Uchumi wa Tanzania: Je, Ni Kitendawili au Ni Mazingaombwe Kwa Maskini?

Uchumi wa Tanzania: Je, Ni Kitendawili au Ni Mazingaombwe Kwa Maskini?

Nyerere atabaki katika historia ya Taifa hili miaka yote kwa vile ndiye aliyekuwa Rais wa wake wa Kwanza. Ni kama ambavyo Stalin na mao walivyoko katika historia ya nchi za Urusi na China. Wenzetu huko wanaendelea tena kwa kasi sana na hawana ngonjera za Mao wala Stalin; sisi tusipogundua makosa hayo tutabaki kuwa walalamikaji dhidi ya Nyerere huku tukiwa hatuoni makosa yenyewe. Tutabaki na viongozi wanaoficha mafedha ya umma usiwsi wakati serikali inahsindwa kulipia majukumu yake halafu bado tukalalamika tena kuwa makosa yote ya serikali kukosa hela ni kutokana na Nyerere. Tena afadhali kabisa Nyerere alijitahidi kujenda viwanda vya ndani, alichokosea ni namna ya unedeshaji wa viwanda hivyo kwani uongozi wake baadaye ukwa kama vile wa kisisa badala ya kuwa uongozi wa kibishara. Tungefanya marekebishao hayo ya kuvifanya viwanda hivyo vijiendesha kibiashara kwa mfano kuuza hisa kwa watu binafsi tungesaidia sana kuimarisha viwanda hivyo. Lakini badala yake sisi tuliposikia neno privatization hatulichukulia kwa maana yake pana ya Private Sector, sisi tukalichukulia kwa maana finyu ya private individual. Kwa hiyo tukawa tunamtafuta mtu mmoja tajiri sana wa kumwuzia ambaye alikuwa anatafutwa kutoka nje ya nchi. Kenya pale walipo-privatize Kenya Airways waliuziana hisa wakenya wenyewe kwa wenyewe na leo unajua shirika hilo liko wapi. Kuuza kiholela viwanda vile vya Nyerere hakukuwa ni kurekebisha bali kulikuwa ni kubomoa kabisa ndiyo maana nchi leo ipo ipo tu ikiwa kama mwendawazimu. Tutaendelea hivi hivi mpaka tukome wenyewe.


Mimi nimeona kuwa swali lililotolewa hapa ni Uchumi wa Tanzania leo, siyo Historia ya Uchumi wa Tanzania Miaka 50 iliyopita. na Hivyo sioni kabisa nafasi ya sera za uchumi alizofuata Nyerere katika maisha ya watanzania wa leo

lakini kama wimbo vile; shule hazina vitendea kazi kwa sababu ya Nyerere. Migodi ya madini inachimbwa lakini serikali haipati chochote kwa sababu ya Nyerere. Miradi ya ujenzi wa miundo mbinu serikali inatolewa kinyemela kiasi kuwa ujenzi wake unakuwa ni substandard kwa sababu ya Nyerere. Manunuzi ya serikali yanakuwa ni ghali sana kuliko thamani halisi, kwa mfano ile rada tulilipa hela nyingi sana, kwa sababu ya Nyerere.
Tawire baba! nimekusikia.

Kosa lililofanyika wakati ule lilikuwa la uchumi kuingiliwa na siasa. Hata hivyo bado nafasi ya kurekebisha ilikuwepo.

Badala ya kutumia fursa hiyo kuendelea tunatumia fursa hiyo kulaumu historia tena iliyojenga misingi mingine mizuri. Hatutumii historia kupata ufumbuzi bali kumtuhumu mtu na wala si sera.

Leo akina Zakumi hawatoi credit kuhusu miundo mbinu iliyoachwa na ambayo haitumiki.
Mfano, Tumeshindwa kutumia TAZARA kuinua uchumi tunalalamika Nyerere kuwekeza katika TAZARA? Inaingia akilini kweli.

Katika mashirika 400 yaliyobinafsishwa sijui ni mangapi yamefanikiwa hadi sasa(PCSRC).
Nimempa Zakumi mifano miwili ya viwanda vya sigara na bia, ameikataa kwasababu anasema hivyo ni vitu vinavyopatikana popote.

Naendelea kumpa mifano
Katika mashirika 400 yaliyobinafsishwa zilikuwepo benki.
CRDB walikwenda kuchukua hisa kwa Mwalimu Butiama.

Hawakuuzwa kwa mwekezaji, wakabaki kuwa benki ya walala hoi.
Leo CRDB ni moja ya benki kubwa katika ukanda wetu.
Nimesoma taarifa ipo katika mabenki 100 ya Afrika.

Tukauza NBC kwa makaburu. Kipande kidogo kikamegwa na kuitwa NMB. Hiki ndicho cha wazawa.
NMB inafanya vizuri sana na mwaka jana ilitoa gawio katika serikali kubwa kuliko benki zingine.

Zakumi, kwanini Tanganyika packers igeuzwe kuwa hotel wakati ng'ombe tunao bado?
Je,ni kiu ya kula nyama za majuu au ndio ujinga tunaoongelea huo wa viongozi wetu.Kwanini isiwe 'CRDB'

Kwanini tununue majembe feki yaliyotengenezwa uani kule china na si UFI Dar es Salaam?
Kwanini tununue spea 'generics' kutoka middle east na siyo Mang'ula au Moshi machine tools.
Kulikuwa na sababu gani za kutelekeza Mang'ula na kuwa ghala la chumvi badala ya kuifanya iwe kama CRDB!

Kuna sababu gani za kiwanda cha Mbolea Tanga kufa na si kiwanda cha Saruji!
Kwanini Saruji Tanga na Wazo hill havikufa kama ilivyokufa Mutex na Mwatex katika mazingira yale yale ya kukosa wasomi na poor management unayozungumzia.

Nitajie ni mashirika mangapi katika yale 400 yaliyofanya vema kuliko ilivyokuwa wakati yanajengwa.

Na kwanini wakati huu tukiwa na business oriented people tunalipa umeme ghali unaoathiri uzalishaji kuliko wakati wa nyuma ili hali mabwawa ya umeme yaliyojengwa na Mwalimu ni yale yale na tena kuna gesi.
Kwanini tushindwe! wasomi wapo, rasilimali zipo tena zaidi kwanini tunashindwa
 
Last edited by a moderator:
NINI KIFANYIKE ILI KUKUZA SCIENCE, TECHNOLOGY AND INNOVATIONS (STI) FOR BETTER ECONOMIC GROWTH.

Tanzania mpaka tunapata uhuru swala STI lilikuwa liko katika kiwango kizuri sana na hata wale wanafunzi wachache waliweza kuwa watundu na wabunifu sana.Nakumbuka baba yangu mzazi aliwah kuniambia kwamba yeye akiwa jkt wakati huo aliwah kutengezeza redio satation na ikawa inarusha vipindi hewan tena ikafanya wakati huo yuko Maktopola kublock matangazo ya redio Tanzania na ikasikika steshen aliyoitengeneza.

Kwangu mimi hii hadithi huwa inanipaga picha moja tofauti sana kwamba kupitia elimu ya siasa ya ujamaa na kujitegemea wanafunzi wa miaka hiyo walipewa nafasi sana ya kuwa innovative na ku apply their local technology kwaajili ya maendeleo kwa ujumla.

Miaka 50 baada ya uhuru badala ya STI kukua inazidi kushuka kw akiwango kikubwa sana, kwa sasa hivi Tanzania kama nchi inategemea zaid imported technology and innovations. sababu kubwa ikiwa ni hakuna tena nafasi ya STI kwa sasa hivi. Ukitizama hatuna viwanda, na kama vipo mwenye kiwanda anataka matokeo(bidhaa) apeleke sokoni na sio vinginevyo. Hata kwenye kili,o ni hivyo hivyo hakuna nafasi zaid watu wanataka mbegu bora basi mvua watamtegemea Mungu na maisha yanaenda.

Imefika wakati sasa kweli tunahitaj kujifua upya kwaajili ya kukuza uchumi wetu hasa wa mwananchi mmoja mmoja. na kama kweli tuna nia ya dhati basi STI lazima ipew kipaumbele zaid.

nini kifanyike nakigawanya katika makundi 2 makubwa kwamba kuwepo na short term plans na long term plans.
Hata hivyo mipango hii igawnywe tena katika makundi mawili makubwa kwamba kuwepo na kundi moja la Beginners na kundi jingine la Professionals.

Labda tuanze na kundi la begginers.
Kundi hili linajumuisha wale ambao ni watoto toka chekecheka hadi secondary schools. Kundi hili ndilo ambalo limebeba vipaji na ari ya kupenda kuona vitu vinatokea tena ambavyo ni unique. Ni kundi kubwa sana ingawa litaonekana kama kundi dogo lisilo na tija zaid ya ksubiri kuhudumiwa tu. Sio kweli kabisa hili kundi likitumika vyema basi laweza kuwa ni msaada sana kwenye kukuza uchumi, sio kundi la kudharau hata kidogo.

Short term plans kwa beginners ziwe hivi
1) TEHAMA ipewe uzito unaostahili na sio siasa. wanafunzi wasomeshwe kwa vitendo na sio nadharia.
2) smart schools ziwe ndio priority kwa serikali kwa sasa baada ya kumaliza kujenda shule za kata basi waziboreshe ziwe smart schools, kwamba ziwe na electrified, ziwe na computer labs, science labs (well furnished), teaching aids,and books.
3) innovation iwe encouraged from pre-primary level, masomo kama VS yapewe uzito wake na wanafunzi wawe rewarded for their innovations.
4) Maonyesho ya kisayansi yaanzie ngazi hii, Hata kama mwanafunzi wa pre primary ataweza kutambua picha ya moyo na akaweza kusema unafanya nini basi huyu ashiriki maonyesho na aonyeshe uwezo wake huo. na kazi zote zinazopelekwa kwenye aonyesho basi zitumike kuinua vipaji vya washiriki.
5) waalimu wa VS na sayansi wapewe mafunzo maalum jins ya kugroom wanafunzi kuwa wanasayansi wagunduzi badala ya kuwafanya kuwa wanasayansi wanaokariri tu kila siku.
6) serikali iamue kugharamia haya kwa moyo wote ikiwa bajeti ya wizara ya elimu iongezwe lkn pia wizara ya sayansi na technolojia na mawasiliano nayo pia iwe na idara itakayo shirikiana na elimu kwaajili ya sayansi na ugunduzi. yaani kuweppo na close link kati ya hizi wizara mbili.

Long term plans kwa beginners
1) Academy growing scientist lazima iwe established and i think COSTECH wanalojukumu la kuhakikisha hili linatokea.Wale wanafunzi wote iwe wa nursery, primary na secondary ambao wanaonenaka kweli watakuwa wanasayansi wazuri kutokana na records basi wakutanishwe kwenye hii academy na wawe sasa wanapewa msaaada wa karibu zaid. Ili kuhakikisha huko mashulen hata kama ni clubs basi kwenye hizi club chochote kinachofanyika kinapata baraka za academy na hii itahusika pia na ama kumtafutia huyu mwanafunzi wapi akajiendeleze zaid kulingana na resources zetu hata ikibidi kumpeleka masomoni.

2)kuwepo na exchange programm ya waalimu na sayansi na waalimu hawa basi mbali na kupewa capacity building seminars wapekekwe shule maalum kwaajili ya kukuza vipaji tu.

3) sio vibaya basi kukawepo na wizara mpya kabisa ambayo itaratibu maswala ya STI kwa begginers.

kwa professionals hapa naongelea ngazi ya diploma hadi vyuo vikuu, hawa tayari wamesha onyesha uwezo fulan mzuri sasa basi short termnm plans kwao ziwe

1) wanapokwenda field wasiende kuwa desk officers wasailiwe kwenye kudemonstrate theri capacities tofauti na siku hizi ambapo yaani wanabaki kuwa clerical officers.
2) kama sehem ya project basi watakiwe kutengenza kitu yaani tangible object, na sio kufanya projects ambazo ni social work based. Mf. Mhandisi maji basi atengeneze mtambo wa kutibu maji ambao kweli ukijaribiwa unaonekana unafanya kazi n marks zipatikane kwa jinsi ambavyo mtambo huu utafanya kazi. mkemia basi atengeneza dawa ya kusafisha maji taka na kweli ikijariiwa ionekane inatibu maji na kuyaacha masafi yenye kiwango kinachotakiwa.
3) kwepo na mwaka wa internship baada ya kumaliza elimu ya darasani, katika mwaka huu mwanafunzi huyu apelekwe katika viwanda, mashamba taasisi za utafiti eetc ili huko akademonstrate capacity yake. hapa kusiwe na longo longo apewe ofisi aambiwe abuni cha kufanya kulingana na aina ya taasisi/kampuni na ambacho kinatija. na akileta uzembe basi aasifanyiwe vetting abaki hapo hapo hadi aperform na kwenye usaili wa kazini basi alichokifanya kwenye project yake na wakati wa intern kiadd value kwake.

4) TIRDO, COSTECH, TANZANIA ACADEMY OF SCIENCE, NIMR, TAFORI, MARI, IHI, NA UNIVERSITIES zishirikiane katika hili ili kuweza kupata namna bora ya kuwasaidia hawa wanafunzi.

5) patent and marketing procedure ziangaliwe kwa upya. lakin cha muhimu ni mwanafunzi aruhusiwe kupatent kazi yake na sheria za patent hasa kwa wanafunzi ziwe amended. wengi wa wanafunzi wankuwa discouraged as kazi zao nyingi zainabaki vyuoni ama waalimu wao wanazitumia ilihali wao ni sehem ya wadau katika kazi ile. Ikiwa kwamba kazi itamilikiwa basi imilikiwe na watu watatu kwamba chuo, supervisor na mwanafunzi mwenyewe, lakini first owner awe ni mwanafunzi.

Long term plans
1) centres for excellency for new technologies lazima sasa ianzishwe, hizi ziwe kulingana na fani mfao Nanotechnology platform, ama kama ilivyo Genomics centre hizi zote tayari zimeshakuwa established kwa hapa kwetu na mimi binafsi ni member wa founder wa hii nanotechnology platform.

2) collaborations with other international partners hili laweza kuwa ni la kwanza kabisa kwenye shor\term plans lakin naliweka kwenye long termplans kwasababu ni jambo ambalo ni endelevu. Hata hivyo tunahitaj long term collaborators zaid.

3) viwanda vyetu sasa viwe vinategema technolojia ya ndani na wasi rely kwenye imported technology. Hakuna sababu ya kusubiri kuajiri expert toka nje ilihali experts tayari tunao.

Hata hivyo bado yapo mambo mengi zaid ambayo serikali kw aupande wake inapaswa kuyaangalia na kuyarekebisha. Kwasasa nawasilisha haya machache na pindi nipatapo muda nitarudi na kuelezea hasara ambazo serikali inapata kwa kutoendeleza STI na faida ambazo serikali itapata kwa kuendeleza STI.
 
Zakumi unadhani Mwalimu angefanya nini kwa wakati huo na hali hiyo ya wasomi? Vitu gani vya kawaida ambavyo hatujaviongelea?

Mafanikio ya Kagame ni yapi kwa kulinganisha hali za watu wa kawaida wa nchi hizi mbili?

Pili, tafadhali soma mabandiko kwa uangalifu. Katika bandiko 48 na yaliyotangulia nimeeleza kuwa kuna culture ya corruptions inayoharibu uchumi katika serikali.

Tatu, lazima uelewe kuwa Mwalimu aliokuwa na wasomi wachache aliwaendeleza kielimu huku akijenga miundo mbinu na hivyo vijiwanda vidogo tulivyo navyo.
Leo miaka 30 baada ya yeye kuwweka misingi hiyo tuna wasomi wa kila fani na kila kiwango.

Je, wasomi wetu wa sasa wa miaka 30 baada ya mwalimu wamefanya kitu gani tunachoweza kusema Mwalimu alishindwa au alikosea.
Je, kukusanya kodi za bia, sigara na vocha za simu ndio mafanikio zaidi ya yale ya vijiwanda vya Mwalimu?
Nguruvi3 naomba tukubaliane kwamba mwl Nyerere yeye alitawala miaka 26 tu ambayo ni michache zaid kuliko hii 30 tuliyonayo kwasasa. Lakini kwa wakati ule kiwango cha elimu kilikuwa kikubwa kwasababu idadi ya waliojua kusoma ilikuwa ni 65% leo hii tunapoongelea idadi ya illiteracy ni 50% kwamba kwasasa wajinga ni wengi kuliko enzi zile za giza za mwal Nyerere.

the point am trying to make here ni kwamba elimu yetu kwasasa tumeshaiua kabisa, tumeweka too much politics kwenye swla ambao ni too technical. hakuna innovations, hakuna cretivity ulaghai ndio mkubwa na hata huko kwenye taasisi za vyuo ndio usiseme.

uwezo wa watu kupata funds ili kufanya tafiti ni mkubwa sana lkn kwasasa hivi hakuna funds tena manake tunajulikana sisi ni watu wa porojo tuu sio watendaji, hata kupublish mtu ni Dr ama Msc atataka apublish paper yake kwenye jouranal ambazo atalipia hivyo kwasababu analipia kama kasema uongo ama la ama kama kaandika kitu ambacho hakipo hakuna nayeweza kuikataa hiyo paper yake.

tafiti nyingi na zenyewe hazipewi kipaumbele 50 yrs bada ya uhuru tunahangaika kumfundisha mtu kunya kwenye choo?? na eti kujenga choo?? enzi za Mwl elimu ya afya bora na usafi wa mazingira ilikuwa inatolewa redioni na ilifika wakti nakumbuka bibi afya alikuwa naapita majumban kukagua vyoo,jiko na usafi wa mazingira baada ya yeye kustaafu na usafi wa mazingira tukastaafu leo hii idadi ya wanaokunywa maji yasiyo safi tena yenye contamination ya vinyesi kwa tanzainia ni 43% ya watanzania mil 45 fikiria.

Kimsingi wanasiasa wetu ni wachumia tumbo na wameua kabisa ile morale ya wasomi and thats why hata leo hii utamkuta prof anagombea ubunge na kulia lia mbele ya wanachi wake kuomba kura kuliko kukaa na kufikiri suluhu ya matatizo ya nchi in a broad way.

leo hii ukiniambia kwamba tunategema sigara na bia nitakuuliza madini ambayo yanaacha mashimo yana changia nini kwenye nchii, sioni, je msistu yenu sioni, je gesi yetu sion ardhi nayo ni zii, haya wasomi je wanachangia nini hakuna nenda UDSM ama MUHAS ama SUA angalia kama wana international patent yyte kwa miaka 10 iliyopita utalia. hakuna lkn kila mwaka vyuo vikuu nchini SA wana struggle kupata international patent kwenye innovations zao.
 
Last edited by a moderator:
mkuu gfsonwin asante kwa darasa, hivi baada ya uhuru zilianzishwa shule ngapi za ufundi? hadi sasa naona ni chache tu ninavyojua, Mbeya Tech. Tanga Tech. Arusha Tech. Dar Tech, Ifunda, na Mwanza sijui shule gani, sijui zingine kama zipo, ni kwanini serikali haikuendelea kuanzisha shule nyingi za ufundi? au m'badala wake ni hivi vyuo vya VETA?
 
Last edited by a moderator:
zumbemkuu naomba nikujibu hivi shule za ufundi zilizoanzishwa enzi za mwl zilikuwa karibu 12 kwa tanzania yote yaani karibu kila mkoa ulikuwa nazo enzi hizo mikoa ilikuwa 20 tu kwa tz bara.

Baada ya awamu ya 4 shule hizi zilibadilishwa na kuwa shule za kawaida mfano Ifunda tech, Moshi tech, arusha tech nk....
Vyuo vya VETA zililetwa kuja kuwa mbadala wa elimu ya sekondari lakn sio kureplace shule za ufundi. Hta hivyo VETA ni mkombozi sana hsa kwa wale ambao they cant go thru ordinary education as labda wako skilled kwenye VS lkn elimu ya kawaida ya kutahiniwa kwa kusoma darasan haimudu. sasa kazi ipo kwenye kurasimisha ujuzi wa hawa wanaotoka veta ndio changamoto kubwa.

hakuna anayekubali kuinvest kwao in real na wala hakuna chombo kinachohakikisha kwamba vijana hawa wakitoka shule basi wanaweza kumudu kujiairi na ama elimu yao itumike kwaajili ya kukuza uchumi.

nakumbuka kikundi kimoja tu ambacho kiko KEKO hapa dar hawa wanajishughulisha na na utengenezaji wa fenicha hawa walitokea VETA. nimewapenda sana ingawa wanalalamika kwamba bidhaa zao hazipewi kipaumbele kama za show rum za kichina simply kwasababu ni made in tanzania despite kwamba zina ubora mzuri.

we still have to do something.

KWASASA HAKUNA TECHNCAL SCHOOL MANAKE HATA IFUNDA TECH SASA NI SHULE TA KAWAIDA INGAWA IMEBAKI NA JINA HILO THE SAME AS IYUNGA TECH MOSHI TECH AND THE LIKE
 
Last edited by a moderator:
Zakumi unadhani Mwalimu angefanya nini kwa wakati huo na hali hiyo ya wasomi? Vitu gani vya kawaida ambavyo hatujaviongelea?

Mafanikio ya Kagame ni yapi kwa kulinganisha hali za watu wa kawaida wa nchi hizi mbili?

Pili, tafadhali soma mabandiko kwa uangalifu. Katika bandiko 48 na yaliyotangulia nimeeleza kuwa kuna culture ya corruptions inayoharibu uchumi katika serikali.

Tatu, lazima uelewe kuwa Mwalimu aliokuwa na wasomi wachache aliwaendeleza kielimu huku akijenga miundo mbinu na hivyo vijiwanda vidogo tulivyo navyo.
Leo miaka 30 baada ya yeye kuwweka misingi hiyo tuna wasomi wa kila fani na kila kiwango.

Je, wasomi wetu wa sasa wa miaka 30 baada ya mwalimu wamefanya kitu gani tunachoweza kusema Mwalimu alishindwa au alikosea.
Je, kukusanya kodi za bia, sigara na vocha za simu ndio mafanikio zaidi ya yale ya vijiwanda vya Mwalimu?

Mchambuzi, Nguruv3 and Co.

Naona kuna maswali mengi nayotakiwa kujibu. Nitajibu kwa ujumla. Nimeulizwa je Mwalimu angefanyanya nini? Ukweli wa mambo Mwalimu asingefanya tofauti na vile vile alivyofanya kwa sababu katika miaka 60, 70 na 80, kila nchi ilikuwa inajitahidi kuanzisha viwanda. Hii ilikuwa ni fashion kwa kila nchi. Kwa mfano miradi ya uzalishaji umeme na kufua chuma iliyofanyika nchini Zaire chini ya Mobutu ilikuwa na gharama kubwa zaidi ya makampuni makubwa 20 yalionzishwa wakati wa Nyerere.

Ujenzi wa makampuni ulikuwa-supported na World Bank, Financial Institutions na Wahisani. Ni taasisi hizi zilizotusaidia kufungua hayo makampuni zilizoshinikiza Tanzania kuuza hayo makampuni.

World Bank, Financial Institutions na Wahisani walitusaidia kujenga viwanda kwa sababu kulikuwa na nadharia inayokubalika kuwa ujenzi wa viwanda unainua maisha ya wananchi haraka. Mchumi mmoja wa Marekani alitoa nadharia yake kuwa watu wanapokuwa hawana cha kufanya (idle) wanakuwa hawana maendeleo. Lakini ukianzisha viwanda katika maeneo ya watu hao, uchumi utakuwa haraka na watu watapata maendeleo.

Nadharia inatokana na observation ya jinsi maendeleo ya viwanda Marekani yalivyobadili maisha ya watu. Wachumi wa Kirusi independently walikuja na nadharia kama hii na kuonyesha jinsi gani nadharia hii ilivyosukuma maendeleo ya Soviet Union.

Vilevile nadharia ilithibitishwa wakati wa vita vya pili vya dunia. Marekani ilikuwa kwenye depression na watu wengu walikuwa idle. Ujenzi wa viwanda vipya na ongezeko la uzalishaji wa bidhaa za kusaidia vita vya pili vilisaidia kukuza uchumi wa Marekani.

Kuna mifano mingi ninaweza kutoa kuonyesha kuwa ujenzi wa viwanda ilikuwa nadharia ya kuleta maendeleo kwa maeneo masikini.

Pamoja na hayo, hili nadharia ifanye kazi ni lazima iwe na assumptions zake. Nadharia hii ilikuwa developed kwa kuangalia maendeleo ya viwanda ya Europe and North America. Maeneo ambayo yalikuwa tayari na taasisi za kiraia, taasisi za kifedha, decent literacy rate, na mambo mengine ambayo mpaka sasa hayapatikani Africa.

Nadhani nimejibu. Kwa kifupi tu mazingira ya 60, 70, na 80 hayakufaa kwa upanuzi wa viwanda.
 
Mkuu Zakumi:

Ningependa kujadili mambo makuu matatu kufuatia bandiko lako #66 kama ifuatavyo:

Kwanza, hoja yako kwamba sababu zinazopelekea taifa to undergo industrialization inalenga ni kuondoa ‘idleness' kwenye jamii ni hoja isiyokuwa sahihi. Vinginevyo unataka kutuambia kwamba watanganyika baada ya uhuru walikuwa idle? Definitely jibu ni hapana, kwani 90% ya watanganyika walikuwa ni peasants, hivyo hawakuwa idle; Hata leo hii hali ni hiyo hiyo kwamba – Majority of labor force Tanzania (ambayo ipo Kilimo) sio kwamba ipo idle, bali inakosa incentives za kuendeleza kilimo kwa sababu mbalimbali ikiwa ni pamoja na low productivity, declining real incomes, among other factors;

Pili, Zakumi, uchumi wowote ambao haujaendelea (any underdeveloped economy) begins with Kilimo as the only existing industry of major proportions ambapo approximately 50-70% of GDP huwa derived from this sector, huku pia about 50-80% of the labour force inakuwa engaged kwenye sekta hii (Kilimo); Uchumi wa aina hii unaanza kupiga hatua ya maendeleo iwapo utafanikiwa kuleta ‘agricultural transformation' ambapo in the process, KILIMO is supposed to aid this structural transformation process by providing CAPITAL for expansion of other sectors, hasa, viwanda/manufacturing; That's how it happened in America, na nchi nyingine zote that underwent agricultural transformation; Kwa Tanzania, kupitia Azimio la Arusha, Mwalimu hakulenga kuwaondoa watanganyika from state of "idleness", bali kuleta transformation ambayo ingesaidia ujenzi wa modern sector, na pia kuifanya nchi ijitegemee - hasa kuondokana na ‘the syndrome of producing what you don't consume and consume what you don't produce';

Tatu, umejadili kwamba viwanda vyetu vilijengwa na International Financial Institutions (IFIs) and donors; Hii sio sahihi, especially kwenye ujenzi wa mass good industries kama vile oil, leather, textiles na vingine. Such industries were financed by STATE CAPITAL (tariffs, export earnings, kodi za ndani); IFIs na Donors, sehemu kubwa ya fedha zao zilienda kwenye miradi mingine ya maendeleo – afya, elimu, maji, umeme n.k; Na kwa mujibu wa mchumi mmoja wa World Bank aliyefanya kazi Tanzania miaka ya 1970s anasema moja ya sababu za msingi juu ya kwanini miradi mingi ya maendeleo nchini haikuwa sustainable ni kwamba - hapakuwa na coordination baina ya wahisani, kila nchi ilikuwa inafanya mambo kivyake vyake and treat eneo lake la kazi kama ni koloni lake; Kwa maana nyingine, kilichokuwa kinaendelea ni kwamba ni kama vile wahisani waligawana maeneo na kuyaendesha kwa top-down approach, hawakuwa wanafuata methods zinazofanana na pia hawakuwa wana-share experience, kwahiyo ilikuwa unakuta kwa mfano Sweden kakamata terrotiry yake, vile vile Britain, Denmark and so forth…

Mwisho ni hoja yako kwamba mazingira ya 60s, 70s, 80s hayakufaa kwa upanuzi wa viwanda. Umejadili hoja hii kwa kuelezea jinsi gani institutional readiness na mambo mengine yalivyojitokeza kwenye nchi za wenzetu (ulaya, marekani n.k); Hivi unaelewa ni jinsi gani jamii ya uingereza kwamba mfano ilipingana vikali na mapinduzi ya viwanda na mara nyingine uharibifu mkubwa wa mashine kwa makusudi kujitokeza? Pia kwa marekani, nadhani unaelewa kilichojiri katika vita baina ya north and south; Lakini in the end, economic motives za wachache prevailed; nachotaka kueleza hapa ni kwamba kila taifa that underwent industrialization zilikuwa na mazingira ambayo hayafanani, kwa mfano, angalia nchi kama South Africa, viwanda viliendelea wakati wa apartheid ambapo 90% ya wananchi walikuwa almost illiterate; Nje ya South Africa, ni nchi moja tu barani afrika ambayo imeweza undergo industrialization kwa mafanikio, na nchi hiyo ni Mauritius;
  • Kwanini hawa (Mauritius) waweze katika kipindi ulichojadili hapo juu kwamba sisi hatuwezi?
 
Last edited by a moderator:
zumbemkuu naomba nikujibu hivi shule za ufundi zilizoanzishwa enzi za mwl zilikuwa karibu 12 kwa tanzania yote yaani karibu kila mkoa ulikuwa nazo enzi hizo mikoa ilikuwa 20 tu kwa tz bara.

Baada ya awamu ya 4 shule hizi zilibadilishwa na kuwa shule za kawaida mfano Ifunda tech, Moshi tech, arusha tech nk....
Vyuo vya VETA zililetwa kuja kuwa mbadala wa elimu ya sekondari lakn sio kureplace shule za ufundi. Hta hivyo VETA ni mkombozi sana hsa kwa wale ambao they cant go thru ordinary education as labda wako skilled kwenye VS lkn elimu ya kawaida ya kutahiniwa kwa kusoma darasan haimudu. sasa kazi ipo kwenye kurasimisha ujuzi wa hawa wanaotoka veta ndio changamoto kubwa.

hakuna anayekubali kuinvest kwao in real na wala hakuna chombo kinachohakikisha kwamba vijana hawa wakitoka shule basi wanaweza kumudu kujiairi na ama elimu yao itumike kwaajili ya kukuza uchumi.

nakumbuka kikundi kimoja tu ambacho kiko KEKO hapa dar hawa wanajishughulisha na na utengenezaji wa fenicha hawa walitokea VETA. nimewapenda sana ingawa wanalalamika kwamba bidhaa zao hazipewi kipaumbele kama za show rum za kichina simply kwasababu ni made in tanzania despite kwamba zina ubora mzuri.

we still have to do something.

KWASASA HAKUNA TECHNCAL SCHOOL MANAKE HATA IFUNDA TECH SASA NI SHULE TA KAWAIDA INGAWA IMEBAKI NA JINA HILO THE SAME AS IYUNGA TECH MOSHI TECH AND THE LIKE
asante mkuu gfsonwin kwa majibu yako murua, mkuu Zakumi ukiachana na nini angefanya nyerere wakati huo, kwa sasa nini kifanyike kuokoa uchumi wetu?
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Zakumi:

Ningependa kujadili mambo makuu matatu kufuatia bandiko lako #66 kama ifuatavyo:

Kwanza, hoja yako kwamba sababu zinazopelekea taifa to undergo industrialization inalenga ni kuondoa ‘idleness’ kwenye jamii ni hoja isiyokuwa sahihi. Vinginevyo unataka kutuambia kwamba watanganyika baada ya uhuru walikuwa idle? Definitely jibu ni hapana, kwani 90% ya watanganyika walikuwa ni peasants, hivyo hawakuwa idle; Hata leo hii hali ni hiyo hiyo kwamba – Majority of labor force Tanzania (ambayo ipo Kilimo) sio kwamba ipo idle, bali inakosa incentives za kuendeleza kilimo kwa sababu mbalimbali ikiwa ni pamoja na low productivity, declining real incomes, among other factors;

Pili, Zakumi, uchumi wowote ambao haujaendelea (any underdeveloped economy) begins with Kilimo as the only existing industry of major proportions ambapo approximately 50-70% of GDP huwa derived from this sector, huku pia about 50-80% of the labour force inakuwa engaged kwenye sekta hii (Kilimo); Uchumi wa aina hii unaanza kupiga hatua ya maendeleo iwapo utafanikiwa kuleta ‘agricultural transformation’ ambapo in the process, KILIMO is supposed to aid this structural transformation process by providing CAPITAL for expansion of other sectors, hasa, viwanda/manufacturing; That’s how it happened in America, na nchi nyingine zote that underwent agricultural transformation; Kwa Tanzania, kupitia Azimio la Arusha, Mwalimu hakulenga kuwaondoa watanganyika from state of “idleness”, bali kuleta transformation ambayo ingesaidia ujenzi wa modern sector, na pia kuifanya nchi ijitegemee - hasa kuondokana na ‘the syndrome of producing what you don’t consume and consume what you don’t produce’;

Tatu, umejadili kwamba viwanda vyetu vilijengwa na International Financial Institutions (IFIs) and donors; Hii sio sahihi, especially kwenye ujenzi wa mass good industries kama vile oil, leather, textiles na vingine. Such industries were financed by STATE CAPITAL (tariffs, export earnings, kodi za ndani); IFIs na Donors, sehemu kubwa ya fedha zao zilienda kwenye miradi mingine ya maendeleo – afya, elimu, maji, umeme n.k; Na kwa mujibu wa mchumi mmoja wa World Bank aliyefanya kazi Tanzania miaka ya 1970s anasema moja ya sababu za msingi juu ya kwanini miradi mingi ya maendeleo nchini haikuwa sustainable ni kwamba - hapakuwa na coordination baina ya wahisani, kila nchi ilikuwa inafanya mambo kivyake vyake and treat eneo lake la kazi kama ni koloni lake; Kwa maana nyingine, kilichokuwa kinaendelea ni kwamba ni kama vile wahisani waligawana maeneo na kuyaendesha kwa top-down approach, hawakuwa wanafuata methods zinazofanana na pia hawakuwa wana-share experience, kwahiyo ilikuwa unakuta kwa mfano Sweden kakamata terrotiry yake, vile vile Britain, Denmark and so forth…

Mwisho ni hoja yako kwamba mazingira ya 60s, 70s, 80s hayakufaa kwa upanuzi wa viwanda. Umejadili hoja hii kwa kuelezea jinsi gani institutional readiness na mambo mengine yalivyojitokeza kwenye nchi za wenzetu (ulaya, marekani n.k); Hivi unaelewa ni jinsi gani jamii ya uingereza kwamba mfano ilipingana vikali na mapinduzi ya viwanda na mara nyingine uharibifu mkubwa wa mashine kwa makusudi kujitokeza? Pia kwa marekani, nadhani unaelewa kilichojiri katika vita baina ya north and south; Lakini in the end, economic motives za wachache prevailed; nachotaka kueleza hapa ni kwamba kila taifa that underwent industrialization zilikuwa na mazingira ambayo hayafanani, kwa mfano, angalia nchi kama South Africa, viwanda viliendelea wakati wa apartheid ambapo 90% ya wananchi walikuwa almost illiterate; Nje ya South Africa, ni nchi moja tu barani afrika ambayo imeweza undergo industrialization kwa mafanikio, na nchi hiyo ni Mauritius;
  • Kwanini hawa (Mauritius) waweze katika kipindi ulichojadili hapo juu kwamba sisi hatuwezi?

Mchambuzi;

Nimesema kuwa nadharia ya kutumia viwanda kuleta maendeleo ilijengwa kwa kufanyia observation ya nchi za Ulaya na North America (ambazo zina urban dwellers). Katika nchi hizi kama huna cha kufanya unakuwa idle au kwa kutumia lugha sahihi ya kisiasa unakuwa unemployed. Na kwa kusema kuwa watanzania walikuwa peasants, unathibitisha kuwa nadharia ya viwanda ilikuwa applied kwa jamii zisizotakiwa. Hakuna jamii inayotakiwa kubaki kuwa peasants. Inakuwa hivyo kwa sababu ya social and environmental constraints. Je unazivuka vipi hizo constraints? Unafikiri kujenga vijiji vya ujamaa pekee yake inatosha?


Kuhusiana na hoja yako ya pili, kuna mambo mengi yanayoleta expansion uchumi. Cha muhimu ni watu na mazingira yao. Kilimo ni bonus tu. Kuhusiana na Nyerere, unaonyesha umempa mesianic role now. Unasema alitaka kututoa kwenye the syndrome of producing what you don’t consume and consume what you don’t produce’. Naona unampa nafasi ya Nabii Musa kuwatoa wana wa Israel utumwani Misri.

Ukweli wa mambo msemo huu "the syndrome of producing what you don’t consume and consume what you don’t produce" violates principals of commerce. Sijuhi nyinyi mlikuwa mnatumia principal gani za biashara? Tanzania ilipokuwa inanunua mitambo ya viwanda tayari ilikuwa ni CONSUMER na Nchi zilizokuwa zinatuuzia mitambo ya viwanda ilikuwa walikuwa PRODUCERS. Au mlikuwa mnaangalia consumer and producer kwa kutumia darubini ya mvaa khanga na mtengeneza wake? Mngejaribu basi kuanzisha na viwanda vya kujenga viwanda muone kama mngeweza?

Ukitaka kuendelea ni lazima ukubali ku-exchange knowledge na vilevile kuwa consumer wa vile usivyo-produce. Otherwise, you will live in isolation.

Kuhusu nani alijenga viwanda. Urafiki alijenga mchina. Mutex - Italy. Kiwanda cha viatu Morogoro -World Bank. Fanya uchunguzi kuangalia ni kiasi gani pesa za misaada na mikopo kutoka nje zilivyochangia kwenye ujenzi wa viwanda. Wakati wa vita ya baridi, misaada na mikopo mingi ilimwagwa hili kuvutia nchi zetu kujiunga na kambi za kisiasa.

Kuhusiana na wahisani kutokuwa coordinated, why should they care?

Kuhusiana na mazingira ya 60,70, na 80. Kinachokusumbua ni uzalendo tu. Waliojenga South Africa ni Wazungu. Na wazungu haohao walijenga Zimbabwe. Kama unabisha jaribu kumjibu aliyeuliza Waafrika ndivyo walivyo?
 
asante mkuu gfsonwin kwa majibu yako murua, mkuu Zakumi ukiachana na nini angefanya nyerere wakati huo, kwa sasa nini kifanyike kuokoa uchumi wetu?

Zumbemkuu;

Ngoja niweke sawa. Nyerere alikuwa na sababu za kufanya makosa kwa sababu yeye alikuwa mtu wa kwanza , PIONEER. Tatizo ni kuwa watu wanataka kurudisha au kutumia vya Nyerere kama msingi wa maendeleo ya sasa. Hapa ndio napokuwa na ugomvi nao.

Kuhusianza na vitu vya kufanya, watanzania waanze kutumia common sense tu. Vitu vingine vitajileta vyenyewe. Kwa mfano watanzania wangesema kuwa ualimu iwe kazi ya watu waliofanya vizuri mashuleni na walipwe vizuri. Katika kipindi cha miaka kumi elimu ya Tanzania itainuka katika ngazi zote.
 
Mkuu Zakumi,

Kufuatia bandiko lako #69 hapo juu, naomba nianze na hoja yako ifuatayo:

Na kwa kusema kuwa watanzania walikuwa peasants, unathibitisha kuwa nadharia ya viwanda ilikuwa applied kwa jamii zisizotakiwa. Hakuna jamii inayotakiwa kubaki kuwa peasants.

Hapa unajichanganya tu. Suala hilo nilijadili kama ifuatavyo katika bandiko langu #67 hapo juu, na nahisi unakwepa hoja yangu ya msingi hapo; Nilijadili kwamba

uchumi wowote ambao haujaendelea (any underdeveloped economy) begins with Kilimo as the only existing industry of major proportions ambapo approximately 50-70% of GDP huwa derived from this sector, huku pia about 50-80% of the labour force inakuwa engaged kwenye sekta hii (Kilimo); Uchumi wa aina hii unaanza kupiga hatua ya maendeleo iwapo utafanikiwa kuleta ‘agricultural transformation’ ambapo in the process, KILIMO is supposed to aid this structural transformation process by providing CAPITAL for expansion of other sectors, hasa, viwanda/manufacturing; That’s how it happened in America, na nchi nyingine zote that underwent agricultural transformation; Kwa Tanzania, kupitia Azimio la Arusha, Mwalimu hakulenga kuwaondoa watanganyika from state of “idleness”, bali kuleta transformation ambayo ingesaidia ujenzi wa modern sector, na pia kuifanya nchi ijitegemee - hasa kuondokana na ‘the syndrome of producing what you don’t consume and consume what you don’t produce’;

Kuhusu suala la producers versus consumers, naomba nirudie nilichokueleza awali kwamba mtazamo wako umejikita zaidi katika muktadha wa Liberalisation, Marketization and Privatization; Aidha kwa makusudi au bahati mbaya, unapuuza ukweli kwamba "Making Africa Produce what it doesnt consume" was an official and deliberate policy strategy ya wakoloni ya kuvunja misingi ya uchumi wetu, na leo hii, we still suffer kutokana na sera hizo; Sielewi kwanini hauoni hilo; Na katika hili, niliuliza huko nyuma je:


  • Tunaweza ondokana na tatizo hili kwa kujikita kwenye export promotion strategies bila mipaka? Hili ni swali ambalo nilimuuliza pia Nguruvi3 awali; Vinginevyo, katika hili, hoja yako juu ya violation of principles of commerce haina mashiko, kwani uchumi imara wa nchi unajengwa kwa uwepo wa both producers and consumers, as long as kunakuwa na comparative advantage in specialization katika production dhidi ya wenzako; Nitajie mataifa yaliyofanikiwa kiuchumi duniani kwa kufuata kanuni yako ya CONSUMERISM KWANZA, PRODUCTION BAADAE.

Kuhusu hoja yako nyingine juu ya umuhimu wa knowledge exchange, hakuna anayebisha, ndio maana hata zile import substitution industries zilizojengwa, kulikuwepo nia ya knowledge and technology transfer na masuala mengine yaliyolenga kutujengea capabilities za kuwa competent producers; Nadhani suala muhimu kujadili hapa ni kwamba je:


  • Baina ya miaka ile ya import substitution strategies na nyakaati hizi za export promotion strategies, ni katika kipindi kipi kilikuwa more effective + committed juu ya suala zima la la technology and knowledge transfer unalojadili umuhimu wake?

Kuhusu mass goods industrialization in Tanzania during the 1960s and 1970s, very little foreign capital was involved, badala yake, local capital ndio ilitumika zaidi; Usiangalie tu ushiriki wa mchina, angalia composition ya ushiriki wake: kulikuwa na a small element of foreign public loans, private management contracts, but Local Capital ndio ili dominate in their establishments!

Nimalizie kwa kusema kwamba haujajibu hoja yangu ya msingi kuhusiana na industrialization ya South Africa, Mauritius, hoja ambayo ililenga kujibu mtazamo wako on how industrialization takes place; Sidhani kama hoja yako kuhusu mimi kukosa uzalendo inajitosheleza kujibu hoja yangu ya awali kwamba:

Mwisho ni hoja yako kwamba mazingira ya 60s, 70s, 80s hayakufaa kwa upanuzi wa viwanda. Umejadili hoja hii kwa kuelezea jinsi gani institutional readiness na mambo mengine yalivyojitokeza kwenye nchi za wenzetu (ulaya, marekani n.k); Hivi unaelewa ni jinsi gani jamii ya uingereza kwamba mfano ilipingana vikali na mapinduzi ya viwanda na mara nyingine uharibifu mkubwa wa mashine kwa makusudi kujitokeza? Pia kwa marekani, nadhani unaelewa kilichojiri katika vita baina ya north and south; Lakini in the end, economic motives za wachache prevailed; nachotaka kueleza hapa ni kwamba kila taifa that underwent industrialization zilikuwa na mazingira ambayo hayafanani, kwa mfano, angalia nchi kama South Africa, viwanda viliendelea wakati wa apartheid ambapo 90% ya wananchi walikuwa almost illiterate; Nje ya South Africa, ni nchi moja tu barani afrika ambayo imeweza undergo industrialization kwa mafanikio, na nchi hiyo ni Mauritius; Kwanini hawa (Mauritius) waweze katika kipindi ulichojadili hapo juu kwamba sisi hatuwezi?

Sijaona ukijadili hoja yangu hii in reference to how you viewed mchakato wa mapinduzi ya viwanda katika taifa hapo awali;
 
Heshima kwenu wakuu wangu! Nami nichangie japo kwa uchache sana.

Kwanza nianze kwa kusema kuwa, Hakuna sera bora za uchumi zinazoweza kusimama imara kama hakuna siasa na utamaduni imara. Vivyo hivyo kwa siasa na utamaduni. Tatizo sasa linakuja kwetu watanzania, tunashindwa kuhusianisha uchumi wetu na siasa na utamaduni wetu, hakuna uchumi utakaosimama kama hautafungamana/kuoana na siasa na tamaduni. Tunataka marubani kama hitaji la nchi, mashuleni wanafundisha unahodha, kwenye media wana-praise udobi, mtaani tunaishi kilimo, wapi na wapi?

Suala la msingi pia ni ATTITUDE ya watanzania juu ya Inward Strategies dhidi ya Outward Strategies, ina mashiko sana katika mafanikio ya pande zote mbili. Mtazamo-FIKRA, once we (majority) have proper attitude towards any of the sides, basi zote zinaweza kuwa na nafasi nzuri za kunyanyua uchumi wetu. Ikimbukwe pia kuwa hiyo proper attitude ni ile inayo-reflect Mazingira na Nyakati zetu halisi, kama wahusika wakuu. Kitu muhimu katika kufikia proper attitude ni our degree of conciousness juu ya mambo hayo, Massmedia, Education na Culture-Arts are responsible katika kukuza our degree of conciousness, political, economica and cultural. Contrary, leo media zetu zinahubiri kitu tofauti na development strategies zetu, vivyo hivyo kwa elimu yetu na sanaa zetu, tutafikaje?

Niungane pia na Mkuuu ZeMarcopolo kwamba, mwisho wa siku ni lazima tutambue kuwa sisi wenyewe kama watanzania, tuna wajibu wa kukamata njia kuu za uchumi. Sisi wenyewe. Nikihusisha na alichosema Mkuu Ngongo, kwamba wenzetu Botswana kupitia serikali yao, wana ubia katika migodi, kwanini isiwe na kwetu? Pia ni sahihi kabisa anaposema 'Mwanasiasa thinking yake iko ndani ya election circles. Anafikiria kimiaka mitano mitano na jinsi ya kupata kura', yote haya ni matokeo na viashiria vya njia batili za kupata uongozi bora.

Mkuu Ngongo amegusia pia ukosefu wetu wa Dira ya Maendeleo na matumizi mabaya ya japo kile kidogo tupatacho, hili liko wazi sana. Tuna-export lakini hata kale kafaida kadogo hatuoni matokeo yake chanya. Kwanza tumekosa vipaumbele kama taifa ndio maana hatuoni hata faida ya kile kidogo tupatacho, vipaumbele ambavyo vingekuwa determined na Dira yetu ya Maendeleo, ambayo nayo inatakiwa izaliwe toka DIRA YA TAIFA ambayo ndio muongozo wa kule tutakapo kufika ikihusianisha Uchumi, Siasa na Tamaduni zetu kulingana na Mazingira na Nyakati zetu.

Mkuu Zakumi anasema kwa jamii kama yetu ambayo ina uhaba mkubwa sana wa skilled labour, Outward Strategies ni muhimu sana katika kutupatia expertise, attract talents na capital. Ni kweli kabisa kwamba sisi ni wahitaji wa hayo yote, lakini Je, hakuna alternative yoyote ile? Kama ilivyohojiwa humu, nini ni kazi ya Economic Intelligence yetu? Naweza kusahihishwa hapa, lakini nachojua mimi ku-side na Outwards Strategies ni ku-side na Neo-Colonialists strategies, si vibaya, ila sasa...... kulingana na Nyakati zetu na Mazingira yetu,

a) Je, hiyo ndio njia pekee ya kukuza uchumi wetu? Kama ndio, Je, tuna mtaji/nguvu ya kutosha kusimama katika njia hizo ili kufikia tunakotaka? (Ikumbukwe pia kuwa Mtaji si teknolojia, pesa, nguvu kazi na malighafi tu, ni FIKRA pia) Je, zipo kwa majority? Mkuu zidane amenena vyema sana katika hili, kwamba Fikra za tulio wengi juu ya World Trade & Industrial policies kama important parameters za Outward Strategies ni kufaidika na misamaha ya kodi, aids, special treatment, etc, hiyo ndiyo sehemu ya mtaji wetu tulionao kifikra, utatufikisha wapi?

b) Je, hiyo njia ina-guarantee gani ya kutufikisha kule tunakotaka kufika? Tumefanya evaluation ya kutosha kujua usefulness yake? In relation ya mtaji tulionao.
c) Je, ipi ni gharama sahihiya kutufikisha tutakapo kupitia Outward Looking?

Mkuu Nguruvi3 ametoa changamoto za msingi pia juu ya Outward policy, kwamba tunatikiwa kuwa competative haswa si kwa kujilazimisha, kulazimishwa, kujaribu ama bora liende. A true competative ni yule mwenye mtaji wa kutosha, nina-doubt mtaji tulionao. Ni wazi haukidhi kutufanya kuwa among the competatives, ndio maana tunafanywa kichwa cha mwendawazimu na kila mtu, hata Kenya nao wanatuona mazuzu eti. Mtaji wetu katika Outward looking ikiwa inafanyika under world network ni kichekesho. Mi naita HILA za wazi, kamwe hatuwezi kumshindanisha sungura na kobe mbio, labda tuwe tunaishi kwa miujiza.

Wadau wengi wamegusia uongozi dhaifu kama chanzo cha uchumi duni. ni sahihi lakini nisingependa tuishie hapo. Kama tunatambua kwamba uongozi ni dhaifu, lakini bado tukashindwa kuupata ulio mzuri, tatizo si uuongozi tena bali ni njia za kupata hao viongozi ndio dhaifu. Kwa maana kama tutaendelea kutafuta viongozi wetu kupitia njia hizi hizi, kupata viongozi bora ni miujiza. TUNA SAFARI NDEFU SANA!

a4afrika
Mungu wetu yu tayari kutupigania vitani. Anaita sasa!
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Zakumi,

Kufuatia bandiko lako #69 hapo juu, naomba nianze na hoja yako ifuatayo:



Hapa unajichanganya tu. Suala hilo nilijadili kama ifuatavyo katika bandiko langu #67 hapo juu, na nahisi unakwepa hoja yangu ya msingi hapo; Nilijadili kwamba



Kuhusu suala la producers versus consumers, naomba nirudie nilichokueleza awali kwamba mtazamo wako umejikita zaidi katika muktadha wa Liberalisation, Marketization and Privatization; Aidha kwa makusudi au bahati mbaya, unapuuza ukweli kwamba "Making Africa Produce what it doesnt consume" was an official and deliberate policy strategy ya wakoloni ya kuvunja misingi ya uchumi wetu, na leo hii, we still suffer kutokana na sera hizo; Sielewi kwanini hauoni hilo; Na katika hili, niliuliza huko nyuma je:


  • Tunaweza ondokana na tatizo hili kwa kujikita kwenye export promotion strategies bila mipaka? Hili ni swali ambalo nilimuuliza pia Nguruvi3 awali; Vinginevyo, katika hili, hoja yako juu ya violation of principles of commerce haina mashiko, kwani uchumi imara wa nchi unajengwa kwa uwepo wa both producers and consumers, as long as kunakuwa na comparative advantage in specialization katika production dhidi ya wenzako; Nitajie mataifa yaliyofanikiwa kiuchumi duniani kwa kufuata kanuni yako ya CONSUMERISM KWANZA, PRODUCTION BAADAE.

Kuhusu hoja yako nyingine juu ya umuhimu wa knowledge exchange, hakuna anayebisha, ndio maana hata zile import substitution industries zilizojengwa, kulikuwepo nia ya knowledge and technology transfer na masuala mengine yaliyolenga kutujengea capabilities za kuwa competent producers; Nadhani suala muhimu kujadili hapa ni kwamba je:


  • Baina ya miaka ile ya import substitution strategies na nyakaati hizi za export promotion strategies, ni katika kipindi kipi kilikuwa more effective + committed juu ya suala zima la la technology and knowledge transfer unalojadili umuhimu wake?

Kuhusu mass goods industrialization in Tanzania during the 1960s and 1970s, very little foreign capital was involved, badala yake, local capital ndio ilitumika zaidi; Usiangalie tu ushiriki wa mchina, angalia composition ya ushiriki wake: kulikuwa na a small element of foreign public loans, private management contracts, but Local Capital ndio ili dominate in their establishments!

Nimalizie kwa kusema kwamba haujajibu hoja yangu ya msingi kuhusiana na industrialization ya South Africa, Mauritius, hoja ambayo ililenga kujibu mtazamo wako on how industrialization takes place; Sidhani kama hoja yako kuhusu mimi kukosa uzalendo inajitosheleza kujibu hoja yangu ya awali kwamba:



Sijaona ukijadili hoja yangu hii in reference to how you viewed mchakato wa mapinduzi ya viwanda katika taifa hapo awali;

Mchambuzi;

Nianze kwanza ni industrilization ya South Africa na Mauritius. Unataka kuwa color blind. Demographic iliyoleta maendeleo katika nchi hizo mbili haifanani ya kwako. Wazungu na wahindi ndio walioleta maendeleo katika nchi hizo mbili. Wazungu na wahindi waliopo Tanzania japokuwa ni wachache kwa idadi lakini wana kipato kikubwa sana kuliko wastani wa kipato cha mtanzania. Kama idadi ya wazungu na wahindi ingekuwa zaidi ya 10% ya idadi ya watanzania labda industrization ingetokea bila ya government intervention.

Sisemi kuwa watanzania wazawa hawawezi kufanya yanayofanywa na wazungu. Wanaweza lakini ni lazima tukubali mabadiliko ya kijamii ambayo yanaweza kuchukua kizazi kimoja au viwili. Chukua mfano wako mwenyewe. Pamoja na kuwa na elimu nzuri, unaweza kupata taabu ya kumshawishi mzazi wako kujiari mwenyewe. Mzazi wako yupo happy akiona unafanya kazi ya kuajiriwa serikalini. Kama shule ulisoma na wahindi au waarabu, wengi wao wapo kwenye private sectors ambazo wanamiliki wenyewe. Na wazazi wao wapo happy na choices za watoto wao.

Mpemba Bakhresa na Mchagga Mengi kuwa matajiri wakubwa sio coincidence. Wachina na wakorea are shrewd in business and education. Hivyo mafanikio yao katika industrial development sio matokeo ya government intervention pekee yake. Maendeleo yao yanasaidiwa na social attitudes ambazo katika jamii zetu hatuna.

Kuhusu majibu yako ya consumer and producer, hakuna mkoloni aliyetoa competitive advantage kwa makoloni yake. Mwingereza aliyafanyia makoloni yake ya Marekani na Canada yaleyale aliyotufanyia Africa. Mwingereza huyohuyo alipata faida kubwa kwa kufanya China soko la madawa ya kulevya. Mwingereza naye alitawaliwa na nchi mbalimbali. Na yeye pia alitendewa mabaya.

Unapodai uhuru unakubali challenges za kuwa mtu huru. Challenges za mtu huru hazipo kwenye industrial development kwa sababu industrial development unaweza kuifikia uku ukiwa unatawaliwa. Challenges za mtu kuwa huru ni watu kuchukua majukumu yao. Marekani hawakudai uhuru hili wawe taifa la viwanda. Maendeleo ya viwanda ni matokeo ya wao kuwajibika na kama watu huru.

Ukisoma posti zako, inaonyesha kuwa tulipigania uhuru hili tuwe na maendeleo ya viwanda. Utakuwaje na maendeleo wakati hutaki kuwajibika? Unatuelezea mipango ya Azimio la Arusha na nia zake. Watanzania hawakudai uhuru wawe na Azimio la Arusha. Walidai uhuru hili wawe responsible na maisha yao. Je unafikiri Marekani ingeendelea kama wangetangaza Azimio linalofanana na la Arusha miaka sita baada ya uhuru?
 
Samahani sana wanajamvi wote kwa makosa yanayoteka katika post zangu za awali huwa kwa sababu mkono wangu wa kulia una spidi kubwa kuliko ule wa kushoto kwa hiyo zile keys za kushoto huwa zinachelewa au zinashindwa kabisa kuingia katika mtililiko na matokeo unaweza kukuta keys za kulia zinafuatana wakati za kushoto zinakuja zimechelewa na kusababisha neno lote lisipate maana. Kwa bahati mabaya huwa sifanyi revision wakati wa kuweka instant pots mpaka baadaye sana.

Nikirudi kwenye mada, ni kuwa Tanzania ya leo tunahitaji mambo mawili makubwa sana ya kufanya katika kubadilisha mweleo wa Taifa letu tukufu.

(1) Jambo la kwanza kubwa ni kutenganisha kabisa siasa na serikali. Serikali ya Tanzania imekuwa inaendeshwa kisiasa kwa muda mrefu sana, na hilo ndilo kosa. Wakati wa vita baridi siasa ilikuwa ni sehemu kubwa mojawapo ya serikali lakini leo hii wakati wa utandawazi serikali ni sehemu kubwa ya biashara na uchumi wa taifa. Serikali iendeshwe kwa kodi wakati siasa inaendeshwa kwa michango ya wanachama wake. Mchango wa serikali katika siasa uwe tu wakati wa uchaguzi na usiwe na upendeleo wowote bali utumike equally kwa vyama vyote vinavyostahili.

Tunaweza kujadiliana kwa hili lakini ukweli ni kuwa siasa imekuwa ndiyo sumu kubwa sana katika maendeleo ya uchumi wa Tanzania. Tunaposema kutenganisha siaa na serikali ni pamoja na kuruhusu mtu yeyote agombee madaraka yoyote ya kiserikali bila kulazimishwa kuwa mwanachama wa chama chochote, anaweza kugombea uraisi, ubunge au udiwani bila kulazimishwa kuwa mwanachama chama chochote cha siasa.

Kukiwa na resistance katika maoni hayo nitayatetea huko mbeleni kwa kueleza kwa nini hatua hiyo itakuwa na positive outcomes kwenye uchumi wa nchi.

(2) Jambo la pili ni kuimarisha vyombo vya serikali; hasa polisi, mahakama na utumishi. Tukiwa tumefanikiwa katika hilo la kwanza hapo juu, itabidi tujenga vyombo hivi vitatu vijue kuwa vina madaraka ya mwisho kiutendaji wala havimwogopi mwanasiasa yeyote yule. Waajiriwa katika vyombo hivi vya serikali wachukuliwe kwa standards za juu sana kiasi kuwa wanapokiuka maadili ya kazi zao waadhibiwe vikali sana kusudi wawe wanafikiri kabla ya kukiuka maadili ya kazi zao. Adhabu kali zihusishe vitu kama kufungwa maisha au hata kunyongwa kulingana na uzito wa kosa lake.

Watumishi wa serikali wakishachukuliwa kwa standard ya juu sana, wao pia watafanya kazi zao kwa standard hiyo hiyo hata kama hawalipwi sana kuliko wale wa sekta binafsi.


Tukishafanikwa kujenga systems inayo-observe mambo hayo mawili bila hata kurekebisaha sera za kiuchumi zilizoko sasa, utashangaa jinsi nchi itakvyoanza kuendelea kiuchumi, tena kwa kasi ya kutisha,
 
Mkuu JingalaFalsafa
Kwanza karibu na heshima mbele, ahsante kwa kugusa kila eneo la mchangiaji.

Maneno haya yamenigusa
`Kwanza nianze kwa kusema kuwa, Hakuna sera bora za uchumi zinazoweza kusimama imara kama hakuna siasa na utamaduni imara. Vivyo hivyo kwa siasa na utamaduni. Tatizo sasa linakuja kwetu watanzania, tunashindwa kuhusianisha uchumi wetu na siasa na utamaduni wetu, hakuna uchumi utakaosimama kama hautafungamana/kuoana na siasa na tamaduni. Tunataka marubani kama hitaji la nchi, mashuleni wanafundisha unahodha, kwenye media wana-praise udobi, mtaani tunaishi kilimo, wapi na wapi` Hiki ndicho Kichuguu na wengine wamekiita uongozi. Katika nchi za wenzetu viongozi hawachaguliwi kwa maneno matamu bali historia na mchango wao katika uchumi. Mambo yanayoangaliwa ni ukuaji wa uchumu, mfumo wa bei, ajira na uwekezaji ikiwemo miundo mbinu na njia nyingine za uchumi. Hizo ndizo siasa za wenzetu tofauti na zetu za kugawa kofia na pilau.
Na hakika hapo ndipo tatizo lilipo.

Pia umejadili suala la elimu amblo gfonwin Zumbemkuu wameliongelea vema tu. Hakuna shaka kuwa elimu ni sehemu ya uchumi. Tatizio ni kuwa hawa viongozi wetu wanajua hilo!!

Zakumi: Tumekuuliza maswali ambayo hujayajibu. Tunauliza ungekuwa ni kiongozi wakati wa Mwalimu ukiwa huna wasomi na changamoto nyingine unefanyaje! Pili, mwalimu alikosea kuhusu viwanda kwa mtazamo wako, wewe ungeanzia wapi katika suala la uchumi. Kusema kuwa alikosea bila kutupa mbadala ni kutuambia hakukosea

Kuhusu hoja ya viwanda nadhani humtendei haki Mchambuzi. Hakuna mahali amesema ili tuendelee lazima tuwe na viwanda. Kinachosemwa ni kuwa maendeleo lazima yaambatane na mkakati wa uchumi. Kwamba tuwe na economic intelligence katika maeneo yote.

Kuhusu viwanda hilo ni sehemu ya maendeleo ya kiuchumi. Hatuzunguzii viwanda vya first world., tunaongelea vile vidogo ambavyo huongeza value za bidhaa. Hivi kweli tunashindwa kusindika machungu ya Muheza hadi yakasindikwe Kenya. Hivi kweli hatuwezi kuwa mashine za kusaga nafaka hadi tuuze nafaka nje.
Kinachotokea Shinyanga ni wakulima kuuza mchele Uganda na kisha kuununua katika mifuko kwa bei ya juu.

Nakumbuka Miji iliyokuwa na viwanda iliinuka sana kicuhumi na matokeo yake yanaonekana hadi sasa.
Viwanda ni sehehmu muhimu sana ya kuifikia jamii kuliko misaada ambayo huishia Uswiss.

Mifano mizuri ni mji wa Moshi, Arusha, Morogoro na Mwanza ambayo imeathirika sana kwa kufa sekta ya viwanda. Mchambuzi kauliza ni nchi gani imeendelea kwa kutumia falsafa ya consumerism

Na mwisho,hujajibu hoja kuwa hivi kulikuwa na tatizo gani kuwa na Magunia, Mwatex, Cement, Maturubai, Viberiti n.k. Je tunahitaji kuwa na vitu hivyo kwa sasa au bado tusubiri.


 
Zakumi,

Kuna sehemu umejadili kwamba vipo viwanda vilivyojengwa na mikopo ya International Financial Institutions; Ni kweli lakini kama nilivyoeleza, sio viwanda vyote vilijengwa kwa fedha hizo in large proportion kuliko STATE CAPITAL, , hasa oil, leather, textiles and a few othwr mass goods industries; Kuna kiwanda kimoja however ambayo kilijengwa entirely na mkopo wa Benki ya Dunia, na kiwanda hicho ni pulp and paper mills, mufindi, kwa ushauri wa world bank; Kuna Loan officer mmoja aliyefanya kazi na World Bank at the capacity ambae ananieleza hivi:

Mid 1970s, WorldBank walikuja na project proposal ya kujenga kiwanda husika; logic ilikuwa appealing enough, kwa mujibu wa huyu former loan officer wa World Bank kwani Nyerere had a firm commitment to universal primary education, and given the country's fast growing populatio (at 3% per year, not that different from annual GDP growth), nchi ilihitaji a large supply of books, na ndio maana mwalimu nyerere alikubaliana na ushauri wa kujenga kiwanda hiki akisema kwamba - "why import paper wakati it can be produced locally"? Hapa pia Zakumi, rejea hoja yako ya awali kwamba logic ni:
consumerism kwanza, production baadae

Tuendelee tuone kwanini kufa kwa viwanda hakutokana na sera za Mwalimu Nyerere peke yake;

Mchumi huyu mstaafu wa worldbank (robert calderisi) anasema kilichofuatia nia wide gap baina ya theory and practice; investment kwenye project ilikuwa ni kubwa sana na technology ilikuwa so advanced na serikali ya Tanzania ikasema haitaweza kuendesha mradi/kiwanda husika; maafisa wa World Bank wakashinikiza technical assistance iingizwe kwenye mradi, lakini haikuwa included kwenye bajeti ya mradi kwa sababu costs zingekuwa kubwa kuliko the expected benefits, hivyo board of directors ya worldbank wasingepitisha mradi husika;

Anasema kwamba hata bila ya technical assistance, the project barely paid off; miaka mitatu baadae, kiwanda kikafunguliwa, na hapo hapo worldbank wakapendekeza fedha nyingine $20 million dollars kwa ajili ya kuendesha kiwanda; kilichotokea, project ika narrow the financial terms na kuegemea zaidi on economics as the $200 million dollars zilizowekezwa sasa zikaangaliwa kama ni something of the past, hivyo haikuwa assigned financial value yoyote; future benefits zote zikawa weighed against the $20 million, na sio $220 million kama total cost of the project;

Ikawa envisaged kwamba safety valve ya mradi itakuwa ni export market (rejea mjadala wetu wa export promotion strategy kwa miaka ile vis a vis import substitution); Assumption ikawa kwamba kama Tanzania haitaweza ku-absorb the full production of the plant, surplus ingekuwa shipped to India ambao ni miongoni mwa nchi zinazoongoza kwa uzalishaji wa makaratasi duniani; Kwa bahati mbaya, india yenyewe ilikuwa ni mzalishaji mkubwa tayari, na gharama za usafirishaji zingefanya bei ya karatasi zetu kuwa kubwa sana;

Mchumi huyu anasema akiwa kama loan officer wa Tanzania (world bank) pale washington DC, aliamini kwamba mradi ule ungekuwa abandoned; wakubwa wake kwenye kitengo pia waliamini hivyo; Lakini senior management ya World Bank wakawa wanasema kwamba benki hiyo imeshawaingiza Tanzania mkenge, mradi umeenda mbali in planning, hawataweza abandon it; then siku chache kabla ya discussion ya board of directors, calderisi akapata phone call kutoka kwa corporate secretary department akimweleza kwamba cover page ya project ilikuwa sio sahihi kwabi ilisema:
The World Bank does not accept responsibility for the completeness or accuracy of this report

Huyo secretary akamuuliza calderisi je, should I recall the documents and chanhe the cover? Calderisi akamjibu, "not at all, you could not have chosen a better project for the mix up"!

Bodi ya wakurugenzi ikapitisha nradi ingawa the project never worked; mwisho wa siku, kiwanda hiki kikaingia katika orodha ya "white elephant projects", na anasema "Tanzania paid the bill for this foolish experiment for the next 20 years"; Mwalimu nasikia alikuwa very upset na utapeli huu wa worldbank;Na ni hawa hawa ambao miaka michache baadae wakaingia katika malumbano makubwa sana na Nyerere pale walipoanza shinikiza mageuzi ya kiuchumi nchini, na kufikia hatua ya mwalimu kuwaita IMF - international ministry of finance;

Cc: gfsonwin, Nguruvi3, Ben Saanane, Zinedine, Kichuguu, zumbemkuu, Ritz, zomba et, Mwigulu Nchemba, Zitto, JokaKuu, @hkigwangala, Jasusi, MTAZAMO, Nape Nnauye et al...



Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
Heshima kwenu wakuu wangu! Nami nichangie japo kwa uchache sana.

Kwanza nianze kwa kusema kuwa, Hakuna sera bora za uchumi zinazoweza kusimama imara kama hakuna siasa na utamaduni imara. Vivyo hivyo kwa siasa na utamaduni. Tatizo sasa linakuja kwetu watanzania, tunashindwa kuhusianisha uchumi wetu na siasa na utamaduni wetu, hakuna uchumi utakaosimama kama hautafungamana/kuoana na siasa na tamaduni. Tunataka marubani kama hitaji la nchi, mashuleni wanafundisha unahodha, kwenye media wana-praise udobi, mtaani tunaishi kilimo, wapi na wapi?

Suala la msingi pia ni ATTITUDE ya watanzania juu ya Inward Strategies dhidi ya Outward Strategies, ina mashiko sana katika mafanikio ya pande zote mbili. Mtazamo-FIKRA, once we (majority) have proper attitude towards any of the sides, basi zote zinaweza kuwa na nafasi nzuri za kunyanyua uchumi wetu. Ikimbukwe pia kuwa hiyo proper attitude ni ile inayo-reflect Mazingira na Nyakati zetu halisi, kama wahusika wakuu. Kitu muhimu katika kufikia proper attitude ni our degree of conciousness juu ya mambo hayo, Massmedia, Education na Culture-Arts are responsible katika kukuza our degree of conciousness, political, economica and cultural. Contrary, leo media zetu zinahubiri kitu tofauti na development strategies zetu, vivyo hivyo kwa elimu yetu na sanaa zetu, tutafikaje?

Niungane pia na Mkuuu ZeMarcopolo kwamba, mwisho wa siku ni lazima tutambue kuwa sisi wenyewe kama watanzania, tuna wajibu wa kukamata njia kuu za uchumi. Sisi wenyewe. Nikihusisha na alichosema Mkuu Ngongo, kwamba wenzetu Botswana kupitia serikali yao, wana ubia katika migodi, kwanini isiwe na kwetu? Pia ni sahihi kabisa anaposema 'Mwanasiasa thinking yake iko ndani ya election circles. Anafikiria kimiaka mitano mitano na jinsi ya kupata kura', yote haya ni matokeo na viashiria vya njia batili za kupata uongozi bora.

Mkuu Ngongo amegusia pia ukosefu wetu wa Dira ya Maendeleo na matumizi mabaya ya japo kile kidogo tupatacho, hili liko wazi sana. Tuna-export lakini hata kale kafaida kadogo hatuoni matokeo yake chanya. Kwanza tumekosa vipaumbele kama taifa ndio maana hatuoni hata faida ya kile kidogo tupatacho, vipaumbele ambavyo vingekuwa determined na Dira yetu ya Maendeleo, ambayo nayo inatakiwa izaliwe toka DIRA YA TAIFA ambayo ndio muongozo wa kule tutakapo kufika ikihusianisha Uchumi, Siasa na Tamaduni zetu kulingana na Mazingira na Nyakati zetu.

Mkuu Zakumi anasema kwa jamii kama yetu ambayo ina uhaba mkubwa sana wa skilled labour, Outward Strategies ni muhimu sana katika kutupatia expertise, attract talents na capital. Ni kweli kabisa kwamba sisi ni wahitaji wa hayo yote, lakini Je, hakuna alternative yoyote ile? Kama ilivyohojiwa humu, nini ni kazi ya Economic Intelligence yetu? Naweza kusahihishwa hapa, lakini nachojua mimi ku-side na Outwards Strategies ni ku-side na Neo-Colonialists strategies, si vibaya, ila sasa...... kulingana na Nyakati zetu na Mazingira yetu,

a) Je, hiyo ndio njia pekee ya kukuza uchumi wetu? Kama ndio, Je, tuna mtaji/nguvu ya kutosha kusimama katika njia hizo ili kufikia tunakotaka? (Ikumbukwe pia kuwa Mtaji si teknolojia, pesa, nguvu kazi na malighafi tu, ni FIKRA pia) Je, zipo kwa majority? Mkuu zidane amenena vyema sana katika hili, kwamba Fikra za tulio wengi juu ya World Trade & Industrial policies kama important parameters za Outward Strategies ni kufaidika na misamaha ya kodi, aids, special treatment, etc, hiyo ndiyo sehemu ya mtaji wetu tulionao kifikra, utatufikisha wapi?

b) Je, hiyo njia ina-guarantee gani ya kutufikisha kule tunakotaka kufika? Tumefanya evaluation ya kutosha kujua usefulness yake? In relation ya mtaji tulionao.
c) Je, ipi ni gharama sahihiya kutufikisha tutakapo kupitia Outward Looking?

Mkuu Nguruvi3 ametoa changamoto za msingi pia juu ya Outward policy, kwamba tunatikiwa kuwa competative haswa si kwa kujilazimisha, kulazimishwa, kujaribu ama bora liende. A true competative ni yule mwenye mtaji wa kutosha, nina-doubt mtaji tulionao. Ni wazi haukidhi kutufanya kuwa among the competatives, ndio maana tunafanywa kichwa cha mwendawazimu na kila mtu, hata Kenya nao wanatuona mazuzu eti. Mtaji wetu katika Outward looking ikiwa inafanyika under world network ni kichekesho. Mi naita HILA za wazi, kamwe hatuwezi kumshindanisha sungura na kobe mbio, labda tuwe tunaishi kwa miujiza.

Wadau wengi wamegusia uongozi dhaifu kama chanzo cha uchumi duni. ni sahihi lakini nisingependa tuishie hapo. Kama tunatambua kwamba uongozi ni dhaifu, lakini bado tukashindwa kuupata ulio mzuri, tatizo si uuongozi tena bali ni njia za kupata hao viongozi ndio dhaifu. Kwa maana kama tutaendelea kutafuta viongozi wetu kupitia njia hizi hizi, kupata viongozi bora ni miujiza. TUNA SAFARI NDEFU SANA!

a4afrika
Mungu wetu yu tayari kutupigania vitani. Anaita sasa!

JLF;

Nimeikubali posti yako na hususa ujumbe wa kubadili attitudes za wabongo. Attitude ya sasa ya kuamini kuwa serikali is a gigantic enterprise with unlimited resources ni lazima iondoke. Serikali ni lazima ifanye vitu inavyoweza kuvifanya kwa ufanisi. Kuiongezea serikali mamlaka katika shughuli ambazo haina uwezo nao kwa kisingizio cha kufuta umasikini ni kujiongezea umasikini.

Tukirudi kwenye majibu ya hoja zangu, kuna alternatives. Lakini kila kitu kina gharama zake. Moja ya alternatives ni kutumia mikopo. Nchi inaweza kutumia mikopo kutoka nje kujenga viwanda. Na baadhi ya viwanda vilivyojengwa kati ya 60-80 vilitumia mikopo. Matatizo ya mikopo ni kuongeza deni taifa. Viwanda vinaposhindwa kutimiza majukumu yake ya kurudisha pesa, ulipaji wa madeni na riba unaweza kuiletea nchi umasikini.


Alternative nyingine ni kutumia misaada ya kutoka nje. Misaada mingi ina masharti yake. Na vilevile tukumbuke kuwa wahisani wana watu wengi wa kuwasaidia. Cha muhimu zaidi kuhusu misaada ni donor fatique. Nchi za scandinavia zilitusaidia, lakini zilipochoka zilianza kutushinikiza kufanya reforms.

Mara nyingi hapa tunatoa mifano ya maendeleo ya viwanda ya China na South Korea. Nchi hizi na zingine za Asian Tiger zilikuwa zinategemea sehemu ndogo ya misaada kutoka nje (2%). Na vilevile hawakuwa na uwiano mbaya wa madeni kutoka nje. Hivyo shinikizo la kutoka nje linakuwa dogo.

Hivyo kwa maoni yangu binafsi si vibaya nchi kuanza kwa kutumia resources zake kwanza. Japokuwa mapato yanaweza yasiwe makubwa, matumizi mazuri ya kipato hicho yataleta mafanikio baadaye. Chukua mfano wa Tanzania. Kwa zaidi ya miaka 30 tuna mashule mengi ambayo hayana waalimu wazuri au wa kutosha. Haya ni matumizi mabaya ya kile kidogo tunachopata. Hii ni kwa sababu wahitimu wa shule hizo hawana manufaa ya kuleta mabadiliko.
 
Mkuu JingalaFalsafa
Kwanza karibu na heshima mbele, ahsante kwa kugusa kila eneo la mchangiaji.

Maneno haya yamenigusa
`Kwanza nianze kwa kusema kuwa, Hakuna sera bora za uchumi zinazoweza kusimama imara kama hakuna siasa na utamaduni imara. Vivyo hivyo kwa siasa na utamaduni. Tatizo sasa linakuja kwetu watanzania, tunashindwa kuhusianisha uchumi wetu na siasa na utamaduni wetu, hakuna uchumi utakaosimama kama hautafungamana/kuoana na siasa na tamaduni. Tunataka marubani kama hitaji la nchi, mashuleni wanafundisha unahodha, kwenye media wana-praise udobi, mtaani tunaishi kilimo, wapi na wapi` Hiki ndicho Kichuguu na wengine wamekiita uongozi. Katika nchi za wenzetu viongozi hawachaguliwi kwa maneno matamu bali historia na mchango wao katika uchumi. Mambo yanayoangaliwa ni ukuaji wa uchumu, mfumo wa bei, ajira na uwekezaji ikiwemo miundo mbinu na njia nyingine za uchumi. Hizo ndizo siasa za wenzetu tofauti na zetu za kugawa kofia na pilau.
Na hakika hapo ndipo tatizo lilipo.

Pia umejadili suala la elimu amblo gfonwin Zumbemkuu wameliongelea vema tu. Hakuna shaka kuwa elimu ni sehemu ya uchumi. Tatizio ni kuwa hawa viongozi wetu wanajua hilo!!

Zakumi: Tumekuuliza maswali ambayo hujayajibu. Tunauliza ungekuwa ni kiongozi wakati wa Mwalimu ukiwa huna wasomi na changamoto nyingine unefanyaje! Pili, mwalimu alikosea kuhusu viwanda kwa mtazamo wako, wewe ungeanzia wapi katika suala la uchumi. Kusema kuwa alikosea bila kutupa mbadala ni kutuambia hakukosea

Kuhusu hoja ya viwanda nadhani humtendei haki Mchambuzi. Hakuna mahali amesema ili tuendelee lazima tuwe na viwanda. Kinachosemwa ni kuwa maendeleo lazima yaambatane na mkakati wa uchumi. Kwamba tuwe na economic intelligence katika maeneo yote.

Kuhusu viwanda hilo ni sehemu ya maendeleo ya kiuchumi. Hatuzunguzii viwanda vya first world., tunaongelea vile vidogo ambavyo huongeza value za bidhaa. Hivi kweli tunashindwa kusindika machungu ya Muheza hadi yakasindikwe Kenya. Hivi kweli hatuwezi kuwa mashine za kusaga nafaka hadi tuuze nafaka nje.
Kinachotokea Shinyanga ni wakulima kuuza mchele Uganda na kisha kuununua katika mifuko kwa bei ya juu.

Nakumbuka Miji iliyokuwa na viwanda iliinuka sana kicuhumi na matokeo yake yanaonekana hadi sasa.
Viwanda ni sehehmu muhimu sana ya kuifikia jamii kuliko misaada ambayo huishia Uswiss.

Mifano mizuri ni mji wa Moshi, Arusha, Morogoro na Mwanza ambayo imeathirika sana kwa kufa sekta ya viwanda. Mchambuzi kauliza ni nchi gani imeendelea kwa kutumia falsafa ya consumerism

Na mwisho,hujajibu hoja kuwa hivi kulikuwa na tatizo gani kuwa na Magunia, Mwatex, Cement, Maturubai, Viberiti n.k. Je tunahitaji kuwa na vitu hivyo kwa sasa au bado tusubiri.



Nguruv3;

Nimejibu maswali yenu mara nyingi. Nimesema kuwa alichofanya Nyerere wasn't unique. Kilifanyika katika nchi nyingine pia. Zaire, Kenya, Zambia na hata Idd Amin wa Uganda alikuwa na mashirika ya umma. Kuanzisha viwanda ilikuwa ni fashion ya wakati huo. Hivyo basi hata mimi, wewe, mchambuzi, mkandara, kichuguu n.k tungekuwa madarakani, tungefanya vile alivyofanya Nyerere.

Katika miaka ya 60 na 70 kulikuwa hakuna ndondoo na wasomi waliobobea kuhusu uchumi wa nchi za kiafrika. Hivyo watu walijaribu vile walivyoona vinafaa. Sasa hivi ni zaidi ya 50 toka Tanzania ipate uhuru na ku-data zinazoweza kutumika kujenga sera nzuri za kuleta maendeleo. Miaka ya leo tunajua ni kitu kifanywe na serikali na kitu gani kiwe mikononi mwa watu binfasi.
 
Nguruv3;

Nimejibu maswali yenu mara nyingi. Nimesema kuwa alichofanya Nyerere wasn't unique. Kilifanyika katika nchi nyingine pia. Zaire, Kenya, Zambia na hata Idd Amin wa Uganda alikuwa na mashirika ya umma. Kuanzisha viwanda ilikuwa ni fashion ya wakati huo. Hivyo basi hata mimi, wewe, mchambuzi, mkandara, kichuguu n.k tungekuwa madarakani, tungefanya vile alivyofanya Nyerere.

Katika miaka ya 60 na 70 kulikuwa hakuna ndondoo na wasomi waliobobea kuhusu uchumi wa nchi za kiafrika. Hivyo watu walijaribu vile walivyoona vinafaa. Sasa hivi ni zaidi ya 50 toka Tanzania ipate uhuru na ku-data zinazoweza kutumika kujenga sera nzuri za kuleta maendeleo. Miaka ya leo tunajua ni kitu kifanywe na serikali na kitu gani kiwe mikononi mwa watu binfasi.

*Mwalimu hakufanya aliyofanya kwa imani kwamba alikuwa anafuata fashion, bali a deliberate move nia to delink us from an international capitalist system that made us permanent consumers of what we don't produce and producers of what we don't consume;

*Unadhani nini kiwe mikononi mwa serikali na nini kiwe mikononi mwa watu binafsi? Na watu binafsi ni kina nani? Mind you, liberalism (neo liberalism) requires that the government stays on the side lines and let the market forces allocate labour, capital and natural resources efficiently;


Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Zakumi,

Kuna sehemu umejadili kwamba vipo viwanda vilivyojengwa na mikopo ya International Financial Institutions; Ni kweli lakini kama nilivyoeleza, sio viwanda vyote vilijengwa kwa fedha hizo in large proportion kuliko STATE CAPITAL, , hasa oil, leather, textiles and a few othwr mass goods industries; Kuna kiwanda kimoja however ambayo kilijengwa entirely na mkopo wa Benki ya Dunia, na kiwanda hicho ni pulp and paper mills, mufindi, kwa ushauri wa world bank; Kuna Loan officer mmoja aliyefanya kazi na World Bank at the capacity ambae ananieleza hivi:

Mid 1970s, WorldBank walikuja na project proposal ya kujenga kiwanda husika; logic ilikuwa appealing enough, kwa mujibu wa huyu former loan officer wa World Bank kwani Nyerere had a firm commitment to universal primary education, and given the country's fast growing populatio (at 3% per year, not that different from annual GDP growth), nchi ilihitaji a large supply of books, na ndio maana mwalimu nyerere alikubaliana na ushauri wa kujenga kiwanda hiki akisema kwamba - "why import paper wakati it can be produced locally"? Hapa pia Zakumi, rejea hoja yako ya awali kwamba logic ni:


Tuendelee tuone kwanini kufa kwa viwanda hakutokana na sera za Mwalimu Nyerere peke yake;

Mchumi huyu mstaafu wa worldbank (robert calderisi) anasema kilichofuatia nia wide gap baina ya theory and practice; investment kwenye project ilikuwa ni kubwa sana na technology ilikuwa so advanced na serikali ya Tanzania ikasema haitaweza kuendesha mradi/kiwanda husika; maafisa wa World Bank wakashinikiza technical assistance iingizwe kwenye mradi, lakini haikuwa included kwenye bajeti ya mradi kwa sababu costs zingekuwa kubwa kuliko the expected benefits, hivyo board of directors ya worldbank wasingepitisha mradi husika;

Anasema kwamba hata bila ya technical assistance, the project barely paid off; miaka mitatu baadae, kiwanda kikafunguliwa, na hapo hapo worldbank wakapendekeza fedha nyingine $20 million dollars kwa ajili ya kuendesha kiwanda; kilichotokea, project ika narrow the financial terms na kuegemea zaidi on economics as the $200 million dollars zilizowekezwa sasa zikaangaliwa kama ni something of the past, hivyo haikuwa assigned financial value yoyote; future benefits zote zikawa weighed against the $20 million, na sio $220 million kama total cost of the project;

Ikawa envisaged kwamba safety valve ya mradi itakuwa ni export market (rejea mjadala wetu wa export promotion strategy kwa miaka ile vis a vis import substitution); Assumption ikawa kwamba kama Tanzania haitaweza ku-absorb the full production of the plant, surplus ingekuwa shipped to India ambao ni miongoni mwa nchi zinazoongoza kwa uzalishaji wa makaratasi duniani; Kwa bahati mbaya, india yenyewe ilikuwa ni mzalishaji mkubwa tayari, na gharama za usafirishaji zingefanya bei ya karatasi zetu kuwa kubwa sana;

Mchumi huyu anasema akiwa kama loan officer wa Tanzania (world bank) pale washington DC, aliamini kwamba mradi ule ungekuwa abandoned; wakubwa wake kwenye kitengo pia waliamini hivyo; Lakini senior management ya World Bank wakawa wanasema kwamba benki hiyo imeshawaingiza Tanzania mkenge, mradi umeenda mbali in planning, hawataweza abandon it; then siku chache kabla ya discussion ya board of directors, calderisi akapata phone call kutoka kwa corporate secretary department akimweleza kwamba cover page ya project ilikuwa sio sahihi kwabi ilisema:


Huyo secretary akamuuliza calderisi je, should I recall the documents and chanhe the cover? Calderisi akamjibu, "not at all, you could not have chosen a better project for the mix up"!

Bodi ya wakurugenzi ikapitisha nradi ingawa the project never worked; mwisho wa siku, kiwanda hiki kikaingia katika orodha ya "white elephant projects", na anasema "Tanzania paid the bill for this foolish experiment for the next 20 years"; Mwalimu nasikia alikuwa very upset na utapeli huu wa worldbank;Na ni hawa hawa ambao miaka michache baadae wakaingia katika malumbano makubwa sana na Nyerere pale walipoanza shinikiza mageuzi ya kiuchumi nchini, na kufikia hatua ya mwalimu kuwaita IMF - international ministry of finance;

Cc: gfsonwin, Nguruvi3, Ben Saanane, Zinedine, Kichuguu, zumbemkuu, Ritz, zomba et, Mwigulu Nchemba, Zitto, JokaKuu, @hkigwangala, Jasusi, MTAZAMO, Nape Nnauye et al...



Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums



Mchambuzi;


Asante sana kwa kunirahishia maisha. Sera kubwa za ujenzi wa viwanda zilikuwa kwenye concept uliyoitaja - "why import paper wakati it can be produced locally"?

This was the driver. Tulitaka kujitosheleza kwa kila kitu. We wanted to produce everything locally without understanding business and economic imperatives.

Nilishakueleza katika posti zilizopita kuwa. Viongozi wa nchi na wanachumi wanafungua viwanda kUkidhi hoja za kiuchumi. Lakini uendeshaji wa viwanda unafanywa na business administrators au businessmen kukidhi hoja za kibiashara.

Working temperaments za wachumi au wanasiasa wanaokidhi hoja za kiuchumi ni tofauti na zile za business administrators au businessmen.

In business world "WHY IMPORT, IT CAN BE PRODUCED LOCALLY" isn't a business imperative. Vilevile, viongozi wa nchi wakishatia saini mkataba tayari wamekubali. Hivyo hakuna kisingizio kama hayo yalikuwa sio makosa yao.

Kuhusiana na state capital, nitapinga hilo kwa sababu economic performance wasn't stellar. Na kama state capital ilitumika, kulikuwa na resource misallocation. Kufikia mwishoni mwa 70 mishahara ya watumishi wa serikali ilikuwa imepoteza thamani kwa asimilia 90 toka nchi ipate uhuru. Hivyo hiyo state capital unayohitaji ilitoka wapi? Unawalipa watu kidogo hili ujenge viwanda?

Kufikia 1974 uzalishaji wa kilimo ulikuwa umeshakwenda chini kwa kiwango kikubwa. Hivyo hiyo state capital inatoka wapi?

Kufikia mwishoni mwa 70, huduma za mijini kama vile kuzoa taka zilishasimama. Hivyo hiyo state capital inatoka wapi? Inaonyesha tulisimamisha baadhi ya huduma za msingi hili tujenge viwanda.

Kiwanda cha viatu Morogoro ilikuwa ni pesa ya kutoka world bank. Kiwanda cha nguo Musoma Mutex, ulikuwa ni msaada kutoka Italy kwa kupitia program ya STABEX.
 
Back
Top Bottom