Uchunguzi ulilenga kumkuta Hamza Mohammed Gaidi

Uchunguzi ulilenga kumkuta Hamza Mohammed Gaidi

brazaj

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2016
Posts
31,698
Reaction score
41,733
Kamanda Wambura ametoa taarifa yake kuhusiana na uchunguzi wa kadhia ya Hamza kuwa alikuwa ni gaidi.

Halipo jipya kwenye taarifa hiyo kwani ni wazi kuwa kilichofanyika ni kuhalalisha tu ambacho polisi kama sehemu ya kadhia wangekitaka.

IMG_20210901_201456_008.jpg


Ikumbukwe pia kamanda Sirro alishahoji hata uhalali wa wazazi wa Hamza kumzaa tu kama binadamu!

Kwanini walioshambuliwa na Hamza walikuwa ni polisi peke yao? Kwanini Hamza hakuonekana kujaribu kujificha ili kuendelea na mapambano kwa siku au hata masaa zaidi?

Kama Hamza alikuwa ni gaidi hakuwa na washirika wowote hapa nchini? Hakuwa na mawasiliano yoyote na washirika hao?

Kama Hamza alikuwa na washirika nje tu, ushahidi uko wapi?

Waliomfahamu Hamza hawakubaliani na ripoti hii ya polisi. Bila shaka CCM alikokuwa kiongozi na kada mtiifu hawakubaliani na ripoti kuwa Hamza alikuwa msiri au mtu wa kujitenga, achilia mbali kuwa gaidi.

Vipi bastola aliyokuwa nayo, ilimilikiwa kihalali? Hivi Hamza alipigwa risasi ngapi? Naye alifyatua risasi ngapi? Ziko wapi taarifa hizi?

Kulisikika pesa kiasi cha 400,000,000/= kuhusiana na kadhia ya Hamza kupotea. Kumesikika kupotea kwa madini ya Hamza na polisi wakihusishwa moja kwa moja kwenye kadhia hiyo.

Kumesikika uwepo wa kikaratasi (suicide note) chenye maelezo yote ya kwanini Hamza alichukua hatua hii.

Polisi ambaye ni mtuhumiwa anakuwa na uhalali upi kutojipendelea kwenye kadhia hii?

My take:

Ilikuwa ni kwa maslahi ya polisi na serikali kwa ujumla kuhakikisha uchunguzi huru, wa haki na unaoaminika unafanyika kwenye kadhia hii.
 
Hii issue ya huyu jamaa nimeona kuna vitu vitatu vilivyotumiwa na wengi kumhukumu kuwa ni gaidi.

- Kofia aliyokuwa amevaa; hii inatumiwa na dini ya Hamza, ni kielelezo cha kuwa muumini wa dini fulani, kwasababu hii naamini polisi na uchunguzi wao wakamaliza huyu alikuwa gaidi.

- Kutaja jina la "Allah"; pia jina hilo hutumiwa na dini ya Hamza kumuwakilisha Mungu wao, hapa pia jamaa zangu wakaunganisha matukio wakapata jibu walilotaka.

- Origin; asili yake ya Somalia panapohusishwa na vitendo vya ugaidi pia inawezekana imesababisha ahukumiwe bila kujua hasa dhamira yake ilikuwa nini wakati anatekeleza lile tukio.

Mwishowe, jamaa zangu walipounganisha matukio ndio wakaja na jibu walilokuja nalo, ukiunganisha na silaha aliyoitumia Hamza kuwashambulia polisi ndio neno gaidi likazaliwa.

Lakini kiuhalisia, nikitazama mlolongo wa matukio uliotufikisha hapo, naona "inawezekana" Hamza alikuwa na tatizo lake binafsi na polisi, kipo alichofanyiwa, na kwa mtazamo wake akaona hawa polisi wananifanyia/tufanyia hivi kwasababu ya dini yetu, ndio maana akatamka yale maneno kwenye ile video, ndio matokeo yake kikatokea kilichotokea.

Dawa ya kumaliza hii issue, Tume Huru ije kuchunguza itoe majibu mjadala ufungwe.
 
Hii issue ya huyu jamaa nimeona kuna vitu viwili vilivyotumiwa na wengi kumhukumu kuwa ni gaidi.

- Kofia aliyokuwa amevaa; hii inatumiwa na dini ya Hamza, ni kielelezo cha kuwa muumini wa dini fulani, kwasababu hii naamini polisi na uchunguzi wao wakamaliza huyu alikuwa gaidi.

- Kutaja jina la "Allah"; pia jina hilo hutumiwa na dini ya Hamza kumuwakilisha Mungu wao, hapa pia jamaa zangu wakaunganisha matukio wakapata jibu walilotaka.

Mwishowe, jamaa zangu walipounganisha matukio ndio wakaja na jibu walilokuja nalo, ukiunganisha na silaha aliyoitumia Hamza kuwashambulia polisi ndio neno gaidi likazaliwa.

Lakini kiuhalisia, nikitazama mlolongo wa matukio uliotufikisha hapo, naona "inawezekana" Hamza alikuwa na tatizo lake binafsi na polisi, kipo alichofanyiwa, na kwa mtazamo wake akaona hawa polisi wananifanyia/tufanyia hivi kwasababu ya dini yetu, ndio maana akatamka yale maneno kwenye ile video, ndio matokeo yake kikatokea kilichotokea.

Dawa ya kumaliza hii issue, Tume Huru ije kuchunguza itoe majibu mjadala ufungwe.

Usisahau pia mkuu maneno kwenye video hupenyezeka vizuri tu.

Hamza hakuwa na taabu na walinzi wengine wa jamhuri ila polisi.

Wangapi tuna yetu na polisi na tulipo tumatumia nguvu kubwa kumwachia mola awashughulikie kwa niaba yetu?
 
Ni sawa na mtabiri wa hali ya hewa kutabiri mvua ilinyesha kwasababu kulikua na mawingu.

Nami nadhani nina haki ya kutabiri:

"Hili ni kama la kuvunda. Wanavyo lifunika funika litavunda tena."

Polisi kama jeshi walitakiwa kujitathmini kuhusiana na haki, rushwa, dhuluma na manyanyaso wanayo wapa watu wasio na hatia.
 
Nami nadhani nina haki ya kutabiri:

"Hili ni kama la kuvunda. Wanavyo lifunika dunia litavunda tena."

Polisi kama jeshi walitakiwa kujitathmini kuhusiana na haki, rushwa, dhuluma na manyanyaso wanayo wapa watu wasio na hatia.
Ni sawa na kumpulizia perfume mwenye kinyesi badala ya kumuogesha.
 
Kwan Gaidi ni mtu gan?

Beberu anamwelezea gaidi vyema kama hivi:

"a person who uses unlawful violence and intimidation, especially against civilians, in the pursuit of political aims."

Ugaidi kama hivi:

"unlawfully using violence and intimidation, especially against civilians, in the pursuit of political aims."

Gaidi hulenga raia. Gaidi ana malengo ya kisiasa.
 
Sijui kwanini hii ishu ya Hamza imenifanya nikakumbuka kisa cha SAID ABDALLAH SIULANGA MWAMWINDI VS Dr. WILBERT KLERUU
Ingekuwa wakati huu wangempachika ugaidi hasa ukizingatia alikuwa anafuga ndevu.
 
Hii issue ya huyu jamaa nimeona kuna vitu viwili vilivyotumiwa na wengi kumhukumu kuwa ni gaidi.

- Kofia aliyokuwa amevaa; hii inatumiwa na dini ya Hamza, ni kielelezo cha kuwa muumini wa dini fulani, kwasababu hii naamini polisi na uchunguzi wao wakamaliza huyu alikuwa gaidi.

- Kutaja jina la "Allah"; pia jina hilo hutumiwa na dini ya Hamza kumuwakilisha Mungu wao, hapa pia jamaa zangu wakaunganisha matukio wakapata jibu walilotaka.

Mwishowe, jamaa zangu walipounganisha matukio ndio wakaja na jibu walilokuja nalo, ukiunganisha na silaha aliyoitumia Hamza kuwashambulia polisi ndio neno gaidi likazaliwa.

Lakini kiuhalisia, nikitazama mlolongo wa matukio uliotufikisha hapo, naona "inawezekana" Hamza alikuwa na tatizo lake binafsi na polisi, kipo alichofanyiwa, na kwa mtazamo wake akaona hawa polisi wananifanyia/tufanyia hivi kwasababu ya dini yetu, ndio maana akatamka yale maneno kwenye ile video, ndio matokeo yake kikatokea kilichotokea.

Dawa ya kumaliza hii issue, Tume Huru ije kuchunguza itoe majibu mjadala ufungwe.
Zungumzia na Ile video aliyokuwa amerekodiwa na abiria waliokuwa kwenye Ile Basi iliyokuwa kwenye eneo la tukio akiongea Yale maneno yanamaanisha nini.
 
Beberu anamwelezea gaidi vyema kama hivi:

"a person who uses unlawful violence and intimidation, especially against civilians, in the pursuit of political aims."

Ugaidi kama hivi:

"unlawfully using violence and intimidation, especially against civilians, in the pursuit of political aims."

Gaidi hulenga raia. Gaidi ana malengo ya kisiasa.

Je Yule Hamza alkua na malengo ya kisiasa?
 
Back
Top Bottom