyiwa maboresho lakini morpco, Polyster, Mwatex, UFI na Mangula vimetolewa kama maghala. Vipi kama tungevifanya kama vya sigara na bia.
Hatuwezi kulaumu 'foundation' nzuri kwa nyumba tuliyoezeka hovyo.
 
Last edited by a moderator:
Nyerere atabaki katika historia ya Taifa hili miaka yote kwa vile ndiye aliyekuwa Rais wa wake wa Kwanza. Ni kama ambavyo Stalin na Mao walivyo katika historia za nchi za Urusi na China. Wenzetu huko wanaendelea tena kwa kasi sana na hawana ngonjera za Mao wala Stalin; sisi tusipogundua makosa hayo tutabaki kuwa walalamikaji dhidi ya Nyerere huku tukiwa hatuoni makosa yetu yenyewe. Tutabaki na viongozi wanaoficha mafedha ya umma uswisi wakati serikali inashindwa kulipia majukumu yake halafu bado tukalalamika tena kuwa makosa yote ya serikali kukosa hela ni kutokana na Nyerere. Tena afadhali kabisa Nyerere alijitahidi kujenga viwanda vya ndani, alichokosea ni namna ya unedeshaji wa viwanda hivyo kwani uongozi wake baadaye ukawa wa kisiasa zaidi badala ya kuwa uongozi wa kibiashara. Tungefanya marekebishao hayo ya kuvifanya viwanda hivyo vijiendesha kibiashara kwa mfano kuuza hisa kwa watu binafsi tungesaidia sana kuimarisha viwanda hivyo. Lakini badala yake sisi tuliposikia neno privatization hatukulichukulia kwa maana yake pana ya Private Sector, sisi tukalichukulia kwa maana finyu ya private individual. Kwa hiyo tukawa tunamtafuta mtu mmoja tajiri sana wa kumwuzia, ambaye alikuwa anatafutwa kutoka nje ya nchi. Kenya pale walipo-privatize Kenya Airways waliuziana hisa wakenya wenyewe kwa wenyewe na leo unajua shirika hilo liko wapi. Kuuza kiholela viwanda vile vya Nyerere hakukuwa ni kurekebisha bali kulikuwa ni kubomoa kabisa ndiyo maana nchi leo ipo ipo tu ikiwa kama mwendawazimu. Tutaendelea hivi hivi mpaka tukome wenyewe.


Mimi nimeona kuwa swali lililotolewa hapa ni Uchumi wa Tanzania leo, siyo Historia ya Uchumi wa Tanzania Miaka 50 iliyopita. na hivyo sioni kabisa nafasi ya sera za uchumi alizofuata Nyerere katika maisha ya watanzania wa leo.

Lakini imekuwa kama wimbo vile; shule hazina vitendea kazi kwa sababu ya Nyerere. Migodi ya madini inachimbwa lakini serikali haipati chochote kwa sababu ya Nyerere. Miradi ya ujenzi wa miundo mbinu serikali inatolewa kinyemela kiasi kuwa ujenzi wake unakuwa ni substandard kwa sababu ya Nyerere. Manunuzi ya serikali yanakuwa ni ghali sana kuliko thamani halisi, kwa mfano ile rada tulilipa hela nyingi sana, kwa sababu ya Nyerere.

Hiyo haitufikishi popote. Itafika wakati ambapo historia kamili itaihukumu vibaya sana awamu ya tatu na kidogo awamu hii ya nne. Historia kamili haisemi uwongo, kwa sasa hivi tutajitahidi kujiandikia historia yetu lakini ile kamili itakapokuja ukweli utajulikana.
 
wanabodi Mchambuzi, Kichuguu, Nguruvi3, Zakumi, Ngongo na zumbemkuu asanteni sana kwa mjadala mzuri na webye tija kabisa katika taifa tena unao chambua mambo kwa uhaisia wake zaid kuliko porojo za kisiasa.

Binafsi naomba nirudi maadae kujadili juu ya nini kifanyike kwaajili ya kuinua science, technology and innovations kwaajili ya kukuza uchumi wa taifa letu. yaani WHAT SHALL BE DONE SO AS TO HAVE DEVELOPED SCIENCE,TECHNOLOGY AND INNOVATIONS FOR BEST ECONOMIC ACHIEVEMENTS.

Kwasasa naomba niwajibike kidogo na majukumu mengine.
 
Last edited by a moderator:
Mchambuzi;7792056]*Ukosefu wa serikali katika ushiriki wa uzalishaji kwenye uchumi (mfano Ngongo), mtazamo ambao kwa kiasi fulani unaendana na wa Nguruvi3, na kupishana na Zakumi; kwa maana nyingine, participation ya serikali as a marginal regulator na mkusanyaji tu kodi (tena barely)inachangia mambo kutokuwa swa, tofauti kama serikali ingekuwa strategically & selectively involved in production, facilitation/providing an enabling environment for the indegenous private and SME sectors kushiriki katika uchumi unaopigiwa makofi na wanasiasa wa ccm;

Last but not least, nigusie masuala mawili: Kwanza ni hoja ya Nguruvi3 kwamba export promotion is a must do strategy, na kwamba ni muhimu kujikita katika maeneo ambayo we have a comparative advantage (ardhi, utalii, madini n.k);

Hapa ningependa kusikia zaidi kutoka kwake on how we can balance between producing for exports and meeting local needs katika muktadha ambao our market is flooded with Chinese products;

Kwa kugusia kidogo tu, south africa kwa kiasi fulani wanajitahidi ku balance between the two, sisi changamoto zipo wapi?

Nguruvi3
kajadili masuala ya viwanda kufeli kutokana na high input costs, je kuna masuala mengine? Anajadili pia juu ya umuhimu wa kujenga core competency katika maeneo fulani ili tuwe competitive, je ni suala la human capital development peke yake?
Nikubaliane kuwa kazi ya serikali ni kuwa 'strategically, selectively and facilitator' for the economic growth. Kwa bahati mbaya na kwa makusudi kabisa kazi haifanaywi hivyo kutokana na culture ya corruptions iliyojengeka. Hakuna mahali rahisi pa kufanya mauza uza kama serikalini.

Si ajabu mradi kutangaza utalii unafanywa na serikali kwa mabilioni na return haina uwiano na investment. Serikali kupitia balozi zake inatakiwa ijenge mazingira kwa kutumia diplomasia ya uchumi kuwezesha mashirika,private, entrepreneur na SME kufanya kazi ya kutangaza utalii. Huu ni mfano ni mingi.


Pili, hatujaitumia vema nafasi ya exports. Nilisema hapo nyuma kuwa kama tungekuwa makini na kilimo pengine exports zetu zingekuwa katika eneo hilo. Kwasasa soko la ndani linajitosheleza kwa kilimo.
Utashangaa kuona kuna njaa, jibu ni rahisi ya kuwa tunazalisha hatujui kuhifadhi.

Katika hali ya kawaida lazima kuwe na grain reserve kila kanda na pengine kila mkoa. Hatuwezi kufanya hivyo kutokana na sababu mbili.
1. Hakuna watu wa kufikiria kuhusu tatizo hilo, na njaa ni sehemu ya miradi ya watu
2. Hakuna miundo mbinu, hakula kinaoza Sumbawanga kuna njaa Kilombero. Na ile miundo mbinu liyopo hatuitumii kurtusaidia. Tunatumia vipi Tazara, reli ya Kilombero-Kilosa, Tanga Ruvu, Dar Mwanza, Kigoma. Arusha Moshi!Zote tumegeuza vyuma chakavu na tunatumia malori ya jeshi kubeba chakula. Kuna mkakati hapo.

Hatujatumia comparative advantage zetu vema kama ardhi, utalii na madini. Ni kiasi gani cha madini kinachangia pato la taifa na kutoa matokeo chanya? Kwanini simu za mikononi ziongoze madini katika pato la taifa na si madini. Definite kuna tatizo

Bidhaa feki za China zipo kwasababu hakuna mbadala. Tulikuwa na Matsushita iliyotengeneza betri bora EA. Hakuna aliyeIngiza betri feki kwasababu hazikuweza kushindana na za nyumbani.

Ndivyo ilivyokuwa kwa General tyre, maturubai na bidahaa n.k. Soko la ndani lipo na linajitosheleza hata kutoa nafasi ya exports. Kwasababu hakuna mpangilio ni rahisi kuona kama kuna mapungufu. Na kwasababu hakuna mpangilio ni rahisi kuona kama kuna imbalance ya local needs na exports


Najaribu sana kuongelea vitu vinavyoathiri maisha ya mtanzania wa dola mbili kwa siku kwa tathmini tu.
Hivi kwanini Revola iliweza kushindana na imperial kutoka Univerliver enzi hizo.

Kilichoua viwanda vyetu ni kukumbatia tax exemptions na kubebesha mzigo kwa viwanda vya ndani.

Hakuna taifa lililoendelea lisilo na 'protectionism'. Marekani wana ugomvi na NAFTA na China kwasababu hiyo.
Ireland imepiga marufuku hata uingizaji wa mayai kutoka nchi nyingine za EU.
Uingereza ina weka kodi kubwa kwa import goods n.k. Lengo si kuzuia ushindani lakini ushindani huo lazima uwe fair.Hili linaua sana sekta binafsi za wazawa tukubali

Kwa ulinganifu na Afrika kusini tuna changamoto nyingi.
1. a)Kufufua na kutengeneza miundo mbinu ya nishati na uchukuzi ili kupunguza gharama za uzalishaji
Hatuwezi kushindana na wenzetu kutokana na ongezeko la gharama kama nishati.

b)Hatuna miundo mbinu ya kusafirisha bidhaa kufikia soko la ndani au la nje. Usafiri rahisi na wa uhakika ni wa reli. Je, ni ngapi tunazitumia katika kiwango tarajiwa. Ni zipi zinaunganisha nchi na sehemu za uzalishaji.

2 a)Ni lazima tuwe na malengo katika uzalishaji na matumizi.
Tunaweza kufanya kilimo kama sehemu ya exports zetu kwa bidhaa za biashara. Kwanini Kenya wauze majani ya chai na kahawa yetu na kuiuza duniani sisi tulale kwa kisingizio cha kuanguka soko.
Kwanini tununue substandard na mitumba ikiwa tunalima pamba na tuna viwanda. Je mchina anawezaje kulitosheleza soko letu la ndani kwa bidhaa feki sisi tushindwe tukiwa na rasilimali zote

b) Tuwe na grain reserve za kutosha, suala la kuagiza chakula liwe historia na ziada ya chakula ambayo ni nyingi hata katika kilimo cha sasa cha ubabaishaji iuzwe nje. Kwanini Uganda waje kuchukua mchele Shinyanga sisi tushindwe kuufikisha Lindi.Hatuna tatizo la soko,rasilimali watu au ushindani. Tuna tatizo la kutojua tufanye nini na kwa njia gani.

3. Tuwekeze katika rasilimali watu. Elimu yetu iwe ya maarifa na si kukariri. Ilenge ushindani na si ufaulu. Tubadili mitaala ili kuandaa watu kwa ajili ya ushindani na si ajira.

4. a)Serikali ijitoe katika shughuli za uchumi bali iandae mazingira mazuri tu na kazi hiyo ifanye na sekta binafasi. Serikali ya south Africa haifanyi biashara, inaandaa mazingira kwa watu wao kufanya biashara.
NBC ipo Dar mahesabu yanafanyika J'burg! Tujiulize kwanini CRDB iweze ushindani na benki za Afrika halafu b) General tyre ishindwe katika ushindani na mitumba ya matairi kutoka China!
Shughuli za uchumi zifanywe na wachumi na si kamati za bunge. Wanasiasa waendelee na malumbano na uchumi usimamiwe na wachumi.

5. Muhimu sana lazima tuwe na vitengo vya ujasusi na si delivery unit. Unakuwaje na delivery unit isiyojua ime invest wapi? Nani anajua kuwa sisi tunaweza kuuza chuma East and central Africa. Nani anajua kuwa tunauza madini ya kioo kuliko nchi nyingine ya EA. Nani anajua kuwa tuna ameneo mazuri ya kilimo cha maua n.k.
Nani anajua tuna best cement in the continent na soko lake lipo wazi.

Juu ya yote hakuna kitakachowezekana bila uongozi wenye mission na vision. Uongozi usio corrupt na ambao ni committed katika uchumi na si cheap politics. Uongozi huo haupo ndani ya CCM


 
Ok, kwahiyo basically tunakubaliana kuwa strategy ya nyerere ya import substitution kuelekea exports promotions ilikuwa sound and viable.

Kilichokosekana na management bora. Kwa mantiki hiyo nakubaliana nawe.
Hapa ndipo Kichuguu amesema tulipaswa tuboreshe yale mazuri kwa kuyafanya kwa njia nzuri zaidi.

Kwanini viwanda vya sigara na bia vipo hadi sasa na vimefanyiwa maboresho lakini morpco, Polyster, Mwatex, UFI na Mangula vimetolewa kama maghala. Vipi kama tungevifanya kama vya sigara na bia.
Hatuwezi kulaumu 'foundation' nzuri kwa nyumba tuliyoezeka hovyo.

Mkuu Nguruv3;

Umeshawahi kujiuliza kwanini hata kwenye nchi kama North Korea and Cuba, viwanda vya bia na sigara bado vinafanya kazi? Vinafanya kazi pamoja na matatizo ya kiuchumi walionayo.

Ukiweza kupata jibu ya swali langu, utaona kuwa kuna factors zinazofanya uendeshaji wa viwanda hivi kuwa kitu kinachowezekana kwa jamii yoyote hile. Sijaona jamii yoyote iliyoshindwa kuendesha uzalishaji wa pombe na sigara. Hivyo basi the survival of cigarette and beer companies wasn't that special.
 
Mkuu Nguruv3;

Umeshawahi kujiuliza kwanini hata kwenye nchi kama North Korea and Cuba, viwanda vya bia na sigara bado vinafanya kazi? Vinafanya kazi pamoja na matatizo ya kiuchumi walionayo.

Ukiweza kupata jibu ya swali langu, utaona kuwa kuna factors zinazofanya uendeshaji wa viwanda hivi kuwa kitu kinachowezekana kwa jamii yoyote hile. Sijaona jamii yoyote iliyoshindwa kuendesha uzalishaji wa pombe na sigara. Hivyo basi the survival of cigarette and beer companies wasn't that special.

Zakumi,

Suala sio kuwa special, suala ni mchango wa viwanda husika in terms of backward and forward linkages in the economy;suala ni mchango wa viwanda husika kwa pato la taifa;suala ni mchango wa viwanda husika kwenye kodi; je unaweza jadili hoja yako hapo juu katika muktadha huu, ikizingatiwa kwamba hizo bia na sigara, ujenzi wake wa viwanda ulitokana na mauzo ya mazao ya wakulima nje ya nchi? Je unajua economics za addictive products kama bia na sigara katika dunia ya sasa?kwanini unadhani Miller walikubali ku merge na SAB to form the second largest beer company in the world if not the first? Mwisho and more importantly, je unajua katika import substitution strategy, busara huwa ni kuanza na viwanda vyenye bidhaa zenye immediate demand katika soko la ndani pamoja na light (not heavy) manufacturing? Mwalimu alikosea nini hapo?

Naomba utafakari attitude yako towards viwanda hivi na hoja yako kwenye bandiko namba kumi na tatu ya mjadala uliposema:

Unapokuwa ni jamii lacking skilled labour, you must export raw materials and natural resources so that you import expertise, talent and capital

How do you merge hoja zako hizi mbili ili ueleweke vizuri zaidi?



Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
Zakumi,

Suala sio kuwa special, suala ni mchango wa viwanda husika in terms of backward and forward linkages in the economy;suala ni mchango wa viwanda husika kwa pato la taifa;suala ni mchango wa viwanda husika kwenye kodi; je unaweza jadili hoja yako hapo juu katika muktadha huu, ikizingatiwa kwamba hizo bia na sigara, ujenzi wake wa viwanda ulitokana na mauzo ya mazao ya wakulima nje ya nchi? Je unajua economics za addictive products kama bia na sigara katika dunia ya sasa?kwanini unadhani Miller walikubali ku merge na SAB to form the second largest beer company in the world if not the first? Mwisho and more importantly, je unajua katika import substitution strategy, busara huwa ni kuanza na viwanda vyenye bidhaa zenye immediate demand katika soko la ndani pamoja na light (not heavy) manufacturing? Mwalimu alikosea nini hapo?

Naomba utafakari attitude yako towards viwanda hivi na hoja yako kwenye bandiko namba kumi na tatu ya mjadala uliposema:



How do you merge hoja zako hizi mbili ili ueleweke vizuri zaidi?



Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums

Mchambuzi;

Mnatoa hoja kwa kutumia emotions. Lakini unapofanya analysis ni lazima utumie numbers. Nyerere alianzisha viwanda vingi. Kwa uchache let's say alianzisha viwanda 100. Katika viwanda hivi ni viwanda 2 vya bia na kimoja cha sigara mnavyoshikia bango. Hii ni asilimia 3 tu ya mafanikio.

Mnaweza kuongeza idadi ya viwanda vilivyofanikiwa, lakini asimilia ya mafanikio bado itabaki kuwa chini ya 20. Kama ni kutoa grade, Tanzania bado inayo F.

Na ukitumia volume ya capital iliyotumika kuanzisha viwanda, uwiano wa capita ya viwanda vilivyofanikiwa kwa viwanda vilivyoanzishwa bado nitaipa Tanzania grade F.

Tukirudi kwenye viwanda vya bia na sigara:

Beverage, alcohol, and cigarette processing plants are easier to start and run. Vinatumika ku-generate revenue. Kama South Korea au China (Asian tigers) wangeridhika kwa sababu wameweza kumudu kuendesha viwanda vya sigara na bia, basi wasingeweza kufanikiwa katika Export Promotion Strategies ambayo ndio theme ya thread hii.
 
Mchambuzi;

Mnatoa hoja kwa kutumia emotions. Lakini unapofanya analysis ni lazima utumie numbers. Nyerere alianzisha viwanda vingi. Kwa uchache let's say alianzisha viwanda 100. Katika viwanda hivi ni viwanda 2 vya bia na kimoja cha sigara mnavyoshikia bango. Hii ni asilimia 3 tu ya mafanikio.

Mnaweza kuongeza idadi ya viwanda vilivyofanikiwa, lakini asimilia ya mafanikio bado itabaki kuwa chini ya 20. Kama ni kutoa grade, Tanzania bado inayo F.

Na ukitumia volume ya capital iliyotumika kuanzisha viwanda, uwiano wa capita ya viwanda vilivyofanikiwa kwa viwanda vilivyoanzishwa bado nitaipa Tanzania grade F.

Tukirudi kwenye viwanda vya bia na sigara:

Beverage, alcohol, and cigarette processing plants are easier to start and run. Vinatumika ku-generate revenue. Kama South Korea au China (Asian tigers) wangeridhika kwa sababu wameweza kumudu kuendesha viwanda vya sigara na bia, basi wasingeweza kufanikiwa katika Export Promotion Strategies ambayo ndio theme ya thread hii.



Nasubiria majibu ya hoja zangu nilizoelekeza kwako kwenye bandiko #43 hapo juu; Wakati tukisubiri hayo, ningependa tujadili numbers kama unavyopendekeza, lakini tuje na namba zilizopo, sio kama ulivyofanya hapo juu; Tuanze kwa kuangalia mchango wa viwanda katika uchumi wa nchi:

Moja:

As of early 1960s, mchango wa viwanda kwenye pato la taifa ulikuwa ni around 3-4%; Kufuatia azimio la arusha, ambapo hapo awali nimekueleza kwamba ndio kipindi tukaanza kuona inflow kubwa ya foreign capital nchini (not before azimio hilo), mchango wa sekta ya viwanda ikafikia 8% mwanzoni mwa 1970s na kufikia hadi 19% in 1995; ndio maana nakuuliza, je, kosa la Nyerere lilikuwa kwenye drawing board au katika utekelezaji? Haujaja na majibu; Katika majibu yako, ni muhimu ujadili both, internal and external factors juu ya kwanini tulianguka katika viwanda;

Pili:

Umuhimu wa viwanda katika uchumi ni potential high economic returns, greater production and employment linkages, and productivity improvements through technological adaptation; Kwa kweli tulijitahidi katika haya yote, given the low economic base tuliyoanza nayo tofauti na nchi nyingine za dunia ya tatu kwa wakati ule; Hata numbers zinadhihirisha juu ya ukweli huu:

Kwanza - mchango wa sekta ya viwanda kama nilivyoeleza ulikuwa unaongezeka siku hadi siku; production &uliku
Je una economic linkages zilikuwa zinaimarika, huku changamoto kubwa ikiwa kwenye productivity improvement kupitia technological adaption; nikipata muda nitaleta takwimu juu ya ujweli huu, ila tujadili tulijikwaa wapi, sio tulianguka wapi; Jiulize - kwanni the west embraced our approach to industrialization and economic development mwanzoni, na je, nini kiliharibika baadae?

Na Tatu:
Pamoja na umuhimu wa kutazama wenzetu wa south korea et al walifanikiwa vipi, ni muhimu tukafahamu kwamba development isn't path dependent, kwahiyo siri ya mafanikio katika dunia ya leo haitatokana na kuiga south korea walifabya nini, badala yake it has to involve zaidi home grown strategies ambazo ni more specific kwa mazingira yetu; Hakuna taifa duniani lililopiga hatua kwa kuiga mwenzake;hata east asin tigers hazikufuata policies and strategies zinazofanana, na leo hii, kila nchi ina strenghts zake na weaknesses zake kutokana na hilo, mfano south korea, singapore, malaysia, taiwan...;

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Mchambuzi;

Mnatoa hoja kwa kutumia emotions. Lakini unapofanya analysis ni lazima utumie numbers.

Nyerere alianzisha viwanda vingi. Kwa uchache let's say alianzisha viwanda 100. Katika viwanda hivi ni viwanda 2 vya bia na kimoja cha sigara mnavyoshikia bango. Hii ni asilimia 3 tu ya mafanikio.

Mnaweza kuongeza idadi ya viwanda vilivyofanikiwa, lakini asimilia ya mafanikio bado itabaki kuwa chini ya 20. Kama ni kutoa grade, Tanzania bado inayo F.

Na ukitumia volume ya capital iliyotumika kuanzisha viwanda, uwiano wa capita ya viwanda vilivyofanikiwa kwa viwanda vilivyoanzishwa bado nitaipa Tanzania grade F.

Tukirudi kwenye viwanda vya bia na sigara:

Beverage, alcohol, and cigarette processing plants are easier to start and run. Vinatumika ku-generate revenue. Kama South Korea au China (Asian tigers) wangeridhika kwa sababu wameweza kumudu kuendesha viwanda vya sigara na bia, basi wasingeweza kufanikiwa katika Export Promotion Strategies ambayo ndio theme ya thread hii.
Kwanza jibu nililokusudia keshalieleza Mchunguzi pengine zaidi ya nilivyokuwa nafikiri.

Hoja ambayo hujibu ni kuwa Nyerere alianzisha viwanda, je hilo lilikuwa kosa kwa kuzingatia mada ya inward and outward looking?
Pili, katika viwanda alivyoanzisha vingapi vilifia mikononi mwake?
Tatu, unafahamu kazi ya PSRC na mashirika yaliyouzwa ilikusudia nini
Nne, Je, hatuthitaji Mwatex, Urafiki, UFI, Cement na Magunia kwa sasa?

Nilitolea mfano wa viwanda vya bia na sigara na sasa naongeza kwanini Viwanda vya saruji havikufa.
Kwanini Mang'ula na Moshi machine tools vilikufa baada ya kuondoka kwake.
Nini mchango wa viwanda hivyo katika pato la taifa kama alivyosema Mchunguzi hapo juu
 
Mkuu Nguruvi3, umejadili hoja za msingi sana #48 ;joja zako zimeniacha na maswali mengi kuliko majibu; Kwa mfano, with all due respect, hivi ni sawa kweli kwa mtanzania tajiri kuliko wote kuwa ni muuza unga wa sembe, ngano, ice cream, majo ya kunywa, na juisi ua maembe? Waziri Muhongo na wenzake wanajisikiaje na hali hii - kwa maana ya kwamba uchuni wetu unakuzwa na sekta ambazo hazina mahusiano na indigenous private sector? Sitashangaa iwapo wenye kufaidika na mafanikio ya kukua uchumi (output sekta za madini, maliasili,...) Ni wanasiasa kuliko wafanyabiashara; pengine mtazamo wangu sio sahihi, lakini nimeona nilisemee hili kidogo;

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
Mchambuzi na Nguruv3:

Nimewajibu mara nyingi hoja zenu lakini mawazo yenu yako kwenye mwelekeo wa maendeleo ya kiformula ambayo inaangalia maendeleo ya Tanzania kwa kutumia darubini ya maendeleo ya kichina au south korea.

Kumtetea Mwalimu, Kichuguu anasema kuwa idadi ya wasomi wakati wa Mwalimu Nyerere ilikuwa ndogo. Hili ni suala lisilopingika. Viwanda mnavyovitaja viliitaji skilled labour hili kuwa na mafanikio. Skilled labour inajumlisha elimu na uzoefu. Enzi ya mwalimu watu walikuwa wanamaliza vyuo na kwenda kuwa mameneja bila kuwa na uzoefu wakazi. Hivyo pamoja na kuwa na nia nzuri, risk factors za kusababisha viwanda kufail zilikuwa tayari zinaongeza kwa kutumia unskilled labour.


Kwa kifupi tu Tanzania ina nafasi kubwa ya kuendelea bila kutumia formulation zenu. Kinachotakiwa ni kufanya vitu vya kawaida tu na kutumia common sense.

Kagame mnayemsifia hapa hana elimu ya kutisha. Na uongozi wake sio dogmatic lakini anafanikiwa kwa sababu anatumia common sense. Kagame anataka walimu wenye sifa wawe madarasani. Kagame anapinga rushwa. Kagame anataka watu wawajibike katika nafasi zao za kazi. Jariibu hivi vitu na kizazi kinachokuja cha watanzania kitaanza kufikiri kwenda mwezini.
 
Mkuu Nguruvi3, umejadili hoja za msingi sana #48 ;joja zako zimeniacha na maswali mengi kuliko majibu; Kwa mfano, with all due respect, hivi ni sawa kweli kwa mtanzania tajiri kuliko wote kuwa ni muuza unga wa sembe, ngano, ice cream, majo ya kunywa, na juisi ua maembe? Waziri Muhongo na wenzake wanajisikiaje na hali hii - kwa maana ya kwamba uchuni wetu unakuzwa na sekta ambazo hazina mahusiano na indigenous private sector? Sitashangaa iwapo wenye kufaidika na mafanikio ya kukua uchumi (output sekta za madini, maliasili,...) Ni wanasiasa kuliko wafanyabiashara; pengine mtazamo wangu sio sahihi, lakini nimeona nilisemee hili kidogo;

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums

Unachozungumza hapa doesn't make any sense in business world. Mfanyabiashara yoyote anachoangalia ni Balance sheet yake. Leo ikitokea kuwa biashara ya kuzoa kinyesi inatoa faida nzuri, kuna uwezekano Bakhresa au Mengi akaasha biashara anazofanya sasa na kujikita kwenye uzoaji wa kinyesi.

Kutokuwa na watu wenye business sense katika mashirika ya umma ilichangia kuanguka kwa mashirika hayo. Bakhresa au Mengi anachofanya ni diversitification ya portifolio za investment zao.
 
Unachozungumza hapa doesn't make any sense in business world. Mfanyabiashara yoyote anachoangalia ni Balance sheet yake. Leo ikitokea kuwa biashara ya kuzoa kinyesi inatoa faida nzuri, kuna uwezekano Bakhresa au Mengi akaasha biashara anazofanya sasa na kujikita kwenye uzoaji wa kinyesi.

Kutokuwa na watu wenye business sense katika mashirika ya umma ilichangia kuanguka kwa mashirika hayo. Bakhresa au Mengi anachofanya ni diversitification ya portifolio za investment zao.

You are correct but only to an extent kwani ni dhahiri mtu kama mengi angependa kuhusishwa na biashara ambayo ni resource based lakini wazawa kwa kawaida wanawekewa vikwazo, vinginevyo tusingemsikia kwenye malumbano na muhongo wiki juzi;

Vile vile hoja zako hapo juu ni self contradictory kwani awali ulitoa hoja za kudharau uwekezaji wa Mwalimu kwenye sigara, bia, saruji ambavyo balance sheets zilikuwa na uhai mpaka kuuzwa kwake, lakini hapa unasema hata biashara ya kuzoa vinyesi ni biashara as long as ina faida;

Vinginevyo to an extent nakubaliana na hoja yako kwamba ukosefu wa watu wenye business orientation kulichangia viwanda vyetu kufa, lakini hii ni kwa sababu, dunia ya wakati ule ilitoa alternatives between business/market orientation and development (developmental state orientation) when it came to industrilization; tatizo lako unamjadili mwalimu kwa lensi ya liberalization, marketization and privatization ambayo hata ulaya na marekani, zilikuja na reagan na thatcher, otherwise the state played a major role katika kipindi cha awali; fanya utafiti kuhusu role of central banks in western europe na USA, and the role that has been preached to us since the emergence of SAPs in mid 1980s;

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Mchambuzi na Nguruv3:

Nimewajibu mara nyingi hoja zenu lakini mawazo yenu yako kwenye mwelekeo wa maendeleo ya kiformula ambayo inaangalia maendeleo ya Tanzania kwa kutumia darubini ya maendeleo ya kichina au south korea.

Sio kweli kwani over and over again nimejadili kwa uwazi kabisa kwamba "development isn't path dependent", hapa na kwenye mijadala mingine; naposema sio path dependent maana yake ni kwamba maendeleo ya nchi hayatokani na kufuata nyayo za nchi nyingine; USA, UK, india, brazil, RSA, south korea, singapore etc, wote wamefuata njia zisizofanana;

Kumtetea Mwalimu, Kichuguu anasema kuwa idadi ya wasomi wakati wa Mwalimu Nyerere ilikuwa ndogo. Hili ni suala lisilopingika. Viwanda mnavyovitaja viliitaji skilled labour hili kuwa na mafanikio. Skilled labour inajumlisha elimu na uzoefu. Enzi ya mwalimu watu walikuwa wanamaliza vyuo na kwenda kuwa mameneja bila kuwa na uzoefu wakazi. Hivyo pamoja na kuwa na nia nzuri, risk factors za kusababisha viwanda kufail zilikuwa tayari zinaongeza kwa kutumia unskilled labour.

Give us an alternative scenario yenye kuendana na wakati ule;

Kwa kifupi tu Tanzania ina nafasi kubwa ya kuendelea bila kutumia formulation zenu. Kinachotakiwa ni kufanya vitu vya kawaida tu na kutumia common sense.

Maendeleo ya nchi yanategemea fomula? Kama zipi?

Kagame mnayemsifia hapa hana elimu ya kutisha. Na uongozi wake sio dogmatic lakini anafanikiwa kwa sababu anatumia common sense. Kagame anataka walimu wenye sifa wawe madarasani. Kagame anapinga rushwa. Kagame anataka watu wawajibike katika nafasi zao za kazi. Jariibu hivi vitu na kizazi kinachokuja cha watanzania kitaanza kufikiri kwenda mwezini.

Wapi mimi nimeyakataa haya...

Mkuu Zakumi, nadhani unapopisha na mwalimu ni padogo tu: Yeye alijaribu kuepuka kuingia kwenye mtego wa nchi "to produce what it doesn't consume and consume what it doesn't produce"; In the process, makosa na mapungufu kadhaa yakajitokeza; Lakini pamoja na hayo, hoja zako zinaonyesha kulenga yale mwalimu aliyojaribu kuepuka;


Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
Mchambuzi;7805526Give us an alternative scenario yenye kuendana na wakati ule;
Maendeleo ya nchi yanategemea fomula? Kama zipi?
Mheshimiwa Zakumi majibu tafadhali.
 
Zakumi;7805425]Mchambuzi na Nguruv3Kumtetea Mwalimu, Kichuguu anasema kuwa idadi ya wasomi wakati wa Mwalimu Nyerere ilikuwa ndogo. Hili ni suala lisilopingika. Viwanda mnavyovitaja viliitaji skilled labour hili kuwa na mafanikio. Skilled labour inajumlisha elimu na uzoefu. Enzi ya mwalimu watu walikuwa wanamaliza vyuo na kwenda kuwa mameneja bila kuwa na uzoefu wakazi. Hivyo pamoja na kuwa na nia nzuri, risk factors za kusababisha viwanda kufail zilikuwa tayari zinaongeza kwa kutumia unskilled labour.
Zakumi unadhani Mwalimu angefanya nini kwa wakati huo na hali hiyo ya wasomi?
Kwa kifupi tu Tanzania ina nafasi kubwa ya kuendelea bila kutumia formulation zenu.
Kinachotakiwa ni kufanya vitu vya kawaida tu na kutumia common sense.
Vitu gani vya kawaida ambavyo hatujaviongelea?

Kagame mnayemsifia hapa hana elimu ya kutisha. Na uongozi wake sio dogmatic lakini anafanikiwa kwa sababu anatumia common sense. Kagame anataka walimu wenye sifa wawe madarasani. Kagame anapinga rushwa. Kagame anataka watu wawajibike katika nafasi zao za kazi. Jariibu hivi vitu na kizazi kinachokuja cha watanzania kitaanza kufikiri kwenda mwezini
Mafanikio ya Kagame ni yapi kwa kulinganisha hali za watu wa kawaida wa nchi hizi mbili?

Pili, tafadhali soma mabandiko kwa uangalifu. Katika bandiko 48 na yaliyotangulia nimeeleza kuwa kuna culture ya corruptions inayoharibu uchumi katika serikali.

Tatu, lazima uelewe kuwa Mwalimu aliokuwa na wasomi wachache aliwaendeleza kielimu huku akijenga miundo mbinu na hivyo vijiwanda vidogo tulivyo navyo.
Leo miaka 30 baada ya yeye kuwweka misingi hiyo tuna wasomi wa kila fani na kila kiwango.

Je, wasomi wetu wa sasa wa miaka 30 baada ya mwalimu wamefanya kitu gani tunachoweza kusema Mwalimu alishindwa au alikosea.
Je, kukusanya kodi za bia, sigara na vocha za simu ndio mafanikio zaidi ya yale ya vijiwanda vya Mwalimu?
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom